Search This Blog

Sunday 19 June 2022

USINIBANIE - 3

 





    Simulizi : Usinibanie

    Sehemu Ya Tatu (3)





    NIKAONA ni jambo la hatari kumruhusu mpinzani akutawale

    mchezoni. Mwanamume nikaanza kupiga ’kaunta ataki’ au kwa

    lugha fasaha mashambulizi ya kushtukiza. Nikawa namgusa zile

    sehemu zitakazomfanya apoteze kasi yake.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nilianza kumtoa kitambaa cha kichwani alichokitumia

    kuzistiri nywele zake, nikaanza kuzichezea nywele zake

    taratibu nikimpiga busu masikioni na kushuka taratibu hadi

    shingoni. Nikamuona akianza kuhema kama mgonjwa wa pumu.

    Tausi alianza kuhema kwa shida akitetemeka, nikajua sasa

    nimeudhibiti mchezo. Nikamlaza pole pole kitandani.



    "Nakupenda sana Hoza" aliniambia akihema.



    Nilimwangalia kwa makini, hakuonyesha masihara akitamka maneno yale. Mambo yote toka tuliache gari pale mbele ya benki yalituchukua takribani dakika kumi na tano, nikaona kuwa

    bado naweza kulifanya nilitakalo kwa muda uliobakia.

    Nikajipa tena dakika tano za ’shoo gemu’.



    "No, no Hoza!" Tausi alisema akinizuia kwa mikono kuendelea

    na pilika zangu za kimuvi muvi. Nikaweka kituo na

    kumwangalia usoni nikimshangaa. Nilimshangaa kwa kuwa yeye ndiye aliyeanzisha pambano kwa pasi zake za haraka haraka iweje sasa asimamishe pambano!



    "Vipi mpenzi!" Nilimropokea neno mpenzi kiasi cha kumfanya

    atabasamu kabla ya kuniambia sababu ya kunizuia vile tena

    wakati nalikaribia lango.







    Alinieleza sababu ya msingi ambayo ilinifanya nikatulia kwanza kabla ya kuamua kumkumbatia kwa nguvu pale kitandani,

    bila kusemezana chochote.



    Mkanganyiko wa mawazo ulitawala kichwa changu, wakati

    mwingine nilijiona mwenye bahati ila wakati mwingine

    nilijiona nina bahati mbaya. "Huyu mtoto atanitia uchizi

    mimi!" Nilijisemea moyoni.



    Ghafla akakurupuka na kunitaka tujiandae kutoka tusije

    kushtukiwa na dereva pamoja na yule binti mtumishi wa ndani.

    Pamoja na kuwa hatukumalizia tulichokianza, tulitoka nafsi

    zetu zikiwa shwari kabisa.



    Burudani tuliyoifanya ilikonga moyo wa kila mmoja wetu.

    Tausi, yaani we acha tu! Mtoto alinipa burudani ya uhakika,

    yaani kama ni timu ya mpira leo ilikuwa ni mechi ya Arsenal

    na Barcelona.



    Ngoma ilikuwa inagongwa moja moja huku tukiachiana nafasi ya kuonyesha vipaji binafsi. "Mi hata ng’ombe mia nalipa kwa

    ajili ya Tausi" nilijikuta nikijisemea wakati nikimwangalia

    anavyojitengeneza kwenye kioo. "Tausi" Nilijikuta nikimuita

    Tausi "Abe mpenzi wangu!"



    Nikaanza kumweleza kilicho moyoni mwangu, nilimweleza kwa

    sauti ya kutulia. Nilimwambia.



    "Nikisema sijawahi kupenda kabla, nitakuwa nakudanganya

    lakini ukweli ni kuwa sijawahi kuwa na penzi tamu kama hili. Tausi, hakuna maneno ambayo yanaweza kutafsiri ninavyojihisi

    moyoni mwangu kwa penzi hili. Nakiri nakupenda sana!"



    Nilipomaliza kumwambia maneno hayo, niliyaona machozi

    yakitoka machoni pake. Aliinuka na kunikumbatia, "We ndio

    mwanamume wa maisha yangu, Hoza. Ila naomba nikuulize kitu!"



    Nilidakia kumruhusu aniulize, akaniuliza kama nitamweleza

    ukweli wa atakayoniuliza. Nikaahidi kujibu ukweli tupu.



    "Umeoa?" Nikamjibu hapana. Akaendelea kuniuliza maswali

    mengi ya kiuhusiano na yote nikamjibu ukweli mtupu. Swala la

    mwisho aliloniambia ndilo lilinibabaisha kuliko yote aliyoniuliza.



    "Unaonekana una ufahamu mkubwa kuliko kazi

    unayoifanya nitatafuta siku unipe historia yako ya maisha."



    Kimtindo nilijuta kuyaanzisha maongezi yale, nilijikuta

    nimejiweka katika mazingira magumu sana endapo angenihoji

    kweli.



    Tukaanza safari ya kurudi garini kupitia njia ile ile,

    nikamuuliza aliijuaje, akaniambia kuna mtu alimhadithia kuwa

    ametapeliwa katika jengo la Ushirika. Niliishia kucheka

    kabla ya kujiweka katika hali ya kuwa tena mfanyakazi na

    bosi wake.



    Tukarudi ndani ya gari, nikimcheka ujinga yule dereva

    aliyekuwa akiniona kimbelembele. Nikamuona akiangalia saa

    kibwegebwege.



    Usiku ule nilijilaza nitandani nikiwazia maneno aliyokuwa

    akiniambia Tausi, Tausi hajawahi kufanya ngono katika maisha

    yake. Alikuwa bikira!



    Na siku ile ilikuwa ndio nimuingize katika ulimwengu

    mwingine. tatizo likawa ni namna atakavyoonekana akitembea

    wakati anarudi! Dah ingekuwa bonge la noma! Halafu ishu

    kubwa aliyokuwa akiiogopa ni tabia ya mama yake kumkagua

    kila akiwa anarudi baada ya kutoka. Hupenda kumwangalia na

    kumhoji sana.



    Mtihani nilioupata ni kuwa natakiwa kuifanyia shughuli hiyo

    chumbani kwake kwa njia ile ile ambayo huwa ninaitumia

    kumbinjukia. Baada ya siku kama kumi za mawasiliano ya simu,

    niliamua kujitoa kimasomaso siku moja kuivamia ngome ya Mzee Nurdin ili nitimize kazi iliyobakia, kuufaidi uroda wa

    Tausi. Nikajiweka tayari kwa ajili mashambulizi.



    Giza lilipoingia tu, nikatoka polepole na kunyata taratibu

    kuelekea nyumba kubwa. Kwanza nikaenda mpaka dirishani

    kumpigia chabo. Nikam’bamba akiwa katoka kuoga, alikuwa

    akijifuta maji. Moyoni niliamini kuwa alikuwa akijiandaa

    kunipokea.



    Hali hiyo ilinipa ujasiri wa hali ya juu, nikazunguka fasta

    na nikaanza kupanda bomba kuelekea juu ya nyumba ya Mzee

    Nurdin ili niitumie njia ile ile kuingilia ndani. Kufika juu

    nikakutana uso kwa uso na walinzi wawili wanaopasha misuli

    moto.



    Mmoja akashtuka, "mwizi!" Akaja kwa kasi kuja kunifuata

    katika kigiza kile akinipelekea ngumi kama nne za kasi

    ambazo moja ilinipunyua na moja ikanipata vizuri haswa huku

    mbili nikizikwepa.



    Kabla sijajiweka vizuri nilijikuta nikichapwa teke moja kali

    sana nikayumba na kutaka kudondoka chini. Nikarudi kwa kasi

    na kulidaka bomba, nikajiselelesha hadi chini. Natua tu

    chini, na yule mlinzi akawa ametua tayari kwa kuniendelezea

    kichapo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nikajua hapa nikilegea tu nitajikuta mikononi mwa Mzee

    Nurdin na kila kitu kitakuwa kimeharibika. Nikaamua kukomaa

    naye, akarusha tena ngumi mbili, nikaziona. Nikampelekea

    teke moja la tumbo, akaguna na kuinama chini, nikampiga

    kifuti cha uso akainuka na kutoa mlio kama mbwa aliyepigwa

    jiwe.



    Nikajikuta nimedandiwa shingoni na mlinzi mwingine,

    nikampiga ugokoni kwa kisigino kwa haraka nikamuongeza

    kiwiko ambacho kilimpata vyema kwenye chembe. Nikamsikia

    akiugulia na kuiachia mithili ya aliyepigwa na shoti ya

    umeme.



    Yule mwingine tayari alikuwa amesogea huku amekinga ngumi

    utafikiri yuko ulingoni. Nilicheza nao kwa takribani dakika

    tatu hivi nikitumia mapigo makali sana na kuwaacha wakiwa

    hoi wanagalagala kwa maumivu.



    Nikakimbia kwa kasi na kurudi kibandani kwangu, nikamtumia

    ujumbe Tausi kuwa sitaenda nimepatwa na dharura. Najihisi

    kichwa kinaniuma sana, akanipa pole tukalala.



    Niliogopa kumwambia kilichotokea kwa kuwa kingemshtua na

    kuzidisha mashaka kuhusu ukweli juu yangu. Asubuhi hali

    ilikuwa shwari sana, wakati nafagia nikapita karibu na wale

    walinzi wa usiku uliopita.



    Walikuwa wakipakana dawa za kuchua misuli. "Ngumi za yule

    babu zinauma sana!" Nikawa nachekea tumboni. Waliniona kama babu kutokana na nilivyovaa usiku ule, nilivaa suruali fupi

    kama za wale jamaa wenye msimamo mkali wa kidini na nusu

    kanzu. Kichwani nilijifunga kitambaa kama kilemba. Vyote

    hivyo vilikuwa ni vyeusi!



    Lengo lilikuwa ni kuuondoa kabisa muonekano ambao ingekuwa rahisi kunishuku endapo ningefumwa na kukimbia. Sikuwahi kufikiria kabla kama ningeingia kwenye mapambano. Na cha kustajaabisha ni kuwa, wale walinzi hawakutoa taarifa ya uvamizi ule. Nahisi waliogopa kuonekana wazembe na kuharibu kibarua. Ila nilijua kuwa ulinzi ungeimarishwa.



    Wakati nimejipumzisha baada ya kazi, nikapokea ujumbe toka

    kwa Tausi, ’jitahidi leo, baada ya leo itabidi usubiri siku

    za hatari zipite na kabla hazijaisha nitakuwa safirini.’



    Sikutaka kufikiri kuhusu hiyo safari anayoisema japo kujua

    tu anapoenda, akili yangu ilikuwa kwenye kulifanikisha zoezi

    la kuingia chumbani kwa Tausi. Kumuingiza katika ulimwengu

    wa mapenzi ndiyo kitu pekee kilichobakia kichwani mwangu,

    nilikuwa nikipanga na kupangua njia za kutumia. Mwisho

    kichwa kilichoka nikapitiwa na usingizi.



    Baada ya saa kadhaa kupita, nilishtuka, usingizi wangu

    haukuwa mzuri kwa kusema ukweli. Nilikuwa naota vitu vya

    hovyo hovyo tu ambavyo havieleweki.



    Saa hazigandi, usiku ukawadia wakati kichwani sikuwa na

    mpango wowote wa kupenya na kuingia chumbani kwa Tausi.

    Kidogo meseji ya Tausi iliingia, alikuwa akiulizia kama

    nitaenda ama la.



    Meseji ile ilinihamasisha na hatimaye kupata njia. Nikamjibu

    ndio nakuja. Nikajiandaa mwanamume, nikatoka. Nikaenda

    lilipopaki gari la kununulia mahitaji ya ndani, nikatoa

    kiasi fulani cha petroli na kukiweka kwenye chupa yangu.



    Nikaiziba na karatasi nililolifinyanga. Nikatambaa hadi karibu na getini, nikikodolewa macho na mbwa ambao nadhani walikuwa wakinishangaa wasijue nilichokuwa

    nakifanya. Nilipokaribia getini nikaliwasha lile karatasi na

    kuirushia ile chupa nyuma ya kibanda cha walinzi.



    Nikarudi mbio hadi nyuma ya nyumba kubwa, ghafla ukasikika

    mlio mkubwa sana. Lilikuwa ni bomu la petroli. Nilisikia

    vishindo vya walinzi wakikimbia huku na kule, nikapanda juu

    haraka kupitia bomba, nikamuona mlinzi wa juu akiwa

    anatumbulia macho getini.



    Nikaingia kwa haraka kupitia ngazini hadi ndani kwenye chumba kidogo kile cha giza. Nikaenda kwenye swichi kubwa ya umeme na kuizima, kisha nikachubua nyaya na kuzikutanisha. Giza likatawala.



    Nikatembea kwa haraka, nikauchokonoa mlango ule mdogo ambao huwa ninautumia kuingia eneo la vyumba. Nikaingia na kwa kasi nikazama chumbani kwa Tausi. Wakati huo wote sikuwahi kufikiria kuwa nitatokaje ndani ya jumba hilo la Mzee

    Nurdin.



    Nje nilimsikia mlinzi akitangaza kuwa kila mtu atulie alipo

    hadi atakapotangaza tena. Ndani nilimkuta Tausi anatweta kwa

    woga, nikawahi kumkumbatia nikijitambulisha ili asije

    akapiga kelele. Akanikumbatia kwa nguvu akiniuliza kuwa ni

    nini kimetokea.



    Nikamjibu kuwa sikuona kitu labda ni hitilafu ya umeme.

    Tukabaki tumekumbatiana huku tumesimama, nikamchukua

    taratibu na kumpeleka kitandani. Tukawa tumejilaza kitandani

    bila kuongea chochote wala kufanya chochote, nilijua kuwa

    Tausi bado hakuwa tayari kuhamia katika ulimwengu wa mahaba.



    Baada ya takribani dakika arobaini hivi, wakawasili polisi

    kadhaa na mafundi umeme. Kila kitu kikarekebishwa hali ikawa

    shwari, mlinzi akathibitisha.



    "Twende tukaoge" nilimnong’oneza Tausi bila kujali kuwa

    alikuwa ameshaoga ama la lakini ilikuwa ndio njia ya

    kumuondoa hofu na kuirudisha akili yake mchezoni.

    Niliinuka kwa haraka, nikimwacha akijiinua taratibu.



    Nikamsaidia kunyanyuka kabla sijambeba ghafla na kumpeleka

    kwenye bafu ambalo limo humo humo ndani ya chumba chake.

    Nikazitoa nguo zangu kama niliyepagawa.



    Tausi akawa akiniangalia kwa wizi wizi huku akiona aibu,

    nikaanza kumtoa nguo zake taratibu. Nikamkumbatia na

    kulifungulia bomba la mvua wakati tayari nimerekebisha

    mchanganyiko uliotoa maji ya uvuguvugu.



    Nilikuwa nikimsugua kwa kugusa zile pointi muhimu ambapo

    nilikuwa pale mahsusi kwa ajili hiyo. Tulipomaliza kuoga

    alikuwa hoi, nikamfuta taratibu na kujifuta mwenyewe.

    Nikamnyanyua kumrudisha kitandani.



    Tausi alikuwa mpole sana mithili ya ngamia aliyepigwa dua na

    kulala akisubiri kisu kipite shingoni, niliendelea

    kumchokoza na kumhamasisha. Naye akijibu kwa kutoa

    ushirikiano unaostahili.



    **********



    Ilikuwa yapata saa saba za usiku tuliporudi bafuni kuoga.

    Ilionekana dhahiri kuwa Tausi hakutaka niondoke usiku ule,

    muda wote alikuwa kaniganda.



    Tulirudi kulala kitandani lakini pamoja na kuifanya shughuli

    iliyonipeleka pale kwa ufanisi wa hali ya juu, akili yangu

    yote ilikuwa juu ya namna ntakayofanya ili niweze kutoka

    katika jumba lile bila kushtukiwa.



    "Saa kumi na mbili walinzi wanabadilishana, utatoka muda

    huo" alisema Tausi huku akipandisha kifua chake juu ya kifua

    changu. Baada ya muda Tausi alikuwa amelala fofofo kifuani

    kwangu kwa kudeka, lakini sikuwa hata na lepe la usingizi.



    Nilishindwa kuelewa ni nini Tausi anachonitakia mtoto wa

    mwanamke mwenzake. Kutokana na uchovu nilionao baadaye

    nilijikuta na mimi nikipitiwa na usingizi.



    Tulikuja kushtuka saa mbili kasoro dakika chache, ilibidi

    aanze kutoka Tausi ili aangalie hali ilivyo. Kote kulikuwa

    kumejaa wafanyakazi na walinzi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Na tayari kulikuwa na wengine ambao walikuwa tayari kwa

    ajili ya kukifanyia usafi chumba cha Tausi. Tausi akarudi

    ndani tulibaki tunaangaliana tusijue la kufanya.



    "Tutafanyaje Hoza?" Aliniuliza Tausi akiwa na hofu.



    Nilimfuata aliposimama, nikamkumbatia kwa nguvu kumtoa hofu. Nilijua kuwa hata nikiogopa isingesaidia kitu sana sana

    ningepoteza uwezo wa kufikiri. "Nitatoka tu, usihofu"

    nilimwambia nikimvutia kitandani na kulianzisha tena.



    "Wee Hoza, huogopi?" aliniuliza akiwa kakosa raha. Nami

    sikumjibu bali niliendelea kumlegeza viungo na kumpagawisha.

    Tukawa tumejilaza kitandani, ’nikimkuza’.



    Baada ya kumalisha shughuli pevu ya kumlea Tausi, tukawa

    kitandani tukipumzika. Nikaanza kumweleza Tausi. "Leo

    itanibidi niondoke, niache kazi." Tausi alishtuka sana na

    kuniangalia.



    "Kwa nini?"



    "Hadi sasa watakuwa wamekwishagundua kuwa sipo, na sitaweza kuelezea nilipokuwa. Kwa hiyo sina budi

    kutoroka!" Machozi yalianza kumtoka Tausi, mwisho akaanza

    kulia akinikumbatia kwa nguvu.



    "Utaishije Hoza mpenzi wangu bila kazi, isitoshe ni lazima

    baba atakusaka ili kujua ulipokimbilia. Atakuumiza au

    atakuweka ndani" aliongea kwa uchungu Tausi. Nilimhakikishia

    Tausi kuwa nitakuwa poa tu.



    Nilijaribu kucheza na akili yake nikafanikiwa kumfanya

    aniamini. Akanifungia kwenye kabati kubwa la nguo lililo

    ukutani kisha yeye akatoka kuelekea sebuleni kwao. Nikasikia

    watumishi wakiingia kufanya usafi, huku wakimteta kuwa

    amechelewa sana kutoka huku wakichunguza ili kujua

    kilichomchelewesha.



    Bahati nzuri mashuka yote yaliyotumika tuliyaficha, alikuwa

    anataka ayafue mwenyewe kwa kuwa yalikuwa na siri kubwa.

    Watumishi walimaliza wakaondoka na umbeya wao. Mara Tausi

    akaingia, akaufunga mlango wake na kunitoa mule kabatini.



    "Njoo tule" Alikuwa kabeba msosi wa maana! Baada ya

    kuhifadhi ile menyu tumboni, tukarudi kitandani na kulala

    huku tukipiga stori na kupanga namna tutakavyokuwa

    tukiwasiliana baada ya mimi kutoka pale.



    Giza lilipoingia alinipa cheni yake ya dhahabu na simu yake,

    mi nikamuachia ile Nokia ya jeneza (3310). Nikaanza safari

    yangu ya kutoka. Kufika kwenye chumba cha giza nikaanza

    kupandisha ngazi taratibu kuelekea juu, kwa tahadhari.



    Ghafla nikahisi nimewekewa kitu cha baridi kichwani, nikajua

    ni bunduki! "Tulia hivyo ulivyo!" ilisikika sauti nzito.

    Niliongozwa kupanda juu huku mtutu ukiwa kichwani. Ilibidi

    nijifanye mwoga sana, nikawa nalia nikiomboleza kuwa

    wasiniue mi sio mwizi.



    Nilifanya hivyo ili nitakapohojiwa iwe rahisi kwao kuamini

    kuwa nasema ukweli hata kama ningewadanganya. Nilipofika juu nikakalishwa chini, wakaongezeka walinzi wengine wawili.

    Wakati huo kote kulikuwa shwari, ni mbwa tu waliokuwa

    wakizungukazunguka.



    "We ni nani na unatafuta nini humu?" Kabla sijajibu mlinzi

    mmoja akanimulika na tochi usoni, nikafumba macho kuzuia

    mwanga mkali wa tochi usiniumize. "Kha! We mgosi! Hoza!"



    Kimya kilitawala kwa sekunde chache, yule aliyeniwekea mtutu

    wa bunduki akautoa kichwani kwangu. Wote wakazunguka na

    kusimama mbele yangu. Walinihoji pale kwa zaidi ya dakika

    kumi, ilibidi niwaambie ukweli kuwa nilienda kum’binjukia

    Tausi.



    Nilijua bila kuwaeleza vile yangefumuka mambo kuhusiana na

    upekuzi nilioufanya ofisini kwa Mzee Nurdin. Hakuna

    aliyeamini kama ni kweli nilikuwa kwa Tausi hadi pale

    nilipompigia Tausi na kumweleza kuwa nimekamatwa na walinzi



    na wanataka kunipeleka kwa Mzee Nurdin.

    Kimsingi nilichomwambia Tausi ndicho nilichoelekezwa na

    walinzi niseme. Alichosema Tausi ni kuwa nimpe mlinzi

    mmojawapo aongee naye. Alichosema na yule mlinzi ni siri yao

    lakini kilichofanyika toka pale ni kwamba nilipelekwa hadi

    kibandani kwangu, nikachukua vitu vyangu vya muhimu.



    Baada ya hapo nilisindikizwa hadi nje ya geti kubwa na

    kuruhusiwa kuondoka. Nijani wale walinzi walikuwa wakinisifu

    japo kwa kutumia maneno ya kuudhi. Eti waliniambia mimi ni

    mchawi, nimemloga mtoto wa bosi wao hadi akaingia laini.



    Nilikereka kwa namna walivyonishusha kiwango lakini sikutia

    neno, niliona ni heri nusu shari. Unajua nikiamuaga

    kujifanya bwege hadi utanichukia, lakini ili mradi ubwege

    huo uwe ni kwa faida yangu.



    Nilipofika mbali na pale kwa Mzee Nurdin, ilinibidi nitoe

    taarifa kwa mkuu kuhusu lililotokea lakini sikumwambia kuwa

    niliuzamia uroda wa Tausi, nilimdanganya kuwa niliingia

    kuendelea na uchunguzi wangu.



    Kikubwa kilichonisukuma kutoa taarifa usiku ule ni usafiri,

    sikuwa na namna yeyote ya kufika nyumbani usiku ule. Mkuu

    akanitumia gari lakini aliniamuru kwamba niripoti ofisini

    kwake usiku ule ule kwa ajili ya majadiliano zaidi.



    Kwa sauti aliyokuwa akiiongea mkuu nilijua wazi kuwa

    kitawaka, ila kwa kulinganisha na uroda nilioupata kwa Tausi

    sikuwa na wasiwasi wowote. Nilichukulia poa tu, kama mbwai

    mbwai!



    Njia nzima nilikuwa nikiwasiliana na Tausi, alionekana

    ameridhika sana na mapenzi niliyompa na alikuwa na matarajio

    makubwa sana kutokana na uhusiano tulioanzisha. Ila kuna

    kitu kimoja kilikuwa kinanitatiza kuhusiana na mapenzi

    nilioyaanzisha na Tausi, nitamwambiaje kuwa mimi ni

    mpelelezi?



    Mara zote nilijisikia kumweleza kutokana na maongezi yake

    ambayo yalinisisitiza nijiendeleze kielimu ili nipate kazi

    nzuri tuweze kuishi maisha ya raha.



    Katika kipindi kile cha takribani miezi mitano kasoro

    nilichokuwa kwa Mzee Nurdin niligundua vitu vingi sana

    kutokana na mienendo ya ingia toka ya baadhi ya watumishi wa

    serikali wasio waaminifu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kikubwa kilichokuwa kikiniweka ni kujua ni lini wangefanya

    biashara yao ili nitoe taarifa wakamatwe, nilikuwa hasa

    naivizia biashara ya kusafirisha binadamu.



    Usiku ule nilikaa na mkuu hadi kunakucha tukijadili mambo

    mbali mbali kuhusiana na uchunguzi wangu. Baada ya

    kuridhika, mkuu akaniruhusu kupumzika kwa siku tatu tu.

    Nikarudi nyumbani kwangu kwa mara ya kwanza baada ya karibia miezi mitano.



    Nyumba yangu iko maeneo ya Boko, haiko mbali sana na bahari

    ya Hindi. Niliingia na kujitupa kitandani ili kupunguza

    uchovu wa kazi na wa kulala sehemu mbovu kwa miezi.



    Jioni ya siku hiyo baada ya kupumzika na kurekebisha masuala

    mbalimbali ya nyumbani, niliinua simu na kumpigia Tausi ili

    nimjulie hali. Simu ya Tausi haikuwa ikipatikana.



    Mapigo ya moyo yalianza kunienda mbio huku nikiijaribu tena

    mara kadhaa bila mafanikio. Kichwa kikaanza kuniuma! Sio

    siri, Tausi nilimpenda toka moyoni, nilimpenda haswa na hilo

    hata mwenyewe alilijua.



    Hadi naamka asubuhi siku ya pili, simu ya Tausi bado ilikuwa

    haipatikani. Nikaanza kufikiria namna ya kuwasiliana na

    Tausi, sikuweza kuvumilia kabisa ukimya ule. Lazima niende,

    lazima nionane na Tausi au nipate habari zake kwa hali

    yeyote.



    Siku mbili za kutowasiliana na Tausi zilikuwa ni ngumu sana

    kwangu. Nilifikiria kumkamata msichana wangu yeyote wa

    zamani anitoe mawazo lakini katika mademu wangu wote

    niliowafikiria hakuna aliyekaribia kiwango cha kunitoa

    mawazo ya Tausi.



    Giza lilipoingia nilivaa suti yangu nyeusi, ndani nilivaa

    fulana ya bluu bahari na kichwani nilivaa pama kubwa jeusi

    lililoficha kidogo uso huku macho nikiyaficha na miwani.

    Nikakachukua kagari kangu keusi aina ya Toyota Starlet na

    kutoka pale kwa mwendo wa kasi.



    Akili yangu yote ilikuwa ni kuhusu Tausi, nikawa

    nimeshapanga cha kufanya. Baada ya muda mchache nikawa

    nakaribia geti la nyumbani kwa Mzee Nurdin, niliongeza sauti

    ya muziki katika gari.



    Kutokana na muziki kuwa mzito, gari lenyewe lilikuwa

    linatikisika. Niliongeza spidi na kuingia kwa kasi katika

    geti ambalo lilikuwa limeachwa wazi na walinzi.



    Nikalisimamisha karibu kabisa na lango la nyumba kubwa.

    Nikafungua mlango wa gari na kutoka bila kuufunga.

    Kutahamaki walinzi wakawa wamenizunguka na silaha mkononi,

    nikaanza kutukana kwa kutumia lugha za Kifaransa na

    Kiingereza.



    Nilikuwa nikitukana huku nikiangalia lango la nyumba kubwa,

    hakuna mlinzi aliyejaribu kunijibu chochote kwa kuwa

    hawakuwa wakielewa nilichokuwa nakizungumza.

    Katika uhalisia, kwa kitendo hicho nilichokuwa nikikifanya

    pale ni tiketi ya kufukuzwa kazi moja kwa moja na

    kufunguliwa kesi kwa mujibu sheria za jeshi. Lakini

    sikufikiria chochote, akili yangu ilikuwa kwa penzi la

    Tausi.



    Nilikuwa nikidai nimemfuata mdogo wangu Hoza ambaye

    amechukuliwa kijijini na kuletwa kutumikishwa kazi kwa Mzee

    Nurdin. Nadhani walinzi walichokuwa wakisikia ni jina tu la

    Hoza.



    Ilibidi atoke Mzee Nurdin mwenyewe ambaye ndiye anayejua

    Kiingereza kwa ufasaha. Nikabadilisha na kuanza kuongea

    kifaransa tupu, nilijua kuwa hawatakuwa na ujanja zaidi ya

    kumtoa Tausi.



    Katika kipindi nilichokaa niligundua kuwa Tausi anakifahamu

    Kifaransa vizuri mno kutokana na kusomea nchi zinazotumia

    lugha ya Kifaransa.



    Muda mfupi kidogo Tausi akaitwa, kitu cha kwanza

    nilichokigundua kwa Tausi ni kwamba, alikuwa akiniangalia

    sana kifuani. Nikagundua kosa nililolifanya, nilivaa mkufu

    alionipa Tausi.



    Nikamwambia kuwa awaambie kuwa mimi ni kaka yake Hoza,

    nimerudi toka ughaibuni na kukuta kuwa mdogo wangu

    amechukuliwa kutumikishwa kazi.



    Tausi akawa anawatafsiria huku macho yake yakinichunguza

    kupita kiasi. Tausi aliniambia kuwa Hoza katoroka, ila

    alivyoufikisha ujumbe huo alikuwa kama anayenitega. "Kama

    Hoza sio wewe, Hoza alitoroka."



    Moyo ukaanza kwenda kasi, nikamuuliza kama kuna ajuaye

    kifaransa pale, akanijibu hakuna. Ila aliniambia kuwa

    anahisi Mzee Nurdin anasikia juu juu ila hataki kujionyesha

    kama anajua. Nikaamua liwalo na liwe, nikamchana laivu.



    "Mbona simu yako haipatikani?" nilimuuliza swali ambalo

    lilimfanya atake kuanguka kwa mshtuko.



    "Ni wewe?" Nilihisi kitu kutokana na mtazamo wa Mzee Nurdin.

    Baadae nililijua kosa langu, unajua nilipofika pale mara ya

    kwanza nilikuwa na mzuka, nilikuwa napayuka hovyo hovyo,

    lakini alipotoka Tausi nilipigwa ganzi.



    Ujasiri wangu wote ulitoweka, nilijisikia kama nimrukie,

    nimkumbatie na kummiminia mibusu isiyo idadi. Nilikuwa

    nimemmisi haswa mpenzi wangu Tausi. Kingine kilichonifanya

    niache kupayuka ni ukweli kuwa nilikuwa nikijaribu

    kumwangalia kwa umakini kama yuko salama, ukimya wake

    ulinitisha sana.



    Sijui nikuhadithieje ili upate picha ya urembo wa Tausi,

    huyu binti amenifanya mtumwa ndani ya moyo wangu. Alikuwa

    amevaa gauni refu na pana huku amejifunika kichwani, lakini

    haikutosha kuufunika urembo wake uliokithiri. Nilijikuta

    nakwama kuendelea kuigiza.



    Nilipomtupia jicho Mzee Nurdin, nilihisi kuwa aliwapa ishara

    fulani walinzi wake. Mlio wa hatari ukalia kichwani mwangu,

    hasa pale walinzi hao walipotawanyika.



    Tausi akarudia tena kuniuliza swali lake, "Ni wewe?"

    Sikumjibu kwa kuwa sikuweza kumdanganya, bali nikamwambia

    kuwa nitarudi siku nyingine kupata habari za Hoza. Ukweli ni

    kwamba nilikuwa najichanganya changanya katika kauli zangu

    ila kikubwa naamini kuwa Tausi alishajua kuwa ni mimi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ila nilijishebedua kumwomba kuwa anipe taarifa yeyote

    atakayoipata kuhusu Hoza, nikajifanya kusema kuwa hata kama

    atakuwa amekufa wasisite kunijuza. Nikamtajia namba yangu

    kwa kuirudia rudia ili hata kama karatasi litakaloandikiwa

    namba yangu likibaki kwa Mzee Nurdin, Tausi naye awe

    kaikariri kichwani mwake.



    Wasiwasi wa kuwa Tausi ni mzima wa afya au la ulinitoka, ila

    nikawa ukaonegezeka wasiwasi mwingine. Kanimwaga? Kama Tausi ni mzima, ni nini kilichokuwa kikimfanya asinipigie? Na kama

    kungekuwa na bifu kati yake na wazazi wake mbona sikuona

    dalili yeyote alipoitwa na Mzee Nurdin.



    Kwa kuwa namba hiyo ni rahisi sana kukaririka, nilikuwa na

    uhakika kuwa Tausi ataikariri. Kazi ilikuwa ni kushika namba

    ya kuanzia ya mtandao tu. Sikutaka kuaga, nikaingia ndani ya

    gari langu na kuligeuza kwa fujo.



    Kufika getini nikalikuta geti limefungwa. Kila nilipopiga

    honi hakukuwa na dalili za kufunguliwa, nikajua kuwa

    nimekwisha.



    Nilianza kujilaumu kwa kuwa mtumwa wa penzi la Tausi, nikawa

    nikiwaza ni nini kingetokea endapo taarifa zingemfikia mkuu.

    Heshima yangu yote ingepotea achilia mbali kupoteza kazi na

    kufukunguliwa mashitaka.



    Nilianza kuingiwa na ubaridi, kutahamaki nikaliona difenda

    la polisi likiingia kwa kasi. Wakati halijasimama vizuri

    wakashuka vijana wakazi kama watano hivi, wote wakiwa na

    silaha. Nikajua hapa tena kumekucha, akili yangu ikaanza

    kwenda spidi japo haikuwa ikiweza kufikiria jambo lolote kwa

    sekunde kadhaa.



    Nikaanza kupata picha ya magazeti ya kesho yake ambavyo

    yangeripoti tukio hilo. ’Mzee Nurdin anusurika kuuawa,

    Jambazi lamiminiwa risasi na polisi’ Nikaanza kusisimkwa

    mwili, nikawa namuona mkuu anavyoipokea taarifa hiyo.

    Nikajiona kweli nimebugi stepu kwenda pale, nikajua tayari

    ’nimeingia choo cha kike’.



    Kabla sijashangaa vizuri likaingia gari jingine la polisi

    likiwa na msaidizi wa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa. Kutahamaki

    gari langu likawa limezungukwa likiwa chini ya ulinzi.



    Kwanza nilifikiria nikubali kukamatwa halafu nikifika

    kituoni nijitambulishe lakini kutokana na mawasiliano

    yaliyokuwa yakifanyika nikahisi hatari. Wangeweza

    kunimiminia risasi kisha wakanisingizia ujambazi, nikapiga

    akili ya haraka haraka nikapata wazo.



    Nikaitoa simu yangu kumtafuta Omar, huyu Omar ni rafiki

    yangu mkubwa na tulikuwa wote mafunzoni ila yeye amepangiwa

    kuwa katika misafara ya rais.



    Mimi na Omar huwa tunasaidiana sana katika vimeo hasa

    ambavyo hatutaki wakubwa wetu wajue japo mwenzangu amenizidi kwa viskendo vya hapa na pale. Wakati huo yule bosi wa

    upelelezi alikuwa akiongea na Tausi na Mzee Nurdin huku gari

    langu likiwa limewekwa chini ya ulinzi na vijana wa kazi.



    Walipomaliza maongezi yao akaja liliposimama gari langu na

    kunionyesha ishara ya kushuka kwa kuwa nilikuwa nimejifungia

    garini. Sikuteremka wala kujibu lolote, mijamaa ikawa

    inalizunguka zunguka tu gari langu. Zilipita takribani

    dakika tano wakiwa wanajadiliana namna ya kufanya.



    Kimsingi wasingepata maelezo ya kutoa endapo wangenimiminia

    risasi mule ndani ya gari lakini endapo ningetoka wangekuwa

    na mengi ya kusema na kuandika.



    Ghafla ulionekana mwanga mkali wa taa za magari kisha

    ulisikika mlio wa magari matatu yanayoongozana. Yakasimama

    nje ya geti.



    Zilikuwa benzi mbili nyeusi zenye namba za ikulu, walinzi

    wakazifungulia huku wale polisi wakibaki wameshangaa. Kule

    barazani pia nilimuona Mzee Nurdin na mlinzi wake mmoja

    wamepigwa na butwaa.



    Akateremka Omar, nikashusha pumzi ndefu. Msaidizi wa mkuu wa

    upelelezi wa mkoa akamsogelea na kutoa heshima. Wakati huo

    kwenye kila benz walitoka watu watatu watatu waliovalia suti

    nadhifu, jumla wakawa tisa, na Omar alikuwa wa kumi.



    Polisi wote wakaamuriwa kukaa mbali na gari langu, sijui

    Omar alimwambia nini yule bosi wa polisi bali baada ya

    kuongea kidogo ndipo amri ile ilitolewa. Nikatoka ndani ya

    gari, Omar na wenzake wakanipa heshima.



    Nikachekea moyoni, na kwa haraka haraka nikajua ilikuwa ni

    namna ya kuwatishia zaidi wakina Mzee Nurdin kuhusu wadhifa

    wangu.



    Nikawapa mikono na kurudi ndani ya gari langu, nikafungulia

    muziki kwa sauti kubwa kama kawaida. Nyumbani kwa Mzee

    Nurdin kukageuka kuwa kama ukumbi wa disko kwa muda kabla

    sijapandisha vioo tena.



    Omar akarudi ndani ya gari na wenzake wakamfuata na kuingia

    kila mtu kwenye gari alilotokea, likaanza kuondoka la kwanza

    kisha nikawasha gari langu na kulifuata. Nyuma lilifuatia

    gari alilopanda Omar, na jingine likamalizia nikaacha

    mshangao mkubwa nyumbani kwa Mzee Nurdin.Ila bado nilikuwa

    na mawazo kuhusu Tausi.



    Tuliongozana kwa umbali fulani kisha tukaachana huku Omar

    akitaka kujua chanzo cha yote yaliyonitokea, ila ’nikampotezea’.

    Nikamwambia ningemhadithia siku nyingine.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ila nilikuja kumhadithia mkasa mzima wa kumfukuzia Tausi

    japo uongo ulikuwa ni mwingi zaidi, sikumwambia kama vile

    hasa ilivyo na kazi niliyopewa na mkuu, nilimdanganya kuwa

    nilionana naye nje ya nchi.



    Baada ya siku moja tu toka niokolewe na kina Omar nyumbani

    kwa Mzee Nurdin nikapokea simu toka kwa Tausi. "Halo..Jhe

    mapele Tausi!" alimaanisha kuwa naitwa Tausi.





    ITAENDELEA



0 comments:

Post a Comment

Blog