Search This Blog

Sunday 19 June 2022

MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI - 3

 







    Simulizi : Mwanamke Mwenye Kovu Jeusi

    Sehemu Ya Tatu (3)



                                                 ****************************************

    Mida ya saa 9 tulianza kujiandaa kwa ajili ya ile oparesheni tunayoenda kuifanya, tulichukua bastola



    kila mtu yake huku tukiwa na risasi za ziada za kutosha kwa kila mmoja kisha tukachukua kamera,



    zile picha tulizozipata kutoka kwenye ile kamera, intelligence auto mobile call, kisha kila mmoja wetu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    akavaa na kifaa cha kuzuia risasi kifuani, halafu mkuu wetu wa kazi pamoja na Amina walivaa



    miwani ambazo zilikuwa zina uwezo wa kuvuta picha umbali wa mita mia mbili. Baada kujihakikisha



    tupo tayari tulichukua moja ya gari zilizopo pale kituoni ambayo ilikuwa na namba za kiraia ili isiwe



    rahisi kugundulika. Tulianza safari yetu taratibu huku tukiwa tunapiga story tu zingine dereva akiwa



    ni mmoja wa wafanyakazi wenzetu pale ofisini aliyejulikana kwa jina la Salimu, ni moja kati ya vijana



    ambao mkuu wetu aliwapenda sana kuwatumia katika shughuri ambazo nay eye alikuwa anahusika



    tulienda taratibu sana kama vile tukiwa hatuna haraka yoyote huku mkuu wetu akisema ya kwamba



    sipati picha jinsi vichwa vya habari kesho au keshokutwa vitakavyokuwa vinapamba na hili tukio,



    sijui wataandikaje MUUWAJI AKAMATWA,MUUWAJI AULIWA, POLISI WAFANIKIWA



    KUMZIBITI MUUWAJI HATARI, mimi nilikaa kimya tu na kumungalia maana nilijua wazi shughuli



    iliyopo mbele yetu si ndogo kutokana na jinsi Yule mwanamke alivyokuwa  mjanja na mwepesi wa



    kucheza na akili zetu pia nilihofia ya kwamba huwenda alikuwa na habari kuwa tulikuwa tunaenda



    hivyo lazima atakuwa amejipanga kwa mawili iwe kukabiliana na sisi au kukimbia, basi tulifika



    mpaka kwenye hilo eneo na kupaki gari yetu mbali kidogo ili isiwe rahisi kufanikiwa kuonekana



    kisha tukashuka na kupanga ni jinsi gani tutelekea lile eneo mkuu wetu wa kazi akasema eti mimi na



    Amina ndio tutangulie halafu wenyewe watakuja kwa nyuma huku wakiwa kama wanafanya kujenga



    duara Fulani,nilijua tu Yule mkuu alitaka kama ni jambo baya litukute sisi halafu yeye aepuke sikuwa



    na jinsi zaidi ya kutangulia kwani kwa sheria zetu za kazi huwezi kumbishia mkuu wako wa kazi kwa



    kila atakalolisema, basi tulitangulia  mimi na Amina huku mimi ndio nikiwa kwa mbele zaidi, wakati



    tunzazidi kukalibia lile eneo mara kwa mbali nikaona mwanamke akiwa amevalia suruali ya kaki na



    juu t-shirt ya rangi ya kijivu akitokea upande wa pili na kuelekea sehemu ambapo palikuwa kama



    kuna mwamba Fulani, Yule dada alikuwa makini sana huku akiangalia upande huu mara ule, alipofika



    pale  akabinua kama jiwe Fulani kisha akazama ndani,atakuwa ndio yeye leo mwisho wake umefika



    sijui anatoka wapi nilimwambia Amina huku nikikimbia kwa kasi sana mpaka pale, ambapo nilikuta



    lile jiwe likiwa limefunikwa sikupoteza muda pale pale akili ikanituma haraka haraka nikamjulisha



    mkuu wa kazi kupitia zile intelligence mobile phones nilizokuwa nimevaa kwamba Yule mwanamke



    tumeshamuona alipoingia hivyo basi aongeze kasi waje kwa maana anaweza kutuzidia, sikutaka hata



    kusikia jibu lake pale pale nilifungua lile jiwe huku Amina akiwa ameshafika lile eneo, nilihangaika



    kwa muda wa kama dakika 2 hivi ndipo nilipofanikiwa kulitoa lile jiwe sikuamini nilichokiona mule



    ndani kwani kulikuwa na ngazi zilizokuwa zinateremka kuelekea chini huku kukiwa na mwanga



    hafifu, niligeuka nyuma kumuangalia Amina vipi upo fiti nilimuuliza akanijibu kwa kuonyesha ishara



    ya dole gumba kwamba yupo sawa, niliangalia kwa mbali nikamuona mkuu wetu akiwa na Salimu



    nao wakija lile eneo pale pale nilimuonyesha ishara ya tuzame chini Amina, kisha mimi nikaanza



    kushuka zile ngazi.

                                     ******************************************

    Nilishuka huku nikiwa na tahadhari kubwa sana kwani sikujua Yule adui yetu alikuwa yupo mahala



    gani na pia alikuwa na silaha gani na isitoshe sikuwa na pafahamu vizuri mule pangoni,basi kila hatua



    niliyozidi kupiga na mwanga ndivyo ulizidi kuongezeka nilipiga hatua kushuka chini huku kwa nyuma



    nikimuona Amina akiwa ananifuata kwa ukaribu kabisa, pia nilisikia na vishindo vya kina inspekta



    Thomas na Yule Salim na wao ndio walikuwa wamefika na kuanza kushuka zile ngazi wakitufuata,



    nilishuka zile ngazi mpaka chini kabisa aithee lilikuwa ni handaki kubwa sana lile kwani kumaliza tu



    zile ngazi nilitumia zaidi ya dakika tano nilipofika chini kabisa sikuamini kwani nilijihisi kama vile



    nilikuwa nipo sebuleni kwa mtu palikuwa mahali pa pana kabisa pale huku kukiwa na baadhi ya vitu



    palikuwa pamechimbwa vizuri kiasi kwamba sikuweza kudhania kama nilikuwa pangoni, palikuwa na



    vitu muhimu ambavyo huwa vinakuwepo sebuleni kama makochi, television meza na kadhalika yani



    kwa ufupi ilikuwa ni sebule iliyokuwa imekamilika,sikutaka kuendelea kushangaa pale sebuleni



    kwani nilijua linaweza kuwa kosa na Yule adui akatukuta pale na kututeketeza wote kwani tulikuwa



    tupo kwenye himaya yake hivyo hatukujua alikuwa yupo upande gani.

    Nilimsubili Amina na yeye akafika pale kisha na mkuu wetu akafika tukaangalia kisha tukapeana



    ishara tutawanyike kwenye ile nyumba iliyokuwa chini ya ardhi tulitawanyika sisi watatu huku mkuu



    wetu wa kazi yeye akiwa amebakia pale  sebuleni, basi mimi nilielekea upande wa kushoto ambapo



    nilikutana na kama chumba Fulani hivi nilipoingia nilikutana na geti la chuma ila likiwa wazi ambapo



    ilinibidi niingie kwa uangalifu sana, baada ya kuchungulia ndipo nilipogundua ya kwamba mule ndipo



    palikuwa selo ya Yule mwanamke kwani kulikuwa na majeraha ya damu damu sana mule huku



    kukiwa na vifaa vya kutesea watu kama shoti za umeme na vingine, nilizidi kushangaa ila sikutaka



    kupoteza muda tena nikachumpa upande wa pili nikajikuta nimetokea mahali ambapo nilihisi ndipo



    palikuwa chumbani  kwake kwa maana palikuwa pazuri ajabu huku kukiwa na mapambo na vifaa



    vya kisasa kabisa kama computer, air condition na vingine, nilijiuliza mule chini umeme Yule



    mwanamke aliupata wapi? Kwa maana palikuwa kama mchana, nilijaribu kupaangalia pia



    nikajihakikisha hapakuwa na mtu nikatoka haraka nikashika korido nyingine nikakuta mahali ni kama



    pa wazi Fulani hivi huku pakiwa na njia kubwa iliyokuwa ikielekea mahali ambapo palikuwa na



    mwanga zaidi nilizidi kuufuata ule mwanga mwisho nilijikuta nimetokea sehemu ambapo palikuwa na



    maji maji yaliyokuwa yamejenga kama mkondo Fulani hivi ukiwa umeingia kwenye kama mwamba



    Fulani pembezoni mwa bahari, wakati natoka ili niweze kupakagua vizuri nikaona boat moja ndogo



    ikitoka pale na kuelekea baharini umbali wa kama mita mia mbili toka nilipokuwa nimesimama,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    mungu wangu atakuwa ndio yeye huyu ametukimbia, nilijikuta nasema kwa sauti ya juu huku



    nikilaani, kugeuka kwa nyuma nikamuona Salimu na Amina nao kumbe walikuwa wameshafika pale,



    ndipo Salim alipoanza kutuambia ya kwamba yeye ndio alikuwa akimfukuzia alimuona mara ya



    kwanza kwa mbele kwenye kona moja akitokomea huku akiwa amebeba mkoba Fulani hivi na begi



    ambapo begi lilimzidi uzito hivyo basi aliliacha chini alimkimbiza  kwa kuhusi kwamba atamkuta,



    hatukuwa na jinsi tena ikatubidi tuanze kuludi sebuleni tumsikilize mkuu wetu atasemaje, tuliludi



    huku tukiwa tumelipitia lile begi alilokuwa amelidondosha na kisha kuludi pale sebuleni, kwa kweli



    wote tulishangaa jinsi ile nyumba ya chini ya mwanga iliyokuwa kwani kama mtu ungebebwa na



    kuwekwa tu pale katu usingehisi chochote kama upo kwenye nyumba iliyopo chini ya ardhi. Tuliludi



    pale sebuleni ambapo tulimkuta mkuu wetu yeye akiwa amekaa hana hata wasiwasi, tulimueleza ya



    kwamba tayari tumeshamkosa, akasema sawa sasa inabidi tufanye upekuzi mule ndani ili kujua kama



    kuna vitu vyoyote ili tuweze kuondoka navyo tulisimama na kuanza kuelekea chumbani kwake



    kwanza wakati tunakaribia kuingia mule chumbani mara umeme ukakatika ghafla, mungu wangu



    Amina alijihisi woga akanishika mkono na kuning’ang’ania

    mule ndani palikuwa giza sana kiasi kwamba hatukuweza hata kuonana sisi kwa sisi na hatukuwa na



    mwelekeo wowote ule tena ilitubidi tusimamekwa dakika kadhaa ili tuweze kulizoea kwanza giza



    kisha ndipo tujue la kufanya, akili ikanicheza haraka haraka nikatoa simu yangu mfukoni ambayo



    ilikuwa na tochi kwa mbele nikaiwasha ile tochi ili angalau tuweze kufanikiwa kutoka mule ndani,



    ilibidi tuailishe kwanza zoezi la kuendelea kusachi mule ndani tukaona njia sahihi ni kutoka nje



    kwanza kwani hatukujua Yule mtu alikuwa amezima vipi ule umeme na isitoshe pia ingewezekana



    akawa ametegehsa hata mabomu mwisho wake tukajikuta wote tunalipuka mule  tulianza kutoka nje



    kwa tahadhari kubwa sana, tuliporudi mpaka pale sebuleni mara tukasikia sauti ya mtu akizungumza



    huku ikiwa na kama mwangwi Fulani hivi, mmeanzisha mapambano sasa sioni hata mmoja wenu



    ambaye atakaepona sasa, tuligeuka ili kungalia wapi sauti ilikuwa inatokea mara simu yangu ilipigwa



    na kitu ikadondoka chini, sikuaimi kile kitendo kwani kama ilikuwa risasi yenyewe ilitoka bila kelele



    yoyote na mlengaji akionekana akiwa na shabaha sana,paligeuka tena mule ndani kuwa giza huku



    wote tukiwa tumekumbatiana kwa hofu, nilianza kusikia sauti ya mkuu wetu wa kazi kwa chini chini



    akiboboja, nilimfunga mdomo asije kuharibu kila kitu, Yule mwanamke alizidi kuzungumza huku sauti



    yake ikiwa kama vile inajirudua rudia “haya kama nyie wanaume kweli tokeni basi tuone leo mwisho



    wenu umefika” nilizidi kuchanganyikiwa kiukweli toka nizaliwe sikuwahi kukutana na wakati mgumu



    kama siku ile, ilibidi tuwe wapole tu pale kwanza

     nilishangaa huyu mwanamkwe si ameondoka na boat sasa ilekuaje tena awepo mule mule ndani



    kipindi kile?na kwa nini alihindwa kutuuwa kama kweli alikuwa anatuona Au huyu mwanamke ni jini



    nini? Halafu tutachukuaje hatua wakati yeye hatujui amejificha upande gani kwani yeye tu ndio



    nilihisi alikuwa anatuona wakati sisi hatukujua alikuwa sehemu gani. Tulikaa pale kwa muda wa zaidi



    ya saa tano huku tukiwa hatuna jinsi ya kufanya kwa kuhofia usalama wetu,mpaka baadaye sana



    sikumbuki ilikuwa ni saa ngapi ila nahisi ilikuwa ni usiku sana ndipo simu ya mkuu wetu ilipoita na



    kuitoa mfukoni tena bila woga na kuanza kuzungumza nahisi ilikuwa ni simu ya mke wake kutokana



    na mazungumzo waliokuwa wakizungumza huku akiwa analalamika mbona alikuwa kimya sana siku



    nzima bila ya kumpa taarifa yoyote , baada ya kumaliza kuzungumza na ile simu mkuu wetu aliwasha



    tochi ya simu yake bila woga  alimulika chini pale tulipokuwa tumesimama kwa kuhofia kumulika



    pengine  kwa kuhisi Yule mwanaharamu angeweza hata kutupa adhabu yoyote ile au kutuuwa pia



    kwa maana Yule mwanamke ki ukweli alikuwa katiri sana,kwa pale chini alipomulika niliweza kuiona



    simu yangu nikainama na kuichukua wakati naichukua ndipo kwa pembeni yake niliweza kukiona



    kama kichuma Fulani chembamba kilichoipiga ile simu mpaka ikaanguka, mimi nilijua ni risasi kumbe



    ilikuwa tofauti  niliwasha simu yangu na kumulika juu kwa woga woga ndipo nilipoona kumbe kule



    juu kulikuwa na vyuma vingi sana hivyo basi kile kipisi kitakuwa kilikuwa kimeanguka tu  pia



    niliweza kuona vi spika vidogo vikiwa vimewekwa kwenye kona juu kabisa ambavyo ndivyo



    nilivyokuja kugundua alikuwa anatumia kutolea ile sauti

    nilipata moyo wa ujasiri ghafla tena kwani nilijua sasa sio risasi kama nilivyokuwa nimedhania



    mwanzo, niliwambia wenzangu kwa sauti ya kuwanong’oneza ya kwamba inatubidi tutoke mule bila



    kuhofia chochote liwalo na liwe,kwani Yule mwanmke alikuwa natuchezea akili tu kwa kutumia



    teknolojia hata hakuwepo tulikubalina wote kwa pamoja kisha tukaanza kutafuta njia yakutokea kwa



    kutumia tochi ya simu yangu na ya mkuu tulifika mpaka pale sebuleni kisha tukaziona zile ngazi za



    kupanda kutoka, pale mwanga hafifu wa nje tulianza kuuona kwani muda ule ilikuwa ni usiku sana



    hivyo isingewezekana kuwa na mwanga sana.

                                  **********************************

    Tulifanikiwa kutoka nje ilikuwa yapata kama mida ya saa sita hivi usiku pale nje kando kando mwa



    bahari palikuwa pametulia sana hakukuwa na pirika pirika zaidi ya kuona kwa mbali boti za wavuvi



    zikieleka kando kando mwa bahari baada ya kumaliza shughuli za uvuvi, tulijiangalia kama wote



    tulikuwa tupo salama, tulijihakikisha wote tupo salama huku Salim akiwa amefanikiwa kutoka na lile



    begi liliokuwa na vitu mbalimbali vya mwanamke mwenye kovu jeusi,tulielekea hadi mahala



    tulipokuwa tumepaki usafiri wetu tuliokuwa tumekuja nao,tulilikuta gari likiwa vile vile kama



    tulivyokuwa tumeliacha.

                                             ****************************

    Nilifika kwangu pakiwa pamepambazuka kabisa mida ya saa kumi na moja hivi, basi kwa kuwa



    nilikuwa nimechoka  na huku usingizi ukiwa umenishika sana niliingia ndani moja kwa moja



    chumbani na kulala,bila hata ya kubadili nguo nilizokuwa nimezivaa.

    Nilikuja kushituka mida ya saa nne asubuhi baada ya simu yangu kuita ambapo baada ya kuangalia



    nilikuta kuna missed call zaidi ya tano, niliangalia simu ilikuwa inatoka kwa Gerald, nilimpigia



    ambapo aliniambia Yule mwanamke mwenye kovu jeusi jana usiku alimpigia simu na kumuambia



    ajiandae kwani zamu yake ilikuwa imefika kisha baada ya yeye nitafuata mimi, nilicheka kidogo



    kisha nikamuambia “sikiliza ndugu yangu huyu mwanamke anatapatapa tu hana lolote kwani mpaka



    sasa tumeshafanikiwa kuzibiti uwezo wake wa kupata taarifa zetu kitu ambacho ni kikubwa na kizuri



    zaidi halafu pia tumefanikiwa kuyagundua makazi yake ya ajabu yaliyo kwenye pango” nilizidi



    kumuhadithia jinsi usiku wa jana yake ilivyokuwa na kila kitu mpaka tulivyofanikiwa kutoka ndipo



    Gerald nay eye pia akanambia ya kwamba basi Yule mwanamke atakuwa ni hatari sana kayajuaje



    yale makazi kwani kwa upeo wake na kumbukumbu yake ndogo ni kwamba ile ilikuwa ni moja ya

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    sehemu ambazo zilikuwa makazi ya waarabu enzi za ukoloni ambapo wakoloni walitumia kama



    sehemu za kujificha na ikiwezekana kutoroka pindi mambo yalivyokuwa hovyo, kisha Gerald



    akanambia ya kwamba mbona hata michoro ya mahala pale yapo mule ofisini na pale panajulikana



    kama pameshafungwa na Yule mwanamke pale sijui alipajuaje.tuliongea mengi huku akiniambia ya



    kwamba mkono wake ulikuwa ukiendelea vizuri nilimwambia ni vizuri basin a kama nikipata muda



    kesho jioni yake nitaenda kumsalimia.

    Nilijiinua pale kitandani kisha kuelekea jikoni kwa ajili ya kupasha maziwa kidogo ninywe kisha



    niendelee na majukumu mengine kabla ya kujiandaa ili nielekee kazini maana tulipanga tukutane



    mida ya saa tisa,

    Wakati naingia jikoni chini ya mlango wangu niliona kuna vitu vilikuwa vimetegeshwa huku vikiwa



    vimefunikwa na karpet niliviangalia ndipo nilipokuja kugundua kuwa vilikuwa ni vinasa sauti



    nilivichomoa pale nikaviweka sebuleni kwa minajri ya kwamba nitavipitia niende navyo ofisini kwani



    nilijua ya kwamba vilikuwa tu vimewekwa na Yule mwanamke mwenye kovu jeusi na swali langu



    kubwa lilikuwa ni wapi Yule mwanamke alikuwa anavitoa vile vifaa kwani vingine kwa jinsi



    vilivyokuwa advanced vingine teknolojia yake hata hapa nchini ilikuwa haijafika kweli mtu



    tuliyekuwa tunapambana naye hakuwa mtu wa mchezo hata kidogo.

                                       *********************************

    Tulikuwa kwenye ofisi ya mkuu wetu inspekta Thomas tukiwa wanne mimi inspekta Thomas Amina



    na Salim, mkuu wetu inspekta Thomas alipandisha juu lile begi tulilolitoa janausiku  kule kwenye ile



    nyumba ya maficho ya Yule mwanaharamu alianza kulifungualile begi na kutoa vitu vilivyomo mule



    ndani, alitoa pesa  ambazo zilikuwa kwa juu juu tu pale ndani ya begi ambazo zilikuwa ni pesa za



    kimarekani zaidi ya dola elfu mbili kisha kwa chini kulikuwa na sura za bandia zaidi ya kumi na mbili



    huku tatu zikiwa ni za kike kisha kulikuwa na kopo Fulani ambali baada ya kulisomoa tuligundua



    kulikuwa na sumu hatari sana, nahisi ndiyo aliyotumia kumchoma nayo Gerald kule makaburini,pia



    kulikuwa na note book moja ambayo mkuu aliitoa alipojaribu kuiwasha kulikuwa na password, humu



    kuna siri kubwa sana inaonekana haiwezekani ifungwa na password ambazo zipo moja kwa moja



    kwenye system, alilalama bosi, huku akimsogezea Salimu ajalibu kuifungua, pia tulikuta palikuwa na



    passport sita mbili zikiwa za Tanzania huku zikiwa na sura tofauti, na majina tofatu, moja ikiwa ya



    Kenya, moja ya Africa kusini, moja ikimuonyesha kama ni raia wa visiwa vya shelisheli humu ya



    mwisho ikimuonmyesha kama ni raia wa brazil,mh mh mh aithe huyu mwanamke ni hatari yani hivi



    vitu vyote jamani lakini mwisho wake umeshafika,alizungumz Amina huku mwili ukiwa



    unamsisimka, chini kabisa ya lile begi kulikuwa na faili ambalo ndani yake kulikuwa na makaratasi



    mengi mengi sana, nililichukua na kuanza kuchambua zile karatasi nilikuta mkataba wa Yule



    mwanamke wa nyumba ya kupanga nchini Victoria sherisheri, ambapo palionekana ndio palikuwa ni



    makazi yake, hapo nilivuta picha na kukumbuka usiku ule aliotukimbia pale na ile boat nahisi ndio



    alikuwa anaelekea huko, pia nilikuta mkataba mwingine ukimuonyesha kama mpangaji kwenye



    nyumba moja iliyokuwepo mikocheni,pia kulikuwa na karatsi ambazo zilionyesha akiwa na akounti



    katika benki ya taifa ya biashara, baada ya kuona karatasi hii pia nikavuta picha za Yule mkaa



    marehemu ambaye dada yake ni mfanyakazi wa benki ya biashara pale makuu Zainabu,tena



    nilishituka sana kwani mara ya mwisho taarifa nilizozipata ni kwamba Yule dada alikuwa hoi hospitali



    ya taifa muhimbili akiumwa sana, mungu wangu nikitoka hapa leo itabidi nijaribu kwenda kumuona



    huyu dada sio vizuri nahisi pia atakuwa na siri nzito sana kuhusu huyu mwanamke,nilijikuta najisema



    mwenyewe huku tukiendekea kuchambua vitu mbalimbali ndani ya lilebegi,

    kwenye  zipu ya pembeni ya lile begi Salim alikuta kuna simu aina ya nokia3350 ambapo baada ya



    kuiwasha ndipo alipogundua ya kwamba hakukuwa na laini ile wenye ile sumu kulikuwa na meseji



    mbalimbali zingine zikioneka  zimetoka nje ya nchi na kilichotushangaza zaidi na kutuchanganya



    kuna baadhi ya meseji tulizikuta mule zilionyesha kwamba Yule mwanamke alikuwa kama anapewa



    maeleko tu ya kufanya kwa malipo huku mtu aliyekuwa akimuelekeza ikionekana kama alikuwa ni



    mtu mmoja mkubwa serikalini kwani alimuambia asiwe na tatizo lolote likitokea yeye atamsaidia,



    wote tulishangaa, mkuu wetu alichukua simu yake na kujaribu kuipiga ile namba ya simu lakini



    haikuita aliambiwa namba aliyopiga haikuwepo, tuliona jambo la msingi ni kuikaihifadhi kisha



    tutaenda tume ya mawasiliano kwenda kuulizia wataweza kutusaidia zaidi,tulichambua sana mule na



    kuhakikisha kila kilichokuwepo tumekiona ilipofika mida ya saa kumi na moja mkuu wetu alisema



    twende tukale kisha mapema kisha tukiludi tumalizie ile kazi kwani yeye alikuwa na njaa sana mimi



    nilimjulisha ya kwamba nilikuwa nimeshiba kwani nilikuwa nimetoka kula si muda kabala sijaja



    kazini lakini mkuu wetu akasema si shida twende nitakunywa hata kinywaji chochote kwani sio



    vizuri nikibakia peke yangu mule ndani, katika kazi kuna muda wa kupumzika alinambia, basi sikuwa



    na kipingamizi zaidi kwa maana ningeonekana kama vile nimekataa ofa yake basi tulitoka kuelekea



    kwenye mgahawa ambao haukuwa mbali sana  pale ofisini huku vile vitu tukiwa tumeviacha mule



    ofisini kwa mkuu wetu.

                                               *************************************

    Tuliporudi kutoka kula ilitushangaza sana baada ya kukuta ofisi ya mkuu wetu ikiwa wazi wakati



    tuliacha pakiwa pamefungwa,baada ya kuingia mule ofisini mule mungu wangu hatukuamini baada



    ya kukuta vile vitu vyote vikiwa havipo…..!!!

                                                    *****************

    Bosi wetu alihamaki kukuta mule ofisini kwake palikuwa peupe ilihali mlango tuliacha akiwa



    ameufunga, huku mlango ukiwa umeludishiwa vile vile, tulihamaki sana kutokana na ile hali

    “Sasa huu utakuwa ni utoto sasa na haya ni zaidi ya matusi” alisema bosi kuhu akiwa amejaa



    ghazabu sana ilibidi tuanze kumshusha zile ghazabu ili tuanza kufuatilia ili kujua ni kipi kilichojiri,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    baada ya mkuu wetu kuwa mpole nilitoka nje na kumuita dada aliyekuwa pale kaunta ili kumchuma



    maelezo atuambie ni kipi kilichojiri,alikuja huku akionyesha wazi hakuna alilokuwa analifahamu,



    baada ya kuingia mule ndani mkuu alianza kumuuliza ya kwamba ni nani aliyeingia mule ndani, kwa



    kipindi kile kifupi ambacho sisi tulinda kula? Alionekana kama ni mtu aliyekwa akijaribu kuvuta



    kumbukumbu kisha akatuambia ya kwamba alipita pale mapokezi mdada ambaye alikuwa amevalia



    sare za kiaskari, na sura yake sio ngeni sana machoni pake, lakini hakumbuki ni nani kwa maana



    muda ule kulikuwa na askari wengi sana waliokuwa wamekuja kutoka depo, na muda ule walikuwa



    tayari wameshatawayika kwenda kwenye ma lindo sehemu mbalimbali baada ya kumaliza gwaride la



    saa 12 pale ofisini, tulimsikiliza kwa makini kisha mkuu wetu akampigia simu mkuu msaidizi wa kituo



    huku akimuomba amletee majina ya watu wote waliohudhuria paredi la saa 12 alikuwa na shida nayo



    sana,basi Yule OCS hakusita alikuja nayo mle ofisini kuhu akionyesha ya kwamba ndio alikuwa



    akiondoka kazini, aliniuliza kama kuna tatizo lolote,mkuu wetu alimjibu ndio kuna vitu vimepotea



    mule ofisini kwake katika muda mchache ambao tulikuwa tumetoka kwenda kula sasa kutokana na



    taarifa za askari aliyepo mapokezi anadai ya kwamba kuna mwanamke ndio alikuja humu kati ya



    wale waliokuwa kwenye paredi lile la jioni.

    Basi walikubaliana ya kwamba itabidi kesho asubuhi na mapema watakapoludi kurepoti kabla ya



    kwenda kwenye makazi yao basi lifanyike paredi la ugunduzi ambalo latafanywa ka kusaidiwa na



    Yule mwanamke wa pale mapokezi, tulitawanyika pale huku mkuu wangu akinisisitizia mimi kesho



    niwahi mapema sana kwa sababu toka pale mnazi mmoja nilipokuwa nimepanga mpaka stesheni



    hapakuwa mbali sana hivyo itanibidi niwahi ili kufanya lile zoezi. Sikuwa na kipingamizi katika lile



    tulikubaliana nao kisha kila mmoja wetu akitawanyika

                                   **********************************

    Nilifika kwangu usiku ule mida ya saa mbili usiku baada ya kuoga nilivaa nguo mahususi kwa ajili ya



    kulalia kisha nikwa nimekaa naangalia taarifa ya habari, mara simu yangu ikaita alikuwa ni Amina



    akinijulisha ya kwamba alikua anaomba kama inawezekana nimsaidie kumpeleka kwake sinza mori



    kwani alikuwa na vitu vingi halafu alikuwa amekaa zaidi ya saa toka nilipomuacha pale stendeni ya



    vidaladala stesheni bila ya gari yoyote kuja, niliona si mbaya kwani Amina alikuwa ni mmoja ya



    wadada niliokuwa nao karibu sana pale kazini yeye pamoja na Jamila ambaye Jamila ni mdada



    niliyekuwa nampenda sana toka nilipomjua kwani alikuwa ni mkimya sana huku akiwa ni mtu



    asiyekuwa na makuu sema kwa kipindi kila Jamila alikuwa ameenda nchini marekani kwenye course



    ya social intelligence kwa takiribani miezi mitatu, muda mwingine nilikuwa namkumbuka sana Jamila



    kwani achilia mbali na kumpenda ila alikuwa ni mchapakazi na huku akili yake ikiwa nyepesi sana



    katika kuchambua mambo.

    Nilimkuta pale stesheni Amina na kumchukua na gari yangu ili kumuwahisha kwakeambapo alikuwa



    akiishi peke yake kwa maana nay eye pia aliniambia atajitahidi kesho kuwahi hata kwa kutumia taxi



    wani alikuwa hajafanikiwa kununua gari, ili tuje tusaidiane katika lile paredi la utambuzi, basi



    tulienda taratibu kutakana na foleni huku tukipiga story mbali mbali tulifika kwake ilikuwa ni mida



    ya saa 4 hivi usiku basi wakati tumepaki gari nje tuliona taa za ndani kwake zikiwa zimeweka,Amina



    alishituka na kuniambia ya kwamba yeye pindi alipoondoka alicha taa amezizima, wakati tunajishauri



    mara kwa ndani kupitia dirishani tuliweza kumuona mtu kwa mbali ambaye baada ya kuona gari



    imesimama nay eye alichokifanya ni kuzima taa mule ndani hivyo basi tukakosa ujanja wa kuingia



    ndani kwa maana tusingeweza kuingia ndani wakati mtu Yule amezima taa na hatukujua ni nani na



    alikuwa na silaha gani.

    Tulishauriana pale huku tukiwa hatuna la kufanya hatukutaka kuita watu kwanza tulijua tu atakuwa



    ni mwanamke mwenye kovu jeusi atakuwa ameingia kutegesha vinasa sauti vyake au kufanya



    upekuzi kama ilivyokuwa ada yake. Lakini kitu kilichotushangaza ni jinsi alivyoweza kucheza na



    muda kwani mara zote kila alipoenda sisi hatukuwepo sasa tulijiuliza kwa siku ile alijuje kama Amina



    atachelewa kazini. Tulijadiliana pale kwa zaidi ya  saa zima kwani yle mtu alikuwa kama akitufanya



    watoto akiwasha simu na kuzima mara ya chumbani mara ya jikoni mara ya sebuleni ili mradi tu



    kutuchanganya kisha nikamwambia Amina liwalo na liwe  nikamuomba bastola yake kisha



    nikachungua fungua na kuanza kuingia mule ndani, nilifungua mlango na kuwasha taa pale sebuleni



    sikuweza kumuona mtu, palikuwa pametulia tulii, nilijaribu kutazama tena kwenye korido sikuweza



    kumuona mtu, nilielekea jikoni wakati natokea tu nikaona mlango wa kule jikoni uliokuwa ukitoka



    nje pia ukifunguliwa na mtu akitoka kwa kasi ya ajabu akikimbia kulekea barabarani basin a mimi



    sikutaka kupoteza muda nilitoka nje ambapo aliniona nikija kwa kasi kumbe alikuwa makuja na piki



    piki akawa ameipaki nyuma ya ile nyumba aliponiona nakuija kwa kasi alishindwa hata kuipanda ile



    pikipiki na kuanza kukimbia kwa miguu akielekea barabarani, sikutaka kumuacha nilianza na mimi



    kumkimbiza huku nikimjulisha Amina kwa sauti sina hakuka kama alinisikia nilimkimbiza alishika



    barabara akawa kama anaelekea sinza parestina alikuwa na mbio za ajabu zijawahi kuona, nilizidi



    kumfuata kwa kasi ya ajabu huku bastola ikiwa tayari tayari mkononi na kwa muda mule barabara



    ilikuwa imeshakuwa nyeupe kwani watu wengi walikuwa maeshalala ilikuwasaa sita hivi inaelekea



    saa saba usiku, basi Yule mtu alipofika sinza makaburini alisimama kidogo na kuningalia kama



    nilikuwa bado namfuata aliponiona nilikuwa bado namfuata akakimbilia ndani ya makaburi, namimi



    sikutaka kujifikiria nilipofika pale na mimi nikaingia mule makaburini, sikuweza kumuona tena mule



    kila upande nilipoangalia hakuonekana, basi nikasimama mule makaburini kwa muda wa kama



    sekunde tano huku mapigo ya moyo yakianza kuongezeka nikasogea mbele kama hatua nane hivi



    palikuwa na kaburi kubwa ambalo lilikuwa limejengwa kifahari sana na likiwa limeinuka juu ambalo

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    lilikuwa chini ya mti mkubwa wa mkuyu, nilimuangalia kama alikwa labda amejificha pale mbele ya



    lile kaburi lakini sikumuona, nilijikuta nakata tamaa na kuona potelea mbali haikuwa siku yake



    kumkamata basi nikageuka ili niludi kwa Amina niende zangu nikalale,mungu wangu kila nilipojaribu



    kupiga hatua nilihisi kama kuna kitu kinanivuta kwa nyuma,nilisimama nikajua kama ni Yule mtu basi



    atazungumza kitu au atafanya jambo lolote,nilisubili kwa muda wa zaidi ya dakika 5 bila kusikia wala



    kuhisi lolote nikajaribu kupiga hatua tena niondoke lakini wapi nilijikuta navutwa tena. Mwili ulianza



    kusisimka kwa maana sehemu yenyewe niliyokuwa ni makaburini palikuwa panatisha na ni usiku



    nilianza kujisemesha pale ili kama ni Yule mtu basi anijibu lakini wapi palikuwa kimya sana,huku



    upepo tu ukivuma kwa mbali,nilijaribu tena kupiga hatua kusogea mbele lakini wapi bado nilivutwa



    hapo hapo nikajua mwisho wangu umefika tayari…..!!

                              *******************************

    Nilijitahidi kukauka pale kwa takribani robo saa bila kufanya lolote ili niweze kuona kipi kingefuata



    lakini hali ilizidi kuwa tofauti kwani muda ulivyokuwa unaenda ndivyo na mimi woga ulivyozidi



    kuniingia, “sasa si unidfanye lolote wewe uliyenishika jamani mbona wanifanyia hivyo” nilijikuta



    nazungumza kwa sauti iliyojaa utetemeshi sana, kila nilivyojaribu kuongea kwa nyuma nilihisi kama



    sauti ya viumbe wa ajabu amabo walikuwa wanazungumza ,mungu wangu haya yatakuwa mashetani



    sasa yamenishika sio bure, nilijikuta najisema mwenyewe moyoni, haiwezekani akawa mtu haya



    yatakuwa ni mashetani tu ni hivi nimekuja hapa makaburini mida hii ni saa saba inanenda saa 8



    mungu wangu au itakuwa ni mizimu tu ya mtu mmoja wapo hapa makaburini, sasa sijui nitafanyaje



    mimi hapa?

    mara kwa mbali sana niliweza kuona watu wakiingia mule makaburini mvulana mmoja na msichana



    wakiwa wanakuja mitaa ile niliokuwa mimi nilijua tu atakuwa jamaa ameopoa mwanamke anayejiuza



    mitaa ile kwani ile ni moja ya sehemu ambapo huwa kuna wasichana wengi wanaofanya biashara ya



    kuuza mili yao,pale pale nikajua itakuwa ni pona yangu labda ile mizimu iliyokuwa imenishikiria



    nyuma itaniachia,nikaanza kunyoosha mkono juu ili wanione, mungu wangu baada ya kuniona



    walikimbia sana huku wakipiga kelele basi namimi nilizidi kushituka huku mapigo yangu ya moyo



    yakizidi kwenda mbio, ooh watakuwa wameyaona haya mamizimu yaliyonishika huku nyuma,



    mungu wangu leo nimepatikana sio bure, au huyu mwanamke mwenye kovu jeusi atakuwa ni mzimu



    nini? Kwanini alikimbilia humu? Na kwa nini namtafuta haonekani jamani,

    ilinibidi nisimame pale potelea mbali litakalokuja kutokea na litokee pia huku muda ukizidi kwenda



    kila nilipotaka kugeuka nyuma moyo ulikuwa unasita kwa kufohia sura yangu kukuta uso kwa uso na



    mizimu, kwani kwa mila za kwetu mtu ukiona sura za mizimu huo ni mkosi kubwa sana katika



    maisha. Nilikaa pale huku usingizi ukiwa unaninyemelea sana muda mwingine nilikuwa najihisi



    kusinzia mara nashituka na kuendelea kusimama sawa.

    Ilipofika mida ya saa 9 hivi nilijaribu kugeuka nyuma kwa minajili ya kwamba litakalokuwa na liwe



    niligeuza shingo yangu pole pole sana kuangalia kule nyume kulipokuwa na lile li mti la mbuyu



    likubwa bahati nzuri sikuweza kuona kitu chochote, nikageuka mbele na kutaka kuondoka sasa lakini



    wapi bado nilijikuta nikiwa navutwa pale pale machozi yalianza kunitoka taratibu na kujua mwisho



    wangu ulikuwa umefika tayari maana ile mizimu itakuwa imekasirika kwa mimi kugekuka nyuma na



    kuangalia sura zao, niliendelea pale kusimama nakumbuka sikuwahi kusimama kwa kiasi kile zaidi ya



    miaka mitano toka nilipotoka kambini, kwa siku ile kwangu ilikuwa ni azabu tosha huku nikijiapiza



    kabisa ya kwamba kama nikiweza kunusurika pale itanibidi niombe kujitoa katika kufuatilia ile kesi



    kwani majaribu niliyokuwa nakutana nayo na jinsi utata uliokuwa ikijitokeza kila siku ulikuwa



    unanchanganya sana.

    Nilisimama pale mpaka mida ya saa kumi na moja na robo hivi bila kukosea ndipo moyo wa jasiri



    ulipoanza kuniludia tena baada ya kuona tayari pameanza kukucha na jua kutokeza ikanibidi nigeuke



    nyuma tena ili kuiangalia ile mizimu ikiwezekana niiombe msamaha kwani muda waliokuwa



    wameniweka pale ilikuwa ni adhabu tosha sana upande wangu basi niligeuka  taratibu tena



    nyuma,sikuweza hata kufanikiwa kuona jambo lolote wala mtu yoyte kula ntuma zaidi ya ndege tu



    waliokuwa wapo juu ya ule mti wa mbuyu huku wakiwa wanalia lia kuashiria ya kwamba palikuwa



    pamekucha sasa,nilishusha pumzi chini kisha na mapigo yangu ya moyo yakaanza kuludi sawa,kwa



    maana wakati nageuka tena mapigo yalikuwa yanenda kasi sana.

    Basi baada ya kujihakikishia pale hapakuwa na kitu chochote wala sura ya mzimuwala umbo kwa



    mara ya pili tena  nikajaribu kutaka kuondoka tena lakini bado nikajihisi navutwa,kuangalia ndipo



    nilipokuja kugundua ya kwamba kumbe kuna kipande cha nondo kilichokuwa kimetokeza kwa



    pembeni baada ya kaburi kujengewa kumbe ndicho kilikuwa kimechoma kwenye ile suruali yangu ya



    kulalia kwa chini na kusababisha nijihisi kama vile nimeshikwa navutwa.nilijichoma pale huku



    nikijilaumu kwa woga wangu wote umenifanya nilale makaburini bila ya sababu za msingi.

    Niltoka pale makaburini haraka haraka ilikuwa yapata kama mida ya saa kumi na moja hivi



    nikaelekea moja kwa moja mpaka nyumabani kwa Amina ambapo nilikuta akiwa na wasiwasi sana



    hhuku akinieleza muda wote ule alikuwa hana amani moyoni kwani ilimbidi ampigie mpaka mkuu



    wetu simu kumjulisha kuhusu lile tukio, sikutaka kukaa sana kwani nilikuwa na usingizi sana



    kutokana na kulala makaburini kwa kujitakia, kisha nilimuhadithia tukio zima kwa nini ilitokea



    mpaka mimi nikalakla mule makaburini, alinionea huruma sana huku akiniomba nimsamehe kwani



    bila ya yeye kumsindikiza kwake haya yote yasingetokea.

    Nilimuambia hakuna shida kwani ile ilikuwa ni kama ajali kazini kisha nikamsisitizia tuondoke naye



    muda ule ili mimi niende kwangu nikalale yeye aelekee kazini kwa ajili ya kwenda kufanya lile zoezi



    la utambuzi kwani jana amri ilitolewa watu wasitawanyike mpaka lilezoezi liwe limekamilika. Hivyo



    basi nilimsisitiza akalifanye lile zoezi kwa uangalifa sana akishirikiana na Yule dada ambaye alikuwa

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    mapokezi pia pale pale tilimpigia simu mkuu wetu na kamanda wa mkoa wa kipolisi wa kinondoni



    kumuelezea hali halisi hivyo kama kuna hatua walikuwa wamepanga kuzichua basi waziache mara



    moja.

                                       **********************************

    Nakumbuka siku ile nililala fofofo sana kwa ajili ya kulala makaburini bila ya kujitakia,ilikuwa



    kuamshwa saa kumi na simu ya Gerald iliyokuwa imeita zaidi ya nusu saa sasa niliipokea huku



    nikiongea kwa uchovu uchovu sana, aliniuliza wapi nilipokuwa nilimjibu nipo nyumbani kwangu



    ndipo kuna kitu kama alikuwa anataka kunielezea kuwa nitafute gazeti jioni ya leo haraka



    sana.nilishituka nikajua itakuwa wamefanikiwa kumzibiti Yule mwanamke mwenye kovu jeusi Au



    ameuliwa wakati akili sasa inatoka kwenye usingizi ili niweze kumuuliza vizuri kwani kulikuwa kuna



    habari gani zaidi hadi anipigie simu na kuongea kwa msisitizo vile mara simu yangu ikakata chaji na



    mtaani        umeme ulikuwa umekatika….!!!

                      *********************************

    Nililaumu sana juu ya ule ukiritimba uliokuwa ukifanywa na shirika letu la umeme kwani  kwa mtu



    kama mimi kukata vile umeme walikuwa wananiathiri sana sababu nilikuwa na vifaa vingi sana



    ambavyo vilikuwa vikihitaji umeme,mungu wangu sasa hapa nafanyaje? Nilijiuliza nikaona hakuna



    jinsi zaidi ya kutoka nje na kwenda kuangalia hilo gazeti lilikuwa na habari gani kwani sikuwa na



    uhakika umeme ungerudi muda gani. Basi nilienda bafuni kwanza kuoga kisha nikavaa track suti



    zangu ambazo nilikuwa napendelea kuzivaa sana mida ya jioni kisha nikatoka zangu nje huku



    mkononi nikiwa nimeshika shilingi elfu moja kwa ajili ya kununulia hilo gazeti nilitoka nje na kushika



    barabara mpaka pale mahakama ya mwanzo ya mnazi mmoja ambapo ndipo palikuwa na vibanda



    vya kuuzia magazeti nilifika na kuanza kuangalia vichwa vya habari pale vya magazeti huku muuza



    magazeti akinitazama kwa umakini sana huku akitazama na gazeti alilokuwa amelishika kama vile



    akifananisha kitu hivi

    Sikuamini baada ya kuliona lile gazeti ambalo Gerald aliniambia kama nimeliona macho yalinitoka 



    sana baada ya kuona kichwa cha habari “AFISA WA POLISI AMEFUMWA MAKABURINI



    AKIWANGA USIKU WA MANANE” huku juu ya lile gazeti kukiwa na picha zangu tatu zimepigwa



    nikiwa natoka makaburini, muyo wangu ulinyong’onyea ghafla nikajihisi mnyonge sana nililichomoa



    lile gazeti na kumpa Yule muuza magazeti pesa yake kisha mimi nikaanza kuludi zangu kwangu,



    nililikunja lile gazeti mkononi kwa kuwa nilipanga nitaenda kulisomea nyumbani.

                                    ********************************

    Niliwaza sana kuhusu ile habari kuwa pale juu ya lile gazeti kwanza nilihisi iliwekwa kwa dhumuni la



    kunichafua kwani habari yenyewe ilikuwa inadai ya kwamba nilienda kuwanga eti ili nifanikiwe



    kumtoa bosi wangu ili  mimi niweze kushika ile nafasi huku wakiwa wamepamba na maneno mengi



    tu ya uongo roho iliniuma sana kwani nilikuwa kwenye wakati mgumu sana  kwanza tayari walikuwa



    wameshaanza kunifitinisha na mkuu wangu wa kazi halafu pia ingeweza kusababisha



    nikatolewakatika kitengo cha upelelezi kwani sasa kila mahala ningepita watu wangekuwa wananijua



    hivyo basi ingeniwia vigumu san katika utendaji wangu wa kazi,nilifikiria lile gazeti la udaku



    ambalolilikuwa linatoka kila siku jioni walijuaje kama mimi nilikuwa makaburini mpaka wakanivizia



    na kunipiga zile picha, niliona tofauti na mazingira ya kazi yangu kuwa ngumu lakini pia jamii sijui



    itanichukuliaje katika lile jambo, hadi kunakipindi nikaanza kujilaumu kwa nini nilikubali



    kumsindikiza Amina usiku ule kwake kwani haya yote yasingetokea nilijipa moyo konde kwani



    nilijua mimi ni mwanaume jambo lile nikilitilia akilini sana lingeweza kuniathiri hata nishindwe



    kufanya mambo mengine niliamua vyovyote itakavyokuwa nitapambana na lolote litakalojitokeza.

    Siku inayofuata sikuweza kwenda kazini kwani niliona ni bora kupumzika kwanza ili kuepuka



    maneno na pole ambazo ningekutana nazo kutokana na ilie tukio huku siku nzima nikishinda kwa



    dada yangu maeneo yak awe.

    Kesho yake niliamka asubuhi na mapema sana ili kuwahi kazini kujua ni kipi kilichojiri kwani siku ile



    nzima simu yangu haikuwa na chaji hivyo sikuweza kupata majibu kutoka kwa Amina kuhusu lile



    zoezi la utambuzi kama lilikuwa limefanikiwa, nilitaka nikapate majibu kisha nielekee kwenye ofisi



    za lile gazeti ili kujua ilikuwaje mpaka wakaniandika vile.  Wakati naingia ofisini pale wakati napanda



    ngazi nilishangaa sana baada ya kuona kila mfanyakazi akinitolea macho huku wakijaribu kama



    kunikwepa hivi roho iliniuma sana baada ya kukutana na dada mmoja pale kazini na kumsalimia kwa



    kumpa mkono akakataa kupokea mkono wangu na wakati naondoka nikasikia akizungumza ya



    kwamba nilikuwa na dawa hivyo basi kwa atakayeshikana mkono na mimi dawa aliyopewa na



    mganga eti itamuingia.

    Roho iliniuma sana kwa lile tukio nilifika mapokezi ambapo nilisaini kisha kuelekea ofisini kwangu



    ambapo Yule dada wa mapokezi pia alikuwa akinitazama kwa wasiwasi. Nilianza kufanya shughuli



    mbali mbali mule ofisini kwangu baada ya kama nusu saa simu ya mezani ya mule ofisini iliita



    ambapo niliambiwa nilikuwa nahitajika katika ofisi ya kamanda mkuu wa mkoa ambaye yeye ndio



    alikuwa mkuu wetu kwa mkoa mzima wa Dar-es-salaam upande wa polisi usalama barabarani na



    upelelezi, moyo ulishituka kwani haikuwa kawaida yake kukutana na watu ambao tulikuwa chini ya



    upelelzi kwani mambo yote alikuwa akitoa maagizo kwa mkuu wetu wa upelelezi wa mkoa inspketa



    Thomas, nilijiinua pale kitini na kutoka na kisha kuanza kupanda ngazi kuelekea floo ya mwisho



    ambapo  ndipo zilikuwepo ofisi zake niliingia mbapo nilimkuta kama mtu aliyekuwa akinisubiri kwa



    hamu sana, alianza kuneleza kwa sauti iliyojaa jazba sana kwamba mimi ni mshirikina sana toka



    zamani nawachezea wenzangu pale ofisini kwamba kila jambo lina mwanzo na mwisho “ si unaona



    sasa mpaka magazeti yamekuona” enhe hii ni fedheha sana katika jeshi letu hatuwezi kuvumilia hii



    hali, aliendelea kuzungumza bila kituo wala kunipa nafasi ya mimi kumjibu, hii haiwezekani hapa



    umeenda kinyume na tofauti zetu za kazi haiwezekani kabisa aliendelea kusisitiza,huku akiniambia



    kwa aibu zangu kutokana na lile tukio ndio maana hata jana sikuweza kwenda kazini, nilikaa kimya



    ambapo alizungumza mengi sana  kwamba mimi navujisha pia siri kwa mwanamke mwenye kovu



    jeusi ndio maana inakuwa ngumu sana kumkamata “usibishe kuna barua pepe zenu mlizokuwa



    mkitumia kuwasiliana nae na simu zenu tumezipata usizani huyo mwanamke wako mnamfuatilia nyie



    tu mpo vikosi vingi sana”  kisha akaniambia ya kwamba kuanzia muda ule nimeshushwa cheo changu



    cha afisa upelelezi msaidizi wa mkoa kwa muda usoijulikana nilijaribu kumuelezea hali halisi jinsi



    ilivyokuwa kule makaburini ya kwamba hata kama wanataka kuamini basi wamuulize Amina lakini



    hakuonekana hata kunisikiliza, sikia bwana Siwah hili ni agizo kutoka kwa kamishina wa polisi idara



    wa upelelezi makao makuu mimi hapa nilipo natimiza amri ya mkuu wangu tu, alisisitizia huku



    akinipa na barua na kuonyesha kama ni mtu aliyekuwa akitaka kutoka mule ofisini.

    Sikutaka kubishana naye sana kwani nilijua tu ningeweza kupandisha hasira zangu tu, nilitoka mule

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ofisini huku roho yangu ikiwa inaniuma sana baada ya kusikia eti mimi nauhusiano na mwanamke



    mwenye kovu jeusi yani juhudi zote nilizozionyesha leo imekuwa vile? Sikuwa na jinsi niliona



    wameamua kutumia tu sababu zisizo na msingi ilimradi tu wanitoe kafara. Basi nilitoka pale ofisini na



    kuelekea mitaa ya gerezani ambapo ndipo zilipokuwa ofisi zalile gazeti la la jioni leo ambalo ndilo



    lilikuwa limeichapa ile habari iliyokuwa inanihusu mimi,nilifika pale mapokezi ambapo nilikutana na



    dada mmoja wa pale mapokezi nilimuomba kuonana na mhariri wa lile gazeti, Yule dada alianza



    kunijibu majibu ambayo sikuridhika nayo mara mhariri hajaja, oh hawezi kuonana na wewe kwa



    muda huu wa asubuhi aliongea mengi nikaona yote hayana maana kisha nikatoa kitambulisho change



    nikakiweka pale juu ya meza, alikiangalisha huku pia akinitazama na mimi usoni kisha akasema “oh



    kumbe ndio wewe”  nilihisi alikuwa tayari ameshajua tu kilichonipeleka pale ni kuhusiana na ile



    habari ya juzi kwenye gazeti lao basi alimpigia simu Yule mhariri kisha akanijulisha ya kwamba



    naweza kwenda huku akisimama na kunielekeza mahali ambapo ofisi yake ilipokuwa ndani ya lile



    jingo.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog