Search This Blog

Sunday 19 June 2022

USINIBANIE - 4

 





    Simulizi : Usinibanie

    Sehemu Ya Nne (4)





    BAADA ya siku moja tu toka niokolewe na kina Omar nyumbani kwa Mzee Nurdin nikapokea simu toka kwa Tausi. "Halo..Jhemapele Tausi!" alimaanisha kuwa naitwa Tausi.



    Kwanza nilichanganyikiwa kuisikia sauti yake, netiweki ya

    mbongo ilianza kuwa luzi. Ilikuwa ikiingia na kutoka, nahisi

    aligundua kuwa nimepagawa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kilichotokea ni kwamba sikujua niheme kwanza au niongee

    kwanza maana hamu ya kuongea ilikuwepo, wakati huo huo pumzi zilikuwa zimenibana. Kuja kutahamaki simu ikawa imekatika, nikaruka hewani mtu mzima. Muito uliendelea kwa muda bila kupokelewa, mwisho simu ikakatika.

    Baada ya myda mfupi, akaruka yeye hewani, nikaipokea fasta.



    "Komatitapel?" Nilimuuliza tena jina lake kwa lugha ya

    kifaransa. "Tausi binti Nurdin" Nikashusha pumzi ndefu,

    kabla sijajitambulisha akaniambia kuwa amepata habari za

    Hoza.



    Nikasita kwanza kujitambilisha ili nimhoji na kuzijua hizo

    habari za Hoza. Nilihisi mwili unaishiwa nguvu pale

    alipokuwa akiniambia kuwa Hoza ni mpenzi wake na muda ule yuko naye! Kwanza nilitoa kicheko cha masikhara, ila kwa sauti aliyoendelea nayo sikuhisi kama alikuwa ni mtu ambaye alikuwa akitania.



    Nikajikaza kiume, nikamwambia kuwa nataka kuongea naye, nikijua wazi kuwa hakuna namna yeyote ya yeye kuwa na Hoza kuwa kuwa mimi ndio Hoza. Na isitoshe ilikuwa ni muda ambao sio rahisi kwa Tausi kuwa karibu na mwanaume yeyote. Ilikuwa inakaribia saa tano za usiku.



    "Haloo!" Ilisikika sauti ya kiume wakati Tausi aliponiambia

    kuwa anampa mpenzi wake Hoza aongee na mimi. Nilijihisi

    nikitetemeka na kushindwa kuongea, nikakata simu. Simu

    ikaita tena nikaipokea. Nikajikuta nikiongea Kiswahili "We

    nani?"



    "Shemeji, mbona huongei na mpenzi wangu Hoza? Si umesema kuwa ni ndugu yako, au sio Hoza huyu?" Naye akaniongelesha kwa Kiswahili. Donge likanishika nikajihisi machozi yakinitoka, ila sikujua nalilia nini.



    Ikasikika tena sauti ya kiume, "haloo, mbona huongei?"

    Nilijikuta nikimpa tusi ambalo nilikuwa na muda mrefu

    sijalitumia, ila cha ajabu wala halijamuuma. Najua

    halijamuuma kwa kuwa aliamua kunicheka.



    "Tusi la kizamani namna hiyo umelipata wapi wakati we

    unajifanya hujui vizuri Kiswahili?" Nikajihisi kutetemeka

    huku jasho likinitoka. Simu bado ilikuwa sikioni.



    "Kama hukuhitaji mawasiliano na mimi nduguyo Hoza ulikuja kufanya nini? Kuanzia sasa hatutakupigia tena simu na wewe usijaribu kuipiga tena namba hii, sawa Mfaransa koko?"



    Liliongea jamaa kwa majivuno ya hali ya juu.





    Baada ya maneno hayo simu ilikatwa na sikuwahi kuipata tena hewani namba hiyo hadi leo hii. Nilibaki nikizunguka huku na kule bila kujua kinachonizungusha na wala sikujua

    nilichokuwa nikikiwaza.



    Kimsingi nilikuwa nazunguka zunguka tu kama mchaga

    aliyeunguliwa na duka lake alilokopea hela Saccos.

    Mara simu yangu ya mkononi ikaita tena nikaanza kuitafuta

    ilipodondokea, nikaja kuikuta imejibana katikati ya mashuka bila mimi kujua kuwa ilifikaje. Nikaiona ni namba ngeni, nikaipokea. Kwa namna nilivyoipokea kwa pupa endapo yangekuwa ni maji ningepaliwa!



    "Koma savaa" nilikimwaga Kifaransa kabla sijapokewa na

    kicheko toka upande wa pili wa simu.



    "Umegeuka mfaransa kaka?"



    "Nani?"



    "Biskuti imeyeyuka kwenye glasi yako ya maji!" Iliniambia

    sauti ya kike toka upande wa pili wa simu.



    Nikashusha pumzi ndefu, nilijua fika kuwa simu hiyo

    inamaanisha nini. Ilikuwa ni simu ya kikazi. Nilipoangalia

    saa ilikuwa yakaribia saa sita na robo za usiku!



    Nikajimiminia pegi kadhaa za whisky ili ubongo ukae vizuri

    kidogo, nikavaa haraka haraka, nikajilodi silaha na kuanza

    safari ya kwenda kwa mkuu.



    "Tausi ushakufa, tutaonana kuzimu!" nilijisemea sio kwa

    sababu kazi niliyokuwa nikielekea kuifanya ilimuhusu Tausi

    bali nilikuwa nikijilazimisha niamini kuwa Tausi amekufa ili

    akili iweze kufikiria mambo mengine.



    Hii ndio njia ambayo huwa naitumia kumtoa mtu akilini,

    lakini kwa Tausi iligoma. Kila nikijilazimisha akilini

    nimuone yuko kwenye jeneza, namuona akiniangalia kwa mahaba.



    Tena nilikuwa namuona kwa picha iliyokuwa wazi utafikiri

    alikuwepo pale, nilimuona kifuani alivyo na mvuto, nilimuona sehemu za tumboni na namna alivyotanuka baada ya kiunoni.



    Niliamua kutumia njia mbadala, nikafungulia muziki kwa sauti ya juu na kujilazimisha kuuimba wimbo ulio hewani kwa sauti kubwa nikiufuatisha lakini wapi.



    Muda si mrefu nilikuwa ofisini kwa mkuu. "Namba tatu,

    sifuri, moja," mkuu wa kazi aliniambia akiniangalia usoni

    kwa makini. Ilikuwa ni kazi ya Mzee Nurdin, ameingia kwenye mtego hivyo ilitakiwa akakamatwe katikati ya uhalifu wanaoutarajia kuufanya.



    Mkuu akanipa taarifa zote, aliniambia kuwa usiku ule

    watakuwa wakiwasafirisha watoto kuwaleta Dar es Salaam kwa ajili ya kuwapandisha ndege.



    Akili yangu ilifanya kazi kwa haraka sana, nikajua kuwa ni

    mojawapo ya fursa chache sana zinazoweza kupatikana.

    Nikamuonyesha dalili fulani mkuu nikitegemea matokeo fulani.



    Mkuu aliponiangalia akaanza kuhisi kuwa siko sawa na ndio

    kitu nilichotaka akiamini, akaniuliza zaidi ya mara tatu

    nikamwambia kuwa niko sawa sawa.



    Unajua kwa nini? Ukimwambia kuwa hauko sawa, atakupa namna ya kulitatua tatizo lako kisha utatakiwa ukaifanye kazi uliyopangiwa. Ila ukimwambia kuwa uko sawa sawa, hawezi kukuruhusu kwenda kazini kama anakuona huna dalili za kuwa uko sawa.



    Mkuu akaniamuru nikapumzike, akampa jukumu mtu mwingine.



    "Naenda kwa Tausi" nilijisemea moyoni.



    Nilijua ulinzi usingezingatiwa kwa kuwa akili ya Mzee Nurdin isingekuwepo pale nyumbani kama mambo yangekuwa yameharibika barabarani.

    "Mkuu ningependa nijue kila hatua" niliomba. Nikapewa namba maalum za kuwasiliana na watu watakaokwenda kwenye hiyo operesheni ya kumliza ba mkwe! Wakati natoka ofisini kwa mkuu ilikuwa yapata saa nane, usiku!



    Niliendesha gari kwa kasi kuelekea kwa Mzee Nurdin. Kwa kuwa tayari nilikuwa tayari niko kikazi sikuwa na sababu ya kurudi kwanza nyumbani. Baada ya muda nilikuwa nikikaribia kwenye himaya ya Mzee Nurdin.



    Nikazima taa nikawa naliendesha gari gizani kwa mwendo wa taratibu ambao haukuwa ukitoa kelele. Nikaliegesha gari

    mbali kidogo na nielekeapo. Hali ya hewa ilikuwa imetulia

    sana, labda ni kutokana na muda wenyewe.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nikaanza kutembea taratibu kwa tahadhari kubwa, nilitembea hadi karibu kabisa na ukuta wa kwa mzee Nurdin. Nilikuwa nimebeba mkoba ambao ndani niliweka mkasi maalum wa kukatia ukuta, vifaa vya kuundia mabomu ambayo hayana madhara na

    kimtungi kidogo cha gesi.



    Ndani ya begi pia kulikuwa na kemikali kadhaa za kuniwezesha kutimiza kazi yangu. Pia bastola yangu ilikuwa mkononi.



    Vingi kati ya hivyo nilivipata wakati nikihudhuria kozi

    maalum ya kijeshi nchini Marekani iitwayo CRT.





    Nilivyokuwa nikimhadithia rafiki yangu mmoja alishangaa

    kusikia kuna mkasi maalum wa kukatia ukuta. Mikasi hiyo ipo na inatumiwa sana kwenye operesheni za uokoaji kwenye majeshi yanayoendeshwa kisasa, inakata ukuta kama karatasi.



    Nikasogea hadi kwenye ukuta, nikaukata tundu kubwa ambalo linaweza kumfanya mtu akapita kwa kuinama. Nikaingia ndani nikikimbia hadi kwenye giza giza hadi karibu na dirisha la Tausi, nikapiga simu kuulizia operesheni inaendaje.



    Nikaambiwa kuwa kila mtu yuko kwenye nafasi yake wakisubiri amri. Nikawatakia kila la heri. Nikawa pale chini nasubiri taarifa, kidogo nikapata ishara fulani kupitia simu yangu.



    Nikafanya mawasiliano, nikajulishwa kuwa vijana wa Mzee

    Nurdin wameshakamatwa na watoto waliokuwa wakitaka

    kuwasafirisha, na tayari kuna kikosi kimetumwa ili kumchukua Mzee Nurdin.



    Nikatambaa hadi chini ya dirisha la Tausi, lile lile

    nililokuwa napigiaga chabo, nikajiinua taratibu. Kulikuwa na mwanga hafifu, lakini niliweza kuona vyema ndani. Tausi

    alikuwa amejilaza kitandani, nikaanza kupata hisia mbaya.



    Nilikuwa namuona kama amechoka choka, nikawa nahisi kuwa Hoza wa bandia ameshafanya mambo.



    Hasira zilinipanda sana, nikajihisi natetemeka. Lakini

    sikufanya pupa. Nikatulia kama dakika kumi hivi nikasikia

    mlio wa gari linaloingia kwa Mzee Nurdin, nikajua akili zote

    za walinzi zitakuwa getini.



    Nikakimbia na kupanda bomba kuelekea juu ya nyumba ya Mzee

    Nurdin, kama hesabu zangu zilivyonipa, mlinzi akawa

    anaangalia getini. Nikaingia chini haraka haraka, nikabetua

    kitasa na kuingia chumbani kwa Tausi.



    Sikuwa na muda tena wa kuremba, nikatoa pamba na kuimiminia

    kemikali kidogo. Nikamkandamizia puani, akahangaika kidogo

    kisha akapitiwa na usingizi. Nikatulia kusikilizia hali ya

    hewa.



    Nikasikia watu wakiongea ongea kisha kukawa kumetulia,

    nikawa nayasikia maongezi kwa mbali. Nikatoka kuchungulia,

    kulikuwa shwari. Nikarudi ndani nikamuweka Tausi begani kama

    kiroba.



    Nikapanda nae juu kupitia zile ngazi, nikamuweka karibu na

    geti kisha nikatoka kuchungulia. Yule mlinzi wa juu, alikuwa

    bado kaganda kuangalia getini. Nikamtua Tausi chini.



    Nikamnyatia mlinzi kisha nikamzimisha, kwa mapigo mawili ya

    nguvu, akatulia chini kimya.



    Nikamrudia Tausi, nikamuweka begani nikaanza kushuka nae

    hadi chini. Kufika chini, nikategesha bomu pale chini. Bomu

    hilo huwa linatoa mlio mkubwa sana lakini halina madhara.



    Nikamuweka begani Tausi na kuendelea na safari yangu gizani

    huku mbwa wa Mzee Nurdin wakitusindikiza. Inaelekea walikuwa

    wamenimisi sana! Nikajibana, kwenye kagiza fulani

    nikisubiria bomu langu, huku nikiwa nimeachama midomo, pia

    nilimtanua midomo Tausi.



    Mlio mkubwa ulisikika ghalfa, nikakimbia hadi kwenye tundu

    la ukuta nililolitengeneza. Nikamuegesha Tausi, nikatoka

    kisha nikamvutia nje. Nikamuweka begani na kukimbia naye

    hadi kwenye gari, nikamuweka kwenye siti ya nyuma. Nikapanda

    gari na kutoka nalo kwa kasi.



    Wakati naiangalia saa yangu ilikuwa yapata saa kumi kasoro

    alfajiri, nilikuwa nakaribia kuingia kwangu Boko. Baada ya

    kuingia ndani nilimbadilisha nguo Tausi, nilimvalisha traki

    suti yangu baada ya kumfuta futa, nikamlaza kitandani

    nikisubiri azinduke.



    Muda huo nikaanza kufanya mawasiliano na watu waliokuwa

    kwenye operesheni, wakaniambia kuwa Mzee Nurdin bado

    anashikiliwa lakini imefanywa ni siri kubwa sana, wanaojua

    ni watu wachache sana.



    Nilirudi chumba alichokuwemo Tausi, nikawa pembeni yake

    nikimwangalia. Nilikuwa na hamu ya kujua hali ikoje nyumbani

    kwa Mzee Nurdin lakini sikutaka kuchukua hatua yeyote

    kufutilia.



    Nilikuwa nasubiria kwa hamu kumuona Tausi wangu, kwa kweli

    sikuweza kuvumilia kusikia yuko na mwanamme usiku ule. Na

    kama ningemkuta, nadhani ningeua.



    Wakati nikiwaza hayo, Tausi alifumbua macho akawa kama

    anayeota. Nilimuacha kwanza aangaze angaze ili akili yake

    ikae sawa. Akajiinua na kukaa chini akiwa anafinya finya

    macho, akageuka akanitazama. Tukakutana macho kwa macho.



    "Tausi!" Nilimuita. Tausi hakujibu kitu, alikuwa kama bado

    anaota. "Hapa uko kwa kaka yangu, walikufuata jana usiku

    kwenu. Waliamua hivyo kwa kuwa nilitaka kujiua baada ya

    kusikia una mwanamme mwingine."



    Tausi akawa bado yuko kimya akinitazama, nilitamani kujua

    anachofikiria lakini nilihisi kuwa anatafakari maneno

    niliyomwambia.



    "Hoza!" Hatimaye aliniita.





    "Tausi" Nilimchukulia juisi na kumpa Tausi, akaipokea. Kabla

    ya kunywa, aliniangalia kwa muda. Akanywa kisha akarudi

    kujilaza. Sikumuelewa kwa muda ule, nikaanza kuingiwa na

    hofu. Alitulia kimya pale kitandani.



    Niliamua kufanya mawasiliano mbadala, nami nikajilaza

    pembeni yake nikamkumbatia. Tukawa kimya! Zilipita takribani

    dakika arobaini tukiwa vile vile, japo sikujua anachowaza

    lakini nilikuwa na uhakika kuwa hanichukii, bado ananipenda.



    "Hoza, ni kweli ulitaka kujiua?" Ni swali la ghafla

    lililonifanya nijihisi ubaridi, ilikuwa ni ngumu kumdanganya

    Tausi wangu ila ilibidi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Siwezi kuishi bila wewe Tausi, ulikuwa na nani?"



    "Baba na msaidizi wake mmoja."



    Akili yangu ilianza kuzunguka, mambo mengi yakipita

    kichwani. Tausi alinielezea mkasa mzima kuwa iligundulika

    kuwa nilikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Tausi, hivyo

    mpango ulikuwa nisingiziwe kesi.



    Kwa kifupi mpango wa Mzee Nurdin ulikuwa ni kunipoteza,

    hivyo mawasiliano yote aliyokuwa akiyafanya Tausi yalikuwa

    yakidhibitiwa ili tu Hoza nikamatwe na kupotezwa.



    Wakati ananihadithia yote hayo hakuwa akinitazama usoni, ila

    sauti yake nyororo iliutuliza moyo wangu. Tatizo lililobaki

    ni kuwa ningemwambiaje ukweli kuhusu mimi?



    Na angeuchukuliaje ukweli huo? "Unaonaje tukienda kuoga?"

    Nilichombeza nikiwa na lengo la kuomba mambo kiaina.

    Tausi akajiinua taratibu, nikainuka haraka zaidi.



    Nikamnyanyua na kumpeleka bafuni. Nikaanza kumvua traksuti,

    kisha nami nikavua nguo zangu. Tukawa kama tulivyozaliwa

    bafuni mule.



    Niliduwaa nikiukagua mwili wa Tausi ambaye alishindwa

    kunikazia macho akawa ananiangalia kwa aibu. Nilifarijika

    sana moyoni nikajisifu kwa uharamia nilioufanya,

    nikamsogelea na kumkumbatia huku mkono mmoja ukibonyeza

    kuyaruhusu maji yatiririke kwenye miili yetu.



    Kilichobaki ilikuwa ni kusuguana kulikopitiliza, na hata

    tulipotoka bafuni hakuna aliyemsemesha mwenzake, tukajilaza

    kitandani tukijifunika shuka kubwa.



    Nilishtuliwa na mlio wa simu, alikuwa ni Mkuu. Haikuwa

    kawaida kwa Mkuu kupiga simu muda kama ule, hivyo nikaanza

    kujiuliza maswali yasiyo na idadi. Kumtupia jicho Tausi,

    naye akawa ameshtuka ananiangalia kwa jicho la kwa nini

    hupokei hiyo simu?



    Nikaifuata na kuipokea, mkuu aliniuliza maswali kama matatu

    hivi lakini uzito wake ulinifanya nitokwe na jasho kwenye

    paji la uso.



    Kimsingi alikuwa akinihoji kama niliona pilika zozote kwa

    Mzee Nurdin kuwa kuna watu wanamfuatilia Tausi, kabla

    hajanitaarifu kuwa ametekwa na watu wenye mbinu za kijasusi.



    Akaniambia kuwa tukio hilo lilipishana muda kidogo sana na

    muda aliokwenda kuchukuliwa Mzee Nurdin kwa ajili ya

    mahojiano.



    Baada ya Mkuu kukata simu, nilijikuta bado nimeishikilia ile

    simu mkononi nisijue jambo la kufanya kwa haraka haraka ila

    sikupata presha sana kwa kuwa mtu aliyeteuliwa kulifuatilia

    suala hilo naujua uwezo wake.



    "Vipi?" Tausi aliniuliza akiwa anajiinua kitandani.

    Nikamdanganya kuwa aliyepiga simu ni kaka.



    "Kuna kitu unanificha Hoza, na bora nikisikie toka mdomoni

    mwako kuliko nikikisikia kwa mwingine. Kwa maana

    sitakusamehe" aliniambia Tausi akionesha kuwa hana masihara

    hata chembe.



    Nilibaki kimya nikimtazama, nilijaribu kupata picha endapo

    angeniacha, nikajihisi maumivu makali sana moyoni. Nikampa

    mkono, akaushika. Nikamwinua, akanyanyuka. Nikammiminia

    mabusu mfululizo huku mikono yetu ikiwa imeshikana vyema.



    Tukaanza michezo michezo yetu, huku tukifurahi kisha

    nikamwambia tutoke tukatembee ufukweni. Akanitania kuwa

    tutembelee majini sio ufukweni, nilicheka lakini

    nilimwelewa. Nikampa bukta na fulana moja nyepesi, nami

    nikabadili tukatoka.



    Baada ya muda mchache tulikuwa katikati ya maji tukiendelea

    na mchezo wetu uliopelekea kuonja mahaba ya ndani ya maji,

    shughuli ilikuwa tamu usipime! Kwa muda wote aliokuwa pale

    kwangu, Tausi alikuwa akiyafaidi mapishi yangu. Alionekana

    kufurahia mno.



    Nakumbuka kilichoniponza. Jioni iliyofuatia nilimchukua

    Tausi tukaenda kukaa ufukweni jua lilipokuwa likikaribia

    kuzama. Tausi alikuwa ametulia akinisikiliza kwa umakini,

    ambacho nilitaka kumwambia.



    Nilimwambia ukweli! Nilimwambia kuwa aliyekuja siku ile ni

    mimi na sina kaka. Nilimwambia wazi kuwa mimi ni afisa

    upelelezi ila nilimficha kuwa nilikuwa pale kwao kumpeleleza

    baba yake.



    Nilichomwambia ni kuwa, nilikuwa likizo nikaamua kwenda pale kwa Mzee Nurdin ili nipate nafasi ya kuwa naye. Nikamueleza

    kuwa niliwahi kumuona siku moja uwanja wa ndege, nikavutiwa

    naye. Nikaamua kuchunguza habari zake nikagundua kuwa yeye

    ni nani na anakaa wapi.



    Nilimweleza mengine mengi na ni kwa kiasi gani nampenda na

    sitaki kumpoteza katika maisha yangu. Muda wote huo Tausi

    alikuwa akiniangalia tu kama anatizama sinema ya kihindi.

    Nilishindwa kujua anafikiria nini ila alikaa kimya kwa muda

    mrefu.



    Nilijaribu kumshika, lakini hakutaka nimshike. Alisema nimpe

    nafasi kwanza akili yake iweze kupembua maneno

    niliyomwambia, niliogopa. Baada ya muda mchache, Tausi

    aliinuka taratibu na kuanza kuondoka akiongozea nyumbani kwangu.



    Nikainuka na kuanza kumfuata nilichanganyikiwa kwa kweli.

    Tausi alirudi moja kwa moja hadi chumbani, akabadili nguo.

    Alivaa nguo nilizomnunulia mchana ule, akajiandaa kama ana

    safari fulani, kisha akakaa kitandani.



    Nilimfuata nikaishia mlangoni nikimwangalia nisijue ni lipi

    la kumwambia, sikujua anawaza nini kwa muda ule. Ila alikuja

    kuniambia neno moja tu, "mimi na wewe basi!"



    Nilijikuta machozi yananidondoka japo sikuwa nalia.





    "Ni heri kumuona mwanamume akikata roho kuliko kumuona

    akitoa machozi!" nilimwambia kwa huzuni nikimkazia macho.

    Nilimwambia, "toka nipate akili timamu, hata mama yangu

    mzazi hajawahi kuliona chozi langu. We ndio mwanamke wa

    kwanza kuliona chozi langu, sitakubali utoke katika maisha

    yangu!"



    Tausi aliniangalia kwa muda, alionekana mwenye huzuni sana.

    Nilipoendelea kumwangalia nilimshuhudia akiangua kilio,

    nilimsogelea nikakaa pembeni yake.



    Alilia kwa muda kisha akageuka kunitazama, moyoni nilijawa

    na huzuni lakini sikulia tena. Nilijikaza kiume tukabaki

    tunaangaliana. "Huwezi kuamini ninavyokupenda Hoz.. sijui

    sasa nikuiteje?" Tausi aliniuliza.



    "Niite Musa, nimeamua nijivue niwe halisi."

    "Ok, nitalizoea taratibu. Nakupenda sana Musa, lakini siwezi

    kukuamini tena!" Maneno ya Tausi yalikuwa ni kama msumari wa

    moto moyoni mwangu, yalinichoma na nikaumia haswa.



    Nikajaribu kumwelezea sana kuhusu namna nnavyompenda lakini

    kwake ilikuwa ni kazi bure, aling’ang’ania msimamo wake kuwa

    mimi na yeye basi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Mara zote nilikuwa nikiambiwa kuwa maaskari hawaaminiki, na

    mimi nilijiapiza kuwa sitakuja kufanya urafiki na askari.

    Tazama leo, mpelelezi ndio amekuwa mwanamme wangu wa kwanza" alisema Tausi akilia.



    Nilijaribu kumwelewesha sana lakini haikusaidia, maswali

    aliyokuwa akiniuliza yalinivunja nguvu. Mfano aliniuliza

    kuwa atajuaje kama sikumtaka yeye ila nimchunguze baba yake.

    Alinielezea kuwa baba yake alishahisi kuwa mimi ni

    mpelelezi, na tayari alishamuonya kuhusu tabia za askari na

    akaniambia kuwa askari hatuna mapenzi ya kweli.



    Nilijihisi napata homa kali, sikuwa na pointi tena za

    kujitetea kwa kuwa Tausi alionekana kudhamiria kunifungia

    milango ya mapenzi. Nikajilaza kitandani nikisubiri hatima

    ya yote, sikuwa na nguvu tena ya kumshawishi Tausi.



    Ila kikubwa nilimpa muda wa kutafakari maneno niliyomwambia.

    Nilikuwa nimefumba macho nikiongea taratibu, ilikuwa ni kama

    namkumbusha Tausi mambo tuliyoyafanya pamoja, niliyachagua

    yale yaliyokuwa yakisisimua. Nilimsikia akishusha pumzi

    ndefu, nikaendelea na simulizi zangu.



    Nilimwambia hadi jinsi nilivyokuwa silali bila ya kumpiga

    chabo, nilipofikia hapo nikamsikia akijizuia kucheka.

    Sikujali japo nami nilijizuia kucheka, niliendelea

    kumhadithia hatua kwa hatua hadi nilipobambwa mara ya kwanza

    nikapigana na walinzi.



    Mwisho nikaanza kumuelezea namna nnavyojisikia moyoni

    kutokana na uamuzi wake, uamuzi ulionifanya nijihisi kama

    mtoto yatima anayekimbiwa na mama yake. Kufikia hapo Tausi

    akausogeza mkono wake na kuushika wangu, akauvuta na

    kuukumbatia.



    Nikawa nalihisi joto la mwilini mwake. Nikaona kuwa ulikuwa

    ni wakati muafaka kuiacha miili ibembelezane na kuchukua

    nafasi ya midomo. Nikamvutia kitandani. Akaanza kunipa

    ushirikiano wa kutosha.



    Tukawa tumezama mapenzini huku maneno yakiwa hayanikauki

    mdomoni, nilimsihi asije kulivunja penzi letu. Tulipomaliza

    Tausi alikuwa amelala kifuani kwangu.



    Aliufungua mdomo na kuniambia maneno niliyoyaelewa japo

    yaliniumiza sana, alinihakikishia kuwa ananipenda na

    anaamini kuwa penzi langu ni la kweli. Lakini tusingeweza

    kufikia tunapotaka kwa kuwa kwanza baba yake asingekubali

    tuoane, akaniambia wazi kuwa hadhani kama kuna mtu

    anayechukiwa na baba yake hapa duniani kuliko mimi.



    Pili kwa yeye isingekuwa rahisi yeye kuniamini kama

    ningeendelea kuwa katika kazi yangu ya upelelezi kutokana na

    mambo anayoyasikia na kuyasoma kuhusu wapelelezi. Ila

    aliniambia kuwa atabaki kunikumbuka katika maisha yake yote

    na hadhani kama kuna mwanamume ambaye angeweza kunitoa

    katika moyo wake.



    Pamoja na kuwa maneno hayo yalinifariji lakini sikuwa

    nahitaji kumpoteza Tausi, nilikuwa naumiza kichwa ni njia

    gani itakayonibakizia Tausi wangu. Tulilala tumekumbatiana

    kwa nguvu sana usiku ule.



    Naukumbuka vizuri usiku ule, joto la Tausi nililihisi hadi

    moyoni mwangu. Kila nilipofikiria kuwa ile ndio ilikuwa ni

    mara yangu ya mwisho, moyo uliniuma sana. "Sikubali"

    nilijisemea usiku ule.



    Tuliendelea kulala vile vile pamoja hadi ilipofika asubuhi.

    Tausi akawa anataka kwenda kwao, nilimsihi asubiri giza

    liingie. Akaniuliza swali gumu kuwa ningemrudisha kama

    nilivyomchukua? Nikamwambia hapana, ningemrudisha kivingine.

    Ila kwa namna ambayo atakuwa salama. Nikarudia tena

    kumwambia namna ninavyompenda, ila alinikatiza kabla

    sijamalizia.



    "Usifanye mambo yale magumu, nielewe mpenzi" aliniambia

    akinibusu mdomoni na kuufanya mdomo wangu uhisi ganzi!

    Baadae kidogo Tausi akaniambia kilichonishangaza,

    sikutegemea kama angenifikiria jambo lile. Akaniomba iwe

    zamu yake kunipikia, nikamuuliza unaweza? Akabaki anacheka,

    akaniambia subiri uone.



    Tausi akaingia jikoni, mi nikawa msaidizi wake. Nikawa

    nasaidia kukatakata vitunguu, mara niambiwe lete chumvi basi

    ilikuwa raha tu. Kikubwa nikawa nasubiri kitakachotoka kama

    utamu wake utafanana na Tausi? Tausi ana tabu kweli, unajua

    alichokuwa amevaa? Alivaa kagauni fulani kafupi, kepesi na

    kanaonyesha.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nilikuwa nikisisimkwa kila nikimuangalia japo nilikanunua

    mwenyewe, mtoto huyu mvuto wake umepitiliza yaani utadhani

    ni binti jini! Uzalendo ukanishinda, ikabidi tuliweke kando

    kwanza suala la kupika likawa ni suala la kupikana humo humo

    jikoni.



    Baada ya kuhakikisha presha zimeshuka, zoezi la kupika

    likaendelea huku Tausi akinionyeshea viwango vya jikoni.



    Siku hiyo tuliinjoi sana, nilijitahidi kupata raha kwa

    kadiri ilivyowezekana pamoja na kumpa raha za kutaka

    kumkomoa ili abadili uamuzi wake.



    Nilimuomba afikirie tena kuhusu uamuzi wake, ila nilimwambia

    asinijibu pale pale. Nilipomwona anakosa raha nikabadilisha

    maongezi nikampa stori za kumchekesha chekesha. Akarudi

    kwenye ’mudi’! Baadae muda wa kuondoka ukawadia!



    Tukaanza kujiandaa, mpango ulikuwa ni kwenda na Tausi hadi

    karibu na nyumbani kwao kisha ningemuacha na watu ambao

    tayari nilikuwa nimewapanga. Kila nilipomwangalia Tausi,

    nilijihisi kuwa ni mwanamume mwenye bahati mno.



    Ni aina ya msichana ambaye hata ukimuhonga gari ukawa

    unatembelea daladala huwezi kujilaumu. Watu hao niliowaandaa

    wangemfikisha Tausi hadi nyumbani kwao kwa madai kuwa

    walimuokota akiwa kapoteza fahamu nje ya mji.



    Kila kitu kilikuwa kimepangwa vyema. Sikutegemea kufeli kwa

    kuwa watu niliowaandaa walikuwa ni kina mama wawili maaskari

    na mzee mmoja. Pia nilitumia ’uchawi wa kizungu’, pesa!



    Wote hao sikuwaambia ukweli ila niliwadanganya kuwa Tausi ni

    demu wangu, lakini kwao geti kali hivyo kwa kuwa

    nilimtorosha nikachelewa kumrudisha ingekuwa kesi nzito. Utu

    uzima dawa, walinielewa vyema japo walikuwa wakininanga

    kizamani. Eti kwa nini usitoe posa, unaendekeza uhuni tu?

    Wazee wengine bwana!



    We unafikiri ningemtangulizia posa Mzee Nurdin hata nafasi

    ya kuongea na Tausi ningeipata? Si Mzee Nurdin angeona

    namletea uchuro tu? Baada ya kumaliza kujiandaa, tulitoka

    kwa kutumia gari la rafiki yangu.



    Sikutaka kutumia gari langu kutokana na sababu maalum. Tausi

    alizifunga tu nywele zake kwa nyuma, akavaa gauni kama lile

    alilovaa siku ile nilipomchukua. Kuna kitu nilitaka

    nisikihaditie lakini ngoja tu niwaambie.



    Unajua alipomaliza kuvaa kama nilivyomchukua, lile gauni

    lilimuonyesha umbile lake vyema. Na kila nilipomtazama,

    mawasiliano kichwani yakaanza kupotea kama netiweki ya simu

    mbovu. Tukakata kiu tena.



    Muda mfupi baadae tukawa tukiingia barabara ya Bagamoyo

    ambako jioni ile hakukuwa na foleni kabisa. Kagiza kalikuwa

    kameshamiri.



    Niliingia barabara hiyo kuu nikiendesha huku mpenzi wangu

    Tausi kanilalia begani na mkono wake ukiwa pajani kwangu

    akinifariji, dunia yote ilikuwa yangu. Muziki laini ulikuwa

    ukiunguruma garini huku Lionel Richie akifanya vitu vyake

    vya kiutu uzima. Kwa kweli ukijipanga pepo inashuka hapa

    hapa bongo!

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    ITAENDELEA



0 comments:

Post a Comment

Blog