Search This Blog

Sunday 19 June 2022

KAFA NA UTAMU WAKE - 1

 





     IMEANDIKWA NA : BABI D'E CONSCIOUS



    *********************************************************************************



    Simulizi : Kafa Na Utamu Wake

    Sehemu Ya Kwanza (1)





    Ukikutana nae lazima utashtuka na kama akikupita lazima utageuza kichwa nyuma kumtazama kwa mara ya pili, Harufu ya marashi ya gharama aliyojipulizia ndicho kitu pekee itachokukufanya utambue kuwa anatoka katika familia inayojiweza, Kweli mungu akiamua kukupa anakupa kila kitu na kama akiamua kukupunja basi atakupunja pia. Mchanganyiko wa rangi toka kwa Mama yake mwenye asili ya kigiriki na baba yake Mdigo wa Pangani Tanga ndio uliopamba ngozi yake kuonekana yenye hadhi zaidi. Macho yake ya gololi na vishimo katika mashavu yake pindi anapotabasamu ndio sukari ya kila jicho lenye uhitaji pindi linapomtazama na kukutana nae akitabasamu si Mwingine ni kijana wa kidigo Moudy.

    Akiwa mwenye huzuni kakaa kwenye kiambaza cha nyumba yao akitazama usawa wa geti kubwa la nyumba yao, Moudy ama Moudylove kama alivyopenda kujiita alikua akiangalia geti huku akiangalia saa kila mara kama anasubiri kitu muhimu kitokee mbele ya macho yake. Ghafla anasikia sauti ya Geti likisukumwa anashtuka na kuamka haraka kulifuata geti.

    …………………………………………………………………………



    Meli ya Mv Sulivia ilikua ikitia nanga katika bandari ya Zanzibar Unguja baada ya safari ndefu kutoka Pemba, Abiria waunguja wanatoa mabegi yao kutoka sehemu za kuhifadhia mabegi na kuanza kushuka katika Meli hiyo kuukuu. Makuli katika bandari ile wanabeba mizigo kuingiza katika sehemu ya nyuma ya Meli ile iliyopangwa mapipa mengi yenye maandishi SOS. Abiria wengine wanapanda kwenye ile meli.

    Babuuu sogea hapo niweke mzigo” kuli alikua akimwambia mzee Mwinyi aliyekuwa amekaa pembeni ya mapipa na Mjukuu wake huku kaegemezea Kichwa katika yale Mapipa. Mzee Mwinyi anasogea upande wa pili Yule kuli anaweka gunia kubwa pembeni ya Mjukuu wa Mzee mwinyi.

    Triii triii tii Sauti ya mlio wa simu inasikika Mzee Mwinyi anaingiza mkono kwenye kanzu yake kuu kuu na kutoa simu kasha anapokea na kusikiliza.” Eeh ndiyo tuko unguja hapa atii, Eeh we ondoa shaka bwana mie nikifika hpo mambo yote yetakuwa sawa mwambie kijana atapona tu. Ok sawaaaa” anatoa simu sikioni kasha anairudisha kwenye mfuko wa kanzu Meli inaanza kuondoka.

    …………………………………………………………………………



    Moudy anafungua geti Mzee Mahmoud Mdigo baba yake na Moudy anaingia Moudy anampokea na maswali, Baba huyo dokta yuko wapi? Mzee Mahmoud anamuangalia Moudy kwa huruma kasha anampa ishara amfuate wanaingia ndani na kukaa kwenye kochi. “Mwanangu nafahamu fika hali uliyokuwa nayo inakutesa sana nimejitahidi kwa kila njia ili uweze kuwa sawa na hapa karata yangu ya mwisho iko kwa Mzee Mwinyi ambaye nimeongea nae muda si mrefu ndo wanatoka unguja kuja hapa kukutibu amini utapona mwanangu” Moudy anafuta machozi “Baba mimi ni kijana sasa nateswa na hali hii na kila sifa ya kuitwa mwanaume ninayo ni hiyo moja tu ndiyo haiajakamilisha uanaume wangu baba please help me” Mzee Mahamoud akimpigapiga Moud mgongoni Usijali mwanangu. Moudy anainuka na kutoka nje ya geti anabamiza geti kwa nguvu.

    ………………………………………………………………………………



    Ndani ya chumba namba 509 katika hoteli ya Blue star kwenye kitanda chenye ukubwa wa futi nane kwa nane alikua amelala kwa tumbo msichana mrembo akiwa amevaa kanga moja tu huku huku vilima vikubwa viwili vikiwa vimeinua kanga aliyovaa huku akiwa bize akichati katika mtandao wa facebook kwa kutumia laptop yake ndogo . Huyu ni Trina Mpenzi wake na Moudlove na siku hiyo ilikua ni siku ambayo waliahidiana kupeana penzi zito baada ya kuwekeana ahadi ya muda mrefu kutokufanya mapenzi mpaka wamalize chuo na siku imewadia. Wimbo mlaini wa westlife uliokuwa ukitoka katika simu ulimshtua Trina na kugeuka kwa haraka ambayo ilisababisha kanga aliyovaa kufunuka na kuonekana mapaja yake meupe malaini huku mkanda wa kufuli la rangi ya pink watoto wa kileo huita G string kuonekana, Trina hakujali kwa kuwa yuko Mwenyewe pale chumbani aliiachia kanga iuache mwili wake wazi akasogelea meza na kuchukua simu alipoitazama akatabsamu na kuponye

    za kitufe cha kupokelea na kupeleka sikioni. Ndiyo mpenzi wangu” Sauti laini ya Trna ilijibu Simu ile, “Chumba namba 509, Ok sawa” Trina akakata simu kwa furaha akaruka kitandani huku akichanua miguu yake na kufanya utajiri wa wasichana wa kileo kuonekana kwa upande mmoja.

    …………………………………………………………………………………





    Meli ya Mv Sulvia iliendelea kukata mawimbi huku ikionekana kuelemewa kwa mizigo na abiria, Nahodha wa meli ile bwana Twalib alishtushwa na mwendo mdogo wa meli ndipo alipotazama engine metter ya meli na kugundua injini moja ilikua imezimika. “Dah ile injini ndio imemalizika” Twalib alimwambia Nahodha mwenzake aitwaye Masoud kwa unyonge. “Sasa hii injini moja itatufikisha kweli” Kabla Twalib hajamjibu Masoud ghafla injini iliyosalia nayo ikazima. Mvua kubwa ikaanza kunyesha ikiambatana na upepo mkali Ile meli ikaanza kusukumwa na mawimbi amakubwa Abiria wakaanza kupiga kelele za woga.

    Moudlove alisukuma mlango namba 509 macho yake yakatua kitandani na kukutana na msichana mrembo Trina. Trina kwa furaha akamrukia Moudlove na kuanguka nae kitandani huu akimbusu mfululizo, subiri kwanza Moudy alimwambia Trina huku akimsukuma. Aah baby mwenzio natakaaa Trina aliongea kwa sauti iliyolemewa na Mahaba mazito. Moudy akasimama na kwenda kukaa katika kochi lililo pembeni ya kile kitanda, Akaegamiza kichwa chake juu ya viganja vya mikono huku machozi yakimtoka. Trina akamfuata huu kalegeza macho kimahaba anamvuta Moudy, Aah njoo unipe Mpenzi” Moudy anasimama na kumuangalia Trina kwa huruma “Trina siwezi mpenzi wangu” Trina kwa mshao “Huwezii? Huwezi nini?” Moudy kwa unyonge “Sikiliza mpenzi wangu Trina mimi unavyoniona hapa Jogoo wangu Hapandi Mtungi na leo nilitegemea ndio naletewa dawa ila shida huyo dokta anatokea Pemba mpaka sasa hajafika ndio maana nilichelewa kufika mpenzi” Trina kwa Hasira “Eeh eti nini yaani Moudy muda wote ulionipotezea kumbe wewe jongoo tu? Yaani wewe ni joka la kibisa huumi wala huna sumu? Sasa sikia leo lazima unishushe pepo langu la ngono haiwezekani kama jogoo hapandi mtungi leo sasa atapanda pipa?” Trina anamshika Moudy kwa nguvu na kumsukumia Kitandani. Moudy kwa upole anambembeleza Trina, Sikiliza Trina leo lazima nitimize ahadi nipe muda huyo dokta afike tatizo langu litakwisha tu” Trina anamuangalia Moudy kwa dharau “mmh uzuri wa bure kumbe sanamu la duka la nguo? Sasa sikia hutoki hapa ndani na hiyo dawa uletewe hapahapa na ukishindwa nitekenya leo basi nitakuitia watu wakutekenye wewe?” Trina anaongea kwa jazba kasha anainuka na kufunga mlango kwa funguo funguo anaiweka kwenye pochi yake.

    …………………………………………………………………………………





    Kelele za abiri ndizo ziliwachanganya manahodha wa meli hiyo na kushindwa kuelewa watafanya nini?. Mimi nafikiri ni lazima tufanye kitu alisema alisema Twalib huku akiamka kutoka nje.Masoud alimfuata nyuma huku akionekana kukosa cha kufanya. Mawimbi makubwa walianza ipiga meli kelele ya woga aliyopiga Mjukuu wa Mzee Mwinyi ilimshtua mzee Mwinyi toka usingizini ile kufumbua Macho mara akashuhudia pipa kubwa lilkishuka kumuelekea mjukuu wake, Mzee Mwinyi aliamka kwa kasi na kumzuia mjukuu wake kwa kumlalia lile pipa likashuka juu ya mgongo wake akapiga yowe kubwa la uchungu kiza cha milele kikatawala mboni za macho yake, Kimya milele.

    ………………………………………………………………….



    Ukimya uliotawala katika kijiwe cha kahawa maarufu Kariakoo kama Radio Mbao ulimshangaza Mzee Mahmoud Mdigo ndipo alipovutiwa na kusogea baada ya kuona kundi la wazee wakisikiliza kitu kwa makini kutikati yao, Asalaam aleykum? Alitoa salamu lakini hakuna aliyemjibu kutokana na masikio yao kuwa makini na sauti kutoka katika redio ndogo ya kianalojia iliyokuwa ikitoa sauti ya kukoroma kama imeishiwa na betri. Mtumee watu miambili wamekufa mpaka sasa? Aliropoka Abdul Mzaramo maneno hayo yakamvutia zaidi Mzee Mahmoud Mdigo kutaka kujua nini chanzo cha maneno hayo na kujikuta akiuliza Kumetokea nini jamani? Abdul Mzaramo alimjibu kwa masikitiko. Meli ya Mv Suliviana imezama ilikua ikitokea pemba kuja Dar na imezama kilometa chache kufika bandarini. Mzee daudi wawi akadakia Imezamia hapo msasani, Mzee Mahmoud Mdigo kwa Taharuki akaondoka huku akiwa anatoa simu yake na kupiga namba Fulani simu yake haikutoa majibu ya kumridhisha akaiweka mfukoni na kuvuka barabara.kuelekea njia inayoelekea Posta.

    …………………………………………………………….



    Mlio wa simu ulimshtua Moudlove kutoka katika lindi la mawazo na kujinyanyua akatoa simu yake mfukoni na kuiangalia akaona jina Dad akatabasamu na kumuangalia Mpenzi wake Trina na kumwambia Jiandae na pambano baada ya dakika chache zijazo ndo utajua jogoo asiyepanda mtungi atapandaje sasa n nilivyo na usongo nitakutafuna mpaka mifupa kwa mbwembwe anapokea simu akichanganya na maneno ya kizungu. Yes Dad…. Whaaat? Moudlove anadondoka chini kama gunia la viazi lililoachiwa toka kwenye gari mpaka chini. Trina akaamka haraka na kuanza kumpepea Moudlove alipoona hkuna matarajio ya kuamka akakimbilia simu iliyo pale chumbani na kupiga mapokezi akiomba msaada. Zikasikika hatua za mtu akija mlango ukagongwa kwa haraka Trina akatoa funguo katika pochi yake na kufungua mlango, Akaingia kijana mtanashati na kumtazama Trina kwa mshangao huku akitoa macho ya tamaaa. Vipi mbona unanishangaa? Trina alimuuliza Yule muhudumu, ah! samahani hujavaa nguo!, Trina kwa woga kama kazinduliwa usingizini akakimbilia kanga iliyo pale kitandani na kujifunika huku akimuangalia Yule muhudumu kwa aibu. Yule muhudumu akamsogelea Moudlove na kumgusa mapigo ya Moyo na kumuangalia Trina kwa wasiwasi Mh dada yangu huyu mwenzako ameshakufa.., Trina akapigwa na butwaa kutokana na yale maneno aliyotoa Yule muhudumu Sasa kaka yangu nitafanyaje? Kwa kweli sijui hichi kifo cha huyu jamaa kitakugharimu kama Yule dada wa Filamu za kibongo, Yule muhudumu alijibu huku akitaka kutoka nje mara Trina akamvuta ndani, Kaka yangu nisaidiee Ghafla kanga ikadondoka chuchu zilizosimama zikachomoza kama jua la saa nne katika mboni za macho ya Yule muudumu na kujikuta macho yake yametulia juu kifua cha binti mrembo Trina, Muhudumu akafunga ule mlango kwa funguo na kumsogelea Trina kwa Tamaa ya ngono. Sikia nitakusaidia ila ni lazima unionjeshe? Yule muhudumu alimjibu huku akitetemeka, Trina alijikuta akitingisha kichwa kuashiria hajaafiki. Sawa kama hutaki basi jela itakua inakuita… Trina alijikuta anampokea Yule muhudumu na kumruhusu kuanza na zile embe ndogo changa pale kifuani na kujikuta akilalamika kwa sauti ya Mahaba tayari Jogoo wa Muhudumu kapanda mtungi ambao Moudlove alishindwa upanda kwa masaa machache yaliyopita.

    ………………………………………………………………………………



    Mtu ajinyonga kwa Mkanda ndani ya hoteli ya Blue star, Sharobaro ajitundika hotelini, Kijana ajimaliza mwenyewe hotelini , Hivyo ni baadhi ya vichwa vya habari ya magazeti asubuhi ni baada ya Mwili wa Moudlove kukutwa ukiwa umetundikewa kwenye feni kwa kutumia mkanda wake. Hiyo ndiyo ilikua mwisho wa filamu ya maisha ya moudlove katika Ulimwengu huu ambayo ilikamilishwa mbele ya mpenzi wake Trina.

    Katika Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili watu walikuwa ni wengi huku wauguzi wakisaidiana na wasamaria wema kuwaingiza wagonjwa huku wakiwaandikia namba, Vitanda vilikua vimejaa na wengine kulazwa chini. Maiti zilikua zikipitishwa kwa mafungu kuelekea katika chumba cha kuhifadhia maiti, Kila mmoja katika hospitali ile alionekana ni mwenye huzuni huku vilio vikisikika kila kona ya hospitali hiyo kutoka kwa ndugu na jamaa za waliopatwa na ajali hiyo. Huyo mpelekeni kule ICU, ilikua ni sauti ya dokta akitoa maelekezo kwa manesi wampeleke chumba cha wagonjwa mahututi mgonjwa mmoja aliyeonekana kapoteza fahamu huku akiwa ameumia sana maeneo ya kichwani hasa sehemu ya Paji la uso wake. Huyo alikuwa ni Jorome mjukuu wa Mzee Mwinyi aliyekuwa ameongozana nae kuja Dar kumletea Moudlove dawa.

    Magari yalikuwa yakiingia pale hospitali yalikuwa mengi sana mpaka ikafikia magari kuzuwa barabarani na makundi ya watu kutembea kwa miguu kuingia hospitali ya Muhimbili. Ajali ile ya Meli ya Mv Sulivia ilikuwa kubwa zaidi ya ajali zote za vyombo vya usafiri wa majini. Rais wa nchi akatoa siku Tano za Maombolezo kwa msiba mkubwa kwa Taifa.

    Nesi mfunikeni huyu mgonjwa ameshakufa, Dokta Lyimo alikuwa akiwaambia manesi wafunike mwili wa Jorome huku Dokta akiwa anatoka nje, Manesi walifunika mwili wa jorome na kuanza kusukuma Kitanda cha matairi kumtoa nje ya ile wodi Ghafla wakasikia Mtu kapiga chafya kwa mshtuko nesi akafunua shuka na kumkuta Jorome akiwa amefumbua macho. Doktaa doktaaa! Nesi aliita huku akimkimbilia dokta Lyimo. Kunashida gani? Dokta Lyimo aligeuka na kuuliza. Yule mgonjwa hajafa ni mzima, Dokta Lyimo alitoka akikimbia mpaka kule ICU na kumvalisha Jorome mirija ya oksijeni.

    ……………………………………………………………………………



    Baada ya mwezi mmoja Jorome alipona kabisa na kuruhusiwa kutoka hospitali huku serikali ikiwa imewalipia wagonjwa wote walioathiriwa na ile ajali gharama zote za matibabu. Jorome alijikuta yupo katikati ya jiji la Dar akishangaa urefu wa magorofa na wingi wa magari tofauti kabisa na mazingira aliyokulia ya huko pemba. Taratibu akajisogeza mpaka kwenye maeneo ya kupumzikia yaliyopo Mnazi mmoja na kuketi huku akifikiri nini atakachofanya ili kimuingizie pesa na apate na sehemu ya kulala katika jiji hilo la wajanja aka Bongo.

    Kuruta muokota makopo ya maji maarufu jijini Dar alikuwa katika kazi yake kabeba mfuko mkubwa huku akiokota kila kopo na kuweka katika mfuko wake uliokuwa na rangi nyeusi kutokana na uchafu. Anafika karibu na alipokaa Jorome nakuweka mfuko wake pembeni kisha anatoa gazeti limefungwafungwa anafungua nakutoa maandazi anakula huku akinywa na maji. Jorome anamuangalia kuruta kisha anajisogeza karibu yake na kumuomba maandazi, kuruta anamshangaa Jorome alivyo na sura mbaya iliyoshonwa shonwa, Eh wewe ni nani? Kuruta alijikuta akimuuliza Jorome kwa mshangao, Miye naitwa Jorome miye mgeni hapa Dar es salaam, Jorome alijibu kwa lafudhi yake ya kipemba. Kuruta alimpa Jorome andazi nay ale maji yaliyobakia huku akimuangalia anavyokula kwa kasi. Huo ndio ukawa m wanzo wa urafiki wa Jorome na Kuruta na ndio mwanzo wa Jorome kuanza kazi ya kulizunguka jiji zima kwa miguu akiokota Makopo ya maji.

    ……………………………………………………………………



    Muite Jorome sura mbaya au gari la Taka kama alivyokuwa akitambulika na wakazi wa jiji la Dar kazi yake ni kupita nyumba hadi nyumba na kubeba taka kisha kuzipeleka dampo kwa ujira wa shilingi mia mbili kwa kila mfuko wa Taka aliobeba katika nyumba. Akiishi katika chumba kimoja cha udongo katika nyumba za mzee mswahili huko Machimbo Yombo vituka anayolipia kwa kodi ya shilingi elfu sita kwa mwezi. Hakuna asiyemjua gari la taka ndani ya jiji la Dar. Ilikuwa ni jumamosi muda wa saa tisa na nusu Jorome alikuwa katika nyumba ya Mary stela mwanamke mwenye mvuto wa kipekee na ni mke wa kanali wa jeshi la wananchi na anayeishi katika nyumba iliyo katika fukwe wa bahari ya hindi eneo la kunduchi. Jorome alikuwa akizibua chemba ya choo iliyokuwa imeziba. Mara mvua kubwa inaanza kunyesha jorome ananyeshewa lakini hajali anaendelea kufanya kazi yake mpaka muda wa saa kumi na mbili kamili za jioni Jorome anapomaliza kazi yake mvua ilikua haijakatika, Mary stela alimuangalia Jorome kwa huruma akamwambia aingie ndani aoge kisha asubiri mvua ikatike. Jorome akaingia ndani Mary stela akampa Taulo jeupe na kumwambia avue nguo hapo sebuleni kisha avae taulo akaoge huku yeye akiingia katika moja ya chumba ya ile nyumba. Chorome akavua na kuingia bafuni kisha akaoga alipotoka akamkuta Mary stela kashika nguo kaka pale sebuleni. Nywele zilizoanzia kifuani mwa Jorome na kushuka mpaka katika tumbo na kuzama katika taulo kuelekea maeneo ya kitovu cha Jorome zilimshtua Mary stela akajikuta damu ikimuenda mbio na kumsogelea Jorome huku akihema juu juu. Njoo huku uvae nguo anamshika mkono na kumvuta kwenye moja ya chumba kingine katika ile nyumba tayari pepo wa ngono alikuwa amekwisha panda katika ubongo wa Mary stela na kukaa katika mfumo wa akili wakati huo alikuwa akiwaza ngono tu. Jorome kwa hofu akamfuata tajiri yake Yule wakaingia ndani akakaribishwa na kitanda kikubwa cha futi sita kwa sita. Mary stela akafungaa mlango kisha akavu nguo nakubakiwa na chupi nyeupe iliyo kama chandarua inayoonyesha kila kitu chake katika mwili wake kilichopaswa kufichwa na chupi ile. Hapana boss nipe nguo nivae miye, Alisema Jorome huku akirudi nyuma. Sikia Jorome mpenzi nitakupa chochote mwenzio nina muda mrefu tokea mume wangu aende kwenye semina sijawahi, Mary stela anavuta taulo alilovaa jorome linaanguka macho yake yananakutana na Pingili ya muwa Bungala ukiwa umesimama vyema. Sikiliza subiri kwanza Jorome anamjibu Mary stela halafu anaokota taulo na kujifunika anakumbuka maneno ya babu yake mzee Mwinyi aliyowahi mwambia “Mjukuu wangu kila kiungo cha mwanamke kina thamani katika mapenzi kabla ya chochote hakikisha unamuamsha kila kiungo kiwe tayari kwa kupokea Mahaba yako ili pindi utakapoachana nacho kila kiungo kikikumbuke” Jorome akatabasamu sura yake ikazidi kuwa mbaya akamshika mary stela na kulmaza kitandani akaanza kucheza na kidole cha mwisho cha mguu wa Mary stela na kuhamia katika unyayo kelele za mahaba toka kwa Mary stela zikaanza kusikika, Jorome akazidisha ufundi kwa kumparua kwa ukucha wake wa kidole chake cha mwisho cha mkono katika mkunjo wa mguu wa kushoto huku ncha ya ulimi wake ikitembea katika mbavu za mary Stela hapo kelele ikazidi kutoka kwa Mary stela ghafla wakasikia sauti ya mlango ukigongwa kwa nguvu wakakurupuka kama huku Jorome akitetemeka Mary stela anachungulia nje kupitia dirishani anaona gari ya mumewe imepaki.

    ……………



    Mary Stela huku akitetemeka akamuingiza Jorome uvunguni kisha akasogelea mlango kwa woga na kufungua huku akichungulia nje kwa Woga, Sura yake ikakutana na Macho makavu ya Wadada Mfanyakazi wake wa ndani kwa woga akamuuliza, Kuna shida gani? Wadada akimpa funguo ya gari, Huu funguo kaleta John Yule fundi wa gari ya baba kaja na gari kasema baba alimuachia gari wakati anasafiri ilileta tatizo sasa keshaitengeneza ndo kairudisha. Mary stela akapokea ule funguo na kufunga mlango kwa hasira akarudi ndani na kumtoa Jorome chini ya mvungu, Jorome akitokwa na jasho la uoga Mary stela akaanza kumchezea nywele za kifuani huku akilalamika kimahaba wakajikuta wako kitandani watupu huku jorome akimliza kilio cha mahaba. Walishtuka ni saa kumi na mbili asubuhi Mary stela alianza kushtuka na kumuamsha Jorome, Mpenzi naomba unipe Bed Tea Mary stela alimwambia jorome huku akimkumbatia. Jorome alianza kwa juice tamu ya Romance kisha akampatia main Tea ambayo ilimliza tena Mary Stela huku akitaja jina la Jorome kwa kkifupi bila kumalizia, Ooh Jo! Aaah jo wangu mwisho wa siku akajikuta anampatia Jorome pesa za kutosha na Kumuaga Jorome akarudi kwake Yombo kwa kazi nzito yenye over Time na marupurupi ya kutosha mfukoni.

    …………………………………………………………………………..

    Kama ilivyo desturi muonja asali haonji mara moja ni saa saba usiku Jorome yupo juu ya kifua cha Mtu mzima Mary stela akitimiza jukumu lake la kazi, Mara wanasikia Geti likifunguliwa Mary stela kama Mcheza mieleka akamweka Jorome pembeni na kuchungulia dirishani akakutana na sura ya Mumewe akiwa kabeba begi kubwa. Jorome akavaa nguo haraka, Mary stela alimwambia jorome huku akitetemeka Jorome akachukua suruali na kuvaa harakaharaka akaweka boxer mfukoni kisha Mery Stela akamshika mkono na kumpitishia mlango wa jikoni akamumwambia asimame katika pembe ya nyumba kisha akakimbia mlango mkubwa wa sebule akampokea mumewe begi, Masaii Mary stela alimuita mlinzi wa getini, Masai akakimbia kuja kumfuata Mary Stela, Embu nisaidie kuingiza begi ndani, Mumewe akatangulia ndani Mary stela akakimbiaa jikoni na kumwambia Jorome atoke geti liko wazi Jorome kwa haraka akakimbia na kutoka nje.

    …………………………………………………………………………………………….

    Ni saa saba na dakika nyingi Jorome anatembea pembezoni mwa fensi za nyumba za matajiri katika eneo la kunduchi Ghafla anasikia sauti za mbwa na mara milio ya risasi inasikika, Anakimbia na kujificha kwenye mtaro anaona watu wanatoka kwenye nyumba moja wamebeba begi kubwa ghafla wanatokea walinzi wenye sare na kampuni ya ulinzi wamebeba silaha wanaanza kufyatuliana risasi, Wale majambazi wanakimbia na kulitupa lile begi katika mtaro Jorome aliolala kisha wanakimbia na kutokomea gizani, Mara anawaona wale walinzi wakirudi na kupotelea katika zile nyumba, Jorome kwa hofu anasogelea lile begi analibeba na kuondoka huku akikimbia.

    ……………………………………………………………………

    Asubuhi katika chumba kidogo cha udongo Jorome kaka kwenye kiroba pembeni kuna lile begi anatoa pesa nyingi katika lile begin a kuweka katika kiroba huku akijaribu kuweka chini kama godoro, Anatabasamu kisha anachukua pesa nyingine anaweka mfukoni, Anatoka nje na kwenda katika kibanda cha Mama chau anakaa na kuagiza chapati maharage na chai, Mama chau anamuangalia kwa hasira, Leo pesa mbele na deni langu unalilipa. Jorome anaingiza mkono mfukoni anatoa noti mbili za elfu kumi kisha anamkabidhi Mama chau, Hizo nimekupa tu we weka nilichokwambia nitakulia, Mama chau kwa mshangao. Eeh umeokota pochi ya mzungu nini anaweka chapatti maharage na chai anampa jorome. Jorome anakula kisha anampa Mama chau noti ya elfu tano anatoka katika kile kibanda bila kudai chenchi.

    ……………………………………………………………………………………….

    Dayana Rose, Dayana Rose au D Rose kama alivyopenda ka kujiita alikuwa akijulikana na watu wengi sana kwa mbwembwe zake anapokuwa katika kiipindi chake cha love story kinachorushwa na Redio Sweet Fm, Sauti yake tamu ndiyo huwateka watu pindi anapozungumza na zaidi ya yote muonekano wake wa kiume ndio uliomfanya kila mtu amzungumzie, Hakuna mwanaume aliyefikiria kumtongoza kwa kuwa alikuwa na muonekano tofauti sana. Wakati watu wakimfikiria D rose hivyo mawazo ya Yassin yalikuwa tofauti kabisa yeye alikuwa akimfikiria D rose kwa upande mwingine, Upande wa Mwanamke mrembo ambaye atapata nafasi ya kulala nae japo usiku mmoja. Yassin alijaribu kila njia ili aweze kumpata D rose lakini aligonga mwamba kwa dharau za D Rose na maneno ya kejeli aliyokuwa akipata toka kwa D Rose. Hivi wewe jinsi ulivyo una hadhi ya kutembea na mimi kweli? Mimi si daraja lako. Ni maneno ya karaha aliyokuwa akiyapata Yassin kutoka kwa D Rose kila mara.

    ………………………………………………………………………

    Jorome akiwa kavalia shati lake la brown iliyofubaa kwa uchafu na jeans ya khaki huku mguuni kava kandmbili zilizoshonwa na kujaa vumbi alikua akipanda ngazi za jingo la Mavuno house kuelekea katika kituo cha redio cha Sweet fm, Eh nikusaidie nini kaka? Ni msichana wa mapokezi alikua akimuuliza Jorome, Samahani namuulizia D Rose, Yule msichana akamuangalia Jorome kwa kumshangaa, Vipi una Miadi nae, Jorome alijibu kwa kujiamini, Hapana mimi ni ndugu yake sasa nimetoka kijijini nimeelekezwa hapa ndo nimekuja muulizia. Mh kaka yangu saa hizi ni ngumu kumuona labda nikupe namba yake ya simu kisha uwasiliane nae, Yule msichana alimjibu Jorome huku akiabinyeza binyeza simu yake, Nitashukuru naomba niandikie alijibu Jorome. Yule msichana akamuandikia Jorome namba na kumpa, Jorome akashuka ngazi kwa kasi breki ya kwanza ni duka la simu, Akanunua simu aina y nokia Tochi akaenda kwa muuzaji wa line akanunua line na kujaza salio la shilingi laki mbili. Kisha akaandika ile namba aliyopewa akaibip ikaita akatabasamu na kukata simu. Samahani bro nataka nimtumie mtu vocha unaweza nielekeza? Jorome alimuuliza Muuza Yule wakala aliyemuuzia line na vocha. Sawa unabonyeza *101* namba kiasi cha vocha kisha alama ya reli. Sawa nashukuru Jorome akaondoka huku akibonyeza bonyeza simu yake, Mara ujumbe ukaingia katika simu yake “ Salio la shilingi 150000.00 ulilotuma kwenda namba 0715470488 limefanikiwa kikamilifu.. Salio la akaunti yako ni……, Jorome akatabasamu mara simu yake ikanza kuita akakata, kisha akaandika ujumbe kwenda ile namba iliyopiga Usijali nitakupigia baadae sasa hivi niko bize kidogo” kisha akabonyeza kitufe cha kutuma simu yake ikaandika neno SEND.



    ..................

    D Rose alikua kaka kwenye mgahawa wa Best bite na Rafiki yake aitwaye Tina, Tina kuna mtu kanitumia vocha ya liki moja nimempigia simu kakata kisha akatuma ujumbe huu. Diana Rose alikua akimwambia Rafiki yake Tina huku akimuonyesha ule ujumbe aliotumiwa na Jorome, Oh huyu atakua ni Papaa anajigonga kwako we mkamue, Tina alimjibu D Rose huku akimuangalia usoni. Rafiki yangu mimi siwezagi hizo mambo, Diana rose alimjibu Tina huku akichukua simu yake toka kwa Tina. Sikia “D” Hawa wanaume si wakuwaonea huruma ni wa kukamua tu we unafikiri ndani ya hili jiji utaishije kama Maji yanauzwa, Daladala za kugombania ni lazima upande Tax au bajaji kama hutaki kubanwa na Lunch ni kama hapa chakula si chini ya Elfu kumi na Tano kwa Mshahara gani wa Sweet Fm tu we zinguka unauza sura hiyo. Tina alimjibu Diana Rose. Duh sasa hao wanaume wewe huwa unawapata wapi? Tina anasimama kisha anajizungusha D rose amuone, Embu nicheki hapa kichwani si mshahara ni jamaa yuko sijui manzese huko ndo kasimamia show ananitumiaga pesa hajawahi hata kuniona na ndo kanitumia hii pesa ya Lunch na pamba ni Mshkaj mmoja nilikutana nae kwenye gari nikiwa natoka arusha akaingia kichwakichwa ndo nampiga kila siku na anapigika tu, D rose anacheka, Sasa huyo jamaa wa manzese ulimjuaje? Eeh si Facebook kashoboka na picha za My Fair anatupa comment tu Sijui You lookin so pretty, Mara I love you, Mara Tunaweza Chati nikajifanya mgumu mwishoni ananifanyia kazi nikimuita baby tu anafunguka. Tina alizidi kufunguka, Mh wewe ni mkali mimi siwezi shost huu mshahara unanitosha mamy D rose alimjibu Tina, Sasa huyo jamaa umempigia sasa? Ah nikipiga namba yake haipatikani, D rose alimjibu. Ok embu hiyo namba? T D rose akamtajia, Sasa niachie hili Game kama ni Michosho nitakujulisha.

    ……………………………………………………………………………………..

    Jorome kaka pembeni yam taro wa maji machafu sururu yake ya kuchimbia mtaro iko pembeni anakula miogo ya kukaanga huku akiangalia barabarani, Anatoa simu yake na kuwasha mara simu inata, Anaangalia kwenye kioo anaona namba mpya anapokea, Halow, Upande wa pili unamjibu, Hi iam Tina naweza jua wewe ni nani kama hutojali? Oh naitwa Jorome, ok mimi naitwa Tina naweza kukuita Jo kama hutojali, Sawa we niite unavyotaka ilimradi moyo wako umeridhika, Ok sawa samahani naweza onana nawe leo jioni pale Samaki samaki? Jorome akamjibu Samahani sitoweza kukuona leo ninasafiri na Rais kwenda Ghana kwenye mkutano wa UN, Oh wewe ni Usalama wa Taifa kwani? Ah hapana ila usijali Tina, Mh poa ningeendelea ongea na wewe ila simu yangu kama imekata redit, Ok poa siku nyingine. Jorome anakata simu halafu anatabasamu anabonyeza bonyeza simu yake huku akitabasamu Mara ujumbe unaingia kwenye simu yake… Salio la shilingi 10000.00 ulilotuma kwenda namba 0656****** limefanikiwa kikamilifu.. Salio la akaunti yako ni 356590.00, Jorome akazima simu yake akachukua kipande cha muhogo akakila na kusimama kisha akachukua Sururu yake na kuendelea kuchimba ule mtaro.

    ………………………………………………………………………

    Saa mbili usiku Tina kakaa Mango Garden Bar mara simu yake inaingia ujumbe kutoka kwa Jorome, “Ikifika saa sita usiku njoo mpaka hapa ikulu ukifika karibu na lango la kuingilia pitiliza kama unashuka Baharini kisha nibip” Tina akajibu ule ujumbe haraka haraka, Sasa Dear kwanini nisiingie tu moja kwa moja huko ndani mimi naogopa kukaa nje?, Akajibiwa Sikia sisi haturuhusiwi kuwa na wanawake sasa nataka nionane na wewe bila mtu kujua. Tina akarudisha jibu, Aah sawa mpenzi wangu nimekuelewa Mwaaah.

    ……………………………………………………………………..

    Diana Rose yupo ndani kwake amekaa kwenye kochi anachezea simu yake mara ujumbe unaingia kutoka kwa Jorome “Hi” D rose anatabasamu halafu anajibu “Hi how are you? Ujumbe unajibiwa niko poa nimependa kukusalimia tu na nakutakia usiku mwema. D rose anajibu “Samahani kwani wewe ni nani? Ujumbe haujibiwi kwa muda mrefu mara ujumbe ukaingis kwenye simu yake akaufungua haraka haraka “Umepokea shilingi 500000 kama muda wa maongezi kutoka kwa 0716 ****** D rose akashusha pumzi na kupiga ile namba akajibiwa Namba unayopiga kwa sasa haipatikani jaribu tena baadae.

    ……………………………………………………………………………………..

    Ndani ya hoteli ya Royal palace kulikua kumetulia muda wa saa tano usiku kauta kaka kijana mtanashati Tony anakunywa soda aina ya Sprite akichanganya na whisk aina ya Magic Moment huku akionekana yuko busy anawasiliana na mtu, Mara ujumbe kutoka kwenye namba yo Jorome unaingia anaufungua na kusoma. We akija hapo hakikisha hicho kidonge unamchanganyia kwenye kinywaji kisha atakuwa mchangamfu na atahitaji kulala na wewe sasa wewe toka nae uje nae mpaka huku Yombo tutakutana usiniangushe, Tony akatabasamu kisha akajibu poa.

    Saa sita na dakika Tano Tina anakaribia Lango la ikulu kisha anashuka na barabara ya kuelekea Baharini huku akibonyeza bonyeza simu yake mara Tax inapaki pembeni yake, Samahani dada wewe ndiye mgeni wa Jorome? Dereva tax alimuuliza, Tina akajibu kwa mbwembwe huku akijishebedua, Yes, Sawa kanituma nije kukuchukua, Tina akaingia kwenye Tax safari ikaishia Royal Palace macho yake yakagongana na kijana Mtanashati Tony Tina kwa mbwembwe akamkumbatia bila kujali macho ya watu akautumbukiza ulimi wake kinywani mwa Tony kisha wakaenda kukaa, Naitwa Jorome, Naitwa Tina huku akitabasamu. Ok karibu kinywaji Tony alimkaribisha Tina, Mmh thanx, akiangalia kaunta ya vinywaji kama anatafuta kitu. A savana Ok naomba Savana Moja ya Moto na Moja ya Baridi na Glass ya kuchanganyia, Tina anamuangalia Tony kwa uchangamfu, Oh Jorome your handsome kweli ikulu kunapendezesha, Tony anatabasamu, Ah kawaida tu. Vinywaji vinaletwa Tina anaanza kunywa huku akitabasamu kila saa, Eeh “Jo” nikuulize swali? We uliza tu, Tony alimjibu. Mmh Sasa huko ikulu hauna Demu kweli. Tony anacheka, Ah haturuhusiwi, Tina anashuka kwenye kiti kisha anaenda kumbusu Tony mmh Mwaah Maana nilikua nishaanza kusikia wivu.. Tony akimkumbatia huku akitumia mkono wa pili kwa mgongoni kuweka ule ungaunga wa kile kidonge katika glass ya kinywaji cha Tina, Tina anamuachia Tony anachukua ile Glass ya kinywaji anaitingisha kisha anamnywesha Tina. Kunywa Mpenzi, Tony anamwambia tina, tina anakunywa huku akifurahi. Dawa aina ya Hearten aliyochanganyiwa Tina ilianza kusambaa katika mishipa ya damu ya Tina, Tina akaanza kuwa na furaha huku akimkumbatia tTony kila dakika na kumporomoshea mabusu huku akimbembeleza wakalale, Macho ya Tina yalikuwa yamelegea na kupoteza uwezo halisi wa kuona Tony akamkokota na kuinia kwenye Gari safari ya kuelekea yombo ikaanza.

    ………………………………………………….



    KONA KALI GUEST HOUSE ni kibao kikubwa cha guest maarufu ya bei ya chini huko Machimbo yombo, Jorome kasimama kaunta akiongea na muhudumu. Kuna vyumba? Ndio vipo unataka short time au unalala? Kwani short time shilingi ngani na kulala shilingi ngapi? Yule muhudumu akajibu huku akimuangalia Jorome machoni, Short time elfu moja miatano na Kulala Elfu mbili miatano.! Poa ninalala, Sawa unalipia hapa kabisa. Jorome anatoa elfu tano kisha anarudishiwa chenchi na kupelekwa kwenye chumba kimoja chenye kitanda futi nne kwa tano kina godoro kuu kuu, Jrome anakaa kwenye kile kitanda huku akiangalia Dari lililojaa utandu wa buibui. Mara ujumbe unaingia, Oyaa nipo hapa nje na Mrembo wako?

    ……………

    Jorome akajibu ujumbe, Ingianae ndani ingieni chumba namba 10 kimeandikwa neno CHACHANDU mlangoni hakikisha unamvua nguo kabisa nitakuongeza pesa. Jorome akatoka nje na kukaa katika benchi lililowekwa mlangoni mwa ile Guest, Tony akampita Jorome pale mlangoni na kuingia ndani moja kwa moja chumba namba 10, Tina kwa sauti ya kimahaba akajilaza kitandani huku akimvuta Tony, Mpenzi natakaa Pipiiiiiii. Tony akaanza kumchezea na kumvua nguo zote kisha akazima Taa Mara mlango ukafunguliwa na Jorome akaingia Tony akatoka na kumuachia Jorome uwanja, Jorome ama Jo kama Tina anavyomuita akamuangalia Tina kwa Tamaa na kuvua nguo haraka haraka, Tina akiwa anajigaragaza pale kitandani huku akiita Jo, Jorome akamfuata pale kitandani na kuanza kuchezea Mifupa ya utamu iliyo katika kiuno cha Tina, Tina akaanza kupiga kelele za mahaba, Jorome akahama taratibu na kuanza kuhesabu pingili za uti wa mgongo huku akitumia ulimi wake kupapasa pembezoni mwa masikio ya Tina, Tina kelele zikazidi huku akiolalamika anakufa hapo ndipo Jorome alipotumia meno yake ya mbele kufinya shingo ya Tina, tina aliruka na kumkumbatia Jorome kisha akashika pipi ya Jorome iliyokuwa tayari kwa kuliwa na kuiingiza kinywani akaanza kuimumunya huku akipapasa kifua cha Jorome. Ndani ya nusu saa tayari Tina alikuwa akifurahia utamu wa kiumbe ambacho hajaruhusu dawa ya Hearten haijaruhusu mboni za macho yake kutambua kilichoko mbele yake, Tina alikuwa akilia huku akimbembeleza Jorome amuoe. Kila baada ya nusu saa baada ya round kuisha Tina alikua akimuomba Jorome ampe tena Pipi afaidi utamu wake.

    ……………………………………………………………………….

    Ni saa nne asubuhi Tina anashtuka yupo kitandani katika eneo asilolifahamu kuangalia pembeni haoni mtu, Anaamka na kuvaa nguo haraka haraka pembeni ya mto anaona noti ya elfu kumi na ujumbe umeandikwa “Nimesafiri Naelekea Taiwan kwa muda wa miezi Tisa nitakumiss mpenzi, Mimi Jo” Tina akaamka kwa nyodo akaenda mpaka pale mapokezi, Samahani naomba maji ya kuoga, Tina alimwambia Yule kijana wa mapokezi, Pole dada hapa ni kulala tu kuoga kwenu, Tina akasonya na kutoka nje kwa hasira.

    ………………………………………………….

    Baada ya kifo cha Moudlove na kumegwa na muhudumu wa hoteli ya Blue palace kwa ajili ya kutunza siri Trina aliamua kuishi peke yake bila mwanaume, Tabia yake ya kujiridhisha mwenyewe kwa kutumia kiungo bandia cha kiume na kazi ya ukarani katika benki ya Swiss cash ndicho kilichomfanya kuwadharau wanaume.

    Postaa posta gari Postaaaa, Ni sauti ya Jorome katika kituo cha daladala Mwenge, Trina kava sketi fupi na bauzi ya pinki mkononi kabeba mkoba wa pink mkubwa anasogelea daladala, Oyaaa dada toa giza hapo kama unaingia ingia hatununui sura hapooo, Jorome alikua akimwambia Trina aliyekuwa kasimama mlangoni mwa daladala, Trina anamuangalia Jorome kwa dharau, We kinyago na mdomo wako mchafu usinizoee, Trina alimjibu Jorome kwa hasira kisha akapanda ile daladala na kukaa kiti kilicho karibu na mlango. Mara simu ya Trina inaita anaipeleka sikioni, Hallow? Aah Neema? Za siku nyingi Shoga angu ni siku nyingi tokea shule, ndio…. Mimi naelekea kazini, Eeh aah wapi kuna mwanaume mwenye uwezo wa kunioa mimi, Ndio nafanya kazi Bank ya Swiss Cash iko posta… Karibu mwaya., Trina anakata simu na kuiweka kwenye pochi. Jorome amnamuangalia Trina na kujisemea Moyoni, Lazima nimle huyu kuku wa supermarket.

    …………………………………………………….

    Inasikika sauti ya Adhana kuashiria ni saa kumi na moja Asubuhi waumini wa dini ya kiislam wanatakiwa wakaabudu, Nje ya mlango wa chumba kimoja kati ya vyumba sita vya nyumba inayotazama barabara ndogo ya waenda kwa miguu kasimama mzee wa makamo anagonga mlango kwa Fujo, Mlango unafunguliwa anatoka Msichana akiwa kajifunga kanga akionekana katoka usingizini, Huyu si mwingine ni Saida kicheche Msichana aliyeanza kufanya ngono tokea akiwa shule ya msingi mpaka ikapelekea wazazi wake kumfukuza na kuamua kupanga chumba Machimbo yombo huku akitegemea pesa kutoka katika baa maarufu iitwayo Kimboka iliyoko Buguruni yeye akiwa kama mfanya biashara wa chakula cha watu wazima nyakati za usiku. Shikamoo mzee, Yule mzee anamuangalia Saida kwa hasira, Mimi sijaja hapa kusalimiwa nataka kodi yangu huu ni mwezi wa tatu unanikimbia tu sijui unaingia saa ngapi wala unatoka saa ngapi? Aah mzeewangu nivumiliee biashara ngumu? Yule mzee akaanza kugomba kwa sauti kubwa.

    Jorome anatoka ndani kwake anafunga mlango anasikia sauti kubwa kutoka nyumba ya jirani anasogea na kumkuta Yule mzee anafunga chumba cha saida kwa kufuli huku saida akiwa kapiga magoti anaomba apewe muda zaidi, Jorome akasogea mpaka pale na kumgusa Yule mzee bega mzee akageuka, Samahani kwani unamdai pesa ngapi? Saida akamuangalia Jorome kwa dharau, We gari la taka haya hayakuhusu wewe mwenyewe muogo wa kukaanga potea, Saida alimjibu Jorome kwa hasira. Jorome kwa tabasamu akarudia kumuuliza yu le mzee. Ni shilingi ngapi? Mzee akajibu Laki tatu na nusu mpaka sasa, Jorome akarudi chumbani kwake na kutoa pesa katika kile kiroba anachotumia kama Godoro anarudi mpaka pale kwa Saida na kumkabidhi Yule mzee zile pesa kisha jorome anamuacha saida akimshangaa.

    ………………………………………………………………..

    Mkononi kashika Mfuko mkubwa wa plastic mweusi, Shati jipya la mtumba jeusi lililojikunja na suruali ya bluu ambayo haijapasiwa yupo katika foleni ya kumuona karani wa Benki ya Swiss Cash inafika zamu yake macho yake yanagongana na Trina, Trina anajifanya hajamuona anainama kama anachezea simu, Dada nahitaji huduma? Jorome alimwambia Trina. Trina akajifanya hajamsikia akawa busy anahepanga pesa kwenye shelfu, Dada naongea na wewe? Trina kwa dharau, We kinyago dirisha hili si la fomu ya mikopo nenda dirisha la Tatu tafadhali. Jorome kwa hasira na sauti ya juu, We pumbavu ninii mimi nije kukopa nina shida gani eeh? Namtaka meneja wako sasa hivi, Mara mlango wa pili unafunguliwa anatoka mzee wa Makamo na kumuangalia Jorome kwa mshangao halafu anauliza kwa upole. Samahani kuna shida gani? Jorome kwa jazba, si huyu msichana wenu hapa hana lugha ya nidhamu mimi ni mteja mpya nina Milioni mia nne hapa nataka kuweka kwenye benki yenu anadhani mimi ni ombaomba? Jorome anazimwaga zile pesa pale chini, Trina anatoa macho huku akitetemeka kwa woga? MEneja anamshika mkono Jorome huku akimuomba radhi anamsaidia kuweka pesa katika mfuko na kumuomba waingie katika kile chumba akamuhudumie Jorome anaingia baada ya muda anatoka akiwa kaongozana na Meneja, Jorome anaondoka Meneja anamuangalia Trina kwa Hasira, Njoo ofisini kwangu. Trina anaingia ofisini kwa Meneja huku akitetemeka, Trina umevunja maadili ya kazi ulitaka kutufukuzia mteja mkubwa sana sasa ili uendelee kufanya kazi hapa inakulazimu umtafute Yule mteja ukamuombe radhi akupe barua ya kututhibitishia kuwa amekusamehe ndio utafanya kazi hapa bila hivyo hatuwezi fanya kazi na wewe. Meneja alimwambia Trina kwa hasira.

    …………………………………………………………………….

    Katika chumba namba 509 ndani ya hotel ya Blue palace Trina amelala kitandani yuko uchi, Mara mlango wa bafuni unafunguliwa anatoka Jorome kava taulo, Binti mimi nataka kuondoka nimeshakusamehe barua yako nitaipitisha pale Bank, Trina anamuangalia Jorome kwa jicho la huba huku akilia, Jo naomba unipe tena penzi lako kabla haujaondoka? Jorome akamuangalia Trina pale kitandani akijinyonga nyonga. Lakini si ulikuwa hutaki wewe? Oh hakuna Mwanamke anayeweza kutosheka na utamu wako Jorome mungu kakupendelea. Trina aliongea huku akisimama na kulivuta Taulo alilovaa Jorome likadondoka Mwanaume wa Jorome akaamka kuandaa silaha ili kukabiliana na adui yeyote mbele yake, Trina akaiwahi kuishika huku akiipeleka katika maeneo yake ya starehe, Jorome akamshika kiuno na kumsukuma kitandani kilichofuata hapo si ruhusa kwa watoto chini ya umri wa miaka 18 kusoma hapa soma mwenyewe ni XXXXXXXXXXXX.

    …………………………………………………………………..

    Kuchelewa kwa mshahara kazini kwa D rose ndiko kulichomfanya D rose kuwa na mawazo, Bili ya maji na umeme katika nyumba anayoishi ndicho kitu kilichomchanganya, Akili yake ikakumbuka namba ya Jorome akachukua simu yake na kutafuta ile namba aliyokuwa kaisevu kwa jina la VOCHA akapiga ile namba simu ikaita kisha ikakatwa, Wakati anajaribu kupiga tena ghafla simu yake ikaita kutazama kwenye kioo ni jina VOCHA akapokea haraka haraka, Hallow? Upande wa pili ukajibu, Ndio nakusikiliza? Samahani kaka yangu ninashida sana naweza kukuona? D rose akaongea harakaharaka, Hapana nipo mbali na Dar ila una shida Gani? Nani mimi..! Aah nilikuwa nina shida na shilingi laki moja tu halafu nitakurudishia? Ok sikia baada ya Saa moja nenda pale Dar Centre club kuna mtu atakuletea pale sawa, D Rose kwa furaha akajibu, Nashukuru. Simu ikakatwa akaikumbatia simu yake kifuani huku akifumba macho.

    ………………………………………..

    Haya sasa Diana Rose au D rose shida zinamuingiza katika Mikono ya Sura mbaya, Gari la Taka Jorome je Atatoka Salama? Na je Saida Kicheche atafanya nini baada ya kusiadiwa na Jorome?



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog