Search This Blog

Monday 20 June 2022

KIZUIZI - 3

 





    Simulizi : Kizuizi

    Sehemu Ya Tatu (3)



     Taarifa inamfikia Emmy, taarifa yenye utata.

    Mwanamama aliyefahamika kwa jina la Devotha John amekutwa amekufa katika taksi. Hilo jina ni sawa na la mama yake mzazi.

    Taarifa ya pili kutoka kwa ndugu wa karibu ikatoa uhakika, Devotha aliyetajwa ni yuleyule mama mzazi na rafiki kipenzi wa Emmy, mama kitumbo akazimia. James akamkuta katika hali ile.

    Sasa wapo hospitali na Emmy anasimulia.

    UTATA MWINGINE...........CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ****



    Hakuna chozi linaloweza kubadili msiba kuwa sherehe, na hakuna kilio kinachoweza kumbadili aliyekufa aweze kurejea.

    Kilio huwa ishara ya uchungu, kisha maisha yanaendelea katika hali ya utofauti kwa muda mrefu kisha huzoeleka.

    Emmy hakupata mtu sahihi wa kumtuliza, kila aliyejaribu kumtuliza ni sawasawa alikuwa anampigia Kondoo zeze ili akate mauno, jambo lisilowezekanika.

    Mama yake alikuwa amekufa kwa kushambuliwa na sumu kali iuayo mara moja baada ya kupenya katika ngozi.

    Mtu aliyejaribu kwa kiasi fulani kumtuliza Emmy japokuwa sio sana alikuwa ni mwanaume shujaa aliyeyakabidhi maisha yake kutetea wengine na kuwalinda.

    Mwanajeshi kamili Lameck John Sulube.

    Emmy alitulia kwa sababu hakuwa na taarifa ya marejeo ya mwanajeshi huyo, na pia ile hatia ya kuzini nje ya ndoa ikaibuka upya. Akausahau msiba kwa sekunde kadhaa. Maneno ya Lameck yalikuwa yaleyale ‘Ni mipango ya Mungu!! Usilie sana utakufuru!!,

    Bwana ametoa na bwana ametwaa!!’. Maneno ambayo huwa hayana maana kwa mfiwa. Ukaribu wa Emmy na Lameck Sulube haukumshtua mtu yeyote ambaye aliijua kwa uchache familia ile. Waliwatambua hawa kuwa ni mtu na baba yake mdogo.

    Hata James mumewe hakutilia mashaka yoyote. Alikuwa anamjua vyema Lameck, anamfahamu fika kwani wakati anamrandiarandia Emmy aliwahi kukunjana mashati na huyu bwana. Lakini hakuchoka hadi alipofanikiwa kumuoa na sasa ni mjamzito.

    Ila jicho moja lilikuwa na mashaka na ukaribu ule.

    Akiwa amejivika suti nyeusi iliyomkaa vyema kijana huyu anayekimbilia miaka ishirini na mbili, kichwa chake kikiwa na nywele fupi zilizopakwa mafuta ya kung’ara, kiatu cha bei ghali kikiuvaa mguu wake. Kijana huyu alikuwa mtulivu sana, leso yake mkononi akipambana na jasho ambalo linataka kumharibia mwonekano wake. Mkono mmoja alikuwa na funguo zilizofanana na za gari.nani anajua huenda nayeye alikuwa ameegesha gari lake nje ya nyumba.

    Kwa kumtazama usingeweza kudhania yupo katika dunia nyingine, akijadili mambo yake tofauti kabisa na msiba unaoendelea.

    Zilipigwa nyimbo za kusihi watu waandae nyoyo zao kwa sababu hatujui saa wala dakika ya mwisho wetu, yeye hakuzisikia bali alihisi anapigiwa makelele na wachina wanaoimba nyimbo zao kwa lugha yao ngumu.

    Hatimaye ukafika wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa marehemu.

    Kutokana na uwingi wa watu katika msiba huu, ilibidi mwongozaji atoe utaratibu maalumu kabisa wa kuuaga mwili wa marehemu Devotha.

    Alianza kwa kuiita familia ya marehemu, hapa akawaita watoto na baba. Wakaaga.

    Dada, mawifi, shangazi, mama wadogo. Wakaaga.

    Baba wadogo, baba wakubwa, mashemeji, wajomba, kaka. Nao wakajongea waweze kuaga. Yule kijana aliyekuwa amejikita katika kujipangusa jasho akasitisha zoezi lile, akaiacha jasho itiririke, akajisahau kuwa alikuwa amevaa suti, akaanza kuhaha huku na huko.

    Akazidi kujiuliza ile sura kwa nini inamvutia.

    Mwanzoni alidhani kuwa ni mteja mmojawapo aliyewahi kufika katika banda lake kwa ajili ya huduma za kuweka na kutoa pesa. Lakini sasa akili ikamruka hakutaka kuamini kuwa yule ni kama anavyomdhani.

    “Samahani kaka mambo vipi. U mwenyeji wa maeneo haya.” Aliuliza kwa sauti tulivu, akiwa amelitoa koti la suti na kulitupia begani.

    Jose B waukweli anaingia kazini.

    “Kiasi fulani kwani vipi?.”

    “Hivi yule jamaa aliyevaa kadeti ndiye Thomas, mdogo wake na marehemu?” alihoji kiujanja Jose B.

    Mng’aro wake na mavazi yake yakamfanya aheshimike. Yule bwana hakuwa anajua sana juu ya ile familia. Lakini alimuita mwenye ukaribu na familia ile.

    Jose B akauliza swali lilelile. Akapatiwa jibu kuwa yule anaitwa Lameck, ni shemeji wa marehemu.

    “Na yule mwanamke waliyekuwanaye ni kama mtoto wake.” Alijibu hata ambayo hajaulizwa.

    Na hivyo ndivyo Jose B alikuwa anapenda. Ili ajue mengi.

    Kuna jambo hapa!! Si bure. Aliwazua Jose, huku akijituliza na kujiuliza inakuwaje amhisi vibaya yule bwana.

    Baada ya ndugu wa karibu kumaliza kuaga. Wasindikizaji wengine nao waliaga.

    Jose B hakwenda kuaga, akabaki kumfuatilia Lameck na nyendo zake.

    Mara Lameck akakutana na kipande cha mtu, kilikuwa kinampa pole.

    Jose B akashtuka, kile kipande alikuwa anakifahamu vyema. Aliwahi kukiona maeneo fulani jijini Dar es salaam.

    Ubungo. Zamzam guest house.



    Kipande kile cha mtu kilikuja kumpokea Emmy, kikamuingiza ndani kisha kikatoka nje. Sasa ikajengeka picha ya mwisho ya kumaliza utata kwa Jose B waukweli mshakunaku wa kimataifa.

    Yule aliyebaki ndani pamoja na Emmy ndiye huyu anayeitwa baba mdogo.

    Jose B akacheka kisha akamshukuru Mungu kwa kumbariki na kipaji hicho cha kipekee. Kwa hiyo baba na mwana wanamahusiano ya kimapenzi....eeh!! Mungu ameumba dunia na maajabu yake, ndo maana nikashangaa kivipi napewa malipo makubwa hivyo.

    Kumbe ni baba na mwana. Jose B akamaliza kwa kicheko kifupi.

    Safari ya kuelekea kuzika ikafuata.

    Jose B alikuwa amekuja na gari ndogo, ilikuwa ngumu kujua iwapo ni yake ama amekodi, aliingia katika gari na kumuamuru dereva aondoe.

    Alifungulia mziki wa taratibu kwa sauti ya chini.

    Wakati mziki ukiendelea, Jose B akaanza kumfikiria upya Emmy, akajisahaulisha kuwa mwanamama huyu kwa sasa yupo katika machungu makubwa ya kumpoteza mama yake mpenzi.

    Jose B akamuwaza kama mwanamke ambaye amejaribu kumtapeli ama wamefanya biashara isiyokuwa sahihi.

    “Mimi nilielewana naye kuwa anipe milioni saba ama nyumba nikidhani kuwa alikuwa na mtu wa kawaida tu wakimsaliti James, lakini kumbe alikuwa na baba mdogo? Hii biashara kamwe nisingeweza kuifanya kwa milioni saba au kinyumba kile, hii ni hasara tena hasara kubwa tu. Yaani mtu na baba yake niiuze kwa milioni saba? Si bora hata nisingeiuza kabisa. Mtu na baba yake unadhani mchezo!! Yaani hapa sikubali kudhulumiwa kiwepesi wepesi. Lazima haki itendeke hapa.” Aliwaza Jose B kwa hisia kali sana kama mtu aliyewekeza mahali kisha akadhulumiwa pesa yake halali.

    Jose B hakuwekeza chochote!! Cha ajabu analalamika.

    Au huyo baba mdogo amsaidie huu mzigo, kweli ngoja nimtwike na yeye mzigo wa kulipia hasara niliyoingia. Alibadili mawazo yake Jose B, akaugeuzia upepo kwa Lameck Sulube.



    ***



    Laiti usingekuwa ukakamavu wa jeshi, huenda Lameck angeweza kuanguka wakati wa kutupia mchanga wa mwisho katika kaburi la Devotha, mama yake Emmy.

    Ama hakika damu ni nzito kushinda maji.

    Lameck kwa mkono wake alikuwa ameteketeza maadui wengi waliothubutu kukatiza mbele yake katika vita huko Sudani.

    Wengine aliwalipua vichwani na wengine aliwapasua matumbo kwa bunduki. Hayo yote yalikuwa ya kawaida kwake, iweje kifo cha mtu huyu kimguse kwa kiasi hicho.

    Alikuwa nyumbani kwake wakati akiwaza haya.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Lakini ni ubishi wake..

    Lameck aliyakumbuka mazungumzo yake ya mwisho na mama yake Emmy katika hoteli iliyopo pembebi kidogo ya jiji. Mazungumzo nyororo yaliyoishia pabaya baada ya mada mpya kuletwa mezani.

    Mtu na shemeji yake wakaanza kulumbana baada ya Lameck kumgusia mama Emmy kuwa anampenda mwanaye sana.

    Kumpenda halikuwa tatizo, Lameck akaleta hoja ya nyongeza kuwa wamewahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi tangu wakiwa watoto.

    “Mnaendelea hadi sasa?” Devotha alimuuliza.

    Lameck akapinga. Devotha akashusha pumzi kali.

    Lameck akaendelea kuikaribia maana aliyoitaka.

    Akamgusia Devotha kuwa Emmy ameolewa akiwa si bikra.

    “Acha upumbavu wewe...mbona mumewe alileta shukrani ng’ombe mbili nyumbani kwa kumkuta Emmy akiwa mzima na usichana wake huko Uganda?” Alijibu kwa kebehi kiasi fulani huku taharuki ikianza kuchukua mkondo.

    Lameck akashtuka, hakutegemea kusikia hayo kutoka kwa yule mama. Kumbe James alienda kujisifu. Kujisifu kwa Bikra feki iliyotengenezwa na daktari mashuhuri Lameck John Sulube, kwa kutumia Shabu, Ndimu na kisha kuiweka makini zaidi ikawekewa dondoo za sabuni aina ya KAISIKI. James akadanganyika na kutoa ng’ombe mbili.

    “Au nimpigie James simu hapa akuumbue??” aliongezea yule mama Lameck akiwa bado kimya.

    “Haina maana shemeji kufanya hivyo” Lameck aliweka nidhamu mbele.

    “Kumbe ulichoniitia.”

    “Kuna jambo la ziada....”

    “Lipi?” aliuliza kisharishari.

    “Ni kuhusu Emmy na mimi, nimeamua nianze kujadili na wewe kiutu uzima kisha tutamuita Emmy.......” kabla hajaendelea yule mama mweupe ambaye uso wake ulikuwa umeanza kuwa mwekundu kutokana na hasira alimkatisha, “Shem Lameck naomba tusivunjiane heshima, yaani mimi wewe na mwanangu tukae kuzungumzia bikra mara sijui mlikuwa na mahusiano utotoni, unamshutumu mwanangu hana bikra, hiyo bikra uliitoa wewe mpuuzi mkubwa, na kwa taarifa yako ni kwamba Emmy ni mama mtarajiwa, ana kitoto kinaimba kwa furaha tumboni, sitaki kabisa umkere mwanangu, nenda ukapambane na wanajeshi wenzako huko si mwanangu....jitu zima hata aibu huna na nitaenda kumwambia mume wake....mshenzi wewe....yaani umekosa wanawake mtaani huko unakuja kujishebedua kwa mtoto wako loooh aibu kweli na nitakushtaki ukiendelea nasema nitakushtaki Lameck...ukome, umkome mwanangu” mama alipaza sauti, ikawa kazi ya Lameck kumsihi mama huyu asiongee sauti ya juu.

    Mara akasimama aweze kuondoka. Lameck akamdaka mkono, akaanza kumlaghai kuwa alikuwa anatania, lakini yule mama alikubali kinafiki tu kuwa hawezi kuyafikisha mahali popote maneno yale.

    Lameck kwa kumsoma macho yake akaugundua unafiki wake. Lameck alikuwa amechukizwa sana na maneno makali kutoka kwa yule mama, hasahasa maneno ya mwisho ya kumtishia kumshtaki. Lameck akaongozwa na hasira, na kwa kujilinda siri ile isitoke mapema.

    Akatumia msemo wa heri mmoja afe wengi wapone.

    Kitendo cha sekunde kadhaa kutoka kwa mwanajeshi huyu.

    Sumu ikaugusa mwili wa mama Emmy.

    Yeye akanawa upesi upesi.

    Akarejea nyumbani, taarifa aliyoitegemea ndiyo ambayo aliipata kuwa mama Emmy alikufa akiwa katika gari iliyokuwa inamrudisha nyumbani akitokea hotelini. Bila kujulikana na nini alikuwa anafanya.

    Sasa amezikwa tayari na ni usiku mwingine Lameck anawaza yaliyotokea.

    Lameck ameua.



    ***

    Kwanza alijihisi yupo katika hatia kubwa sana ya mauaji, lakini aliamini fika kuwa si mategemeo yake kufanya mauaji yale. Akafikiria kwa nukta kadhaa ni nani wa kumbebesha mzigo ule wa mauaji ama la waweze kugawana naye.

    Akafumba tena macho yake akayakumbuka maneno ya daktari wa kijeshi nchini Sudani aliyemhakikishia kuwa kamwe hatoweza kuzalisha kwa hali aliyonayo.

    Anakumbuka kwa mara ya kwanza katika maisha yake alilia kama mtoto mdogo akabembelezwa na wenzake pasi na mafanikio.

    Walimbembeleza sana huku wakimpamba na maneno tele ya kishujaa. Walimwita jasiri ambaye amedhurika kishujaa akilipigania bara lake la Afrika, maneno hayo hayakumuingia akilini hasahasa akifikiria hao waliokuwa wakimwambia walikuwa na familia zao tayari, na hata ambao hawakuwa na familia bado muda wowote ule wangeweza kuzianzisha maana walikuwa na uwezo wa kufanya hivyo.

    Lameck alijikaza kiume akawakubalia kwa shingo upande. Nafsi yake ilikuwa inamlaumu naye akailaumu kwa kitendo cha kumwonea huruma yule msichana asiyemfahamu katika nchi ya Sudani kusini, ni msichana huyo aliyepelekea risasi ya bwana wa kiarabu kumlipua na kusambaratisha eneo lililo jirani na sehemu zake za siri kwa kiasi kikubwa!!

    Giza likatanda.

    Mwanga ukatokea baada ya siku tano, alijikuta akiwa na bandeji kubwa katikati ya mapaja yake. Hakuwa anakumbuka ni nini kimetokea mpaka pale aliposimuliwa jinsi alivyookolewa na wanajeshi wa jeshi la umoja wa mataifa kutoka Senegal na Ghana.

    Walimuelezea kama mfu aliyekishinda kifo katika dakika za majeruhi.

    Hakuna hata mtu mmoja aliyetegemea kuwa angeweza kupona, lakini imewezekana na alikuwa hai tena.

    Baada ya upasuaji ndipo yakatolewa yale majibu kuwa kizazi kimevurugwa huku akisaliwa na kipisi cha maungo yake.

    Jambo lililomtia simanzi kubwa.

    Jambo kuu aliloweza kufanyiwa ni kuwekewa maungo ya bandia ambayo hayakuwa na kazi kubwa zaidi ya kumpamba. Siri alibaki nayo yeye.

    Anarejeshwa katika nchi yake kabla ya mapambano kumalizika. Siri ile inazikwa katika mioyo ya wanajeshi shupavu wa umoja wa mataifa.

    Siri nzito isiyotakiwa kuvuja juu ya hali ya Lameck.

    Kimyakimya anarejeshwa nchini baada ya kidonda kupona.

    Kisingizio kikatangazwa kuwa ni hali ya hewa nzito ya nchi ya Sudani imepingana na afya yake. Habari hiyo ikapambwa zaidi kuwa licha ya kuzidiwa na mgandamizo wa hewa Lameck alipigana kiume na alikuwa mfano wa kuigwa na kila mwanajeshi, na jeshi la umoja wa taifa limemwandalia zaweadi ya ushindi na ushujaa.

    Sababu za uongo lakini kwa ajili ya kuutunza utu wa Lameck. Na zawadi aliyoahidiwa ilikuwa pole kwa kizazi kilichopotea vitani.

    Risasi ya mwarabu.

    Baba, mama na ndugu wote hawakujua lolote. Walimpa pole kwa maswaibu huku wakijipongeza wao kwa wao kwa ushindi mkubwa wa mwanao na sifa aliyowaletea.

    Kati yao hakuna aliyekijua kilio cha mwanajeshi huyu.

    Baada ya mapokezi haya. Lameck akaendelea na maisha ya uanajeshi huku akiwa na likizo ya muda mrefu ili aweze kutulia kiakili.

    Ni katika likizo hii anawaza juu ya maneno ambayo baba yake alimwambia siku ya kumpongeza; ukizaa mtoto atajisifu sana kwa kuwa na baba kama wewe, tena ikibidi na yeye ajiunge kabisa na jeshi.

    Maneno haya ya mzee yakamkumbusha matatizo aliyokumbana nayo nchi za kigeni. Lameck akawaza na kuwazua akamkumbuka Emmy. Aliyakumbuka mapenzi motomoto aliyompa siku ya kuagana naye. Kisha akakumbuka lililo kubwa zaidi. Mimba ya Emmy. Lameck na akili zake za kiutu uzima alikuwa na uhakika kabisa kuwa ile mimba haikuwa ya James kama inavyodhaniwa, aliamini kuwa ilikuwa inamuhusu yeye na mtoto atakayezaliwa alikuwa halali yake. Kile kichefuchefu ambacho Emmy alimtangazia kuwa kinamsumbua kwa kutumia zile dawa za kurejesha bikra kilizidi kumshawishi kuwa Emmy alikuwa mjamzito na amefunga ndoa akiwa na mimba ya takribani mwezi mmoja mimba ambayo sasa inadhaniwa kuwa ni ya James.

    Lameck akaamua kuipigania damu yake ambayo ipo katika tumbo la Emmy ambaye kiukoo ni ndugu wa karibu sana.

    Lameck anaamua kuzungumza na mama yake Emmy kiutu uzima ili wapate pa kuanzia. Tofauti na matarajio yake mama Emmy anataka kuvuruga mambo mapema zaidi, Lameck anajikuta anafanya mauaji kwa kutumia sumu kali inayopenya katika ngozi upesi.

    Devotha yu kaburini, Lameck katika kitanda akiwa na siri nzito.

    Hatua iliyofuata Lameck akaamua kumfuata mtu mwingine ambaye anaweza kumshirikisha katika jambo lile zito



     Wakati Lameck akiumaliza usiku wake katika namna ya kuwaza na kuwazua. Kamanda mwingine wa jeshi la mtaani alikuwa katika kitanda chake akirusharusha miguu huku akifanya tafakari. Alikuwa akimtafakari huyu bwana aliyemaliza siku yake akiwa na mawazo lukuki.

    Aliwaza jinsi ya kuchuma pesa kutoka kwake. Alipofikiria kuhusu pesa akaanza kumthaminisha Lameck, kwanza alimchukulia kama maskini wa kutupwa ambaye anaweza kumwajiri katika banda lake la kuweka na kutoa pesa. Alimshusha thamani kutokana na mahali ambapo alimuona kwa mara ya kwanza; Zamzam guest house. Alimchukulia kama mtanzania mwenye kipatgo cha chini sana na kamwe asingeweza kuzikimu gharama za hoteli kubwa kubwa.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Pia siku ya msiba bwana Lameck alikuwa hajachana nywele zake na nguo alizokuwa amevaa zilizidi kuishusha thamani yake mbele ya Jose B waukweli.

    Jose B hakujua kama Lameck ana mambo mengi magumu yanapita kichwani mwake, mambo ambayo yangevuja na kumfikia yeye basi ni biashara kubwa.

    “Hivi yule hata laki moja anaweza kutoa kweli? Hoteli nzuri imemshinda kulipia amempeleka yule malkia uswahilini” Jose alijiuliza huku akiijenga picha ya Lameck. Akajichagulia jibu kuwa ni hapana. Bwana yule hana pesa.

    Kwa jibu hilo Jose B akahisi ni kujipotezea muda kumfuatilia maskini kama yule.

    Jose B akalala huku akiuvunja mpango wa kumfuatilia Lameck. Ule mzigo aliotegemea kumtwisha Lameck akaamua kuurejesha kwa muhusika ambaye anaweza kutoa pesa. Emmy.

    Jose B aliamini kabisa kuwa ataonekana mnyanyasaji sana, mshipa wa aibu ukakumbuka kufanya kazi yake, akajifikiria mara mbilimbili aanze vipi kumweleza Emmy juu ya siri hiyo. Hakutaka kumweleza ana kwa ana.

    Akiwa katika banda lake la biashara siku iliyofuata alikuwa analo jibu tayari.

    Akafanya mawazo yalivyomtuma. Akachukua simu yake na kumpigia Emmy.

    Alipopokea akamuuliza kama yuko peke yake, akakubali kuwa alikuwa peke yake ofisini.

    Jose B akamwomba afike nyumbani kwake jioni ya siku hiyo akitoka kazini kuna jambo la kuzungumza.

    Emmy akakereka kutokana na huu usumbufu lakini hakutaka kumwonyesha Jose B waziwazi kwa sababu angeharibu mahusiano yao ambayo yameanza kuwa katika urafiki.

    Emmy akakubali wito.



    Majira ya saa kumi jioni Jose B alikuwa katika hekalu lake dogo akimngoja Emmy. Hapo kinywani alikuwa amepanga maneno ya kumweleza yule binti.

    Majira ya saa kumi na moja jioni. Emmy akiwa amemuaga James kuwa atachelewa kiasi kurudi nyumbani kwani atapitia saluni, alielekea nyumbani kwa Jose B. Kichwani akijiuliza huyu kijana alikuwa na lipi jingine la kumshirikisha.

    Kutokana na foleni za hapa na pale Emmy akafika kwa Jose B majira ya saa kumi na mbili jioni. Alimkuta Jose akiwa anamngoja.

    Jose B alipoteza dakika kadhaa kumpa Emmy pole ya msiba na stori nyinginezo za kumfariji kutokana natukio lile.

    Katika kupewa pole ya msiba, Emmy akamkumbuka mama yake, mara akaanza kulia. Jose B alikuwa pekee katika nyumba ile, akamsogelea Emmy na kuanza kumbembeleza, Emmy aliendelea kulia Jose B naye akazidi kumfariji huku akimfuta machozi, kigiza kiliendelea kutanda pale ndani kumaanisha kuwa usiku unaingia.

    Jose B ambaye hakuwa mtu wa wasichana hovyohovyo akajikuta yu majaribuni, Emmy alikuwa amemlalia huku akiendelea kulia kwa kwikwi. Zile bastola zilizomteka James nchini Uganda, zikakichoma kifua cha Jose B.

    Akili ikamuhama kijana huyu mara akampapasa.

    Emmy kimya.

    Akampapasa tena bado Emmy alikuwa kimya.

    Kigiza kikawalaghai wawili hawa kikazitwaa aibu zao na kusafiri nazo mbali.

    Mama mjamzito hatakiwi kuvaa nguo ngumu wala zile zinazombana. Emmy naye akiwa na kitumbo kidogo alifuata masharti haya na alikuwa amevaa dela la kitambaa chepesi.

    Joto likapenya na kumpasha Jose B katika namna ya kushangaza.

    Akasahau mahesabu yote aliyopanga kumpigia Emmy. Shetani akabisha hodi, akapokelewa kama mfalme mwenye kuheshimiwa.

    Akawaomba wawili hawa akae kati yao, wakakubali kwa roho safi.

    Shetani akawaomba awafundishe kitu. Wakakubali. Shetani akachukua chaki akaanza kuwafundisha. Wawili hawa walikuwa werevu sana hawakusumbua katika kuuliza maswali ya itakuwaje baada ya hapa.

    Wakatenda walilofundishwa.

    Baada ya saa zima shetani alikuwa amewakimbia akawaacha wakijitambua.

    Aibu tupu. Wawili hawa walikuwa wamezini.

    Hakuna aliyeanza kumsemesha mwenzake.



    ***



    Emmy alirejea nyumbani majira ya saa mbili usiku, hakumkuta James. Na aliambiwa kuwa James hakuwa amerejea. Hali hii ilikuwa tofauti sana, James kuchelewa kurudi nyumbani bila kutoa taarifa yoyote.

    Emmy hakutaka kuhoji zaidi, akaingia chumbani kwake huku akijutia kitendo chake cha kuzini na Jose B, aliamini kuwa amejiongezea kizuizi kingine katika maisha yake. Alinyanyua simu yake na kumpigia Jose B.

    Simu ikachelewa kupokelewa lakini hatimaye ilipokelewa, kwa sauti tulivu ya Jose B.

    “Sam....” aliita Emmy, Jose B akaitika.

    Wakati Emmy anataka kuanza kuzungumza, mara mlango uligongwa, akaingia James akiwa katika taharuki fulani. Emmy akaligundua hilo.

    Akamkaribisha na kisha kumuuliza huku akikumbwa na hatia juu ya kitendo alichotoka kufanya na Jose B.

    “Una nini husband.”

    “Nimepata safari ya ghafla natakiwa kuondoka kuelekea Mwanza kuna tatizo la kifamilia.” Alijibu kwa ufupi.

    Kisha akajieleza kwa urefu, akaeleweka.

    Akamkabidhi Emmy majukumu kadhaa aliyoyaacha ya kiofisi. Emmy akayapokea.

    Asubuhi ya siku iliyofuata James akaondoka.

    Haikuwa safari ya kwenda Mwanza, alikuwa anaelekea machale yake yalipomtuma.

    James hakuamini hata kidogo juu ya misiba mitatu iliyotokea. Baba kuchomwa visu, mdogo wake kunyongwa na mama mkwe kuuwawa kwa sumu kali.

    James alirejesha akili yake miaka kadhaa, kisha akazikumbuka siri kadhaa alizokuwa anazihifadhi katika moyo wake. Akakumbuka kuwa si katika moyo wake tu bali pia katika moyo wa marehemu baba yake.

    Akapanga majina kadhaa ambayo aliamini kuwa yanaweza kuwa yanahusika katika mauaji haya. James aliamua kuchukua maamuzi upesi baada ya kuhisi kuwa hataweza kuishi tena ulimwenguni iwapo atapata taarifa ya kuuwawa kwa Emmy na mwanaye aliye katika tumbo lake.

    Kamwe asingeweza kumshirikisha juu ya siri hizo kwani huo ungekuwa mwanzo wa kuvuruga penzi lao na yeye kujiweka katika hatihati ya usalama wake hasahasa katika vyombo vya dola.

    James anaamua kuondoka kimyakimya huku akidanganya kuwa anaenda Mwanza kutatua matatizo ya kifamilia. James alikiri kimya kimya kuwa upendo wake kwa Emmy ulikuwa unakua kwa kasi kadri mimba inavyozidi kukomaa.

    Subira ya mtoto ilimfanya James awe mtumwa wa mapenzi. Alimfanyia Emmy kila kitu alichokuwa nahitaji. Hata pesa ambazo zilitumika kumpangishia Jose B nyumba zilikuwa za James.

    James alikuwa radhi kufanya lolote kwa ajili ya Emmy. Sasa aliamua kuwasaka wabaya wake kwa manufaa ya penzi na mtoto mtarajiwa.

    Katika orodha ndefu iliyopita katika kichwa cha James ilihitimishwa kwa jina ambalo halikuwa na uzito sana.

    Mamu. Hili lilikuwa jina la mwisho kabisa ambalo halikumtetemesha James, na aliamini kuwa huenda halipo tena katika ulimwengu huu.

    James akalikimbia jiji, safari ya kwenda kuwasaka anaohisi wanamuharibia mipango yake.

    Usiku wa manane James alikumbuka kitu, akakurupuka kutoka usingizini. Akaliendea kabati, akatoka na kibegi kidogo, kile alichokiwaza akakikuta. Kilikuwa kijitabu kidogo.

    Akakutana na namba ya simu. Akafanya mfanyo wa tabasamu, akaitwaa simu yake akajaribu kuipiga ile namba, badala ya kuita akapokea taarifa ya kuwa hana salio la kutosha katika simu yake. Alitamani kununua salio kutoka katika akaunti yake ya benki lakini akahisi ni kupoteza muda.

    Akaiona simu ya mkewe ambaye alikuwa anakoroma.

    Akatazama salio lilikuwepo la kutosha.

    Akaingiza zile namba katika simu ya mkewe kwa matarajio kwamba baadaye ataifuta ile namba na mkewe hatajua aliwasiliana na nani.

    Akaenda jikoni aweze kumsikia Jose B.

    Alipoanza kupiga mara likatokea jina. Jina katika simu ya mkewe.

    SAM WA PILI.......

    James akataharuki, akakata ile simu mara moja.

    Wasiwasi ukatanda, Sam wa Pili ndiye Jose B waukweli. Maajabu.

    Na ameanza lini kuwasiliana na mkewe, na alimjuaje? Ina maana mkewe anajua juu ya KIZUIZI ambacho kiliondoka na roho za Bibiana na Deo.

    James akahisi kijasho chembamba kikipenya katika uti wa mgongo wake.

    Kisha akagundua kuwa alikuwa anatetemeka.

    Hofu. Hofu kubwa ikatanda.

    KIZUNGUMKUTI........



    James akabaki katika sintofahamu, alitamani kumwamsha mkewe usiku huohuo aweze kumuuliza Sam wapili ni nani. Akakiendea chumba kwa mwendo mkali wa kisharishari.

    James hakuwahi kufikiri kuwa ipo siku anaweza kukumbwa na hasira za kuwaza kumpiga mwanamke lakini siku hiyo alijihisi yupo katika jinamizi la kufanya kitu kama hicho.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alipofungua mlango alikutanisha macho na kiwiliwili cha mkewe kikiwa hoi kwa usingizi. Akataka kumuamsha, mara akasita. Akajiuliza swali moja tu.

    Kipi kilikuwa bora kwake, mke na mtoto ama ukweli.

    Akatumia sekunde kadhaa kuchambua majibu haya. Alifikiria jinsi anavyojisikia amani kuwa na mwanamke kama Emmy, amani inayozidishwa na kitoto kinachorukaruka kwa furaha tumboni. James akakiri kuwa vitu vile vilikuwa vinakamilisha furaha yake na hakuwa tayari kuvipoteza.

    Akahamia upande wa pili. Akafikiria namna atakavyoukabili ukweli, ukweli asioufahamu juu ya ni kitu gani Emmy anajua juu ya Jose B.

    Vipi kama anajua kuhusu Kizuizi? Huu utakuwa mwanzo wa maelewano kupotea na kisha kuachana. James akaumizwa na fikra hizo za kuachana na Emmy.

    Akanywea, akaamua kuachana na ukweli, kizuizi cha kugombana na Emmy kikawa kimemzuia.

    Siku iliyofuata asubuhi alimuaga Emmy, wakakumbatiana kisha akatoweka.

    Kichwani akiwa amevurugwa kabisa bila kujua ni wapi mahali sahihi anataka kuelekea.



    ***



    Jose B hakuwa mtulivu katika kijiwe chake, kila mara aliwaza juu ya tukio lililotokea baina yake na Emmy, lilikuwa tukio ambalo hakulitegemea hata siku moja lakini sasa lilikuwa limetokea na aliburudika.

    Jose B akafumba macho na kumfikiria James. Akaanza kumuonea wivu kwa jinsi anavyofaidi kuchangia kitanda kila siku na msichana mrembo kama Emmy. Jose B akajiona kuwa na yeye alikuwa ana haki ya kufaidi ladha tamu kama ile.

    Jose B akajiona kama ni mjinga kwa kutaka kuchangia penzi na mwanaume mwenzake tena ambaye amefunga ndoa kabisa.

    Kwanini nisitafute msichana mwingine? Alijiuliza.

    Ni hapo alipogundua kuwa licha ya kuwa mwongeaji sana na mjuaji wa mengi hakuwa na uwezo wa kumsimamisha msichana kwa ajili ya kumtaka kimapenzi. Mara yake ya mwisho kuwa katika mahusiano alisaidiwa na rafiki yake ambaye ndiye alikuwa mzungumzaji mkuu.

    Sasa yupo jijini Dar na rafiki yule yupo Mwanza.

    Jose B akaona hali hiyo inamtia katika kizuizi.

    Ni kweli kuna wasichana wengi tu walikuwa wanamchekeachekea na yeye anawachekea, hakuzijua ishara za watoto wa mjini, akangoja msicha amfuate na kumwambia ‘Jose nakupenda....’ jambo ambalo aliendelea kulingoja bila mafanikio hadi siku anayokutana kimwili na Emmy bila kutarajia.

    Jose B akawa anataka tena mchezo huo ujirudie, lakini uzito wa mdomo wake angeanza vipi kumweleza mama yule mtarajiwa? Kamwe asingeweza.

    Siku mbili zikakatika bila hali ile kutoweka katika kichwa chake.

    Kila alipokuja msichana kutoa ama kuweka pesa Jose B alijikuta akimtamani. Tatizo hili likawa kero isiyostahimilika.

    Hakufanya mawasiliano zaidi na Emmy, alijaribu kufanya hivyo ili aweze kusahau lile tukio lakini kumbe kufanya vile ndio kujitesa zaidi.

    Uvumilivu ulipozidi. Akamtumia ujumbe mfupi wa kuhitaji kuonana naye.

    Emmy aliupokea ujumbe huu majira ya mchana akiwa jikoni anapika. Siku hii hakwenda kazini, ilikuwa siku yake ya mapumziko.

    Nyumbani alikuwa peke yake. Mdogo wake Jose na mdogo wake walikuwa wameenda shuleni.

    Uvivu wa Emmy kumfuata Jose B alipo, na pia hali ya mumewe kuwa safarini akaamua kumuita Jose B nyumbani.

    Jose B hakutegemea majibu yale.

    Majibu yale hayakumfurahisha, kikubwa cha kwanza alichowaza ni fumanizi ama kuabishwa mbele ya mume wa Emmy.

    Jose akajiuliza mara kadhaa kisha akamuona Emmy kama msichana mpumbavu anayetaka kuiharibu ndoa yake kirahisi namna ile.

    “Akiniumbua natibua kila kitu tena nasema kabisa alifanya mapenzi na ndugu yake...hawezi kunifanya mimi mjinga namna hii.” Aliapa Jose B.

    Baada ya saa zima, kijana mtanashati, ndani ya mavazi ya kisasa alitinga katika nyumba ya Emmy.

    Emmy ambaye bado alikuwa katika mapishi, alikuwa amevalia kanga moja pekee, kanga iliyoonyesha vyema maungo yake.

    Alikuwa ameumbika haswaa. Jose B akafanya kukohoa kidogo.

    “Sam....kuna nini?” Emmy aliuliza huku akionyesha waziwazi kuwa hajaupenda ujio wa Jose.

    “Tunaongea huku tukiwa tumesimama ama....”

    Emmy akashusha pumzi kwa nguvu kisha akamkaribisha Jose B sebuleni.

    Jose akajilazimisha kuizoea ile nyumba akachukua rimoti akabadilisha chaneli katika luninga.

    “Sam.....” Emmy akaita.

    Jose akamtazama kwa makini akiwa amejiandaa kumsikiliza.

    “Naomba tusahau yale yaliyotokea na ya siwe chanzo cha wewe kuwa karibu yangu zaidi ya awali. Nakuomba sana Sam, nina ndoa yangu na nimekulipa tayari ulichotaka. Au kuna kipi kingine Sam. Nakuomba Sam kuwa na utu kidogo, nyumba nimetimiza, nimekufungulia lile banda na kodi nimelipia ya mwaka mzima.....” Emmy akashindwa kuendelea kuongea midomo ikawa inamtetemeka, na machozi yakaanza kumtoka baada ya kugundua kuwa ndoa yake ipo hatarini.

    Akanyanyua upande wa kanga aweze kujifuta machozi, akiwa amesahau kuwa amevaa hiyo kanga pekee.

    Jicho la Jose B likakutana na paja lililonona. Midadi ikampanda.

    Hakuwa tayari kuikosa ladha aliyoonjeshwa.

    “Emmy, kwani nimewahi kuitikisa ndoa yako.”

    “Hapana, sasa hapa umekuja kufanya nini?”

    “Ni wewe umeniita hapa....”

    “Baada ya wewe kuhitaji kuonana na mimi.” Emmy alijibu kwa hasira.

    Jose B akiwa katika matamanio alijikuta anapata ujasiri. Akazungumza.

    “Nina kesi na wewe Emmy. Kubwa kuliko ya awali.”

    “Kesi?”

    “Na malipo yake ni ya kawaida tu, kwa sasa sio nyumba tena. Wala sihitaji banda jingine la kutoa na kuweka pesa. Kwa kifupi sihitaji chochote kitakachokufanya uwaze mara mbili.”

    “Sam acha kunichanganya tafadhali.”

    “Ninahitaji ulichonipa siku ile nyumbani kwangu.”

    “Sam unasemaje? Sam....unasema...sikiliza, naomba usimame na uiache nyumba hii katika utulivu ulioukuta awali.”

    Jose B akasimama, akaanza kutoka nje, akitembea kwa majivuno.

    Emmy alikuwa ameiva kwa hasira, alijisikia msaliti mkubwa kwa jambo alilofanya na Jose B ambaye alimtambua kwa jina la Sam wa pili.

    Jose B alipoufikia mlango aligeuka kisha akakiruhusu kinywa chake kuzungumza.

    “Nadhani unaikumbuka vizuri biashara yetu ilikuwa inahusiana na wewe kumsaliti Jose kwa mwanaume mwingine huko uswazi Zamzam guest house. Hilo tumelimaliza, lakini kumbe yule mwanaume anaitwa Lameck....na kama hiyo haitoshi ni baba yako mdogo. Emmy una hatari wewe. Yaani na baba mdogo? Ujue hata siamini. Ila sawa ni maamuzi, kama uliweza kumpa baba mdogo Lameck ambaye mnafahamiana na mnachangia damu, sijui kinakushinda nini kunipa mimi mtu usiyenifahamu. Lakini bado unaweza kuamua, aidha niiuze siri hii kwa jamaa mwingine ama utimize nilichokuomba kistaarabu.

    Halafu kuna jambo pia nimesahau, umemsaliti James kwa kijana fulani hivi juzi kati...anaitwa Sam wa pili. Biashara nyingine hiyo tunaweza pia kuizungumza ukipenda. Au la nitaiuza mamilioni mengi.

    Usiku mwema mama kijacho...” Jose B alimaliza huku akitabasamu.

    Emmy alitamani kumzuia asiondoke lakini akagundua kuwa miguu yake ilikuwa haina nguvu tena. Alijaribu kusema neno, mdomo ukawa mzito.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Geti likasikika likibamizwa kwa nguvu, Jose B hakuwa pale tena.

    Mshikemshike.



     Miji miwili katika mikoa tofauti ilikuwa imebeba viumbe wawili wa jinsia tofauti kila mmoja na harakati zake.

    Jiji la la Mwanza lilikuwa limemtunza mwanaume jasiri ambaye alikuwa ameamua kuzirudia enzi zake kwa ajili ya kuokoa kile alichokuwa anakipenda kwa dhati.

    Huyu alikuwa ni James.

    Hakumtaarifu mtu yeyote juu ya uwepo wake katika jiji la Mwanza.

    James alikuwa anafanya msako wa kimya kimya. Harufu ya kuua ilinukia katika pua zake.

    Aliitamani roho moja baada ya nyingine ili kuuficha ukweli.

    James alihitaji kumkabili Jose B ambane ili auseme ukweli wote ambao ameuropoka kwa mkewe kisha amuue ili kuondoa ushahidi.

    James aliamini kuwa siri ambayo mke wake anaimiliki haitakamilika bila kuwa na ushahidi. Na kama hapatakuwa na ushahidi atakuwa na uwezo wa kumruka Jose B na kudai kuwa alikuwa anamsingizia.

    Na endapo Jose B atatafutwa ili aweze kutoa ushahidi, mwili wake utakuwa ukiendelea kuoza katika aidha ardhi ama utakuwa umeliwa na samaki. Inategemeana kifo atakachokufa.

    Uamuzi huu James akauona kuwa ni uamuzi sahihi zaidi.

    Sasa yupo katika jiji la Mwanza kumsaka Jose B waukweli aweze kuiondoa roho hii inayoushikilia ukweli.

    Jiji la Dar es salaam, lilikuwa limetembelewa na mwanamke wa makamo, akiwa na pete katika kidole chake cha shahada.

    Hasira yake ilikuwa imepungua kwa kiasi fulani japo alikuwa hajaridhika.

    Hii ilikuwa safari yake kubwa ya mwisho katika mlolongo wa safari zake za siri tangu alipodhaniwa kuwa ni mfu.

    Hakuna aliyedhania roho hii ilikuwa inaishi, japo suala la kifo chake lilibakia kuwa katika mabano. Hakuna aliyeweza kukielezea.

    Hata baba yake alibaki katika sintofahamu. Akishindwa kumtupia mtu yeyote lawama juu ya kifo hicho. Akaufuga uchungu wake, uchungu uliokuwa unamtesa.

    Hatimaye ule uchungu ukamkondesha kisha ukazalisha magonjwa ya ajabu ajabu katika mwili wake. Akaiaga dunia huku akiwa haamini kama mwanaye amekufa. Lakini hakuyasema hadharani.

    Akazikwa huku ile roho aliyoamini kuwa bado inaishi ikibaki duniani.

    Na sasa roho hii ipo katika jiji la Dar es salaam. Roho yenye chuki kali. Chuki ya miaka kadhaa iliyopita, chuki kali, na aliamini kuwa yu hai ili aweze kufanya mambo mawili tu. Kulipa kisasi na kuuweka ukweli wazi kwa kila mwenye mashaka.

    Kisasi cha damu ndiyo kisasi pekee alichoamini kuwa ni sahihi kwa majina hayo.

    Roho hii ya mwanamke iliyojihifadhi katika mwili dhaifu ilikuwa katika chumba namba kumi na nane katika nyumba ya kulala wageni pembeni kidogo ya jiji.

    Majina kadhaa yalipangana katika kichwa chake.

    Kindo, Keto na Kakele.

    Aliwahitaji kwa hali na mali.

    Na aliamini kuwa kwa kumpata mmoja wao lazima atampata na mwingine, kisha huyo mwingine naye lazima atamtaja mwenzake. Kazi ikapangwa kuanza rasmi siku inayofuata.

    Katika jiji hilohilo la Dar es salaam.



    ***



    Emmy alipatwa na maumivu ya kichwa, makali kuliko yoyote ambayo aliwahi kuyapata katika maisha yake. Licha ya kichwa chake kumiliki elimu ya chuo kikuu kwa hili tatizo aliamini elimu ya darasani sio tiba ya kila tatizo.

    Hali ilikuwa tete. Baada ya kuhimili milima na mabonde ya kuvikwepa vishawishi vya wanaume walaghai katika ngazi mbalimbali akiwa shuleni hadi kazini, mwisho akaangukia kwa baba yake mdogo, Lameck, akafuatia mume wake wa ndoa James, sasa yupo katika sintofahamu ya nini kimemsibu hadi akajirahisisha kwa Jose B wa ukweli ambaye anatambulika kama Sam wapili.

    Licha ya kujirahisisha sasa kuna mzigo mwingine wa hatari.

    Jose B anataka apewe penzi kama malipo ya kuificha siri ya Emmy kufanya uzinifu na baba yake mdogo.

    Emmy aliliona sharti hili kama dharau na kejeli iliyopitiliza akamtolea nje mara moja Jose B kisha akamtimua nyumbani kwake. Lakini maneno makali kutoka katika kinywa kipana cha Jose B yakamwachia simanzi na kumrejesha katika kushika makali huku mpini wa kisu ukikamatwa ipasavyo na Jose B.

    Maamuzi yakawa mawili tu, aidha avutane na Jose aliyekamata mpini jambo ambalo lingemletea jeraha na kumwacha Jose B akiwa mshindi, ama la amwachie Jose B ushindi mapema kwa kukubaliana na masharti hayo. Emmy alijilazimisha kuamini kuwa hii ni ndoto anaota na akishaamka itasahaulika na kuondoka zake. Lakini la haikuwa ndoto. Lilikuwa tukio halisi. Na Jose B alikuwa ametamka maneno yale akiwa hana utani hata kidogo.

    Emmy akamkumbuka marehemu mama yake, akatamani angekuwa hai angemweleza ukweli wote na angeweza kupata ushauri wa kiutu uzima. Hakuonekana mtu mwingine ambaye angeweza kumpatia ushauri wa kumwokoa katika hili, alijaribu kuwawaza marafiki mmoja baada ya mwingine akawachambua hakupata hata mmoja wa kumshirikisha.

    Aliamini kwa kufanya hivyo angejichafulia jina lake mapema na ungekuwa mwanzo wa kufanana na yule mwanamke mpumbavu anayeivunja nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe.

    Emmy hakuwa tayari kuwa mwanamke mpumbavu.



    Akayafumba macho yake kwa kutumia viganja vya mikono yake. Alipoyaacha wazi akakutana na picha kubwa ukutani. James na msichana fulani wakiwa wanacheka kwa furaha, James alikuwa amevaa suti na mwanamke alikuwa amevaa shela.

    Ilikuwa siku ya ndoa yao takatifu.

    Emmy akaona aibu. Akamtazama James kama mwanaume jasiri tena mvumilivu na mwerevu asiyekuwa na papara katika maisha yake, na pia anatimiza kile ambacho anakuwa ameahidi.

    James alivumilia kwa miaka kadhaa bila kufanya zinaa na Emmy, alimfanyia kila kitu na wala upendo haukupungua hadi wamefunga ndoa, akaishia kupewa bikra feki.

    Dharau ya hali ya juu.

    Emmy alikiri kimya kimya kuwa ana tabia mbaya tena anafaa kuitwa malaya aliyekubuhu lakini amevikwa vazi la utukufu.

    Emmy akaamua moja, kulipigania penzi lake ili asiwe mwanamke mpumbavu ambaye jamii itamdharau kila kukicha.

    Akaitwaa simu yake akabofya jina alilolinitaji. Akaanza kungoja simu iweze kuita.

    Jose B aliondoka na usafiri wa bajaji, iliyomuwahisha nyumbani kwake. Alijihisi anaonewa sana kwa kunyimwa kile alichokihitaji.

    Jose aliamini kabisa kuwa Emmy ana dharau tena dharau iliyopitiliza. Jose B akahisi ni haki yake kupewa kila anachohitaji kwa kuwa tu anamiliki siri.

    Alikifikia kitanda chake, akakirukia bila hata kuvua viatu. Akagalagala kidogo na kujihisi ameaibishwa sana kwa kukataliwa kwake.

    Simu ilimkatisha vurugu alizokuwa anafanya kitandani pale.

    Akaitazama. Alikuwa Emmy.

    Akaipokea upesiupesi. Hakusema neno akamsikiliza Emmy.

    “Sam...nisamehe kwa yaliyotokea rafiki yangu. Ni hasira tu na sijui zilitoka wapi. Sikia

    Sam sahau yaliyotokea. Nakuomba unisikilize....”

    Akiwa anaendelea kuongea mara simu ilikatwa. Akajaribu kupiga ikakatwa tena, mara nne hali hiyo hiyo.

    Emmy akapagawa Jose B akawa anacheka kwa kutambua ni kiasi gani alikuwa anamchanganya mtoto huyu wa kike.

    Emmy alipoona jitihada za kupiga simu zinashindikana.

    Akafanya kosa kubwa kupindukia.

    Kosa la kumtumia ujumbe Jose B. Ujumbe wa kukubaliana naye katika kuwa mtumwa wa ngono lakini kwa malipo ya kumtunzia siri yake.Katika ujumbe huo majina ya Lameck na

    James yaliambatanishwa.

    Emmy hakujua madhara ya ujumbe.

    Ujumbe ni ushahidi tosha unaoweza kukufunga.

    Jose B aliupokea kwa shangwe ushindi ule.

    Akajitwalia medali ya dhahabu na mkongojo wa utawala. Akaanza kuiongoza nchi ya Emmy kadri alivyotaka.

    Emmy akawa mtumwa wa ngono kwa Jose B.

    Walau mara moja kwa juma. Hayo yakawa makubaliano ambayo yangedumu hadi mimba ikifikisha miezi saba.

    Makubaliano ambayo yalitakiwa kuanza rasmi. Siku mbili baadaye.

    Emmy hakuwa na ujanja akakubaliana na Jose B.

    Siku ya miadi ilifika, siku iliyomfanya Emmy ajitambue kama msichana changudoa ambaye yupo katika ndoa. Alikuwa ameomba ruhusa kazini siku hiyo maalumu kwa ajili ya kujiuza kwa kijana machachari Jose B waukweli.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akiwa katika kuwaza na kuwazua juu ya jambo analoenda kulifanya alijikuta anatokwa machozi na wala hakuweza kumsikia mtu aliyeingia uani baada ya kulipita geti akiwa amegonga kwa muda mrefu sana.

    Emmy aliyasugua macho yake ili kuyaweka sawa na kuyapa mwangaza. Akakutana na mwanaume mbele yake. Alikuwa anatabasamu.

    Emmy badala ya kulijibu tabasamu lile akapigwa na butwaa.

    “Lameck.....” akaita, mwanaume akasogea karibu.

    “Nambie Mama James..”

    “Sijui hata la kusema lakini afadhali kama umekuja.”

    “Nami pia niseme kuwa afadhali nimekukuta. Huenda nakuhitaji zaidi kuliko wewe unavyonihitaji.” Lameck aliketi baada ya kuhakikishiwa kuwa James alikuwa safarini.

    Lameck hakutaka kupoteza muda. Wala kuishusha hali aliyokuwanayo.

    Emmy akawa mtulivu kumsikiliza bwana huyu. Mada ikaanza rasmi.

    Lameck akaelezea utata wake juu ya mimba aliyobeba Emmy. Wasiwasi huu ukamshangaza Emmy.

    “Una maana gani sasa. Nina mimba mimi wewe wasiwasi wa nini Lameck.”

    “Sio mimba ya James hii...” Lameck akasema huku akimtazama Emmy usoni.

    Emmy akaduwaa. Lameck hakutetereka akajieleza juu ya kukutana kwao kimapenzi mara ya kwanza na kisha mara ya pili.

    “Kile kichefuchefu ulichosema, mimba ilikuwa tayari imeingia. Sasa vipi useme kuwa ni ya James.” Lameck akasisitiza.

    Hapa Emmy akajisikia kupasuka vipandevipande kisha dunia imsahau. Maisha yake yakajawa na changamoto lukuki.

    Akapingana na Lameck kwa ukali mkubwa, akatoa matusi jambo ambalo hakuwahi kulifanya hapo awali. Matusi haya yakamkera mwanajeshi huyu aliyepoteza kizazi katika nchi ya Sudani.

    Mwanajeshi akasimama imara. Hakutaka kumdhuru Emmy. Lakini alikereka.

    “Emmy nisikilize...huyo mtoto uliyembeba ni damu yangu. Tena damu yangu halali. Usijidanganye kuwa ni wa James. Ni vyema tukae mimi na wewe tuzungumze namna ya kufanya.”

    “Yaani mimi nikae na wewe tuzungumze juu ya mimba niliyoipata ndani hya ndoa,bamdogo umechanganyikiwa?? Jeshi limekuchanganya baba yangu.....hivi kumbe walikuwa sahihi waliosema ukitaka kuwa mjeshi lazima akili zako zipunguzwe.” Emmy alikaripia. Huku akitetemeka. Lameck alikuwa mkimya akiwa wima, Emmy akaendelea kuzungumza kwa jazba, “wewe ni mjinga tena mpumbavu sana nasema. Mjinga wa mwisho kabisa...unikome nasema Lameck unikome nisije nikakushushia heshima yako.”

    Lameck alimtazama huku hasira ikimkabili na kujikuta akitokwa na neno baya kabisa lisilopaswa kutamkwa hasahasa ukiwa na hasira.

    “Emiliana Emiliana...TUTAONA NANI MJANJA...” Alimaliza akaondoka.

    Emmy akasonya. Alikuwa ametaharuki.

    Wakati Lameck anatoweka kwa kupitia getini akiwa ametaharuki. Majira ya saa kumi na moja jioni simu ya Emmy ikaita. Alikuwa Sam wapili.

    Akaipokea kwa shingo upande. Jose B akamuita nyumbani.

    Emmy akakubali. Alipomaliza kuzungumza na Jose b.

    Akampigia simu James na kumwambia kuwa anatoka anaelekea kwa rafiki yake.

    James akatoa ruhusa akiwa jijini Mwanza. Ruhusa ya mkewe kwenda kumgawia mwili, Jose B waukweli ambaye James alikuwa ameenda kumsaka jijini Mwanza.

    Emmy akajiandaa akatoka majira ya saa kumi na mbili.

    Aliondoka kwa kutumia taksi tofauti tofauti tatu. Akafika nyumbani kwa Jose B waukweli.



    Majira ya saa tatu usiku. Kiwiliwili kimoja kilitangulia katika nyumba ya James. Kisha viwiliwili vingine viwili vikafuatia kwa nyuma.

    Mlango ukagongwa kwa muda mrefu. Hatimaye ukafunguliwa.

    Kiwiliwili kimoja kikatangulia ndani kisha kikafuatiwa na vile vingine. Aliyefungua mlango alikuwa amepigwa kabali ya nguvu na aliongoza njia kuelekea ndani.

    Mchuano huu ulienda kimya kimya.

    Hakuna kelele iliyopigwa.

    Emmy aliporejea majira ya saa nne usiku alikuta geti likiwa limerudishiwa.

    Akasukuma likafunguka.

    Akaanza kugomba kuanzia nje huku akielekea ndani, hasira kali za kuchezewa mwili wake na Jose B zilikuwa zinamkabili.

    Akaamua kuzihamishia kwa yeyote aliyeliacha geti lile wazi.

    Alipofika ndani akagundua kuwa alikuwa anagombezana na hewa. Hakuna aliyemjibu.

    “Haya matoto yamelala wakati geti lipo wazi..naua mtu leo.” Akawatukania mama zao kikabila huku akiifunga vyema kanga kiunoni, akaenda mbiombio katika vyumba vyao, akafungua huku akiporomosha matusi mazito. Kimya akakutana na kitanda tupu.

    “Ina maana wameanza kwenda disko hawa watoto.” Alijiuliza huku akimuwazia mdogo wake James kama kiongozi wa mambo hayo. Aliamini kabisa kuwa binamu yake kamwe asingeweza kuwa na mambo hayo.

    Emmy mwenye hasira akaingia jikoni.

    Huko ndipo aliposhindwa kuvumilia. Ujasiri pembeni akalainika, akaanguka chini.

    Lakini hakuzimia.

    Alikutana na mwili wa shemeji yake (mdogo wake James) ukiwa umefungwa kamba zilizokazwa haswa. Lakini alikuwa anapumua.

    Binamu yake atakuwa wapi? Lilikuwa swali la kwanza.

    Baada ya nguvu kumrejea kidogo akausogelea ule mwili.

    Akakutana na karatasi kubwa kiasi ikiwa imeandikwa kwa kalamu ya wino mzito.

    “TUTAONA NANI MJANJA”

    “Mungu wangu...Lameck Lameck.....” Emmy alipatwa na nguvu akatokwa maneno hayo.

    Aliyakumbuka kuwa aliwahi kuyasikia mahali, na yalitamkwa na Lameck masaa kadhaa yaliyopita baada ya kukataliwa juu ya suala la mimba anayobeba.

    Emmy akataharuki zaidi alipomkosa binamu yake. Akamuweka Lameck katika hatia ya kutenda yale. Akachukua simu aweze kutoa taarifa polisi. Akasita.

    Kama akitoa taarifa kuhusu Lameck, katika ushahidi lazima aseme nini kilitokea hadi wakakwazana na baba yake mdogo. Na kisha kufikia hatua ya kuambiana maneno yale makali.

    Emmy akagaili, akampigia simu jirani yake. Kisha baada ya jirani kufika akamweleza kilichojiri na kumwomba awasiliane na mume wake jijini Mwanza.

    Ilikuwa sasa sita usiku James alipoona namba ya mkewe ikipiga.

    Akapuuzia simu ya kwanza, mara ikaita tena. Haukuwa utaratibu wa Emmy kupiga simu mara mbili kwa mumewe. Jambo hili likamfanya James ahisi kuna tatizo.

    Akakaa kitako akapokea.

    Hakuwa Emmy ilikuwa sauti ya kiume.



     “Mungu wangu...Lameck Lameck.....” Emmy alipatwa na nguvu akatokwa maneno hayo.

    Aliyakumbuka kuwa aliwahi kuyasikia mahali, na yalitamkwa na Lameck masaa kadhaa yaliyopita baada ya kukataliwa juu ya suala la mimba anayobeba.

    Emmy akataharuki zaidi alipomkosa binamu yake. Akamuweka Lameck katika hatia ya kutenda yale. Akachukua simu aweze kutoa taarifa polisi. Akasita.

    Kama akitoa taarifa kuhusu Lameckm, katika ushahidi lazima aseme nini kilitokea hadi wakakwazana na baba yake mdogo. Na kisha kufikia hatua ya kuambiana maneno yale makali.

    Emmy akagaili, akampigia simu jirani yake. Kisha baada ya jirani kufika akamweleza kilichojiri na kumwomba awasiliane na mume wake jijini Mwanza.

    Ilikuwa sasa sita usiku James alipoona namba ya mkewe ikipiga.

    Akapuuzia simu ya kwanza, mara ikaita tena. Haukuwa utaratibu wa Emmy kupiga simu mara mbili kwa mumewe. Jambo hili likamfanya James ahisi kuna tatizo.

    Akakaa kitako akapokea.

    Hakuwa Emmy ilikuwa sauti ya kiume.



    Mchomo wa wivu ukapenya katika masikio ya James kisha ukaunguza moyo wake.

    Akahisi Emmy ameamua kuwa na mwanaume mwingine kama ishara ya kulipa kisasi baada ya kuambiwa siri zote za James.

    Lakini haikuwa hivyo. Kulikuwa na tatizo. Mpigaji ambaye hakukumbuka kujitambulisha alisema kila kitu juu ya kilichotokea.

    Kisha akalikumbuka neno “TUTAONA NANI MJANJA”

    Jose B akakata simu baada ya kusikia maelezo hayo. Neno la mwisho likamchanganya. Ni kama halikuwa neno analolisikia kwa mara ya kwanza. Alikuwa amewahi kulisikia hapo kabla.

    Hofu ikatanda. Akajaribu bahati yake kwa kuwapigia wahusika wa tiketi za ndege anaofahamiana nao.

    Pesa ikazungumza. Tiketi ikapatikana kwa gharama za juu sana.

    James ambaye alikuwa ameweka mipango yake madhubuti ya kuishambulia familia ya Jose B ili kijana huyo aweze kuonekana kiwepesi. Mipango ambayo iliangukia kwa kumtoa muhanga mama yake Jose B ambaye anapatikana kwa wepesi zaidi ikaishia hapohapo.

    Ikawa ngekewa kwa roho ya mama Jose B asiyekuwa na hatia na asiyejua lolote kuhusu mchezo unaoendelea kutanuka kwa kasi.

    Siku iliyofuata mapema sana. James anayekaribia kuchanganyikiwa alikwea ndege. Katika safari nzima aliyawaza maneno yaliyoachwa na mtekaji katika nyumba yake.

    “TUTAONA NANI MJANJA.”



    *****



    Majira ya saa tano asubuhi, taksi ilipiga honi lakini haikupishwa, umati ulikuwa mkubwa ukimsikiliza Gloria. Fahamu zilikuwa zimemrudia. Vyombo vya dola vilikuwa makini kunukuu kila neno lililosemwa na Grolia.

    “Walikuwa wamejifunika usoni, sikumtambua hata mmoja. Lakini kuna mmoja alikuwa ni mwanamke. Walimpiga sana Grace kisha wakaondoka naye. Nilipojaribu kuleta vurugu walinipiga kisha wakanifunga kamba.” Alijieleza huku akibubujikwa na machozi.

    Alikuwa anaelezea mkasa uliotokea usiku uliopita.

    James aliamua kushuka katika ile taksi baada ya kuona uwezekano wa kupishwa haupo. Hima hima akaliendea kundi lililokuwa limemzunguka Gloria, pupa zikamponza akaanza kusukuma watu wasiofahamu uhusika wake katika tukio lile.

    Papara zikamtokea puani, kwanza akatukanwa matusi ya nguoni. Kisha akadhalilishwa kwa kukutana na vibao vikali kutoka kwa polisi waliovaa kiraia.

    Kabla hajajitetea zaidi ndipo akaokolewa na mkewe aliyekuwa hajitambui kuwa amevaa kanga moja inayomfanya awe mfano wa kituko flani.

    Umati ukasambaratishwa baada ya Gloria na familia yake kuhitajika kituoni kwa ajili ya mahojiano zaidi.

    Emmy alikana vikali kuwa na ubaya wowote na mtu. Na hakuewa na la kusema juu ya maneno yaliyoandikwa katika kile kikaratasi. Maneno yake ya kukana kuhusu kujua lolote juu ya maandishi yale yalimfanya amfikirie Lameck kama muhusika. Akataka kumtaja lakini akapatwa na hofu juu ya usalama wa ndoa yake. Aliamini kuwa kwa kumtaja tu mwanaume huyo mjeshi, lazima angechukuliwa kituoni kwa ajili ya kutoa maelezo yake juu ya tuhuma hizo.

    Emmy akaamua kukaa kimya.

    James naye aliruka maili mia juu ya kuwa na kisasi na jamii yoyote ile. Na aliruka zaidi juu ya yale maneno akakiri kuwa ilikuwa mara ya kwanza kuyasikia.

    Wakati akijibu haya alikuwa na wasiwasi mkubwa sana juu ya mwanamke wa miaka kadhaa nyuma. Alikitazama kidole chake cha shahada kwa makini, akaiona alama ikimdhihaki. Alama ya pete ambayo kamwe isingeweza kutoka kutokana na jinsi ilivyotolewa kwa kulazimisha.

    Akahisi huenda kuna mzimu unafanya kisasi badala ya Mariam.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Imani yake ikameguka kiasi fulani na kuamini katika ulimwengu huo wa giza.

    Kama ni mizimu nimekwisha? James katika dimbwi la mawazo alijikuta akinong’ona, sauti ikatoka. Ilikuwa bahati kuwa afande mmoja alikuwa anaongea katika simu kwa sauti ya juu.

    Hakuna aliyeisikia kauli hii.

    Mahojiano yakamalizika. Dola ikaingia kazini kufuatilia ni wapi Grace amepelekwa.

    Sala za James na Emmy zilikuwa zikihangaika kumfikia Mungu wanayemuamini juu ya uzima wa Grace.

    Hakuna aliyekuwa tayari kupokea taarifa juu ya umauti wa mtoto huyu asiyekuwa na hatia. Emmy akiwa na James pamoja na Grolia na wauguzi kadhaa walioandama pamoja kwa ajili ya kumfikisha Grolia hospitali kwa ajili ya vipimo zaidi, ilisikika sauti kwa mbali ikiita.

    “Emmy.....James....” James akasikia, Emmy hakuwa amesikia.

    “Bamdogo yulee.” James akasema, Emmy akasikia akageuka.

    Mapigo ya moyo yakabadili mwendo wake baada ya kumuona Lameck akija hima. Hofu ikatanda. Akaamini siku ya kuumbuka imefika.

    Alitamani kukimbia, lakini akajizuia asije akazua hata yasiyokuwepo. Akajikaza.

    James hakutilia maanani kumtazama Emmy usoni. Fursa hiyo ilimtosha Emmy kujilazimisha kurejea katika hali ya kawaida.

    Lameck akafika. Akawasalimia wote wawili.

    Emmy akajibu bila kumtazama Lameck usoni. James akamchangamkia mwanajeshi yule ambaye pia ni kijana mwenzake.

    Kisha akamuelezea kwa kifupi juu ya mkasa uliotokea. Lameck akasikitika sana, Emmy akanung’unika moyoni kwani aliamini ni yeye ambaye amemteka ama amemuua Grace.

    Cha ajabu anajifanya kusikitika mbele yake.

    Emmy akakumbwa na hasira za ajabu akawa anatetemeka. Ile siri aliyoificha ikawa inamtesa. Kidogo aufungue mdomo wake na kumtuhumu Lameck lakini akasita baada ya kukumbuka kuwa James atapata walakini wa tuhuma hizi na akiamua kuchunguza basi ndoa inavunjika.

    Emmy akajizuia kwa kuichukua simu yake na kujikita katika kubofya ilimradi tu asitazamane na Lameck.

    “Emmy...we Emmy” James aliita baada ya Emmy kuonekana amejikita na mambo mengine mbali kabisa na mazungumzo hayo.

    “Bee...samahani..nilikuwa aaah...”

    “Ba’mdogo anakuuliza ...” James alizungumza huku akiwa amekereka. James alisifika kwa kuwaheshimu ndugu wa mwanamke na hakupenda Emmy awakosee heshima hata kidogo.

    Lameck alikuwa ndugu yake na Emmy. Baba mdogo.

    “Eti Emmy...wewe umerejea nyumbani ilikuwa saa ngapi? Na hukuona alama za tairi za gari ama....”

    “Sijaona chochote na sikumbuki nilirudi saa ngapi.” Alijibu kwa jeuri, James na Lameck wakatazamana kwa mshangao. James akapandwa na jazba lakini Lameck akawa wa kwanza kumtetea Emmy kuwa amevurugwa na tukio hilo. James akamuelewa.



    Safari ya kuelekea hospitali.



    ***



    James alitangulizana na mgonjwa hadi ndani huku nyuma akiwaacha Lameck na mwanaye Emmy ambaye ni mjamzito.

    Hakuna aliyemsemesha mwenzake. Emmy alikuwa ameuvuta mdomo kwa hasira.

    “Hivi Emmy unadhani haya mambo ukileta hasira zako za jana yataisha kwa usalama. Wewe kuwa mtulivu tuzungumze tujue tunayamaliza vipi. Ona sasa unataka mume wako ajue mapema kuwa nina tofauti na wewe...” Lameck alizungumza huku akitazama mbele kama vile hazungumzi na Emmy ambaye yupo pembeni yake.

    Emmy hakujibu kitu, Lameck akaendelea, “Sikia kwa sasa nakusihi uwe mtulivu wakati tunatafuta hatma ya Grace....lakini Emmy au kuna mtu ulikwazana naye nd’o analipiza kisasi...” hapa Emmy akageuka na kumtazama Lameck.

    Sasa hasira zikakosa subira. Akarusha kiganja katika shavu la Lameck.

    Kati ya vitu ambavyo wanajeshi hufuzwa katika kambi zao ni kutomwamini adui yako na pia kumtilia mashaka mwenzako kwa asilimia kadhaa. Lameck akafanikiwa kukwepa kile kibao.

    Emmy akapepesuka, Lameck akawahi kumdaka.

    Mshangao ukamkumba Lameck, hakuamini kama Emmy anaweza kufanya kitendo kile cha kumwaibisha.

    Emmy baada ya kusimama imara alianza kulia kana kwamba amefiwa. Emmy hakuwa na ujanja wa kuzikabili hasira zake zaidi ya kuangua kilio. Ikawa kazi ya Lameck kumbembeleza.

    James alipotoka katika huduma iliyompeleka alimkuta Emmy akiwa amenyamaza tayari.

    Safari ya kurejea nyumbani.

    Polisi wakiwa wanaendelea na upelelezi wao juu ya utekaji huu wa kushtukiza.

    Chumbani hapakuwa na la kuongeleka. James kama baba mwenya nyumba alilazimika kujikita katika tukio hili zaidi ya mkewe ilimradi tu aitafute ile furaha ambayo tayari ilikuwa imetoweka kwa mkewe.

    James aliamini kwa asilimia zote kuwa ni yeye alikuwa chanzo cha haya yote yanayotokea kuanzia kifo cha baba yake, mdogo wake, na mama mkwe na sasa binamu yake mkewe alikuwa ametekwa bila sababu kuwekwa wazi.

    James aliumiza kichwa na kujihisi kuwa anadhalilishwa kwa kiasi kikubwa na huyo adui yake ambaye hadi wakati huo alikuwa hajajiweka wazi. Alikuwa anashambulia kimya kimya.

    Inamaana atakuwa ni Mariam? James alijiuliza tena kwa mara nyingine.

    “Mariam amefanyaje?” Emmy aliuliza.

    James akajishtukia kuwa alizungumza badala ya kuwaza.

    Hakujibu lolote. Emmy naye hakuuliza tena. Walikuwa wameelekezeana migongo.

    Usiku ukapita. Grace akiwa hajapatikana.



    ***



    Taarifa za vifo vya Keto na Kakele vilimshangaza sana msichana huyu ambaye aliamini kuwa katika orodha hiyo ndipo atakapoupata ukweli kabla ya kumkabili Kindo.

    Wasiwasi ukatanda baada ya kuambiwa kuwa vifo vyao vilitokea katika juma moja lakini siku tofauti.

    Kakele akiuwawa kwa risasi na Keto akichomwa visu katika mwili wake.

    Katika kufuatilia zaidi tarehe za matukio hayo, akapata jambo jingine jipya kuwa vifo hivyo vilitokea kabla Kindo hajafunga ndoa.

    KIZUIZI.

    Ina maana Keto na Kakele walidhurumiwa na Kindo ama. Alijiuliza yule mwanamke ambaye alijihisi ni mfu anayeishi kutokana na majanga aliyopitia, lakini yu hai sasa na yupo jijini Dar es salaam.

    Wazo la kumvaa Kindo moja kwa moja akaliona kama ni la hatari sana na pia litalifanya zoezi lake kuwa gumu sana.

    Akaamua kuanzia mbali ilimradi tu amnyanyase Kindo mpaka hatua ya mwisho.

    “Atanitambua mimi ni nani, na pia atajulikana nani mjanja kati ya mjeruhi na mjeruhiwa.” Aliapa mwanamke huyu ambaye alikuwa na majeraha kadhaa mwilini mwake.

    Usiku wa siku hiyo akiwa na vijana wake kadhaa ambao alisafiri nao kutoka mbali aliingia katika kupigania ukweli uliofichika.

    Siku kadhaa za kuwa katika jiji la Dar es salaam tayari alikuwa amepeleleza mambo kadhaa na alikuwa amepafahamu nyumbani kwa Kindo na mengine mawili matatu.

    Usiku wa siku hiyo hakufanya makosa.

    Akaivamia nyumba ya Kindo ambaye anajiita James.

    Akamteka Grace.

    Sasa amezua kizungumkuti, Emmy anahisi ni Lameck amemteka Grace.

    James bado hajawa na uhakika ni nani amemteka Grace na hataki kuamini kabisa kama Mariam anaweza kufanya hivyo.



    Upelelezi haukuwa na lolote jipya. Mkono wa dola ulitapatapa huku na huku bila mafanikio. Bado Grace hakupatikana.

    James akajiona kuwa yeye ni bwege mkubwa. Anamuhisi mtu fulani kuwa yawezekana anaweza kuwa anahusika na utekeji huu lakini anapuuzia na kukaa kimya akiwangoja polisi wasioisha kusema neno lao la siku zote ‘upelelezi unaendelea.’

    James akatamani kumshirikisha Emmy juu ya hisia zake. Lakini akahofia maswali kadhaa kutoka kwa Emmy juu ya huyo Mariam.

    Akiniuliza tulikuwa na mahusiano gani na kwanini aandike kuwa ‘tutaona nani mjanja’ nitajibu nini? Maswali haya ambayo majibu yake ni magumu sana yakazua kizuizi kwa James kuthubutu kufanya jambo lile.

    Emmy naye alikuwa na tatizo kama la James. Alijua kitu lakini alihofia maswali kutoka kwa mumewe ambaye alimuamini kwa asilimia mia kuwa alikuwa yu mtakatifu pasi na hatia.

    Wote wakawa wanawaziana mazuri lakini wakikumbwa na kizingiti cha kuuachia ukweli huru.

    Sintofahamu ikawazunguka.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Emmy akiwa katika kuwaza juu ya Grace, mara akamkumbuka Lameck na kauli yake kuwa ile mimba ilikuwa halali yake.

    Tumbo likaanza kutetemeka, akaanza kuhisi huenda kuna ukweli fulani katika maneno ya Lameck. Emmy akamfikiria Lameck kuwa si mtoto mdogo azalishe ghafla tu mada ile bila kuwa na hisia fulani.

    Mahesabu ya mimba yake kuingia yakamvuruga kabisa.

    Akafumba macho yake kabla ya kukatishwa na hodi getini, alipofungua macho yake akakutana na yule mwanaume aliyekuwa anamuwaza kichwani.

    Lameck!!

    Tumbo la kuhara likamkamata, akanyanyuka na kutimua mbio kuelekea ndani chumbani, safari ikaishia chooni.

    Hakuna kilichotoka. Ilikuwa hofu tu.

    Huko maliwatoni, Emmy akawaza kuwa hatimaye Lameck ameamua kumkomesha kwa namna nyingine. Pigo la mwisho lenye hatari kupita yote.

    Lameck ameamua kumshirikisha James siri nzito.

    “Emmy.....” James aliita.

    Emmy akauchuna kana kwamba hasikii lolote.

    Bado alikuwa maliwatoni bila lolote la kufanya.

    Nguo zake zilikuwa nusu zimevulika na nusu bado zikiutawala mwili wake. Alikuwa anajiuliza aitike ama aendelee kuuchuna.

    “Wifi....” sauti ya Gloria ikaita kutokea mlangoni. Emmy akazidi kuchanganyikiwa.

    Emmy akapandisha nguo zake na kutoka nje.

    “Kuna nini?” akauliza.

    “Simu yako ilikuwa inaita....naona imekatika....hii inaita tena...” Gloria kwa nidhamu akamkabidhi Emmy simu.

    Mlango ukafungwa akaitazama namba inayompigia.

    Mshtuko. Alikuwa ni Jose B waukweli ama Sam wapili.

    Simu ilikuwa imepigwa mara tatu bila kupokelewa.

    Jose matamaa . akaingiwa na tamaa na wivu kutokana na simu yake kuacha kupokelewa. Akatuma ujumbe.

    “Nakuja nyumbani kwako.” Ujumbe huu Emmy aliusoma baada ya kuwa amekata simu badala ya kupokea.

    Emmy akajikuta anapiga yowe, yowe ambalo halikusikiwa nje ya chumba hicho.

    Akapagawa na ujumbe ule. Mume wake alikuwa nyumbani na baba yake mdogo pia alikuwa nyumbani.

    Aibu ya karne!!

    Emmy akaingia maliwatoni akajisafisha uso wake kwa maji na sabuni.

    Mara akanogewa akaamua kuoga kabisa. Akajifungia maliwatoni.

    Hakuweza kuisikia simu ilivyoendelea kuita.

    Alitumia dakika kumi na tano bafuni.

    Aliporejea akakutana na simu saba zisizojibiwa.

    Akatamani kumtumia Jose B ujumbe lakini akajikuta akisahau na kuendelea kuvaa upesi upesi.

    Kosa kubwa!!

    Wakati akihangaika, Jose Matamaa alikuwa ametaharuki katika teksi aliyokodi imfikishe nyumbani kwa Emmy, Jose kijana mdogo kabisa asiyejua uchungu anaoupata mwanaume akiibiwa mke wake ama kijana mwingine yeyote anayempenda na kumthamini mpenzi wake anapogundua kuwa anasalitiwa. Alikuwa anafurahia kummiliki Emmy. Ilifikia wakati akawa anatamani kuwa mume wa Emmy ambaye ni mke wa mtu tayari.

    Kwa jinsi ambavyo Emmy alijirahisisha kuuachia mwili wake ndivyo Jose alivyopata nafasi ya kumtawala zaidi.



     Akatamani kumtumia Jose B ujumbe lakini akajikuta akisahau na kuendelea kuvaa upesi upesi.

    Kosa kubwa!!

    Wakati akihangaika, Jose Matamaa alikuwa ametaharuki katika teksi aliyokodi imfikishe nyumbani kwa Emmy, Jose kijana mdogo kabisa asiyejua uchungu anaoupata mwanaume akiibiwa mke wake ama kijana mwingine yeyote anayempenda na kumthamini mpenzi wake anapogundua kuwa anasalitiwa. Alikuwa anafurahia kummiliki Emmy. Ilifikia wakati akawa anatamani kuwa mume wa Emmy ambaye ni mke wa mtu tayari.

    Kwa jinsi ambavyo Emmy alijirahisisha kuuachia mwili wake ndivyo Jose alivyopata nafasi ya kumtawala zaidi.

    Sasa bila kujali ni kwa kiasi gani anahatarisha ndoa ya Emmy alikuwa anaelekea nyumbani kwake.

    Emmy alitoka nje upesi akamuaga James kuwa anaonana na mtu kwa dakika kadhaa nje. Usoni alikuwa ametaharuki, James naye hakuwa na amani moyoni kwani ile hali ya kuona simu ya Emmy ikionyesha jina la Sam wapili. Akamkumbuka Jose B na jina hili lilikuwa na namba ya simu ya Jose.

    Alitamani kutoka pamoja na Emmy lakini ile tabia yake ya kutopenda kuwadharau ndugu wa mwanamke ikamtafuna akamheshimu Lameck na kuendelea kubaki akimsikiliza huku Emmy akitokomea nje ya geti upesi.

    Jose B hakuwa na utani hata kidogo. Hata yeye hakujielewa ni nini anafanya. Hakujisikia kumuogopa James, alifanya kile ambacho moyo wake ulimtuma kufanya. Sasa alikuwa jirani kabisa na nyumba ya Emmy. Penzi alilopewa na Emmy likamvuruga akili yake na kuwa kama mwendawazimu.

    Umri wake wa miaka ishirini na ushee uliruhusu kabisa kuwa katika hali hii. Hali ya kuwa mtumwa katika jambo jipya katika maisha.

    Emmy alikuwa wa kwanza kumuona Jose B akiwa amejiweka mbali kidogo na geti akiwa ameuegemea mti mkubwa wa mwembe usiokuwa na matunda.

    Emmy akatembea kwa mwendo kasi, akawa anatembea nusu na nusu anakimbia akiwa amelikamata gauni lake vyema.

    “Sam......nini hiki unanitaka...eeh”

    Jose B akageuka, alikuwa amenuna. Akamtazama Emmy kwa jicho kali.

    “Unataka kunifanya mtoto mdogo sivyo?” akahoji kwa jeuri.

    Emmy akashusha pumzi zake.

    “Sikia Sam...nakuomba tusizungumze kwa sasa kesho nakuja nyumbani kwako tutakaa muda mrefu tu....niamini tafadhali, James yupo hapo na bamdogo, wanatoka sasa hivi Sam, nitaelewekaje mie pliiz nakuomba Sam nakuomba sana.” Sauti yenye kitetemeshi cha hofu ilimkumba Emmy wakati anasihi. Hofu ilikuwa imetawala.

    Jose B akakumbwa na sintofahamu baada ya sauti ile kupenya katika masikio yake, akajikuta akitabasamu.

    Jose B alipenda sana kunyenyekewa.

    Akamkubalia Emmy. Wakaachana bila kuagana.

    James hakuwa anaelewa lolote lililosemwa na Lameck juu ya kupotea kwa watoto, alikuwa anawaza juu ya Jose B ambaye ana wasiwasi ndiye Sam wa ukweli.

    Ana hila gani na mkewe wa ndoa tena ambaye ana mimba tayari? Alijiuliza.

    Hakupata majibu.

    Akajisikia mchomo wa wivu ukimuandama, akaanza kupata suluba ya aina yake, akafumba macho na kumuona bwege mmoja waliyekutana jijini Mwanza, akamuuzia Kizuzizi kwa shilingi milioni sita, akapewa utangulizi wa shilingi milioni mbili akatoweka. Leo hii anaigusa ndoa yake.

    James akahisi kuwa Emmy anaweza kuwa ana mahusiano ya siri na Jose B ambaye kwa sasa anajiita Sam.

    Kwa hiyo huyu bwege amefikia hatua anamfuata mke wangu hapa hapa nyumbani kwangu? Haiwezekani hata kidogo wanichezee shere hawa. Hivi wananijua vizuri kweli?

    James alihamaki.

    Lameck aliigundua hali ya utulivu jinsi ilivyopotea katika uso wa James. Akaona asiendelee kuongea sana akamtazama na kumsikitikia kwa mengi.

    Likiwemo la kulea mimba ambayo si yake na sasa ana wasiwasi na mkewe baada ya kupigiwa simu kisha akatoka nje.

    Lameck akaamua kuaga na kuondoka zake.

    Kitendo cha Lameck kuaga kikampa James nafasi ya kipekee kujaribu kuuliza juu ya mtu aliyekuja nyumbani na kisha Emmy kutoka nje.

    James aliingia chumbani na kumkuta mkewe akiwa amejilaza kitandani, hakuwa na furaha hata kidogo, na kitendo cha mtu kuingia pale chumbani kikampagawisha.

    Akataharuki waziwazi.

    “Emmy...ni nani alikuja pale nje ukamkimbilia mbiombio.”

    “Nani? Mimi?” aliuliza swali la kipumbavu Emmy kwa hofu.

    “Kwani humu ndani tupo wangapi?” James alijaribu kuzuia jazba yake.

    “Hapana ni rafiki yangu...nani huyu mzoa taka alikuwa anadai.....naniii” Emmy alitia huruma, hakuwa na cha kujibu mbele ya mumewe.

    James akakunja ngumi yake imara ili aweze kuikabili hasira yake. Akafanikiwa kwa kiasi kidogo.

    “Mlipeana namba lini na huyu mtupa uchafu?” James kwa sauti ya chini aliuliza, bado alikuwa amesimama na Emmy alikuwa ameketi.

    “Hajanipigia simu wala.”

    “Kwa hiyo alikuita kupitia dirisha la chumbani sivyo?” mwanaume akazidi kukoroma. Sasa alikuwa anatetemeka midomo.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Haikuwahi kutokea hata siku moja katgika kipindi cha mahusiano yao.

    Emmy akakosa cha kujibu.

    James akaitwaa simu ya Emmy pasipo binti huyu kutarajia. Akapekuapekua sehemu ya namba zilizoingia, akakutana na majina kadhaa ya kike. Hapakuwa na jina la Sam wa pili.

    Akajaribu kulitafuta jina lile. Hakuna kitu.

    Kijasho chembamba kikamtoka.

    Akataka kuliendea kabati ili arejee na ile namba ya Jose B aiingize katika simu ya Emmy akahofia kuzua utata baadaye, alimjuaje Sam wa pili.

    Kama Emmy na Sam wana mahusiano lazima atamshirikisha na hapa ndipo mkanda utakapoharibika.

    “Na uhakika hujapigiwa simu na mwanaume wakati nipo na baba yako?”

    “Haki ya Mungu tena mume wangu.” Akaapa.

    James akashikwa na hasira kali akakumbuka kuwa wanawake ni sumu kali, sumu isiyostahili kuguswa hovyo. Hasira zikampanda, ameua kwa ajili yake na sasa hana imani kwa ajili yake.

    Mkono ukawa mwepesi ukalishambulia shavu la Emmy.

    Kipigo kitakatgifu cha kwanza katika ndoa kikafuata.

    James akamwadhibu Emmy kwa kujaribu kumficha.

    Ugomvi wa kwanza ukazua kipigo.

    Emmy alidhani anapigwa kwa sababu za wivu pekee hakujua kama kuna lolote ambalo James anamuwazia kuwa huenda analifahamu.

    Wakati anapokea kipigo alijisifu kimya kimya kwa machale yaliyomcheza kwa kuifutilia mbali namba ya Sam wa pili, na pia meseji zake zote, hajui ni mizimu gani ilimtuma lakini alijikuta tu akitekeleza hisia.

    Emmy alijisifu kwa kuamini kuwa laiti kama James angeipata namba ya Sam angeweza kumpigia na mwisho wa siku angeujua ukweli juu ya mahusiano yake ya kimapenzi na baba mdogo. Jambo ambalo lingepelekea siri tatanishi ya mimba aliyonayo kuchukua nafasi ya kuwa wazi.

    Ilikuwa bora kupigwa kuliko siri hiyo kuvuja.

    Emmy hakujua kama mumewe naye kuna siri zake ametunziwa na Sam wa pili ambaye ni Jose B waukweli.

    Laiti angejua.......



    Baada ya kugawa kipigo kile, James hakuweza kuhimili kuwa karibu na Emmy ambaye alikuwa analia kwa kwikwi, sauti ambayo iliisumbua nafsi ya James na kujiona kama amefanya kosa kubwa sana kumpiga malaika yule.

    Usiku uleule, James akaondoka bila kumuaga mtu yeyote.

    Akaelekea anapofahamu mwenyewe.

    Emmy akabaki na maumivu makali ya moyo. Maumivu ya usaliti.

    Maumivu ambayo yalimfanya aamini kuwa asilimia kadhaa ya upendo kutoka kwa mumewe ilikuwa imeporomoka. Na aliamini kuwa kwa kuendelea kufuga siri zile lazima upendo utaisha na mwisho wa siku James ataamua kujihusisha na wasichana wengine kimapenzi.

    Emmy alipofikiria juu ya James kuamua kuwa na msichana mwingine. Akaziona dalili za waziwazi za talaka, aliamini kuwa iwapo msichana atakayejihusisha na mumewe atakuwa na mapenzi ya kweli basi huo utakuwa mwanzo wa kupendekezwa kuwa mke, na kama sheria za kikatoliki zinambana kufunga ndoa nyingine basi ataishi naye kama mke pasi na ndoa.

    Mawazo haya yakamtetemesha Emmy, akashikwa na kichefuchefu akakimbilia bafuni kwa kuchechemea akatapika kidogo.

    Usiku huu ukawa moja kati ya siku zake ngumu na mbaya maishani mwake. Mfarakano katika ndoa. Emmy kwa mara nyingine tena akasita kuwafikiria marafiki katika ndoa yake.

    Akaumiza kichwa chake na kisha kugundua kuwa hakuwa na uwezo wa kutatua tatizo hili peke yake

    Emmy akajaribu kufikiria ni nani atakayemshirikisha. Mtu wa kwanza ambaye angeweza kumsaidia alikuwa ni mama yake ambaye katika namna ya kustaajabisha iliyosahaulika alikuwa marehemu tayari.

    Wa pili alikuwa ni James, ambaye ni mume wake. Lakini huyu ndiye ambaye ametoka kumchapa makofi muda mfupi uliopita na sasa hakujulikana ni wapi ameenda.

    Huyu naye kwenye orodha akafutika.

    Likajitokeza jina jingine, jina ambalo lilijaa sintofahamu pia.

    Emmy alimfikiria mtu huyu kwa maisha ya ukaribu wao kwa muda mrefu. Ni mengi walichangia, ladha ya ukaribu wao ikaongezeka baada ya kuibuka kwa hisia za mapenzi kati yao. Wakazidi kuwa marafiki.

    Elimu ikawatenganisha lakini mioyo yao ikiishi katika upendo wa dhati. Nani hakujua kama wawili hawa walikuwa wanapendana?

    Haikuwa siri tena...

    Maisha yakawakutanisha tena lakini kila mmoja akiwa na ndoto yake mpya.

    Hisia zikaamuka walipokutana, mara hii zilikuwa hisia maradufu, wakaliendeleza penzi na sasa yametokea ya kutokea.

    Wamekorofishana. Chanzo kikiwa mimba.

    Lameck na Emmy wakawa maadui.

    Emmy akatafakari mema waliyofurahia pamoja akalinganisha na ugomvi wa siku kadhaa, akairejesha imani kwa baba yake mdogo.

    Akamuona kuwa yu mtu sahihi kwake.

    Akaamua kujivika ujasiri. Akamtumia ujumbe wa kuhitaji kuonana naye siku inayofuata.

    Baada ya hapo akafanya jitihada za kumtafuta James katika simu huku akitetemeka ili kutimiza ule usemi wa mwanamke na ajinyeyekeze kwa mumewe ili ailinde nyumba yake.

    Simu ya James haikuwa hewani. Akajaribu mara nyingi zaidi bado hali ikawa ileile. Akatuma jumbe kadhaa za kumsihi mumewe arejee nyumbani lakini hazikupokelewa. Emmy akafadhaika lakini hakuweza kumlaumu James, kwani ilikuwa haki yake kuwa katika hali ile kutokana na wivu

    Usiku huu alichelewa kulala lakini baadaye alilala. Peke yake bila mumewe. James.



    ***



    Kigiza kilikuwa kimetanda, taa zilizofifia ziliwezesha macho ya viumbe hawa kuona chupa za bia na soda katika meza zao.

    Wacheza kamali waliwashiwa taa kali zilizowawezesha kucheza kwa makini kamali yao bila mtafaruku wa kuibiwa ama kuibiana.

    Mashine zilikuwa zikiwajibika kutenda kazi ya kuwaghiribu wachezaji na wao kuzidi kuingiza pesa zao. Waliobahatika kushinda walikuwa wakihesabu kete zao za rangi ya shaba. Moshi wa sigara ukiitawala anga ile ndogo.

    Katika moja ya mashine za kamali alikuwepo kijana ambaye ilikuwa mara yake ya kwanza kushiriki katika michezo hii ambayo ni maarufu katika makasino na hoteli kubwa kubwa.

    Shilingi elfu hamsini zilikuwa zimemtoka tayari na hakuna alichofanikiwa kushinda.

    Mashine hizi za ajabu zikaendelea kumvuta huku zikimghiribu kuwa atashinda mamilioni kadri anavyoendelea kucheza. Akafuata ‘tokeni’ nyingine, ikatimia shilingi elfu sabini.

    Jasho lilikuwa linamtoka. Ubahili wake ukamzonga akajikuta akiwa na mfano wa majuto ya kushiriki katika mchezo huo uliohalalishwa kitaifa.

    Hasira zile hakujua ni wapi anaweza kuzitua. Akakitazama kiatu chake, akakumbuka kuwa alikinunua kwa shilingi elfu thelathini.

    “Hiyo hela ningeweza kununua viatu viwili kama hivi na hela nyingine ingebakia.” Alijisemea wakati akimalizia tokeni ya mwisho ambayo pia haikumwezesha kushinda chochote.

    Akarejea na kujibweteka katika kiti kilichokuwa wazi kikimngoja.

    Kiti kilikosa ladha kabisa, akajiona kama kila mtu anamtazama kwa jinsi alivyoliwa pesa nyingi.

    Ghafla akanyanyuka ili aweze kwenda kununua ‘tokeni’ nyingine aendelee kujaribu bahati yake. Sasa alipigia mahesabu ya kukamilisha shilingi laki moja kabisa.

    Iwapo ataliwa tena basi ataondoka.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wakati anatembea jicho lake likakutana na sura ambayo haikuwa ngeni sana machoni pake.

    Akasita kutembea akamkazia macho kwa tahadhari kubwa, akahisi ni yeye.

    Akajisogeza pembeni akamgoja yule mtu aweze kunyanyua uso.

    Aliponyanyuka kupiga funda la bia yake, uso ukaonekana.

    Alikuwa ni yeye.

    Jose B waukweli akiwa na hasira za kuliwa katika kamali, akapata sababu ya kutabasamu.

    Akajisogeza pembeni zaidi, akakifikia kiti akajiegesha. Muhudumu akafika.

    “Samahani nikuhudumie nini??”

    “Pumbavu mashine zenu zimekula pesa zangu hamjaridhika tu...nipishe hapa.” Jose B akakaripia pasipo kufikiria kuwa muhudumu yule hausiki katika mashine zile.

    Muhudumu aliyezoea kuitwa malaya, na kutukanwa kila aina ya matusi akatoweka bila kuaga.

    Jose B akaweka sawa fikra zake.

    Akatia akilini mwake msemo wa duniani wawili wawili.

    Atamjuaje kuwa huyu ni yeye?

    Swali gumu.

    Akajifikiria kwa sekunde kadhaa.

    Akajikokota hadi kaunta, akamwomba muhudumu wa kaunta, kalamu na karatasi. Akaandika vitu kadhaa kisha akatoweka.



    ***



    James alikuwa anakaribia kurukwa na akili, aliwashirikisha rafiki zake baadhi juu ya ugomvi kati yake na mkewe lakini baadaye akagundua kuwa anafanya ujinga kuzitangaza siri za ndani ya ndoa yake nje.

    Akawa amechelewa kujikosoa.

    Akaamua kuzima simu zake. Akaelekea katika uelekeo usiokuwa maalumu. Akaifikia baa iliyokuwa na watu wachache.

    Akaingia na kujiweka katika eneo lenye mwanga hafifu, akaanza kuagiza moja baada ya nyingine. Picha ya mkewe akimsaliti ikazidi kujengeka kila alivyokuwa analewa. Mara anamuona na Jose B mara anamuona na matajiri wengine wa jijini Dar. Picha hizi zikazidi kumvuruga, akazidi kugida nyingine na nyingine zaidi.

    Ulevi ukamkamata vyema. Picha ya Emmy akiwa anamsaliti nayo ikawa inatoweka.

    Mara likawa giza. James alisinzia katika meza aliyokuwa anaitumia kulewa. Hakuna ambaye alimwamsha, hakuwa akidaiwa bali ni yeye alikuwa akiwadai wahudumu pesa zake walizozibana bila kumrudishia.

    Mwanga ulirejea tena baada ya muhudumu kumtikisa James.

    Akaamka akiwa hajielewi.

    Akabwatuka tusi zito. Halikumshtua muhudumu, alikwishayazoea. Maana ni dakika kadhaa zilizopita alikuwa ametoka kutukanwa na mteja mwingine tena yale yalikuwa mazito kuliko haya anayotukanwa na mlevi huyu mwenye pete ya ndoa kidoleni.

    “Unasema nini wewe malaya...” aliuliza James kilevilevi.

    Muhudumu hakujibu kitu akamkabidhi kikaratasi, James akakinyakua, akakielekezea katika mwanga ule hafifu, akajaribu kusoa haikuwezekana.

    “Malaya...soma hapa...”

    “Malaya mama yako...fala wewe” muhudumu akajibu mapigo huku akikipokea kile kikaratasi, akaitumia vyema elimu yake ya darasa la saba kukisoma.

    “Bibiana na Deo” alikisoma kwa sauti ya juu ili aweze kupambana na mziki uliokuwa unapiga.

    Kama vile amepigwa shoti ama kiti kimeota miba James akasimama wima, akakinyakua kile kikaratasi. Pombe zikawa zimepungua kiasi.

    Alipokisoma mwenyewe kwa macho yake dhaifu pombe zikakata.

    Ujumbe ulikuwa ukitaja majina ya marehemu. Marehemu ambao mkono wake unahusika.

    Akaanza kutetemeka, pombe nyingi alizokunywa hazikuwa na maana yoyote tena. Akataka kukimbia lakini akajishangaa kuwa alikuwa ni mjinga sana kwani adui yake alikuwa amemuona hapo kabla na kama ni kumdhuru angeweza kumdhuru wakati amelewa. Na hata kama ni kumuua angeweza kumuua.

    James akasimama kama bwege, muhudumu yule aliyeleta ule ujumbe alikuwa maili nyingi akiendekea na shughuli zake. Hakuwa na muda na mlevi aliyeshtuka.

    James akataharuki, akauficha ule ujumbe.

    Akauendea mlango wa kutoka.

    Jicho la Jose B lilikuwa makini kumtazama bwana James alivyochanganyikiwa.

    Mbavu zake hazikuwa na hali.

    “Nitayalia pesa haya mabwege mpaka yakome” alisema kwa sauti ya chini huku akigida soda kidogo iliyosalia katika chupa.

    Mtihani wake wa kutaka kugundua iwapo kweli yule ni James ama la ukawa umefanikiwa.

    Akajiona mtu mwenye bahati kupita wote duniani, akaupinga vikali ule usemi wa bahati haiji mara mbili kwani kwake yeye sasa ilikuwa ni bahati nyingine kati ya nyingi zinazojileta kila siku katika maisha yake.

    Jose akasahau kuhusu kuliwa pesa nyingi katika kamari, akarejea nyumbani akiwa na furaha. Sasa aliamini kuwa anaweza kubuni mradi mwingine wa kufanya na James huku akiendelea kumtumia mkewe kama chombo cha starehe, na banda la kutoa na kuweka pesa kama ofisi tu.

    Sekta tatu muhimu sana.

    Nani kama Jose B waukweli??

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ITAENDELEA



0 comments:

Post a Comment

Blog