Search This Blog

Sunday 19 June 2022

MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI - 2

 





    Simulizi : Mwanamke Mwenye Kovu Jeusi

    Sehemu Ya Pili (2)







    Nilitoka kwenye zile ofisi za mamlaka ya mawasiliano na kuingia kwenye gari yangu ndogo tayari



    kulekea ofisini ili kujua pia wenzangu ni kipi wamekipata maana tuliahidiana ya kwamba  saa 6 wote

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    watatu mimi Gerald na Amina tuwe ofisini tufanye kakikao kadogo kujua ni kipi cha kufanya,



    niliendesha gari yangu taratibu huku nikwa nazungumza na simu nakumbuka nilipofika pale



    magomeni kulikuwa na foleni kubwa sana kwani msafara wa rais wetu ulikuwa unapita basi



    nilipungumzamwendo na kuendelea kuzungumza na simu huku nikiwa nimeshusha kioo cha gari



    yangu kwani air condition yangu ilikuwa imeharibika mara ikaja pikipiki aina ya baja kwa nyuma



    kwenye ile foleni ya magari ikiendeshwa na mtu mmoja ambaye alikuwa amevalia helment ya blue



    kichwani akiwa amevalia utazani ni mtu aliyekuwa anaenda safari ya mbali sana kwani kwenye



    mikono na miguu alikuwa amevaa plastiki za kuzuia michubuko ile pikipiki ilikuja mpaka usawa wa



    gari yangu kisha Yule mwendesha pikipiki akanitazama kwa sura ya tabasamu hapo ndipo



    nilipogundua ya kwamba ni mwanamke akanisalimia kaka habari, nilimuitikia kwa kichwa kwani



    nilikuwa nazungumza na simu bado, mara akatupia bahasha mule ndani kwenye gari yangu halafu



    huyo akaondoka kwa mwendo wa kasi nilishituka nikajikuta nawepa pembeni simu yangu na



    kuiangalia ile bahasha huku nikimtazama na Yule mwanamke kwenye kioo cha gari yangu kwa mbele



    akiondoka bila hata kusimama pale kwenye mataa kiasi kwamba mpaka akasababisha ajali maeneo



    yale kati ya daladala nagari moja lililokuwa limebeba maji ya kunywa ya uhai ambalo lilionekana



    lilikuwa ni gari la kusambaza maji sehemu mbalimbali hapa mjini.

    Niliitazama ile bahasha kwa wasiwasi sana kwa juu ilikuwa imeandikwa jina langu halisi, huyu mtu



    amelijuaje jina langu halisi? Hii ni hatari potelea mbali nikaichukua ile bahasha na kuichana kujua



    mule ndani kuna nini, nilkuta kuna ujumbe uliokuwa umeandikwa kwa rangi nyekundu uliokuwa



    ukisomeka

                             Dear Siwah Erique

     mimi naitwa Mwanamke mwenye kovu jeusi kwa leo nilikuwa nakusalimia tu na kukuambia ya



    kwamba karibu sana kwenye himaya yangu nitaludi tena kukusalimia vizuri baaadaye kazi njema.

    Nilipousoma ule ujumbe nilishangaa sana kisha nikajikuta nacheka mwenyewe,amakweli mimi ni



    mjinga yani nashindwa kumkamata mtuhumiwa mbele yangu kweli kazi ipo mwaka huu sawa na aje



    tu mimi hata simuogopi hata kidogo. Upande wetu uliruhusiwa na trafiki nikaondoa gari yangu



    taratibu kuelekea stesheni ambapo ndipo ofisi zete zilipokuwa.

    Niliwakuwa wenzangu wameshafikia wakinisubili mimi, tuliingia kwenye ofisi ya Amina kwa ajili ya



    kufanya kakikao kadogo cha watu watatu, alianza Gerald kuzungumza ya kwamba hakumkuta



    Zainabu kazini siku ile kwa taarifa aliyoikuta ni kwamba alikuwa mgonjwa, alipoomba namba yake



    ya simu alimpigia ambapo alipokea mdada mmoja aliyejitambulisha kama mdogo wake ambaye



    alisema ya kwamba Zainabu jana aliludi toka kazini akiwa hajisikii vizuri wakampeleka hospitali



    ambapo yupo hoi wodi ya wagonjwa mahututi alizidi kuleza Gerald ya kwamba allipofika pale



    muhimbili na kujitambulisha aliambiwa ya kwamba kuwa Yule mwanamke jana imeonekana alipigwa



    na kamera ya mionzi ambayo ndio imekausha damu yake na pale alipo uhakika wa kupona ni mdogo



    sana.

    Basi baada ya kueleza hayo na mimi nilieleza ya kwangu toka pale ofisi za mamlaka ya mawasiliano



    mpaka kule barabarani nilipotupiwa ile bahasha na Yule mwanamke mwenye gari yangu  kisha



    tukaanza kujadili jinsi ya kupambana na Yule mwanamke, Amina alitueleza ya kwamba Yule



    mwanamke tu ndio atakuwa amempiga hiyo mionzi Zainabu, hivyo basi inabidi tuongeze umakini,



    tulijadiliana na kufikia mahitimishoa ya kwamaba  ni lazima kesho asubuhi tuanza kumsaka, kaka hili



    zoezi ni gumu ten asana tututa,tafutia wapi? Hata pa kuanzia hatupajuai kila anayegusa anga zake



    anaondoka duniani hapa nilipo mimi sina hata raha kwa maana sijui hata mtoto wa watu Furaha



    anaendeleaje.Gerald alilaamika tulikubaliana tukaanze kumsaka mitaaa ya mbezi beach ambapo



    ilisemekana kuwa alikuwa akiishi na mdogo wake Zainabu kabla hajafa, tulielewane tukajaribu kwa



    siki nzima ya kesho kwenda kufanya upelelezi upande wa kule.

     Wakati tumemaliza kujadiliana mara simu ya Gerald ikaita kuangalia alishangaa kuona namba yake



    simu ndio ilikuw ikimpigia, jamani nashangaa hapa simi inaita namba inayoonekana kwenye screen ni



    namba ya ngu what is this? Mimi hata kuipokea naiogopa alisema huku akiiweka wenye  meza pale



    ofisini mara Siwah akaichukua na kuipokea  haraka haraka enhe nani  mwenzangu? Ni mimi



    mwanamke mwenye kovu jeusi sauti iliongea upande wa pili huku ukiacha isikike sauti Siwah



    aliiweka simu loudspeaker ili wasikie wote, walishangaaa sana kusikia yale mazungumzo yao ambayo



    yalikuwa hayana hata dakika 2 yakizungumzwa kupitia ile simu yakiwa yemerekodiwa mwisho wa



    yale maongezi Yule dada alisema ya kwamba nilikuambia ujitoe kufuatilia hili jambo lakini



    inaonekana wewe sio mwelewa si ndio? Sasa nakusubili kwako ile sauti ya kike ilizungumza kisha



    ikakata simu. Gerald alijihisi kuogopa sana pale pale wakaanza kujadili hivi huyu mwanamke

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    inakujae haya mazungumzo yetu tunayazungumza hapa hapa na anayapata hapa hapa? Kwa staili hii



    hatufanyi lolote sasa nilijikuta nazungumza kwa ukali kidogo, usikasilike hapa ni kujua haya



    maongezi anayapataje?

    hebu tusachi kwanza humu ndani Amina alizungumza huku akianza  kuangalia kila mahali kuona



    kama kuna kinasa sauti chochote…!

                                     ****************************

    Amina aliangalia kila mahali bila kuona kinasa sauti chochote huku mimi na Gerald tukiwa tu



    najaribu kujadili kuhusu hatima ya Yule mwanamke mwenye kovu jeus,i basi wakaafikiana ya



    kwamba kwa usalama zaidi wa Gerald ni bora siku hiyo asiende kulala kwake kwa maana siku zote



    mambo aliyoyazungumza Yule mwanamke yalikuwa yanatokea, waliagana nakuelekea nyumbani



    kwa Siwah kwa ajili ya kulala.

                                  **************************

    Kesho yake asubuhi na mapema baada ya kuwasili ofisini  mimi Gerald na Amina tulipewa askari



    kanzu watano wa ziada kwa ajili ya kuelekea maeneo ya mbezi beach kujaribu kumtafuta mwanamke



    mwenye kovu jeusi, tuliaacha wote gari zetu pale kwenye maegesho ya magari ya kazini na kuchukua



    gari zingine kabisa za kazini lakini zenye namba za kiraia ambazo huwa tunazitumia kwenye shughuri



    zetu mbali mbali maalumu ambazo hatukupenda kujulikana, tulichukua gari tatu moja nikiwa nayo



    mimi na dereva nyingine Amina na nyingine Gerald akiwa na askari kanzu mmoja, bai tulienda moja



    kwa moja kufika mbele tukagawana majukumu, mimi nitakuwa napita kwenye ma ofisi mbali



    mbali,Gerald kwenye nyumba za wageni na nahotel huku Amina tukimpa kazi ya kupeleleza



    ufukweni

    ,nilipita kwenye viwanda na ofisi mbalimbali nikijitambulisha kisha na kuomba list ya wafanyakazi na



    picha zao ambapo nilikuwa najaribu kuangalia baadhi ya wafanyakazi na kuwahoji kidogo na



    wengine kuwaahidi ya kwamba nitawatafuta wakati natoka kwenye kiwanda cha kutengeneza dawa



    za mswaki na mafuta ya  mwili mara nikasikia ile simu ya Furaha mchumba wa Gerald ikiita kwani



    mpaka kipindi hicho ilikuwa bado nonayo mimi toka juzi tulipotoka nyumbani kwa Gerald kuangalia



    kumbe ilikuwa ni meeji imeingia ikisomeka ya kwamba niliwaambia mjitoe kujihusisha na kunifuatilia



    mimi sasa subilini majibu baada ya masaa kadhaa,kuangalia kama kawaida namba ya aliyetuma



    haikuonekana nikajua tu atakuwa Yule dada mwanaharamu tunayemtafuta, nilitafakari nikaona



    nikiwajulisha wenzangu nitawaondoa kwenye morali ya kufanya kazi, nikaona si mbaya nitawajulisha



    baadaye tukikutana,wakati nikiendelea kutafakari mara simu yangu ya mkononi ikaaita kuangalia



    kumbe alikuwa ni Yule injia wa pale mamalaka ya mawasiliano, “Ndio injinia nakusikiliza, sasa



    kakaleo asubuhi niliitegesha hiyo namba hivyo nimefanikiwa kuipata namba ya simu ya huyo mtu



    anayewasumbua na pia inaonyesha muda huu anapatikana mitaa ya bahari beach inspekta, alimalizia



    kuniambia yule injinia wa mamlaka ya mawasiliano. Sawa kaka basi naomba unitumi hiyo namba



    yake  ili tuanze kumtafuta kwa maana tupo mitaa ya karibia na hapo unaposema alipo sasahivi,



    nilimjulisha Yule injiniaalinielewa na baada ya kama dakika 2 alinitumia data zote ile namba ya simu



    jina lililotumika kuisajili ile laini na umbali ambapo ilionekana Yule mwanamke yupo kutokea kwenye



    mnara wa simu, nilimjibu kwa kumshukuru kisha nikawapigia simu Gerald na Amina kuwaambia ya



    kwamba tukutane karibia na hayo maeneo si chini ya nusu saa kwa ajili ya kuhakikisha tunamtia



    nguvuni Yule mwanamke, basi tulijongea pale lile eneo ambalo lilikuwa kando kabisa mwa bahari ya



    hindi, mimi nikiwa wa kwanza kufika, tulipofika lile eneo niliwambia vijana wangu niliokuwa



    nimeongozana nao kuwa makini kwani tupo kwenye eneo hatari sana,tulikaa pembeni kidogo



    kwenye mwamba Fulani uliokuwa pale ukingoni mwa bahari tukiwa tukiwasubiri kina Gerald pamoja



    na Amina, mara nao walifika lile eneo bila kukawia kila mmoja akitokea upande wake,alipofika lile



    eneo Amina aliliangalia kisha akaniambia kwa sauti ya majonzi, “maeneo hay ndipo tulipoikuta maiti



    ya marehemu Yule mdogo wake na Yule dada anayefanya kazi benki” kisha akaendelea nahisi huyu



    mtu atakuwa yupo haya haya maeneo,mwili ulinisisimka sana kusikia vile kwani kumbe nilikuwa



    kwenye eneo hatari ambapo muda wowote umauti unaweza kutukuta, haya hakuna muda wa



    kupoteza hapa cha msingi tuanze kumsaka haya maeneo kwa maana nimeambiwa ya kwamba yupo



    maeneo haya haya, nilianza kuwaambia ili tuanze kuwajibika huku kila mmoja wetu nikimwambia



    achukue tahadhari, tulipnaga mikakati pale na kungalia asili ya lile eneo kiukweli kulikuwa na watu



    kwa mbali ndani ya bahari wakiendele na shughuli zao za uvuvi hasa mida ile nazani walikuwa



    wakikagua tu zana zao za uvuvi kwa ajili ya maandalizi ya uvuvi siku ile usiku, lile eneo lilikuwa



    tulivu sana kwani kwa muda wa takribani kumi tulizokaa pale tukipanga mipango yetu mbalimbali



    hapakuonekana mtu wa aina yoyote kupita lile eneo, kweli haya yatakuwa ni maficho yake lakini



    katika mazingira haya mbona kuna wavuvi tu? Sioni nyumba wala mwatairi ya magari, wala sasa



    anaishi vipi? Gerald alijikuta akutuambia pale, au inawezekana huyo injinia wa mamlaka ya



    mawasiliano nchini amenunuliwa au ni huyo mwanamke pia amefanya utundu wake kwenye simu ili



    kutupoteza jama maana hili eneo huyo mtu ataishi wapi? Aliendelea kusisitiza Gerald, ndio



    inawezekana huyu mwanamke itakuwa alianza kushituka au alihisi kuwa tumekaribia kumpata ndio



    akafanya hivi, haiwezekani hili eneo halina mtu bwana Amina pia alendelea kusisitiza.

    Ilinibidi niwashushe munkari kidogo ili tuweze kuelewana, sawa jamani yote yanawezekana hapa cha



    msingi ni tufanye yafuatayo tutawanyike kutokea hapa kuelekea sehemu mbali mbali kama yupo



    maeneo haya tutampata sawa na kama hayupo basi tuendelee na zoezi letu

    Tulitawanyika pande zote huku tukiambina kwa yoyote atakayohisi au kumuona basi atujulishe



    mapema sana iwezekanavyo, tuliendelea na lile zoezi la kumtafuta mara kwa umbali kama wa mita

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    70 nilimuona mwanamke akiwa chini amelala kwenye mchanga ule wa kando kando ya bahari huku



    akiwa kama ni mtu asiyekuwa na nguvu akiomba msaada alionekana kama ni mtu ambaye kuna



    jambo baya lilikuwa limemkuta ,basi pale pale nilimuamrisha mmoja wa wale askari kanzu niliokuwa



    nimefuatana nao awajulishea kina Gerald na Amina wote wafanye kuja upande ule tuliokuwepo huku



    sisi tukizidi kumsogelea lakini kwa tahadhari kubwa sana kwani tulijua fika atakuwa ni mwanamke



    mwenye kovu jeusi ameamua kutumia ile mbinu baada ya kuona tayari tumeshagundua makazi yake,



    nilimuambia Yule askari kanzu atoe maelekezo waje upande  ule ila wafanye kama vile kuzunguka



    kwani wote tukielekea upande mmoja anaweza kutuzidi ujanja kwani wote tulikuwa hatujui alikuwa



    na silaha gani pale..!!

    Tuliendelea kumsogelea Yule dada kwa tahadhari kubwa sana huku kila mmoja wetu akiwa ameweka



    silaha yake tayari kwa lolote litakalotokea,tulizidi kumsogelea Yule dada moaka zikabakia kama mita



    kumi hivi huku tukiwa tumemzunguka, pande zote dada Yule alionekana wazi akiwa hana nguvu hata



    kidogo kwani likuwa akijaribu kujivuta lakini alishindwa, Gerald ambaye alikuwa upande wa kulia



    tukiwa tunaangaliana mara nikasikia Gerald akitamka kwa nguvu, my god mpenzi wangu Furaha



    jamani muacheni mpenzi wangu alizidi kusema kwa sauti ya juu Gerald, basi tuliacha kumuelekezea



    silaha Yule dada wote kisha tukamskimbilia kwa kasi Yule dada.

    Tulipofika tulimkuta hali yake ikiwa si nzuri kwani alikuwa anaonekana ni mtu aliyechoka sana huku



    akiwa kama vile amekimbia mateso Fulani,ohh mpenzi wangu jamani kumbe alikueleta huku



    alizungumza Gerald huku machozi yakiwa yakimtiririka,bila kupoteza muda nilinyayua simua yangu



    ya mkononi na kuwapigia simu hospital ya taifa ya mwanayamala ili waje na gari la kubebea



    wagonjwa waje kumchukua kwani hali yake ilikuwa ni mbaya sana,Gerald alikuwa akijaribu



    kumsemesha lakina Furaha hakuwa hata na nguvu ya kuzungumza alikuwa akijaribu kuonyesha kwa



    ishara na macho pande wa kaskazini ambapo sisi wote tulipojaribu kupaangalia hatukuona



    kitu.tuliamua kufanya maamuzi ya haraka haraka kwa kuwa tuliona pale muda unaenda na kwa



    foleni ya jijini ingewezekana akatufia mikononi wakati tukiwa na usafiri hivyo tuliamua kusogea na



    gari tuliyokuwa naye ili tukutane nao barabarani

                                         *********************************

    Tulimfikisha hospitali ya mwananyamala huku hali yake ikiwa bado si nzuri wauguzi na madakatari



    walimpeleka wodini na kumutundika na dripu za kumuongezea nguvu kwani ilionekana fika alikuwa



    hajapata cjakula kwa zile siku mbili alizokuwa kwa Yule mateka,sisi tulitoka nje na kukaa kusubili



    ripoti ya madaktari watuambie alikuwa anaendeleaje tulikaa pale kwa muda wa takiribani saa 2 ndipo



    muuguzi akatoka nje na kutuambia kwa muda ule tungeweza kuingia ndani na kwenda kumsalimia



    tuliingia kwa ukweli tulimkuta akiendelea vizuri sana japo aliweza kuzunguma maneno mawili ma



    tatu japo kwa shida shida sana tuliwashukuru ma daktari na kuwataka sisi tuende huku tukiahidi



    kuludi kesho yake kwa ajili ya kumchukua mahojiano kuhusiana na mwanamke mwenye kovu



    jeusi..!! mimi na Amina pamoja na wale askari kanzu wengine tuliondoka huku tukimuacha Gerald



    akiwasubili ndugu zake na Furaha waje wamuone kisha na yeye aende kujipumzisha.

                                            *****************************

    Niliamka asubuhi na mapema kama kawaida yangu baada ya kufanya mazoezi ya viungo asubuhi



    kwa kufuatiliza kipindi cha mazoezi cha kituo cha hbari cha terevisheni cha ITV nilienda kujoga na



    kujiandaa kwa ajili ya kuelekea kazini, nilifika ofisini asubuhi na mapema baada ya kusaini kitabu



    cha mahudhurio nilielekea moja kwa moja ofisini kwangu nilishika faili la ile kesi ya huyu



    mwanamke aliyejiita mwenye kovu jeusi na kuanza kulipitia hatu kwa hatua huku nikijaribu kunote



    baadhi ya vitu amabvyo nilihisi ya kwamba vitakuwa vya muhimu kwa siku hiyo kabla sijaelekea



    hospitali kwenda kumuona Furaha.niliendelea kufanya ule uchambuzi kwa kama dakika 20 hivi



    ndipo alipoingia Amina ofisini kwangu kunijulia hali na kuniambia ya kwamba kama nipo tayari basi



    tutoke wote tuelekee hosptali ya mwananyamala kwenda kumjulia hali mgonjwa ikiwezekana na



    tufanye nae mahojiano kidogo kisha sisi tuendelee na majukumu mengine,nilimuelewa Amina tulitoka



    wote ambapo tulielekea mwanayamala hospital tukiwa na usafiri wangu binafsi ambapo tulipitia



    kwenye mgahawa mmoja mitaa ya kinondoni kwa ajili ya kupata kifungua kimywa kwanza kisha



    ndio tuendelee na safari yetu. Wakati tupo pale tunakunywa chai kwa pembeni yetu alikuwepo dada



    mmoja ambaye alikuwa kama mtu aliyekuwa hajiamini kabisa huku akiwa yupo makini akifuatilia



    maongezi yetu, ila sisi ahtukumjali mpaka pale tulipokuja kutoka nje kuendelea na safari ndipo



    ujumbe wa meseji ulipoingia kwenye simu yangu ya mkononi kwanza sikutaka kuusoma kwani ni



    vibaya kuendesha gari huku ukiwa unasoma meseji au unazungumza na simu. Tulifika hospitali



    ambapo tulimkuta Gerald akiwa tayari ameshafikaakiwa nje ya wodi  huku akiwa na na dada yake na



    Furaha sura ya Gerald ilionekana ikiwa ni yenye tabasamu bashasha, karibuni sana jamani



    alizungumza dada yake na Furaha kwa rafudhi ya kihehe ambaye baadaye nilikuja kugundua ya



    kwamba alikuwa akiitwa Witness,tuliingia wodini ambapo tilikuta daktari na nesi wakijaribu



    kuangalia maendeleo ya afya yake “samahani daktari tunaweza kumchukuwa mahojiano kidogo?



    nilimuuliza daktari baada ya kuona tayari wameshamaliza kumungalia maendeleo ya afya yake, ndio



    ila mpaka kwa sasa hali bado haijamludi sawa hivyo basi inabidi mumulize taratibu hasa itakuwa



    vizuri kama huyu mpenzi( wake huku akimshika shati Gerald na kumvuta mbele yetu) yeye ndio



    kama akifanya hiyo kazi alizungumza Daktari, basi Gerald alikaa kwenye kitanda na kumvuta mpenzi



    wake Furaha na kumlalia kwenye mapaja kisha akaanza kumuuliza maswali madogo madogo huku



    akimnywesha uji ili azidi kupata nguvu. Furaha alijaribu kutuelezea japo kwa shida sana kwamba

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Yule dada hakuwahi kumuona kabla ila kwa sasa akimuona atamkumbuka alijaribu kutueleza ya



    kwamba anamakao yake kwenye yumba moja iliyopo kando mwa bahari mitaa ya mbezi



    beach.wakati mazungumzo yanaendelea ghafra aliingia nesi akiwa amevalia sare ya nguo za kinesi na



    kutuomba tumpishe kidogo kuna dawa anataka kumpa mgonjwa Yule nesi alionekana akiwa na



    wasiwasi Fulani hivi, basi bila ya hiyana tulimpisha wote tukatoka nje alichomoa sindano na



    kumchoma Furaha kisha akaondoka zake baada ya kama dakika 5 hivi na sisi ndipo tulipoludi wodini



    ile kufika tu, tukakuta hali ya Furaha imebadilika tena asaivi imekuwa mbaya zaida hata ya jana



    tulivyomleta pale hospitali  palepale Witness akatoka nje haraka na kwenda kumuita nesi kwenye



    chumba chao nesi alikuja na kustaajabu, vipi tena hapa imekuaje? Alianza kusema jamani jamani



    mpenzi wangu mmemfanyaje yani mmemchoma sindano baada ya dakika tano tu amekuwa zezeta?



    Alizungumza Gerald kwa machungu machozi yakimtiririka hapana sio sisi alianza kuruka nesi mbona



    sisi tulishapita mida na dakitari yalianza pale mabishano kati ya Witness, Gerald na Yule nesi,mimi



    niliona ya kwamba tukiendeleza yale mabishano wakati hali ya mgonjwa inazidi kuwa mbaya sio



    vizuri basi pale pale nikatoa simu ili niwapigie muhimbili wajiandae kumpokea mgonjwa mahututi



    ikiwa kama order kutoka kituo cha polisi, wakati naitoa ile simu ndipo nikakumbua ya kwamba kuna



    msejeji iliingia kipindi tumetoka kunywa chai pale kinondoni halafu sikuisoma kipindi tunakunywa



    chai kwanza nlitaka kuiacha lakini nikaona sio mbaya ngoja niisome mungu wangu sikuamini ule



    ujumbe niliousoma kwenye ile simu yangu….!!!

    Ujumbe ulikuwa umekuja kwa namba isiyofahamika ukisema ya kwamba “najua mnaenda



    kumchukua mahojiano Furaha ila haitawezekana mwanamke mwenye kovu jeusi” mwili



    ulinisisimuka kwani nilijua ya kwamba basi atakuwa ni yeye aliyejifanya nesi pale hospitali na



    kumchoma sindano ile Furaha ili kupoteza ushahidi,mungu wangu tatizo la kutokumjua sura huyu



    mtu ndio kunasababisha haya yote haiwezekani mtuhumiwa anatukimbia hapa hapa, nilijikuta



    nasema kwa sauti ya chini chini huku nikisubili kuzungumza na simu upande wa pili,baada ya



    kumaliza kuwataarifu hospitali ya muhimbili furaha aliingizwa kwenye gari ya wagonjwa tayari kwa



    ajili ya kupelekwa muhimbili,  huku mimi Amina na Geral tukitoka nje kwa ajili ya kushauriana kipi



    hasa cha kufanya ambapo Gerald alikuwa kama amechanganyikiwa vile kutokana na lile tukio,ilibidi



    niwaeleze kila kitu kuhusu ule ujumbe nilioupata kutoka kwenye namba isiyojulikana, hivyo basi



    niliwaomba tusilaumiane bali tuwe makini na tumuombe tu mwenyezi mungu Furaha afifariki kwani



    yeye ndio atakayeweza kutusaidia ile kazi ya kumkamata Yule mtuhumiwa hatari anayefanya mauaji



    ya hovyo kila siku pale jijini.

    Tulimaliza kupanga baadhi ya mikakati kisha na sisi tukajipakia kwenye gari kwenda hospitali ya



    taifa ya muhimbili kwenda kuona ni kipi kilikuwa kinaendelea kule. Ki ukweli tulikuta hali ya



    mgonjwa ikizidi kuwa mbaya tena mbaya sana kwani japo kuwa alikuwa amelazwa kwenye wodi ya



    wagonjwa mahututi lakini pia walituamba hata mapigo yake ya moyo yalikuwa yakiende taratibu



    sana kwa mwendo wa kusua sua sana hivyo tumuombe sana mwenyezi mungu kauli ile ilizidi



    kumchangaya Gerald na sisi pia kwani pale ndio ilikuwa mahali ambapo tuliona panafaa kupata



    habari zote tulizokuwa tunazihitaji basi tuliona hakuna jinsi zaidi ya kumuomba mwenyezi mungu tu



    amsaidie lakini wakati bado tunaendelea kushauriana mara akatoka Witness ambaye alikuwa ni dada



    wa Furaha alitoka nje akija pale tulipokuwa tumekaa huku akilia sana pale pale indicator ikanigonga



    kichwani ya kwamba Furaha atakuwa tayari ameshatutoka, basi Gerald baada ya kusikia hivyo



    alianza kulia sana pale pale ilibidi tufanye zoezi la kumuondoa Gerald na Witness pale hospitali.

                                  *************************************

    Baada ya kumaliza msiba wa mpenzi wake na Gerald nakumbuka vizuri sana Gerald alipewa likizo



    ya mwezi ofisi hivyo basi zoezi la kuendelea kumsaka Yule mwanaharamu aliyejiita mwanamke



    mwenye mkono wa bandia lilibakia mikononi mwangu na Amina huku mkuu wetu kazini akizidi



    kulalamika kabisa kwa nini tunashindwa kumtia kizuizini wakati kuna wahalifu wengi zaidi yak wake



    ambao tuliweza kuwazibidi tena kirahisi tu sana, nilimhakikishia mkuu wetu wa kazi atupe muda



    zaidi kwani Yule dada alionekana ni mjanja sana hivyo tusipokuwa makini anaweza kutumaliza wote



    hadi yeye, mkuu japo alikuwa ni muelewa ila alikuwa ni mtu mwenye papara sana alitaka kila jambo



    limalizike kwa muda aliotaka bila hata kuangalia uzito wa jambo lenyewe na aina ya watu au mtu



    tuliyekuwa tukikabiliana naye. Basi tulimaliza maongezi na mkuu wetu huku tukitoka ofisini mimi



    nilimwambia Amina ya kwamba naelekea nyumbani kwa Gerald maana aliniomba siku ile nimsindike



    makaburini kwenda kuangalia kaburi la mpenzi wake, basi tulikubaliana vizuri yeye Amina huku



    nikiwa nimemuagiza aelekee kule maeneo ya mbezi beach karibia na tulipomkuta marehemu Furaha



    akajaribu kama kufanya uchunguzi kwa njia yoyote ile kwani angeweza kuambulia lolote, kwa



    sababu ni mtu wa pili sasa anakutwa mitaa ya kule kwani hata mdogo wake na Zainabu Yule mdada



    aliyekuwa akifanya kazi benki ya biashara mwili mwa maehemu mdogo wake ulikutwa maeneo



    yaleyale,basi tulikubaliana akaniahidi nisijali ataenda na atahakikisha anakuwa makini sana,



    alichukua baadhi ya camera za cctv akaziweka kwenye begi lake baadhi ya vinasa sauti pamoja na



    nyaraka zingine ndogondogo kwa ajili ya kwenda nazo kulepamoja na bastola moja ili ikiwezekana



    zile kamera akazifunge mahali ziwe zinachukuwa matukio yote ya mahali pale, pia alichukua kile



    kiatu ambacho tulikihisi ni cha Yule mwanaharamu ambacho tulikikuta kule nyumbani kwa Gerald



    siku ile ambapo alikidondosha pindi alipoenda kumteka marehemu Furaha. Baada ya hapo tuliondoka



    wote kwa pamoja nikimpa lifti na kwenda kumucha mwenge kisha mimi nikaelekea zangu nyumbani

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kwa bwana Gerald kwenda kumchukua ili tuelekee makaburi ya kinondoni kwenda kutembelea 



    kaburi la mpenzi wake furaha ambaye kutokana na maelezo ya madaktari tuliamni ya kwamba



    atakuwa amekufa kwa kuchomwa sindano ya sumu ili kuficha ushaidi na Yule mwanamke aliyejiita



    eti anakovu jeusi. Bai nilifika nyumbani kwa rafiki yangu Gerald nikamkuta akiwa tayari



    ameshajiandaa akiwa amevalia t-shirt nyeupe yenye picha ya marehemu Furaha mbele ya



    kifua,suruali nyeupe huku pia akiwa amejifunga kitambaa cha rangi yeupe mkononi sikujua alikuwa



    akimaanisha nini.

    Tuliondoka taratibu kutokanna nafoleni ya jijini mpaka mida ya yaa 5 asubuhi tukawa tumeshafika



    tayari makaburini, basi tulipofika kwanza tulitafuta mahali tukapaki gari kisha tukaelekea kwenye



    kaburi lile ambapo baada ya kufika Geral alisali juu ya lile kaburi kisha akawa kama vile anafanya



    usafi na kupanga mashada juu ya lile kaburi, wakati anaendelea nilisikia sauti ya mlinzi wa pale



    makaburini akiniita kwa mbali huku akionyesha ishara ya kwamba gari langu nilikuwa nimelipaki



    vibaya kuna mtu ambaye tulikuta gari yake imepaki pale aina ya escudo rangi ya kijani alidai alikuwa



    anataka kulitoa gari lake basi sikuwa na jinsi zaidi ya kumwambia Gerald anisubili naludi baada ya



    kama dakika 5  nilifika na kulitoa gari kisha nikampisha Yule mtu ambaye alikuwa anatoka mule na



    gari lake wakati naludi kwa mbali nilimuona Gerald akiwa amepiga magoti akisali huku akiwa



    amepiga magoti na mwanamke mkmoja jirani yake nahisi alikuwa hajamuona kwanza sasa nilianza



    kujiuliza Yule atakuwa ni nani? Maana tulienda watu wawili tu na Gerald hakunambia kama alikuwa



    amemuambia mtu yoyote wakutane pale,baada ya Gerald kufngua macho alishituka sana kisha



    nikawasikia kwa mbali kama wakiwa wanazozana na Yule mwanamke basi na mimi nikaongeza



    mwendo kuwahi lile eneo kwa maana niliona kama vile mazozano yamezidi na sio vizuri kwa mtu



    kama yeye kwani ule ulikuwa muda mzuri sana kwake kutuliza akili  Yule mwanamke aliponiona



    nakuja kwa kasi kwanza alishituka kisha akachoma kama kifaa Fulani chenye insha nyembamba kwa



    mbele akamlushia nacho Geral mkononi kisha huyo akakimbia zake kwa kuluka ukuta upande wapili



    nilifika na kumkuta Gerald akiwa tayari amesha kichomoa kile kifaa lakini mkono wake ukiwa kama



    unavimba vile nilimuuliza Yule ni nani na kwa nini imekuwa vile?

    Alinijibu ya kwamba Yule mwanamke ni Yule mwanaharamu ambaye ndio tulikuwa tukimtafuta na



    pale anadai alikuwa ananisubili kwa hamu sana na siku yangu ilikuwa imefika huku akisisitizaya



    kwamba kama tukitaka kuwa salama basi tuachane na ule mpango wetu wa kumfuatilia..!! nafsi



    ilishangaa sana palepale nilijikuta nakosa mpaka raha inamaana nani kamuambia sisi muda ule



    tungekuwa pale?na amejiamini vipi mpaka kutufuata mpaka pale? Je kwanini alimfuata Gerald pindi



    mimi nilipoenda kuondoa gari kwenye parking ili aipite? Nilianza kuhisi sasa ya kwamba Yule



    mwanamke hakuwa peke yake walikuwa wengi waliokuwa wanafanya ule michezo huku



    wakishirikiana pia nilijiuliza Na kile alichomchoma nacho Gerald mkononi ni nini? Kwa maana



    mkono ulikuwa kivimba tu..!! japo alikuwa ameshakichomoa je angekuwa bado ingekuwa aje…?





                                 *******************************************

    Nilimuambia Gerald tuondoke haraka kwani mahali pale palikuwa sio salama tena hatukujua Yule



    mdada alikuwa amejipangaje kama aliweza kuja hadi pale makaburini na kuweza kutufanyia ule



    ushenzi basi tusingeweza kujua alikuwa amejiandaje basi tulielekea kwenye gari nakuondoka zetu



    huku tukipitia hospitali ya regency kwenda kunda kuangalia ule mkono Gerald alikuwa amechomwa



    na nini? Basi tulipofika hospitali daktari alitueleza ya kwamba kile kitu kilichomchoma Gerald



    kilikuwa na sumu kali sana kwanza Yule daktari wa kihindi alianza kutuangalia kwa wasiwasi sana



    huku akishindwa hata kutuelezea akidai ya kwamba kwa kuwa tayari wameshampa dawa basi



    inatosha, baada ya kumsisitizia ndipo akajaribu kutafafanulia kuhusu ile sumu ya kwamba ile ni sumu



    hatari sana na inapatikana nchi ya vietnamu ambayo unapichomwa nayo usipokichomoa hicho kitu



    ulichochomwa nacho ndani ya dakika kama kumi basi uwezekano wa kuendelea kuishi unakuwa



    haupo kabisa,Yule daktari alisema yeye sio mzoefu sana ila anachokijua ni kwamba ile sumu huwa



    wanaitumia huko nchini Vietnam kwenye mapigano yao ya jadi ambapo watu huwa wanaiweka



    kwenye silaha zao za jadi. Tulijikuta mimi na Gerald tukistaajabu sana na kisha kuangaliana bila ya



    kujua ni vipi imekua vile na ile sumu imeingiaje nchini.

    Basi tulimshukuru sana daktari kwa matibabu yake kisha tukaondoka zetu ambapo tulipitia fast food



    kupata chakula cha mchana kisha nikamludisha Gerald mpaka nyumbani kwake na mimi nikaelekea



    nyumbani kwangu sikutaka hata kuludi kazini tena kwani nilihisi ya kwamba muda ulikuwa umeisha



    na isitoshe ni bora niwahi nyumbani nikapumzike nifanye usafi kwani ni mara chache sana huwa



    Napata muda wa kufanya usafi ukizingatia nilikuwa naishi mwenyewe.

                                         *************************************

    Nilifika nyumbani kwangu nakumbuka ilikuwa kama mida ya saa kumi na moja jioni, baada ya kufika



    nikaona nitoe nguo nifanye usafi, ila wakati hata sijatoa nguo nje mara ukaingia ujumbe wa simu



    kutoka kwa Amina ukunitaka tukutane mwenge yeye akiwa anatokea mbezi beach,kuna jambo la



    muhimu sana nilinyanyua simu na kumpigia Amina lakini simu ilikatwa nilijaribu tena vile vile



    ikakatwa mara ikaingia meseji tena samahani jpo mazingira mabaya boss wewe fanya hivyo, basi



    sikuwa na jinsi zaidi kuvaa nguo za jioni kisha kupanda gari yangu na kwenda mwenge kuwahi



    kuonana na Amina, nilitumia kama muda wa saa moja na nusu mpaka kufika lile eneo nilipaki gari



    yangu pale mbele kidogo mwa benki ya efatha kisha nikachukua simu yangu na kumpigia Amina



    ambaye baada ya kupokea aliniambia ya kwamba mbona yeye hakuniambia lolote na wala hajatuma



    meseji yoyote isitoshe yeye alikuwa bado yupo kule mbezi beach akiendelea na uchunguzi, nilikata

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ile simu kisha nikashangaa hii imekaaje? Inamaana kuna mtu alitumia simu ya Amina kuwasiliana na



    mimi au meseji zilijituma zenyewe nilifungua simu yangu upande wa meseji kisha na kuangalia kama



    zile meseji  kweli zilikuwa zimetumwa na Amina au nilikosea nilikuta ni kweli zilikuwa zinaonyesha



    zimetoka kwa Amina, basi sikuwa na jinsi akili ilinicheza haraka haraka nikajua tu atakuwa Yule



    mwanaharamu anatuchezea akili tu hakuna jingine pale pale niligeuza gari kwa kasi ya ajabu na



    kuanza safari ya kuludi nyumbani kwangu.

    Nilipofika nyumbani kwangu hali niliyoikuta haikuwa ya kawaida nilikuta tofauti sana, nilikuta vitu



    vimechambuliwa hovyo hovyo huku ikionyesha dhahiri mule ndani palikuwa pamepekuliwa sana



    nilipoingia ndani chumbani kwangu pia baadhi ya nyaraka zangu sikuzikuta hazikuepo, lakini



    kilichonishangaza ni jinsi milango yangu nilivyoikuta kwani niliikuta kama nilivyokuwa



    nimeiacha,akili ilinicheza nikajua tu Yule mwanaharamu atakuwa amepita kwangu,mungu wangu



    yani inamaana mpaka sasa sisi watu wa usalama tunaanza kuishi kwa woga kisa mhalifu? Hii si sawa



    haina maana ya kuwa wanausalama sasa haiwezekani huyu dada maisha yangu na mimi ayaweke



    hatarini? Na kwa nini hasemi anachokitaka? Na pia huyu mtu anajiamini nini? Na anaweza vipi



    kutuchezea akili kiasi hiki? Na kwanini kila mtu anayejua anajua siri kuhusu yeye au kumfuatilia



    lazima amuondoe duniani? Hii haiwezekani hata kidogo, kwanza kajuaje kama naishi hapa? Nahisi



    kuna mtu atakuwa anampa baadhi ya data pale ofisini kama ikiendelea hivi itabidi mimi nijitoe tu



    katika kufuatilia hii kesi kwa maana sijawahi kukutana na kesi ngumu kama hii.

    Huyu mtu hana huruma hata kidogo kamuuwa kikatili mchumba wa Gerald mchana wa leo tena



    kataka kumuuwa Gerald? Sasa kama uwezo wake ni huu sizani kama atashindwa kumfuata Gerald



    hata nyumbani kwake kumtoa na kumtoa  uhai, nilijikuta natafakari mwenyewe huku nimekaa juu ya



    kitanda changu huku nikitazama jinsi chumba changu kilivyokuwa kimenyambulika,kwa kusachiwa,



    nilijikuta machozi yakianza kunitiririka taratibu pale juu ya kitanda kila nilipojaribu kuoanisha



    matukio kuhusu Yule mwanaharamu, haiwezekani yani afisa upelelezi kabisa wa jeshi la polisi naishi



    kwa wasiwasi hivi hii haina maana kabisa nilijikuta najisemea kila muda maneno yale mpaka usingizi



    ukanipitia pale pale juu ya kitanda.

    Nilikuja kushituka mida ya saa 8 usiku baada ya kuhisi kama kulikuwa na watu wakipita pita nje ya



    kile chumba changu,nilijiweka sawa juu ya kitanda kisha nikashika bastola yangu kwa ajili ya jambo



    lolote kama lingeweza kutokea, niliinuka na kuanza kuangalia kila upande kama kuna usalama au



    vipi, nilizunguka mpaka sebuleni kisha nikachungulia na dirishani nikajihakikishia palikuwa salama



    ndipo nilipogundua tu ya kwamba kilichokuwa kinanitesa ni woga.hivi huyu mwanamke inakuwa



    anatuzidi maarifa?atakuwa mwanamke mmoja kweli? Au watakuwa ni kundi la watu maana siamini



    kama mwanmake mmoja anaweza kuwa na ujasiri wa hivi..!hii itakuwa ni ngumu sana sasa hapa



    najitoa mhanga ngoja nilivagae hiliswala kwa muda wa wiki 2 likinishinda namwambia mkuu



    kwamba basi nimenyoosha mikono. Maana kwa sasa anamuwinda tena Gerald sasa sijui anahisi



    marehemu Furaha kuna vitu alimwambia Gerald? Yani hii ni mbaya na aibu kwa jeshi letu yani



    watoto wa mjini wapelelezi wazima tunazidiwa mbinu kweli hii ni mbaya sana.

                                      *************************************

    Asubuhi kama kawaida yangu niliamka na kufanya mazoezi ya viungo vya mwili kisha nikajiandaa



    kwa ajili ya kuelekea ofisini kwenda kulipoti kisha kundelea na majukumu mengine.nilipofika ofisini



    nakumbuka vizuri sana siku ile nilimkuta Amina akiwa tayari ameshafika tuliingia ofisini kwangu



    kisha akaanza kunihadithia kuhusu jana yake alivyokuwa kule mbezi alipoenda kumfuatilia huyu



    mwanaharamu,kaka yangu zile kamera nilizifunga kisha mimi nikaenda kukaa mahala kwa mbali



    kidogo ambapo kulikuwa na mama lishe huku nikiwa nalaptop yangu nikifuatilia kila kitu



    kilichokuwa kikiendelea pale, alisimama kuzungumza Amina huku akivuta pumzi kwa juu.huku mimi



    nikimtazama usoni kwa umakini na macho yangu yaliyokuwa yamekata tama.ndio nakusikiliza



    nilimwambia,huku nikimuona akitoa laptop yake na kuanza kunionyesha baadhi ya matukio,



    nilimuona mwanamke aliyekuwa amevalia suruali ya blue poolneck la rangi ya kaki miwani mieusi



    akitokea mhali pasipojulikana maana palikuwa kama kuna mfuniko Fulani hivi mahali pale nahisi



    alikuwa kama ametoka kwenye pango Fulani hivi kisha akaenda moja kwa moja mpaka kwenye zile



    kamera na kuzichukua zote,shiit huyu mwanamke alijuaje kama umefunga kamera hayo maeneo?



    Inamaana huyu mwanamke anaakili kuliko sisi nilimwambia aludishe ludishe nyuma pale alipokuwa



    akitoka na kuigandisha sura yake ambapo tuliipiga picha afadhali huyu mwanamke hapa ndipo



    yatakuwa makazi yake. Mitaa hii nilianza kumwambia Amina ila kinachonishangaza ni jinsi kila



    jambo tunalopanga anakuwa analijua hapo ndipo panapo nitatiza na kisha nikamuhadithia jinsi jana



    mimi na Gerald yaliyotukuta kule makaburini na jioni alivyonichezea akili kisha akaingia nyumbani



    kwangu na kufanya ukaguzi na kuondoka na baadhi ya nyaraka basi tulimaliza mazungumzo pale na



    Amina kwa kuahidiana ya kwamba inabidi tujipange tukafanye uvamizi tukiwa na askari kwa



    kutosha lie eneo, tuliagana na Amina huku akiwa anatoka nje ya ofisi yangu huku akiniachia laptop



    yake ili niendelee kumuangalia kwa umakini Yule mwanamke katika zile crip mara nikasikia simu ya



    mezani pale ofisini kwangu ikiita nikanyayua waya kupokea ile simu upande wa pili kulikuwa na



    sauti ya kike ambapo ilianza kuzungumza bila kupumzika kwa maneno makali.

                                                            ********************************

    Nilitulia tulii nikimsikiliza Yule mwanamke ambaye alikuwa akitoa vitisho sana hasa kuhusu



    kumfuatilia kwangu akijitambulisha kwamba yeye ndio mwanamke mwenye kovu jeusi, na ya



    kwamba kila kitu alikuwa anakijua, tunachokifanya kwani mtandao wake ulikuwa ni mkubwa sana,



    alizungumza kwa vitisho sana, nilitulia kimya nikimsikiliza kwa makini mpaka alipomaliza kuongea,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ndipo nilipomuuliza sawa dada umemaliza? Hakunijibu zaidi ya kukata simu tu, nilijaribu kuangalia



    tena namba ya simu aliyonipigia kwenye simu yangu lakini sikuikuta hata nikajua itakuwa kama



    kawaida yake huyu mwanamke atakuwa ametumia private namba ili tusiweze kumtambua kwani



    namba yake ilikuwa hata haisomi kwenye mitandao ya simu, basi niliendele kuiangalia ile picha yake



    pale kwenye laptop huku nikiigandisha ili kuiangalia kwa umakini zaidi, nilipojilizia na ile picha



    nilimpigia simu Amina aje ofisini kwangu huku akiwa na nyaraka mbalimbali zote zilizohusu Yule



    mwanamke baada ya dakika 5 Amina aliingia huku akiwa amebeba nyaraka zote wakati anaingia



    mule ofisini kwangu mara Amina alijikwaa yale mafaili na vitu vingine vyote alivyokuwa amebeba



    vikadondoka chini,mungu wangu nusura ajipigize kidevu kwenye meza iliyokuwa pale ofisini kwangu



    bahati nzuri aliwahi kuweka mkono pale mezani, nilimpa pole huku nikisimama na kwenda kumsaidia



    kuokota yale mafaili na vitu vingine ambavyo alikuwa amevibeba na kuja navyo mule ofisini kwangu



    wakati nakusanya vitu pale chini nikakiona kiatu cha kike kile ambacho tulikichukua nyumbani kwa



    Gerald siku marehemu Furaha alipoenda kutekwa nyara na Yule mwanamke haramu kama mimi



    nilivyopenda kumuita ambacho tulisadiki kitakuwa ni kiatu cha Yule mwanaharamu, nilipokiinua kile



    kiatu pale chini mara kwenye kisigino nikaona kama kumetikisika hivi halafu kukawa kama kuna vitu



    vinacheza cheza kwa ndani nilipokibinua na kukitoa kile kisigino mungu wangu mule ndani ya kile



    kiatu niliona kuna vifaa Fulani hivi vya mawasiliano, japo mimi sikuwa mtaaramu sana wa mambo ya



    erectronics ila niliweza kuona kuna kama kipaza sauti kidogo hivi, huku kikiwa kimeambatanishwa



    na vitu vingine vikiwa vimewekwa kwa ustadi mkubwa mule kwenye kile kisigino cha kile



    kiatu,nilijikuta naacha hata kuendelea kukusanya vitu vingine na kuludi kwenye kiti changu huku



    Amina akinitazama sana akiwa hajui ni kipi kilikuwa kinaendelea,nilimuonyesha vile vinasa sauti



    alishangaa sana pia na yeye, kumbe ndio maana kila siku tunakuwa tunalaumiana ya kwamba  huyu



    mwanamke siri zetu anakuwa anazipata wapi kumbe hiki kiatu ndio tukiwa tunazungumza yeye



    anazipata habari zote moja kwa moja mungu wangu, alizungumza Amina kwa sauti ya upole ila



    iliyojaa udadisi sana huku akitazama kile kiatu na kuitoa ile microphone na kuwa kama anaichezea



    chezea vile  mipango yake sasa mwisho wake umefika, nilimtazama kisha nikamuambia sikia hicho



    kiatu kitoe kwanza nje ndipo tuanze mazungumzo kwani hadi hapa tunapozungumza maongezi



    anayasikia huyu mwendawazimu, Amina alitii kile nilichomuambia akakitoa kile kiatu nje kisha



    akaludi mule ofisini kwangu tukaendelea na maongezi.

    Kwetu tuliona ni hatua kubwa sana kwani mpaka pale tulikuwa tumefanikiwa kupata mkanda wa



    video uliokuwa na picha ya Yule mwanamke japo haonekani vizuri sana, lakini pia tulikuwa



    tumefanikiwa kugundua kifaa alichokuwa akikitumia kunasa mazungumzo yetu ambayo kuna kipindi



    mpaka sisi wenyewe ilikuwa inatuchanganya mpaka tukawa tunahisi wenyewe tunasalitiana,



    tulipanga usiku ule ule kwenda kuweka kambi mitaa ile huku tukiwa na kikosi cha kutosha



    kuhakikisha Yule mtuhumiwa tunamtia kifungoni siku ile kwani karibia mambo yote muhimu



    tulikuwa tumefanikiwa kupata basi nilitoka pale ofisini kwangu huku nikiwa nimemuacha Amina



    mule ndani na kwenda ofisi ya mkuu wetu wa kazi kwa ajili ya kumuambia maazimio tuliyokuwa



    tumefikia ili ikiwezekana aweze kutupatia vitendea kazi vya kutosha pamoja na wasaidizi wa kwena



    nao kwenye operesheni ya usiku ,mkuu wetu alituelewa akadai pia na yeye atashiriki katika ile



    operesheni siku ile akiwa kama msimamizi mkuu pia akasema tusiende wengi twende watu wa nne



    tu, tunatosha kumdhibiti, sikuwa na la kumpinga, nilijua pia ya kwamba mkuu na yeye alitaka



    akashiriki kwa minajili ya kujijengea umaarufu hasa kama tukifanikiwa kumkamata kwani kazi yote



    itaonekana kama aliifanya yeye ili aweze kujenga sifa nzuri ikibidi apandishwe hata cheo kwani



    mabosi wengi wa upelelezi huwa hapo hivyo wanapenda sana wao kupata sifa za mwishoni



    mwishoni, basi tulikubaliana pale na inspekta Thomas ambaye ndio alikuwa mkuu wetu wa kazi



    kwamba itabidi mida ya saa kumi tuanze safari ya kuelekea huko,basi tulitawayika kila mmoja

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    akiendelea na shughuri zake.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog