Search This Blog

Sunday 19 June 2022

MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI - 4

 





    Simulizi : Mwanamke Mwenye Kovu Jeusi

    Sehemu Ya Nne (4)







    Niliingia mule kwenye ile ofisi na kumkuta Yule mhariri ambaye alikuwa kijana wa makamo tu kama



    mimi, tulisalimiana kisha nikamwambia ya kwamba nilikuwa nahitaji maelezo ilikuwaje mpaka



    wakaniweka kwenye habari mbele kwenye gazeti lao bila hata ya mimi kuniuluza, alionekana kujaa



    wasiwasi na woga hasa baada ya kuona mimi nilikuwa serious huku nikiwa sicheki ili kuonyesha

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    msisitizo

    Alianza kuniambia ya kwamba zile habari pamoja na picha wao walitumiwa na mwandishi mmoja



    kwa njia ya barua pepe aliyejitambulisha kwa jina la “ mwanamke mwenye kovu jeusi”.

    Niliguna  kisha nikamwambia aendelee kunipasha, aliendelea kuniambia ya kwamba Yule mwandishi



    wa habari aliwatumia ile habari huku akiwa ameambatanisha na namba yake ya simu basi wao



    walichokifanya ni kumpigia simu na kumuuliza ili kupata uhakika zaidi ambapo aliwambia ni kweli



    kabisa, nilimkatisha kisha nikamuuliza “ je ile ilikuwa ni mara ya ngapi kwa yule mwanamke



    kuwapatia habari”

    Aliniambia ya kwamba ilikuwa ni mara ya kwanza nay a kuwa Yule dada ni mwandishi wa habari za



    uchunguzi ndivyo yeye alivyodai ndio maana hata jina lake hakutaka lifahamike. Nilisononeka sana



    baada ya kusikia vile nilijua Yule mwanamke amefanikiwa kunivuruga kabisa kuanzia kwenye jamii



    hadi kazini kwangu.enhe unaweza labda kuniambia huyo mwanamke mmeshawahi kufanya nae kazi



    labda na pia yupo vipi mounekano wake? Halafu anakaa wapi? Nilijikuta namuuliza maswali



    mfululizo bila hata ya kusubili nijibiwe, Yule mhariri alijiua fika jilikuwa nimepaniki kwani alianza



    kunishusha hasira zangu kwa maneno yaliyojaa samahani na utetezi mwingi ili nisimchukulie hatua



    yoyote , tulijaribu kupiga ile namba aliyokuwa nayo ya Yule mwanamke lakini haikupatikana, baada



    ya kumaliza kupiga ile simu nilimwambia Yule mhariri awe makini na kazi yake kama miiko ya kazi



    yao imewashinda basi aachane na hiyo kazi akatafute kazi nyingine. Niliondoka pale ofisini huku



    hasira zikiwa zimenijaa sana kifuani kwani mpaka pale Yule mwanamke alikuwa amefanikiwa vizuri



    sana kunipotezea mwelekeo alionekana Yule mwanamke alikuwa ni mtu mjanja sana huku akiwa ni



    mtu mwenye mbinu mbalimbali ili aweze kufanikisha malengo yake.

    Kule kusimamishwa kazi kwa muda usiojulikana kusema kweli kulinichanganya sana nilijaribu



    kuwasiliana na Amina na Gerald ili wanieleze ni kipi kilikuwa kinaendelea, lakini wote walionekana



    kama vile walikuwa wakinikwepa, nilijihisi mnyonge sana kwa kutengwa kwa sababu zisizo na



    maana nilijua watakuwa wameamliwa vile na mkuu wetu wa kazi eti kwa lengo labda siri zisivuje



    kwani walidai mimi nilikuwa na uhusiano na Yule mwanamke mwenye kovu jeusi. Nilikaa wiki nzima



    nyumbani bila hata ya kwenda popote nikisubilia labda nitaitwa kazini lakini ilikuwa tofauti mwisho



    nikaamua ni bora niende nyumbani Tanga nikapumzike na kusalimia wazazi kwani kuendelea kukaa



    Dar es salaam nilikuwa nazidi ku kuweka matatani maisha yangu bila ya sababu za maana.

    Basi siku iliyofuata nilianza safari ya kuelekea nyumbani kwetu Tanga ambapo nilipanga niende



    nikapumzike angalau kwa muda wa wiki nzima kupumzisha akili huku nikiwa nasubili hatima yangu



    kazini nilondoka mida ya saa 6 hivi kwani Tanga sio mbali sana tena kwa mimi ambaye nilikuwa



    natumia usafiri wangu binafsi isingeweza kuchukua zaidi ya saa 4 kufika Tanga mjini maeneo ya



    chumbageni ambapo ndipo wazazi wangu walipokuwa wakiishi niliwachukulia wazazi wangu zawadi



    ndogo ndogo kwa maana ingekuwa ni aibu kwenda nyumbani nikiwa sina hata zawadi ya



    kuwapelekea wazee kwani ilikuwa imepita zaida ya miezi ita bila ya mimi kwenda  Tanga kwani mara



    ya mwisho nakumbuka ilikuwa kwenye msiba wa mtoto wa mama yangu mdog ambapo napo nilienda



    lakini sikukaa sana kwani ofisini nilipewa likizo ya siku mbili hivyo basi nilienda kuzika na kuludi tu.



    Nilianza safari yangu taratibu sana kwani nilijua hiki kipande cha Dar es salaam mpaka chalinze



    huwa kinakuwa na magari mengi sana hivyo sikutaka kwenda mwendo wa kasi bure nisije kupata



    ajali ya bila kujitakia  wakati naendelea kuendesha gari iliingia meseji kwenye simu yangu lakini



    sikutaka kuisoma kwanza kwani nikiwa naendesha gari hasa kwenye barabara kubwa kama ile



    morogoro road huwa sipeni kabisa kusoma meseji au kabisa hata kuwasiliana na mtu yoyote na simu



    ili kujiepusha na ajali zisizo na ulazima niliendelea na safari yangu huku nikiwa naskiliza nyimbo ya



    zilipendwa ya otto jazz ambao siku hizi wanaitwa msondo ngoma wosia kwa watoto, kwani ule



    wimbo mara zote ulikuwa ukinikumba enzi za zamani wakati baba yangu bado anafanya kazi katika



    mashamba ya mkonge kule hale muda mwingi alikuwa akiludi toka kazini basi alikuwa anawasha



    redio yake ya kanda kisha anauweka ule wimbo na kuniita mimi niusikilze,basi kwa kuwa nilikuwa



    naelekea nyumbani kila nilivyokuwa nausikiliza ulikuwa ukizidi kunipa hamu ya kufika nyumbani.

    Nilipofika chalinze nilipaki gari njiani kwa ajili ya kununua bidhaa zingine za kwenda nazo nyumbani,



    wakati wale wafanya biashara wakiniwekea zile bidhaa kwenye gari ndipo nilipokumbuka ya



    kwamba kuna kipindi kuna ujumbe wa meseji uliingia kwenye simu yangu ya mkononi nilikuta ni



    ujumbe wa meseji kutoka kwa Yule mwanamke mweye kovu jeusi kama kawaida yake lakini akidai



    ya kwamba mpaka mimi ndio nilikuwa hatari katika kumfuatilia hivyo amejitahidi kunidhibiti kama



    niliendelea tena basi atanitoa uhai,niliguna huku nikiwa na hasira sana huku nikijiapiza nitakapoludi



    Dar-es-salaam nitaanza kumtafuta mwenyewe kwa siri nilitangaza kisasi nay eye mpaka nimpate



    kama ni uhai basi na mimi anitoe niliwasha gari nakuendelea na safari yangu taratibu sana.

                                                   *******************************

    Nyumbani niliwaelezea kisa chote ambapo walinionea huruma sana kisha mama akaniambia inanibidi



    niwe makini sana na watu wa mule ofisini kwani inawezekana kabisa tukawa tunachezeana mchezo



    kwa sabau ya wivu na kuona jinsi labda nilivyokuwa makini sana katika kazi zangu.sikiliza



    mwanangu katika hizi ofisi watu hawapendani kabisa bora utambue hilo huwezi jua itakuwa labda



    wametumia kigezo hicho ili kukuondoa ofisini alinieleza mama yangu huku tukiwa tumekaa



    varandani jioni tukinywa chai kwani nyumbani kwetu tulipenda sana kunywa chai jioni pamoja na



    chapatti mihogo,bagia,na nyama ya kusaga,basi pale mama alinihusia mambo mengi sana moja wapo



    likiwa ni kuoa kwani umri ulikuwa unanitupa mkono sana, alivyozungumza vile nilimkumbuka sana



    Jamila mwanamke shupavu ambaye tulikuwa tukifanya nae kazi lakini ilikuwa muda sasa akiwa



    masomoni akiwa ameenda kuoneza ujuzi wa elimu yake, nilimkumbuka kwa sababu alikuwa



    mwanamke mzuri sana mwaminifu mwenye heshima huku akiwa ni mtu aliyenijali sana japo kila

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nilipomuomba tuanzishe uhusiano alikuwa akikataa bila ya sababu za  muhimu eti ya kwamba



    alikuwa akinionea huruma.

    Usiku ule nilijaribu kumuandikia barua pepe kwani ndio nji niliyokuwa naitumia kuwasiliana naye



    huku nikimpa mkasa mzima ulionikuta,nililala siku hiyo usiku sana kwani kwani muda mwingi



    niliutumia kuwa kwenye  net huku nikifungua kurasa mbalimbali kusoma njia mbalimbali za



    kiitellejensia zilizokuwa zinatolewa kwa njia ya mtandao nilijikuta nikijifunza njia mbalimbali za jinsi



    ya kuchunguza  na kufuatilia uhalifu ambazo kwangu niliona zingenisaidia sana .

    Kesho yake baada ya kumaliza mizunguko ya hapa na pale huku nikipita sehemu mbalimbali kuona



    jinsi mkoa wangu wa Tanga ulivyokuwa umebadilika kwani sikuwa nimepata kwa muda



    mrefu,nilizunguka sana kwa kutumia gari yangu huku nikiwa na mdogo wangu wa kiume  William,

    Jioni nilimwambia sio mbaya kama tukielekea raskazoni ambapo ndipo palikuwa na beach nzuri



    twende tukapunge upepo maana pia sehemu zile nilikuwa na muda sana sijapata kuhudhuria kwani



    kwa Dar-es-salaam muda mwingi nilikuwa nakuwa bize sana kaziBasi tuliona kuingia katika beach za



    Kiswahili isingekuwa vizuri sana hivyo basi tukaona ni bora tuingie Mkonge hotel ambapo pale



    tulikuwa tukipigwa na upepo moja kwa moja wa bahari huku tukiziona meli zilizokuwa zikiingia na



    kutoka katika banadri ya tanga tulikaa pale huku mdogo wangu yeye akiwa anatumia kilevi ila mimi



    sikutaka kunywa kwani akili yangu ilikuwa bado haijakaa sawa tuliendela kukaa pale huku nikitumia



    muda ule kumshauri mdogo wangu kwani nilipata malalamiko kutoka kwa mama kuhusu baadhi ya



    mienendo yake wakati tunaendelea na mazungumzonilitaka kumpigia simu mama kumjulisha ya



    kwamba chakula cha jioni wasituhesabu kwani tungeweza kuchelewa ndipo nilikumbuka ya kwamba



    nilisahau simu yangu moja niliisahau kwenye gari, nilimpa ufunguo wa gari yangu mdogo wangu na



    kumwambia aende kunichukulia simu yangu. Aliondoka pale tulipokuwa lakini baada ya kama dakika



    saba nilimuona akitokea kwenye kona huku akiwa analudi kasi sana pale nilipokuwa huku akiwa



    ananiita jina langu kuashiria kabisa hapakuwa salama.

    Nilishituka na kumfuata ili tukutane nae njiani, alikuja kasi sana na aliponifikia alinishika huku



    akihema na kunielekeza tutoke nje haraka sana pombe zote ilionekana zilikuwa zimeshamtoka



    kichwani, kaka  kaka Mary nimekutana nae akitoka kweny gari yako, alizungumza huku akiwa



    anathema sana kiasi kwamba amneno yalikuwa yanatoka huku yakiwa yamekatika katika sana



    mpaka maneno mengine nikawa siwezi kuyasikia tulitoka nje mpaka kwenye parking ambapo tulikuta



    gari langu mlango wa mbele ukiwa wazi , mdogo wangu alianza kunieleza ya kwamba wakati anatoka



    nje alikutana na Mary akiwa kama vile anapekuwa kwenye lile gari langu na baada ya kumuona



    anatoka alichomoka haraka haraka sana na kuondoka huku akiwa ameondoka na simu yangu,



    nilimsikiliza kwa makini sana kisha nikamuuliza wewe unamjua huyo mtu? Alinjibu huku akili ikianza



    kumludi sawa baada ya zile pombe alizokuwa amekunywa kuanza kumuisha kichwani, ndio namjua



    japo sio sana kuna siku alinipigia simu na kukutana nae pale capchino ambapo ambapo tulizungumza



    nae mambo mbali mbali ya biashara. Mh niliguna baada ya kusikia mambo ya biashara kisha



    nikamwambia aendelee kunielezea, alidai ya kwamba Yule mwanamke ni mfanya biashara akiwa



    anajihusisha na biashara ya kuuza milungi akiitoa nchini Kenya hivyo basi alikuwa anataka nimsaidie



    kumkutanisha na wewe ili iwe rahisi kwake yeye kuwa anaiingiza Dar-es-salaam, sikuweza kupata



    muunganiko kati ya biashara na mimi gari yangu kusachiwa kisha kuondoka na simu yangu, niliingia



    ndani ya ili gari nakaiangalia angalia ndipo nilipokuja kugundua ya kwamba kumbe alikuwa ameweka



    kinasa sauti kidogo sana mbele ya gari kwenye ubao ulioshikilia kioo nahisi baada ya kumuona



    mdogo wangu alikurupuka ndio maana hakuweza hata kukiweka vizuri kile kinasa sauti, hapo hapo



    akili yangu iligutuka na kujua atakuwa tu Yule mwanaharamu, sasa nilianza kujiuliza je alijuaje kama



    mimi nimeenda nyumbani? Hapo ndipo palianza kunitatiza nilimpa pesa ya kulipia vinywaji mdogo



    wangu na kisha kumuambia ya kwamba yeye aende akalipe kisha aje tuelekee zetu nyumbani kwani



    siku yangu nilihisi ilikuwa imeshaharibika tayari.

    Tuliondoka pale mkonge  hotel huku akili yangu ikiwa imezidi kuvurugika nilijihisi kama maisha



    yangu yanazidi kuwa hatarini hivyo nilikuwa nahitajika kuchukua hatua za tahadhari mapema



    sana.wakati tunakaribia kmitaa ya makataba mdogo wangu alinionyesha kwa mbali Yule mwanamke



    huku akiwa amevaa hijabu kabeba na mkoba akiteremka kuelekea bondeni ambapo palikuwa na



    barabara ya kuingia bandarini basi na sisi tuliongeza mwendo na kwenda kushika njia ya kuingia



    bandarini  tulifika pale bandarini ambapo palikuwa na harakati sana kwani kulikuwa na meli ya



    mizigo iliyokuwa inapakia sementi nilishika kwenye gari na kuwauliza wale walinzi wa bandari, kama



    wamemuona mdada mmoja akiingia mule walinijibu ndio Yule dada alikuwa akielekea shelisheli na



    ile meli ya sementi mume wake ndio alikuwa amechukua ule mzigo. Nilishangaa sana kusikia vile,



    mara kwa ndani nikamuona Yule mwanamke akiwa anazunguka mule ndani alipotuona tupo getni



    alijifanya kama kushituka vile ahalafu akaongeza mwendo kuelekea kwenye gati palipokuwa



    pamepaki ile meli ya mizigo na mimi niliona wale askari wa bandari walikuwa wananichelewesha



    wakati mbaya wangu namuona kwa mbele akipotea kwenye macho yangu nilitoa kitambulisho



    changu haraka haraka kisha nikamuachia mdogo wangu ufunguo wa gari kisha na mimi nikazama



    mule bandarini niliingia mule moja kwa moja mpaka kwenye ile meli na kuanza kumsaka huku



    nikiwa na tahadhari kubwa sana. Niliendelea kumsaka mule bila mafanikio mpaka mida ya saa 4



    usiku huku nikiwa nasaidiwa na baadhi ya askari wa bandari, mwisho meli ilimaliza kupakia mizigo



    na kuanza kupiga honi kuahiria kwamba ilikuwa tayari kwa safari, sikuwa na jinsi zaidi ya kujikatia



    tama na kuanza kutoka nje wakati meli inaanza taratibu kuacha ardhi na kuelea baharini kwa muda



    kama dakika ishirini hivi huku nikiwa nimejisimamia nikiwa sina la kufanya ndipo nilipomuona kwa



    mbali Yule mwanamke kwenye ile meli ya mizigo akipanda ngazi kutokea chini akieleka juu roho

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/-

    ilinimua sana kwani kwa pale nisingeweza kumpata tena nilitoka mule bandarini nikiwa sina jinsi tena



    mungu wangu huyu adui kweli kama kucheza na akili yangu basi amefanikiwa sana tu,

                                *****************************

    Kwa kuwa nilikuwa bado nipo likizo niliamua kufanya maamuzi magumu ya kwenda shelisheli kwani



    nilijua Yule mwanamke kule patakuwa ndipo panamakazi yake kwani nakumbuka hata mule pangoni



    katika zile hati za kusafiria tulizozikamata moja ilikuwa ikimtambulisha kama ni mtu wa visiwa vya



    shelisheli basi nilijua inaweza kuwa kweli kwa maana nilikusudia kumsaka mahala popote kwani



    salama yangu ilikuwa ni yeye kukamatwa kwani sasa ilibainika ya kwamba mimi pia nilikuwa



    nahusika na Yule mwanamke sasa ilinibidi kutumia juhudi zangu binafsi ili niweze kuwathibitishia ya



    kwamba sio mimi pale kazini walinisimamisha tu kutokana na chuki zao binafsi.siku ile ile asubuhi



    niliwaaga nyumbani kuwa niludi Dar-es-salaam kulikuwa na dharura imetokea kumbe upande wa pili



    nilikuwa nataka niende nikafanye utaratibu ili ikiwezekana siku ile ile niweze kupata visa ya visiwa



    vya sheli sheli ili jioni yake nianze safari ya kuelekea kule kwani nilijua kama nikiweza kupata usafiri



    wa ndege nilikuwa na uhakika kabisa wa kuiwahi ile meli kabla haijafika hivyo  basi ningeweza



    kumuona Yule mwanamke pindi ile meli ikiwa inashusha mizigo.nilifika Dar-es-salaam mida ya saa 5



    asubuhi ambapo nilipitiliza mpaka kwenye ofisi za ubalozi wa shelisheli nchini niliingia pale na



    kukutana na afisa mmoja katika ule ubalozi nilimueleza ya kwamba nilikuwa naenda mapumziko



    mwezi mmoja, nashukuru kati ya nchi ambazo zilikuwa na uhusiano mzuri na Tanzania na ambazo



    hazikuwa na taratibu ngumu sana sisi kwenda Shelisheli nilogongewa pale visa yangu kisha moja kwa



    moja nikaelekea ofisi za afrifight agent ambazo zlikuwa ni ofisi za mawakala wa tiketi za ndege,



    niliwauliza wahudumu wa pale waliangalia kwenye computer kisha  waliijibu ya kwamba kwa siku ile



    kulikuwa na Kenya airways ambapo ilikuwa inanipasa niende mpaka Nairobi kisha niunge na ndege



    nyingine.ya shirika lile lile mpaka shelisheli basi baada kumaliza ile booking ya ile ndege ambayo



    walisema ilikuwa inaondoka saa kumi na moja jioni, basi sikuwa na jinsi zaidi ya kuelekea nyumbani



    kwangu kwenda kupaki gari langu kisha nichukue taxi iweze kuniwahisha uwanja wandege kwani



    muda uliokuwa umebakia ulikuwa ni mdogo sana kwani pale ilikuwa tayari imeshafika saa 8 na robo.



    Hivyo ilinipasa kuongeza mwendo.

                                     **************************************

    Nilifika kwangu na kuchukua tu nguo zangu chache sana nikaziweka kwenye begi lagu dogo, laptop



    yangu, viatu na raba pea moja kisha nikachukua na atm yangu ya Barclays bank kwani sikutaka



    kubeba hela nyingi ule ulikuwa ni utaratibu wa kizamani sana ndio niliona hivyo nilichukua ile ya



    Barclays ili nikifika kule niweze tu kupata huduma kupitia visa card na master card nilikuwa nipo



    simple sana kiasi kwamba kama mtuangeniona asingezania kama nilikuwa na safiri.

    Nilimaliza kupaki vitu vyangu huku muda ukiwa umeenda sana kisha nilitoka nje na kuchukua taxi



    kwani pale nyumba niliyokuwa naishi kwa nje kulikuwa na tax nyingi sana zilizokuwa zinapaki



    nilipanda kwenye taxi moja kisha na kumuambia dereva anikimbize uwanja wa ndege kwani muda



    ulikuwa ni saa tisa kasoro kama dakika kumi hivi dereva alitoka kwa mwendo mzuri sana huku



    akijaribu kupita sehemu zingine kwenye panya road ilimradi tu tuwahi kufika tulipofika stesheni



    tulikutana na foleni kubwa sana kwani trafiki pale alikuwa amkasirika kisa deriva daladala mmoja



    alimwambia kwa nin alikuwa akivuta magari ya upande mmoja tu?basi kwa hasira ule upande



    akaamua kuuacha kabisa kuruhusu magari kupita kwa muda wa zaidi ya saa sasa niliangalia pale



    ilikuwa tayari imeshafika saa kumi na robo. Mapigo ya moyo yalizidi kuongezeka kwani ndege



    ilikuwa inaondoka saa kumii na moja kamili na muda wa kufika ilikuwa na saa moja kabla basi pale



    pale nikaampa Yule dereva taxi elfu kumi kisha mimi nikashuka zangu nakupanda boda bodaili niwee



    kuwahi ndege kwani ilikuwaimefika kwenye saa kumi na dakika ishirini hivi.

    Yule dereva wa boda boda aliniondoa  kwa kasi ya ajabu sana pale tazara huku akijitahidi kuvuka



    magari kwani yalikuwa mengi sana kutokana na ile foleni iliyosababishwa na yule trafiki pale kwenye



    mataa, nilifika uwanjani ilikuwa saa kumi na moja kasoro dakika ishirini, niliruka kwenye pikipiki



    kisha nikamkabidhi yule dereva wa boda boda kiasi cha shilingi elfu tano sikutaka hata kuulizui



    chenji kwani juda ulikuwa umeenda sana ,nilikimbia kama mtu aliyekuwa anakimbia hatari Fulani



    hivi nilifika mahali palipokuwa na wale wakaguzi walitazama tiketi yangu huku begi langu likipita



    mahala pa ukaguzi nilipita haraka na kuelekea kwenye line namba moja kwani ndipo ndege



    niliyokuwa nasafiri nayo ndipo ilikuwa imepaki ikijiandaa kupaa niliikimbilia ndege huku nikipiga



    kelele za wanisubili kwani jamaa walikuwa wanataka kufunga mlango sasa.Nashukuru sana mungu



    nilifanikiwa kuingia kwenye ndege japo kwa kuchelewa sana nilikaa kwenye seat huku ndege ikianza



    kuiacha ardhi taratibu.

                                               *****************************

    Nilifika  visiwa vya shelisheli mida ya saa 7 usiku kwani tulichelewa sana uwanja wa ndege wa Jomo



    Kenyatta Nairobi nchini Kenya, kwani ndege nyingine tulikuwa tukiisubili kutokea Egpty ilichelewa



    sana, nilishuka pale uwanja wa ndege wa visiwa vya shelisheli uliokuwa ukijulikana kwa jina la



    aeropor intertanional de seyc pointe larue, uliopo kwenye mji mkuu wao unaojulikana kwa jina la



    Victoria basi nilienda mpaka mapokezi ambapo nilitoa hati yangu ya kusafiria yule dada wa pale



    uhamiaji aliikagua ambapo aliona nilikuwa nimeingia mule kama mtalii kisha akaigonga mhuri na



    kuniruhusu kuengia huku upande wa pili begi langu nalo pia likipita kwenye  mkanda wa kukagua



    mizigo ambapo pia hawakuona kitu. Nilipitia katika duka la kubadilisha fedha lililokuwa pale pale



    uwanja wa ndege ambapo nilibadili pesa zangu chache nilizokuwa nazo kutoka kwenye shilingi



    kwenda kwenye rupee kwani pale shelisheli walikuwa wanatumia rupee kisha nilitoka njen a kukuta



    taxi nyingi zikiwa zimepaki zikisubili abiria wanaoshuka kutoka kwenye ndege

    Nilimuomba yule dereva wa taxi anipeleke kwenye hoteli ambayo haikuwa na gharama kubwa sana



    ili niweze kuzimudu kwa muda wote nitakaokuwa mule kwani sikuwa na kiasi kikubwa sana cha pesa

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    na pia ile safari nilikuwa nimejigharamikia mimi mwenyewe kwa pesa yangu ya mfukoni, aliniskiliza



    kwa makini kwani nchi ile watu walikuwa wanatumia lugha mbili kiingereza na kifaransa sasa yule



    dereva ilionekana yeye alikuwa anajua sana kifaransa kuliko kiingereza kwani hata kunijibu kwake



    kulikuwa kwa wasiwasi japo alikuwa mchangamfu sana tulianza safari ya kutoka pale uwanja wa



    ndege na kuelekea kwenye hoteli ambayo ndio nilikuwa naenda kufikia iliyojulikana kwa jina la



    silhouette island hotels, moja ya hotel yenye hadhi nzuri huku ikiwa na bei ya kumudu kwa mtu



    yoyote yule huku ikiwa jirani na bandari kwani nilimdanganya ya kwamba mimi nilikuwa ni



    mfanyabiashara nilikuwa nasubili meli yamgu iwasili niweze kupakua mizigo, basi usiku ule niliweza



    kuuona ule mji wa Victoria kiukweli ulikuwa ni mji mzuri sana huku kuna sehemu kukiwa na  mifereji



    kutoka baharini na kuingia ardhini huku sehemu zingine kukiwa na madaraja tuliyotumia kuvuka



    kutoka kisiwa kimoja kwenda kingine yani ile nchi sikuwahi kuona ilikuwa nchi yenye visiwa vingi



    vidogo vidogo sana vingine vikiwa vimeungana vingine vikiwa vimeachana na kutenganishwa na



    mfereji mdogo wa maji ya bahari.

    Nilimlipa yule dereva wa taxi pesa yake kisha mimi nikajivuta na kuingia kwenye ile hoteli nilikuta



    vyumba bado vikiwepo nilichukua chumba ambacho kilikuwa kipo juu ambapo nilikuwa na uwezo



    wa kuona shughuri zote zilizokuwa zinaendelea katika bandari yao ya pale Victoria nilifurahi sana



    kwani nilijua ya kwamba kupitia pale ningeweza kuifuatilia ile meli ambayo nilikuwa na uhakika siku



    ile asubuhi lazima ingewasili tu pale bandarini.

                                                   *******************************

    Kesho asubuhi na mapema baada ya kumaliza kunywa chain a kuosha mwili wangu niliamua sasa



    kuianza ile kazi moja kwa moja ya kumsaka yule mwanamke nilivaa kofia za wapanda farasi kisha



    nikaweka na miwani usoni ili kiasi kwamba isiwe rahisi kwa mtu kunitambua kirahisi kwa maana



    nilijua yule mtu ni hatari nisipokuwa makini itakuwa tatizo ukizingatia hata sikuwa nimeaga mtu



    yoyote nilitoka nje na kuanza kutembea taratibu kuelekea kule palipukuwa na bandari yao nilifika



    pale mapokezi na kujifanya naulizia kama kulikuwa na meli yoyote iliyokuwa inatikea Tanzania 



    kama ilikuwa imeshafika kwani kulikuwa na mzigo wangu yule dada wa pale mapokezi wa bandari



    alinitazama sana kisha akaguna na kunijibu ya kwamba mbona wao wanavyojua meli iliyokuwa



    imeenda kubeba simenti Tanzania ilikuwa imekodiwa yote  na mkodishaji alikuwa ni serikali ya pale



    shelisheli na ilikuwa imeende kubeba simenti kwa ajili ya kutekereza mpango wao wa kujenga



    nyumba za bei nafuu kwa wananchi wa shelisheli, nilijikuta Napata kigugumizi kisha nikamwambia



    ya kwamba niliwamomba na mimi nipakie mzigo wangu wa  machungwa kwa makubaliano



    maaalumu, yule dada alisema lile ni tatizo kwani kwa nchi yao pale itahesabika kama rushwa hivyo



    lazima yule msimamzi wa ile meli atakuwa hatianika kwani atakuwa amevunjwa sheria za nchi



    niliona yule dada maneno yakiwa mengi ndipo nikaamua kumwambia “ sawa basi nimekuelwea ila



    nachokuomba hapa ni kunijulisha tu lini hiyo meli inaingia lini hayo mengine itajulikana nikifika”



    alinijibu inaingia leo mchana kwani ilipita pia Mombasa kupakia sementi zingine  kutoka kiwanda cha



    East Africa Portland cement,hivyo basi itanipasa kugeuka pale mchana kuanzia mida ya saa tisa hivi,

    Nilianza kuondoka pale huku nikiwa na wasiwasi baada ya kusika ile meli imepitia Mombasa kwani



    nilijua moja kwa moja inawezekana yule mwanamke akawa ameshukia Mombasa, nilianza kujiuliza



    maswali mengi sana  kuhusu yule mwanmake na ile meli uhusiano wao baada ya kuambiwa ya



    kwamba ilikuwa imekodiwa na serikali ya shelisheli, au inawezekana yule mwanamke atakuwa na



    uhusiano na kati ya nahodha au baharia katika ile meli ndio swali nililojiuliza kichwani,ok sawa yote



    yatajulikana ngoja kwanza hiyo meli ifike ndipo nitajua kipi cha kufanya, nilijirudisha katika ile hoteli



    niliyokuwa nimefikia ili niweze kupata chakula cha mchana kisha nikae dirishani kuangalia iyo meli



    kuona pindi itakapoanza kuingia, nilimazlia kula kisha nikasogelea computer iliyokuwa ipo mule



    chumbani kwangu  mahususi kwa ajili ya wateja kisha nikaiwasha na kuanza kufungua mitandao



    mbalimbali ya kitanzania ili niweze kitambua ni kipi kilikuwa kinaendelea nyumbani nilifungua barua



    pepe yangu ambapo nilikuta kuna ujumbe mbalimbali kutoka kwa rafiki zangu mbalimbali huku pia



    na kipenzi change Jamila akiwa amenijibu na kunijulisha ya kwamba baada ya wiki atakuwa



    ameshaludi nchini huku akiniambia alikuwa ameshamaliza mafunzo yake kule marekani huku akinipa



    pole sana kutokana na masahibu yaliyonikuta   na kuniomba ni bora niache kujishughurisha na



    kumfuatilia yule mwanamke mwisho na mimi nisije kupotea duniani bure wakati yeye akiwa bado



    ananihitaji, nilijitahidi kumjibu vizuri huku nikijitahidi kupangua zile hoja zake kwa njia tofauti



    kwamba hata kama yule mwanamke nikiachana naye ila kwa yale mauaji yake ya kutisha siku moja



    angeweza kuniua kama sio mimi basi hata yeye pia kwani alikuwa akifanya mauaji hovyo na hata



    bila ya kutoa sababu za msingi wala kusema ni kipi alichokuwa kikitaka.

    Baada ya kumaliza kumjibu barua pepe Jamila ndipo nilipofungua mtandaa wa kijamii wa Darhotwire



    sikuamini nilipokutana na picha ya mwanaume aliyelala hku damu zikimtoka sehemu mbalimbali na



    pia kukiwa na alama nyeusi ikiwa imeziba sehemu zake nyeti huku kukiwa na kichwa cha habari



    “afisa wa polisi afanyiwa mauaji ya kutisha” akatwa na kisu nyeti zake sehemu za siri mwili ulianza



    kusisimka nakujihisi kupata kibaridi Fulani hivi cha woga baada ya kungalia picha ile kwani ilikuwa



    ni picha ya mkuu wangu wa kazi inspekta Thomas.

                                     *******************************

    Mwili ulinisisimka sana nikajihisi kuishiwa nguvu huku machozi yakiwa yananitoka kwani nilijua kifo



    cha mkuu wangu wa kazi na hivi nilikuwa nipo kwenye mgogoro nay eye basi ungeniweka matatani



    kabisa kwani tulikuwa tupo kwenye mgogoro na yeye kabla ya kifo chake sasa kitendo cha yeye kufa



    tena kifo cha kutatanisha ilimaanisha kabisa ningehisiwa ni mimi nimefanya vile ili kuwakomoa au



    kuonyesha ya kwamba sio mimi japo wamenisimamisha kazi lakini bado mbona mauaji yanatokea,



    mwili ulinisismka sana nilijikuta nashindwa kuendelea kuisoma ile habari nakuludi na kukaa kwenye



    kochi lililokuwa mule kwenye chumba change na kuanza kufikiria ni kipi cha kufanya, baada ya



    kuwaza kwa muda kidogo niliona ngoja nijikaze kiume nilitoa kijitabu change kidogo ambacho



    kilikuwa kimejaa namba za watu mbalimbali kisha nikaangalia namba ya Gerald na kuamua



    kumpigia, simu iliita sana bila hata ya kupokelewa mpaka nikajikuta nakata tama ya kwamba labda



    atakuwa yupo msibani na yupo kwenye taratibu za mazishi, niliacha kuipiga ile namba na kuamia



    namba ya Amina nayo iliita pia bila kupokelewa nahisi wote waliogopa kuipokea baada ya kuona ni



    namba ngeni halafu ilikuwa sio namba ya ndani ya nchi basi nilijikuta nakaa tu bila ya kujua ni lipi la



    kufanya kwani watu wote niliokuwa nawategema kupata habari kutoka kwao ndio hivyo tena simu



    walikuwa hawpokei tena basi wakati najiandaa kutoka mule chumbani niludi kule bandarini ili



    kwenda kuangalia kama ile meli itakuwa tayari imeshawasili, mara simu ya mule chumbani kwangu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ndipi ilipoanza kuita kwanza nilihisi labda watakuwa ni wale wahudumu wa mule labda kuna jambo



    wanataka kuniambia au kulikuwa na mtu yoyote alikuwa ananitafuta,lakini baada ya kuipokea ile



    namba mambo yalikuwa ndivyo sivyo kwani yule aliyekuwa amepiga simu alianza kwa kucheka sana



    tena kwa kicheko cha dharau sana,nilikuta nashituka kwani sauti nilihisi kama naijua ila ni sauti



    amabyo nilikuwa sijaisika muda mrefu sana, ile sauti y kike iliniambia ya kwamba nilikuwa najifanya



    mjanja wakati mimi ni mpumbavu sana, kuwa alinitega ili niondoke nchini ili yeye huku aendeleze



    mipango yake, aliniambia kuwa na Gerald alikuwa tayri ameshamteka anasubili siku yoyte aamue



    amfanye lolote, mwili ulisisimka na mapigo ya moyo yalianza kwenda kasi sana, kwani nilijua



    kwamba pale pia nilikuwa nimuzwa na yule mwanamke, niliikata simu kwa hasira kisha na kuangalia



    ile namba iliyokuwa imetumika kupiga nilikuta ni namba ya Gerald, nilizidi kuishiwa nguvu kwani



    nilijua ni kweli basi Gerald atakuwa ametekwa nayule mwanamke, nilijiona kama ni mpelelezi



    niliyekuwa situmii akili kwa kuuzwa kijinga kule Tanga mpaka nikakurupuka na kufunga safari



    mpaka kule visiwani huku mtuhumiwa nikiwa nimemuacha nchini, nilijjishangaaa sana lakini nikaona



    sio mbaya lazima nihakikisha nafanya uchunguzi kwanza kwenye ile meli nikisha jihkikisha ndipo



    niweze ondoka kule shelisheli.

    Nilifika pale bandarini na kukuta meli ile ikiwa imeshafika huku wakisema ya kwamba itaanza



    kupakuwa mzigo kesho yake basi nilikaa sehemu na kuvizia kuona wafanyakzi wa ile meli pindi



    watakapopita basi mmoja wao nimuite niweze kuzungumza nae maneno mawili matatu. Nilijua



    ningeweza kupata kitu basi baada ya kukata tama kama baada ya saa zima ndipo nilipoona watu



    nilijua kabisa walikuwa wafanyakazi wa ile meli nilimuona mmoja ambaye alikuwa na rangi ya



    kiafrika zaidi tofauti na wale wengine ambao rangi zao zilikuwa ni mchanganyiko, alikuwa amevalia



    overolly la rangi ya blue huku akiwa ameshika begi lake la nguo mkononi, baaada ya kumuita



    kwanza alisita kisha ila nahisi baada yak union kwamba mimi ni mwafika mwenzake alikuja bila



    wasiwasi huku akiona kama mtu aliyekuwa na haraka sana, nilimsalimu kiingereza, alinijibu huku



    akiniuliza mimi ni mtu wa wapi nilijitambulisha kwamba ni mtanzania ambaye nilikuwa nipo mule



    visiwani kwenye utalii, alinichangamkia sana baada ya kusika hivyo aliniambia kwamba yeye



    alikuwa ni mmadagaska ila kutokana na kazi yake ya ubaharia ilimuwezesha kwenda sehemu



    mbalimbali ndani ya Afrika tulianza kuondoka naye yae maeneo huku tukuwa tunazugumza taratibu,



    aliniambia ya kwamba yeye kazunguka nchi nyingi lakini Tanzania ni wakarimu sana kuwa walikuwa



    Tanzania siku nne zilizopita, nilizidi kufurahi baada ya kuona mimi na yeye tumeanza kuelewana vile



    kwani ingenirahisishia mimi shughuri yangu ya kujua yule mwanamke ilikuwaje mpaka akapanda



    kwenye ile meli na yuppo wapi kwani kwa muda wote niokuwa pale langoni ikuweza kumuona



    akishuka pia nakumbuka alinipigia simu kupitia namba ya Gerald ya kwamba alikuwa ameniuza mimi



    niondoke ili yeye aweze kutimiza mipango yake mingine, yule kaka maybe baadaye nilikuja



    kugundua kwamba alikuwa naitwa Frednando aliendela kunuambia kuwa pamoja nayote ila



    wanawake wa Tanzania walikuwa wajanja sana, nilihisi kama aliuwa anataka kuja kwenye mada



    niliyokuwa naitaka,  “kwa nini?” nilijikuta namuuliza haraka haraka sana, kuna mwanmake mmoja



    rafiki yangu alimpata Tanga juzi lakini walipofika Mombasa yule mwanamke aliwatoroka bila ya wao



    kujua huku akiwa amebeba kiasi kikubwa sana cha pesa kutoka kwenye ile meli. Ambazo zilikuwa za



    nahodha nilijifanya nasononeka kisha nikamuuliza kwani alimjuaje? Aliniambia  ya kwamba yule



    mwanamke walikuta naye chichi club walipoenda siku moja kabla hawajondoka,huku akinimabia ya



    kwamba wakati anatoroka alidondosha pochi yake ambayo walifanikwa kukuta baadhi ya vitu vyake,



    nilimuuliza ni wapi tunaweza kuupaa hoa mzigo, alinitazama kisha akawa kama anajaribu kunijibu



    kwa lugha ya Kiswahili lakini kilionekana kumshinda kabisa,kisha ndipo akaniambia tu kwa lugha ya



    kiingereza kwamba vipi umetumwa au kakupigia simu ulifuatilie nini? Nilicheka kinafiki ili kupoteza



    lengo kwani yule kaka alianza kuinyesha kama kuchoka hivyo basi nikaona kama nisipokuwa mjanja



    basi sitojua lile begi lipo wapi, alinimbia ya kwamba hana uhakika ila anahisi litakuwa tu mule



    kwenye meli, kwani lilikuwa na vitu vya kike kike tu, tuliendelea kuzungumza mpaka tukafika



    barabarani ambapo yeye alipanda taxi na kuelekea hoteli ambayo ndio huwa wanafikia, nilipia



    hesabu ni vipi nitaweza kuingia kwenye ile meli bila ya kuonkena, basi pale pale wazo likanijia



    namimi nikakodi taxi na kuingia mjini kwenye maduka.

    Jioni ile nilivaa overlloy la blue na viatu vigumu chini nikawa kama vile mmoja wa mabaharia nilifika



    getini pale bandarini na kujifanya kama na mimi nilikuwa baharia wa ile meli huku nikijifanya ya



    kwamba nimesahau ndani baadhi ya vitu vyangu ikiwemo hati yangu walinitazama kisha yule dada



    niliyemkuta mchana akanitazama kama vile alikuwa anafananisha kitu hivi, aliniuliza jina nikamtajia



    la yule jamaa yangu niliyekuana naye pale, walilitazama kwenye daftari la mabaharia walioshuka



    kisha akaniruhusu, sikuamini kwani mapigo ya moyo yalikuwa yakinienda kasi sana, niliondoka pale



    getini kwa kasi ya ajabu sana huku nikiwa naogopa hata kuangalia nyumna,niliingia kwenye ilemeli



    ambapo nilikuta shughuri ya upakiaji ikiwa bado inaendelea,wale wapakuaji hawakuwa na muda hata



    na mimi nilisogea mpaka kwenye mlango wa kuelekea kwenye chumba cha nahodha nilijaribisha



    kuufungua nikakuta upo wazi, basi nikaingia  huku nikitazama kila upande kama naonekana nilianza



    kufanya upekuzi haraka haraka sana mara kwenye kabati kwa juu nikaona mkoba mweusi wa kike



    basi nikajihakikishia kuwa ndio wenyewe niliuchukua na kuanza kuuweka kwenye mfuko mweusi



    niliokuwa nimeingia nao. Wakati namalizia kuuweka mara nikasikia vishindo na sauti ya watu



    wakielekea mule kwenye kile chumba nilichukuwamo..

    Mapigo ya moyo yalianza kunienda mbio sana wale watu walizidi kusogea kwenye kile cumba huku



    wakiwa wanazungumza kifaransa, niliinuka na kuanza lutafuta mahali pa kujificha kwani niljua kama

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    walikuwa ni baadhi ya wale ma baharia wangenitambua kuwa sio mwenzao hivyo ningekuwa



    matatani sana, nililisogeza kabati mule chumbani na kupenya kwa chini ambapo palikuwa na uvungu



    mkubwa tu kiasi kwamba kama wangeingia isingekuwa rahisi kwa wao kuniona, nilikaa mule kwa



    takiribani zaidi ya dakika kumi na tan bila ya mtu kuingia huku zile sauti zikionekana zikizidi



    kupotelezea, nilishusha pumzi kisha nikatoka mule uvunguni na kuanza kuangalia njia sasa ya kutoka



    nje kwani muda ulkuwa umeenda sana.

                                             **************************

    Baada ya kuingia chumbani kwangu pale hotelini cha kwanza kabisa nilikuwa na hamu ya kujua je ni



    kipi kilichokuwepo ndani ya lile begi. Nililifungua lile begi na kukuta kuna vitu vya kike  tu kama



    nguo za ndani, marashi, sabuni, na mapambo mengine, roho iliniuma sana kwani nilijiona kama



    nimepoteza muda wangu na kujiweka hatarini bila ya sababu ya maana, nililitupa lile begi chini kwa



    hasira sana, nililipo anguka chini ndipo nikaona kama kuna vitu vikitoka kwenye zipu ya pembeni,



    basi nililiinua haraka tena lile begi kisha na kuanza klikagua tena kumbe lilikuwa na zipu ya pembeni



    niliifungua haraka haraka sana, nilikutana na kijiabu kikiwa na namba mbalimbali za simu baada ya



    kuanza kuzipia moja baada ya nyingine nilikuta namba karibia za wafanyakazi wote wa pale ofisini



    zikiwepo, nilishituka sana baada ya kuona hivyo, niliendelea kufunua kile kjitabu nikakutana na



    sehemu ambapo alikuwa ameandika kumbukumbu zake mbali mbali kila jambo na tukio nilishangaa



    sana baada yakukuta karibia kila tukio alilokuwa akifanya likiwa lipo kwenye kile kijitabu, mpaka



    tukio la mwisho ambalo lilikuwa ni kuonana na mimi kule Tanga, niliendelea kukikagua kile kitabu



    mwisho nilikuta na majina ya watu mbalimbali ambao walikuwa kwenyempango wake wa



    kuwaondoa duniani ambapo kulikuwa na mlolongo waa majina mbalimbali,nilishangaa baada ya



    kukta pia jina la marehemu bosi wangu huku jina la mwisho likiwa ni mkuu msaidizi wa idara ya



    mafunzo katika chuo cha mafunzo ya upolisi, mwili ulinisisimka sana kwani kwani kile kitabu



    kilikuwa kinaelezea kila mtu na sehemu anayoishi, vitu anavyopendelea na jinsi ya kumuondoa



    duniani, nilijikuta nashindwa kuendelea kukisoma kile kitabu na kukiweka pembeni kwani kilikuwa



    siri nyingi sana za yule mwanamke,

    Niliendelea na kukagua kwenye ile zipu ya pembeni ambapo pia nilikutana na  nailony eyes za bandia



    pamoja na sura tatu za bandia, nilikuta na hati ya kusafiria ikimuonyesha kama ni raia wa shelisheli



    huku pia kukiwa na funguo ambazo zilionyesha kwamba zilikuwa za nyumba yake kwani kwenye



    key holder yake zilikuwa zinaonyesha kila ufunguo na mlango wake, nilijikuta nafurahi huku nikijua



    sasa kumbe ile safari yangu haikuwa ya bure kabisa nikajikuta sasa naanza kuvipanga vile vitu vizuri



    huku nikiviamisha kutoka kwenye begi lake kwenda kwenye begi langu vile nilivyohisi ni vya maana.

    Nilimaliza na kuanza kulikung’uta lile begi Wakati naendelea na lile zoezi mara nikasikia kitu 



    kigumu kikianguka chini baada ya kukiangalia vizuri ilikuwa ni simu ya mkononi huku ikiwa



    imeviringishwa na pedi kiasi kwamba isingekuwa rahisi kuonekana, niliichukua ile simu  aina ya htc



    na kujaribisha kuiwasha lakini lionekana kutokuwa na chaji, nikaona sio mbaya nitatafuta chahi yake



    niichaji iliniweze kujua ni kipi kimehifadhiwa mule ndani, mpaka pale nilikuwa na matumani sana ya



    kuweza kumtambua yule mwanamke kutokana na vile baadhi ya vitu nilivyoweza kuvipata siku ilea



    ma kweli mtembea bure si sawa na mkaa bure.

                                               **********************************

    Nilifika Dar es salaam salama kabisa nilitoka mule uwanja wa ndege mpaka barabarani kisha



    nikapanda zangu daladala kama vile nilikuwa ni mtu niliyekuwa katika mihangaiko yangu ya kila siku



    nilishuka mnazi mmoja kisha na kuelekea nyumbani kwangu, ambapo nilikuta papo kama ilivyokuwa



    nimepaacha tofauti na mwanzo nilivyokuwa nimefikiria kwamba nitakuta pamekaguliwa ila haikuwa



    hivyo basi jambo kwanza niliwasha simu zangu na kangalia ni nani walikuwa wamenitafuta kwa



    kipindi kile chote ambacho sikuwepo, uliingia ujumbe wa meseji  mbalimbali huku pia na namba za



    simu ambazo zilionekana kunitafuta kwa ule muda ambao sikuwepo, nilijaribu kuzipia nyingi



    zileonyesha tu zilikuwa zikinijulisha kuhusu msiba wa mkuu wetu wa kazi, sikuzijali sana kwani kama



    taarifa nilikuwa tayari naijua hivyo basi sikuona kama ni kitu kigeni sana.

    Baada ya kumaliza kuosha mwili wangu naa kubadili nguo basi moja kwa moja nilitoka nje nikaingia



    mitaa ya nyuma ili nijirabu kutafuta chaji ya ile simu ili niweze kujua kulikuwa na nini niliingia



    maduka ya simu ya kariakoo muda ule ule wa jioni kwani navyojua mara nyingi yale maduka huwa



    ikifika jiona mara zote vitu huwa vinashuka bei kwani kuwa mwingine unakuta hajauza siku nzima



    hivyo hawezi kukataa pesa, basi baada ya kupita pita kwenye yale maduka mengi hayakuwa na chaji



    ya ile simu mpaka mwisho kabisa nilienda kuipata kwenye duka moja ambalo lilikuwa kwenye



    uchochoro mmoja uliokuwa ukitokea  mtaa wa Swahili nipo nilikuta mhindi mmoja akiwa nayo basi



    sikutaka sana kubishana nae sana kwenye bei nilimpatia pesa yake kisha nikaondoka zangu haraka



    sana kuludi nyumani kwani sikutaka nionekane sana kwani nilihofia kukutana na mtu yoyote ambaye



    nilikuwa namjua, basi baada yakuichaji ile simu na kuiwasha nikakkuta na password, nilijua tu yule



    mwanamke atakuwa amefanya vile ili isiwe rahisi watu kujua  je ni kipi kilikuwapo mule ndani, basi



    nika download programmer ya kiuwa ile password kwenye computer yangu ili niweze kujua mule



    ndani kulikuwa kuna nini niliiwasha kwa shauku kubwa sana ya kutaka kujua kilichokuwepo mule



    ndani, moja kwa moja niliaanza nu sehemu ya ujumbe mfupi ambapo pale sikuweza kukutana kitu



    chochote cha maana,sikupajali,nikaingia kwenye faili liliokuwa na picha na video, pale niliweza



    kukutana na picha za matukio mbali mbali pia niliweza kuuta baadhi ya picha za msichana mmoja



    akiwa amepiga kwenye nyumba moja hivi basi nilihisi moja kwa moja atakuwa ni yeye, niliachana na



    mahali pa picha nikijua kwa zile nilizokuwa nimeziona zinatosha kuweka kumtambua basi nikaamua



    kuhamia kwenye upande wa barua pepe kwenye ile simu yake, wakati nanaendelea na ile shughuli



    mara mlango wangu nikasikia ukigongwa kwa nguvu sana niliamka taraibu na kwenda kufuungua,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    mwili ulinyon’gonyea nilipokutana na baadhi ya wafanyakazi wenzangu wakiniambia ya kwamba



    nilikuwa natafutwa sana naitajika makao makuu kwa ajili ya mahojiano.

                           ****************************************

    Niliguna baada ya kusikia vile nilijua moja kwa  moja nilikuwa nahisiwa kuhusika na kifo cha



    mkubwa wangu wa kazi,niliwaomba dakika kadhaa niweze kujiandaa kwani nilikuwa nipo kifua wazi



    huku nikiwa nimevaa suruali ya kulalia tu, waliniambia hukuna tatizo, nilijua ingekuwa ngumu kwa



    mimi kunipeleka kama watu wengine kwani baadhi yao pale nilikuwa nawazidi cheo ofisini, basi



    niingia ndani na kujiandaa kisha nikabeba na baadhi ya vitu kwenye mkoba wangu na kutoka kwa



    ajiliya kuanza safari ya kuelekea makao makuu muda ule ule wa jioni kwa ajili ya mahojiano kama



    wao walivyokuwa wamenambia, niliinia kwenye ile discover ya polisi na kuanza kuelekea makao



    makuu.mule ndani ya gari wale wafanyakazi wenzangu walionekana kama ni watu waliokuwa



    wakinihofia sana kwani hata mazungumzo na mimi walkuwa wanazungumza kwa kusita sit asana



    hasa baadhi ya maswali ambayo nilikuwa nahitako ufafanuzi wao na ushirikiano wao. Nilijua tu



    itakuwa ni sumu iliyokuwa imesabazwa kuwa mimi nilikuwa nikishirikiana na yule muuaji katika



    kufanya yale matukio,kitu ambacho mimi kilinishangaza sana kwani sikuona ushirikiano baina ya



    mimi na yule mwanamkepia sikuona umuhimu wake ule wa kuuwa watu hovyo basi sikuwa na jinsi



    nianza kujiona kama mpweke Fulani hivi na mtu ambaye nilikuwa ninategwa na jamii bila ya sababu



    zisizo na maana, sikuwa na jinsi niona njia ya kulitatua lile tatizo ni moj tu nalo ni kuhakikisha yule



    mwanamke namkamata na kumfiksiha mbele yao hiyo ndio itakuwa njia yangu mimi kujosha kwani

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    tofauti na pale bado jamii na wafanyakazi wenzangu watahisi ni mimi.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog