Search This Blog

Sunday 19 June 2022

MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI - 1

 







    IMEANDIKWA NA : AMANI KIZUGUTO



    *********************************************************************************

    Simulizi : Mwanamke Mwenye Kovu Jeusi

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    Nakumbuka vizuri ilikuwa siku ya jumapili ambayo kama ilivyoada kwangu huwa sikosi kwenda

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kanisani hasa misa ya kwanza kwani huwa napenda sana kusali misa ya kwanza ili baadaye niweze



    kuendelea na mambo yangu mengine,siku hiyo niliamka asubuhi na mapema kutoka pale nyumbani



    kwangu mnazi mmoja karibia na ofisi za chama cha mapinduzi za mkoa wa Dar-es-salaam na



    kuelekea kanisani pale saint.alban posta taratibu kwa miguu kwani gari yangu ilikuwa imeharibika



    wiki ya pili sasa na isitoshe pale nyumbani kwangu mpaka pale posta hapakuwa mbali sana kiasi cha



    kama dakika 20 tu hasa kwa kijana kama mimi ambaye damu ilikuwa bado inachemka.niliingia pale



    kanisani nikiwa sijachelewa sana misa ilikuwa imeanza kama dakika 7 hivi nakumbuka sana somo la



    siku hiyo alilolitoa padri Kiaka lilikuwa linahusu umuhimu wa kuombea siku yako ya kufa kwani



    haina siku wala saa.





    Misa ilipoisha mida ya saa 3 asubuhi niliona nijivute mpaka mitaa ya upanga pale nyuma ya diamond



    jubilee mwendo wa pole pole nikamuone  rafiki yangu Martin ambaye pia alikuwa ni mfanyakazi



    mwenzangu. Sikutaka hata kumtaarifu kwenye simu kwani simu yangu haikuwa na pesa pia nilijua



    kwa kuwa tuliahidiana jana kwamba kesho nikitoka kanisani nitaenda kwake basi haina shaka



    nitamkuta tu kwani pia Martin huwa sio mzururaji sana hasa mida ya asubuhi kama haendi



    kazini.Wakati naingia ndani kwa rafiki yangu kipenzi  Martin nakumbuka ilikuwa ni mida ya saa 4



    asubuhi mlangoni nilipishana na mdada wa makamo mweusi kiasi ambaye nakumbuka vizuri alikuwa



    amevalia dela la rangi ya kijani kibichi likiwa linamichirizi ya rangi ya zambarau na kwa ndani



    alikuwa amevaa suruali ya jeans ya rangi  nyeusi huku kichwani akiwa amejifunga mtandio mweusi



    kufunika nywele zake nilimsalimia aliitikia haraka haraka huku akikwepesha sura yake na huku



    akionyesha ni mtu aliyekuwa na shauku ya kuondoka lile eneo haraka sana, mimi hata sikumjali



    nilijua atakuwa ni mmoja kati ya wasichana ambao alikuwa na uhusiano nao bwana Martin kwa



    kuwa rafiki yangu Martin alikuwa ni mtu aliyependa sana wasichana,nilifika mpaka pale alipokuwa



    amepanga Martin ilikuwa ni nyumba ya uwani akiwa amepanga chumba na sebule huku nyumba ya



    mbele kukiwa hakuna mtu hata mmoja aliyekuwa amepanga kwa maelezo yake ile nyumba ya mbele



    kulikuwa na mpangaji lakini amehama na sasa mwenye nyumba alikuwa yupo akiifanyia



    marekebisho tayari kwa kuingia mpangaji mwingine. Ile nimefika tu mlangoni nikakuta mlango upo



    wazi kitu ambacho kikawaida sio busara kuingia nyumba ya mtu bila kugonga basi nikajivuta pale



    mlangoni na kuanza kuugonga ule mlango hallow Martin hallow  niligonga kama dakika tano bila



    kupata jibu lolote kutoka mule ndani ilinibidi nishangae kidogo kwa maana hata kama angekuwa



    msalani ni lazima angesikia ile sauti yangu na kwa nini akae kimya sikuamini kama alikuwa amelala



    wakati nimepishana na Yule dada anatoka chumbani kwake muda si mrefu,ikanibidi niingie tu ndani



    kama hayupo atanikuta mule mule nikimsubili, mungu wangu sikuamini nilipoingia pale sebuleni



    kwake nilikutana na michirizi ya damu kutoka pale sebuleni kuelekea chumbani kwake mh ikanibidi



    nipitilize haraka moja kwa moja kule chumbani kwake ile kuingia tu nikakutana na mwili wa Martin



    akinikodelea macho huku ukiwa umekakamaa huku pia ukiwa  umegandana na damu na alama



    kubwa ya kisu kwenye shingo yake,nilimkimbila pale alipokuwa amelazwa na kumuangalia mungu



    wangu alikuwa tayari ameshakufa,nilifikiria pale haraka haraka ni kipi nifanye nikaanza kuitafuta



    simu yake mule ndani mpaka nikaipata nikawapigia simu polisi na kuwaeleza lile tukio sikutaka



    nijihusishe moja kwa moja na lile tukio ndio maana niliamua kutumia simu yake pia simu yangu



    nilikuwa bado sijaweka vocha kisha nikaanza kutoka nje kabla sijatoka nje ya chumba chake macho



    yangu yakatua kwenye meza ndogo iliyokuwa mule chumbani kwake mara nikakutana na karatasi



    imeandikwa kwa Wino Mwekundu

    “NILIYEMUUWA NI MIMI MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI” shiti moyo ulijikuta



    unasisimuka na kuanza kudunda dunda kwani lile jina si mara ya kwanza kwangu kukutana nalo hasa



    kwenye kazi zangu,mungu wangu huyu mwanamke amemuuwa tena na Martin? Martini



    amemfanyaje tena huyu mwanamke hatari kama amemuuwa na Martin basi na mimi siku zangu



    haziko mbali hapana inabidi nimzibiti kwa kila hali nilijikuta nimekaa naangalia ile karatasi



    aliyoandika huku nikiutazama na mwili wake pale chini kwa muda wa dakika kadhaa mpaka machozi



    yakaanza kunitiririka kwa mbali,nilishitushwa na kelele zilizotoka nje nikahisi polisi watakuwa tayari



    wameshafika pale basi nikaona haina haja ya kuondoka tena nikachukuwa  shuka pale na kuanza



    kuufunika ule mwili hallow inspector vipi tayari umeshafika? Habari umeipataje? Ilikuwa ni sauti ya



    bwana Gerald mmoja wa ma afisa upelelezi pale makao makuu, ndio mimi niliyewapigia simu



    nilimjibu kwa mkato huku nikimsaidia kutoa vifaa vya kuchukulia finger print pamoja na camera



    digital ya kipelelezi kupiga picha mule chumbani kwa ajili ya kupata nyayo zake na alama zingine za



    Yule muuwaji,mkuu wangu wa kazi pia inspector Thomas na yeye pia alikuwa ni mmoja ya watu



    waliokuwa wamefika pale kwa ajili ya kushuhudia lile tukio wakati kina inspector Gerald



    wakiendelea kukusanya baadhi ya kumbukumbu mule ndani bosi wangu aliniita nje alipiga simu



    hospitali ya taifa ya muhimbili kuwajulisha kuhusu lile tukio kisha akaanza kuniuliza maswali kadhaa



    kuhusu lile tukio aliniuliza kwanza nilijuaje kama Martin amekutwa na lile tukio nikamjibu mimi



    mwenyewe imetokea tu kama bahati kwani tulikuwa tumepanga kukutana naye siku ya leo nikitoka



    kanisani ili tuelekee bagamoyo kusherekea siku ya mchumba wake ya kuzaliwa,ndio na mbona hili



    tukio tumejulishwa kupitia simu yake aliendelea kunihoji, ni mimi ndiyo nilitumia simu yake



    kuwajulisha kwani simu yangu haina pesa kabisa, je huyo muuwaji unamjua au unaweza kuwa



    unamhisi nani? Ni MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI bosi wangu alijikuta anashituka ohh



    wewe umejuaje? Aliniuliza kwa shauku kubwa ya kutaka kujua nimefahamu vipi aliyefanya lile tukio



    ni mwanamke mwenye kovu jeusi nikamwambia kuwa kama kawaida yake ameacha note juu ya



    meza mule chumbani mwa Martin ameandika kwa wino mwekundu, basi bosi wangu alinituma



    nikamletee ile karatasi aliyoiacha huyo mwanamke mwenye kovu jeusi,basi nilienda na kutoka nayo



    pale nje na kumpa aiangalie, aliiangalia kwa muda wa kama dakika 2 hivi halafu akaludisha macho



    kwangu na mimi muda ule nilikuwa pia nimemetolea macho basi tukajikuta tumetoleana wote



    macho,hivi hakuna anayemjua huyu muuwaji? Kwa maana sasahivi amezidisha haya mauaji



    alianzisha tena mazungumzo,

    simjui ila uwezo wa kumpata upo kwa nini asipatikane kwa maana tukimchekea tutajikuta na sisi

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    wote anatuondoa wakati nazunguma haya tayari gari ya kubebea wagonjwa kutoka muhimbili



    hospitali ilikuwa tayari imeshafika pale nyumbani kwa marehemu Martin tayari kwa kuchukua ule



    mwili kuupeleka hospitali ili ufanyiwe pia uchunguzi mwingine wa kitabibu .Wale manesi walishuka



    kutoka ndani ya ya ile gari ya kubebea wagonjwa na kuingia mule ndani tayari kwa kuuchukuwa ule



    mwili kwa ajili ya kuupeleka hospitali.

                                 *************************************

    Baada ya mwili kuondolewa pale nyumba ambayo  Martin alikuwa amepanga kwenda hosptali kwa



    ajili ya uchunguzi zaidi bosi wetu inspekta Thomas alituita wafanyakazi wote pamoja na askari kanzu



    ambao tulikuwa pale kwenye lile tukio,ndio nimewaita hapa tuzungumze kidogo nazani mmeona



    tukio lililotokea leo,hii hi fedheha sana kwa jeshi la polisi, huyu mwanamke haiwezekani tumshindwe



    kiasi hiki mwanzo alikuwa anawauwa watu wengine lakini sasahivi ameingia mpaka kwenye jeshi



    letu lapolisi, hapa maswali ya kujiuliza haraka haraka ni kwamba huyu mwanamke amejuaje kama



    Martin ndio alikuwa anajukumu la kufuatilia hili faili lake? Inamaana kuna watu ndani ya ofisi yetu



    watakuwa wanampa siri huyu mwanamke bosi alianza kuzungumza huku akionyesha kwenye sura



    yake wazi kwamba kile kitendo kilikuwa kimemuumiza sana.

    Basi taratibu mkuu haya tutaenda kuyazungumza ofisini mkuu maana hapa tulipo hatuwezi kujua



    inawezekana akawa bado yupo au ameweka hata vinasa sauti maana inaonekana huyu mtu ni hatari



    sana ,ilikuwa ni sauti ya Jamira mmoja wa askari shupavu sana tuliokuwa nao pale kituo cha kati



    kwenye jeshi letu la polisi, ilionekana bosi aliafiki ule ushauri aliopewa na Jamira kwani baada ya



    hapo alituambia ya kwamba tunaweza kwenda huku akimwabia Gerald ahakikishe baadaye



    wanakutana ofisini kwake.

                                         *******************************

    Habari ya kifo cha kutatanisha cha Martin kila mmoja pale ofisini kilimhudhunisha sana kwani



    Martin alikuwa mmoja ya vijana wachapakazi sana pale ofisini hadi siku umauti yanamkuta



    nakumbuka yeye ndio alikuwa mtu anayefuatilia faili la huyu mtu aliyekuwa akijiita MWANAMKE



    MWENYE KOVU JEUSI sasa tena na yeye kuuliwa na mtu aliyejitambulisha kwa jina hilo kila mtu



    alishituka sana.

    Basi baada ya uchunguzi wa kitabibu hospitali ya taifa Muhimbili kukamilika ilibidi zianze taratibu za



    kusafirisha mwili wa marehemu. Tuliusafirisha mwili wake mpaka wilayani Bunda ambapo ndipo



    palikuwa nyumbani kwa wazazi wake. Na mimi ni mmoja ya watu tuliochaguliwa na bosi wangu



    kusindikiza maiti ya marehemu nadhani hili lilitokana na ukaribu wangu baina ya mimi na Martin.



    mazishi yake yalifanyika huko kwao kwenye kijiji kilichojulikana kwa jina la Kasunguti,kwa mimi



    ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kufika mkoa wa Mara toka nizaliwe mara nyingi safari zangu



    nyingi nilikuwa naishia mkoa wa Mwanza tu. Nakumbuka siku ile tulipoingia nyumbani kwa wazazi



    wake tulikuta umati wa watu wengi sana, wazazi wake walikuwa hawaamini kama mtoto wao



    amefariki mpaka pale walipoliona jeneza likishuka kutoka kwenye gari iliyokuwa imebeba ile maiti



    ya Martin. Mama yake alikuwa akilia huku akilalamika ya kwamba Martini ndio alikuwa mtoto



    tegemewa kwani alikuwa anawasomesha wadogo zake watatu sasa sijui watafanyaje. Sikuamini siku



    ile kama ilikuwa ndio siku ya mwisho kuuona mwili wa rafiki yangu kipenzi Martin.

                                   ******************************

    Ilikuwa imepita wiki moja baada ya kurudi kutoka Bunda kumzika Maritin nakumbuka siku hiyo



    nilikuwa nipo ofisini nikijaribu kupitia faili moja lililokuwa linamhusu jambazi mmoja ambaye mpaka



    siku ile ilikuwa bado sijamjua ni nani ila nilikuwa nimeshafanikiwa kupata baadhi ya nyaraka



    muhimu kuhusu huyo mtuhumiwa mara ofisini kwangu akaingia Gerald, tuliongea mambo mbalimbali



    kisha akaniambia ya kwamba lile faili la mwanamke mwenye kovu jeusi alikuwa amekabidhiwa yeye 



    na ameambiwa ndani ya wiki tatu ahakikishe tayari mtuhumiwa ameshajulikana na kukamatwa,



    nilimwambia ajitahidi na awe makini sana kwani huyo mtu anaonekana hatari sana,akasema hakuna



    shida kwani yeye kama iliyo ada siku zote huwa yupo makini. Alijaribu kuniomba ushauri pakuanzia



    kumfuatilia Yule mtuhumiwa nilimshauri aanzie kwanza kupitia lile faili alilokabiziwa ili ajue ni wapi



    Martin aliishia nadhani mpaka hapo atakuwa na nafasi nzuri ya kujua wapi pa kuanzia, tulizungmza



    nae sana mambo yetu mengine nakumbuka sana siku hiyo mpaka muda wa kutoka kazini saa 9



    arasili.

                            *******************************************

    Basi kama iliyo ada ya majukumu ya kikazi Gerald alianza kuifuatilia ile kesi ya Mwanamke mwenye



    kovu jeusi maana aliambiwa ndani ya wiki tatu awe tayari ameshajua kila kitu kuhusu huyo muuaji



    wa kutisha ikiwezekana pia awe tayari ameshatia ndani ya mikono ya sheria, alianza kwanza kwenda



    kufanya mahojiano na mwanadada mmoja  ambaye alikuta jina na mahali alipokuwa anaishi pamoja



    na sehemu aliyokuwa akifanyia kazi kwenye faili aliloliacha marehemu Martin huyo dada alikuwa



    anafanya kazi benki ya taifa ya biashara makao makuu pale alijulikana kwa jina la Zainabu Athuman



    akiwa mmoja wa maafisa mikopo pale makao makuu. Basi siku hiyo asubuhi na mapema Gerald



    alidamkia pale benki kwani alihofia kwamba akichelewa Yule dada anaweza asimkute kwani mara



    nyingi huwa anazunguka sehemu mbalimbali hasa kwenye maofisi kutoa elimu kuhusu mambo ya



    mikopo. Ofisi ilipofunguliwa tu  Gerald alikuwa mmoja wa watu wa kwanza kuingia mule ndani ya



    jingo la benki moja kwa moja mpaka mpaka mapokezi,”samahani naweza kuonana na Zainabu



    Athuman?” ilikuwa ni sauti ya Gerald akimuuliza mmoja wa wahudumu pale meza ya



    mapokezi,samahani  una ahadi naye? Mdada mmoja wa pale mapokezi alimuuliza, hapana sina ahadi



    naye ila ninashida naye. Ya kiofisi au ya binafsi? Ya kiofisi, ilibidi Gerald adanganye kidogo ili apate



    nafasi tu ya kuonana naye,kuepuka usumbufu ambao huwa hauna maana uliojaa katika ofisi nyingi

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    hapa Tanzani ok sawa nenda gorofa ya kwanza mkono wa  kulia utakuta ofisi imeandikwa ofisi ya



    afisa mikopo ndio hapo hapo,Gerald alishukuru na kupanda ngazi kuelekea kuonana na Zainabu.



     alipofika pale mlangoni, alikuta mlango ukiwa wazi na kwa ndani alimuona Zainabu akipanga mafaili



    yake vizuri juu ya meza mule ofisini, Gerald akamuuliza,samahani naweza kuingia? Ndio hakuna



    shida wewe pita Zainabu alimjibu Gerald huku akikaa kwenye kiti chake na kuanza kukizungusha



    pale kwenye kiti kushoto kulia, Gerald aliingia na kukaa kwenye kiti cha wageni kisha na kumtazama



    Zainabu hivi kama dakika 2 mpaka Zainabu akamshitua kaka vipi nakusikiliza wewe maana nataka



    kuondoka hapa, alimwambia Gerald huku akimshusha chini juu chini juu,

    Basi Gerald alianza kujitambulisha, kisha akatoa na kitambulisho chake halafu akamueleza nia ya



    yeye kuwa pale ofisini muda ule,Zainabu alionekana kuishiwa nguvu kisha akaanza kumwelezea



    Gerald ya kwamba mbona tayari alishakuja mwenzako na nilimueleza kila kitu lakini? Ndio hilo



    nalijua lakini mimi imekuja ili kupata uhakika zaidi kuhusu hili jambo,Gerald alizungumza kwa



    umakini huku akimkazia macho kuongeza msisitizo, hivyo basi na maswali kidogo naomba nikuulize



    ili nipate majibu ya kuridhisha kutoka kwako. Unamfahamu vipi huyu mwanamke anayejiita eti



    anakovu jeusi? Kiukweli simfahamu huyu mwanamke ila nachojua ni kwamba alikuwa na uhusiano



    na mdogo wangu mpendwa Rashid,hapo hapo Gerald alimkatisha, huyo Rashid yupo wapi?



    Alishafariki, maskini Zainabu aliendelea kuongea huku akionekana kama ni mtu aliyekumbuka mbali



    sana. Unaweza ukaendelea, Gerald alimwambia, ndio huyu mdada simfahamu vizuri ila naweza



    kusema kuwa alikuwa na uhusiano na mdogo wangu ambaye baadaye alikuja kufa kifo cha



    kutatanisha kule bahari beach,mimi huyu mwanamke nimewahi kumuona mara mbili na hata hapa



    pia nikimuona namkumbuka ilaaah ilaah ilaah alianza kusita kuendelea kuongea Zainabu, ila nini?



    Wewe usiogope sema yote sawa maana hapo utakuwa umelisaidia sana jeshi la polisi.unajua Napata



    tabu sana kwani huyu mwanamke ni wa ajabu sana kwanza aliacha ujumbe wa karatasi kwenye



    mfuko wa marehemu mdogo wangu Rashidi pia na hata hapa ofisini wiki mbili baada ya kifo cha



    mdogo wangu alikuja na kusema ya kwamba nikithubutu kumtaja jina lake basi kabla yeye



    hajakamtwa mimi nitakuwa sipo duniani na pia kwa yoyote nitakayemtajia jina lake akijua pia lazima



    atamuondoa duniani, ndio maana nakuwa na  hofu ya kumzungumzia kwani pia mdogo wangu



    Maimuna alikaidi huo ujumbe hapa napozungumza wiki ya pili sasa tumetoka kwenye msiba wake



    hivyo mimi siwezi kuzungumza zaidi ya hapo samahani sana alimalizia Zainabu huku machozi



    yakimtiririka ..

    Gerald alibakia asijue la kufanya kwani wakati anaendelea kumbembeleza Zainabu amwambie



    kuhusu Yule mwanamke aliyejiita mwenye kovu jeusi alisikia mlango wa ofisi ya Zainabu ukigongwa



    kuashiria kuna mtu alikuwa anahitaji kuingia.

    Basi pale pale Gerald alimuaga na kuondoka huku akimuahidi ya kwamba ataludi tena siku



    nyingine,Zainabu hakumjibu kitu zaidi ya kujifuta machozi na kujiandaa kuzungumza na Yule mgeni



    aliyekuwa pale mlangoni. Gerald alitoka mule kwa kasi ya ajabu huku yule mtu aliyekuwa anahitaji



    kuingia mule ofisini akimshangaa mpaka nje kisha akaelekea kwenye sehemu ya maegesho ya magari



    tayari kwa ajili ya kuchukua gari lake kuondoka basi Gerald akufungua gari lake na kuingia wakati



    anataka kukaa kwenye siti akahisi kama amekalia kitu kigumu kilicho chini ya kava la siti ya kiti cha



    gari ikabidi ainuke ili aangalie ni kitu gani hicho kwani gari ni ya kwake na ndio aliyokuja nayo pale



    basi ikambidi ainue lile kava la siti ya gari alikuta kuna bahasha ya kazi ikabidi ashangae ni nani



    aliyeiweka pale akaichukua na kuiangalia kujua inahusu nini, kuifungua akakuta kuna barua



    imeandikwa kwenye karatasi ngumu yenye rangi nyekundu maandishi yakiwa ya rangi nyeusi,



    maandishi yenyewe yalikuwa yanasema ifuatavyo

    Ndugu Gerald najua ni wewe ndio uliyepewa jukumu la kunifuatilia mimi ila nakuomba utambue ya



    kwamba mimi ni mtu hatari na hilo utaamini ukifika nyumbani kwako ni mimi “MWANAMKE



    MWENYE KOVU JEUSI”

    Gerald aliisoma ile karatasi zaidi ya mara 5 huku akiangalia kila upande kuona kama atamuona Yule



    mwanamke  hakufanikiwa alizidi kuchanganyikiwa pale huku akijiuliza huyu mwanamke amejuaje



    kama mimi leo asubuhi nitakuwepo hapa? Nani amemwambia wakati hakuna hata mtu mmoja



    aliyemwambia kuwa leo ataenda pale, pili Yule mwanamke aliweza vipi kupitisha ile bahasha mpaka



    pale chini ya lile kava la siti ya gari lake,wakati alifunga na ufunguo,alijikuta akishangaa mpaka akaja



    kushituliwa na mlinzi wa lile eneo la kuegeshea magari, “kaka samahani mbona gari umeliweka



    vibaya wengine wanashindwa kuegesha magari yao”.ilikuwa ni sauti ya Yule dada aliyekuwa



    anakusanya ushuru wa kuegesha magari,ilimbidi  Gerald aombe radhi kisha akaondoa gari lake



    kuelekea ofisi kwake aliendesha gari huku kichwani akiwa na mawazo, amakweli huyu mwanamke ni



    hatari kwa staili hii inanibidi niongeze umakini.

                                    ******************************

    Wakati Gerald yupo ofisini akiendela na kazi mara akipigiwa simu na jirani yake ya kwamba



    anahitajika mapema sana yumbani kwake kwani kunatatizo ilemetokea,kusikia hivyo Gerald



    alichanganyikiwa kwani alihisi Yule mwanamke mwenye kovu jeusi atakuwa ameshafika kwake na



    kufanya jambo lisilo jema,

    Naomba unisindikize kwangu samahani sana,Gerald alimuomba Siwah amsindikize nyumbani kwake,



    Siwah alishangaa sana kwani kwa muda ule iliwapasa kuwa kazini, samahani bwana nisindikize kuna



    dharura nimepigiwa simu hivyo sina budi kuwahi nyumbani alizidi kusisitiza huku akichukua simu



    yake na kujaribu kumpigia mpenzi wake Furaha ambaye walikuwa wakiishi wote japo walikuwa



    hawajafunga ndoa, alipiga simu zaidi ya mara tatu iliita bila kupokelewa,Gerald alijihisi

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kuchanganyikiwa, Siwah tafadhari twende nyumbani kwangu nahisi si salama, aliomshika mkono



    Siwah na kumvuta nje waelekee kwenye gari tayari kwa ajili ya safari ya kuelekea kwake. Wakati



    wapo ndani ya gari wakielekea nyumbani kwa Gerald ndipo alipoanza kumuelzea kisa kizima



    alichokutana nacho siku ile asubuhi toka alipoenda kazini kwa dada Zainabu maongezi yao yote



    yalivyokuwa na mwisho alimueleza jinsi ile bahasha aliyoikuta china ya siti ya gari lake.Siwah



    alishangaa sana kusikia yale maneno “sikia ndugu yangu huyu mwanamke ni hatari sana hata Martini



    alikuwa analeta masihara nayeye umeona yaliyomkuta?” inabidi umakini uongezeke mara dufu



    katika kufuatilia hili swala kwani bosi amekupa siku ngapi? Alimalizia Siwah kwa kumuuliza Gerald



    huku wakiwa wamekaribia kabisa nyumbani kwake. Amenipa wiki tatu na sasa ni siku ya 4 hata



    sijapata pa kuanzia wewe acha tu kama ni kazi basi hii imetia fola.

    Walifika nyumbani kwa Gerald na kukuta watu wakiwa wamejaa sana ukizingatia ile nyumba



    walikuwa wamepanga watu kawa  wa 5 hivi, majirani pia wa nyumba za jirani pia walikuwa



    wamekusanyika pale uwani kwenye ile nyumba. Waliposhuka kwenye gari wale watu walimtazama



    kwa sura ya hudhuni sana Gerald kisha jirani yake mmoja akamuambia afadhali umekuja jirani hali



    ya hapa nyumbani ni mbaya sana,Gerald aliona wanachokiongea hata hakieleweki moja kwa moja



    akaelekea upande wa pili ambapo ndipo alipokuwa amepanga yeye, “sasa unaenda wapi bwana



    mbona unakuwa kama sio mwelewa hebu subili kwanza hapa tuwasikilize tujue tatizo nini” ilikuwa



    sauti ya Siwah huku akimshika shati Gerald asiondoke. Ilimbidi ahairishe kuondoka pale  kwa



    kufuata ushauri wa rafiki yake na kusimama kuwasikiliza  kujua tatizo ni nini, samahani sana jirani



    hapa nyumbani hali sio nzuri mida ya saa 5 hivi alikuja mdada mmoja akiwa amejifunika vitenge



    akiwa na gari aina ya Toyota surf, alipofika hapo getini alipiga honi sana akatoka shemeji kwenda



    kufungua ile kufika tu na kufungua lile geti, mbona wajiuma uma wewe nambie sema usiogope kama



    wamemuuwa au vipi Gerald alidakia haraka haraka akongea kwa sauti iliyojaaa wasiwasi na shauku



    ya kutaka kujua ni nini kimetokea, hapana siwezi kusema moja kwa moja wamemuuwa ila baada ya



    kufungua tu geti Yule dada alishuka akiwa ameshikilia bunduki na kumuelekezea walekee ndani



    kwako ndipo pale tulipokupigia simu, inamaana bado wapo ndani? Alidakiwa Siwah kumuuliza swali



    Yule jirani aliyekuwa akihadithia pale, hapana waliingia ndani baada kama ya dakika 5 alitoka naye



    na kumpakia kwenye gari huku wakiwa wamebeba baadhi ya makaratasi,shiiti  ngoja kwanza hebu



    twende ndani Gerald alimwambia Siwah hukua akitoa pisto yake ndogo na kutangulia, mbona una



    haraka sana Gerald hata hawajamaliza kutuelezea wewe umeshaanza kukimbilia ndani haya hebu



    endeleeni kunielezea mim,i Siwah aliwaambia wale majirani.

    Gerald kuingia ndani alikuta vitu vimefumuliwa fumiliwa na kuchambuliwa sana huku kwenye kabati



    za chumbani kwake zikiwa zimepekuliwa na baadhi ya karatasi zikiwa zimepekuliwa na zingine



    zikionyesha wazi zimechukuliwa kuangalia pembeni mwa kitanda akaziona simu za mpenzi wake



    zikiwa kwenye kabati dogo la vipidozi  mule chumbani, akakuta kuna missed call nyingi na za kwake



    zikiwepo pia, basi Gerald akachukua zile simu na kuziweka kwenye mfuko wake wa suruali wakati



    anataka kutoka kuelekea sebuleni kuangalia juu ya mlango ule wa kuingia chumbani kwake



    akakutana na maandishi yaliyoandikiwa kwa marker pen nyekundu MWANAMKE MWENYE



    KOVU JEUSI LEO AMEKUTEMBELEA CHUMBANI KWAKO..

                                                 *******************************

    Gerald baada ya kuona yale maandishi yalimchanganya sana pale pale alijihisi kuchanganyikiwa



    ikawa mara  atoke aelekee sebuleni mara aludi chumbani mara aingie chooni, haiwezekani huu ni



    usanii wa hali ya juu huyu mtu amejuaje kama mimi naishi hapa, mtoto wa watu pia ameondoka naye



    mimi nitawajibu vipi ndugu zake hapana  huu ni usanii nafanyiwa wakati anaendelea kuzunguka mle



    ndani peke yake huku akiongea mara Siwah akingia mule ndani akiwa ameshika kiatu kimoja cha



    kike mkononi,kaka huyo mwanamke hatari amedondosha kiatu kimoja hiki hapa kinaweza kutusaidia



    katika upelelezo wetu,mbona hueleweki Siwah alimuuliza Gerald baada ya kumuona amekaa kwenye



    kochi sebuleni kwake huku akizungumza peke yakena kurusha rusha ngumi na mikono hovyo,Siwah



    alimsongele kwenye kochi Gerald na kuanza kuzungumza naye kwa upole sana, Gerald alimulezea



    kila kitu huku akimumbia aende chumbani kwake juu ya mlango akasome kilichoandikwa, wakati



    wanaendelea kuzungumza mara simu ya mpenzi wake ikaita mfukoni Gerald aliitoa na kuipokea tu



    mara akasikia sauti nzuri ya kike, samahani sana mimi naitwa Candra,Gerald alimjibu upande wa pili



    samani mwenye simu hayupo, ndio hilo nalijua mwenye simu nipi naye kwangu hapa mimi naye



    zungumza naitwa Candra au ukipenda niite wanamke wenye kovu jeusi nipo kwenye haraki za



    kulifuta hili kovu langu jeusi unanisikia lakini? Alizungumza Yule mwanamke ambaye kwa sauti yake



    ilikuwa ni ngumu sana kuamini kwamba ni yeye ndio aliyekuwa akifanya vile vituko, ndio nakusikia



    Gerald alijibu kwa upole ndio sasa hebu sikiliza kwanza hii sauti alimwambia huku akimsogezea sauti



    ambayo ilikuwa ikitoka kwenye kama redio Fulani hivi, Gerald alisika sauti yamaongezi baina yake



    yeye na bosi wake siki alipokuwa akikabidhiwa lile faili, kisha akasikia na sauti ya maongezi baina



    yake yeye na Zainabu siku ile asubuhi alipoenda ofisini kwake kwa ajili ya kumhoji,

    mwisho Gerald alichoka kabisa aliposikia sauti ya mazungumo yake  yeye na wale majirani wake



    pale nje na maongezi yake yeye na Siwah ambayo yalikuwa hayana hata dakika 10 mule



    ndani,Gerald alijikuta akichoka kabisa pale juu ya lile kochi.unanisika kwa makini sasa nakuomba



    ujitoe kufuatilia hili jambo nakupa siku tatu kama unataka mpenzi wako aendee kuwa hai ilimalizia



    ile sauti na kukata simu,Gerald akaichuka simu ili aangalie ile namba ainpigie kwa simu yake ajalibu



    kuzungumza na mpenzi wake ajue kaka yu hai kuangalia kwenye received call hakuiona

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    namba,aliitafuta ile namba wapi hakuiona hata kidogo,Siwaha siwah hii kali huyu mwanke kila jambo



    nalofanya analijua sasa ndio nini mbona hii kazi inazidi kuwa ngumu hivi? Gerald alimhadithia kila



    kitu alichokisika kwenye ile simu.kaka inabidi siku yakesho asubuhi uombe kikao na bosi wetu



    umueleze kila kitu bwana maana haiwezekani huyu mtu atuzidi maarifa kiasi hiki hapana hapana hiyo



    haikubaliki hizo ni dharau sana





                                       ****************************

    Baada ya kikao kilichokuwa takribani dakika 50 kati ya mkuu wa upelelezi mkoa wa Dar-es-salaam



    na ma afisa wapelelezi waandamizi kuhusu jinsi ya kumdhibiti Yule mwanamke mwenye  kovu jeusi



    kama yeye alivyopenda kujiita, mkuu wa upelelezi aliwaongeza watu wawili washirikiane na Gerald



    akatika kumtafuta Yule mwanamke mwenye kovu jeusi kati ya watu waliongezwa Siwah pia likuwa



    ni mmoja wapo na dada mmoja aliyejulikana kwa jina la inspekta Amina, baada tu ya kikao kuisha 



    wote walitawanyika kila mmoja akieleka mahali pa kuanza  kumtafuta Yule mwanamke,

    Mimi niliondoka moja kwa moja mpaka makao makuu ya mamalaka ya mawasiliano huku Gerald



    akielekea kule benki ya taifa ya biashara kwenda kumuhoji tena dada Zainabu wakati Amina akibaki



    pale pale ofisini akijalibu kupitia lile faili la Yule dada. Nilipofikia pale ofisi za mamalaka ya



    mawasiliano nilijitambulisha na kuingia moja kwa moja mpaka kwenye ofisi ya injinia upande wa



    mawasiliano ya simu nilifika pale huku nikiwa na simu ya Furaha mpenzi wa Gerald



    aliyetekwa,ambayo aliitumia jana kumpigia Gerald, nilipofika mule ndani nilimkata kaka mmoja



    ambaye alionekana ni mtu asiye na utani hata kidogo wala asiyependa masihara, haya kaka nambie



    unashida gani? Na nani amekuruhusu kuja mpaka huku ofisini kwangu? Kwa maana shida zote za



    wateja na malalamiko yanasikilizwa japo chini? Jamaa aliongea kwa sauti iliyojaa kejeli na dharau



    sana,

    Samahani sana kaka kwa kukuingilia kwenye ofisi yako huku ukiwa na kazi nyingi za kufanya, ahaa



    acha maneno mengi bwana eleza shida yako nijue kama inanihusu ama vipi? Yule  jamaa alinikatisha,



    sawa kuna nambo moja imenipigia simu jana usiku sasa nilikwa nahitaji msaada jinsi ya kumtambua



    huyo mtu mwenye iyo namba na anapatikana wapi,nilianza kumeleza Yule injinia. Sasa hiyo shida



    ndio ya kuileta hapa? Mbona watanzania mnakuwa sio waelewa kabisa? Kwani amekutukana? Na



    sisi hapa sheria zinasema ya kwama haturuhusiwi kutoa taarifa yoyote ile bila barua ya polisi na pia



    hizo taarifa inabidi waje kuzichua polisi wenyewe sio mtu binafsi sijui unanipata kaka? Jamaa



    alinieleza huku akiwa bize na kompyuta iliyokuwa juu ya meza yake pale ofisini.

    Sikutaka kuendelea kuzungumza naye sana nilitoa kitambulisho changu na kukambidhi akitazame



    alikipokea akakitazama kama sekunde 25 kisha mwenye akawa mpole, samahani sana afisa, hamna



    shida nilinjibu, samahani sana unajua humu huwa kuna watu wengine wanakuja bila sababu za maana



    mtu ameona meseji kwenye simu ya mpenzi wake basi huyo anakuja hapa au anaenda kwenye



    kampuni za simu ajue ni nani yupo wapi  samahani sana kiongozi, Yule injinia alizidi kujitetea huku



    akiacha kuchezea kompyuta yake na kukaa kunisikiliza kwa makini. Ndio kaka hebu tuzungumze



    sasa kaka hebu nambie tatizo nini? Kaka jifunze kuheshimu wa tu sio vizuri hivyo inamaana kama



    mimi nisingekuwa afisa wa polisi ungeendela na majibu yako utumbo? Hata shida yangu



    usingeisikiliza si ndio? Hapana kaka samahani sana watu ni wasumbufu sana kaka kama



    nilivyokuambia niwie radhi kaka sikutaka kuendelea kujibishana nae Niliitoa ile simu ya furha na



    kumuonyesha kuwa siku ya jana kuna simu iliingia lakini baada ya kumaliza tu kuongea nayo



    haijabaki kwenye call list, aliichukua ile simu nay eye kuikagua hakuiona pia, kisha akainambia



    nimtajie namba ya simu ya furaha, nilimtajia aliingiza kwenye computer yake na kuangalia, pia



    hakuona ile simu kwenye data base zao, kaka nimeshagundua kitu kwani aliyewapigia simu



    amezungumza nini? Sikutaka kumueleza kila kitu ila nilimuambia tu ya kwamba huyo mtu aliyepiga



    simu ni mtuhumiwa na tunamtafuta, hapo hapo alidakia ah sawa nimeshamgundua…!!

    Nilidakia hapo hapo, umeshamjua huyu mwanamke anayetusumbua? Bora hii zoezi liishe maana



    tumeshachoka sasa, nilijikuta namtamkia huku akinitazama machoni na pia akinisikiliza maneno



    niliyokuwa namuambia,hapana simaanishi namjua huyo mtu namanisha nishamgundua huyu mtu njia



    aliyotumia kupiga mpaka namba yake isionekane, nilijikuta nachoka kabisa kwa maaana nilijua zoezi



    linaweza kuwa limefika mwisho kumbe wapi, haya hebu nambie endelea nilijikuta nazungumza



    kivivu na kwa nafsi ya kukata tama, huyu mtu atakuwa amekaa sana Columbia na brazili aliendelea



    kuniambia, huko ndio huu kchezo upo pia atakuwa na utaaalamu sana na compyuta hapa hata



    tufanyaje namba yake hatuwezi kuipata kirahisi maana alichokifanya hapa ni kuingilia kwenye



    syteam ya wave transformation katika satellite yetu kuna code atakuwa ametumia kufanya



    hivyo.niliishiwa nguvu kabisa, sasa tutaipataje kuipata nilimuuliza, hapo ndipo kazi ilipo kuipata iyo



    namba ni kipindi tu pale itakapokuwa inazungumza ndipo hapa itasoma lakini baada ya hapo huwa



    inafutika hii huwa inatumiwa sana na wauza madawa ya kulevya Brazil na Columbia kwa lengo la



    kuwezesha shughuri zao pia huwa inatumiwa na watekaji wa watu huko chile ambapo kuna magenge



    ya wahuni huwateka watoto wa matajiri na kuwapigia simu wazazi wao watoe pesa lasiivyo



    watawauwa watotot wao hivyo huwa wanatumia hii system ili kuepuka kukamatwa,

    Jamaa alizidi kuleta hadithi na maneno mengi mpaka akajikuta ametoka nje ya mada, kaka

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nakuelewa sasa unajua nini lengo hapa ni moja tu jinsi ya kumkamata huyu mwalifu sasa



    tunafanyaje? Tatizo ni kwamba naweza kutegesha hapa ikiita nijue lakini akibadili laini tu hapa



    inakuwa kazi nyingine sipati kitu ila nakuahidi hili jambo nitalifanyia kazi kwa nguvu zote naomba



    unipe siku tatu samahani sana tuwasiliane ijumaa aliniambia Yule injinia basi tuliagania huku



    tukibadilishana naye namba za simu.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog