Search This Blog

Sunday 19 June 2022

AHADI YA NDOTONI - 3

 



    Simulizi : Ahadi Ya Ndotoni

    Sehemu Ya Tatu (3)













    “Dada ulichonituma nimekipata hata kabla ya kufika uliponituma tena kwa bei nafuu.”

    “Sikiliza Sara kukutuma kule nilikuwa na maana yangu nakuomba urudi upesi kachukue pesa ndani uwahi haya mafuta siyataki,” aliyapigiza mafuta ukutani kwa hasira, chupa ilipasuka na mafuta kutawanyika.



    “Sasa dada mbona ni kitu kile kile tu.”

    “Sara siku hizi tumekuwa tunabishana?”

    “Dada siwezi kurudi roho inaniuma.”

    “Kwa nini?”



    “Kwa uamuzi unayotaka kuchukua.”

    “Uamuzi gani?”

    “Ya kutaka kuyakatisha uhai yako.”

    “Wewe Sara umejuaje?” Jeska alishtuka kusikia vile.

    “Nijueje? Wakati uso wako unaonesha una dhamira mbaya ya kutoa uhai wako.”



    “Aah!” Jeska alipigwa na bumbuwazi mpaka kisu kikamponyoka.

    “Lakini dada kwa nini usimsikilize mgeni?”

    “Mgeni, mgeni gani?”



    “Eeh, yule kaka aliyekuleta mchana.”

    “Alisemaje?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Si alisema atakusaidia kila kitu.”

    “Basi Sara nimekuelewa.”

    Jeska alisema huku akigeuka arudi ndani, alishtuka kumuona mlinzi akiwa anatokwa machozi.



    “Ha! Mnyalu umerudi saa ngapi?”

    “Sijaenda popote bosi.”

    “Kwa nini hujaenda popote na kwa nini unalia?”

    “Sijaenda kwa kuhofia nikiondoka utajiua na ninalia kwa vile ukifa nitafanya wapi tena kazi.”

    “Umejuaje dhamira yangu.”



    “Inajionesha usoni kwako.”

    Kauli ile ilimshtua sana Jeska na kujiuliza uso wake unaonesha vipi dhamira iliyokuwa moyoni mwake. Alipanga akienda ndani akajitazame usoni ili aione dhamira yake usoni kwake inaonekana vipi.



    “Mnyalu si unajua maisha magumu unafikiri baada ya kufa mzee mimi nitawezaje kuyahimili maisha haya. Kwa sasa hivi nina uwezo lakini huko mbele mambo yatakuwa magumu sana, nitatakiwa nilipe kodi ya mwaka milioni mbili na laki nne kazi sina nitazipata wapi.



    “Bado mshahara wenu kula yetu mnafikiri Jeska mimi nitafanya nini, Mnyalu wewe si mgeni kwangu nimeisha kueleza siri yangu ya maisha. Umeona jinsi mikosi inavyoniandama unafikiri mwisho wake nini?”

    “Lakini mbona mgeni alisema atakusaidia?”



    “Mnyalu umejuaje?”

    “Ma mdogo Jeska si muhimu kujua nimejuaje ila kumsikiliza mgeni alivyokuonya asiyakatishe maisha yako pia yupo tayari kukusaidia.”



    Maneno ya Sara na Mnyalu yalizidi kumchanganya Jeska na kukubaliana na ombi la wafanyakazi wake kuwa asiyakatishe maisha yake. Aliamua kurudi ndani huku moyo ukimuuma kwa uamuzi wa kijinga wa kutaka kuitoa roho yake bila sababu.



    Aliingia hadi chumbani kwake na kupiga magoti mbele ya kitanda kumuomba Mungu amsamehe kwa yote aliyoyataka kufanya. Baada ya kuomba toba ya majuto huku akilia alijikuta akilala kwenye zuria bila kujijua. Alishtushwa na sauti ya Sara.



    “Dada...dada.”

    Kabla ya kuitikia alijiangalia alipokuwa amelala kwenye zuria pembeni ya kitanda. Alijinyanyua alipokuwa amekaa kwenda kufungua mlango, alikutana na Sara akitweta huku jasho likimtoka.



    “Vipi Sara mbona hivyo?”

    “Samahani dada nilikuta foleni kubwa.

    “Ya nini?”

    “Si uliponituma.”

    “Kukutuma nini tena?”



    “Dada si ulinituma nikufuatie mafuta.”

    “Mafuta! Mbona sikuelewi si uliishaleta.”

    “Dada nimeleta saa ngapi na mimi sasa hivi ndio nafika.”



    “Sara mbona sikuelewi unafika vipi wakati mafuta umeishaleta.”

    “Dada utakuwa anachanganyikiwa, umenituma mafuta na kunieleza nisinunue popote zaidi ya uliponituma na sasa ndiyo narudi.”



    “Sasa haya ni maajabu, sasa Sara aliyeniletea mafuta ni Sara gani?”

    “Kwani kuna mtu kakuletea mafuta?”

    “Sio mtu bali wewe Sara, hebu acha kunichezea akili.”

    “Kweli dada mimi ndiyo nafika.”



    “Mmh, mbona nazidi kuchanganyikiwa aliyekuja na kunikataza nisijiue ni Sara gani?”

    “Ha! Dada ulitaka kujiua?”

    “Ha..ha..a..pana.”



    Wakati akiwa bado yupo njia panda mlinzi wake aliingia.

    “Ma mdogo Jeska ulichonituma nimezunguka kila kona nimekosa.”

    “Mmh, Mnyalu na wewe unataka kunichezea akili kama Sara au mmepanga kunitania?”



    “Kivipi Ma mdogo?”

    “Wewe si uliniambia hukuondoka baada ya kugundua nataka kujiua?”

    ”Mungu wangu! Mamdogo ulitaka kujiua?”



    “Jamani mbona unanichezea akili?”

    “Dada kwani vipi mbona kama umechanganyikiwa?” Sara alimuuliza Jeska ambaye aliamini walikuwa wakimchezea akili.



    “Jamani hebu acheni kunichezea akili ni kweli ndio mnafika?”

    “Dada tokea lini nikakudanganya, sijui kaka Mnyalu.” Sara alijitetea.



    “Hata mimi sijawahi kukutania, unasema kuna mtu kama mimi alikuja kukueleza usijiue labda malaika hakutaka kuona unaukatisha uhai wako.”



    “Hata siamini bado hayajaniingia kichwani.”

    “Dada kwa upande wangu ndio nafika toka uliponituma nitawezaje kwenda kule na kisha niwepo hapa kwa wakati mmoja?”



    “Sawa hamkuwepo ni nani anayefanana na wewe na mwingine na Mnyalu waje kwa wakati mmoja kwa umbile na mavazi yenu?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Dada labda ulikuwa umelala ukaota lakini mimi sikiwepo,” Sara alizidi kujitetea.

    “Hata mimi,” Mnyalu naye alikana kuwepo.

    “Mmh, sawa.”



    “Lakini dada kwa nini ulitaka kujiua?” Sara alitonesha kidonda.

    “Jamani naomba mniache kwanza.”

    “Tutakuacha tu dada, lakini kwanini unataka kututia ukiwa?” Mnyalu naye aliuliza.



    “Jamani nimechanganyikiwa mwenzenu na maisha,” Jeska alijitetea baada ya kubanwa sana.



    “Ma mdogo Jeska kujiua bado si suruhisho la matatizo kwa vile kila kiumbe kina haki ya kufa, kuingilia kazi ya Mungu ni kujiongezea matatizo.”

    “Basi jamani nimekosa nisameheni sirudii tena kuchukua uamuzi kama huo.”

    “Sawa dada.”



    Walimuacha Jeska akirudi chumbani kwake kupumzika na kila mmoja alikwenda kuendelea na kazi yake. Jeska akiwa kitandani amejilaza alijikuta akijawa na mawazo mengi juu ya kile kilichomtokea cha Sara na Mnyalu kuonekana wakimsihi asijiue na baadaye kuonekana katika sura nyingine kila mmoja akikana hakuwepo muda ule.



    Bila kujielewa usingizi ulimpitia, aliposhtuka alishangaa kujikuta amelala kwenye nyumba ngeni kwake. Lakini chumba kilikuwa kizuri sana kilichokuwa na mapambo na harufu nzuri hewa yake ilikuwa nzuri sana. Pembeni yake alikuwa amelala yule bwana msamalia mwema aliyemuahidi kumsaidia.



    Yule bwana alikuwa kwenye usingizi mzito, Jeska alijiuliza pale ni wapi na amefikaje. Alijikuta akiwa na shauku ya kutaka kumuamsha yule bwana amuulize pale ni wapi na amefikaje.



    Kabla hajamshika upepo mwanana mzuriii wenye harufu nzuri ya manukato ulimpiga usoni na kujikuta ukipatwa na usingizi na kujilaza pembeni ya yule bwana. Jeska alishtuka siku siku ya pili na kujikuta amelala kitandani kwake.



    Alikurupuka kitandani na kutoka hadi nje ya chumba chake.

    Milango ilikuwa bado imefungwa kuonesha hakuna aliyeingia wala kutoka. Alitamani kuita lakini ajabu aliyetaka kumwita hakumfahamu jina. Alikwenda msalani na bafuni lakini hakumuona mtu.



    Alijiuliza mtu yule aliyekuwa naye usiku yupo wapi?

    Bado hakuamini alitoka hadi kwa mfanyakazi wake wa ndani kumuuliza.

    “Sara.”



    “Abee dada.”

    “Mgeni umemuona?”

    “Mgeni gani?”

    “Si yule kaka wa jana.”

    “Wala sijamuona.”

    Hakuongeza neno aliondoka hadi getini kwa mlinzi.

    “Mnyalu kuna mgeni yoyote?”

    “Hataa.”



    “Mnyalu ina maana gari la mgeni wa jana mchana hukuliona?””Sijaona gari wala mtu.”

    “Sasa atakuwa amekwenda wapi?” aliuliza swali bila kujua anayemuuliza hajui lolote.



    “Nani?”

    “Ok, basi.”

    Jeska aligeuka kurudi ndani huku akiamini kabisa mgeni alilala naye chumba kimoja, kingine kilichomchanganya ni sehemu aliyokuwa amelala kwenye chumba chenye hewa na uzuri wa ajabu. Jeska aliamini alichokiona hakikuwa ndoto bali kitu cha kweli.



    Kilichomshangaza zaidi kidoleni pete yake ya uchumba aliyovalishwa na mzee Ezekiel haikuwepo, kila dakika alijikuta akizidi kuchananyikiwa na kila kilichokuja mbele yake. Alizidi kuingiwa na wasiwasi na kujiuliza yule mgeni ni nani ni mtu wa kawaida au jini. Lakini bado hakukubaliana na mawazo yake, alijikuta akiwa na shauku kuonana na mgeni kutaka kumuuliza mambo yanayomtatiza juu yake.



    Asubuhi kama alivyoelezwa na mgeni alikwenda chini ya mto na kuzitoa fedha alizopewa na mgeni za matumizi. Alifunua mto na kuzitoa zile fedha ambazo alinunua vitu muhimu kwa ajili ya chakula cha siku ile. Wazo lilikuwa kumpikia chakula mgeni kama atakuja mchana, lakini hakujua mgeni anakula chakula gani.



    Baada ya kuzigawa pesa kwa ajili ya matumizi ya siku ile, alioga na kufungua kinywa kisha alifanya usafi wa kitanda. Ajabu wakati akiondoa mto ili atandike alishtuka kuzikuta tena noti mpya za elfu tano tano kama alizozitoa asubuhi zipo chini ya mto.



    Alijiuliza zile pesa alichukua au vipi, alitandika na kuzirudisha chini ya mto, alipanda kitandani na usingizi haukuchelewa ulimchukua.





    Aliposhituka alitaka kuhakiki alichokiona ni kweli au alikuwa akiota alifunua tena mto na kuzikuta pesa zipo kweli. Alizitoa na kuzihesabu, hesabu yake ilikuwa ile ile noti mpya nne za elfu tano. Alijikuta akishtuka na kujiuliza iweje pesa zile azitoe kisha alipoangalia alizikuta zipo vilevile.



    Wasiwasi ulianza kumjaa huenda kaka yule si mtu wa kawaida, lakini kilichomshangaza ni upole na ucheshi wake ambaye alionekana ni mtu mwenye huruma sana.



    Alijinyanyua kitandani na kwenda bafuni kuoga alipomaliza kulirudi sebuleni kuangali vipindi kwenye runinga, kengele ya mlangoni ilimfanya ananyuke kwenda kufungua. Alipofungua mlangoni alikutana na kaka msamalia mwema ambaye hakuwahi kumuuliza jina japo yeye alikuwa akilifahamu lake.



    “Ha! Karibu,” Jeska aliachia tabasamu pana.



    “Asante,” ilikuwa tofauti na alivyomzoea akiwa mtu mwenye tabasamu na bashasha muda wote huku akizungumza kwa sauti ya chini na upole. Lakini uso wa mgeni ulikuwa imejaa hasira kitu kilichomtisha Jeska na kutaka kujua kulikoni.



    “Karibu kaka mwema,” Jeska alimkaribisha kwa mashaka kidogo.



    Mgeni aliingia bila kujibu neno na kutembea taratibu mikono nyuma na kumpa mgongo Jeska aliyekuwa akimshangaa baada ya kuketi kwenye kochi alitembea taratibu mikono nyuma na kichwa amekiinamisha kuonekana mtu mwenye maweazo mengi.



    Jeska alikosa la kusema na kuendelea kumsindikiza kwa macho huku akiwa hajui kuna nini, alikwenda kusimama mbele ya ukuta na kutazamana nao bila kugeuka alimwita Jeska.



    “Jeska,” sauti nzito ambayo hakuwahi kuisikia masikioni kwake ilimwita.



    “A..a..be..e..e.” Jeska alijibu kwa kubabaika huku mapigo ya moyo yakimwenda kwa kasi kutokana na hofu iliyomshika moyoni.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kwanini hunisikii?” Mgeni alimuuliza akiwa bado amempa mgongo.



    “Sa..sa..sa..mahani.”



    “Jeska kwa nini unataka kujiua?”



    “Sa..sa..mahani... kaka.”



    “Hujanijibu, unaniomba samahani ya nini?”



    “Nina matatizo yasiyokwisha.”



    “Una matatizo gani?”



    “Sina mtu wa kuyaongoza maisha yangu toka kifo cha baba nimebakwa na niliyekuwa namtegemea amefariki.”



    “Jeska.”



    “A..a..be.”



    “Nilikuambia nini?”



    “Nisijiue.”



    “Hapana Jeska la kwanza kabla ya kukueleza hili?”



    “Utanisaidia.”



    “Sasa kwa nini unakaidi ninachokueleza?”



    “Nisamehe nimekosa sirudii tena,” Jeska alimfuata mgeni na kupiga magoti nyuma yake kwa vile uso wake alikuwa ametazama ukutani.



    “Nimeniomba msamaha mara ngapi?”



    “Najua nimekosa mimi ni kiumbe dhaifu nahitaji kusamehewa.”



    “Jeska ni matatizo gani umeyapata baada ya kifo cha mzee Ezekiel?”



    “Sijapata ila ni wasiwasi wa moyo tu.”



    “Au hupendi msaada wangu nikuache ujiue?”



    “Hapana kaka, wewe ni kiumbe muhimu maishani mwangu naomba usiniache.”



    Mgeni aligeuka na kumnyanyua Jeska aliyekuwa amepiga magoti kuomba msamaha.



    “Basi nyanyuka,” ajabu sauti ile ilibadilika na kuwa sauti aliyoizoea ya chini yenye upole.



    Jeska alishtuka kuuona uso wa mgeni umejaa machozi na fulana yake imelowa kwa machozi.



    Mgeni alimvutia kifuani kwake huku mikono yake laini ikimpigapiga taratibu mgongoni na kumfanya Jeska asisimke.



    “Pole sana Jeska najua umekata tamaa lakini nakuhakikishia kukusaidia na kukulinda kama nilivyokuahidi awali.”



    “Nashukuru kaka mwema , samahani lakini wewe ni nani?”



    “Kwa nini ya muhimu hutaki kufanya unataka kunijua?”



    “Kutokana na matukio ninayo kutananayo naomba uniweke wazi ili nijue niliyenaye si wa ndotoni bali wa kweli.



    Matukioni ninayokutananayo huona kama nipo ndotoni yasiyo na ukweli.”



    “Kwa jina naitwa Lakashi.”



    “Mmh, jina zuri sana.”



    “Asante, ningependa nawe siku moja uitwe Lakashina.”



    “Jina zuri lakini mbona kama la Kihindi?”



    “Kwani mimi Mhindi?”



    “Ila kwa mbali kama mpemba vile?”



    “Ni kweli nina asili ya arabuni, unajua maana ya majina hayo?”



    “Hata.”



    “Lakashi ni mume mwenye huruma.”



    “Na Lakashina?”



    “Mke msikivu.”



    “Kwa hiyo unataka kunioa?”



    “Itabidi nifanye hivyo ili kukuondolea mawazo najua shetani wa kifo bado hachezi mbali na wewe kitu kimenifanya nisicheze mbali na wewe kuyaokoa maisha yako.”



    “Asante Lakashi nakuahidi sitakusaliti nakupenda sana Lakashi.”



    “Nashukuru Lakashina.”



    Walikumbatiana kwa nguvu huku kila mmoja akionesha mapenzi mazito kwa mwenzake.



    Siku ile Lakashi alishinda na kulala pale wakiwa kama wapenzi wa muda mrefu kwa jinsi walivyokuwa. Furaha ya Jeska ilirudi upya na kujikuta akifurahia maisha na kusahau tabu zilizomkabili.



    Usiku wakiwa kitandani wamejilaza kila mmoja alilalia mto wake, Lakashi alimwita Jeska.



    “Lakashina.”



    “Abee.”



    “Napenda uniitikie rabeka saidi yangu.”



    “Rabeka saidi yangu.”



    “Swadakta, ni hivi japo hatujakaa pamoja muda mrefu sikupenda tutengane kwa sasa.”



    “Kwa nini unasema hivyo mpenzi?”



    “Muda wangu wa kukaa na wewe ulikuwa bado kwa vile nina safari ya mbali ambayo itaniweka mbali nawe kwa muda mrefu.”



    “Lakashi safari gani hiyo? Na unasafiri lini?”



    “Usiku huu natakiwa nisafiri, kilichonifanya leo niwe karibu ni kutokana na dhamira yako mbaya. Nimerudi kukuhakikishia kuwa nipo kwa ajili yako na kila nililokuahidi kukusaidia nitafanya hivyo.



    Japo sitakuwepo lakini nakuhakikishia kukurudishia vyote vilivyochukuliwa na baba zako wadogo.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Lakashi mpenzi wangu wewe ni nani, mwanasheria au mpelelezi?”



    “Mimi ni mtu wa kawaida ila ni mtetezi wa haki za watu.”



    “Sasa utaipataje?”



    “Hiyo kazi niachie ila kuna kitu nilisahau kukuambia kuhusu mama Edna, sasa hivi hali yake ni salama.”



    “Lakashi umejuaje?”



    “Lakashina huu si wakati wa kuulizana ni kukujulisha usichokijua, ila nakuonya kitu kimoja usiende kwa kina Edna kufanya hivyo ni kosa kubwa ambalo utalijutia maishani kwako.”



    “Kwa nini Lakashi?”



    “Unajua vizuri kuliko mimi.”



    Majibu ya Lakashi yalimfanya Jeska abakie kimya asihoji lolote, Lakashi aliongeza kusema;



    “Lakashina unafahamu kabisa kifo cha mzee Ezekiel kinatokana na yeye kutoka kwako, uongo?”



    “Kweli.”



    “Sasa unataka kwenda kufanya nini? Pia unakumbuka ulipokutana na Edna alipokuelezea ukamuone mama yake alikuwa mahututi hukuonesha ushirikiano kama kweli familia ile ilikulea. Leo ukienda utawaambia nini?”



    “Basi Lakashi nimekuelewa.”



    “Tuachane na hayo la muhimu usiku huu ni kufunga ndoa ya mimi na wewe kuwa mke na mume.”



    “Lakashi tutafungaje ndoa ya watu wawili bila shehe wala padri?”



    “Lakashina unakubali mimi niwe mumeo?”



    “Hilo halina shaka.”



    “Hujajibu, nakuuliza tena unakubali Lakashi kuwa mumeo?”



    “Nakubali.”



    ”Lakashina hujanijibu vizuri, ngoja nikufundishe, mimi Lakashina nakubali Lakashi kuwa mume wangu.”



    “Mimi Lakashina nakubali Lakashi kuwa mume wangu.” Jeska alirudia kama alivyoelekezwa na Lakashi.



    Lakashi alirudia kumuuliza Jeska mara tatu naye Jeska alijibu mara tatu, baada ya hapo usingizi ulimpitia Jeska.



    Usiku wa manane Lakashi alimuamsha Jeska kumuaga.



    “Mahabuba amka nikuage muda huu ni muafaka wa kuondoka, ila sijui lini nitarudi lakini nakuhakikishia ukiwa na shida na mimi, utaniota ndotoni nami nitatokea na kukufariji kwa lolote utakalo.”



    “Lakashi ndotoni utanitokea vipi nawe haupo?”



    “Niamini kwa hilo, kesho kuna mtu atakuletea pesa za matumizi”



    “Mmh Haya! Nakutakia safari njema.”



    “Asante, ila nakuomba kitu kimoja kuanzia tulipofunga ndoa jina lako ni Lakashina usikubali kuitwa Jeska na wewe sasa hivi ni Muislamu.”



    “Jamani nitaweza masharti ya dini?”



    “Si ngumu utayaweza tu, kuanzia leo vaa nguo za heshima usinywe pombe.”



    “Nitajitahidi.”



    “Kwa heri mpenzi.”



    “Nikusindikize.”



    ‘Hapana usiku ni mkubwa wee lala.”



    Jeska alimvutia kifuani Lakashi kwa muda machozi yalimtoka kisha alimtazama usoni na kusema;



    “Kwa heri mume wangu, nakuomba uwahi kurudi nina imani wewe ndiye mwanaume wangu sahihi. Kwa nini hukusubiri urudi ili tufanye hili?”



    “Ni kweli usemacho dhamira yako mbaya ndiyo iliyosababisha yote haya, la muhimu zingatia, nikirudi nakuhakikishia kukupa maisha nusu ya peponi.”



    “Kwa heri mpenzi wangu, nakuahidi kufanya kila ulilonieleza.”



    Lakashi alimuaga Jeska na kutoka nje, Jeska alibakia amekaa kitandani hata usingizi ulivyompitia hakujua. Aliota yupo kwenye harusi kubwa ambayo hakuwahi kuiona katika maisha yake yote. Yeye akiwa bibi harusi aliyepambwa na kupambika na Lakashi akiwa bwana harusi. Katika harusi hiyo alivishwa pete ya almasi na mkufu wa dhahabu wenye jina la Lakashina.



    Alipozinduka asubuhi alijikuta amelala kitandani kwake shingoni kulikuwa na mkufu wa dhahabu na mkononi pete ya almasi alishtuka.



    Jeska aliishangaa pete ya almasi na mkufu wa dhahabu wenye jina la Kashina, alijiuliza ndoa ile kaifunga saa ngapi, mbona alikuwa kwenye njozi na kuota yupo kwenye ndoa lakini ajabu asubuhi kajiona akiwa na vitu alivyoviona ndotoni.



    “Mmh, hii ina maanisha nini? Au? Hapana bwana huyu huenda ni Jini haiwezekani. Mungu wangu kama nimefunga ndoa na jini itakuwaje...Eeh Mungu nisaidie mimi.” Jeska alisema kwa sauti ya chini huku mkono mmoja kashikilia kifuani.



    “Mmh, kama kweli sijui nitakuwaje?...Mbona kaniaga sijui anakwenda wapi na atarudi lini? Na...na...na nini hatima ya maisha yangu...Mmh! Ngoja tuone!”



    Jeska alijinyanyua kuelekea bafuni kuoga, alijimwagia maji kujitoa uchovu baada ya kuoga alisimama mbele ya kioo kikubwa kujitazama. Juu ya ziwa la kushoto alishangaa kuona kuna maandisha rangi ya dhahabu yenye kumeremeta yaliyokuwa yameandikwa Lakashina.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ilikuwa ajabu ya mwaka kuona maandishi yakimeremeta kama ndani ya mwili wake kuna taa. Alijaribu kufuta kwa mkono sehemu iliyokuwa na maandishi, vidole navyo vilianza kumetameta na hatimaye alijiona mwili mzima ukimetameta na sehemu yenye jina likimeta zaidi.



    Kwa mshtuko alijikuta akianguka chini na kupoteza fahamu, aliposhtuka alijikuta amelala kitandani. Alijishangaa na kujiuliza maswali yasiyo na majibu juu ya kilichomtokea, pete ilikuwa kidoleni na mkufu ulikuwa kwenye droo ya kitanda. Aliiangalia pete iliyokuwa na uzuri wa ajabu lakini hakujua ni madini gani.



    Alipotupa jicho pembeni lilitua kwenye mkufu uliokuwa na jina lake, aliubeba na kuutazama na kulisoma jina na kuurudisha kwenye droo ya kitanda. Alikwenda tena bafuni kuoga ili aende mjini kwa sonara kuulizia ile pete ni ya madini gani na mkufu una thamani gani.



    Baada ya kuoga alisimama tena mbele ya kioo kuangalia alichokiona kilikuwa kweli au ndoto. Jibu lilikuwa lile lile kwenye ziwa la kushoto kuna jina lililoandikwa kwa maandishi ya dhahabu yenye kumetameta. Hakutaka kuhangaika nayo, alirudi chumbani na kubadili nguo ili awahi mjini.



    Kutokana na maandishi yale aliona aibu kuvaa nguo alizozizoea za mikanda na matiti nje. Ilibidi avae za kujistiri mwili ili kuogopa watu kumuona kituko. Alipotoka sebuleni alikutana na mfanyakazi wake wa kike akiwa katika gauni lililonakshiwa uzi wa halili.



    Alipomuangalia alishtuka, lakini Sara hakuonekana kushtuka.



    “Za asubuhi Sara?”



    “Nzuri tu dada Lakasina.”



    “Wee Sara umeniitaje?”



    “Lakashina au ulitaka nikuite Mrs Lakashi.”



    “Nani kakutajia jina hilo?”



    “Dada wewe mwenyewe jana kwenye harusi ulitueleza tusikuite tena Jeska bali Lakasina.”



    “Mmh! Haya.”



    “Safari ya wapi asubuhi asubuhi?”



    “Nafika mjini mara moja.”



    “Ni kweli shemeji amesafiri jana usiku?”



    “Ni kweli wewe umejuaje?”



    “Dada Lakashina mbona kila kitu kwako kigeni au jana ulikuwa unatutania si jina lako?”



    “Ni kweli langu.”



    “Sasa tatizo nini au tuendelee kukuita ulilolizoea la Jeska?”



    “Hapana, kama umeweza kulishika hili jipya ni vizuri.”



    Jeska wakati anajiandaa kutoka kengele ya mlango ililia, alimruhusu aingie alikuwa mlinzi wa mlangoni aliyekuwa amevaa suruali nyeupe na shati jeupe lenye maua shingoni, mikononi na pembeni.



    Juu alivalia kikofia kidogo chenye maua kama ya kwenye shati na suruali, miguuni alivaa makubazi.



    “Mnyalu leo umevaaje?”



    “Dada si unajua tumerudi muda mbaya kutoka kwenye sherehe, nikaona niendelee na kazi zangu baadaye nitabadili.”



    Maneno ya Mnyalu yalizidi kumchanganya na kujiuliza hiyo harusi wao waliijuaje wakati yeye muolewaje ameifunga kwenye njozi. Hakutaka kumshangaa sana, aliona kushangaa kumemchosha kila aliposhangaa walimshangaa yeye.



    “Vipi Mnyalu ulikuwa unasemaje?”



    “Kuna mgeni.”



    “Anatoka wapi?”



    “Sijamuuliza ila alitaka kukuona.”



    “Mwanamke au mwanaume?”



    “Mwanaume.”



    “Mwambie apite ndani.”



    Mnyalu alitoka na baada ya muda alirudi na mgeni aliyekuwa amevalia nguo kama za Mnyalu zilifanana kwa kila kitu hata makubazi aliyovaa. Wazo la haraka alijua ndugu yake Mnyalu.



    “Karibu.”



    “Asante, habari za hapa?” Mgeni alimsabahi huku akimpa mkono Lakashina (Jeska).



    “Nzuri,” Lakashina alimtazama mgeni aliyekuwa amekaa kwenye kochi ameshikilia mfuko mdogo.



    “Pole na pilikapilika za jana usiku?”



    “Nn...nn...nzuri,” kauli ile ilimshtua na kujikuta ni yeye peke yake aliyehudhuria ndoa yake kwenye njozi tofauti na wote waliohudhuria kama kawaida.



    “Mbona kama hujiamini?”



    “Aa...aa...kawaida.”



    “Nina imani una taarifa yangu?”



    “Ipi?”



    “Kutoka kwa Lakashi”



    “Yupo wapi?” Lakasina alishtuka kumsikia Lakashi.

    “Shemu ina maana hujui kama amesafiri?”

    “Jamani mbona mnanichanganya?”



    “Kivipi?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mnasema jana kulikuwa na harusi yangu na Lakashi mbona mimi sijui?”

    ”Shemu hizi piko umechorwa kwa ajili ya nini?”

    ”Mmh! Tuachane na hayo, karibu.”



    “Asante.”



    Mgeni aliketi kwenye kochi na kutulia huku akipepesa macho kila kona ya nyumba ile.



    “Mmh! Shemu karibu.”



    “Asante.”



    “Unatumia kinywaji gani?”



    “Hapana mi si mkaaji niliagizwa nilete huu mzigo mara moja,” mgeni alisema huku akikabidhi mkoba wa ngozi uliokuwa wa saizi ya kati.



    “Asante, na...na...,” Lakashina hakumalizia alichotaka kuuliza.



    “Uliza tu shemeji.”



    “Lakashi kaenda wapi?”



    “Shemeji wewe mke wake usijue nitajua mimi?”



    “Na atarudi lini?”



    ”Bado hilo ni swali gumu kwangu kwa vile siri ya mtu humpa mkewe.”



    “Asante,” Lakashina hakutaka kuuliza kitu kutokana na kumuona mgeni hajui lolote zaidi ya kuleta mzigo alioelezwa na mumewe ambaye yeye anaamini ni wa ndotoni.



    “Lakashi alinieleza nikueleze kuwa, tafadhali mkoba huo usiufungue, ukitaka pesa ingiza mkono na kuchukua kiasi chochote utakacho.”



    “Kwani una shilingi ngapi?”



    “Siwezi kujua ila kanieleza usiufungue huo mkoba wewe chukua kiasi chochote ukitakacho.”



    “Hata milioni?”



    “Si milioni tu hata zaidi ya milioni.”



    “Kwa hiyo hata kununulia nyumba na gari.”



    ”Chochote kasoro pombe na nyama ya nguruwe.”a“Mmh!”



    “Pia alinieleza kuwa usihame nyumba hii mpaka atakaporudi.”



    “Sawa nimekuelewa.”



    “Kingine amesema hivi haina haja ya kwenda kwa sonara kuijua thamani ya vito alivyokuvisha siku ya harusi yenu. Kwa vile vina thamani kubwa kuliko mtu utakaye mpelekea. Kibaya zaidi tamaa yao itakusababishia matatizo makubwa hata kukutoa uhai wako.”



    “Ha! Shemu amejuaje?”



    “Amesema muhimu ni kufuata maelekezo na si kujua amejuaje.”



    “Sawa shemu, nimekuelewa.”



    “La muhimu kuzingatia yote kama utakwenda kinyume utajiingiza kwenye matatizo ya kujitakia.”



    “Nimekuelewa.”



    “Nikuache, vipi unatoka?”



    “Hapana.”



    Mgeni aliaga na kuondoka huku Lakashina akibakia na maswali juu ya yale aliyoelezwa. Alijiona kama mtu aliyetembea uchi wakati kavaa nguo kutokana na Lakashi kumfahamu kila alilokuwa akiwaza. Alijikuta akijiuliza Lakashi ni nani. Aliubeba mkoba wake na kwenda kuuweka chumbani ndani ya kabati na safari ya kwa sonara ilikufa.



    ***



    Maisha ya Lakashina yalibadilika ghafla ya kujikuta akiishi maisha mazuri na ya kifahari. Alinunua magari ya kifahari ya kutembelea, nyumba aliyokuwa akiishi mwenye nyumba alimuuzia na kuwa yake. Siku moja akiwa amejipumzisha sebuleni baada ya kutoka kuswali simu yake iliita alipoangalia ilikuwa namba ngeni alipokea.



    “Haloo.”



    “Haloo Jeska.”



    “Mimi siitwi Jeska.”



    “Mbona aliyetupa namba alituambia wewe ni mtoto wetu Jeska.”



    “Wewe nani?”



    “Mimi Zebedayo baba yake mdogo na Jeska.”



    “Aah, kumbe ni ninyi, mnataka nini wakati mliyofanya sikutaka kuwapeleka kokote tafadhalini achaneni na mimi. Najua mmejua nina pesa mumeanza kunifuata tena ili mnidhurumu, lakini sasa hivi nitakufa kwa mali yangu.”



    “Siyo hivyo Jeska.”



    “Siitwi Jeska naitwa Lakashina.”



    “Hilo jina kama la Kihindi au umebadili dini?”



    “Ndiyo.”



    “Sasa ni hivi tunaomba utupe muda ili tuikusanye mali yako tukukabidhi.”



    “Muikusanye ili iweje? Nimewafuata kuwaomba?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hapana mama, ile ni mali ya wazazi wako lazima tukurudishie wewe mwenyewe.”



    “Mliponinyang’anya si mliona ni haki yenu na kunitishia kuniua sasa mnanitaka nini tena?”



    “Hapana mama tupo chini ya miguu yako, tunakuomba tukurudishie mali yako.”



    “Sipo tayari kuipokea nimewaachieni, endeleeni na maisha yenu nami niacheni niendelee na maisha yangu.”



    “Jeska, ooh, samahani Lakashina, tunaomba uipokee tupo chini ya miguu yako.”



    “Jamani niwaeleze mara ngapi kuwa mali hizo sina shida nazo, ni miaka mingapi imepita, hamkujua nimeishi maisha gani, hamkunionea huruma mwana yatima baada ya uchungu wa kifo cha wazazi wangu ninyi ndiyo mliotakiwa kunitunza kwa vile tayari wazazi wangu waliacha mali. Lakini kwa tamaa zenu mlinitupa na kunitishia maisha yangu.



    Sikwenda polisi wala mahakamani nilimshtakia Mungu, leo hii mmekumbuka nini? Naomba muachane na mimi, “ Lakashina alikumbuka mambo mengi ilikuwa sawa na kuchubua kovu lililokuwa limepona. Alijikuta akishindwa kuzungumza na kuangulia kilio.



    Simu ile ilimtia hofu Lakashina kuona muda si mrefu mali zake zitachukuliwa na baba zake wadogo, aliizima simu ili wasiendelee kumsumbua. Wazo la haraka lilikuwa kutoiwasha mpaka atakapobadili namba ya simu. Alijiuliza ni nani aliyempa namba yake ya simu.



    Akiwa bado anatafakari kuhusiana na simu za ndugu wa baba yake watu ambao kwake aliamini ni maadui na kuapa kutowasamehe mpaka anaingia kaburini, simu yake iliita tena, alishtuka na kuamini kabisa labda hakuizima, hakuipokea mpaka ilipokata. Aliichukua ili aizime lakini cha ajabu simu ilikuwa imezimwa, aliiangalia mara mbili na kuhakikisha ameizima.



    Haukupita muda simu iliita tena, alishtuka na kuitazama kwa muda akijiuliza ni kweli au anaota. Iweje simu aizime itoe mlio wa kuita huku ikitetemeka kama haikuzimwa.



    Japo miujiza aliianza kuizoea lakini ule kidogo ulimtisha, hakutaka kuipokea aliitazama iite mpaka inyamaze yenyewe. Lakini simu haikunyamaza iliendelea kulia kwa muda mrefu. Kila muda mlio uliongezeka na kufanya hahisi ngoma za masikio kutaka kupasuka. Aliamua kuipokea na kusema kwa sauti ya juu.



    “Nimesema sitaki.”



    “Sikiliza Lakashina,” sauti ya upande wa pili ilikuwa nzito iliyoufanya moyo wake kwenda mbio.



    “Siwezi kukusikiliza nimewaambia sizitaki hizo mali nani kawaomba?”



    “Wampelekee nani?”



    “Watajua wenyewe.”



    “Lakashina naomba ufuate maelekezo yangu,” sauti ile nzito iliyokuwa ikijirudia kama kwenye mwangwi ilimchanganya na kuamini lile ni jambazi lilitumwa kuchukua mali zake. Kutokana na kutetemeka kwa hofu iliyomjaa moyoni simu ilimponyoka, lakini sauti ile iliendelea kusema na kuonekana kutawala chumba kizima;



    “Lakashina hofu ya nini?”



    “We...we...eee nani?” Aliuliza kwa kitetemeshi.



    “La muhimu sikiliza maelekezo yangu, washa simu na kubaliana nao kuhusu kurudishiwa mali zako, ni halali yako wala usimuonee huruma mtu yeyote. Kama wao hawakukuonea huruma basi nawe usiwaonee huruma hata kidogo.”



    “La...la...kini...we...e...we...e nani?” Lakashina aliuliza kwa hofu.



    “Lakashinaaa, nikueleze mara ngapi usipende kuuliza, fuata maelekezo yangu washa simu.”



    “Wewe ni nani, Lakashi?”



    “Huwezi kunijua kutokana na hofu iliyokujaa moyoni, la muhimu chukua mali yako. Lakashina washa simu...washa simu.”



    Sauti ile ilipotea taratibu huku ikijirudiarudia ikitoka katika uzito na kuwa nyepesi iliyokuwa kama ikimbembeleza Lakashina aliyepitiwa na usingizi, mfanyakazi aliyekuwa amemtuma aliporudi alimkuta amesinzia.



    “Dada...dada.”



    “Mmh.”



    “Vipi?“



    “Aah, kwani vipi?”



    “Naona umelala huku ukitabasamu na kutikisa mguu unaota upo kwenye muziki nini?”



    Lakashina aliposhtuka, alimuangalia mfanyakazi aliyekuwa amerudi toka dukani alipomtuma.



    “Dada vipi mbona kama unanishangaa?”



    Kabla ya kumjibu aliitazama simu yake aliikuta imezimwa, alimtazama Sara aliyekuwa amesimama mbele yake akimtazama. Alijinyoosha na kupiga miayo kisha alimuuliza.



    “Eti Sara umekuja saa ngapi?”



    “Mmh, muda ila mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani ikanibidi nisubiri labda una kazi zako, baada ya muda mlango nilisikia ukifunguliwa na kujua umemaliza shughuli zako. Nilipousukuma niliukuta upo wazi, lakini cha ajabu nimekukuta umelala mkono kifuani ukitabasamu na mguu ukiuchezesha.”



    “Sara unasema kweli?”



    “Kweli, kwani vipi?”



    “Mmh, tuachane na hayo, ulipokuwa nje hukusikia sauti yoyote?”



    “Mmh, palikuwa kimya kama nyumba haina watu, kama usingenituma au mtu angekuja siku ya kwanza angeamini nyumba haina mtu. Kilichonifanya niamini kuna mtu, muziki wa kiarabu unaopenda kuupiga.”



    Lakashina alitulia kwa muda akitafakari ya nyuma kabla hajatokewa na sauti ya ajabu ndani ya simu aliyoizima baada ya kukerwa na kauli za baba zake wadogo kutaka kumrudishia mali zake walizomdhurumu muda mrefu na kumtishia kumuua. Lakini sauti ya ajabu ilimsisitiza awashe simu.



    “Dada upo sawa?” Sara alimuuliza.



    “Nipo sawa, ila kuna watu wanataka kunichanganya...,” alinyamaza ghafla baada ya simu kuita tena, si yeye hata Sara aliiona, lakini ilikatika. Hakusema kitu aliichukua simu ile na kuiwasha. Baada ya kuiwasha hazikupita hata sekunde kumi iliita kwa mlio aliouzoea. Aliipokea kwa unyenyekevu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Haloo,” alisema huku akimuonesha kwa ishara Sara atoke nje, Sara alitekeleza bila kuhoji.



    “Haloo Lakashina tupo chini ya miguu yako tunaomba tukurudishie mali zako, tunakuomba utuombee msamaha vitu vingine hatuna.”



    “Jamani mbona siwaeleweni niwaombee msamaha kwa nani?”



    “Kwa mumeo.”



    “Mume wangu? Nitawaombea vipi naye kasafiri?”



    “Atarudi lini tunateseka tuonee huruma, mateso tunayopata ni makubwa.”



    “Mateso gani?”



    “Tumekuwa watu wa kipigo kila kukicha ili turudishe mali zako.”



    “Kipigo! Toka kwa nani?”



    “Mumeo, tena amekuwa akitufuata ndotoni na kutusumbua turudishe mali zako zote bila kuacha kitu chochote.”



    “Ina maana bila kupata kipigo msingenirudishia mali yangu?”



    “Hapana Jeska...ooh samahani Lakashina tulikutafuta muda mrefu bila mafanikio, lakini sasa hivi mali zote zimekatika, sasa hivi maisha yetu yamekuwa ya kubahatisha.”



    “Sasa mimi niwafanyeje?”



    “Muombe mumeo atusamehe au atupe muda tuitafute.”



    “Mmh, mimi sina neno labda mwenyewe.”



    “Basi mwambie umetusamehe ili atuache.”



    “Nitamwambia akirudi.”



    “Amekwenda wapi?”



    “Sijui.”



    “Atarudi lini?”



    “Sijui.”



    “Lakashina mtumie ujumbe hata kwa njia ya simu kumueleza umetusamehe ili kutupunguzia mateso.”



    “Mume wangu sijawahi kumuona na simu hata siku moja, na muda huu hayupo.”



    “Basi akija nitamueleza kuwa umetusamehe.”



    “Mmh! Sawa.”



    Baada ya simu kukatwa Lakashina alijikuta akijawa na mawazo juu ya kauli za baba zake wadogo waliomdhulumu mali yake. Moyoni alikuwa radhi kuwasamehe, aliamini mali ile isingewafikisha popote. Lakini alikumbuka kauli ambayo hakujua ni ya nani iliyomuelekeza awashe simu na kuikubali mali yake yote na asiwaonee huruma hata kidogo.



    Lakashina aliamini kama ni mali yake, alikuwa na uwezo wa kusamehe hata kuigawa kwa mtu aliyempenda. Hakuona umuhimu wa kung’ang’ania kulipwa mali asiyokuwepo. Akiwa katika lindi la mawazo simu yake iliita, aliipokea.



    “Asalamu aleykum,” Lakashina alisalimia.



    “Waleyku musalam,” sauti nzito ilijibu upande wa pili na kumfanya Lakashina ashtuke na simu kumponyoka, lakini sauti ilisikika kama ameweka ‘loud speaker’.



    “A..a..abee.”



    “Lakashina nani kakuita, acha kujitia hofu usipokuwa na kosa.”



    “Sa...sa...wa,” alijibu kwa kutetemeka.



    “Lakashina.”



    “Abee.”



    “Tuliza moyo wako kabla hatujazungumza lolote.”



    “Nimetuliza,” Lakashina alisema huku akijiweka vizuri kwenye kochi na kufuta mikono usoni kujipa ujasiri.



    “Lakashina,” Sauti ile nzito ilimwita tena.



    “Abee.”



    “Umetulia?”



    “Ndiyo.”



    “Vizuri, umewasikia baba zako wadogo?”



    “Ndiyo.”



    “Wamesema wataleta lini mali yako yote?”



    “Mmh, wameomba niwaombee msamaha kwa vile mali yote hawana kwa sasa.”



    “Lakashina hakuna kitakachobadilika mali yako inatakiwa mara moja.”



    “Wamesema tuwape muda.”



    “Ha...ha...ha...he...he...he...ee,” sauti ilicheka sana mpaka ikamkera Lakashina.



    “Lakashina,” sauti ilimwita baada ya kicheko.



    “Abee.”



    “Unataka tugombane?”



    “Hapana.”



    “Sasa nisikilize, nakuomba hiyo mali iletwe mara moja, mbona wao hawakukusubiri mpaka upate akili ndipo wakudhurumu...Lakashina,” sauti ilijirudia kama mwangwi.



    “Hii ni amri na siyo ombi, nataka uwakaripie wakuletee mali yako mara moja, kila kitu walichochukua warudishe. Hawakukuonea huruma wakati unamatatizo kwa nini unawasamehe. Kilio chako ndicho kilichofanya niitafute mali yako na kukupa maisha mazuri. Kama hutafanya hivyo adhabu yao itakurudia wewe.”



    Sauti ile ilinyamaza ghafla na kumfanya Lakashina azidi kuchanganyikiwa, sauti ya adhana ndiyo iliyoufanya moyo wake utulie. Alinyanyuka na kwenda kutia udhu kwa ajili ya swala ya adhuhuri. Alipomaliza kuswali alirudi sebuleni kujipumzisha simu iliita tena moyo ulimpasuka, aliichukua na kuzungumza.



    “Asalamu aleykum.”



    “Lakashina, mama wewe pekee wa kuiokoa familia yako, bila huruma yako tunateketea wote,” sauti ya upande wa pili iliyoambatana na kilio pili ilikuwa ya baba yake mdogo.



    Lakashina alishindwa awajibu nini, huruma ilimjaa moyoni lakini onyo alilopewa muda mfupi lilimtisha kwa kuhofia maisha yake. Alijikuta akiporomokwa na machozi na kukosa la kuwaeleza baba zake wadogo.



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Lakashina huruma ilimjaa moyoni jinsi baba zake wadogo walivyokuwa wakilalamika mateso waliokuwa wakipata kutoka kwa mumewe. Pamoja na kulazimishwa kuchukua mali zake bado aliona kuna umuhimu wa kusimama yeye kama yeye kuwatetea baba zake wadogo.



    Alikumbuka siku moja ndotoni aliyaona maisha ya tabu ya baba zake wadogo baada ya kumdhulumu mali yake. Alijikuta akiwahurumia wao badala ya kuwachukia na asubuhi alipoamka alikosa raha kabisa.



    Alijifikiria kama ni kweli baba zake wadogo ndivyo walivyo, kwa muda ule hakukuwa na haja ya kuwalazimisha warudishe mali zaidi ya kuwasamehe.



    Akiwa bado anabubujikwa na machozi huku upande wa pili wa simu ukiendelea kuomba msaada wake kuwaokoa na mateso. Aliwasikia wakisema;



    “Mama siku hizi hatulali ni mateso mtindo mmoja ili turudishe mali yako, japo tunajua tuna kazi ya kurudisha vitu vyote.



    Basi mtupe muda, nasema laana yako kwetu ilikuwa kubwa kwani baada ya kukufukuza haikupita muda tukaanza kugombana wenyewe kwa wenyewe na kufikia uamuzi wa kuuza sehemu kubwa ya mali, hata pesa tulizogawana iliyeyuka bila kufanya jambo lolote la maana.



    “Lakashina tunakuomba utusamehe tunajua tulikutenda, lakini hakuna tulichopata toka kwenye mali ya wazazi wako zaidi ya dhambi na mateso.”



    Maneno yale yalizidisha kuumiza moyo wa Lakashina kuona jinsi gani dhuluma ilivyo na malipo mabaya. Machozi yalimtoka bila kizuizi kila alipotaka kuzungumza alikosa maneno zaidi ya kuendelea kulia.



    Ghafla sauti ya upande wa pili ilibadilika na kuwa nzito, haikuwa ngeni tena masikioni kwake wala hakuishangaa, aliisikiza ina ujumbe gani tena.



    “Lakashina...Lakashina,” sauti ilijirudia kama mwangwi zaidi ya mara tatu.



    “Moyo wako unaonekana kabisa unataka kuniudhi, sitaki ubadili uamuzi wangu.”



    “Siwezi...siwezi.”



    “Lakashina huwezi nini?”



    “Nasema siwezi.”



    “Sikia Lakashina najua kabisa unataka kuwahurumia baba zako wadogo viumbe wasio na huruma, kama huwezi niachie hiyo kazi mimi watarudisha tu.”



    “Watatoa wapi?” Lakashina alijikaza na kujibu.



    “Hiyo hainihusu, watapata mateso mpaka wanaingia kaburini.”



    “Hapana...hapana.”



    “Hapana nini?”



    “Nasema tena hapana.”



    “Huwezi kuzuia hasira zangu huenda zikakurudia wewe.”



    “Sawa...sawa na zinirudie, lakini nakuomba uwaache kama mateso uliyowapa yanatosha na mali hawajarudisha.”



    “Hapana Lakashina hata siku moja mwanamke hana kauli kwa mumewe.”



    “Ha! Kumbe ni wewe mume wangu Lakashi?”



    “Si muhumu kujua.”



    “Kama si muhimu kujua nakuomba uachane nao mara moja.”



    “Unanishurutisha?”



    “Ndiyo, kama mali zako chukua niache na maisha yangu ya mateso,” Lakashina alijibu kwa ujasiri mkubwa.



    “Lakashina ujasiri huo umeutoa wapi?”



    “Si muhimu kujua.”



    “Lakashina,” sauti nzito ilimuita, lakini hakuitikia aliendelea kulia kuonesha hasira zake zipo kwa yule mtesaji asiye na chembe ya huruma.



    “Lakashina umekasirika?”



    Hakumjibu aliendelea kulia kilio cha kwikwi, kifua kikiwa kimefura kwa hasira, alijiegemeza kwenye kochi. Mkono laini uliokuwa ukimpapasa shingoni ukifuatiwa na manukato aliyoyazoea yalimfanya anyanyue uso. Alishtuka kumuona mumewe Lakashi katika uso wa tabasamu.



    “Laazizi unalilia nini?”



    “Unajua, unajua Lakashi,” Lakashina alilia kilio cha kwikwi.



    “Kuhusu nini?”



    “Mimi nani yako?”



    “Mke wangu.”



    “Kwa nini hutaki kunisikiliza?”



    “Kuhusu nini?”



    “Baba zangu wadogo.”



    “Ni hilo tu mpenzi?”



    “Ni hilo, pia ni maisha gani ya kutishana.”



    “Nani kakutisha?”



    “Sijui nani kanipigia simu amesema kama nikiwasamehe basi nitamtambua.”



    “Asikutishe, mwenye mamlaka juu yako ni mimi mumeo na si mwingine.”



    “Na aliyekuwa akizungumza ni nani?”



    “Achana naye ila nakuahidi baba zako hawataguswa tena na ikiwezekana nitawabadilishia maisha yao.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Asante mpenzi,” Lakashina alitabasamu na kumkumbatia mumewe kwa furaha.



    Aliposhtuka alijikuta amelala kitandani peke yake na kujiuliza yaliyotokea ilikuwa ndoto au kama kweli mume wake kipenzi yupo wapi ila harufu ya manukato ilitawala chumba kizima.



    Lakashina alitoka hadi sebuleni, lakini hakumuona mtu. Milango ilikuwa imefungwa kama alivyoifunga ila manukato ya Lakashina yalitawala kila kona. Hakutaka kumuuliza mtu kwani alijua mumewe alirudi kwa ajili ya kutuliza akili lakini hakurudi rasmi.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog