Search This Blog

Monday 20 June 2022

SITAISAHAU FACEBOOK - 4

https://pseudepigraphas.blogspot.com/2019/11/sitaisahau-facebook.html

Simulizi : Sitaisahau Facebook

Sehemu Ya Nne (4)


“Kwani mtu akifa anakuwaje?” aliniuliza, sikujibu.Akaendelea, “hebu tuachane na hayo..msichana mdogo kama wewe ukifa sio vizuri ujue.”“Kama ukiwa makini hautakufa. Tena wewe hautakufa, nitakusaidia usife sawa!!”“Sawa!!” nilijibu kwa nidhamu kubwa.“Njoo huku…”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Nikamfuata hadi mahali patulivu kabisa. Sasa hii ilikuwa ofisi kweli. R.I.P akanipokea. Akaniacha ofisini kwa muda, kisha akaingia tena baada ya dakika kadhaa.Hakuwa yule tahira, hakuwa mchafum,chafu kama nilivyokueleza mwanzoni. Huyu alikuwa na hadhi ya yule mvulana ninayemuhitaji. Alikuwa mtanashati.Hakuwa akicheka hovyo! Alikuwa makini na mtaratibu.Roho Iliyo Potea (R.I.P). Alianza kwa kujitambulisha jina lake halisi. Kisha akaniupongeza sana kwa ujasiri wangu hadi kufika hapo.Akajieleza kwa ufupi maisha yake ya utafutaji huku na kule hadi alipojikuta akitafuta kwa njia za mashetani. Ni katika maelezo haya alinieleza juu ya namba 666. Nilishangazwa sana na maelezo yake lakini nilipiga moyo konde nikiamini tiba ipo.Baadaye akanieleza jinsi alivyojitoa katika harakati hizo za kumtumikia shetani. Haikuwa njia rahisi. Aliwapoteza ndugu zake kadhaa lakini mwisho akawa amejikomboa.Hiyo chapa uliyopigwa lazima ifutwe! Ni njia hiyo tu ya kukukomboa kutoka ufalme huo.Nilikuwa makini nikimsikiliza.!USIKU MNENESafari ya kuelekea kuitoa ilea lama ilikuwa imewadia. Pesa taslimu milioni moja ilikuwa imenitoka tayari ili kufanikisha jambo hili.Tulitumia usafiri wa gari binafsi. Tulikuwa watatu. Mimi, RIP na mwenzake ambaye sikuwa namjua jina. Yeye alikuwa anaendesha gari.Sasa gari ilisimama. Tukashuka garini. Nilikuwa nimevaa upande wa kanga kama RIP alivyoniagiza. Tulitembea kwa muda hadi tukakifikia kichaka. Hapakuwa na vibuyu wala dawa za kienyeji lakini tulikuwa mbele ta kaburi, hilo kaburi lilikuwa likimsubiri mtu limmeze. Yaani lilikuwa wazi.Mara akachomoa kisu, akachomoa na kisahani.Nikaamuriwa kuvua nguo!! Nikavua. Nikawa uchi mbele ya wanaume hawa wawili. Sikuwa na aibu!!R.I.P akatoa sindano akavuta dawa. Akanigeuza, nikageuka.Akanidunga sindano. Hii ya sasa ilipenya. Nikaisikilizia maumivu yake kisha taratibu nikasikia mguu wangu wa kulia unakufa ganzi.Kisu kikatwaliwa upesi. Ilikuwa saa sita kasoro dakika sita. Hii ni kwa mujibu wa RIP.Sikujua kinachoendelea lakini nilipotazama chini niliona kitu kama maji vile. Ghafla ikasikika sauti. Sauti ya kike ikiniita kwa mbali. Sauti ile ilikuwa inanisihi sana nikimbie.Nikimbie kwenda wapi sasa.RIP na mwenzake walikuwa wameshikilia kile kisahani. Sasa niliweza kuona kipande cha nyama. 666 zilionekana zikiwa katika mng’aro wa dhahabu.Nikiwa sijajua lolote linaloendelea. Mara ghafla ile sauti sasa iliweza kusogea zaidi na zaidi.Hatimaye aliyekuwa anaita kwa juhudi zile nikamuona. Alikuwa ni Maria, yule rafiki yangu tunayeishi naye. Alikuwa yu uchi wa mnyama. Alikuwa akikimbia kwa juhudi zote lakini hakuwa akikimbia bure kuna kitu ama mtu alikuwa anamfukuza.Nikajaribu kupiga kelele. RIP na mwenzake hawakunisikia.Maria alikuwa anakimbizwa na nyoka. Nyoka mkubwa alikuwaanang’ara sana. Nashangaa wenzangu hakumuona.Nikajikuta natimua mbio uchi. Na nilikuwa kitendo cha sekunde chache yule nyoka akavamia eneo lile. Sikushuhudia sana kilichowatokea wenzangu. Sasa nikaanza kuhangaika huku na huko katika pori hilo ambalo sikuwa nalifahamu.Mguu mmoja ukiwa umekufa ganzi. Ningeweza vipi kukimbia mbio ndefu. Isabela mimi nikaanguka chini. Sasa nikawa najivuta kama nyoka. Nalia kama mtoto. Sikuwa na uelewa bado kwa nini mguu wangu ulikufa ganzi. Lakini kumbukumbu za kuchomwa sindano ile kali zilikuwa kichwani mwangu.Nikiwa bado sijapata jibu sahihi. Lile joka la maajabu sasa likatokeza mbele yangu. Mdomoni likiwa na kipande cha nyama. Nyama ile yenye namba 666.Nikajiinamia kwa uchungu. Nikafanya dua fupi. Nikajilaani kwa kila hatua ya maisha yangu niliyopitia. Nikatamani ningekuwa na nguvu niweze kutimua mbio. Lakini tayari nilikuwa nimelegea. Macho yakazidi kuhesabu hatua za yule nyoka kunifikia. Sijawahi kuona nyoka mkubwa kama huyu!!! Nakufa kwa kumezwa na nyoka. Inauma sana!!Joka likazidi kusogea!! Joka kuu likawa linatambaa!!!Kabla joka halijanifikia. Lilibadilisha uelekeo. Ni kama kuna kitu lilikuwa limehisi. Likaanza kutambaa kuelekea upande mwingine.Joka linatoka mara sasa namuona John. John yule mpenzi wangu ambaye alipotea katika mazingira ya kutatanisha pale chuoni.“John…John!!” nilianza kumuita. Sauti ilikuwa imekauka. Haikutoka.Joooooh!!! Nikajaribu tena, nikawa kama ninafanya mnong’ono. John akawa anaenda zake. Nikalia sana kuikosa nafasi hii hadimu ya kusikiwa na John!! Huenda angeweza kuwa msaada mkubwa kwangu.Ubaridi ulipenya katika mwili wangu. Mwanzoni niliuhisi kuwa wa kawaida lakini baadaye nikahisi kama maumivu hivi. Nikajipapasa. Nilipoutazama mkono wangu ulikuwa na damu. Nikageuka kujitazama sehemu zangu za nyuma.Maajabu!! Nilikuwa na kovu kubwa sana!! Na palikuwa pamechimbika. He! Ina maana nilikatwa nyama yangu ya…..!! niliduwaa.Maumivu yakazidi. Na sasa giza likazidi kuchukua nafasi yake baada ya mbalamwezi kutoweka. Giza nene!! Hapo bado nilikuwa sijaweza kunyanyuka imara. Nikajaribu kujikunjua nisimame. Maumivu makali katika makalio. Nikaanguka kama mzigo. Nilipoanguka palikuwa na kisu kipya, kikiwa na damu.Nikaendelea kulia. Sauti haitoki.!! Nilikuwa katika jaribio kuu maishani.Ikiwa bado sijaweza kusimama. Lile joka lililopotea njia sasa lilionekana tena. Safari hii lilikuwa linakuja kwangu tena.Bora nife!! Nilijiapiza. Sasa nikaanza kutambaa kumfuata huyo nyoka. Mkononi nikiwa na kisu ambacho nilikiokota, bila shaka ni kile kilichotumika kunikata nyama.Nikawa natambaa kama joka lile linavyotambaa. Sikuwa naijua nia yangu. Lakini nilihisi ni vyema kufa kuliko mateso haya.Lile joka likazidi kunisogelea, macho yake makali yakiangaza huku na huko. Urefu wa joka lile la dhahabu likiwa na kipande cha nyama mdomoni ulinitia kwenye hofu. Nikajiuliza iwapo kisu changu kinaweza kupenya katika ngozi yake, nikajipuuza maana kisu changu kilikuwa kidogo sana. Nikasita kutambaa. Nikatulia tuli, huku nikiamini kuwa ni heri linimeze kistaarabu kuliko kunimeza likiwa na hasira baada ya mimi kujaribu kupambana nalo. Nikafumba macho nikakitupa kisu changu chini, nikajinyoosha tayari kwa kumezwa.Haikuwa ndoto kwamba nikifumbua macho nikutane na mashuka yangu masafi ya kuvutia yakinibembeleza kulala badala yake nilipofumbua macho. Joka kuu hili hapa!!Ubaridi wake ukapenyeza sasa, lilikuwa juu ya mwili wangu, pumzi zikawa zinaniishia. Ndio ninamezwa au? Nilijiuliza.Nikaanza kugalagazwa kadri lilivyokuwa linajivuta. Sasa ile hamu ya kufa ikatoweka baada ya lile kovu langu makalioni kupatwa maumivu makali. Maumivu yaliyosimamisha misuli yangu. Nilipogeuka kujitazama nikakuta kuna mwiba umezama nikajivika ujasiri nikauchomoa. Sikuwa navutwa tena. Nilitazama mbele nikalishuhudia lile joka likienda zake.Inamaana huyu nyoka hakuniona ama!! Nilitafakari. Nikashangaa.Damu zilikuwa zikinitoka tena, sasa haikuwa katika kovu tu, bali na sehemu nyingine. Lile joka lilikuwa limenivuta hadi katika mti wa miiba na ni hapo nilipojitonesha.Pori likatulia kimya, kimya kikawa kirefu sana. Nikawa nahisi kiu kikali. Lakini hapakuwa na maji. Usingizi ukanisaidia kuikwepa karaha hii. Nikasinzia.Mwanga wa jua ndio ulionishtua. Nikakurupuka. Ni uchi!! Nikajishangaa kisha nikawahi kujiziba lakini bahati mbaya hakuwepo ambaye alikuwa ananichungulia. Nilikuwa peke yangu katika pori lile.Hakuna mnyama, hakuna mmea ninaoufahamu, hakuna hata mdudu!! Lilikuwa pori la maajabu, pori la mateso makali kwa kiumbe hai.Nilisimama wima, nikajisikia dhaifu sana lakini sikutakiwa kuendelea kuwa lelemama, nikiwa nachechemea nilianza kuzunguka huku na kule niangalie uwezekano wa kupata msaada. Harakati zangu sasa zikazaa matunda, kwa mbali nilimuona mtu akiwa analima. Alhamdulilah!!Lilikuwa jambo maalumu kwa wakati maalumu. Nikajongea kwa kujikaza hadi nikalifikia lile shamba. Hakika mtu huyu alikuwa mchapakazi. Alikuwa peke yake na shamba lilikuwa kubwa sana.“Kaka!!....Kaka…” Sauti ilitoka kwa taabu, nadhani hakuweza kunisikia.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Nikataka nimsogelee. Lakini ghafla akageuka. Ni kama aliuhisi uwepo wangu pale.Japo alikuwa amechakaa sana. Nguo zikiwa zimeraruka, lakini niliweza kumtambua. Huyu mtu alikuwa ni marehemu. Zaidi ya kuwa marehemu, kifo chake niliwahi kukiota. Basu!!Hakusema neno alipogeuka na wala hakunitazama, ni mimi niliyeiona alama ya 666 kifuani pake. He! Anamilikiwa!! Nilitafakari. Nikatimua mbio. Mbio za kuchecheme ziliniumiza lakini nitafanyaje??Akili yangu ilikuwa sawa kabisa. Nilikuwa namkumbuka vyema Davis. Nilijuta kukutana na bwana huyu katika mtandao na kumuamini sana. Nilijutia na pesa alizokuwa akinipatia.Mara nikaanguka!! Nilikuwa nimegongana na kitu kigumu. Ajabu na kweli haukuwa mti bali mtu. Jesca! Jesca na urembo wake alikuwa amebeba ndoo kubwa ya maji, alikuwa peku na alikuwa amepauka sana. Hata Jesca naye hakunitazama, badala yake aliendelea na safari zake huku akinipa nafasi ya kuitazama alama ya 666 katika mkono wake.“Jesca!! Jesca!!” hakunijibu na dhani hakunisikia. Akatoweka.Sasa sikukimbia tena, ina maana hawa watu hawanioni. Na kamahawanioni hata lile joka halinioni. Nilijiuliza.Kwani kuna kitu gani sifanani nao? Nilipojiuliza hivyo. Nikaikumbuka alama ya ‘666’ iliyokuwa imetolewa katika upande mmoja wa makalio yangu.Alama hii ni ile ninayoijua ama kuna utofauti? Nilitafakari. Jesca huyo akawa ametoweka. Nilipoendelea mbele kidogo nikakutana na kile kisu nilichokitupa. Nikakitwaa. Nikazunguka huku na huko nikiwa uchi nikaipata ile kanga yangu, nikaivaa, wakati naivaa ndipo nilikumbuka juu ya watu wawili niliokuja nao huku katika kujisafisha na alama hiyo mbaya.Nilipowakumbuka nikalikumbuka na kaburi lililokuwa wazi. Nikazungukazunguka na sasa nilikumbana nalo. Huenda walikuwa wamejichimbia kaburi hili. R.I.P na mwenzake walikuwa wamejizika huko.Amakweli wewe ni Roho Iliyo Potea!!! Nilikiri kimoyomoyo baada ya kugundua kuwa sasa RIP amepotea kweli. Nilisikitika kuwa hakuwa amenieleza mambo mengi juu ya alama hizi za maajabu.Jambo moja la muhimu alilonieleza ni kwamba nilikuwa namilikiwa. Kuna mtu alikuwa ananimiliki. Ili nisimilikiwe ilikuwa lazima alama hiyo ifutwe.Sasa nilikuwa nimekatwa kipande cha nyama. Damu ya hedhi hainitoki tena na sihisi kichefuchefu cha mimba. Ina maana ndio similikiwi tena? Na mimba nayo imetoka. Nilishangaa.Lakini sasa mbona siwezi kutoka humu porini? Nilijiuliza sikupata jawabu.Mawazo yangu yalikatishwa na sura ya mtu mwingine aliyekatisha mbele yangu. Huyu alikuwa ni marehemu mwingine ambaye tulisoma chuo kimoja enzi za uhai wake.Hivi niko peponi ama jehanamu? Kwa nini sasa nakutana na maiti tu.Huyu naye hakuonekana kunifahamu. Alikuwa na alama yake sikioni. Nikakumbwa na moyo wa kujaribu. Kama mimi nimekatwa kipande cha nyama na alama imetoweka, nikaamua kujaribu kutumia mbinu ya RIP ambaye sasa ni marehemu.Nikamnyatia yule binti. Nikakiweka kisu changu tayari nikamkaba. Bila kukumbuka maumivu atakayoyapata nikafyeka sikio lake. Nikasisimuka lakini katika nafsi nikikiri kuwa kile kisu kilikuwa kikali sana. Sikio chini!! Yule binti naye chini, akawa anatoa kilio kikubwa sana. Kitu cha ajabu hakuna msaada alioupata. Mimi nikajiweka mbali niweze kuwa shahidi wa nini kitakachotokea.Mara upepo mkali ukaanza kuvuma. Miti ikayumba, pori likatulia na sasa alitokeza nyoka mkubwa, ni yule yule wa awali. Nikataka kukimbia, nikakosa ujasiri nikaendelea kujificha, joka lile likatambaa hadi katika ule mwili unaogalagala, kisha likakwapua lile sikio na kisha kuanza kuzurura huku na huko hadi lilipotoweka ndipo nilipomsogelea yule binti. Alikuwa ametulia tuli na damu haikuwa ikivuja sana.Nikamgusa. Akajigeuza, akanitazama. Mungu wangu!! Tiba inafanya kazi ile. Aliniita jina langu. Akakaa kitako.Sikuwa nikiamini lakini sasa nikampongeza RIP yule tahira niliyemdharau sasa alikuwa njia.“Na wewe umejiua?”“Nimejiua?” nilimuuliza.“Isabela kwa nini uliniua?” alinihoji. Nikashangaa.“Mimi nilikuua wewe.”Yule binti alinieleza kila kitu, akanisimulia alivyouwawa akiwa ndotoni. Akakiri kuniona mimi nikimmaliza huku ninacheka. Akanielezea juu ya sauti alizozisikia. Ni sauti zile zile na mimi nilizisikia katika kifo chake na pia katika mazishi ya yake, hata Jesca alipokufa zilisikika.Niliamini tena kauli ya RIP kuwa kuna mtu ananimiliki na ananifanya anavyotaka yeye kwa wakati wake. Huyu mtu ni nani? Nilijiuliza huku tuhuma za kwanza nikizitupia kwa Dokta Davis.******(OPARESHENI UKOMBOZI)Jenipher alinieleza mambo mengi huku akinisaidia kupata chakula na maji. Chakula kilikuwa kizuri na maji yalikuwa safi lakini namna ya kuvipata ilikuwa ya namna yake. Wakati huo na yeye hakuweza kuonekana.Chakula na maji pekee havikuwa vitu tulivyokuwa tukihitaji. Kikubwa tuliuhitaji ukombozi wetu na wanadamu wengine wanaomilikiwa na watu wabaya.Sasa ilikuwa ni lazima kuuvaa moyo wa ujasiri ili kufanya harakati za ukombozi. Tuliwahitaji wanaume wenye nguvu waweze kuungana nasi.Basu akawa chaguo la kwanza! Tulimtegea siku akiwa katika kulima shamba kubwa lisilotoa mazao.Tulifanikiwa kumpata kwa wakati. Huku tukiwa tunajiamini kabisa. Tulimvaa kwa nguvu akaanguka chini huku akiwa haoni lolote. Anaangaza kushoto na kulia. Nikachomoa kisu.Alama ipo kifuani!! Huu sasa ukawa mtihani. Nichome au nisichome..nikimchoma maana yake ninamuua. Nikabaki kujiuliza.Hali hiyo ya kujiuliza, ikapoteza sekunde kadhaa. Ni katika sekunde hizo, nilimshuhudia Jenipher akirushwa mbali kisha nikamwona nyoka akimshambulia. Nikajitoa katika mwili wa Basu nikiwa na kisu changu nimesimama wima. Nilimshuhudia Jenny anavyohangaika. Na nyoka yule alikuwa ni mdogo sana. Nikajitoa muhanga.Bila kusita mbio mbio. Kisu mkononi huku nikipiga kelele nikamfikia yule nyoka nikamfyeka. Akagawanyika vipande viwili.Jenny akasimama. Hakuwa amejeruhiwa. Tukatoweka mahali hapo. Tukamwacha Basu akiwa katika taharuki asijue nini kimetokea.Hatukuwa tumezungumza lolote. Hadi pale tulipokutana na mwanaume mwingine. Huyu alikuwa ametoka kukata kuni. Tulimpisha njia kisha tukamfata kwa nyuma tukamvamia, akapiga mweleka. Alipojaribu kurusharusha miguu. Alama ile chafu ikaonekana katika paja lake. Bila kujiuliza Isabela mimi nikafanya kama nachuna mbuzi. Nikaikata nyama ya paja lake. Mwanaume huyu akalia kama mtoto.Nilipoiondoa nikaitupia mbali. Baada ya muda akatokea yule nyoka akakichukua kile kipande.Sasa tukazidi kufunguka akili kuwa yule nyoka anawaona watu wenye alama. Na yawezekana ni nyoka huyu yupo katika kuwamiliki wanadamu kwa chapa yake ya hatari.Swali kuu likabaki. Tunatoka vipi katika pori hilo.Mwanaume yule hakuzimia, alikuwa na timamu zake. Tukamweleza kwa kifupi naye akajieleza kuwa, tamaa ya utajiri imemtupia katika shimo hili baya.Yule mwanaume alijitambulisha kwa jina la Samson alikumbuka vyema kuwa kabla ya kufika hapo alikuwa mkazi wa jijini Mwanza na alikuwa mwanafunzi katika chuo cha biashara (CBE) tawi dogo la jijini Mwanza.Huyu alikuwa Samson kweli maana alikuwa ni mbabe sana. Lile kovu lake la kwenye paja halikumsumbua. Tulitembea kidogo akachuma majani fulani akayasagasaga akayaweka katika lile kovu. Hapa sasa aligumia kwa maumivu. Bila shaka ile dawa ilikuwa kali sana.Akaniwekea na mimi katika kovu langu. Nikapiga mayowe. Akanikamata imara. Hadi maumivu yalipotulia kidogo. Jenipher hakutaka kovu lake la sikioni liguswe aliweza kuyakadiria maumivu makali ya dawa ile.Siku mbili zilipita. Kovu lilikuwa linakauka kwa kasi. Nilimshangaa kijana huyu.Siku hiyo ya pili harakati za kujikomboa zilianza rasmi. Jeshi letu bado lilikuwa dogo. Tulihitaji jeshi kubwa zaidi.Samson alituongoza hadi katika ngome ambayo yeye alikuwa akishi hapo kabla. Walioishi katika ngome hii ni wanaume wababe wanaoweza kufanya kazi ngumu. Tuliindia hapa na kuwakuta wanaume sita waliojaa haswahaswa. Kama ilivyo kawaida hawakuweza kutuona japo kila mmoja alikumbwa na hisia za namna yake mwenyewe.Mimi kisu mkononi. Samsoni panga kubwa mkononi, Jenipher kazi yake kukaba kwa bidii zote. Sisi wawili tukawa tunakata tu!!Iwe sikioni hiyo alama. Sikio sio lako tena!!Iwe kwenye mkono. Samsoni anaushusha mzima mzima.Kama ni kiganja. Mimi naondoka nacho kwa kutumia kisu changu. Ikishindikana tu, panga kubwa la Samson linatimiza wajibu.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Waliokuwa wamewekewa alama katika vifua vyao hawa walitupa wakati mgumu sana na tulilazimika kuwaacha wanaume wawili. Wanne tukaungana nao.“Sam kwani we kabila gani?” nilimuuliza wakati tunaondoka.“Msukuma wa Bariadi!!” alinijibu huku akijaribu kutabasamu.Amakweli!! Hana huruma mtu huyu kama vile…kama kabila gani vileee…..Nilipotea katika mawazo nikarejea katika uhalisia. Joka kuu tukapishana nalo. Wenzangu wakakumbwa na uoga. Mimi sikuogopa tena. Nilijua kazi gani linaenda kufanya.Jeshi lilikuwa kubwa sasa na kila mmoja alikuwa na nia ya kuwa huru hivyo tulipambana kwa bidii sana.Mapambano yalikolea sana kwani kila siku tuliongeza timu ya ukombozi.Kilichotutatiza ni kuijua njia ya kutokea. Sasa tukiwa tunajiamini kabisa siku hii hatukutembea kwa kundi kubwa bali kila mmoja alienda njia yake huku akijiamini kabisa kuwa hawezi kuonekana. Nia ikiwa kutafuta njia.Shughuli hii ilianza asubuhi kabisa. Mimi na Jenipher tulienda njia yetu. Huku jeshi jingine nalo likienda njia tofauti.Masaa yakapita na jioni ikawadia. Ile jioni ambayo tulikuwa tumekubaliana tukutane.Tulingoja kwa muda mrefu lile eneo tulilokubaliana tukutane lakini wenzetu hawakutokea.Tulisubiri sana, hatimaye giza likaanza kuiingia. Nikaingiwa na wasiwasi, huenda wenzetu waliipata njia na sasa wapo huru wametusahau sisi. Nilijilaani kwa kuruhusu hali hii ya kila mmoja aende kivyake.“Jenny”“Bela” aliitika.“Unaweza kuwa unajua lolote kuhusu hawa watu.”“Mh!! Kwakweli hata mimi nipo katika mashaka.”“Wanaweza wakawa wamepata njia na kutoroka?” nilimuuliza.“Kama hawajatoroka basi kwenye kambi ya usiku lazima watakuwepo.”“Kambi ya usiku ndio nini?”“Kila usiku wanachama ama wananchi wa mji huu huwa wanaitishwa kitu kama gwaride hivi, tena leo ni gwaride kuu.”“Linafanyika wapi.”“Nitakupeleka Bela. Lakini panatisha sana huko. Na sijui kama patakuwa salama.”“Jenny pawe salama ama pasiwe salama..kwa sasa haina maana ujue bora kufa sasa..maisha gani haya unadhani.”Jenny alikubaliana na mimi, akaniongoza kwenda katika kambi kuu. Kila mtu alikuwa kimya sana. Nilikuwa namfuata Jenny anapoelekea. Hadi tulipoona mahali panafuka moshi“Huko wanakula nyama…na damu pia.”“Kwa mifugo gani sasa?” nilihoji kwa sauti ya chini.“Wananchi wanaotaka kutoroka huwa wananyonywa damu.” Nilishtuka sana kuisikia kauli hiyo.“Na leo kuna mwananchi alitumwa damu kutoka Naijeria, ndio leo anaileta sasa.”“Na wewe umekula nyama ya mtu?” nilimuuliza.“Hapana hizo wanakula viongozi wakubwa tu. Mwananchi ukila ama kunywa damu wanasema unakuwa kama wao. Kwa hiyo hairuhusiwi hata kidogo”Alinieleza kwa utulivu mkubwa.Tukaifikia KAMBI YA USIKU.Shangwe zilikuwa kubwa na watu takribani hamsini walikuwa wakisheherekea.“Ndio watu wote hawa ama kuna wengine?”“Ni hawa tu!! Ujue hii ardhi ndio kwanza ilikuwa imeanzishwa.”Nilikuwa kimya nikiwatazama watu kwa mbali tulipojificha. Nilimuona John, nikamtambua na Jesca. Baadaye kila mmoja akatulia kuna mtu alitaka kuzungumza neno.“Leo raisi atakuwa amekuja. Isabela tuyondoke hapa.”“Raisi ndio nani?” niliuliza kwa jeuri. Kuna kitu kama hasira kilikuwa kimenikaba kooni na sikuhisi uoga hata kidogo.“Mkuu wa Nchi hii. Huwa haoneshi sura yake lakini anaitwa mtukufu raisi.”“Na yule anayeonekana ni nani?”“Yule tulitambulishwa kwake kama waziri wa miundombinu…njia zote anazifahamu yeye.”Niliposikia hivyo nikatamani sana kumtia mikononi, mtu yule aliyeitwa waziri wakati namfahamu kwa jina la Osmani!! Huyu alikuwa ni Osmani mwanaume aliyenipatia namba ya simu 6666666. Na ni huyu huyu aliyenijia ndotoni akiwa na John wakimkwapua mama yangu mzazi.Sikuwa na uoga. Nilipiga hatua sasa nikawa nimejichanganya na watu hawa wachache waliokuwa wakimtumikia shetani.Osmani alikuwa akiongea kwa maringo na kutumia amri sana.Kila mtu alikuwa anamsikiliza.“Leo damu ipo nyingi, nyama za kusaza.”“Manson, Fanson, Rinzon, Wenton, Zeiron.” Alitaja vitu nisivyovijua na kila alipotaja kuna mtu aliitika na kwenda mbele. Walikuwa wanaume watano waliojaa vyema.Bila shaka walikuwa wanaujua wajibu wao. Niliwaona wakizichukua kamba nene kabisa. Pamoja na visu.Walitulia kwa dakika kadhaa, mara wakaletwa mbele yao watu ambao walionekana wazi kuwa walikuwa wamechoka sana.Nilimuona Samson akiwa amevimba sana kutokana na kipigo. Hasira ikanipanda. Nikatulia tuli!!Wanaume wale walioitwa kwa majina ya ajabu wakatumia kamba zile kutengeneza namna ya vitanzi, kisha wakavitundika mtini.Mwanaume mmoja akamchukua mvulana kutoka katika lile kundi. Mvulana yule hakuwa na sikio. Nikamkumbuka ni mimi niliyemkata ili kumtoa katika ulimwengu huu wa giza.Nikiwa sijatafakari nini cha kufanya, nikashuhudia damu ikikingwa kutokea shingoni. Kisha akatupwa katika kitanzi. Alikuwa maiti!!Samsoni akavutwa akataka kuleta ukorofi. Akachapwa na mjeledi akapiga yowe kubwa huku akitukana matusi mazito mazito kwa kabila la kisukuma.Alipotukana akanikumbusha wakati aliokuwa ananiambia jina lake. Nikajisikia uchungu.Liwalo na liwe!! Nikaanza kusogea mbele. Bado Samson alikuwa akiwasumbua. Maajabu nikafika mbele ya hawa wanaume hawakuweza kuniona. Nikajaribu kumsukuma mmoja aliyekuwa na kisu tayari kwa kumchoma Samson. Haya yakawa maajabu makubwa. Isabela mimi namsukuma mwanaume mkubwa kama yule anaanguka kwa kishindo hivyo. Samson mwamba wa kisukuma, msukuma kutoka Bariadi akafanya jambo ambalo hadi leo ni kumbukumbu kwangu. Haraka akaokota visu viwili, akavimba kwa hasira kifua chake kikaweka mfereji mkubwa. Samsoni alikuwa amevimba kama mcheza mieleka.Nikabaki kushangaa. Akamrukia mwanaume mmoja sijui ndio Frazon, Manson ama vipi. Kisu kimoja. Mwisho wa uhai.Akakichomoa akamrukia yule ambaye alikuwa chini baada ya mimi kumsukuma. Visu viwili vikazama katika sehemu zake za siri. Damu ikaruka. Nikasisimka sana!! Samson hakujali.Sasa yule Osman akawa ametaharuki. Hajui nini kinatokea. Na yeye hakuwa ananiona. Nikamwona akimjaribu kumfuata Samsoni huku akiwa na jambia. Samson hakuwa anamuona.“Saaam!! Saam!! Nilimuita.” Maskini hakunisikia.Osmani na jambia. Akalichomoa mahali ambapo linahifadhiwa.Akalielekezea alipo Samson. Alipoanza kukimbia na mimi nikashtuka nikaanza kukimbia. Kabla hajamfikia. Mimi nikamfikia. Nikafanya kumsukuma. Akapepea kama karatasi. Takribani mita arobaini kutoka pale nilipokuwa. Samson alipogeuka, hakunitazama mimi bali alitazama chini. Akakumbana na jambia.Msukuma huyu mkali kabisa wa mapambano akatupa visu chini akatwaa jambia.Ilimchukua dakika chache. Manson, Fanson, Rinzon, Wenton, Zeiron. Wote wakawa tayari kwa kuzikwa kama hiyo nchi yao ina huo utaratibu wa kuzika.Samson alikuwa kidume!! Nilikiri.Kidume yule ambaye hakuzisikia sifa nilizokuwa nampa. Alizidi kunidhihirishia kuwa kile kifo cha yule mvulana cha kuchomwa kisu shingoni kilimuuma. Aliendelea na zoezi la kuwaondoa wananchi kadhaa kwa fujo zile alama za 666 popote zilipo katika miili yao. Ilimradi tu hakuwaua.Nia ikiwa kukuza jeshi letu!!Nami nikamuunga mkono!! Jenny naye huyo akaokota kisu kikubwa kaanza kufanya kazi.Tulilolifanya hapo lilikuwa kosa kubwa sana. Alama za 666 zilizokuwa zinaanguka katika mfumo wa vipande v ya nyama. Ukaleta balaa.Joka kubwa kuliko lile la awali likaibuka. Joka hili sasa lilikuwa halijulikani wapi mbele na wapi nyuma.Lilikuwa na vichwa viwili. Mbele na nyuma.Halikujulikana linatambaa kwenda kaskazini ama kusini, magharibi wala mashariki.Yule bingwa wa mapambano Samson akajikuta analiachia jambia lake, Jenny aliyekuwa anaanza kunogewa na shughuli ya kukata nyama za watu naye akatulia tuli.Nami nikakumbwa na uoga na nikakiona kifo kikibisha hodi.Isabela nakufa!! Nakufa nikiwa katika u…”Kabla sijamaliza kuwazua. Ghafla……..Ghafla!!!!!Ilikuwa ghafla sana!!!!Joka lilijinyanyua juu. Sote tukawa chini yake. Joka lenye rangi ya dhahabu!! Sasa ikawa patashika kila mtu analazimisha kujificha nyuma ya mwenzake. Hakuna aliyetaka kufa. Mimi, Jenipher na wale wengine waliokuwa wanatambua yule nyoka amekuja kufanya nini pale tulijiweka mbali na vile vipande vya zile nyama zenye namba 666.Joka likavimba kama linataka kutema sumu. Likavimba zaidi kama linataka kupasuka. Hatimaye likautoa ulimi nje. Likatanua mdomo kama linataka kutumeza sote. Kisu chan gu bado kilikuwa mkononi.Mara likajirusha na kujizungusha kama pangaboi. Hapa hakuna kitu kilichosalia. Kila mmoja wetu alirushwa mbali kabisa. Mimi sikuumia lakini wenzangu waliumizwa.Nilipogeuka nilimwona kiumbe akiwa amelowa damu akiwa na jambia mkononi. Alikuwa akikimbia mahali ambapo joka lipo. Alikuwa ni Samson yule jasiri wa kisukuma.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Macho yako yalifumba kisha yalipofumbua alikuwa ameingia mzimamzima katika kinywa cha yule nyoka. Jambia na yeye wakawa wamemezwa.Hali ya hatari!! Nilijitahadharisha.Joka lilikuwa linameza vile vipande vya mabaki ya nyama yenye chapa ya 666. Ndipo hapa nilimuona tena yule Osmani aliyetambuliwa kama waziri wa miundombinu. Nikakumbuka kuwa ni huyu bwana nimeambiwa kuwa anazijua njia zote za kutoka katika mji huu wa kishetani. Nikamnyemelea huku nikiwa makini na yule joka na pia nikiwa makini asiweze kuhisi chochote kile.Nikamfikia nikamkaba shingoni. Nilikuwa na nguvu za ajabu sana. Nikamvuta hadi katika kichaka nilichokuwa nimejihifadhi hapo.Hakuwa ananiona!! Jambo hilo lilinipa nafasi nzuri ya kumtawala. Kwa ukombozi wa wengi na kujitoa katika adha ya kufia katika mji huo. Nikanyanyua kisu changu nikazamisha katika paja lake. Akatoa kilio kikubwa sana. Kilio kile kikasababisha lile joka linyanyuke mara moja. Likaanza kuangaza huku na huko. Nami nikatulia tulii kuangalia nini kinatokea. Joka likanyanyuka kisha likatanua midomo yake. Kisha likionekana dhahiri kuwa na hasira lilitapika. Maajabu!! Samson yule jasiri katika vita hiyo akatangulia kisha jambia lake likafuata.“Njia ya kutoka hapa ni ipi?” nilimuuliza Osman huku bado akiwa katika himaya yangu.“Sijui.” Akanijibu kwa jeuri. Nikamchoma tena kisu katika sehemu ileile kilipopitia awali.“Nasemaaaaa!” akapiga kelele.“Dakika moja tu nakupa sema upesi.”Osman akaanza kutoa maelekezo ya namna gani ya kutoka katika kijiji hicho cha maajabu!!Maelezo yalikuwa yamenyooka!! Japo yalikuwa na masharti. Sikuwa na budi kuendelea kumshikilia. Ni huyu angetuwezesha kutoka.Joka lilizidi kuhangaika.Sasa lilitazama mahali alipokuwa Osmani na mimi. Likatambaa kwa hasira kali sana likawa linatufuata. Nikajikuta namuiachia Osmani. Nikaanza kukimbia. Joka likawa linaufuata uelekeo wangu.Mungu wangu!! Kumbe linaniona sasa hivi. Nimekwisha.Nilizidi kutimua mbio. Hatimaye mbio za sakafuni zikaishiaukingoni! Nikaanguka chini. Joka nalo hilo likanifikia.Likaachama mdomo wake mkubwa.Sasa nakufa! Nilikubali yaishe.Achaaaaaa!! Nilipiga kelele za mwisho za kutokwa na roho. Huku nikitegemea zitakuwa kelele za mwisho. Haikuwa hivyo. Niliweza kuwa hai tena. Joka lilikuwa limeufumba mdomo wake. Likatulia tuli.Nikaduwaa kulikoni nyoka huyu hajanimeza. Au! Au! …nikakosa majibu.Joka likaendelea kutulia kama lina urafiki na mimi. Kwa uoga nikasimama na kuanza kutambaa taratibu. Joka limetulia halina habari. Nikasimama. Bado tuli! Nikaanza kuondoka hadi nikatokomea! Nyoka ametulia.Maajabu makubwa sana haya!!*****Nilirejea hadi kule walipokuwa wanakijiji wenzangu. Osmani alikuwa amehitisha mkutano tena. Alionekana mwenye furaha sana na ni kama alikuwa anatoa karipio kali.Samson niliyedhani amekufa kumbe alikuwa amezimia tu baada ya kutemwa na yule nyoka. Nilimkuta akiwa amefungwa kamba nyingi sana. Bila shaka adhabu yake ilikuwa imewadia.Nilimuona Jesca pia. Lakini John pekee ndio nilikuwa sijamuona.Nilikuwa na hasira. Nikatumia ule mwanya wa joka kutulia. Nikamvamia Osmani. Nikamkaba tena. Safari hii sikutaka mambo mengi sana, nilihitaji njia ya kutokea.“Wakati wa kuwa watumwa wa shetani umekwisha. Tunatakiwa kuishi maisha yetu tuliyoshi awali. Manyanyaso haya yote na yasiendelee. Tusikubali kabisa uonevu huu. Sasa tunatoka humu. Kila mwenye nia na aungane nami sasa. Tunatokaa!!” niliunguruma kwa sauti kuu. Wale wasiokuwa na Chapa walinisikia na kuniona. Wale waliokuwanayo waliduwaa wasijue kinachoendelea.Samson alifunguliwa kamba alizokuwa amefungwa. Sasa Osmani akawa anatuongoza kuielekea njia ya kutokea.Chapa ya 666 ilikuwa katika mkono wake wa kuume.Kijiji kilikuwa kikubwa sana. Tulipenyeza njia hadi njia bado hatukufika tulipokuwa tunahitaji.Sasa tulifika mahali palipokuwa na majani makavu lakini laini sana. Tulipokuwa pale. Osmani akaniponyoka. Kisha akapiga mluzi fulani hivi. Wakatokeza kenge wa ajabu. Wakubwa kama mamba. Walikuwa wanne. Na dhahiri walikuwa na njaa. Walishambulia katika namna yha ajabu na upesi sana.Waliua! Watu kumi wakaanguka chini. Mamba wale badala ya kula nyama wakawa wananyonya damu.Ilikuwa zamu yangu sasa. Osmani alikuwa pembeni akitucheka. Kuna unga fulani alijipaka usoni, sasa aliweza kuniona vizuri.“Achaaaa!!” nilijikuta natamka neno lililoniokoa midomoni mwa joka lile kuu. Kenge hawa wa ajabu wakatulia palepale wakafunga vinywa vyao. Osmani akashangaa na mimi pia nikashangaa.Samson ambaye naye alikuwa amekata tamaa alishangaa.Nikawahi kuipoteza hali yangu ya kushangaa. Nikamwendea Osmani. Nikamkaba tena. Nikampiga makofi mawili akaanza kutema damu.“Njia ya kutokea!!” niliamuru.Akageuka, akatunyooshea mkono. Palikuwa na mlango mdogo wa mbao zilizooza. Nikawaamuru wanakijiji wsaliosalia wapite. Wakapita!!Hadi walipomalizika ndipo mimi na Osmani tulipita. Kabla hatujamaliza kupitia nilisikia kilio kikubwa. Kuna mtu alikuwa akiniita.Sauti ile ilikuwa ya John!Nikasita kutoka. Nikarejea nyuma niweze kuchungulia.John alikuwa anagalagazwa na lile joka kubwa.Huruma na mapenzi yangu kwa John ikanijia. Nikaweka kando yote aliyowahi kunitendea. Nikarudi kwa kasi. Neno acha likiwa mdomoni mwangu. N ilipofika nikaamuru kwa sauti kuu. Joka lile likatii kwa nidhamu. Nikaduwaa. Nikamchukua John na kuanza tena kuitafuta njia ya kutokea.Kosa kubwa! Nilimuacha mbali waziri wa miundombinu!Osmani akawa amepotea! Sikujua ni wapi pa kupita.John hakuwa akiniona wala kunisikia. Nilitamani ajue ni mimi nipo naye. Lakini haikuwa hivyo.Nilifanikiwa kukipata kisu. Nikaamini sasa nitaiondoa alama ya 666 katika mwili wake na ataweza tena kuona.Hofu! Na kukata tamaa. John alikuwa na alama ile shingoni mwake. Mwili ukafadhaika.Siwezi kumchinja John!! Siwezi!! Niliapa.Lakini nitafanya nini sasa.Kitu kama tetemeko la ardhi likatwaa mawazo yangu. Nikamvuta John asiyejielewa nikamkumbatia. Tetemeko hilo lilivyopita hapakuwa tena na lile joka.Lakini kitu kipya kikajitokeza. Ulikuwa mwanga mkali kama jua vile!! Nikatafakari ni kitu gani hicho. Sikuweza kutambua.Mara ule mwanga ukapotea. Nikaja kushtuka nimepigwa kibao katika shavu langu. Nikaanguka.Niliposimama nikapigwa tena, na sikumuona kiumbe aliyekuwa ananifanyia hivyo.Mapigo yakaongezeka. Nikawa navuja damu.Sikuweza kusimama tena.Sauti ya Jenipher ikanijia kichwani, “Ukinywa damu unakuwa kama wao!!”Maneno hayo yakanifanya nipatwe na ari mpya. Nikatambaa nikamfikia John.Badala ya kumchinja! Nitamnyonya damu walau kidogo tu.Nikamfikia. Nikamkamata. Akaanguka chini, nikajirusha shingoni mwake. Nilipoifikia shingo yake nikamkumbuka yule mganga wa kinaijeria. Hapo sasa nikakumbuka sio mara yangu ya kwanza kunywa damu. Nikapenyeza meno yangu pale pale kwenye alama ya 666 aliyopigwa shingoni.Damu ikaanza kutoka. Nikaimeza huku nikiwa nimeikunja sura yangu.Nguvu za ajabu zikaniijia.Amakweli wa giza pambana naye kigizagiza.Sasa niliweza kumuona adui yangu aliporejea tena. Alikuwa ni Dokta tuliyekutana katika mtandao, alikuwa ni Dokta Davis.Alikuwa ananisogelea tena aweze kunipiga. Nikaudaka mkono wake. Akataka kujitoa hakuweza. Nikaweka sawa kisu changu nilichokuwa nimekificha kwa nyuma. Nikazamisha katika sehemu zake za siri huku nikipiga kelele.Akaanguka chini na kuanza kujirusharusha.Nikamkumbuka yule ninja wa kisukuma, Samson ambavyo hakuwa na huruma. Na mimi nikamuiga. Nikamrukia Davis na kuanza kumchoma visu.Nilimchoma kwa fujo zote.Nikafadhaishwa baada ya yule Davis ambaye sasa niliamini naenda kummalizia alipogeuka kuwa joka kubwa la kijani. Haraka nikawahi kujitoa lakini nilikuwa nimechelewa sana. Joka lile likawahi kujiviringisha kuanzia kiunoni likawa linapanda juu. Sasa lilikuwa limenifunga hadi kifuani.Ajabu!! Lilikuwa linawasha sana nilitamani kujikuna lakini haikuwezekana na mikono ilikuwa imefungwa tayari.Nililiamuru liniachie lakini halikuiheshimu amri yangu. Nikazidi kuwashwa, nikajaribu kujigalagaza, haikuwezekana. Sasa likaanza kujikaza, muwasho ukaenda likizo, maumivu yakaingia kati. Lilizidi kukaza, mara likaongeza kujiviringisha hadi likaniziba usoni. Kifo kikanukia harufu ya kukera.Nikabaki jicho moja tu kuona nje!! Viungo vingine vyote vilikuwa vimefunikwa. Sikuwa na ujanja. Jicho langu likamuona John akiwa ameshangaa kama tahira. Nilijaribu kutoa sauti haikutoka, nilikuwa namwomba John kwa mara ya mwisho aweze kuniokoa. Hakuweza kunisikia.Nikatazama juu nikakutana na mawingu yenye rangi inayoshabihiana na buluu, nikaikumbuka rangi ya mtandao wa kijamii. Ni huku nilikutana na Dokta Davis. Akanipa zawadi ya utajiri, akanipatia kazi nyepesi inayonipatia kipato kikubwa. Nikamuamini sana. Sasa alikuwa amegeuka joka kubwa na lilikuwa linaniua.Hakika lazima nife!! Jitihada zangu zote hazikuwa na maana tena.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/John hakuwa msaada wowote kwangu. Na hakuwepo mwingine wa kunipa msaada.Nilipofikiria ni nani mwingine wa kunisaidia akili yangu ikarejea kwa mwalimu Nchimbi. Mama yangu mzazi. Nikajaribu kuita sauti haikutoka. Mama naye hakuwa na msaada katika hali hii.Nikayakumbuka maneno ya mama. Miaka mingi sana nikiwa mdogo aliwahi kunikambia maneno.“Yupo mtu anakusikia hata usipotoa sauti.” Hili lilikuwa jibu alilonipa baada ya kumuuliza iwapo mabubu na viziwi wanaweza kuzungumza na Mungu. Jibu lake hadi ukubwani halikunitoka.Nami sasa nilikuwa bubu. Jaribio la mwisho kabisa ni kuzungumza na yule anayesikia wakati wote. Ajuaye unachokiwaza. Kila wakati, mahali popote.Mungu!“Eeh! Baba sijui kama nilistahili adhabu hii. Na kama ilikuwa stahili yangu baba. Nichukue kwako sasa. Nimeumia na IMETOSHA.” Nilizungumza katika nafsi yangu. Kisha nikasubiri kuiaga dunia hii chungu.(HARAKATI NDOLLA ZAMBIA)Nilijikuta naifuatilie ile njia tuliyopita awali hadi nikaufikia ule mlango. Nikamtanguliza John nami nikatoka.Maajabu mengine. Niliwakuta wale waliotangulia wakiwa katika sintofahamu wasijue nini cha kufanya.Kwa kukadiria muda ilikuwa saa sita mchana. Na tulikuwa katika ulimwengu halisi lakini hatukutambua ni wapi hapo tulipo.Magu, Bariadi, Sumbawanga, Songea!! Kila mtu alifanya utabiri wake.Hatukuendelea kukaa pale. Tukaanza safari kuelekea tunapoelekea bila kutambua ni wapi.Baada ya kilometa takribani sita tukaingia kijijini.Mimi nikiwa na upande wa kanga pekee. Wenzangu wakiwa na nguo zilizochakaa sana. Tukakiona kijiji. Baadaye tukaanza kukutana na watu.Kila mtu akiwa na lake la kufanya. Hakuna aliyetuuliza swali. Walikuwa weusi sana, wengine walifanana na nyani huku wanawake wengi wakiwa na maziwa makubwa.Ni wapi sasa hapa? Nilijiuliza.Tulitamani sana kuzungumza na watu hawa lakini hawakuwa wakarimu.Njaa iliuvunja uamuzi wetu wa kusubiri watuanze. Njaa ilituuma na hatukuwa na chochote cha kuweka tumboni.“Ha…habari..”“Nkesuu…” sijui kama aliniuliza ama alinijibu salamu.Lugha ya wapi hii!! Niliwahi kusikia mahali, ni wapi vile. Niliumiza kichwa. Kila mmoja alikuwa ananitazama mimi kama mwokozi katika mapambano haya.“Me come great…” nilizungumza kiingereza kibovu ili nipate kujua wanazungumza lugha gani na ni watu wa wapi. Hakunijibu akanikazia jicho kwa shari. Ni hapo nikapata jawabu sura hizi nimewahi kuziona wapi. Ni kwenye basi. Siku ya safari yangu kuelekea Ndolla Zambia kwa Dokta Davis kusaini mkataba ule ulionifikisha hapa nilipo.“Sam…it’s either Congo or Ndolla….(Sam ni aidha Kongo ama Ndolla)” nilimnong’oneza yule msukuma.“Ndolla??”“Yes! Ndolla Zambia..” nikamjibu. Akashangaa. Yule bwana tuliyemuuliza akawa amesonya na kutoweka.Watu hawa sio wazuri hata kidogo. Wameathiriwa na vita za wao kwa wao. Wakitugundua ni hatari. Naamuru!! Hakuna mtu kuzungumza na mgeni yeyote, I WILL!!! Nilitoa tamko kama amiri jeshi mkuu wa mapambano hayo.Kila mmoja akanielewa.Safari ikaendelea, tulikuwa tumechoka lakini tuliuhitaji sana ukombozi, tulihitaji uhuru wetu.NDOLLA TOWN 40 KM AHEAD. Kilisoma hivyo kibao kigumu cha chuma. Nikajipongeza katika nafsi yangu kwa kuwa na kumbukumbu nzuri.Jesca alikuwa mtu wa mawazo mazito. Hakuwa akiongea na ule urembo wake wa enzi zile haukuwa na nafasi hapa. Pia ugomvi wetu wa kumuwania John kimapenzi haukupewa nafasi pia. Kila mmoja alitazama anajikomboa vipi.Tulitembea kimafungu mafungu. Jumla tulikuwa watu ishirini na moja lakini, tulikuwa kama hatufahamiani. Kila mmoja na lake. Likitokea la kuzungumza nilikuwa nachukua nafasi hiyo.Tulipoufikia mto, kila mmoja aliyatumia maji anavyoweza, wengi walikunywa na wachache walioga. Pumziko la dakika ishirini kisha tukaendelea mbele. Tukaufikia mti wa maembe. Hapa sasa kila mtu alikula kulingana na ukubwa wa tumbo lake. Angekuwa mjinga ambaye angeacha kubeba akiba ya maembe matamu ya Zambia.Sasa kasi ikaongezeka na mazungumzo yakaibuka. Njaa kitu kibaya sana.Mimi na John tulikuwa tumeambatana. Ile hali ya yeye kutoniona iliniumiza sana lakini sikuwa na namna.Kilometa zikazidi kukatika, tulitembea hadi usiku, kwa kukadiria tulitumia masaa yanayozidi kumi. Kuzikamilisha zile kilometa.Mji wa Ndolla ukatukaribisha. Ulikuwa mara yangu ya pili kuja katika mji huu na mara ya kwanza kufika nikiwa katika matatizo.Nilijipongeza tena kwa tabia yangu niliyoionyesha siku ya kwanza. Tabia ya kushangaa shangaa. Hivyo kuna baadhi ya vitu nilivikumbuka. Hadi tukaipata stendi.Kama nilivyoamuru kila mmoja alijitenga kama hatujuani. Kanga yangu ikiwa imefungwa vyema. Ni hiyo pekee ilikuwa ngao yangu. Nikaingia katika stendi ile ambayo ilikuwa inazidiwa hadhi na stendi ya Ubungo jijini Dar es salaam katika nchi yangu ya Tanzania.Nilizunguka hapa na pale. Nikaiona ofisi ya magari ambayo nilikuwa naitaka.“Mambo vi wewe…inakuwaje…mishemishe vipi…oya acha kuzingua…” maneno haya yalikuwa yanazungumzwa katika ofisi hizi.Nikainama chini jicho langu la kulia likatangulia kumwaga chozi la kushoto nalo kwa uchungu likamwaga chozi. Nikajiinamia chini nikalia kwa uchungu mkubwa. Uchungu wa kuikumbuka nchi yangu Tanzania. Kilio hichohichoi kwa namna ya kipekee kilikuwa kilio cha furaha. Ndio lazima nifurahi. Sasa ningeweza kumvuta mtu na kuzungumza naye Kiswahili.Ni hivyo nilifanya. Mwanaume kipande cha mtu akavutika kunisikiliza. Kwanza sikutaka kumuelezea kuwa tupo wengi. Niliitetea nafsi yangu. Nilikuwa natetemeka kwa baridi. Akanipatia sweta zito nikajistiri. Nikajielezea kuwa nimepotezana na bwana aliyenileta Zambia.“Umesema wewe mwenyeji wa Makambako.”“Ndio kaka.”“Makambako sehemu gani hiyo?”“Ni karibia na stendi kuu. Hapa Magegele …..”Alaa Magegele napafahamu sana huko…kabla ya kuhamia huku nilikuwa naenda na mabasi ya Dodoma Mbeya…sasa hapo Magegele kuna mgahawa tulikuwa tunakula tulimzoea sana yule mama kiukweli..hata wewe nikutajia lazima utakuwa unamjua..”“Mama Kesho.” Niliwahi kumjibu. Akacheka sana, hakuna mtu wa Makambako ambaye hakumjua mama huyu. Alikuwa mkarimu sana.Tulizungumza mambo mengi usiku ule. Alizungumza nami kwa ukarimu. Ni nani alikwambia kuwa watanzania sio wakarimu.Kuna tofauti kubwa kati ya mtanzania na mbongo!! Mtanzania ana utu lakini mbongo anajifanya mjanja mjanja. Huyu bwana alikuwa mtanzania haswaa.Upesi nikapata chakula. Kisha akaingia ndani akatoka na nguo. Zilikuwa za kike.Akanieleza abiria huwa wanasahau nguo zao na kamwe hawarudi tena kuzichukua. Nikamshukuru. Akanipatia na kiasi cha pesa. Akaniomba nirejee majira ya saa tano asubuhi aweze kunifanyia utaratibu wa kunisafirisha kurejea Mbeya kisha Makambako Iringa.Ilikuwa bahati ya kipekee sana kupata msaada huu. Lakini hapo hapo ilikuwa bahati mbaya sana maana nisingeweza kusafiri peke yangu. Na yule bwana sikumueleza tupo wengi zaidi ya kikosi cha timu ya mpira wa miguu.Ubarikiwe sana!! Nilimpa Baraka hizo.Kisha nikiwa na mavazi kamili sasa. Nikapiga hatua kwa hatua. Kigiza giza kikanifanya nionekane kama kivuli. Mkono mmoja mfukoni kuzilinda Kwacha (Pesa halali kwa matumizi ya Zambia) nilizopewa, mkono mwingine ukiwa umeshika kiroba cha nguo nilizopewa na yule bwana. Isabela nikiwa na raba nyepesi miguuni. Nikatoweka huku nikiamini nina mzigo mkubwa wa kuwaokoa rafiki zangu ambao walinitazama kwa jicho la huruma.Nilijihesabu kama mshindi wa vita ya 666. Lakini bado nilikuwa na vita nyingine ya kurejea nyumbani.Mshindi akifia ugenini huyo ni mshindwa lakini akirejea nyumbani hata kama amejeruhiwa vipi bado ataitwa mshindi.Mapambano yameanza rasmi!!! Nilikiri huku nikiwa nayatamani hayo mapambano ambayo yatakuwa magumu kushinda vita ya joka kuu la msituni.Nilimchukua Jenipher, Jesca na Samson. Kikawekwa kikao cha dharula. Mada kuu ikiwa tunatoka vipi.Nilimpatia Jenipher na Jesca baadhi ya nguo. Wakajihifadhi.Mazungumzo yalikuwa marefu sana na pambazuko lilikuwa linakaribia. Mengi yalizungumzwa na sasa tukawa tumefikia katika maamuzi mawili. Kubwa kabisa likawa kukimbilia ubalozini kupata msaada.Wazo la kupata simu tuweze kufanya mawasiliano nyumbani pia lilitujia vichwani!! Lakini hatukulitilia sana maanani katika nchi za kigeni. Tulitaka tufike kwanza Tanzania ndipo tufanye mawasiliano.Ubalozini!! Hiyo ndio ikawa mada.Lakini swali likaja kwa John ambaye bado alikuwa na alama 666 na hakuwa akionekana. Lakini kama hiyo haitoshi, tukapata hofu ya usumbufu wa maswali mengi kutoka kwa chombo husika kitakachokuwa kinahusika na mambo ya uhamiaji.Kwa jinsi tulivyokuwa wengi tuliamini kuwa itatuwia ngumu sana kupata msaada upesi. Pia ubalozi wa Tanzania katika nchi ya Zambia ulikuwa una makao yake Lusaka. Mji mkuu wa Zambia.Hilo lilikuwa gumu sana. Tulikuwa tunahitaji pesa. Pesa!!Kama tukipata pesa tunaweza kupanda mabasi yatakayotufikisha Mbeya. Hapo sasa tutakuwa katika ardhi salama ambayo tunaweza kupata msaada.Pesa tutaitoa wapi? Hilo likawa swali.Tukakubaliana kuingia katika mapambano ugenini. Mimi, Jesca, Jenipher na Samson. Tukafunga mjadala.Asubuhi ikazidi kujongea. Hapa sasa nikachukua maamuzi. Nikatembelea kundi moja baada ya jingine. Nikawapatia chakula kidogo kidogo nilichonunua kwa kutumia pesa niliyopewa na kaka yule wa kitanzania. Huku katika kila kundi nikiwapa moyo kuwa tumekaribia kuondoka kurejea nyumbani.Siku iliyofuata kila mtu alikaa kwa tahadhari bila kuzungumza na raia wa Zambia.*****Majira ya saa nne asubuhi nilikuwa katika ofisi ya yule mwanaume wa kitanzania aliyeahidi kunisaidia niweze kufia Mbeya. Nilimkuta akiwa amebanana kulingana na majukumu. Nikatulia mpaka alipomaliza. Nikaingia.Alinichangamkia sana. Akamkabidhi mwenzake ofisi akanipeleka mgahawani. Chai ya maziwa na chapatti nzito kabisa.Mazungumzo yakiendelea!!!CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Akanielezea mpango wake huku akinisihi niwe mvumilivu katika safari maana patakuwa na tatizo la kuhamishwa siti na wakati mwingine kukosa kabisa pa kukaa maa nitasafiri kama ‘staff’. Hilo halikuniumiza kichwa sana, maana niliamini naweza kusimama cha msingi nia yangu kutimia. Kilichoniumiza kichwa ni hawa wenzangu. Itakuwaje!!Nilimshukuru yule bwana. Akanipatia namba yake ya simu. Ni hapo nilimtambusa jina lake aliitwa Saidi.“Ukinipigia simu we niite Side boy.” Aliniambia wakati ananiaga.Alinipatia kiasi kingine cha pesa.Nilishukuru kwa kuzaliwa mwanamke maana bila hivyo sidhani kama ningepata msaada.Jioni ilipofika. Jesca hakuwa ameambulia lolote. Na Sam hadi wakati huo hakuwa amerejea. Tukajipa moyo kuwa huenda amefanikiwa kupata kibarua chochote huko alipo. Ikafika giza nab ado Sam hakuwa amerejea. Hofu ikaanza kutuingia na kuamini kuwa Sam anaweza kuwa aliongea Kiswahili na kugundulika kuwa ni mtanzania asiyekuwa na uhalali wa kuishi Zambia.Hatukujua kuwa ni wapi tuanzie kumtafuta. Kama tukisema twende polisi na sisi tutakuwa matatani. Tatizo jipya!!Jesca na Jenipher wakawa wananisikiliza mimi.Kimya kikatanda!! Makundi mengine hayakujua nini kinaendelea.Nilijiuliza maswali mengi sana bila kupata majibu. Samson amefanya jambo gani la kitofauti hadi wakati huu hajarejea.Au amerejea tena katika kijiji cha Dokta Davis. Niliwaza peke yangu bila kumshirikisha mtu yeyote hisia zangu.Saa nne usiku nilikuwa nimepitiwa usingizi.Nilisikia kama natikiswa nikadhani ni Jesca amejigeza lakini nilikuwa naendelea kubughuziwa. Japokwa nilikuwa nimelala chini niliutamani usingizi.Nilijikaza nikafumbua macho.Usingizi ukakatika palepale. Alikuwa ni Sam!!“Bella!! Bella!!” alinong’oneza. Nikamtazama usoni nikahisi kuna nhali ya tahadhari. Nikajipa utulivu wa lazima.Akanishika mkono akaninyanyua. Akanivuta pembeni kidogo.“Ulikuwa wapi Sam.”“Bwana Mkubwa!!.”“Kafanyaje…ndio nani?” nilitaharuki.“Sio mtu ni sehemu inaitwa hivyo.”“Pamekuwaje…”“Nimekutana na mtu!! Aah!! Nimemuona mtu….amepata madini.”Bado sikuweza kumuelewa Sam anamaana gani. Nikamuomba anielezee kwa kirefu.Akanieleza juu ya mgodi wa Bwana Mkubwa ambao upon je kidogo ya mji wa Ndolla. Mgodi huu alipoutaja tu! Sikuwa na swali lolote. Nilikumbuka somo la Historia kidato cha pili hadi cha tatu. Mgodi huo ukanikumbusha madini hadimu ya Risasi (Copper) ambayo hupatikana kwa wingi katika nchi ya Zambia. Hasahasa Ndolla.Sam akaendelea kunielewesha. Na sasa akanigusia juu ya bwana ambaye amepata madini hayo siku hiyo.“Kwa hiyo ulikuwa huko.”Akanijibu kwa kutikisa kichwa juu na chini akimaanisha kuwa ni kweli alienda ‘Bwana Mkubwa’.Samson alikuwa amekuja na habari ambayo mwanzoni nilikuwa ninapingana nayo lakini hatimaye kulingana na shida tuliyokuwanayo nikaamua kukubaliana naye. Wizi!Samson alinihakikishia huyo bwana ana pesa nyingi sana. Amefuatilia nyendo zake hadi alipofanikisha kuyauza yale madini.“Alinipa lifti kwenye gari yake. Nilijifanya sijui lolote lile. Aliponishusha mjini nikamfatilia na kumuona aliyauza.”“Sasa tunampata wapi?”“Yupo anakunywa pombe sasa hivi. Ni hapo pekee pa kumkamatia.” Alinisisitiza.“Nzuri zaidi ni mtanzania…” alinisisimua kwa kauli hiyo. Nikamwomba Mungu huyo bwana asiwe na tabia za kitanzania bali awe mbongo.Nilitulia kwa dakika chache kisha nikamuamsha Jesca. Hakunisikia. Nikapekua huku na huko. Nikachukua mafuta. Nikaenda bafu za kulipia nikaoga. Nikajipaka mafuta. Nikavaa kanga moja.Samson akawa kioo changu akakiri kuwa kwa namna ile lazima anitamani.Samson akaniongoza hadi nikafika eneo la tukio.Jirani na bwana huyu palikuwa na kiti kipweke ambacho hakikuwa na mlevi aliyekikalia. Nilikitoa upweke nikajiweka juu yake.Haraka akafika muhudumu wa kizambia, mweusi na mbaya kumtazama. Nikaagiza soda.Meza yangu haikuwa mbali sana na yule bwana ambaye Samson alinielekezea. Nilikunywa soda taratibu huku nikiisoma akili ya yule bwana aliyepata bahati ya kupata madini Bwana mkubwa.“Yaani wahudumu wengine nao….ona sasa.” Nilizungumza kwa hasira. Kama najiongelesha. Sauti ikamfikia mlengwa ambaye ni yule bwana anayekunywa pombe.Akajileta mtegoni.Akasogeza kiti karibu nami.“Wewe ni mtanzania kumbe..ama unaibiaibia Kiswahili. Nimefurahi kukusikia ukisema Kiswahili.”Nikatabasamu, nikalegeza jicho kimaksudi.“Yeah! Mtanzania halisi…..na wewe je?”“Mimi ndio orijino kabisa.” Alijibu. Nikacheka tena.“Dah!! Miezi miwili sijarudi nyumbani aisee. Maisha haya.” Nililalamika.“Aaah! Mimi kila wiki huwa naenda aisee.”Maongezi yakawa maongezi. Kama bahati alinipendelea vile. Yule bwana alikuwa na tabia za kibongo. Akaniingizia mada za mapenzi.Sasa nane usiku tukawa tunatafuta chumba kwa ajili ya kutimiziana haja. Yeye akinitaka kimwili na mimi nikimtaka kipesa.Alilipia chumba cha bei ghali sana. Nilimshuhudia wakati anauacha mkoba wake mapokezi. Nikagundua mchezo unataka kuharibika.Nikajipa moyo. Nikaenda hadi chumbani!!Hapakuwa na jipya huko. Mzee huyu mwenye matamanio. Alinivagaa na kuanza kunisumbua huku na huko. Sikuwa na hisia hata kidogo. Niliwaza pesa tu.Nilipomtazama umri wake nikagundua huyu hana lolote la kuweza kunishinda. Akili ya maajabu ikanivaa, nikajikuta nimevamiwa na wazo kuwa kama nisipokuwa makini naweza kutumika kimwili na nisipate chochote kile.Nikaamua kutumia nafasi moja tu kusawazisha mambo haya!!!Pata potea!!“Mh!! Hauna kinga?” nilimuuliza baada ya kuwa nimempelekesha akalegea kabisa macho yake na nikajua kuwa alikuwa anahitaji mwili wangu.Ni hapa nilikuwa napahitaji.“Sina mpenzi wangu…njooo tu hivyo hivyo” akajibu. Nikamtukania mama yake kimoyomoyo kwa ujinga aliozaa.Nikasimama. Nikamtazama kwa jicho la kimapenzi huku moyo wa chuki ukimtusi. Ubongo unaohitaji pesa nao ukifanya kazi kwa bidii kubwa.“Ngoja niende kuchukua mpenzi wangu, naogopa mimba mwenzako, ujue nimeolewa eeh!!” nilimlaghai. Akaingia mkenge. Nikachukua upande wangu wa kanga, nikashusha ngazi mpaka mapokezi.Nikamkuta mwanadada mweupe akiwa ameuchapa usingizi.“Nipatie mkoba wa mzee!!” nilimwambia huku nikiwa nimetega mkono!! Moyo ukiwa hauamini kama nitafanikiwa.“Mmm. Hapana mwambie aje mwenyewe dada, hajaturuhusu kumkabidhi yeyote zaidi yake.” Alinipinga yule dada kwa kingereza chake kibovu kisha akaendelea kuuchapa usingizi. Nilitamani sana kumrukia nimkabe. Lakini alikuwa ametenganishwa na nondo. Nisingeweza hata kumgusa.Niliondoka pale nikiwa nimetaharuki sana, mpango ulikuwa unakaribia kushindikana sasa, na asubuhi inayofuata nilitakiwa kusafiri kuelekea Mbeya.Nikapanda hadi juu kule chumbani nikaufungua mlango kwa ghadhabu kubwa.Yule bwana akashtuka.“Ndio ujinga gani huu huku Zambia I hate such embarrassment!!” nililalamika.“Nini tena mamito.” Aliniita kimapenzi akiwa amelegea.“Yaani hadi kuchukua kinga I need to go with you!!”“He!! Wamekunyima?” aliponiuliza swali hilo, nikajikuta Napata nafasi ya mwisho.“Fanya hivi naomba umpigie umwambie anipe!! No discussion!!” niliwaka, zile hasira za kutaka kuikosa pesa ile zilikuwa zimenipanda.Mbongo akachukua simu akainyanyua. Nikaomba mizimu yote asije akasemam maneno mengi kwenye simu.“Halo!! Chumba namba 12….mpe huyo dada nilichomuagiza…na muache mambo ya kipumbavu” akakoroma kwa kiingereza kilichonyooka. Kisha akakata simu kwa hasira.Sikusema neno!! Nikafungua mlango, nikatoka.Nikiwa nimeukunja uso kwa ghadhabu nikafika mapokezi. Yule dada usingizi ulikuwa umekatika!! Tukatazamana!!Yeye anaogopa na mimi naogopa!!!Maskini yule dada bila kujua kwamba ameambiwa anipatie kinga. Akadhani yule mbongo amemaanisha ule mkoba. Akaniomba msamaha kwa kila namna kisha kwa ukarimu kabisa akanipatia ule mkoba. Ulikuwa mzito kiasi. Nilipotaka kuondoka yule dada aliyekuwa amejikita katika kutafuta anachojua yeye, aliniita, nikageuka na kumshangaa kidogo.“Unatakiwa kuweka sahihi.” Alinielezea kwa ukarimu.Nikaona kama huyu binti ana nia mbaya na mimi. Nikabaki wima najiuliza iwapo niende mbele ama nirudi. Tukatazamana kwa sekunde kadhaa. Nikaona isiwe tabu. Nikarejea nikachukua kalamu niweze kuweka sahihi. Mara nikasikia fujo za mlango kufunguliwa.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Nikaomba Mungu usiwe mlango wa yule jamaa mbongo. Kisha nikasikia hatua kubwa kubwa zikitambaa.“How long does it take to…to…..hell..” (Inachukua muda gani ku…ku…. ). Ilisikika sauti yenye kitetemeshi cha hasira. Alikuwa yule mbongo.Sasa badala ya kuweka sahihi nikabaki kulishikashika tu lile daftari na kalamu. Mkojo ukatoka safari yangu ya mbali na sasa ulikuwa unahitaji kutoka. Nikabana miguu yangu!! Mkoba mkononi.Ninafumaniwa Isabela mimi!!Nikataka nikimbie!! Miguu ikawa mizito. Sikuwahi kufanya kitendo cha wizi hivyo lazima hali kama hii ingenitokea.ingenitokea.“Iam sorry boss..i have already given her (samahani mkuu..nimempatia tayari.)” yule dada wa mapokezi alijitetea kwa uoga.Mara vile vishindo vikasita.Yakafululiza matusi ya nguoni kutoka kwa yule mlevi wa kibongo.Hapo sasa nikaangusha saini yangu.Narudi vipi na ule mkoba sasa!! Nikajikaza nikaanza kuondoka.Nilipogeuka nikakutana na kosa ambalo nililitegemea. Yule dada wa mapokezi alikuwa amebonyea chini tena.Asante! Nilimshukuru kwa kitendo hicho.Ghafla nikabadili uelekeo. Nikaelekea katika vyoo.Upande huu, nikaambaa na korido hadi nikaufikia mlango wa kutokea. Nikamuachia tabasamu mlinzi aliyekua kwa nje na yeye akatabasamu. Tabasamuu la kizee. Kisha nikatoweka. Nikapiga hatua kwa hatua hadi nikalifikia geti kuu la kutokea. Hapa nilitakiwa kuandika jina. Nikaandika jina lililokuja kichwani mwangu lakini sio jina sahihi.Geti likafunguliwa. Mimi na mkoba wangu. Nikatoka.Nilipogeuka nyuma nikakutana na maneno mazuri ya kupendeza.The Savoy Hotel12 Buteko AvenueNdolaZambiaHaya hayakuwa yananihusu. Niligeuka na kutazama mbele. Nikaanza kutokomea. Nikashtuliwa kwa kuguswa begani.Nikageuka upesi nikaikuta amani ambayo nilikuwa naihitaji.Samson…jemedari wa kisukuma.Akanikumbatia kunipongeza. Lile joto lake likanikumbusha mengi. Nikapuuzia.Oparesheni ilikuwa imekamilika.****Pesa zilikuwa kwa mafungu yanayolingana. Zilikuwa zinang’ara kuonyesha kwamba hazikuwa zimepitia mikono mingi.Ilikuwa saa kumi alfajiri. Sasa nikiwa pamoja na Samson tulipita katika vijiwe ambavyo wenzetu walikuwa wanalala. Wote wakaamshwa. Hatimaye tukawa na mkutaniko wa pamoja wa kwanza tangu tuwe katika ardhi ile.Niliwakumbusha juu ya ahadi yangu!! Sasa ilikuwa imetimia.Hakuna aliyekuwa anafahamu thamani ya kwacha ya Zambia katika shilingi ya kitanzania. Hilo halikutupatia shida. Nikawachukua wenzangu watano wa kwanza. Nikaliendea basi linalotoka Ndolla kuelekea Mbeya mjini.“Kwacha ngapi?” niliuliza. Akanijibu. Nikalipia nafasi za watu watano.Wakaingia garini. Kiongozi wao akiwa JescaNikarejea na kuwachukua wengine. Hawa kiongozi wao akawa Jenipher.Kundi la nne nikalikabidhi kwa Samson.Kisha nikabakisha kundi lililosalia mikononi mwangu.John!! Akiwa ameambatana nami!! Nilichukua siti ya watu wawili. Nikamuweka John kisha nikambebesha mfuko fulani.Hakuruhusiwa mtu kukaa pale.Safari ikaanza huku maelekezo yota ya tunakutana vipi yakiwa kwa viongozi wa msafara.Hatimaye tukaiacha Ndolla majira ya saa kumi na mbili. Safari ya kurejea Tanzania.*****Pesa zilibaki nyingi sana. Hivyo tuliamini kabisa hakuna kitakachoharibika. Jesca alikuwa na akiba yake, Jenipher na Samson vilevile.(Mshikemshike )TUNDUMA, Mbeya.Mji ulikuwa umetulia sana. Hapakuwa na harakati za hapa na pale. Ilinishangaza sana kwa boda kama hii kuwa katika utulivu huu.Tulikuwa tukihangaika kutafuta mahali pa kulala. Nyumba za kulala jirani na kituo cha mabasi zilikuwa zimejaa. Hivyo ilitulazimu kidogo kuzunguka. Hatukupata mahali pa kulala kwa wingi tuliokuwa nao. Sasa tuliamua kuishi maisha yetu ya Zambia. Tukaamua kulala katika stendi ya mabasi.Baada ya kufikia uamuzi huo. Sasa mwenye kutafuta chakula aliruhusiwa lakini pa kulala tulikuwa tumeamua kabisa ni hapo hapo stendi.Wanaume watatu waliamua kusindikizana kwenda kutafuta chakula.Mkuu wa msafara huo Jesca aliwapatia pesa wakatoweka kwa ahadi ya kurudi upesi.Ahadi ikavunjwa maradufu!! Hawakurudi.Hadi tuliposinzia. Haikuwa kama yaliyomkuta Samson kule Ndola. Hawa hawakurudi kabisa.Kesho yake. Tulipotoa taarifa polisi tulikutana na taarifa ya vifo vya watu watatu kwa kukatwa na mapanga.Walikuwa wenzetu!! Lakini hatukukiri!! Hatukuhitaji kuwa karibu kabisa na polisi. Kwa kifupi hatukuwa tunajua hatma yetu. Hasahasa mimi ambaye nilikuwa na siri nzito.Baada ya taarifa hizo kutapakaa. Tukajua nini kinachoendelea ndani ya mji wa Tunduma. Majambazi wa ajabu walikuwa wameuvamia mji. Hawa walikuwa na hadhi ya kuitwa majambazi wastaarabu. Walibandika matangazo kabisa kuwa kama mwanaume anatembea usiku basi awe na tahadhari aidha simu ama kiasi cha pesa shilingi. Elfu hamsini lakini bila hilo wakikutana ama zao ama zake.Kumbe ndicho kimewasibu wenzetu!! Nilisikitika kuzipoteza roho hizi.Asubuhi hiyo nilitaka kwenda kubadili pesa. Lakini bahati mbaya sikuwa na kitambulisho chochote. Nikaitupa kazi hiyo kwa Samson. Akazunguka mtaani kuzibadili baada ya kugundua kuwa Kwacha moja ni sawa na shilingi 0.3 ya kitanzania.Baada ya zoezi lile kukamilika na kupata pesa ya kutosha sasa kila mmoja alitakiwa kuubeba mzigo wake mwenyewe. Aliyesema kuwa anaishi Dar alipewa nauli aondoke zake, wa Arusha naye vilevile. Na pesa ya ziada kila mmoja alipewa.“Muutangaze ushuhuda huu bila kuipunguza wala kuongeza neno!” niliwaambia wakati tunaagana. Kila mmoja alikuwa na furaha huku wakiniona mimi kama Mungu wao. Sikujali sana!!Safari ya Mwanza tukabaki watano. Mimi, Jesca, John, Jenipher na Samson.****Siku ya safari kama ilivyo kawaida nikalipia siti ya watu wawili, Jesca na Jenipher wakakaa siti moja huku Samson akikaa peke yake.Alama ya John shingoni ilinikwaza sana. Nilitamani aweze kutuona. Lakini alikuwa anauona ulimwengu wake mwenyewe.Safari nzima ilikuwa tulivu sana. Nilikuwa natafakari mambo mengi sana. Nilitamani kwenda Makambako kwa mama lakini niliamini haukuwa wakati sahihi.Nilihitaji nkujua kitu kuhusu Maria. Maana alinitokea kule porini siku ya kwanza kabisa na kamwe sikumuona tena.Nini kilimsibu? Nilijiuliza.Tulipita miji mbali mbali. Tukaipita Makambako, nikainama nikajifuta machozi, tukaiacha Mafinga, tukaingia Iringa mjini. Na hapa hatukusimama sana tukaendelea na safari.Sasa gari lilisimama!! Hatukushangaa sana. Tulidhani ni kwa madhumuni ya kuchimba dawa. Lakini hatukuiona dalili hiyo.Dereva akateremka. Akaangaza gari lake bila kuona tatizo.Akaangaza tena. Hakuna tatizo.,Msaidizi wake naye akashuka. Hakuna msaada!!Wakashuka mafundi wakajaribu kugusa hapa na pale. Gari lilikuwa limezima.Walijaribu kufanya kila wanaloweza lakini hapakuwa na matumaini. Dakika zikaanza kwenda. Masaa yakaenda. Hatimaye jioni.Abiria wakashindwa kuvumilia. Wakatoa matusi mengi lakini haikusaidia. Gari halikuweza kuwaka.Duh! Leo tunalala njiani!! Nilimweleza John japo hakunisikia.John alichoweza kuona ni chakula na mengineyo lakini si watu!! Na watu halisi pia hawakuweza kumuona yeye.Simu ilipigwa ili gari jingine liweze kuja kutuchukua. Basi lilifika likiwa na abiria wengine. Likazimishwa ili tuweze kubananishwa wote twende Dodoma. Abiria walilaani kitendo kile kwa lugha zote, huku wakilalamikia usalama wao.“Kama hutaki basi hili hapa lala utasafiri kesho!!.” Zilikuwa kauli ngumu kutoka kwa mpigadebe. Hakuna aliyependezwa na kauli hiyo. Wakati huu sikuweza kukaa na John badala yake tulikuwa tumesimama. Ni Jesca pekee aliyepata nafasi ya kukaa. Yalikuwa mateso.Walipofanikiwa kutubananisha kama viroba. Dereva akisifiwa na wapambe wake akaingia garini aweze kuendesha tuondoke.Ikaanza tena kama utani, akachokonoa kwa mara ya kwanza likagoma, akajaribu mara ya pili bado hali ileile.Akajaribu tena na tena. Injini haikuweza kuwaka. Kila mmoja akawaza lake.Watu wakakimbilia kwenye imani za kishirikina.Lakini huyo mshirikina ni nani? Hakuna aliyejua.Abiria wakashuka. Kila mmoja akarejea kwenye basi alilokuwa amepanda awali. Hapakuwa na safari tena.Usiku ukafika wanakijiji wakapika chakula na kutuuzia kwa bei mbaya sana. Hatukuwa na ujanja tukanunua.Saa nne usiku mambo yakananza kubadilika. Hali ya hewa ilibadilika na kuwa ya kushangaza hata wanakijiji walikiri kuwa hiyo haijawahi kutokea. Badala ya baridi kali la Iringa sasa lilitanda joto.Joto hilo ni kama lilimshtua John. John akasimama akataka kuondoka. Nikamzuia. Akawa anatumia nguvu!! Nikamzuia John, John akanitazama kwa jicho la hasira. Macho yake yakiwa mekundu sana.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/John alikuwa ananiona? Nilijiuliza.Lile joto likazidi. Abiria wakashuka garini.Kuna kitu hapa!! Mapambano mapya!! Nikajisemea huku nikiendelea kumzuia John.John sasa akanizidi nguvu.Akanitoka. Akashuka chini. Nikajaribu kumkimbilia.Huko nikamkuta akiwa anafanya jambo la ajabu. John alikuwa anajarfibu kuisukuma gari kwa kuitikisa.Ajabu! Ikaanza kutikisika kweli. Mtikisiko ule ukawashtua wengi. Sasa vilio vikaanza kusikika. Kila mtu kuitetea nafsi yake.Watu wakashuka upesi kwa kugombania mlango. Basi likaanguka.Lilipoanguka John akatazama mahali. Na mimi nikageuza jicho kutazama. Yalikuwa makaburiMakaburi yaliyo na historia ya kushangaza. Makaburi ambayo yalimtoa nishai mchina alipojaribu kupitisha umeme juu yake. Umeme ukagoma kuwaka.Haya yalikuwa makaburi ya Kiyeyeu.Yalikuwa yanafuka moshi wa dhahabu!!Vita!!ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog