Search This Blog

Sunday 19 June 2022

KAFA NA UTAMU WAKE - 4

 





    Simulizi : Kafa Na Utamu Wake

    Sehemu Ya Nne (4)





    Trovina kwa sauti ya taratibu huku akishika tumbo akajikuta anasema "Hii mimba ni ya Shemeji Jorome"

    D Rose kwa Sauti ya mshangao akajikuta amesimama huku kamshika Trovina blauzi kwa kumkunja.

    "Mimba ya Jorome wanguuuuuuuuuuuuuu???"



    *************************************



    Endelea.....................



    Tamaa ya kupata fedha zaidi ya ile aliyopatiwa ndiyo ilikuwa ikimtesa kwa wakati huo, Akiomba daladala ifike haraka kule anapoelekea. Trafiki aliyesimamisha daladala aliyopanda alimkera kwa kutumia muda mrefu kukagua gari lile. Kupitia dirishani alitokeza kichwa na kumpungia mkono yule askari akamtazama kisha akaruhusu ile gari kupita kwa sababu yake hiyo ikawa nafuu kwake kuweza kuwahi kule anapoelekea. Kwa mwendo wa kijeshi akishuka katika ile daladala mpaka mbele ya chumba kidogo anagonga kwa Tahadhari. Macho mekundu ya kijana mwenye kifua kipana yalikuwa yanatazamana na Afande John.

    "Vipi shida yako nini?" Yule kijana alimuuliza Afande John kwa shari. Afande John kwa tabasamu la kuigiza.

    "Sijaja kwa shari kaka, Nimekuja kukusaidia usife" John alimjibu yule kijana kwa kujiamini.

    "Nisife? Ni ishu gani hiyo?" Yule kijana alihoji kwa shauku huku akijiweka sawa katika ule mlango.

    "Ni kuhusu demu wako Nyanso" "Nyanso? Nyanso kafanya nini?" Yule kijana alijikuta akiropoka kwa kutojiamini. Meno thelathini na moja yakiwa nje na pengo moja lililosababishwa na kujituma kwake kipindi akiwa Askari polisi baada ya kuruka katika gari wakati wanakimbizana na vibaka kitendo hicho ndicho kilichosababisha kupoteza juno lake la pembeni baada ya kujigonga katika chuma ya bodi la gari. "Jibu la swali lako linatolewa kwa pesa" Yule kijana akashusha pumzi na kumuangalia John kwa wasiwasi. "Shilingi ngapi?" Yule kijana aliuliza. "Toa mwekundu mmoja tu" John alitoa jibu huku akiangalia chini. " Aah kaka fanya buku tano" John akamuangalia yule kijana kisha akageuka na kuondoka. "Siwezi kufanya biashara hiyo, Mimi nataka kukuokoa wewe unaleta biashara zako za kimachinga hapa." Yule kijana alimfuata John na kumzuia kisha akatoa noti ya shilingi Elfu kumi na kumkabidhi John. Kicheko cha ushindi kikantoka John na kumuangalia Yule kijana kwa huruma.

    "Sasa sikia Demu wako sasa hivi yupo Kona kali Guest House na fala mmoja ana sura mbaya wanalambishana asali saa hizi" Macho yalimtoka yule kijana na kukimbilia ndani akatoka akiwa anavaa shati mkononi kashika panga akikimbia kuelekea kituo cha daladala. Huyu ni Dafa kibaka maarufu kimara mwisho.



    ***************************



    Ukubwa wa tumbo la Trina ulizidi kumchanganya, Mawazo ya kumtafuta muhusika aliyemjaza mimba kwa penzi zito la siku moja kama malipo ya msamaha aliokuwa akiuhitaji toka kwake baada ya kutishiwa na bosi wake asipopata msamaha toka kwa mteja yule kibarua kitaota nyasi. Akivuta mdomo huku asijue pakuanzia ni mara nne tu amewahi onana na yule mtu, Mara ya kwanza katika kituo cha daladala alikuwa akipiga debe, Mara ya pili ni ndani ya benki alipozua kizaa zaa kilichozalisha wao kuonana ndani ya hoteli yenye kitanda cha sita kwa sita na kusababisha mbegu kukutana na yai la uzazi kisha kuumbwa kiumbe kinachokua kwa kasi ndani ya tumbo lake wakati mara ya nne muhusika kaja bank na hundi ya fedha nyingi. "Lazima nimtafute sina jinsi, Japo anasura mbaya ila mashine yake inasaga mpaka chuma" Alijiapiza huku akijipa matumaini.

    **********************************



    Akiwa na mpenzi wake Mwamtumu wamelewa kupita kiasi, Ni weekend wakiwa wanakokotana na kujikuta mbele ya mapokezi mwa Hoteli ya Dar Luxury hotel, Funguo wa chumba namba 11 ndio ulikua mkononi mwake, Waliingia ndani kisha yule mwanamke akajilaza pale kitandani, Umbo la Mwantumu halikutofautiana na mke wake wa ndoa aliyefunga naye ndoa na kuahidi kumpenda katika shoda na raha, Akielekea mapokezi kwa ajili ya kununua pombe aina ya amarula huku chumba kikiwa kimerudishiwa kwa mwendo wa kuyumba akajikuta kafika mbele ya Muhudumu wa mapokezi na malipo ya chupa ndogo ya amarula yalikuwa ndio yanafanyika.



    ***********************************

    Nani ya chumba kidogo chenye jina la Mbayuwayu mlangoni katika guest ya uswahilini Mwanamke jasiri na katili alikuwa akivuta bangi huku akiangalia bastola yake iliyowekwa juu ya kitanda, Akiwa kavaa chupi tu peke yake huku juu kavaa Tisheti nyeusi alijikuta akizima kipisi cha bangi alichokua akivuta baada ya kukerwa na sauti ya mwanamke aliyekuwa akilia kwa sauti chumba cha pili. Maamuzi magumu ya kwenda kuchungulia kile anachopewa mwanamke mwenzake katika chumba cha pili ndiyo yaliamuliwa na kuvaa suruali yake harakaharaka mpaka mbele ya mlango wa chumba kile huku sauti ya msichana yule aliyekuwa akilalamika kwa mahaba ilikuwa ikizidi kupasua mawimbi katika ngoma za masikio yake. Chaurembo akiinama na kuchungulia kupitia tundu la funguo macho yake yakagongana na mwanamke aliyekuwa akikatikia Bakora ya mwanaume ambaye hakuweza kumtambua kutokana na kugeukia upande mwingine. Vitu vilivyopita katika kiuno chake na kumfanya asisimkwe vilimfanya chaurembo ainuke na kutoa simu Tayari alikuwa keshamkumbuka Jorome wake na wakati huo alimuhitaji ampe Kile anachompaga kila siku, Kile kilichofanya amlinde dhidi ya maadui wake.

    "Namba unayopiga kwa sasa haipatikani" Jibu la kukera lilitoka katika simu ile. Jicho la Chaurembo likashuka tena kwenye tundu la funguo na kuendelea kushuhudia mechi ya majirani zake.



    ***********************************



    Jorome akiwa kifua wazi akikimbia kwa kasi huku akikatisha chini ya nyumba zilizojengwa bila mpangilio, Tax iliyofunga breki mbele ya miguu yake baada ya kumkosakosa kumgonga, Tayari Jorome alikuwa ndani ya Tanx na neno moja tu likamtoka. "Ubungo" Tax iligeuzwa kwa mwendo wa kasi na safari ikaanza kuelekea eneo la Ubungo.



    Akiwa na chupa yake ya Amarula mkono wa Amani Lyaruu ukasukuma mlango wa chumba namba 12 na kuingia ndani, Mwanamke alikuwa kalala, Amani kwa fujo akaanza kunywa ile pombe huku akimuangalia yule mwanamke pale kitandani kwa Tamaa.



    Tax ikiwa nje ya hotel ya Dar Luxury hotel noti mbili za elfu kumi zilikuwa mkononi mwa dereva tax tayari Jorome alikuwa akipotelea ndani ya ile hoteli. Mbele ya mlango wa chumba namba 12 akasukuma umefungwa atembea mbele kidogo huku kashika kichwa, Mlango wa chumba namba kumi ulikuwa wazi macho yake yakatua kitandani Fikra za manka zikamsonga akasukuma mlango na kuingia ndani. Suruali ikiwa pembeni Dozi nene akishushiwa Mwamtumu mpenzi wa Amani Lyaruu huku akilia kwa sauti akitaja jina la Aman huku akimsifia kwanini hakuwahi kumpa penzi kama analompa kwa wakati huo.



    Juu ya kifua cha Manka Amani Lyaruu akihema haraka haraka Manka akishangaa udhaifu wa Amani huku akifikiri ni Jorome. Sauti ya Amani iliyomuita Manka jina la Mwamtumu ilimshtua Manka na kumtupa amani pembeni na kukimbilia katika switch ya kuwashia Taa. Macho ya Amani yakatua katika Umbo la mke wake aliyemuacha kijijini Mbahe na kushangazwa uwepo wake pale, Kelele ya woga iliyoambatana na mueleka mkubwa uliosababisha amani alale milele kwa tatizo la Brain Congusion.



    *****************************************





    Dafa akiwa kashika panga lake vizuri kwa kupitia mlango wa uani Tayari alikuwa akipita chumba kimoja baada ya kimoja katika Guest ya Kona kali huku akiwa kalikamata panga lake vyema. Harufu kali ya bangi aliyokutana nayo katika chumba chenye maandishi yaliyoandikwa Mbayuwayu mlangoni ilimfanya asimame kwa dakika kisha akaridhishwa na mtu aliyeko ndani ya kile chumba si anayemuhitaji akasogea mbele huku akikakagua chumba kimoja baada ya kingine. Sauti ya msichana akilia kwa uchungu ilimfanya azidi kusogelea mlango sauti ile ile inapotokea alipogusa mlango ulikuwa wazi akajipenyeza ndani macho yake yakagongana na Mwili wa Nyanso ukiwa umefungwa kwa shuka huku unavuja damu katika mikono na miguu ukiambatana na kilio cha maumivu kilichosababisha sauti ya nyanso kutoka kwa taabu ni kamba aliyofungwa mdomoni na kutenganisha mdomo wa juu na wa chini. Kwa hamaki panga lilikuwa chini katika Dimbwi la damu machozi yakimtoka huku akimkumbatia nyanso kwa uchungu.



    *********************************



    D Rose akichomoa bisibisi iliyowekwa vyema kiunoni mwake huku kamshika vyema Trovina tayari harufu ya damu inayoashiria mauaji mbele yake, Tayari roho ya kinyama ilikwishamvaa na kilichobaki kwa wakati huo ni kulinda penzi zito alilonalo dhidi ya Jorome mwanaume aliyevunja bikira yake kwa penzi zito alilopatiwa kwa mara ya kwanza. Trovina kwa woga akirudi nyuma na kujikuta anaishia kwenye ukuta huku macho yake yakitazamana na Bisibisi ndefu iliyokuwa ikishushwa na mwanadada aliyeuma meno yake kwa nguvu huku anaonekana hana hata chembe ya huruma.

    "Sali sala zako za mwisho" ni nafasi ya mwisho aliyopatiwa Trovina ya kuungama dhambi zake. Huku akilia kwa uchungu akaanza kusali.

    "Eeh Baba tazama mwanao uliyeniumba nikiwa mkamilifu, Ukanipa kila nilichohitaji katika dunia hii, ila ulininyima mpenzi mwenye uwezo wa kuziridhisha hisia zangu, Baba nimetenda kosa kwa kumsaliti mpenzi wangu Thum na ukanikutanisha na kijana uliyemtunuku uwezo wa ajabu katika kitanda bila kujali sura yake mbaya akanipa kile nilichokikosa na ambacho sijawahi kupewa na mtu yeyote katika hii dunia, Nisamehe kwa kila nilichotenda ila siwezi kusema kingine zaidi ya kusema nampenda sana Jorome" "Nyamazaaaaaaaaa" Sauti ya ukali na ya kutetemesha ilitoka katika kinywa cha D Rose huku Bisibisi ikishuka kuekekea katika Tumbo la Trovina.



    ***********



    Sauti ya tofauti aliyokuwa akiitoa Mwantumu ilimchanganya Jorome huku akijiuliza iweje mchaga aongee lafudhi ya kizaramo katika siku chache alizokaa Jijini Dar. Akijitoa katika kifua cha Mwantumu huku mwantumu akimvuta aendelee kumpa kile kilichomchanganya zaidi. Moja kwa moja kwenye swichi ya Taa kidole kikabonyeza swichi taa ikawaka, Weupe wa mafuta maarufu ya karolit ulimshtua Jorome na kugundua Mwanamke aliyelala nae si Manka. Akivaa nguo zake haraka haraka Jorome alitoka katika kile chumba huku Mwantumu akimfuata nyuma bila kujali yuko uchi. Akisukuma mlango wa chumba namba 10 macho yake yakagongana na Sura ya manka ikiwa na huzuni huku Amani akiwa kalala chini kimya. Mwantumu bila kujali anachokiona pale chini alikuwa hatambui yeyote zaidi ya kuendelea kutaka apewe alichokuwa anapewa dakika chache zilizopita. Macho ya Manka yalipotua juu ya mwili wa Mwantumu ulio mtupu yalihamisha akili zake na kugonga katika utamu aliopewa na jorome na kuona kuna mtu katoka kulamba utamu wake dakika chache zilizopita, Mwanamke wa kichaga ambaye hakuwahi pewa penzi zito katika maisha yake tayari alikuwa kageuka mbogo kwa kutumia meno yake yupo juu ya sikio la Mwantumu na wakaanza kupigana.

    Uwezo wa Jorome kunyanyua vitu vizito ndio uliomsaidia kumtoa manka juu ya Mwantumu na kuwatenganisha huku kanga aliyokuwa kajifunga manka ikiwa pembeni na kubaki mtupu kama alivyozaliwa. Kila mmoja akiwa na hasira na mwenzake Jorome aliwaangalia kwa huruma kisha akaanza kuvua nguo. Wakiwa wamepigwa na butwaa macho yao yakiwa chini ya kitovu cha Jorome, Bakora iliyosimama vyema ilikuwa ikicheza kwenda juu na chini

    "Si wakati wa kugombana nitawapa kila mmoja haki yake" Jorome aliwaambia kisha akamsogelea Manka na kumshika mkono kisha akamfuata Mwantumu akawapeleka kitandani. Tayari Bakora ndefu yenye joto la asili ilikuwa ikizunguka katikati ya Tundu dogo linalozalisha raha ya ajabu katika mwili wa Mwantumu huku ulimi wa Jorome ukiwa unatalii katika eneo la mbele lifunikwalo na chupi aktika mwili wa Manka. Kelele za utamu kutoka kwa wasichana wawili zilikuwa zikisikika bila kujali kama pale ndani kuna Maiti ya Mwanaume wao imelala.



    *****************************

    Status ya Trina katika ukurasa wa UWANJA SIMULIZI ulioko katika ukurasa wa Facebook iliwavutia wengi na kuhoji kuhusu mtu anayezungumziwa kwa wakati huo, Sifa za Jorome alizokuwa akizitoa Trina zilizidi kuwavutia wapenzi wa ukurasa huo na kuendelea kudadisi kuhusu sifa za mtu huyo. Nima binti wa kimasai na mtoto wa Tajiri mkubwa anayeishi Mererani alikuwa mmoja kati wa watu waliovutiwa na Habari za Jorome, Maswali mengi yalikuwa yakimiminika kutoka kwa Nima kwenda kwa Trina yalifanya Nima kumjengea Picha Jorome kwa jinsi alivyo kulingana na maelezo.

    "Sijali sura yake lazima niuonje huo utamu" Nima alijiapiza huku akijiahidi kutumia fedha ya baba yake bila kujali ni kiasi gani ilimradi tu auonje utamu wa Jorome.

    Ni jumamosi ndani ya Ndege ya Precision Air katika siti ya Daraja la kwanza, Akiwa kavaa Skin Jeans nyeusi iliyomkaa vizuri, Viatu vyenye rangi nyeusi na nyekundu huku juu katupia blauzi nyekundu yenye maandishi makubwa yanatosomeka DIVA. Mawazo na akili yake ni kuhusu Mwanaume aliyesikia sifa zake kupitia ukurasa wa Facebook.



    *****************************

    Bisibisi ndefu iliyo katika mkono wa D Rose ikawa inashuka juu ya Tumbo la Trovina huku Trovina akiwa kafumba macho. Sauti ya mlango kugongwa kwa fujo ndiyo iliyomzindua D Rose katika Roho ya kinyama kwa Haraka Bisibisi ilikuwa ikitambaa chini ya kochi huku tabasamu la kuigiza likiwa mbele ya uso wa Trovina.

    "Mh kumbe shost wewe ni muoga hivyo, Nilikuwa nakuzingua" D Rose alitoa jibu lililofanya Trovina afungue macho na kukutana na Tabasamu la D Rose huku akipokea busu katika shavu lake toka kwa D Rose. Sauti ya mlango kuendelea kugongwa ndiyo iliyomsukuma Trovina kuusogelea mlango na kufungua. Macho yake yakagongana na Askari polisi waliokamata vyema bunduki zao. "Uko chini ya ulinzi" Sauti isiyo na mzaha ilitoka katika kinywa cha mmoja wa askari wale. "Nimefanya kosa gani jamani?" Ni swali lililobeba alama nyingi za mshangao toka kw Trovina.

    "Twende utajua kituoni" Askari alitoa jibu huku wakimsukuma Trovina kuelekea katika gari lililoegeshwa nje ya nyumba ya Trovina, D Rose bilaambua kinachoendelea alijikuta akisindikiza Gari lile lililombeba Trovina kwa Macho.

    "Trovina Ahusika na kifo cha mpenzi wake" Ni kichwa cha habari cha Gazeti la udaku lililotoka asubuhi na kuweka wazi kuwa Trovina aingia katika utata wa kifo cha Thum.



    ********************************



    Jina la Jorome liligonga katika Masikio ya Nima wakati akishuka katika Tax nje ya Hotel ya Dar Delux huku akishuhudia wasichana wawili na mwanaume mmoja wakipakiwa katika gari la polisi. "Yule ni nani?" ni swali lililomtoka Nima kwenda kwa muhudumu aliyekuwa akishangaa lile tukio. "Yule jamaa anaitwa Jorome kakutwa na wanawake wawili Chumbani pamoja na maiti ya Mwanaume mmoja" Yule muhudumu alimjibu Nima huku akiondoka. Nima akili yake ikafanya kazi haraka na kufikiri uwezo wa baba yake na jinsi baba yake alivyokuwa akitumia fedha kwa polisi.

    Kama mcheza filamu wa sinema za action akarudi katika tax na kumuamuru dereva alifuate lile gari. Katika kona ya kuingia Ubungo maji ghafla tax ikasimama ikasababisha gari la polisi kufunga breki Tayari Nima alikuwa nje ya Tax na kuelekea lile gari la polisi huku askari walio nyuma ya lile gari wakiweka silaha zao vizuri. Nima kwa Tabasamu akaingiza mkono kwenye pochi na kutoa burungutu la pesa na kuliweka juu ya Dashboad ya lile gari huku akiwaangalia polisi waliokaa nyumba. "Hii ni taarifa kabla ya habari. Tukikubaliana ndio habari kamili" Nima alitoa maneno yale huku akiwaangalia wale askari wawili pale mbele wenye vitambi. Macho ya askari yakiwa juu ya lile burunguti la pesa tamaa zikiwaka ndani ya ubongo wao walijikuta wakimtukuza Nima. "Tufanye nini Mkuu?" Waachieni hao watu nitawaongeza marambili ya fedha hizi. Kama kapigwa funguo Askari mmoja akashuka toka pale mbele na kutoa amri Wakina Jorome washushwe na akakabidhiwa Nima tayari walikuwa wakielekea ndani ya ile tax huku Nima akiwaacha na Fedha Nyingi katika Mikono ya wale askari.



    ********************************

    Panga lililotapakaa Damu alilokutwa nalo Dafa lilimuweka hatihani na kujikuta akibeba kesi nzito ya kumjeruhi Nyanso huku akishinikizwa aonyeshe silaha aliyotumia kumjeruhi Nyanso. Jina la Afande John ndilo lililotoka kinywani mwa Dafa na kupelekea John kuingizwa katika hatia ya kushiriki katika uhalifu ule. Uonevu aliokuwa akiufanya kwa raia akiwa uraiani alijikuta akipokea malipo kutoka kwa watu aliowasingizia kesi ambao alikutana nao ndani ya Gereza la Keko wakati John akisubiri Hukumu ya kesi yao. Shahidi muhimu aliyekuwa akisubiriwa kwa wakati huo ili hukumu itolewe alikuwa ni nyanso ambaye hali yake ilikuwa ikiendelea vyema. Siku ikawadia mbele ya Mahakama Nyanso akamtaja John kama Muhusika na kuongezea kuwa yeye ndiye aliyemfunga kamba baada ya kumpiga kwa risasi katika viungo vyake, Huku akilia alikuwa akimtoa hatiani Dafa kwa kumuita mtu pekee aliyekuja kumuokoa ila alikamatwa wakati akijitahidi kuokoa maisha yake. Ni ushahidi wa hasira uliotolewa na Nyanso baada y kugundua John ndiye aliyemwambia Dafa habari ya yeye kuwa kule Guest. Bila huruma na hukumu ya Fundisho kwa watu wengine Miaka kumi na Tano Jela na Kazi ngumu ndiyo iliyomuhamisha John kutoka Mahabusu na kuwa Mfungwa kamili. Katika Mikono ya Mbabe wa Gereva aliyefungwa miaka ishirini kwa ajili ya John tayari alikuwa kampokea Kiherehere John na kumsajili kama mke wake ndani ya Gereza hilo. Maisha ambayo John akuyategemea kugeuzwa mke kwa kuingiliwa kinyume na maumbile na Bond msambazaji wa dawa za kulevya maarufu katika vijiwe vya mateja jijini Dar.

    "Kweli ukipenda kula tuu lazima uliwe" John alikuwa akifikiri huku akilia wakati ameinamishwa katika chuma za mlango wa Gereza usiku wa manane akitoa huduma kwa Mumewe wa Gerezani si mwingine ni Bond.



    ********************************

    Kumkosa kwa muda wa siku mbili ilikuwa ni adhabu kubwa sana kwa Chaurembo, Tokea Jorome akimbie katika Fumanizi alilowafumania Akiwa na Nyanso na kuamua kumpa Adhabu kali Nyanso, Chaurembo alikuwa katikati ya Mitaa akimtafuta Jorome bila mafanikio. Kila kijiwe alichopita na kumuulizia aliambulia jibu lisiloridhisha toka kwa wale anaowauliza kuhusu Jorome. Akiwa kakata tamaa maji yanayofungwa katika paketi yalikuwa mkononi huku akinyonya Taratibu, Macho yake yalikuwa yanatazama Tax iliyopaki nje ya Hotel iliyo nje kidogo ya jiji la Dar es salaam iitwayo Sunlight Hotel, Wasichana wawili walioshuka katika ile Tax na kisha kuonekana kama wanapokea maelezo kutoka kwa mtu aliyekaa mbele ya ile gari yaliyopelekea wale wasichana kurudi katika gari. Mlango wa mbele wa ile gari ukafunguliwa msichana mrefu mweusi akiwa kashika pochi kubwa mkononi akashuka, Chaurembo akili yake iliendelea kumtuma kuangalia filamu inayoendelea. Sura ya Jorome akishuka katika lile gari ilimshtua Chaurembo na kujikuta akipapasa bastola yake kama iko Salama. MAcho yake yakashuhudia Jorome na Nima wakiingia ndani ya ile Hoteli. "Chumba namba 69" Sauti ya muhudumu iliyokuwa ikitoa maelekezo kwa kina Jorome ilipokelewa vyema na masikio ya Chaurembo. Akiwa kakamata bastola yake vyema akisogelea chumba namba 69 huku maamuzi magumu yakipita katika akili yake. "Leo namuua pamoja na yeye, Huyu mwanaume malaya sana" Ndicho kilichokuwa kikipita na kuamuliwa katika akili ya Chaurembo. Sauti ya mlango kugongwa ndiyo ilimtoa Nima kitandani na kusogelea mlango ili aufungue.





    Ilikuwa ni siku ya Furaha sana kwa Madame Mutamegwa, Akiwa kasimama mbele meza kubwa iliyoshehena vipodozi vya kutosha yenye kioo kipana. Weusi wake wa rangi ya pepsi na umbo lake lililokaa bila mpangilio ndilo lililokuwa likimfanya mama huyo kuonekana kituko mbele ya watu, Akijipulizia marashi aina ya Zone love marashi ghali sana duniani yanayotengenezwa katika kampuni kubwa ya utengenezaji wa Pafyumu bora iliyoko Paris Ufaransa. Akiangalia muda katika saa yake mara kwa mara tayari akaongoka kwa mwendo wa kasi kuelekea nje na kuingia kwenye gari akatulia mpaka dereva wake, Mzee Abdi alipowasha gari na kuondoka, Msongamano wa magari ndio uliokuwa ukimkera kwa umahiri wa kulijua jiji la Dar mzee Abdi alikatisha katika Vichochoro na kujikuta wamefika mbele ya Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jk Nyerere. Ndege ya Gulf Air ndiyo ilikuwa ikisubiriwa na Mama huyo Tayari kwa kumpokea Mume wake aliyekuwa akitokea Dubai kununua mzigo wa biashara Zake. Mlio wa simu ndio ulimshtua Madam Mutamegwa na kupokea haraka haraka, Sauti ya mumewe iliyokuwa ikitoka katika Spika ya ile simu ilimfanya akunje sura yake, Ni taarifa kutoka kwa mumewe kuwa amehairisha safari baaada ya mzigo wake kuchelewa kukaguliwa hivyo atarejea wiki moja baadaye. Huku akiongea ovyo akiwa keshakaa kwenye kiti cha gari alimlaumu mume wake sana.

    Vidonge vya Emotion X ndivyo vilikuwa vikimpelekeshaMadame Mutamegwa, Tabia yake ya kutumia vidonge hivyo ili kuamsha hisia za Mapenzi siku hiyo iligeuka kuwa mbaya sana kwake. Akiwa mwenye hasira. "Endesha gari unashangaa nini?" Sauti ya ukali toka kwa Madame ilishtua ngoma za sikio za mzee Abdi na kujikuta akiwasha gari. Kimya ndani ya gari lile kilivunjwa na sauti ya kusonya toka kwa Madame Mutamegwa. "Yule mtu wa kuzibua chemba ya choo mbona hukumleta?" Shambulizi jingine lilielekezwa kwa mzee Abdi.

    "Nitamleta kesho" Mzee abdi alijibu huku macho yake yakiwa makini kuangalia mbele.

    "Sitaki kusikia habari ya kesho hiyo kazi ifanyike leo" Madame alitoa amri iliyopokewa na Mzee Abdi kwa unyonge.



    *************** **********************



    Hasara iliyopata Bank ya Swiss Bank tokea kuanzishwa kwake nchini Tanzania, Ilisababisha Mkutano wa Dharura toka kwa wanahisa wa Bank hiyo kujadili njia ya kunusuru Bank hiyo iliyo maarufu Duniani kote. Faida ndogo waliyokuwa wakiingiza ndiyo ilikuwa chanzo cha kushindwa kuendesha benk hiyo nchini Tanzania. Uamuzi wa kuwarudishia Wateja wao Fedha zao uliazimiwa na Bank hiyo kufungwa kabisa. Taratibu za Kuifahamisha BOT kuhusu maamuzi hayo zilikwishakamilika na Mtaji wao ulioko hazina uliazimiwa utumike kulipia madeni ya wateja.



    Ikiwa zimeisha wiki mbili Tokea Tangazo la wateja wa Bank hiyo kufanya Taratibu za kutoa Fedha zao ni mteja mmoja tu mwenye kiasi kikubwa cha Fedha alikuwa bado hajafika. Meneja wa benk hiyo akiwa kashika File lenye jina la Jorome kiasi cha shilingi Milioni Mianane za kitanzania kilikuwa katika akaunti ya Jorome. Jina la Ally Maugo kama balozi wa eneo analoishi Jorome ndilo lilikuwa msaada kwao ili kupata Maelezo ya kumpata Mteja wao huyo.



    **************** *********************



    Mkono wa Nima ukinyonga kitasa cha mlango wa kile chumba na kuvuta kwa ndani, Mwanya mdogo uliopitisha mwanga kutoka nje ukaonekana na kuzidi taratibu, Mdomo wa bunduki uliomuangalia Nima ulizidi kusogea ndani, Chaurembo akiwa na sura ya Tofauti inayoashiria Mauaji ilimuogopesha Jorome aliyekuwa kakaa kitandani. Tabasamu alilokuwa kalitoa Nima ndilo lilimchanganya Nima Jorome huku akishangazwa na Tabasamu lile. Kidole cha Chaurembo Tayari kilikuwa katika kitufe cha kufyatulia Risasi, Akiwa kafumba macho anashtushwa na sauti ya kikohozi kilichotolewa na Nima, Kosa la kufumbua Macho ndilo lilimgharimu chaurembo, Teke lilikuwa limetua Juu ya mkono ulioshika bastola na kusababisha bastola kudondoka chini, Chaurembo kwa haraka akajiweka sawa huku jicho lake moja likiwa linaangalia Bastola iliyokuwa chini huku mguu mmoja wa Nima ukiwa umeikanyaga Vyema. Mate yaliyotua vyema katika paji la uso la Chaurembo yalimkera na kupeleka mkono kuyafuta ndio lilikuwa kosa la pili tayari teke lilishautingisha mshipa wa fahamu ulio nyuma ya shingo na kusababisha Chaurembo kutua Chini kama gunia la chumvi, Tayari alikuwa amekwisha zimia.



    Tao Yan mjapani aliyelipwa pesa nyingi sana na Baba yake na Nima Tajiri wa Kimasai aishie Arusha mmiliki wa Machimbo ya Madini Ghali Duniani aina Ya Tanzanite ndiye aliyekuwa akimfundisha Nima njia za kujilinda. Ukorofi wa vijana wengi Mererani ndio ulimpelekea Baba yake na Nima kutumia Gharama kubwa kuhakikisha Nima anaweza kujilinda Toka akiwa Kidato cha kwanza. Tayari mbinu za Tao Yao zilikuwa zimemlaza kimya Chaurembo.



    ************** *********************

    Uzuri wa Tanzania ndio uliomvutia Serena na kuamua kupanga safari ya kuja Tanzania kutembelea, Akiwa ndani ya Ndege pamoja na Mpenzi wake Aitwae Scotch serena alikuwa Akiwaza Mlima mrefu kuliko Yote Barani Africa Mlima kilimanjaro. Jarida la BANG lilikuwa mkononi mwake akiangalia Picha kubwa ya mlima huo katika ukurasa wa katikati wa Gazeti lile.



    Sauti laini ya Muhudumu wa ndege ile kupitia spika ndogo za kwenye ile ndege ilikuwa ikiwataarifu Abiria Kufunga Mikanda na kujiandaa Tayari kwa ndege kutua katika Uwanja wa Kimataifa wa JK Nyerere. Serena akiwa na Tabasamu Alimuamsha mpenzi wake Scotch aliyekuwa usingizini na wakafunga Mkanda Tayari kwa ndege kutua.



    ****************** *******************



    Kwa mwendo wa Maringo Nima akamsogelea Jorome na kumpapasa kifuani kisha akamnong'oneza taratibu. "Nataka unipe ulichowapa wale wadada" Jorome akatabasamu na kuangalia chini. Nima akageuza shingo na kumuangalia Chaurembo kisha akazalisha swali lililoenda kwa Jorome. "Embu niadithie siku ya kwanza ulivyompa huyu" Hadithi za ngono ndicho kitu pekee zinachoamsha hisia za binti wa kimasai Nima. Jorome kwa sauti ya Chini huku akiwa na hofu na binti yule.



    "Siku ya kwanza nilianza kwa kuzipapasa kokwa zake taratiibu, Kisha ulimi wangu ukatalii katika sikio lake la kushoto, Nilishuka taratibu mpaka eneo muhimu linalobadilisha akili za wanadamu pindi tunapolifikiria hapo Akaanza lia mwenyewe. Sehehemu iliyotengwa katika eneo hilo kwa ajili ya kuhamsha hisia, Baada ya hapo nikaanza kazi Rasmi inayonifanya niitwe mwanaume" Sauti ya Nima ikitokea puani ilimfanya Jorome kunyamaza na kuinua kichwa ndipo alipokutana na Nima akiwa uchi huku akiwa hoi anamvuta Jorome. "Oooh ashhhh nipe na mimiiiiii" Nima alimwambia Jorome huku akipenyeza mkono wake katika tundu lililoshtahili kuwa na zipu katika suruali aliyovaa Jorome, Pini iliyoziba eneo lile ilifunguka na kumpa urahisi Nima kukutana na Nyoka asiye na Meno aliyevimbisha kichwa chake kukabiliana na kilicho mbele yake. Nima akiwa anakula koni ya Jorome Mara Anashtushwa na sauti ya Mlango kugongwa taratibu...................



    ****************



    Kila mtu alikuwa akishangaa magari matatu mazuri yaliyokua yamepaki nje ya nyumba ya kuu kuu, Minongono ya watu yakijadili uwepo wa magari yale ilizidi kusambaa na kutengeneza mikusanyiko ya watu kwa mafungu, Uvumi ulioenea miezi miwili iliyopita kuwa serikali imewauzia kinyemela raia wa Afrika ya kusini eneo lile na kutaka kufungua kujenga kiwanda bila kuwashirikisha wananchi husika uliwafanya watu wale kuzidi kuongezeka na kupelekea kuzunguka yale, Ukimya ulio ndani ya ile nyumba ulizidi kuwapandisha wakazi wa eneo lile hasira, Wakazi wa eneo lile walikaa tayari kwa tukio lolote litakalotokea Mara baada ya mlango wa ile nyumba kufunguliwa. Mwanamama mmoja mnene wa makamo kutoka akifuatiwa Ally Maugo balozi wa eneo lile kisha wakatoka wazee wawili wakifuatiwa na Meneja wa Bank ya Swiss Cash, Wingi wa watu eneo lile ulimuogopesha Ally Maugo na kujikaza huku akijivika sura ya kutokuwa na woga akapita katikati ya watu huku wakimuangalia nyuma akiwa kafuatiwa na wageni wake. Wananchi wakiwa wanafuatilia lile tukio kwa ukaribu Safari ikaishia mbele ya nyumba anayoishi Jorome.

    "Ni hapa anapoishi" Ally Maugo aliwaelekeza wale wageni, Meneja wa bank ya Swiss Cash alisogea mbele huku akishangaa nyumba anayoishi Jorome.

    "Balozi nafikiri tutakuwa tumekosea" Meneja alimjibu BAlozi huku akigeuka kuondoka.

    "Lakini hapa ndipo anapoishi Jorome mnaomuulizia huyo ambaye picha yake ipo kwenye fomu yenu" Balozi alijibu huku akichungulia ndani kwa jorome kupitia mwanya uliopo mlangoni. Meneja wa Bank ya Swiss Cash akamsogelea Yule mama wa makamo na kuongea nae. "Hivi Madame inaingia akilini Mteja mwenye zaidi ya milioni Mia nane akaishi hapa?" Swali lile lilipelekea Yule mama kutikisa kichwa kuashiria pia yeye hakubaliani nalo. "Ok tunashukuru Tutarudi siku nyingine, Ila kama akija mwambie aje Bank ya Swiss Cash kesho" Meneja wa bank alijibu huku wakielekea walipopaki magari na kuondoka.

    "Maugo hao watu ni wakina nani?" Mwananchi mmoja alijikuta akimuuliza swali maugo baada ya kuvumilia kwa muda mrefu. "Mimi najua wasiwasi wenu, Mnachofikiri hakiwezi kutokea kamwe na mimi siwezi kushiriki, Hawa watu ni watu wa Bank wanamtafuta yule Jorome Mzoa Taka" Jibu la Maugo lilitosha kuwaridhisha wananchi wa Yombo Machimbo na kutawanyika.



    ******************** ************************

    Sura ya msichana Mrembo akiwa kavaa nadhifu mkononi kashika kitabu kikubwa iligongana na Macho ya binti wa kimasai akiwa katokeza kichwa nje kiwiliwili kikiwa ndani.

    "Samahani nimewaletea Menu mchangue chakula cha jioni mtakachokula" Sauti ya yule msichana ilimkera Binti yule wa kimasai na kujikuta akijibu kama hataki.

    "Samahani tutakupa taarifa tukihitaji huduma" Jibu lile liliambatana na Sauti ya Mlango kufungwa na kupokewa na sauti ya viatu vikikanyaga sakafu ya hoteli na kuzalisha mlio uliokuwa ukipokezana kulia kutoka chini ya viatu vya yule binti.



    Kama mbogo aliyejeruhiwa tayari Nima alikuwa juu ya kifua cha Jorome na kazi nzito ya kulijenga Taifa la Wapendanao ilikuwa ishaanza huku minong'ono midogomidogo ikiwa inazalishwa kutoka kwa wapenzi hawa wawili bila kujitambua. Kilichoendelea wanajua wanandoa tu na wale wazinifu wote.



    *********** *************

    Dereva tax wakiwa katika harakati za kushawishi abiria kupanda Tax zao, Wingi wa watu eneo lile waliokuwa wamebeba mabango makubwa mikononi mwao yenye majina wa yatu, Macho yao yakiwa katika mlango wanaotumia Abiria kutokea ndani ya Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere, Binti wa kizungu akiwa anasukuma toroli lililobeba begi lake kubwa nyuma akifuatiwa na kijana wa kizungu mwenye kifua kipana, Macho ya binti huyo yakatua juu ya Maandishi yaliyo katika gari moja yaliyoandikwa TAX alisogea moja kwa moja mpaka kwenye ile gari na kutabasamu. "Please we need a good Hotel" {Tafadhali tunahitaji Hoteli nzuri} Kingereza kibovu kilichozungumzwa na binti yule wa kizungu kilipokewa na Dullah dereva Tax maarufu pale uwanja wa ndege, Akawaashiria wapande ndani ya gari na safari ikaanza.

    "My name is Dullah" {Naitwa Dullah} Dullah alianza kuwasemesha wageni wake, "Oh thanx, My name is Serena and this is my Boyfriend he dont know english, me i know a litle but we speak Rusian language" {Oh Nashukuru, Mimi naitwa Serena na huyu ni Scotch, Ni mpenzi wangu ila yeye hajui kingereza, Mimi najua kidogo ila tunaongea kirusi} Serena al alijielezea kwa kingereza chake kibovu, Dullah alitabasamu na kugundua hawezi kupiga hadithi na wateja wake. Safari yao ikaishia mbele ya hotel ya Fiesta zone. Tayari Dullah alikuwa akigeuza gari na kuwaacha wakina Serena wakiingia nadani ya ile hoteli.



    ***************** ********************



    Sauti ya Mlio wa simu yake kutoka ndani ya suruali iliyo mfukoni mwake ndiyo, Akigeuka huku akimtazama Nima aliyelala ovyo pale kitandani huku mguu mmoja ukiwa mashariki na mwingine ukiwa magharibi, Moja kwa moja mpaka kwenye suruali akachukua simu na kuisikiliza. "Aah ndio..." Ok nakuja sasa hivi" Jorome akakata simu na kukamata suruali yake akavaa nguo harakaharaka na kutoka nje huku akinyata.

    Tayari ndani ya Bajaj na ilikuwa ikipaki nje ya nyumba kubwa ya Madame Mutamegwa, Jorome alisimama nje ya geti kwa Tahadhari akabonyeza kengele na kusubiri, Sauti ya miguu ya Mtu ikisogelea geti ilisikika vyema katika Masikio ya Jorome, Sura ya Mama aliyevaa Cheni kubwa ya Dhahabu shingoni iligongana na Jorome, "Nikusaidie nini?" Mama yule alimuuliza Jorome. "Samahanani nimeagiziwa na Mzee Abdi." Jorome alijibu kwa unyenyekevu. "Ooh wewe ndiye yule mtu wa kuzibua chemba ya choo?" Mama Mutamegwa alijibu kwa Tabasamu. "Ndio" Jorome akaonyeshwa eneo penye Chemba akavua suruali na kubakiwa na kaptula kisha akaanza kufungua mfuniko wa Chemba. Bustani ya nywele zilizo katika kifua cha Jorome zilimchanganya Mama Mutamegwa na kujikuta Joto kali la Mahaba likiuvamia mwili wake, Vidonge vya Emotion X alivyokunywa vilizidi mchanganya Mama Mutamegwa. "Kijana njoo huku" Mama Mutamegwa alimuita Jorome huku akielekea katika Maegesho ya Magari pale ndani. "Oh samahani kavae nguo" Mama Mutamegwa alimwambia Jorome huku Akitabasamu, Jorome akavaa nguo na kurudi mbele ya yule mama akamuonyesha ishara apande Gari.



    Akili ya Mama Mutamegwa ilikuwa ikiwaza ngono tu na mwanaume aliye mbele yake ndiye aliyekuwa sahihi kwa wakati huo, Mawazo ya kutafuta eneo zuri na lililojificha atakalotumia kukata kiu kupitia Bomba la Jorome lenye koki ngumu ambayo itamridhisha kufungua mpaka pale litakapotoa maji ya kukata kiu yake.



    ************** ********************



    Mzee Mutamegwa baada ya kuwasiliana na Mpenzi wake wa nje ambaye waligombana nae kwa muda mrefu na kumaliza Tofauti yao kupitia Mtandao wa Facebook walikuwa wamekubaliana kukutana na kupeana penzi la kufungua ukurasa wao wa Mapenzi, Kuwahi kumwambia Mke wake juu ya Safari yake ya Kurudi Nchini kulimfanya kuukiza kichwa sana. Uamuzi wa kumdanganya kuwa harudi nchini wiki hii ndio aliuona wa Busara ili apate nafasi ya kufaidi penzi la Nance mpenzi wake wa Muda Mrefu. Kwa kutumia Software ya Fake Call iliyo katika Computer yake ndogo ya mkononi alimpigia mkewe wakati yeye akiwa keshafika nchini na yuko ndani ya Chumba namba 78 ndani ya hoteli ya Fiesta Zone wakila Raha na Nance.

    Meno yote yakiwa nje baada ya mke wake kuridhika na maelezo yalimfanya amkumbatie Nance aliyejilaza pale kitandani huku wakiahidiana kukaa wiki nzima ndani ya ile hoteli bila kutoka nje.



    ************** ****************

    Mama Mutamegwa akiendesha gari kwa kasi kuelekea barabara ya Morogoro Road, Alipofika Kimara Stop over akaingia kushoto na kufuata Barabara ya Vumbi Gari likashika Breki kali mbele ya Hoteli ya Fiesha Zone. Jorome alibaki akimshangaa mama yule bila kujua kinachoelea akajikuta anaambiwa ashuke na Tayari walikuwa Mapokezi na Funguo wa Chumba namba 79 ulikuwa mkononi. Jorome akapanda ngazi kivivu mpaka mbele ya mlango wa chumba namba 79 kisha akasimama. "Tunaenda wapi?" Ni swali lililotoka barabara toka kwa Jorome. "Kwani wewe ni Mtoto? Sikia kijana nitakupa peasa unayotaka naomba unipe penzi lako" Mama Mutamegwa alitoa Jibu lililomchosha Jorome. "Mama sitoweza" Jorome alijibu huku akiwa anageuka kuondoka, Mama Mutamegwa alimshika mkono na kumpa ishara asuburi, Tayari mkono ulikua ndani ya Pochi ukatika na Bastola ikamuelekea Jorome. "Sasa utanipa hiyo kitu yako" Mama Mutamegwa aliongea huku akiangalia eneo la zipu la Jorome. Jorome kwa Shock akajibu kwa wasiwasi. "Sijakataa kukupa ila nina njaa sitoweza?" Mama Mutamegwa akamuangalia Jorome kwa Huruma. "Ok ingia ndani utaletewa chakula na utakula nitakupa chakula ya mzee wangu halafu nitakuongeza na pesa" Mama Mutamegwa aliongea huku akimvuta Jorome Mkono kuingia ndani kisha mlango ukafungwa.



    ****************



    Akiwa kakaa ndani ya Chumba chake kalamu mkononi akiwa anaandika baadhi ya vitu vinavyohusiana na kazi aliyopewa na ofisi kuifuatilia, Ni tukio la Wizi wa dola Milioni moja alizoibiwa Mgeni katikati ya jiji la Dar es Salaam, Uamuzi wa kufuatilia hoteli aliyokuwa akiishi mgeni apate mawili matatu ndio ulifuata.



    Mawazo juu ya Jorome yaliiwasili ghafla na kumtawala D Rose, Akaacha kila kitu na kujiegemeza katika kochi kubwa pale ndani kwake. Kauli ya Marehemu Rafiki yake aitwaye Tina aliyemtanguliza Mbele ya haki kwa wivu wa Penzi alilopewa na jorome lililoambatana na uzinduzi rasmi wa ufunguzi wa mlango utumiwao na wapenzi. Hakutaka mtu yeyote aingie katika mlango aliyeufungua Jorome. Kauli ya kuwa Jorome ni afisa wa ikuli alianza kuiamini taratibu baada ya kuunganisha tukio la Muuaji hatari aliyeshindikana kuuawa na Jorome kutokomea kusikojulikana, Hofu ya Jorome kujua Mpango wake ndiyo iliwaka ndani ya mawazo yake, Hofu kuu aliyonayo D Rose ni kama Diblo alimwambia Jorome kama yeye ndiye Muhusika nyuma ya tukio lile. Hofu na Mawazo vilizidi kumsonga. Kwa ujasiri D Rose akaamka na kuchukua Kitabu chake pale mezani na kuweka katika Mfuko wa kaptula yake raba tayari zilikuwa katika miguu yake na safari ya kutekeleza jukumu la ofisi ikaanza.



    **************** ******************

    Tatizo la Mama Mutamegwa Kulia kilio kama cha kufiwa wakati anafanya ngono lilikuwa likimkera sana mama huyo, Matumizi ya pombe kali kabla ya kufanya ngono ndio yalikuwa sehemu yake kubwa ya kuficha aibu hiyo, Makelele ya Mama Mutamegwa ndicho kitu pekee ambacho kilikuwa kikimkera mume wake mpaka kuamua kutafuta nyumba ndogo.



    Ndani ya chumba chenye hadhi ya juu Mama Mutamegwa alikuwa anamimina Pombe aina ya Amarula katika kinywa chake pasipo kutumia Glass, Jorome akiwa anakula chakula akiwa kakaa katika kochi kubwa lililo pembeni ya kitanda akiwa kajifunga Taulo. Macho ya Mama Mutamegwa yaliyo na Ujumbe mzito wa Kuhitaji Apatiwe kile mwili wake unachohitaji kwa wakati huo huku Dawa ya Emotion X ikizidi kupandisha joto la Mahaba katika mwili wake. Akivua nguo zake haraka haraka na kubaki mtupu kama alivyozaliwa Macho ya Jorome yakatua katika ikulu ya Mama yule iliyofichwa na Mkusanyiko wa nyama nyingi za Mapaja yake. Mama Mutamegwa kwa mwendo wa Kilevi akamsogelea Jorome na kumuinua pale kwenye kochi akaanza kumpapasa. Eneo lililo rasmi kwa wakati huo katika mwili wa Jorome likasimama wima na kusababisha Taulo kudondoka chini Macho ya mama Mtu mzima yakatua katika kifaa kinachowachanganya wakina dada wengi waliowahi kumfahamu kiumbe hichi.

    "Ni yako mwenyewe hiyo?" Mama mutamegwa alijikuta akiuliza huku akitolea macho umbile la mbele la Jorome. Jorome kama alivyo nyani anapofumania Mgomba wenye ndizi zilizoiva vyema katikati ya Msitu huku akiwa na njaa akaanza kumparamia mama yule na kuanza kumuandaa kwa ajili ya kumpa adhabu kali kwa kosa la kumleta pale ndani kijeshi.



    ************ *****************

    Mwanaume mmoja akiwa katika boti yake ndogo ikiwa kasi katikati ya Bahari ya hindi, Mara ile boti inapunguza mwendo yule Mwanaume anatoa ndoano yake ya kuvulia samaki anaitupa katika Maji huku akitumia kifaa maalumu cha kuvutia ile nduano. Mara Nduano ile inavutwa anavuta kwa nguvu anazidiwa nguvu na kujikuta anavutwa katika yale maji, Mkono mrefu kutoka ndani ya Maji unampokea kisha Mdomo mkubwa wenye meno marefu unafunguka na kummeza yule mtu.

    "Shit" Ni sauti ya Serena huku akifunga kitabu cha hadithi cha mtunzi maarufu wa vitabu duniani William Burrough kiitwacho Deadman on way, Alichokuwa akisoma. Akiwa kakaa katika eneo la kupumzikia lililo ndani ya ile Hotel ya Fiesta Zone Serena anachukua glass ya mvinyo aliokuwa anakunywa na kuipeleka moja kwa moja kinywani kisha anaendelea kusoma hadithi ile ya Deadman ambayo ilikuwa imeshaanza kumteka.



    *************** *********************



    Kilio kikubwa kama cha msiba kilisikika ndani ya chumba namba 79, Ni Mama Mtu mzima alikuwa akiadhibiwa na kijana wa kipemba mjukuu wa Mzee Mwinyi aitwaye Jorome aliyeingia ndani ya Jiji la Dar es Salaam na kupokelewa na Chumba cha wagonjwa Mahututi cha Hospital ya Rufaa ya Muhimbili Baada ya kunusurika katika ajali mbaya ya Meli ya Mv Sulivian. Utaalamu wake wa kupiga mashuti ya nguvu ndio uliomfanya aweze kuwavua nguo za ngani wasichana wengi ndani ya Jiji hilo. Sasa alikuwa yupo juu ya Kifua cha Mama Mutamegwa anaondoa nguvu ya Dawa ya Emotion X na chupa ndogo ya Amarula aliyokunywa Mama Huyo.



    Kelele zile zilimshtua Mzee Mutamegwa aliyekuwa katekwa na usingizi mzito, Kelele za mkewe ambazo hutoaga pindi wanapopata chakula cha usiku zilikua zikirindima katika masikio yake, Akaamka na kukaa kitandani huku akifikicha macho bado ile sauti ilikua ikisikika wazo la ndoto likamuondoka akajikuta akipigwa na butwaa, Kutajwa kwa jina lake kutoka katika chumba cha pili tena kwa kashfa kulimuhakikishia kuna mtu kazama ndani ya mgodi wake na muda huo ndio anachota madini yake. Akajikuta kajifunga taulo bastola ikiwa Tayari mkononi na kuelekea katika mlango wa kutokea katika kile chumba chake.



    **************** *****************

    Wingi wa kiasi cha Fedha alichokuwa nacho Jorome katika Benk yao ndicho kitu kilichomchanganya Meneja msaidizi wa Benki ya Swiss Cash Neria Lwanko au Madame kama anavyopenda kuitwa, Akiwa ndani ya ofisi yake ndani ya Bank hiyo huku akitokwa na jasho japo kuwa kiyoyozi kilicho hapo ndani kilikua kikifanya kazi vyema. File lenye maelezo ya Jorome na Picha ndogo ya Jorome vilikuwa vikimchanganya, ubaya wa sura ya Jorome na kiasi cha Pesa alichokuwa nacho havikufanana kabisa, Akavuta kumbukumbu ya nyumba anayoishi Jorome havikufanana hata kidogo na thamani ya fedha zake ndani ya akaunti yake. Mawazo ya utajiri anaomiliki wa zaidi ya milioni mia na hamsini ambao ameupata kwa muda wa miaka kumi aliyotumikia katika bank ya Swiss Cash na njia nyingine binafsi lakini haukufikia hata Robo ya Fedha alizonazo Jorome.



    Tabia yake ya kuingia katika mahusiano na wanaume wenye fedha na kisha kuwarubuni na kuwafukuza ilikuwa imeshajijenga katika akili yake na sasa alikuwa akifikiri kuhusiana na Jorome na alitamani yeye ndiye awe mmiliki wa Mali zile.

    Akiandika namba za simu za Jorome zilizo katika File lile na kuzipiga jibu la kutokupatikana kwa namba zile kilimkatisha tamaa na kujiapiza lazima aamrubuni kwa kumpa penzi zito Jorome mpaka amkabidhi utajiri huo na kisha kutokomea kwao Rwanda na kumuacha Jorome katika Mataa ya Tazara.



    ************** *****************

    D Rose akiwa nje ya Mapokezi ya hotel ya Fiesta Zone, Daftari la kusajili wageni likiiwa mkononi akitazama kitu na kuandika andika katika kitabu chake.

    "Kwa siku huwa mnaweza kupokea wateja wangapi?" Swali toka kwa D Rose lilienda kwa Muhudumu wa mapokezi wa Hoteli ile. "Mh inategemea mara nyingine wateja 30 mpaka 50" D Rose anaandika katika kile kitabu kisha anamuangalia yule muhudumu.

    "Huwa mali za wateja za thamani kama fedha mnahifanyi nyie au wanahifadhi wenyewe?" Swali jingine kutoka kwa Mwandishi wa Habari na Mtangaji wa kituo cha Radio cha Sweet Fm mwanadada D Rose lilimfikia muhudumu yule. Wakati anajiandaa kujibu swali lile mara unasikika mlio mkubwa wa Risasi ndani ya Hotel ile..........!

    "PAaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah"



    ************* ******************



    Haya sasa utamuuu utamuuuu, D Rose hofu imemkamataaa, Mama Mutamegwa tayari kaanza kilio cha msiba usio na Maiti, Mumewe kashtukia.... Neria aka Madam Tamaa ya Pesa inampeleka mikononi mwa Mtu mzima Joromeee na Ukisikia PAAAAAAAAAA! Ujueeee!



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog