Search This Blog

Monday 20 June 2022

SITAISAHAU FACEBOOK - 5

https://pseudepigraphas.blogspot.com/2019/11/sitaisahau-facebook.html

Simulizi : Sitaisahau Facebook

Sehemu Ya Tano (5)


John alikuwa ananiona? Nilijiuliza.Lile joto likazidi. Abiria wakashuka garini.Kuna kitu hapa!! Mapambano mapya!! Nikajisemea huku nikiendelea kumzuia John.John sasa akanizidi nguvu.Akanitoka. Akashuka chini. Nikajaribu kumkimbilia.Huko nikamkuta akiwa anafanya jambo la ajabu. John alikuwa anajarfibu kuisukuma gari kwa kuitikisa.Ajabu! Ikaanza kutikisika kweli. Mtikisiko ule ukawashtua wengi. Sasa vilio vikaanza kusikika. Kila mtu kuitetea nafsi yake.Watu wakashuka upesi kwa kugombania mlango. Basi likaanguka.Lilipoanguka John akatazama mahali. Na mimi nikageuza jicho kutazama. Yalikuwa makaburiMakaburi yaliyo na historia ya kushangaza. Makaburi ambayo yalimtoa nishai mchina alipojaribu kupitisha umeme juu yake. Umeme ukagoma kuwaka.Haya yalikuwa makaburi ya Kiyeyeu.Yalikuwa yanafuka moshi wa dhahabu!!Vita!!Mayowe yakatawala, akinamama wakiwa wamesahau watoto wao na wanaume nao wakiwasahau wake zao sasa kila mmoja alikuwa akiipigania nafsi yake. Sikuwa katika umoja na akina Jesca tena! Hapa sasa kila mwenye macho hakungoja kuambiwa tazama!!Makaburi yale mawili yaliendelea kufuka ule moshi wa rangi ya dhahabu.Wenyeji wa kijiji kile walikuwa katika taharuki kubwa sana huku wakizungumzia juu ya kukasirika kwa mizimu.Nani sasa aliyeikasirisha? Walijiuliza.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Vilio vilisikika tena kutokea gizani. Watu wakakimbilia huko. Waliporejea ilikuwa taarifa ya mama mmoja aliyekuwa anakimbia ameshambuliwa na kitu kisichofahamika na hatamaniki tena. Amekufa!!Hali ikatulia kwa muda. Akajitokeza mzee mmoja wa makamo akitembea kwa kutumia mkongojo.Huyu hakuogopeshwa hata kidogo na hali iliyokuwa inaendelea. Alisimama mbele ya kundi na kuanza kusema anachokifahamu, alielezea historia fupi ya makaburi ya Kiyeyeu na majanga yanayotokea iwapo wazee wale waliolala katika makaburi yale wakikerwa na jambo. Hapa sasa akafikia kusema kuwa kuna mtu mmoja katika msafara alikuwa ameikasilisha mizimu!!Ni lazima abaki ili kuwanusuru wenzake. Kama akiendelea mbele basi litatokea balaa kubwa zaidi ya hili. Alizungumza kwa sauti ya juu na kila mmoja aliweza kusikia. Sauti yake na umri wake vilikuwa vitu viwili tofauti!!“Hivyo kama unajua una lolote la kuikera mizimu hii ni heri ubaki nyuma kuwanusuru wenzako.” Alizungumza kisha akatuachia mtihani wa kuamua aidha kujitokeza ama la!Maneno yake niliamini kabisa yalikuwa yanamlenga John. Nilijisikia uchungu sana, John alitakiwa kubaki nyuma. Yaani harakati zangu zote hizo zinaishia hapa!! Niliumia sana.Niliangaza huku na huko. Sikumuona John!! Nilitaka kumuita lakini niliamini kuwa hawezi kunisikia.Kimya kilitawala akisubiriwa mtu huyo ambaye ameikera mizimu aweze kujitoa kundini. Hakuna aliyejitokeza.Mzee akaendelea kusubiri!! Bado hakujitokeza mtu yeyote.Kimya kilikatishwa na sauti ya mwanaume akipiga mayowe. Tukageuka nyuma kumtazama. Alikuwa amejishika shingo yake huku akipiga kelele. Mara damu zikaanza kumtoka puani, masikioni na mdomoni. Badala ya kumsaidia kila mtu akawa anamuogopa!!Hatimaye akaanguka na kutulia tuli! Alikuwa amekata roho!!Kina mama wakapiga kelele sana, wanaume wakabaki kushangaa.Yule mzee wa kimila akaipaza tena sauti yake, “Kama asipojitokeza mtu huyu majanga yataongezeka. Mizimu inakasirika.”Sasa watu wakaanza kusemezana huku wakisisitizana kuwa mtu huyu ajitokeze ili mizimu itulie. Bado hakuweza kujitokeza mtu yeyote.Zikaanza kutolewa hirizi miilini mwa watu, lakini yule mzee wa kimila akapinga kuwa hizo ndio tatizo.Waliokuwa na dawa za kienyeji wakatoa. Bado haikuwa tiba.Kiza kinene kikatanda kama dalili ya mvua. Mwanga mkali ukamulika bila kutoa kelele. Watu watatu wakasalimia na ardhi.Ilikuwa radi!! Na walikuwa maiti tayari.Roho ikaniuma sana, nikajiona mimi ndiye muhusika. Nikatamani John atokezee nimtangaze kuwa ndiye chanzo. Lakini John hakuwepo tena!!Vile vifo vya radi ya ghafla vilimshtua kidogo yule mzee.Mara akabadilika sura na kuwa kama aliyekasirika!!Akatoa amri ya watu kujipanga msitari. Amri ikasikilizwa. Wanaume na wanawake mstari mmoja, mistari ilipopangwa ndipo nilimuona John. Na yeye alikuwa amepanga mstari. Akaanza kupita na kufanya kile anachokijua mwenyewe. Alimfikia John, na yeye akamuona akamshika mkono. Ina maana John anaonekana? Nilijiuliza.Nikiwa katika hali ya mashaka ya kila kinachoendelea. Mara yule mzee mkongwe alinifikia, alikuwa anatabasamu, mgongo wake uliopinda ulimfanya awe ameinama na kuwa mfupi sana!!“Shkamoo babu.” Nilimsalimia.“Marahaba mjukuu wangu.” Alinijibu kwa ukarimu sana.Kisha akanishika mkono.Alipofanya hivyo kwa wasafiri wengine hakutumia muda mrefu, lakini kwangu ni kama alitumia sekunde nyingi.“Unaitwa nani binti.”“Isabela!!”“Nani alikwambia unaitwa Isabela.” Aliniuliza huku akinitazama usoni.“Naitwa Isabela mzee.” Nilitaharuki kutokana na maswali ya mzee huyu.“Hilo sio jina lako binti.”“Sio jina langu?”“Na litakugharimu sana na kuwaumikza wengine katika maisha yako.” Kauli nzito za mzee huyu zilinishangaza.Isabela sio jina langu? Ni miaka zaidi ya ishirini tangu nipewe jina hilo. Sasa leo ananiambia kuwa hilo sio jina langu? Maajabu haya.“Hautaendelea na safari hii…kuwaepusha wenzako na mabalaa yasiyowahusu.” Alininong’oneza. Nikahisi ubaridi ukinipenya mwilini, mapigo ya moyo yakapungua kasi. Nikakata tamaa.Mimi tena? Sio John!! Maajabu haya.“Kama unao upendo waruhusu wenzako waende zao. Janga lako haliwahusu hata kidogo.” Alinisihi. Nikatikisa kichwa kukubali. Huku nikiamini kwa asilimia kadhaa kuwa tatizo ni John na yule mzee hajui kitu.Mzee akawatangazia watu kuwa tatizo limekwisha. Na kweli nilipokubali tu waondoke zao. Nilipogeuka makaburini. Ule ukungu haukuwepo tena.Abiria wakaingia katika basi lile la ziada lililokuja kutuchukua.Tofauti na mawazo yangu. Kuwa John atazuia basi lisiondoke baada ya yeye pia kuwa mmoja kati ya abiria. Haikuwa hivyo. Basi liliwaka vyema. Na kutoweka!!Ilikuwa usiku mnene lakini kinyume na taratibu za usafiri Tanzania, basi lile lilisafiri usiku. Hayakusikika malalamiko ya kubanana tena. Kila mmoja alitaka kutoweka eneo lile. Hata madereva na makondakta wote walikuwa waoga.Nilibaki na yule babu!!! Akina Samson, Jesca, na Jenipher walitaka kubaki na mimi lakini kwa maneno ya yule babu kuwa mzigo wangu hauwahusu. Niliwaruhusu waende zao huku nikiwapatia pesa nyingine ya ziada.“Nendeni mkautangaze ushuhuda huu popote pale. Msifiche hata moja lililotokea. Hata kama sitafika huko mtakapokuwa. Naamini sisi ni washindi.” Niliwaeleza. Wakalia kwa uchungu. Samson akagoma kabisa kuondoka lakini hatimaye alikubali kuondoka.Nilibaki na mzee yule tukizungumza. Alinieleza juu ya jina langu. Akadai kuwa hakuwa akijua nilikuwa naitwa nani lakini Isabela halikuwa jina langu.“Rejea nyumbani ukalitafute jina lako. Jina lako limepotea ama limefichwa. Na ukiendelea kuamini kuwa wewe ni Isabela basi maisha yako yatakuwa ya tabu sana. Utawatesa wenzako nawe utateseka sana.” Alinieleza yule babu.“Unaweza kwenda kupumzika nyumbani kwangu. Kesho upatafute nyumbani kwenu. Ukalitafute jina lako.”Tuliongozana na yule mzee hadi nyumbani kwake. Hapo tulipokelewa na mbwa wengi sana waliomlaki bwana huyu kwa furaha.Wahehe na mbwa!! Niliwaza.******Nililala katika mkeka. Ni kama nililala kwa sekunde kadhaa hatimaye pakapambazuka.Mzee akaniamsha, akanisihi sana nihakikishe Napata jina langu halisi na hapo nitaendelea na maisha yangu vizuri.“Jina langu ni nani?” nilijiuliza kwa sauti akanisikia.“|Hata mimi silijui lakini ni lazima ulipate ili kuzikwepa laana za ukoo wako. Fuatilia historia yako vyema mwanzo hadi mwisho. Historia ya kweli ipo kwa mama…kamuulize mama yako. Wewe ni nani? Lakini nakukumbusha kuwa wewe sio Isabela”Mzee alinisindikiza hadi njia ya mabasi.“Usizungumze na mtu yeyote, kwa usalama wako na abiria wenzako.” Alifanya kunisemesha kwa sauti hafifu. Nikamsikia na kumwelewa.Basi likapita. Nikapanda!! Mzee alinilipia nauli huku akichukua fursa ya kuzungumza na kondakta.Safari ya kurejea Makambako. Safari ya kwenda kulitafuta jina langu. Jina lililopotea.Kaka aliyekuwa pembeni yangu alikuwa anaongea maneno mengi sana. Lakini sikuwa namjibu chochote.Hatimaye tukaifikia Makambako!! Nikashuka garini nikaikanyaga ardhi ya Makambako kwa huzuni sana!! Hatua kwa hatua nikaanza kuelekea nyumbani.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/SIRI SIRINIMwanamke wa makamo ambaye sasa mvi zilikikaribia kichwa chake chote alikuwa anafagia uwanja. Alikuwa akiimba nyimbo anazozijua yeye huku akionekana kuzifurahia. Nilimtazama kwa makini. Nikatamani ningekuwa nimekuja kwa mazuri huenda ningemshtua kisha tukacheka wote. Lakini nilikuwa nimekuja kwa mengine magumu sana.Huyu alikuwa ni mwalimu Nchimbi. Mama yangu mzazi.Nikanyemelea. Akashtuka akageuka.“Belaaa….Belaaa mwanangu.” Akautupa ufagio, akanikimbilia, akanikumbatia kwa nguvu. Joto lake likaupenya mwili wangu ulio dfhaifu. Nikaamini kuwa nilikuwa nimemkumbuka sana. Chozi likanitoka. Nikamkumbatia kwa nguvu zaidi.“Karibu mwanangu…mbaya wewe..yaani kimya kimya au uliongea na Suzi..wabaya sana nyie.” Alilalamika nikajilazimisha kutabasamu.Tuliingia ndani. Tukafanya mazungumzo ya hapa na pale. Hadi tulipokatishwa na nyimbo nyingine kutoka kwa mlevi. Huyu alikuwa baba yangu mzazi. Asubuhi sana alikuwa anatokea kilabuni.Sijui alilala huko? Nilimuuliza mama./“Hamna sema ameamkia huko.”“We Helena wewe…Aaah!! Suzy..ina maana haunioni uje kunipokea…si ku hizi hamsalimii watu!!” alizungumza kilevi. Macho yake hayakumwezesha kujua iwapo mimi ni Isabela.Akapita akiacha nyuma harufu ya pombe kali. Akaingia chumbani.Baada ya kelele za hapa na pale akasikika akikoroma!!!Nilijikaza sana na sasa nikaamua kumueleza mama kilichonileta pale nyumbani.“Mama hivi hili jina la Isabela ni nani alinitungia.”“Mbona wauliza hivyo mwanangu.”“Nipe jibu mama..ama ukoo wangu ni upi.”“We mtoto umekuwaje lakini.”“Nijibu mama.”“Mbona kila kitu kipo wazi..ukoo wako ni huu wa baba yako, na jina hilo ni mimi na baba yako tulikupatia.” Alinijibu.Niliondoka sebuleni nikaenda chumba cha wasichana nikajinyoosha. Nikapitiwa na na usingizi.Nilikuja kushtuka nikiwa na njaa kali.Nikaliendea jiko.Nikajihudumia vilivyokuwepo, kisha nikareje chumbani.Majibu ya mama yalikuwa hayajaniridhisha hata kidogo.Nitamuuliza baba pia!! Huenda kuna kitu anajua.Kwa nini aliniita Isabela.Nikasinzia huku nikiwa nimejiahidi hivyo kichwani mwangu.*****Asubuhi na mapema nilikuwa wa kwanza kuamka. Nilihitaji kumuwahi baba akiwa katika akili zake vyema kabisa.Kabla hajalewa!!Niliwahi na kujifanya naosha vyombo.Hatimaye nikasikia mlango wa chumbani unafunguliwa. Baba akatoka.“Aaah!! Bela mwanangu…lini tena umetuvamia wewe…umemaliza mitihani lakini.”“Nimemaliza..shkamoo baba….”`aliijibu salamu. Tukabadilishana mawazo na hatimaye kama kawaida yake akaniomba pesa.“baba kabla ya hilo…nahitaji kukuuliza kitu.”Alinisikiliza kwa makini, nikamueleza kile nilichomueleza mama. Baba alionekana kushtushwa na habari hiyo. Alijaribu kujiweka sawa lakini nilikuwa nimemsoma.“Fanya hivi…nipatie hiyo pesa nikirejea tutaongea ni stori ndefu kidogo..si unataka kujua maana ya Isabela na kwanini tulikuita hivyo..nifanyie kwanza nienda kupata supu kidogo.” Alijaribu kukwepesha mada.Niliheshimu maamuzi yake. Nikaingia ndani nikarejea na pesa kidogo nikampatia. Akatoweka.Moyoni nilipata matumaini makubwa sana!! Niliyaamini yale maneno ya yule mzee.Sasa mimi ni nani kama sio Isabela? Na kuna siri gani inazunguka hapa. Nilijiuliza. Wa kunijibu alikuwa ni baba.Nilisubiri sana. Hadi pale ilipokuja taarifa kuwa baba amekutwa mtaroni. Hana jedraha lakini haijafahamika bado kama anapumua ama amekufa!!Hii ilikuwa ni habari ya kushtua sana.Mimi na mama tukakimbia kuelekea hospitali ambayo tulielezwa kuwa amelazwa.Bahati mbaya zilikuwa mbio za kuwahi upepo.Baba yangu hatukuwa naye tena!! Kifo cha utata. Hakuwa amelewa. Alikutwa na ile pesa niliyompa.Hakika mimi sio Isabela, na kuna siri mzee wangu amekufa nayo!! Nilizungumza na nafsi yangu.Jina langu ni nani sasa? Na kwa nini waliniita Isabela?****Ulikuwa msiba wa mtu maskini hata utata ungegubika vipi bado angezikwa na kusahaulika. Ndivyo ilivyokuwa kwa baba yangu.Licha ya kifo chake kuwa na utata hapakuwa na la ziada alitakiwa kuzikwa.Msiba huu ulivuta watu wengi kiasi kutokana na jina la mwalimu Nchimbi ambaye ni mama yangu. Mwalimu!! Hivyo wanafunzi walijaa sana.Historia fupi ya marehemu ilisomwa.“….marehemu ameacha mjane na watoto wanne..mmoja wa kiume na watatu wa kike….Sebastian John, Suzan John, na Helena John.” Alimaliza kutaja majina ya watoto wa marehemu.Sauti za kuguna zukatawala ghafla, watu wakawa wanaulizana hao watoto wanne mbona hawajatimia? Kina mama wakashindwa kumezea wakauliza palepale.Ujumbe ukamfikia msomaji baada ya kijana mmoja kuagizwa.Msomaji akaanza kupekua hapa na pale. Kimya kikatanda!!!“Anaitwa Isabela John huyu hapa.” Shangazi yangu alipaza sauti akanitambulisha ili kuondoa ile sintofahamu. Nikanyoosha mkono juu. Watu wakageuka na kunitambua.Tendo lile la watu kugeuka kuniangalia likanifanya nipatwe na aibu kidogo. Inakuwaje mimi jina langu linasahaulika?Sikuuliza!!! Nikauchuna.“Kwa hiyo mtoto wa nne ni Isabela John….samahani sana kwa mkanganyiko huu.” Aliomba radhi yule msomaji. Waungwana hawakulalamika.Alipotaka kuendelea kusoma yanayoendelea katika risala hiyo akawa anatawaliwa na kigugumizi. Hali hii sasa ikaanza kuwakera watu. Lakini kabla hili halijapita akaanza kupiga chafya.“Samahani!” akaomba radhi tena.Haikukoma, ikaongezeka chafya ya pili, mara ya tatu ya nne, chjafya mfululizo. Akaachia lile karatasi lililoandikwa risala. Hali ikaonekana dhahiri kuwa si nzuri!!Akajikunja kunja huku akionekana kuzitafuta pumzi zake. Mwili ukakosa muhimili akaanguka chini.Wale waliokuwa na ghadhabu sasa ikawalazimu wakimbilie kutoa msaada. Msoma risala akatulia akiwa amejishika kifuani. Akafanana na ile maiti ya baba iliyopo katika jeneza.Baadhi ya wanaume wakamchukua garini.Tuliosalia tukaendelea na taratibu nyingine, hatimaye tukazika. Watu walikuwa wanajiuliza kimemsibu nini yule bwana. Hakuna hata mmoja aliyeweza kutoa majibu hata mimi pia nilikuwa katika sintofahamu.Siku iliyofuata asubuhi na mapema la mgambo likalia. Msoma risala alikuwa amepoteza maisha!!!*****Suala la baba kuondoka na siri kubwa aliyotakiwa kunieleza lilikuwa ni jambo lililoutafuna sana mwili wangu. Nilikuwa najiuliza bila kufikia muafaka.Maisha yaliendelea. Chuo kilikuwa kimefungwa jijini mwanza na nilikuwa nina kumbukumbu kuwa niliomba ruhusa maalumu kabla ya mitihani haijaanza. Hivyo nilitakiwa sasa kufuatilia iwapo mtihani umekaribia ama la.Nilitafakari nani wa kumuuliza. Nikamkumbuka Maria. Nilijilazimisha kuamini kuwa yale ya mimi kumuona katika pori nchini Zambia zilikuwa ni ndoto tu.Nikajaribu kuvuta kumbukumbu za wapi nimewahi kuhifadhi namba yake sikupata jawabu. Hilo nalo likawa tatizo.Nikafikia uamuzi wa kwenda katika huduma za internet cafĂ© sio mbali sana kutoka nyumbani kwetu. Wakati huo sikuwa na nywele kichwani hivyo nilikuwa nimejitanda ushungi.Nilifika kwa wakati muafaka nikapata nafasi, nikatazama yaliyonipeleka kisha nikalipia huduma ile.Wakati nasimama niweze kutoka nikagonganisha macho yangu na mtu ambaye niliamini kuwa haikuwa mara yetu ya kwanza kuonana. Alikuwa ni msichana mnene. Nikavuta kumbukumbu lakini sikulipata jina lake.“Mambo…” nilimsalimia, akatabasamu kisha akanijibu.“Ujue nilidhani nakufananisha. Nilikuangalia wakati unaingia ujue nikahisi nimekufananisha.”“Na mimi hivyo hivyo!!” nilimuunga mkono.Tukasogea nje na kupiga stori za hapa na pale.Wakati wa kuagana ndipo tukakumbuka kuulizana majina.“Naitwa Isabela.”“Mh!! Isabela!! Ulibadilisha jina ama..maana nakumbuka walikuwa wanakuita nani vilee.” Alijaribu kuvuta kumbukumbu. Mimi nikawa namtazama tu! Nilibadilishaje jina sasa mimi.“Hata sijabadili mbona.” Nilimwelewesha. Akazidi kupinga.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Hatukufikia makubaliano, akapigiwa simu akaniaga huku akisisitiza kuwa nimemdanganya jina. Mimi sio Isabela.Nilimsindikiza kwa macho hadi akatokomea. Nilijitazama iwapo nilifanana na mmoja kati ya ndugu zangu lakini hakuna niliyefanana naye ambaye ningeweza kumtupia lawama kuwa watu wananifananisha naye.*****Kile kitendo cha yule dada kuonekana kana kwamba amenifananisha kisha akakataa kuwa jina la Isabela si la kwangu nilikipuuzia na kumchukulia yule dada kuwa amepoteza kumbukumbu zake kwa kuwa miaka imepita mingi sana.Nilivyotoka pale moja kwa moja nikaenda nyumbani kwa dada Suzi kwani tangu nirejee Makambako sikuwa nimeenda kumsalimia mume wake na familia kwa ujumla zaidi ya kukutana msibani.Nilimkuta yupo nyumbani akiwa na familia yake jikoni wakiandaa chakula.Alinipokea vyema tukasalimiana kisha nikataka kumsaidia kupika.“Kuliko kunisaidia kupika ni heri unisaidie kumbeba huyu mwanao.” Alizungumza huku akijitoa mtoto aliyekuwa amembeba mgongoni. Nikampokea na kumbeba.Ghafla mtoto akaanza kulia taratibu kisha anaongeza kilio.“He! Haka nako lini tena kameanza kuchagua watu.” Nilimuuliza dada. Hakunijibu zaidi ya kuguna akimaanisha kuwa huenda ni jambo la kawaida.“We dogo wewe..mama yako mdogo huyo.” Alisema akimaanisha kumweleza yule mtoto mdogo wa mwaka mmoja. Japo hakumuelewa.Mtoto akazidi kutoa kilio.“Hebu mchukue mwanao nadhani ana kisilani cha usingizi.”Nilimkabidhi dada Suzi mtoto wake, cha ajabu hakunyamaza zaidi ya kuongeza kulia. Sasa Suzi akashtuka na kulichukulia uzito hili suala ambalo mwanzo ulikuwa kama mzaha fulani hivi. Alimkagua mwanae kama amechubuka mahali. Hakuna kitu!Huenda basi ameumwa na mdudu, hata hilo pia halikuwepo!!!Mapishi yakakoma kwa muda. Mtoto analia kwa sauti ya juu sana. Machozi yanamtoka kwa wingi mno. Hatari!!Ilianza dakika moja na sasa zilikuwa zinatimia sitini, yaani saa zima bila kilio kukoma. Mtoto alikuwa analia sana.Majirani wakakisikia kilio hicho kikuu wakajongea pale nyumbani kwa Suzi. Na wao pia wakashangaa.Suzi akajaribu kumpa titi mtoto aweze kunyonya, akalikataa. Kila mmoja alijaribu kumbeba bila mafanikio.Kimbilio lililofuata likawa hospitali.Huko napo hapakuwa na nafuu yoyote. Madaktari walimfanyia uchunguzi na kurejea na majibu yasiyoridhisha hata kidogo. Walisema kuwa mtoto hakuwa na ugonjwa wowote ule. Hivyo hawakuwa na msaada wowote ule.Tulirejea nyumbani. Tulipofika huku kila aliyetazama tukio hili akiwa katika mfadhaiko wa hali ya juu na kuegemeza imani zao katika mambo ya kishirikina. Ni hapa na mimi nilijishtukia na kuanza kuamini kuna jambo. Lakini jambo lenyewe ni mimi!!Niliamini kuwa ni mimi baada ya kuyakumbuka maneno ya yule mzee kule Iringa. Aliyeniambia nisipofuatilia jina langu basi nitasababisha majanga mengi sana popote nitakapokuwa.Usiku mzima mtoto alikuwa analia. Na kama hiyo haitoshi mara mkono wake wa kushoto ukaanza kujikunja. Suzi naye akawa analia sasa maana hakuwa na njia nyingine.Baba wa mtoto alipigiwa simu akiwa safarini kuelekea Songea akalazimika kuhairisha safari, mama yetu alikuwa hapo nyumbani pia.Suzi alikuwa Amelia sana na alikuwa amewaacha walokole wenzake wakimwombea kwa namna zote mtoto yule. Lakini hali iliendelea kuwa tete.Mtoto huyu akifa itakuwa juu yangu!! Niliwaza na kufikia maamuzi.Dada Suzi alikuwa mtu pekee ambaye angeweza kunisaidia katika hili. Maana tayari tulikuwa tunamtambua kuwa alikuwa mwanamke wa kipekee aliyeweza kuhifadhi siri nzito nzito.Huenda hata siri aliyokufa nayo baba nayo angeweza kuwa nayo!! Nikarusha karata yangu.Nikamfuata dada Suzi nje alipokuwa amekaa chini ya mti akilia kwa juhudi zote.“Da Suzi.” Nilimuita, akageuka akanitazama na macho yake mekundu yaliyovimba kutokana na kulia kwa muda mrefu.“Nahitaji kuzungumza nawe dada.”Alinitazama tena bila kusema lolote.“Kuna jambo nahisi….”“Nini?”“Naweza kuwa najua chanzo cha tatizo hili.”Suzi akageuka mzima mzima akanitazama kwa umakini kabisa akisubiri niseme neno.Sikuwa na haja ya kumueleza kuwa ile ninayotaka kumwambia ni siri, nilikuwa namuamini sana.“Suzi…” nilianza kumuelezea kwa kirefu na mapana juu ya maisha niliyopitia, nikamueleza juu ya ile mimba ya maajabu ambayo mwisho wake ulikuja baada ya kukatwa ilea lama ya 666 katika makalio yangu, nilimueleza pia juu ya Dokta Davis na pesa zake haramu, ndoto za maajabu zote pia nilimuelezea.Dada Suzi alinisikiliza vyema sana nilipokuwa namueleza juu ya makaburi ya Kiyeyeu huko Iringa na jinsi nilivyokutana na babu nisiyemfahamu aliyenieleza kuwa jina la Isabela sio jina langu. Natakiwa kulitafuta jina langu.Alishangazwa na kukwama kwa basi letu hadi pale niliposhuka mimi, kifo cha mwanaume aliyekuwa anasoma risala ya marehemu baba pia alishangaa nilivyomweleza kuwa yawezekana ni moja ya majanga niliyoyasababisha.“Hata baba alikuwa ameniahidi kunieleza jambo fulani lakini ajabu kabla hajaweza kunieleza ametutoka. Nahisi ni yaleyale. Najua dada yangu hauamini mambo haya lakini niamini mdogo wako.”Nilimsisitiza na ili kumfanya aamini tuliingia ndani nikamfunulia kovu langu. Hapo sasa aliweza kuniamini.“Kwa hiyo mwanangu anaweza kufa pia.” Aliniuliza kwa wasiwasi.“Sijui nisemeje lakini kiukweli naogopa sana…” nilimjibu.“Sasa Bela mimi nafanyaje hapa katika hili.”“Dada kama unaweza kujua lolote lile kuhusiana na mimi tafadhali nieleze tumuokoe mtoto. Hana makosa hata kidogo.” Nilimsihi Suzi. Kilio cha mtoto kilikuwa juu kama kilivyoanza na alikuwa anazidi kujikunja mkono.Suzi alinitazama usoni kama anayesoma kitu fulani kwangu.“Bela…yapo baadhi ninayoyajua….nitakueleza, sio kwa imani za kishirikina hapana!! Nakueleza kwa kuwa ni lazima uyajue. Kama mwenyezi Mungu amenipa pigo hili ili nikueleze siri hii basi nakueleza. Lakini jitahidi kuwa na moyo mgumu.” Nilianza kutetemeka kwa maneno hayo ya dada, hakika nilikuwa namuheshimu kwa kuwa na siri nzito nzito.Kabla ya kunieleza aliniongoza katika sala. Nikamfuatisha hadi alipomaliza.Sasa uwanja ukawa wake nami nikawa katika zamu ya kusikiliza.“Siri hii hata aliyenieleza hajui kama alinieleza.”“Kivipi?”“Mzee alikuwa amelewa siku hii. Na pesa ya kulewa nilimpa mimi. Baada ya kulewa akawa anasemezana nami kwa njia kama ya kupitiwa ama hajui anazungumza na nani.”Nikakubali kwa njia ya kichwa.Suzi alinielezea juu ya upendo wa baba kwa mama yangu ulivyomlazimisha kufanya jambo hili la ajabu. Tendo la kuiba mtoto na kumpatia mama bila yeye kujua.“Aliiba mtoto…kivipi?”“Baada ya mimi kuzaliwa mama alizaa mtoto mwingine, akafariki dunia akiwa tumboni. Siku chache kabla ya kuzaliwa. Baada ya hapo akashika mimba nyingine tena. Alipojifungua tu mtoto akafariki tena.” Alinieleza dada Suzi, taarifa ile ya pili ikanisisimua kuliko ile ya kwanza, maana nilikuwa naifahamu hiyo kuwa iliwahi kutokea. Hii ya pili sikuwa naifahamu.“Baba akazungumza na manesi, akawapatia pesa nyingi ambazo ziliwafanya wasahau wajibu wao. Wakakiuka maadili wakaiba mtoto na kumpelekea mama halafu yule mtoto aliyekufa akapelekwa wanapojua wao.”“Kwa hiyo mama alipozinduka?”“Akajikuta ana mtoto wa kike….akaamini ni mtoto wake wa kumzaa.”“Kwa hiyo mama anajua kuwa hayo yalitokea?” niliuliza kwa hamaki.“Si yeye wala ndugu mwingine anayefahamu jambo hili. Kama nilivyokwambia hata mimi baba alinieleza akiwa amelewa.”“Sasa huyo mtoto mwingine yupo wapi sasa hivi? Na anaitwa nani jamani”Ndiye huyu mbele yangu, anaitwa Isabela.”Nilipiga yowe la mshtuko!! Suzi akawahi kuniziba mdogo na kunikanya kuwa niwe mtulivu kama kweli nimeamua kuichukua siri hiyo. Nikajilazimisha kutulia.“Isabela…wewe sio mtoto wa familia hii ya mwalimu Nchimbi, mimi sio dada yako wa damu, mwalimu sio mama yako na hata marehemu pia hakuwa baba yako.” Alisema Suzi huku akiwa amenitazama usoni moja kwa moja. Nikashtushwa na kauli hiyo. Nilitegemea kuwa Suzi atabadili kauli hiyo huenda amesema kimakosa, lakini hakubadili.Mapigo ya moyo yakaenda kasi sana!! Nikatamani ile iwe filamu na itamalizika baada ya muda fulani. Lakini hali ikaendelea kuwa kama ilivyo.“Dada Suzi, kwahiyo mimi…eeh!” nilikuwa nimepegawa.“Hiyo ndiyo siri Isabela. Haya je inahusika kwa namna yoyote na tatizo la mwanangu???”“Dada yawezekana kweli yahusika sana. Kwa maana hiyo mimi sio Isabela. Hili jina alinipa nani.”“Baba na mama….namaanisha mwalimu Nchimbi na marehemu mume wake.”“Basi mimi sio Isabela. Mama yangu na baba yangu watakuwa wapi Mungu wangu!!” nilijiuliza huku nikijikuna kichwa changu pasipo kuwashwa.Wakati najikuna kichwani zikarejea zile kumbukumbu za kudekezwa sana na mwanamke huyu ambaye sasa naambiwa kuwa sio mama yangu. Upendo wa dhati alionionyesha tangu nikiwa mdogo ulizidi kunifanya kimya kimya nipingane na kauliza dada yangu. Lakini ule uwezo wa dada kutunza siri ulinirejesha kuamini kuwa ule ni ukweli.“Kwa hiyo inakuwaje.” Alinishtua Suzi na kunifanya nikumbuke kuwa tulikuwa na tatizo.Natakiwa kulipata jina langu na ukoo wangu!! Nilimwambia Suzi.*****CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Kama ilivyokuwa kwangu ndivyo ilivyomuwia mwalimu Nchimbi ugumu sana kuweza kuamini alichokuwa anaelezwa na dada Suzi. Alimanusuru azimie kama zisingekuwa jitihada za dada Suzi kulegeza maneno makali na kuyafanya laini.Hatimaye mama aliyekuwa mbishi kipindi chote cha maziungumzo alikubali kwa shingo upande kuwa mimi sio mwanaye.Kwa kuokoa maisha ya mtoto wa dada Suzi ambaye alikuwa analia mfululizo tuliamua kwa pamoja kushirikiana kulitatua tatizo hili.Hospitali!! Hapa ndio tulianzia kumtafuta mama yangu. Ilikuwa hospitali ya serikali na ni miaka mingi sana ilikuwa imepita. Kila kitu kilikuwa kimebadilika, hakuwepo wa kuweza kutusikiliza na kutusaidia.Mtoto akiwa amebaki nyumbani, sisi tukiwa katika hekaheka hizi ndipo mama alipokuja na wazo la kumwendea mkunga ambaye alimzalisha. Mama alikiri kumkumba mama huyo ambaye ni mstaafu tayari.Hakuna aliyelalamika kuhusu kuchoka. Tulitembea kwa miguu. Tulipofika maeneo ambayo mama alihisi kuwa ndipo anaishji yule mkunga tulianza kuulizia. Ilituchukua muda mfupi tu kuweza kuyapata makazi yake.“Ameenda sokoni lakini atarudi muda si mrefu.” Msichana tuliyemkuta pale nyumbani alitujibu.Tukajiweka katika mkeka tulioukuta pale nje na kumsubiri.Kama tulivyoelezwa mama huyo mkongwe kiasi alifika, kwa kumtazama alionyesha kuwa ujanani alikuwa mrembo sana lakini mwenye maringo.Licha ya uzee huo bado alikuwa na maringo kiasi katika sauti yake.Alitukaribisha huku akiwa amesimama kwa namna ya kutusikiliza shida yetu ni ipi.Kila mmoja akamwachia mama jukumu la kuzungumza.“Naitwa mama Isabela au …” kabla hajamaliza kujitambulisha ilisikika sauti kutokea dirishani, “Shakamoo mwalimu!!”“He! We ni nani tena unanisalimia umejificha…” alisema mama kwa kitetemeshi cha ualimu.Yule mkunga akasaidiana nasi kutazama mlangoni. Akatoka msichana kwa makisio ni umri wa miaka kumi na moja.Akamsalimia mama kwa kupiga magoti.Kabla ya kujibu mama akaanza kuvuta kumbukumbu.“Eliza….nimekosea!!!” alimkumbuka jina lake kwa usahihi.“Mjukuu wangu huyu, kumbe ni mwanafunzi wako.” Yule mkunga aliyekuwa amesimama akasema huku sasa akikaa. Mwanafunzi yule akawa ameujenga urafiki kati yetu.Tukakaribishwa ndani!!!Baada ya utambulisho mama alianza kujielezea juu ya jambo lililotuleta. Alianzia mbali sana hadi akalifikia lengo letu.Mama yule kwanza, alishtushwa na taarifa hiyo kisha akasema kuwa hajui lolote kuhusu tukio hilo.“Kwa hiyo una uhakika kuwa nilizaa mtoto na akawa hai?” mama alimuuliza akiwa amemkazia macho. Mkunga akawahi kukwepesha macho yake, nikamsoma na kugundua anatudanganya.“Sikumbuki..ujue nimewazalisha akinamama wengi sana…hakika sikumbuki.” Alijitetea huku akiwa na hofu.Aliusimamia uongo wake huo hadi pale nilipoamua kuyaingilia mazungumzo haya, hasira ilikuwa imeanza kunitawala.Nikarusha karata yangu!!!“Mama mimi nadhani nimpigie simu yule baba aliyeshuhudia tukio hili, najua nikimpigia atakuja na yule askari. Kwa hiyo tutaufahamu ukweli.”Yule mama akatowa yowe la hofu huku akizungumza kikabila cha kwao, hakika alitaharuki kusikia polisi.“Mwanangu…usipige simu subiri tunayazungumza haya yanaisha.”Uwanja ukawa wake akazungumza.Kama dada Suzi alivyosimuliwa na marehemu baba juu ya uwepo wangu katika familia ile ndivyo ilivyokuwa kwa nesi huyu ambaye mara kwa mara alitusihi tuyamalize kindugu.“Na mama yangu ni yupi?” nilimuuliza ghafla akashangaa.“Sikuelewi unaniuliza mimi au?”“Ndio nakuuliza wewe…..mimi ni huyo mtoto azliyeibiwa.”Akakodoa macho yake kwa hofu. Nikaiskia hasira ikinichemka sana nikatamani kumrukia.“Kwakweli mimi sijui labda Gloria ndio atakuwa anafahamu.”“Gloria ndio nani?” mama alimuuliza.“Tulikuwa naye..huyo ndiye aliyenishawishi.*****Hatukupoteza muda, tulimpa nafasi kidogo ya kujiandaa tukaondoka kuelekea kwa huyo aliyemuita Gloria. Haikuwa safari ndefu sana, tulitumia taksi.Na yeye tulimkuta vilevile akiwa yupo katika uzee.Baada ya salamu mbili tatu. Moja kwa moja ikawa zamu ya yule nesi kumueleza mwenzake juu ya tukio la miaka zaidi ya ishirini iliyopita.Kama ilivyokuwa wakati tunamueleza na yeye alileta ujanja wa kutaka kumruka mwenzake lakini alipothibitishiwa kuwa akileta udanganyifu yupo shahidi na polisi pia. Naye akanywea!“Tunachohitaji kujua ni kitu kimoja tu!! Mama aliyeibiwa mtoto ni nani.” Nilikoroma kwa hasira. Suzi na mama wakawa wakimya.“Ni Dina….Dina yule…..”“Dina ni nani na anakaa wapi.”“Dina ni kichaa…eeh! Mungu nisamehe mimi nisamehe…” alianza kulia yule mwanamke.” Hakuna aliyembembeleza.Neno lake la kuwa Dina ni kichaa liliniacha njia panda, ina maana mama yangu ni kichaa na anaitwsa Dina? Hapana haiwezi kuwa!!! Nilipinga kimya kimya.Baada ya kutulia tena akatueleza juu ya kichaa aliyepewa mimba miaka mingi iliyopita. Mimba iliyotaka kuchukua uhai wake kwa sababu ya kukosa matunzo. Ilikuwa kama bahati diwani wa kata hiyo ambaye alikuwa mwanamke alipata kukutana na kichaa huyu. Wakati huo mimba ilikuwa na miezi saba. Huruma ilimshika kutoka na na imani yake ya kiroho..”“Ooh!! Jesus jesus!!” Suzi alinong’ona huku akiwa kama anasali.Akaendelea yule mama. “Basi akafika mwenyewe hospitali na kutoa amri ya mwanamke yule kusaidiwa. Hatua za haraka zikachukuliwa. Mwanamke akaanza kukamatwa kinguvu na kupelekwa kliniki. Baadaye akafungiwa kabisa bila kutoka hospitali. Hatimaye miezi tisa ikatimia akajifungua bila kufanyiwa upasuaji. Mtoto wa kike!!!!Wakati anajifungua mtoto huyu ndipo ilipatikana biashara hii ya kuiba mtoto. Hakika hali ilikuwa ngumu sana kiuchumi. Utawala wa serikali ya awamu ya kwanza ulikuwa umechachamaa sana hivyo kwa pesa tuliyotangaziwa na yule kijana ambaye simkumbuki jina mimi na mwenzangu hatukuweza kuikataa.Pia tuliamini kuwa yule kichaa asingeweza kumlea mtoto wake. Hivyo kwa huruma tukamchukua yule mtoto na kumuuza.”Simulizi ile ilinisisimua sana!! Nilikuwa natetemeka kwa kila neno alilotamka yule mwanamama. Nilijihisi kama nusu mwanadamu nusu nimekufa!!Kimya kikatanda. Kila mmoja akiwaza lake. Mimi nikizidi kuamini maneno ya mzee yule wa Iringa. Kuwa lile halikuwa jina langu na wala haukuwa ukoo wangu.“Mama yangu yupo wapi?” hatimaye niliuliza.“Kwa kweli ni siku ya nne hivi sijamuona lakini huwa anapatikana stendi na majalalani.” Nikasisimka tena kusikia maneno haya. Mama yangu anaishi majalalani!!!Niliumia.Hapakuwa na jipya tena kwa pale. Kwa kuwa huyu mama alikuwa anamtambua Dina ilimlazimu kuzunguka nasi siku nzima kumtafuta.Siku ya kwanza hatukufanikiwa kumuona.Siku ya pili majira ya mchana baada ya kuzunguka siku nzima bado kimya. Tukapewa taarifa za juu juu kuwa aliingia katika gari ya kwenda Mbeya.Huo ukawa mwanzo wa safari nyingine.“Tulimshusha Uyole.” Kondakta alitueleza baada ya kufanikiwa kulipata lile gari alilosadikiwa kupanda mama yangu.Wakati huu nilikuwa mimi na mama pamoja na yule mkunga. Dada Suzi alirejea nyumbani kwa ajili ya kulea mtoto ambaye sasa kilio kilikuwa kinapungua na kidogo alikuwa ananyonya.Safari ya kwenda Mbeya ikafuata. Tukaweka kituo Uyole. Kama vile chokoraa tulianza kuzurura huku na huko bila mafanikio. Yule mkunga ndiye aliyekuwa anaulizia mara kwa mara maana ni yeye alikuwa anaujua muonekano wa huyo Dina.Siku mbili Uyole bila mafanikio. Mama alikuwa amechoka dhahiri lakini asingeweza kusema, nadhani kwa kuwa aliamini nipo katika matatizo pia ni kama mwanaye wa kumzaa, maana hata titi lake nilikuwa nimenyonya.Siku ya nne inakuja habari nyingine kuwa Dina alionekana sokoni. Asubuhi na mapema tukafunga safari kuelekea Uyole sokoni.Tulisubiri kwa masaa kadhaa.Kelele za akina mama zilitushtua, walikuwa wanahangaika huku na huko kutaka kushuhudia jambo huku wengine wakiwa wanakimbia.“Yule pale Dina!!” mkunga alipiga kelele huku akitujelekezea kwa kidole.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Mwanamke mnene, akiwa na malapulapu mwilini alikuwa akiwaponda watoto na mawe. Huku akiwa na fimbo mkononi. Alikuwa anajongea eneo la soko. Jambo hilo liliwapagawisha akina mama na sasa walikuwa wanapiga kelele.Nilimtazama mwanamke huyu anayesadikiwa kuwa ni mama yangu. Mara ghafla nikajikuta nipo wima, nikakimbia mbio mbio. Umati ulikuwa unashangaa na hata mwalimu Nchimbi alibaki kunitazama tu asijue la kufanya.Macho yetu yalipogongana nikaona kitu!!Ni kama kioo mbele yangu na nilikuwa najitazama.Damu nzito kuliko maji!!!Sikuogopa mawe aliyoshikilia, mavazi yake machafu!!Nikamsogelea na kumkumbatia.Maajabu!! Na yeye akanikumbatia huku akizungumza kabila nisilolielewa. Kimya kikuu kikatawala!!Hakuna aliyetusogelea.“Mama!!” nilinyanyua kinywa changu na kumuita!!“Su…Subira…..” aliniita kwa mshangao.Alipotaja jina hilo. Nikajikuta kama nasukumwa chini. Nikaanguka kama mzigo.Nikajikuta katika filamu ya ajabu huku mimi nikiwa wa ajabu zaidi.Nilikuwa napambana na mamia ya watu. Na sasa nilikuwa ana kwa ana na Dokta Davis. Alikuwa ananiogopa sana, nami sikuwa na huruma. Nikiwa na panga kubwa mkononi. Nilimkaribia na kumfyeka.Nikatazama maadui wengine wanaonikabiri na wao nikawatenda nilichomtenda Davis.Likafuata pambano kuu la kupambana na joka la maajabu.Lilinisumbua lakini kila liliponijeruhi na mimi niliondoka na kipande kimoja cha mwili wake.Pambano lilikuwa kali hadi walipotokea viumbe weupe sana wakaniweka kando kisha wakalimaliza joka.Kisha wakakiteketeza kijiji kile cha maajabu. Lakini cha kushangaza mimi sikuungua kabisa.Moto ulipokwisha nikajikuta nimesimama peke yangu. Uchi wa mnyama. Nilikuwa nimechoka na nilikuwa natokwa jasho.Ule ujasiri niliokuwanao ukayoyoma na sasa nikawa naogopa.Mara ghafla…”Mamaaaaaa!!” nikapiga kelele kubwa na kutaka kukimbia.Nilipojaribu kufanya hivyo nikakabiliana na kamba ngumu zikiwa zimeifunga mikono yangu na miguu. Nilikuwa natokwa jasho sana.Niliangaza huku na kule bila kupata majibu.Mara kundi la watu likafika pale chumbani.Wote walikuwa wakinishangaa. Nikamuona mwalimu Nchimbi.“Mama ni nini hiki…mbona nimefungwsa hivi.” Niliuliza huku nikiwa nashangaa.Mwanaume mmoja nisiyemtambua akaanza kunielezea juu ya vurugu nilizokuwa nafanya licha ya kupigwa sindano ya usingizi.“Ni ugonjwa wa kushangaza sana.”Alinielezea tukio zima la kuanguka baada ya kukumbatiana na kichaa ambaye alitoweka pia baada ya mimi kuanguka.“Mama yangu!!” niliwaza!! Kisha nikatabasamu na akili ikiwa imerejea sawia.Nilipofunguliwa kamba niliwaelezea juu ya yote yaliyokuwa yananikabili katika maono yangu ya ajabu.“Nimeikamilisha kazi!!!” hatimaye nilitamka hayo.Tulikuwa hospitali ya mkoa ya Mbeya. Baada ya siku nne niliruhusiwa kuondoka. Niliambatana na mwalimu Nchimbi.“Naitwa Subira!!” nilimweleza mama.“Najua!!” aliniambia, nikashangaa.“Umejuaje.”“Ulisisitiza sana wakati ukiwa umepoteza fahamu zako.”Nilitabasamu naye akatabasamu.*******Mtoto wa dada Suzi alikuwa halii tena japo mkono wake ulibaki kuwa vile umejikunja.Amani ikautawala moyo wangu!!!Taarifa pekee iliyoniumiza ni juu ya kifo cha mama yule kichaa aliyekufa baada ya kugongwa na gari.Japo nilipata nafasi ya kusikia neno moja tu kutgoka kwake lakini alikuwa amenisaidia mengi mno.Familia yangu ilimzika kwa heshima zote kama ndugu.Baada ya kuyaweka haya yote pembeni niliirejesha akili yangu jijini Mwanza.Mama alikopa pesa nikasafiri kurejea chuoni.Safari ilikuwa njema sana.Maria akawa mwenyeji wangu jijini Mwanza. Akanielezea juu ya yote yaliyotokea. Hapakuwa na lolote baya, zaidi ya maajabu ya kanisa fulani kudai limemtoa John msukule kutoka gamboshi.Nilitabasamu na kukiri kuwa dini imegeuka biashara. Lakini sikumwelezea Maria juu ya yote tuliyoyapitia.“Jesca na Jenipher je?” nilimuulizia na kutegemea jibu la maajabu tena.“Kumbe mwenzangu na wao hawakufa..eti vilizikwa vinu badala ya watu!! Dunia ina mambo.” Alijibu.“Kwa hiyo bado wapo chuo.”“Hapana hawapo kwa sasa. Lakini Jesca yupo mtaani.’“Amakweli dunia ina mambo…” nilimuunga mkono.Maria hakujua lolote lile kuhusu yaliyonisibu mimi. Na alikuwa kama anayenifahamisha juu ya yaliyotokea huku akiamini kuwa ile ruhusa niliyoomba ndio iliyonifanya nitoweke ghafla.“mwenzangu na mimi siku moja sijui nikaota madudu gani. Wacha nipagawe..” Maria alinisimulia alichokiota na kilikuwa sawa na kilke kichotutokea msituni.Maria hakujua kama ni kweli alikuja kule msituni!!!“Nilipiga kelele wewe nikamuita Mungu, mama na mizimu yote!!” aliendelea kusimulia.Baada ya mazungumzo hayo marefu. Niliingia kuoga.Baada ya kuoga nikiwa katika kutafuta nguo ya kubadilisha nikakutana na kadi ya benki. Nikaitazama huku nikiweka mbali kabisa tamaa.Nilipokuwa nimebadilisha nguo, nikaanzisha moto mdogo nyuma ya nyumba na kuviteketeza baadhi ya vitu ambavyo nilihisi vitakuwa vinanikumbusha juu ya Dokta Davis. Nilitaka kuiteketeza kadi ya benki pia lakini nikakumbuka kuwa ilikuwa pia kwa ajili ya matumizi ya chuoni. Nikaghairi zoezi hilo.******Baada ya wiki moja nikapata fursa ya kukutana na John!! Nilikutana naye akiwa anaelekea kanisani.“Bwana asifiwe dada..Bela.” alinisalimia huku akionekana kutokumbuka lolote.Nikamjibu, tukabadilishana naye mawili matatu. Akaenda zake huku akinisihi kuwa akitoka kanisani atanitafuta.Niliondoka pale nikiwa natabasamu na kujipongeza kwa vita ile kuu ambayo nimeibuka kuwa mshindi. Vita ambayo nimepoteza kipande kidogo tu cha nyama yangu lakini kwa ukombozi wa mamia ya watu..kutoka katika milki ya Shetani na chapa yake ya 666.Japo sikutaka tena kurejea katika mtandao huo lakini nilikiri kwa kila neno la lugha ninayoifahamu kuwa kamwe SITAISAHAU facebook.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/MWISHO

SITAISAHAU FACEBOOK - 4

https://pseudepigraphas.blogspot.com/2019/11/sitaisahau-facebook.html

Simulizi : Sitaisahau Facebook

Sehemu Ya Nne (4)


“Kwani mtu akifa anakuwaje?” aliniuliza, sikujibu.Akaendelea, “hebu tuachane na hayo..msichana mdogo kama wewe ukifa sio vizuri ujue.”“Kama ukiwa makini hautakufa. Tena wewe hautakufa, nitakusaidia usife sawa!!”“Sawa!!” nilijibu kwa nidhamu kubwa.“Njoo huku…”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Nikamfuata hadi mahali patulivu kabisa. Sasa hii ilikuwa ofisi kweli. R.I.P akanipokea. Akaniacha ofisini kwa muda, kisha akaingia tena baada ya dakika kadhaa.Hakuwa yule tahira, hakuwa mchafum,chafu kama nilivyokueleza mwanzoni. Huyu alikuwa na hadhi ya yule mvulana ninayemuhitaji. Alikuwa mtanashati.Hakuwa akicheka hovyo! Alikuwa makini na mtaratibu.Roho Iliyo Potea (R.I.P). Alianza kwa kujitambulisha jina lake halisi. Kisha akaniupongeza sana kwa ujasiri wangu hadi kufika hapo.Akajieleza kwa ufupi maisha yake ya utafutaji huku na kule hadi alipojikuta akitafuta kwa njia za mashetani. Ni katika maelezo haya alinieleza juu ya namba 666. Nilishangazwa sana na maelezo yake lakini nilipiga moyo konde nikiamini tiba ipo.Baadaye akanieleza jinsi alivyojitoa katika harakati hizo za kumtumikia shetani. Haikuwa njia rahisi. Aliwapoteza ndugu zake kadhaa lakini mwisho akawa amejikomboa.Hiyo chapa uliyopigwa lazima ifutwe! Ni njia hiyo tu ya kukukomboa kutoka ufalme huo.Nilikuwa makini nikimsikiliza.!USIKU MNENESafari ya kuelekea kuitoa ilea lama ilikuwa imewadia. Pesa taslimu milioni moja ilikuwa imenitoka tayari ili kufanikisha jambo hili.Tulitumia usafiri wa gari binafsi. Tulikuwa watatu. Mimi, RIP na mwenzake ambaye sikuwa namjua jina. Yeye alikuwa anaendesha gari.Sasa gari ilisimama. Tukashuka garini. Nilikuwa nimevaa upande wa kanga kama RIP alivyoniagiza. Tulitembea kwa muda hadi tukakifikia kichaka. Hapakuwa na vibuyu wala dawa za kienyeji lakini tulikuwa mbele ta kaburi, hilo kaburi lilikuwa likimsubiri mtu limmeze. Yaani lilikuwa wazi.Mara akachomoa kisu, akachomoa na kisahani.Nikaamuriwa kuvua nguo!! Nikavua. Nikawa uchi mbele ya wanaume hawa wawili. Sikuwa na aibu!!R.I.P akatoa sindano akavuta dawa. Akanigeuza, nikageuka.Akanidunga sindano. Hii ya sasa ilipenya. Nikaisikilizia maumivu yake kisha taratibu nikasikia mguu wangu wa kulia unakufa ganzi.Kisu kikatwaliwa upesi. Ilikuwa saa sita kasoro dakika sita. Hii ni kwa mujibu wa RIP.Sikujua kinachoendelea lakini nilipotazama chini niliona kitu kama maji vile. Ghafla ikasikika sauti. Sauti ya kike ikiniita kwa mbali. Sauti ile ilikuwa inanisihi sana nikimbie.Nikimbie kwenda wapi sasa.RIP na mwenzake walikuwa wameshikilia kile kisahani. Sasa niliweza kuona kipande cha nyama. 666 zilionekana zikiwa katika mng’aro wa dhahabu.Nikiwa sijajua lolote linaloendelea. Mara ghafla ile sauti sasa iliweza kusogea zaidi na zaidi.Hatimaye aliyekuwa anaita kwa juhudi zile nikamuona. Alikuwa ni Maria, yule rafiki yangu tunayeishi naye. Alikuwa yu uchi wa mnyama. Alikuwa akikimbia kwa juhudi zote lakini hakuwa akikimbia bure kuna kitu ama mtu alikuwa anamfukuza.Nikajaribu kupiga kelele. RIP na mwenzake hawakunisikia.Maria alikuwa anakimbizwa na nyoka. Nyoka mkubwa alikuwaanang’ara sana. Nashangaa wenzangu hakumuona.Nikajikuta natimua mbio uchi. Na nilikuwa kitendo cha sekunde chache yule nyoka akavamia eneo lile. Sikushuhudia sana kilichowatokea wenzangu. Sasa nikaanza kuhangaika huku na huko katika pori hilo ambalo sikuwa nalifahamu.Mguu mmoja ukiwa umekufa ganzi. Ningeweza vipi kukimbia mbio ndefu. Isabela mimi nikaanguka chini. Sasa nikawa najivuta kama nyoka. Nalia kama mtoto. Sikuwa na uelewa bado kwa nini mguu wangu ulikufa ganzi. Lakini kumbukumbu za kuchomwa sindano ile kali zilikuwa kichwani mwangu.Nikiwa bado sijapata jibu sahihi. Lile joka la maajabu sasa likatokeza mbele yangu. Mdomoni likiwa na kipande cha nyama. Nyama ile yenye namba 666.Nikajiinamia kwa uchungu. Nikafanya dua fupi. Nikajilaani kwa kila hatua ya maisha yangu niliyopitia. Nikatamani ningekuwa na nguvu niweze kutimua mbio. Lakini tayari nilikuwa nimelegea. Macho yakazidi kuhesabu hatua za yule nyoka kunifikia. Sijawahi kuona nyoka mkubwa kama huyu!!! Nakufa kwa kumezwa na nyoka. Inauma sana!!Joka likazidi kusogea!! Joka kuu likawa linatambaa!!!Kabla joka halijanifikia. Lilibadilisha uelekeo. Ni kama kuna kitu lilikuwa limehisi. Likaanza kutambaa kuelekea upande mwingine.Joka linatoka mara sasa namuona John. John yule mpenzi wangu ambaye alipotea katika mazingira ya kutatanisha pale chuoni.“John…John!!” nilianza kumuita. Sauti ilikuwa imekauka. Haikutoka.Joooooh!!! Nikajaribu tena, nikawa kama ninafanya mnong’ono. John akawa anaenda zake. Nikalia sana kuikosa nafasi hii hadimu ya kusikiwa na John!! Huenda angeweza kuwa msaada mkubwa kwangu.Ubaridi ulipenya katika mwili wangu. Mwanzoni niliuhisi kuwa wa kawaida lakini baadaye nikahisi kama maumivu hivi. Nikajipapasa. Nilipoutazama mkono wangu ulikuwa na damu. Nikageuka kujitazama sehemu zangu za nyuma.Maajabu!! Nilikuwa na kovu kubwa sana!! Na palikuwa pamechimbika. He! Ina maana nilikatwa nyama yangu ya…..!! niliduwaa.Maumivu yakazidi. Na sasa giza likazidi kuchukua nafasi yake baada ya mbalamwezi kutoweka. Giza nene!! Hapo bado nilikuwa sijaweza kunyanyuka imara. Nikajaribu kujikunjua nisimame. Maumivu makali katika makalio. Nikaanguka kama mzigo. Nilipoanguka palikuwa na kisu kipya, kikiwa na damu.Nikaendelea kulia. Sauti haitoki.!! Nilikuwa katika jaribio kuu maishani.Ikiwa bado sijaweza kusimama. Lile joka lililopotea njia sasa lilionekana tena. Safari hii lilikuwa linakuja kwangu tena.Bora nife!! Nilijiapiza. Sasa nikaanza kutambaa kumfuata huyo nyoka. Mkononi nikiwa na kisu ambacho nilikiokota, bila shaka ni kile kilichotumika kunikata nyama.Nikawa natambaa kama joka lile linavyotambaa. Sikuwa naijua nia yangu. Lakini nilihisi ni vyema kufa kuliko mateso haya.Lile joka likazidi kunisogelea, macho yake makali yakiangaza huku na huko. Urefu wa joka lile la dhahabu likiwa na kipande cha nyama mdomoni ulinitia kwenye hofu. Nikajiuliza iwapo kisu changu kinaweza kupenya katika ngozi yake, nikajipuuza maana kisu changu kilikuwa kidogo sana. Nikasita kutambaa. Nikatulia tuli, huku nikiamini kuwa ni heri linimeze kistaarabu kuliko kunimeza likiwa na hasira baada ya mimi kujaribu kupambana nalo. Nikafumba macho nikakitupa kisu changu chini, nikajinyoosha tayari kwa kumezwa.Haikuwa ndoto kwamba nikifumbua macho nikutane na mashuka yangu masafi ya kuvutia yakinibembeleza kulala badala yake nilipofumbua macho. Joka kuu hili hapa!!Ubaridi wake ukapenyeza sasa, lilikuwa juu ya mwili wangu, pumzi zikawa zinaniishia. Ndio ninamezwa au? Nilijiuliza.Nikaanza kugalagazwa kadri lilivyokuwa linajivuta. Sasa ile hamu ya kufa ikatoweka baada ya lile kovu langu makalioni kupatwa maumivu makali. Maumivu yaliyosimamisha misuli yangu. Nilipogeuka kujitazama nikakuta kuna mwiba umezama nikajivika ujasiri nikauchomoa. Sikuwa navutwa tena. Nilitazama mbele nikalishuhudia lile joka likienda zake.Inamaana huyu nyoka hakuniona ama!! Nilitafakari. Nikashangaa.Damu zilikuwa zikinitoka tena, sasa haikuwa katika kovu tu, bali na sehemu nyingine. Lile joka lilikuwa limenivuta hadi katika mti wa miiba na ni hapo nilipojitonesha.Pori likatulia kimya, kimya kikawa kirefu sana. Nikawa nahisi kiu kikali. Lakini hapakuwa na maji. Usingizi ukanisaidia kuikwepa karaha hii. Nikasinzia.Mwanga wa jua ndio ulionishtua. Nikakurupuka. Ni uchi!! Nikajishangaa kisha nikawahi kujiziba lakini bahati mbaya hakuwepo ambaye alikuwa ananichungulia. Nilikuwa peke yangu katika pori lile.Hakuna mnyama, hakuna mmea ninaoufahamu, hakuna hata mdudu!! Lilikuwa pori la maajabu, pori la mateso makali kwa kiumbe hai.Nilisimama wima, nikajisikia dhaifu sana lakini sikutakiwa kuendelea kuwa lelemama, nikiwa nachechemea nilianza kuzunguka huku na kule niangalie uwezekano wa kupata msaada. Harakati zangu sasa zikazaa matunda, kwa mbali nilimuona mtu akiwa analima. Alhamdulilah!!Lilikuwa jambo maalumu kwa wakati maalumu. Nikajongea kwa kujikaza hadi nikalifikia lile shamba. Hakika mtu huyu alikuwa mchapakazi. Alikuwa peke yake na shamba lilikuwa kubwa sana.“Kaka!!....Kaka…” Sauti ilitoka kwa taabu, nadhani hakuweza kunisikia.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Nikataka nimsogelee. Lakini ghafla akageuka. Ni kama aliuhisi uwepo wangu pale.Japo alikuwa amechakaa sana. Nguo zikiwa zimeraruka, lakini niliweza kumtambua. Huyu mtu alikuwa ni marehemu. Zaidi ya kuwa marehemu, kifo chake niliwahi kukiota. Basu!!Hakusema neno alipogeuka na wala hakunitazama, ni mimi niliyeiona alama ya 666 kifuani pake. He! Anamilikiwa!! Nilitafakari. Nikatimua mbio. Mbio za kuchecheme ziliniumiza lakini nitafanyaje??Akili yangu ilikuwa sawa kabisa. Nilikuwa namkumbuka vyema Davis. Nilijuta kukutana na bwana huyu katika mtandao na kumuamini sana. Nilijutia na pesa alizokuwa akinipatia.Mara nikaanguka!! Nilikuwa nimegongana na kitu kigumu. Ajabu na kweli haukuwa mti bali mtu. Jesca! Jesca na urembo wake alikuwa amebeba ndoo kubwa ya maji, alikuwa peku na alikuwa amepauka sana. Hata Jesca naye hakunitazama, badala yake aliendelea na safari zake huku akinipa nafasi ya kuitazama alama ya 666 katika mkono wake.“Jesca!! Jesca!!” hakunijibu na dhani hakunisikia. Akatoweka.Sasa sikukimbia tena, ina maana hawa watu hawanioni. Na kamahawanioni hata lile joka halinioni. Nilijiuliza.Kwani kuna kitu gani sifanani nao? Nilipojiuliza hivyo. Nikaikumbuka alama ya ‘666’ iliyokuwa imetolewa katika upande mmoja wa makalio yangu.Alama hii ni ile ninayoijua ama kuna utofauti? Nilitafakari. Jesca huyo akawa ametoweka. Nilipoendelea mbele kidogo nikakutana na kile kisu nilichokitupa. Nikakitwaa. Nikazunguka huku na huko nikiwa uchi nikaipata ile kanga yangu, nikaivaa, wakati naivaa ndipo nilikumbuka juu ya watu wawili niliokuja nao huku katika kujisafisha na alama hiyo mbaya.Nilipowakumbuka nikalikumbuka na kaburi lililokuwa wazi. Nikazungukazunguka na sasa nilikumbana nalo. Huenda walikuwa wamejichimbia kaburi hili. R.I.P na mwenzake walikuwa wamejizika huko.Amakweli wewe ni Roho Iliyo Potea!!! Nilikiri kimoyomoyo baada ya kugundua kuwa sasa RIP amepotea kweli. Nilisikitika kuwa hakuwa amenieleza mambo mengi juu ya alama hizi za maajabu.Jambo moja la muhimu alilonieleza ni kwamba nilikuwa namilikiwa. Kuna mtu alikuwa ananimiliki. Ili nisimilikiwe ilikuwa lazima alama hiyo ifutwe.Sasa nilikuwa nimekatwa kipande cha nyama. Damu ya hedhi hainitoki tena na sihisi kichefuchefu cha mimba. Ina maana ndio similikiwi tena? Na mimba nayo imetoka. Nilishangaa.Lakini sasa mbona siwezi kutoka humu porini? Nilijiuliza sikupata jawabu.Mawazo yangu yalikatishwa na sura ya mtu mwingine aliyekatisha mbele yangu. Huyu alikuwa ni marehemu mwingine ambaye tulisoma chuo kimoja enzi za uhai wake.Hivi niko peponi ama jehanamu? Kwa nini sasa nakutana na maiti tu.Huyu naye hakuonekana kunifahamu. Alikuwa na alama yake sikioni. Nikakumbwa na moyo wa kujaribu. Kama mimi nimekatwa kipande cha nyama na alama imetoweka, nikaamua kujaribu kutumia mbinu ya RIP ambaye sasa ni marehemu.Nikamnyatia yule binti. Nikakiweka kisu changu tayari nikamkaba. Bila kukumbuka maumivu atakayoyapata nikafyeka sikio lake. Nikasisimuka lakini katika nafsi nikikiri kuwa kile kisu kilikuwa kikali sana. Sikio chini!! Yule binti naye chini, akawa anatoa kilio kikubwa sana. Kitu cha ajabu hakuna msaada alioupata. Mimi nikajiweka mbali niweze kuwa shahidi wa nini kitakachotokea.Mara upepo mkali ukaanza kuvuma. Miti ikayumba, pori likatulia na sasa alitokeza nyoka mkubwa, ni yule yule wa awali. Nikataka kukimbia, nikakosa ujasiri nikaendelea kujificha, joka lile likatambaa hadi katika ule mwili unaogalagala, kisha likakwapua lile sikio na kisha kuanza kuzurura huku na huko hadi lilipotoweka ndipo nilipomsogelea yule binti. Alikuwa ametulia tuli na damu haikuwa ikivuja sana.Nikamgusa. Akajigeuza, akanitazama. Mungu wangu!! Tiba inafanya kazi ile. Aliniita jina langu. Akakaa kitako.Sikuwa nikiamini lakini sasa nikampongeza RIP yule tahira niliyemdharau sasa alikuwa njia.“Na wewe umejiua?”“Nimejiua?” nilimuuliza.“Isabela kwa nini uliniua?” alinihoji. Nikashangaa.“Mimi nilikuua wewe.”Yule binti alinieleza kila kitu, akanisimulia alivyouwawa akiwa ndotoni. Akakiri kuniona mimi nikimmaliza huku ninacheka. Akanielezea juu ya sauti alizozisikia. Ni sauti zile zile na mimi nilizisikia katika kifo chake na pia katika mazishi ya yake, hata Jesca alipokufa zilisikika.Niliamini tena kauli ya RIP kuwa kuna mtu ananimiliki na ananifanya anavyotaka yeye kwa wakati wake. Huyu mtu ni nani? Nilijiuliza huku tuhuma za kwanza nikizitupia kwa Dokta Davis.******(OPARESHENI UKOMBOZI)Jenipher alinieleza mambo mengi huku akinisaidia kupata chakula na maji. Chakula kilikuwa kizuri na maji yalikuwa safi lakini namna ya kuvipata ilikuwa ya namna yake. Wakati huo na yeye hakuweza kuonekana.Chakula na maji pekee havikuwa vitu tulivyokuwa tukihitaji. Kikubwa tuliuhitaji ukombozi wetu na wanadamu wengine wanaomilikiwa na watu wabaya.Sasa ilikuwa ni lazima kuuvaa moyo wa ujasiri ili kufanya harakati za ukombozi. Tuliwahitaji wanaume wenye nguvu waweze kuungana nasi.Basu akawa chaguo la kwanza! Tulimtegea siku akiwa katika kulima shamba kubwa lisilotoa mazao.Tulifanikiwa kumpata kwa wakati. Huku tukiwa tunajiamini kabisa. Tulimvaa kwa nguvu akaanguka chini huku akiwa haoni lolote. Anaangaza kushoto na kulia. Nikachomoa kisu.Alama ipo kifuani!! Huu sasa ukawa mtihani. Nichome au nisichome..nikimchoma maana yake ninamuua. Nikabaki kujiuliza.Hali hiyo ya kujiuliza, ikapoteza sekunde kadhaa. Ni katika sekunde hizo, nilimshuhudia Jenipher akirushwa mbali kisha nikamwona nyoka akimshambulia. Nikajitoa katika mwili wa Basu nikiwa na kisu changu nimesimama wima. Nilimshuhudia Jenny anavyohangaika. Na nyoka yule alikuwa ni mdogo sana. Nikajitoa muhanga.Bila kusita mbio mbio. Kisu mkononi huku nikipiga kelele nikamfikia yule nyoka nikamfyeka. Akagawanyika vipande viwili.Jenny akasimama. Hakuwa amejeruhiwa. Tukatoweka mahali hapo. Tukamwacha Basu akiwa katika taharuki asijue nini kimetokea.Hatukuwa tumezungumza lolote. Hadi pale tulipokutana na mwanaume mwingine. Huyu alikuwa ametoka kukata kuni. Tulimpisha njia kisha tukamfata kwa nyuma tukamvamia, akapiga mweleka. Alipojaribu kurusharusha miguu. Alama ile chafu ikaonekana katika paja lake. Bila kujiuliza Isabela mimi nikafanya kama nachuna mbuzi. Nikaikata nyama ya paja lake. Mwanaume huyu akalia kama mtoto.Nilipoiondoa nikaitupia mbali. Baada ya muda akatokea yule nyoka akakichukua kile kipande.Sasa tukazidi kufunguka akili kuwa yule nyoka anawaona watu wenye alama. Na yawezekana ni nyoka huyu yupo katika kuwamiliki wanadamu kwa chapa yake ya hatari.Swali kuu likabaki. Tunatoka vipi katika pori hilo.Mwanaume yule hakuzimia, alikuwa na timamu zake. Tukamweleza kwa kifupi naye akajieleza kuwa, tamaa ya utajiri imemtupia katika shimo hili baya.Yule mwanaume alijitambulisha kwa jina la Samson alikumbuka vyema kuwa kabla ya kufika hapo alikuwa mkazi wa jijini Mwanza na alikuwa mwanafunzi katika chuo cha biashara (CBE) tawi dogo la jijini Mwanza.Huyu alikuwa Samson kweli maana alikuwa ni mbabe sana. Lile kovu lake la kwenye paja halikumsumbua. Tulitembea kidogo akachuma majani fulani akayasagasaga akayaweka katika lile kovu. Hapa sasa aligumia kwa maumivu. Bila shaka ile dawa ilikuwa kali sana.Akaniwekea na mimi katika kovu langu. Nikapiga mayowe. Akanikamata imara. Hadi maumivu yalipotulia kidogo. Jenipher hakutaka kovu lake la sikioni liguswe aliweza kuyakadiria maumivu makali ya dawa ile.Siku mbili zilipita. Kovu lilikuwa linakauka kwa kasi. Nilimshangaa kijana huyu.Siku hiyo ya pili harakati za kujikomboa zilianza rasmi. Jeshi letu bado lilikuwa dogo. Tulihitaji jeshi kubwa zaidi.Samson alituongoza hadi katika ngome ambayo yeye alikuwa akishi hapo kabla. Walioishi katika ngome hii ni wanaume wababe wanaoweza kufanya kazi ngumu. Tuliindia hapa na kuwakuta wanaume sita waliojaa haswahaswa. Kama ilivyo kawaida hawakuweza kutuona japo kila mmoja alikumbwa na hisia za namna yake mwenyewe.Mimi kisu mkononi. Samsoni panga kubwa mkononi, Jenipher kazi yake kukaba kwa bidii zote. Sisi wawili tukawa tunakata tu!!Iwe sikioni hiyo alama. Sikio sio lako tena!!Iwe kwenye mkono. Samsoni anaushusha mzima mzima.Kama ni kiganja. Mimi naondoka nacho kwa kutumia kisu changu. Ikishindikana tu, panga kubwa la Samson linatimiza wajibu.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Waliokuwa wamewekewa alama katika vifua vyao hawa walitupa wakati mgumu sana na tulilazimika kuwaacha wanaume wawili. Wanne tukaungana nao.“Sam kwani we kabila gani?” nilimuuliza wakati tunaondoka.“Msukuma wa Bariadi!!” alinijibu huku akijaribu kutabasamu.Amakweli!! Hana huruma mtu huyu kama vile…kama kabila gani vileee…..Nilipotea katika mawazo nikarejea katika uhalisia. Joka kuu tukapishana nalo. Wenzangu wakakumbwa na uoga. Mimi sikuogopa tena. Nilijua kazi gani linaenda kufanya.Jeshi lilikuwa kubwa sasa na kila mmoja alikuwa na nia ya kuwa huru hivyo tulipambana kwa bidii sana.Mapambano yalikolea sana kwani kila siku tuliongeza timu ya ukombozi.Kilichotutatiza ni kuijua njia ya kutokea. Sasa tukiwa tunajiamini kabisa siku hii hatukutembea kwa kundi kubwa bali kila mmoja alienda njia yake huku akijiamini kabisa kuwa hawezi kuonekana. Nia ikiwa kutafuta njia.Shughuli hii ilianza asubuhi kabisa. Mimi na Jenipher tulienda njia yetu. Huku jeshi jingine nalo likienda njia tofauti.Masaa yakapita na jioni ikawadia. Ile jioni ambayo tulikuwa tumekubaliana tukutane.Tulingoja kwa muda mrefu lile eneo tulilokubaliana tukutane lakini wenzetu hawakutokea.Tulisubiri sana, hatimaye giza likaanza kuiingia. Nikaingiwa na wasiwasi, huenda wenzetu waliipata njia na sasa wapo huru wametusahau sisi. Nilijilaani kwa kuruhusu hali hii ya kila mmoja aende kivyake.“Jenny”“Bela” aliitika.“Unaweza kuwa unajua lolote kuhusu hawa watu.”“Mh!! Kwakweli hata mimi nipo katika mashaka.”“Wanaweza wakawa wamepata njia na kutoroka?” nilimuuliza.“Kama hawajatoroka basi kwenye kambi ya usiku lazima watakuwepo.”“Kambi ya usiku ndio nini?”“Kila usiku wanachama ama wananchi wa mji huu huwa wanaitishwa kitu kama gwaride hivi, tena leo ni gwaride kuu.”“Linafanyika wapi.”“Nitakupeleka Bela. Lakini panatisha sana huko. Na sijui kama patakuwa salama.”“Jenny pawe salama ama pasiwe salama..kwa sasa haina maana ujue bora kufa sasa..maisha gani haya unadhani.”Jenny alikubaliana na mimi, akaniongoza kwenda katika kambi kuu. Kila mtu alikuwa kimya sana. Nilikuwa namfuata Jenny anapoelekea. Hadi tulipoona mahali panafuka moshi“Huko wanakula nyama…na damu pia.”“Kwa mifugo gani sasa?” nilihoji kwa sauti ya chini.“Wananchi wanaotaka kutoroka huwa wananyonywa damu.” Nilishtuka sana kuisikia kauli hiyo.“Na leo kuna mwananchi alitumwa damu kutoka Naijeria, ndio leo anaileta sasa.”“Na wewe umekula nyama ya mtu?” nilimuuliza.“Hapana hizo wanakula viongozi wakubwa tu. Mwananchi ukila ama kunywa damu wanasema unakuwa kama wao. Kwa hiyo hairuhusiwi hata kidogo”Alinieleza kwa utulivu mkubwa.Tukaifikia KAMBI YA USIKU.Shangwe zilikuwa kubwa na watu takribani hamsini walikuwa wakisheherekea.“Ndio watu wote hawa ama kuna wengine?”“Ni hawa tu!! Ujue hii ardhi ndio kwanza ilikuwa imeanzishwa.”Nilikuwa kimya nikiwatazama watu kwa mbali tulipojificha. Nilimuona John, nikamtambua na Jesca. Baadaye kila mmoja akatulia kuna mtu alitaka kuzungumza neno.“Leo raisi atakuwa amekuja. Isabela tuyondoke hapa.”“Raisi ndio nani?” niliuliza kwa jeuri. Kuna kitu kama hasira kilikuwa kimenikaba kooni na sikuhisi uoga hata kidogo.“Mkuu wa Nchi hii. Huwa haoneshi sura yake lakini anaitwa mtukufu raisi.”“Na yule anayeonekana ni nani?”“Yule tulitambulishwa kwake kama waziri wa miundombinu…njia zote anazifahamu yeye.”Niliposikia hivyo nikatamani sana kumtia mikononi, mtu yule aliyeitwa waziri wakati namfahamu kwa jina la Osmani!! Huyu alikuwa ni Osmani mwanaume aliyenipatia namba ya simu 6666666. Na ni huyu huyu aliyenijia ndotoni akiwa na John wakimkwapua mama yangu mzazi.Sikuwa na uoga. Nilipiga hatua sasa nikawa nimejichanganya na watu hawa wachache waliokuwa wakimtumikia shetani.Osmani alikuwa akiongea kwa maringo na kutumia amri sana.Kila mtu alikuwa anamsikiliza.“Leo damu ipo nyingi, nyama za kusaza.”“Manson, Fanson, Rinzon, Wenton, Zeiron.” Alitaja vitu nisivyovijua na kila alipotaja kuna mtu aliitika na kwenda mbele. Walikuwa wanaume watano waliojaa vyema.Bila shaka walikuwa wanaujua wajibu wao. Niliwaona wakizichukua kamba nene kabisa. Pamoja na visu.Walitulia kwa dakika kadhaa, mara wakaletwa mbele yao watu ambao walionekana wazi kuwa walikuwa wamechoka sana.Nilimuona Samson akiwa amevimba sana kutokana na kipigo. Hasira ikanipanda. Nikatulia tuli!!Wanaume wale walioitwa kwa majina ya ajabu wakatumia kamba zile kutengeneza namna ya vitanzi, kisha wakavitundika mtini.Mwanaume mmoja akamchukua mvulana kutoka katika lile kundi. Mvulana yule hakuwa na sikio. Nikamkumbuka ni mimi niliyemkata ili kumtoa katika ulimwengu huu wa giza.Nikiwa sijatafakari nini cha kufanya, nikashuhudia damu ikikingwa kutokea shingoni. Kisha akatupwa katika kitanzi. Alikuwa maiti!!Samsoni akavutwa akataka kuleta ukorofi. Akachapwa na mjeledi akapiga yowe kubwa huku akitukana matusi mazito mazito kwa kabila la kisukuma.Alipotukana akanikumbusha wakati aliokuwa ananiambia jina lake. Nikajisikia uchungu.Liwalo na liwe!! Nikaanza kusogea mbele. Bado Samson alikuwa akiwasumbua. Maajabu nikafika mbele ya hawa wanaume hawakuweza kuniona. Nikajaribu kumsukuma mmoja aliyekuwa na kisu tayari kwa kumchoma Samson. Haya yakawa maajabu makubwa. Isabela mimi namsukuma mwanaume mkubwa kama yule anaanguka kwa kishindo hivyo. Samson mwamba wa kisukuma, msukuma kutoka Bariadi akafanya jambo ambalo hadi leo ni kumbukumbu kwangu. Haraka akaokota visu viwili, akavimba kwa hasira kifua chake kikaweka mfereji mkubwa. Samsoni alikuwa amevimba kama mcheza mieleka.Nikabaki kushangaa. Akamrukia mwanaume mmoja sijui ndio Frazon, Manson ama vipi. Kisu kimoja. Mwisho wa uhai.Akakichomoa akamrukia yule ambaye alikuwa chini baada ya mimi kumsukuma. Visu viwili vikazama katika sehemu zake za siri. Damu ikaruka. Nikasisimka sana!! Samson hakujali.Sasa yule Osman akawa ametaharuki. Hajui nini kinatokea. Na yeye hakuwa ananiona. Nikamwona akimjaribu kumfuata Samsoni huku akiwa na jambia. Samson hakuwa anamuona.“Saaam!! Saam!! Nilimuita.” Maskini hakunisikia.Osmani na jambia. Akalichomoa mahali ambapo linahifadhiwa.Akalielekezea alipo Samson. Alipoanza kukimbia na mimi nikashtuka nikaanza kukimbia. Kabla hajamfikia. Mimi nikamfikia. Nikafanya kumsukuma. Akapepea kama karatasi. Takribani mita arobaini kutoka pale nilipokuwa. Samson alipogeuka, hakunitazama mimi bali alitazama chini. Akakumbana na jambia.Msukuma huyu mkali kabisa wa mapambano akatupa visu chini akatwaa jambia.Ilimchukua dakika chache. Manson, Fanson, Rinzon, Wenton, Zeiron. Wote wakawa tayari kwa kuzikwa kama hiyo nchi yao ina huo utaratibu wa kuzika.Samson alikuwa kidume!! Nilikiri.Kidume yule ambaye hakuzisikia sifa nilizokuwa nampa. Alizidi kunidhihirishia kuwa kile kifo cha yule mvulana cha kuchomwa kisu shingoni kilimuuma. Aliendelea na zoezi la kuwaondoa wananchi kadhaa kwa fujo zile alama za 666 popote zilipo katika miili yao. Ilimradi tu hakuwaua.Nia ikiwa kukuza jeshi letu!!Nami nikamuunga mkono!! Jenny naye huyo akaokota kisu kikubwa kaanza kufanya kazi.Tulilolifanya hapo lilikuwa kosa kubwa sana. Alama za 666 zilizokuwa zinaanguka katika mfumo wa vipande v ya nyama. Ukaleta balaa.Joka kubwa kuliko lile la awali likaibuka. Joka hili sasa lilikuwa halijulikani wapi mbele na wapi nyuma.Lilikuwa na vichwa viwili. Mbele na nyuma.Halikujulikana linatambaa kwenda kaskazini ama kusini, magharibi wala mashariki.Yule bingwa wa mapambano Samson akajikuta analiachia jambia lake, Jenny aliyekuwa anaanza kunogewa na shughuli ya kukata nyama za watu naye akatulia tuli.Nami nikakumbwa na uoga na nikakiona kifo kikibisha hodi.Isabela nakufa!! Nakufa nikiwa katika u…”Kabla sijamaliza kuwazua. Ghafla……..Ghafla!!!!!Ilikuwa ghafla sana!!!!Joka lilijinyanyua juu. Sote tukawa chini yake. Joka lenye rangi ya dhahabu!! Sasa ikawa patashika kila mtu analazimisha kujificha nyuma ya mwenzake. Hakuna aliyetaka kufa. Mimi, Jenipher na wale wengine waliokuwa wanatambua yule nyoka amekuja kufanya nini pale tulijiweka mbali na vile vipande vya zile nyama zenye namba 666.Joka likavimba kama linataka kutema sumu. Likavimba zaidi kama linataka kupasuka. Hatimaye likautoa ulimi nje. Likatanua mdomo kama linataka kutumeza sote. Kisu chan gu bado kilikuwa mkononi.Mara likajirusha na kujizungusha kama pangaboi. Hapa hakuna kitu kilichosalia. Kila mmoja wetu alirushwa mbali kabisa. Mimi sikuumia lakini wenzangu waliumizwa.Nilipogeuka nilimwona kiumbe akiwa amelowa damu akiwa na jambia mkononi. Alikuwa akikimbia mahali ambapo joka lipo. Alikuwa ni Samson yule jasiri wa kisukuma.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Macho yako yalifumba kisha yalipofumbua alikuwa ameingia mzimamzima katika kinywa cha yule nyoka. Jambia na yeye wakawa wamemezwa.Hali ya hatari!! Nilijitahadharisha.Joka lilikuwa linameza vile vipande vya mabaki ya nyama yenye chapa ya 666. Ndipo hapa nilimuona tena yule Osmani aliyetambuliwa kama waziri wa miundombinu. Nikakumbuka kuwa ni huyu bwana nimeambiwa kuwa anazijua njia zote za kutoka katika mji huu wa kishetani. Nikamnyemelea huku nikiwa makini na yule joka na pia nikiwa makini asiweze kuhisi chochote kile.Nikamfikia nikamkaba shingoni. Nilikuwa na nguvu za ajabu sana. Nikamvuta hadi katika kichaka nilichokuwa nimejihifadhi hapo.Hakuwa ananiona!! Jambo hilo lilinipa nafasi nzuri ya kumtawala. Kwa ukombozi wa wengi na kujitoa katika adha ya kufia katika mji huo. Nikanyanyua kisu changu nikazamisha katika paja lake. Akatoa kilio kikubwa sana. Kilio kile kikasababisha lile joka linyanyuke mara moja. Likaanza kuangaza huku na huko. Nami nikatulia tulii kuangalia nini kinatokea. Joka likanyanyuka kisha likatanua midomo yake. Kisha likionekana dhahiri kuwa na hasira lilitapika. Maajabu!! Samson yule jasiri katika vita hiyo akatangulia kisha jambia lake likafuata.“Njia ya kutoka hapa ni ipi?” nilimuuliza Osman huku bado akiwa katika himaya yangu.“Sijui.” Akanijibu kwa jeuri. Nikamchoma tena kisu katika sehemu ileile kilipopitia awali.“Nasemaaaaa!” akapiga kelele.“Dakika moja tu nakupa sema upesi.”Osman akaanza kutoa maelekezo ya namna gani ya kutoka katika kijiji hicho cha maajabu!!Maelezo yalikuwa yamenyooka!! Japo yalikuwa na masharti. Sikuwa na budi kuendelea kumshikilia. Ni huyu angetuwezesha kutoka.Joka lilizidi kuhangaika.Sasa lilitazama mahali alipokuwa Osmani na mimi. Likatambaa kwa hasira kali sana likawa linatufuata. Nikajikuta namuiachia Osmani. Nikaanza kukimbia. Joka likawa linaufuata uelekeo wangu.Mungu wangu!! Kumbe linaniona sasa hivi. Nimekwisha.Nilizidi kutimua mbio. Hatimaye mbio za sakafuni zikaishiaukingoni! Nikaanguka chini. Joka nalo hilo likanifikia.Likaachama mdomo wake mkubwa.Sasa nakufa! Nilikubali yaishe.Achaaaaaa!! Nilipiga kelele za mwisho za kutokwa na roho. Huku nikitegemea zitakuwa kelele za mwisho. Haikuwa hivyo. Niliweza kuwa hai tena. Joka lilikuwa limeufumba mdomo wake. Likatulia tuli.Nikaduwaa kulikoni nyoka huyu hajanimeza. Au! Au! …nikakosa majibu.Joka likaendelea kutulia kama lina urafiki na mimi. Kwa uoga nikasimama na kuanza kutambaa taratibu. Joka limetulia halina habari. Nikasimama. Bado tuli! Nikaanza kuondoka hadi nikatokomea! Nyoka ametulia.Maajabu makubwa sana haya!!*****Nilirejea hadi kule walipokuwa wanakijiji wenzangu. Osmani alikuwa amehitisha mkutano tena. Alionekana mwenye furaha sana na ni kama alikuwa anatoa karipio kali.Samson niliyedhani amekufa kumbe alikuwa amezimia tu baada ya kutemwa na yule nyoka. Nilimkuta akiwa amefungwa kamba nyingi sana. Bila shaka adhabu yake ilikuwa imewadia.Nilimuona Jesca pia. Lakini John pekee ndio nilikuwa sijamuona.Nilikuwa na hasira. Nikatumia ule mwanya wa joka kutulia. Nikamvamia Osmani. Nikamkaba tena. Safari hii sikutaka mambo mengi sana, nilihitaji njia ya kutokea.“Wakati wa kuwa watumwa wa shetani umekwisha. Tunatakiwa kuishi maisha yetu tuliyoshi awali. Manyanyaso haya yote na yasiendelee. Tusikubali kabisa uonevu huu. Sasa tunatoka humu. Kila mwenye nia na aungane nami sasa. Tunatokaa!!” niliunguruma kwa sauti kuu. Wale wasiokuwa na Chapa walinisikia na kuniona. Wale waliokuwanayo waliduwaa wasijue kinachoendelea.Samson alifunguliwa kamba alizokuwa amefungwa. Sasa Osmani akawa anatuongoza kuielekea njia ya kutokea.Chapa ya 666 ilikuwa katika mkono wake wa kuume.Kijiji kilikuwa kikubwa sana. Tulipenyeza njia hadi njia bado hatukufika tulipokuwa tunahitaji.Sasa tulifika mahali palipokuwa na majani makavu lakini laini sana. Tulipokuwa pale. Osmani akaniponyoka. Kisha akapiga mluzi fulani hivi. Wakatokeza kenge wa ajabu. Wakubwa kama mamba. Walikuwa wanne. Na dhahiri walikuwa na njaa. Walishambulia katika namna yha ajabu na upesi sana.Waliua! Watu kumi wakaanguka chini. Mamba wale badala ya kula nyama wakawa wananyonya damu.Ilikuwa zamu yangu sasa. Osmani alikuwa pembeni akitucheka. Kuna unga fulani alijipaka usoni, sasa aliweza kuniona vizuri.“Achaaaa!!” nilijikuta natamka neno lililoniokoa midomoni mwa joka lile kuu. Kenge hawa wa ajabu wakatulia palepale wakafunga vinywa vyao. Osmani akashangaa na mimi pia nikashangaa.Samson ambaye naye alikuwa amekata tamaa alishangaa.Nikawahi kuipoteza hali yangu ya kushangaa. Nikamwendea Osmani. Nikamkaba tena. Nikampiga makofi mawili akaanza kutema damu.“Njia ya kutokea!!” niliamuru.Akageuka, akatunyooshea mkono. Palikuwa na mlango mdogo wa mbao zilizooza. Nikawaamuru wanakijiji wsaliosalia wapite. Wakapita!!Hadi walipomalizika ndipo mimi na Osmani tulipita. Kabla hatujamaliza kupitia nilisikia kilio kikubwa. Kuna mtu alikuwa akiniita.Sauti ile ilikuwa ya John!Nikasita kutoka. Nikarejea nyuma niweze kuchungulia.John alikuwa anagalagazwa na lile joka kubwa.Huruma na mapenzi yangu kwa John ikanijia. Nikaweka kando yote aliyowahi kunitendea. Nikarudi kwa kasi. Neno acha likiwa mdomoni mwangu. N ilipofika nikaamuru kwa sauti kuu. Joka lile likatii kwa nidhamu. Nikaduwaa. Nikamchukua John na kuanza tena kuitafuta njia ya kutokea.Kosa kubwa! Nilimuacha mbali waziri wa miundombinu!Osmani akawa amepotea! Sikujua ni wapi pa kupita.John hakuwa akiniona wala kunisikia. Nilitamani ajue ni mimi nipo naye. Lakini haikuwa hivyo.Nilifanikiwa kukipata kisu. Nikaamini sasa nitaiondoa alama ya 666 katika mwili wake na ataweza tena kuona.Hofu! Na kukata tamaa. John alikuwa na alama ile shingoni mwake. Mwili ukafadhaika.Siwezi kumchinja John!! Siwezi!! Niliapa.Lakini nitafanya nini sasa.Kitu kama tetemeko la ardhi likatwaa mawazo yangu. Nikamvuta John asiyejielewa nikamkumbatia. Tetemeko hilo lilivyopita hapakuwa tena na lile joka.Lakini kitu kipya kikajitokeza. Ulikuwa mwanga mkali kama jua vile!! Nikatafakari ni kitu gani hicho. Sikuweza kutambua.Mara ule mwanga ukapotea. Nikaja kushtuka nimepigwa kibao katika shavu langu. Nikaanguka.Niliposimama nikapigwa tena, na sikumuona kiumbe aliyekuwa ananifanyia hivyo.Mapigo yakaongezeka. Nikawa navuja damu.Sikuweza kusimama tena.Sauti ya Jenipher ikanijia kichwani, “Ukinywa damu unakuwa kama wao!!”Maneno hayo yakanifanya nipatwe na ari mpya. Nikatambaa nikamfikia John.Badala ya kumchinja! Nitamnyonya damu walau kidogo tu.Nikamfikia. Nikamkamata. Akaanguka chini, nikajirusha shingoni mwake. Nilipoifikia shingo yake nikamkumbuka yule mganga wa kinaijeria. Hapo sasa nikakumbuka sio mara yangu ya kwanza kunywa damu. Nikapenyeza meno yangu pale pale kwenye alama ya 666 aliyopigwa shingoni.Damu ikaanza kutoka. Nikaimeza huku nikiwa nimeikunja sura yangu.Nguvu za ajabu zikaniijia.Amakweli wa giza pambana naye kigizagiza.Sasa niliweza kumuona adui yangu aliporejea tena. Alikuwa ni Dokta tuliyekutana katika mtandao, alikuwa ni Dokta Davis.Alikuwa ananisogelea tena aweze kunipiga. Nikaudaka mkono wake. Akataka kujitoa hakuweza. Nikaweka sawa kisu changu nilichokuwa nimekificha kwa nyuma. Nikazamisha katika sehemu zake za siri huku nikipiga kelele.Akaanguka chini na kuanza kujirusharusha.Nikamkumbuka yule ninja wa kisukuma, Samson ambavyo hakuwa na huruma. Na mimi nikamuiga. Nikamrukia Davis na kuanza kumchoma visu.Nilimchoma kwa fujo zote.Nikafadhaishwa baada ya yule Davis ambaye sasa niliamini naenda kummalizia alipogeuka kuwa joka kubwa la kijani. Haraka nikawahi kujitoa lakini nilikuwa nimechelewa sana. Joka lile likawahi kujiviringisha kuanzia kiunoni likawa linapanda juu. Sasa lilikuwa limenifunga hadi kifuani.Ajabu!! Lilikuwa linawasha sana nilitamani kujikuna lakini haikuwezekana na mikono ilikuwa imefungwa tayari.Nililiamuru liniachie lakini halikuiheshimu amri yangu. Nikazidi kuwashwa, nikajaribu kujigalagaza, haikuwezekana. Sasa likaanza kujikaza, muwasho ukaenda likizo, maumivu yakaingia kati. Lilizidi kukaza, mara likaongeza kujiviringisha hadi likaniziba usoni. Kifo kikanukia harufu ya kukera.Nikabaki jicho moja tu kuona nje!! Viungo vingine vyote vilikuwa vimefunikwa. Sikuwa na ujanja. Jicho langu likamuona John akiwa ameshangaa kama tahira. Nilijaribu kutoa sauti haikutoka, nilikuwa namwomba John kwa mara ya mwisho aweze kuniokoa. Hakuweza kunisikia.Nikatazama juu nikakutana na mawingu yenye rangi inayoshabihiana na buluu, nikaikumbuka rangi ya mtandao wa kijamii. Ni huku nilikutana na Dokta Davis. Akanipa zawadi ya utajiri, akanipatia kazi nyepesi inayonipatia kipato kikubwa. Nikamuamini sana. Sasa alikuwa amegeuka joka kubwa na lilikuwa linaniua.Hakika lazima nife!! Jitihada zangu zote hazikuwa na maana tena.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/John hakuwa msaada wowote kwangu. Na hakuwepo mwingine wa kunipa msaada.Nilipofikiria ni nani mwingine wa kunisaidia akili yangu ikarejea kwa mwalimu Nchimbi. Mama yangu mzazi. Nikajaribu kuita sauti haikutoka. Mama naye hakuwa na msaada katika hali hii.Nikayakumbuka maneno ya mama. Miaka mingi sana nikiwa mdogo aliwahi kunikambia maneno.“Yupo mtu anakusikia hata usipotoa sauti.” Hili lilikuwa jibu alilonipa baada ya kumuuliza iwapo mabubu na viziwi wanaweza kuzungumza na Mungu. Jibu lake hadi ukubwani halikunitoka.Nami sasa nilikuwa bubu. Jaribio la mwisho kabisa ni kuzungumza na yule anayesikia wakati wote. Ajuaye unachokiwaza. Kila wakati, mahali popote.Mungu!“Eeh! Baba sijui kama nilistahili adhabu hii. Na kama ilikuwa stahili yangu baba. Nichukue kwako sasa. Nimeumia na IMETOSHA.” Nilizungumza katika nafsi yangu. Kisha nikasubiri kuiaga dunia hii chungu.(HARAKATI NDOLLA ZAMBIA)Nilijikuta naifuatilie ile njia tuliyopita awali hadi nikaufikia ule mlango. Nikamtanguliza John nami nikatoka.Maajabu mengine. Niliwakuta wale waliotangulia wakiwa katika sintofahamu wasijue nini cha kufanya.Kwa kukadiria muda ilikuwa saa sita mchana. Na tulikuwa katika ulimwengu halisi lakini hatukutambua ni wapi hapo tulipo.Magu, Bariadi, Sumbawanga, Songea!! Kila mtu alifanya utabiri wake.Hatukuendelea kukaa pale. Tukaanza safari kuelekea tunapoelekea bila kutambua ni wapi.Baada ya kilometa takribani sita tukaingia kijijini.Mimi nikiwa na upande wa kanga pekee. Wenzangu wakiwa na nguo zilizochakaa sana. Tukakiona kijiji. Baadaye tukaanza kukutana na watu.Kila mtu akiwa na lake la kufanya. Hakuna aliyetuuliza swali. Walikuwa weusi sana, wengine walifanana na nyani huku wanawake wengi wakiwa na maziwa makubwa.Ni wapi sasa hapa? Nilijiuliza.Tulitamani sana kuzungumza na watu hawa lakini hawakuwa wakarimu.Njaa iliuvunja uamuzi wetu wa kusubiri watuanze. Njaa ilituuma na hatukuwa na chochote cha kuweka tumboni.“Ha…habari..”“Nkesuu…” sijui kama aliniuliza ama alinijibu salamu.Lugha ya wapi hii!! Niliwahi kusikia mahali, ni wapi vile. Niliumiza kichwa. Kila mmoja alikuwa ananitazama mimi kama mwokozi katika mapambano haya.“Me come great…” nilizungumza kiingereza kibovu ili nipate kujua wanazungumza lugha gani na ni watu wa wapi. Hakunijibu akanikazia jicho kwa shari. Ni hapo nikapata jawabu sura hizi nimewahi kuziona wapi. Ni kwenye basi. Siku ya safari yangu kuelekea Ndolla Zambia kwa Dokta Davis kusaini mkataba ule ulionifikisha hapa nilipo.“Sam…it’s either Congo or Ndolla….(Sam ni aidha Kongo ama Ndolla)” nilimnong’oneza yule msukuma.“Ndolla??”“Yes! Ndolla Zambia..” nikamjibu. Akashangaa. Yule bwana tuliyemuuliza akawa amesonya na kutoweka.Watu hawa sio wazuri hata kidogo. Wameathiriwa na vita za wao kwa wao. Wakitugundua ni hatari. Naamuru!! Hakuna mtu kuzungumza na mgeni yeyote, I WILL!!! Nilitoa tamko kama amiri jeshi mkuu wa mapambano hayo.Kila mmoja akanielewa.Safari ikaendelea, tulikuwa tumechoka lakini tuliuhitaji sana ukombozi, tulihitaji uhuru wetu.NDOLLA TOWN 40 KM AHEAD. Kilisoma hivyo kibao kigumu cha chuma. Nikajipongeza katika nafsi yangu kwa kuwa na kumbukumbu nzuri.Jesca alikuwa mtu wa mawazo mazito. Hakuwa akiongea na ule urembo wake wa enzi zile haukuwa na nafasi hapa. Pia ugomvi wetu wa kumuwania John kimapenzi haukupewa nafasi pia. Kila mmoja alitazama anajikomboa vipi.Tulitembea kimafungu mafungu. Jumla tulikuwa watu ishirini na moja lakini, tulikuwa kama hatufahamiani. Kila mmoja na lake. Likitokea la kuzungumza nilikuwa nachukua nafasi hiyo.Tulipoufikia mto, kila mmoja aliyatumia maji anavyoweza, wengi walikunywa na wachache walioga. Pumziko la dakika ishirini kisha tukaendelea mbele. Tukaufikia mti wa maembe. Hapa sasa kila mtu alikula kulingana na ukubwa wa tumbo lake. Angekuwa mjinga ambaye angeacha kubeba akiba ya maembe matamu ya Zambia.Sasa kasi ikaongezeka na mazungumzo yakaibuka. Njaa kitu kibaya sana.Mimi na John tulikuwa tumeambatana. Ile hali ya yeye kutoniona iliniumiza sana lakini sikuwa na namna.Kilometa zikazidi kukatika, tulitembea hadi usiku, kwa kukadiria tulitumia masaa yanayozidi kumi. Kuzikamilisha zile kilometa.Mji wa Ndolla ukatukaribisha. Ulikuwa mara yangu ya pili kuja katika mji huu na mara ya kwanza kufika nikiwa katika matatizo.Nilijipongeza tena kwa tabia yangu niliyoionyesha siku ya kwanza. Tabia ya kushangaa shangaa. Hivyo kuna baadhi ya vitu nilivikumbuka. Hadi tukaipata stendi.Kama nilivyoamuru kila mmoja alijitenga kama hatujuani. Kanga yangu ikiwa imefungwa vyema. Ni hiyo pekee ilikuwa ngao yangu. Nikaingia katika stendi ile ambayo ilikuwa inazidiwa hadhi na stendi ya Ubungo jijini Dar es salaam katika nchi yangu ya Tanzania.Nilizunguka hapa na pale. Nikaiona ofisi ya magari ambayo nilikuwa naitaka.“Mambo vi wewe…inakuwaje…mishemishe vipi…oya acha kuzingua…” maneno haya yalikuwa yanazungumzwa katika ofisi hizi.Nikainama chini jicho langu la kulia likatangulia kumwaga chozi la kushoto nalo kwa uchungu likamwaga chozi. Nikajiinamia chini nikalia kwa uchungu mkubwa. Uchungu wa kuikumbuka nchi yangu Tanzania. Kilio hichohichoi kwa namna ya kipekee kilikuwa kilio cha furaha. Ndio lazima nifurahi. Sasa ningeweza kumvuta mtu na kuzungumza naye Kiswahili.Ni hivyo nilifanya. Mwanaume kipande cha mtu akavutika kunisikiliza. Kwanza sikutaka kumuelezea kuwa tupo wengi. Niliitetea nafsi yangu. Nilikuwa natetemeka kwa baridi. Akanipatia sweta zito nikajistiri. Nikajielezea kuwa nimepotezana na bwana aliyenileta Zambia.“Umesema wewe mwenyeji wa Makambako.”“Ndio kaka.”“Makambako sehemu gani hiyo?”“Ni karibia na stendi kuu. Hapa Magegele …..”Alaa Magegele napafahamu sana huko…kabla ya kuhamia huku nilikuwa naenda na mabasi ya Dodoma Mbeya…sasa hapo Magegele kuna mgahawa tulikuwa tunakula tulimzoea sana yule mama kiukweli..hata wewe nikutajia lazima utakuwa unamjua..”“Mama Kesho.” Niliwahi kumjibu. Akacheka sana, hakuna mtu wa Makambako ambaye hakumjua mama huyu. Alikuwa mkarimu sana.Tulizungumza mambo mengi usiku ule. Alizungumza nami kwa ukarimu. Ni nani alikwambia kuwa watanzania sio wakarimu.Kuna tofauti kubwa kati ya mtanzania na mbongo!! Mtanzania ana utu lakini mbongo anajifanya mjanja mjanja. Huyu bwana alikuwa mtanzania haswaa.Upesi nikapata chakula. Kisha akaingia ndani akatoka na nguo. Zilikuwa za kike.Akanieleza abiria huwa wanasahau nguo zao na kamwe hawarudi tena kuzichukua. Nikamshukuru. Akanipatia na kiasi cha pesa. Akaniomba nirejee majira ya saa tano asubuhi aweze kunifanyia utaratibu wa kunisafirisha kurejea Mbeya kisha Makambako Iringa.Ilikuwa bahati ya kipekee sana kupata msaada huu. Lakini hapo hapo ilikuwa bahati mbaya sana maana nisingeweza kusafiri peke yangu. Na yule bwana sikumueleza tupo wengi zaidi ya kikosi cha timu ya mpira wa miguu.Ubarikiwe sana!! Nilimpa Baraka hizo.Kisha nikiwa na mavazi kamili sasa. Nikapiga hatua kwa hatua. Kigiza giza kikanifanya nionekane kama kivuli. Mkono mmoja mfukoni kuzilinda Kwacha (Pesa halali kwa matumizi ya Zambia) nilizopewa, mkono mwingine ukiwa umeshika kiroba cha nguo nilizopewa na yule bwana. Isabela nikiwa na raba nyepesi miguuni. Nikatoweka huku nikiamini nina mzigo mkubwa wa kuwaokoa rafiki zangu ambao walinitazama kwa jicho la huruma.Nilijihesabu kama mshindi wa vita ya 666. Lakini bado nilikuwa na vita nyingine ya kurejea nyumbani.Mshindi akifia ugenini huyo ni mshindwa lakini akirejea nyumbani hata kama amejeruhiwa vipi bado ataitwa mshindi.Mapambano yameanza rasmi!!! Nilikiri huku nikiwa nayatamani hayo mapambano ambayo yatakuwa magumu kushinda vita ya joka kuu la msituni.Nilimchukua Jenipher, Jesca na Samson. Kikawekwa kikao cha dharula. Mada kuu ikiwa tunatoka vipi.Nilimpatia Jenipher na Jesca baadhi ya nguo. Wakajihifadhi.Mazungumzo yalikuwa marefu sana na pambazuko lilikuwa linakaribia. Mengi yalizungumzwa na sasa tukawa tumefikia katika maamuzi mawili. Kubwa kabisa likawa kukimbilia ubalozini kupata msaada.Wazo la kupata simu tuweze kufanya mawasiliano nyumbani pia lilitujia vichwani!! Lakini hatukulitilia sana maanani katika nchi za kigeni. Tulitaka tufike kwanza Tanzania ndipo tufanye mawasiliano.Ubalozini!! Hiyo ndio ikawa mada.Lakini swali likaja kwa John ambaye bado alikuwa na alama 666 na hakuwa akionekana. Lakini kama hiyo haitoshi, tukapata hofu ya usumbufu wa maswali mengi kutoka kwa chombo husika kitakachokuwa kinahusika na mambo ya uhamiaji.Kwa jinsi tulivyokuwa wengi tuliamini kuwa itatuwia ngumu sana kupata msaada upesi. Pia ubalozi wa Tanzania katika nchi ya Zambia ulikuwa una makao yake Lusaka. Mji mkuu wa Zambia.Hilo lilikuwa gumu sana. Tulikuwa tunahitaji pesa. Pesa!!Kama tukipata pesa tunaweza kupanda mabasi yatakayotufikisha Mbeya. Hapo sasa tutakuwa katika ardhi salama ambayo tunaweza kupata msaada.Pesa tutaitoa wapi? Hilo likawa swali.Tukakubaliana kuingia katika mapambano ugenini. Mimi, Jesca, Jenipher na Samson. Tukafunga mjadala.Asubuhi ikazidi kujongea. Hapa sasa nikachukua maamuzi. Nikatembelea kundi moja baada ya jingine. Nikawapatia chakula kidogo kidogo nilichonunua kwa kutumia pesa niliyopewa na kaka yule wa kitanzania. Huku katika kila kundi nikiwapa moyo kuwa tumekaribia kuondoka kurejea nyumbani.Siku iliyofuata kila mtu alikaa kwa tahadhari bila kuzungumza na raia wa Zambia.*****Majira ya saa nne asubuhi nilikuwa katika ofisi ya yule mwanaume wa kitanzania aliyeahidi kunisaidia niweze kufia Mbeya. Nilimkuta akiwa amebanana kulingana na majukumu. Nikatulia mpaka alipomaliza. Nikaingia.Alinichangamkia sana. Akamkabidhi mwenzake ofisi akanipeleka mgahawani. Chai ya maziwa na chapatti nzito kabisa.Mazungumzo yakiendelea!!!CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Akanielezea mpango wake huku akinisihi niwe mvumilivu katika safari maana patakuwa na tatizo la kuhamishwa siti na wakati mwingine kukosa kabisa pa kukaa maa nitasafiri kama ‘staff’. Hilo halikuniumiza kichwa sana, maana niliamini naweza kusimama cha msingi nia yangu kutimia. Kilichoniumiza kichwa ni hawa wenzangu. Itakuwaje!!Nilimshukuru yule bwana. Akanipatia namba yake ya simu. Ni hapo nilimtambusa jina lake aliitwa Saidi.“Ukinipigia simu we niite Side boy.” Aliniambia wakati ananiaga.Alinipatia kiasi kingine cha pesa.Nilishukuru kwa kuzaliwa mwanamke maana bila hivyo sidhani kama ningepata msaada.Jioni ilipofika. Jesca hakuwa ameambulia lolote. Na Sam hadi wakati huo hakuwa amerejea. Tukajipa moyo kuwa huenda amefanikiwa kupata kibarua chochote huko alipo. Ikafika giza nab ado Sam hakuwa amerejea. Hofu ikaanza kutuingia na kuamini kuwa Sam anaweza kuwa aliongea Kiswahili na kugundulika kuwa ni mtanzania asiyekuwa na uhalali wa kuishi Zambia.Hatukujua kuwa ni wapi tuanzie kumtafuta. Kama tukisema twende polisi na sisi tutakuwa matatani. Tatizo jipya!!Jesca na Jenipher wakawa wananisikiliza mimi.Kimya kikatanda!! Makundi mengine hayakujua nini kinaendelea.Nilijiuliza maswali mengi sana bila kupata majibu. Samson amefanya jambo gani la kitofauti hadi wakati huu hajarejea.Au amerejea tena katika kijiji cha Dokta Davis. Niliwaza peke yangu bila kumshirikisha mtu yeyote hisia zangu.Saa nne usiku nilikuwa nimepitiwa usingizi.Nilisikia kama natikiswa nikadhani ni Jesca amejigeza lakini nilikuwa naendelea kubughuziwa. Japokwa nilikuwa nimelala chini niliutamani usingizi.Nilijikaza nikafumbua macho.Usingizi ukakatika palepale. Alikuwa ni Sam!!“Bella!! Bella!!” alinong’oneza. Nikamtazama usoni nikahisi kuna nhali ya tahadhari. Nikajipa utulivu wa lazima.Akanishika mkono akaninyanyua. Akanivuta pembeni kidogo.“Ulikuwa wapi Sam.”“Bwana Mkubwa!!.”“Kafanyaje…ndio nani?” nilitaharuki.“Sio mtu ni sehemu inaitwa hivyo.”“Pamekuwaje…”“Nimekutana na mtu!! Aah!! Nimemuona mtu….amepata madini.”Bado sikuweza kumuelewa Sam anamaana gani. Nikamuomba anielezee kwa kirefu.Akanieleza juu ya mgodi wa Bwana Mkubwa ambao upon je kidogo ya mji wa Ndolla. Mgodi huu alipoutaja tu! Sikuwa na swali lolote. Nilikumbuka somo la Historia kidato cha pili hadi cha tatu. Mgodi huo ukanikumbusha madini hadimu ya Risasi (Copper) ambayo hupatikana kwa wingi katika nchi ya Zambia. Hasahasa Ndolla.Sam akaendelea kunielewesha. Na sasa akanigusia juu ya bwana ambaye amepata madini hayo siku hiyo.“Kwa hiyo ulikuwa huko.”Akanijibu kwa kutikisa kichwa juu na chini akimaanisha kuwa ni kweli alienda ‘Bwana Mkubwa’.Samson alikuwa amekuja na habari ambayo mwanzoni nilikuwa ninapingana nayo lakini hatimaye kulingana na shida tuliyokuwanayo nikaamua kukubaliana naye. Wizi!Samson alinihakikishia huyo bwana ana pesa nyingi sana. Amefuatilia nyendo zake hadi alipofanikisha kuyauza yale madini.“Alinipa lifti kwenye gari yake. Nilijifanya sijui lolote lile. Aliponishusha mjini nikamfatilia na kumuona aliyauza.”“Sasa tunampata wapi?”“Yupo anakunywa pombe sasa hivi. Ni hapo pekee pa kumkamatia.” Alinisisitiza.“Nzuri zaidi ni mtanzania…” alinisisimua kwa kauli hiyo. Nikamwomba Mungu huyo bwana asiwe na tabia za kitanzania bali awe mbongo.Nilitulia kwa dakika chache kisha nikamuamsha Jesca. Hakunisikia. Nikapekua huku na huko. Nikachukua mafuta. Nikaenda bafu za kulipia nikaoga. Nikajipaka mafuta. Nikavaa kanga moja.Samson akawa kioo changu akakiri kuwa kwa namna ile lazima anitamani.Samson akaniongoza hadi nikafika eneo la tukio.Jirani na bwana huyu palikuwa na kiti kipweke ambacho hakikuwa na mlevi aliyekikalia. Nilikitoa upweke nikajiweka juu yake.Haraka akafika muhudumu wa kizambia, mweusi na mbaya kumtazama. Nikaagiza soda.Meza yangu haikuwa mbali sana na yule bwana ambaye Samson alinielekezea. Nilikunywa soda taratibu huku nikiisoma akili ya yule bwana aliyepata bahati ya kupata madini Bwana mkubwa.“Yaani wahudumu wengine nao….ona sasa.” Nilizungumza kwa hasira. Kama najiongelesha. Sauti ikamfikia mlengwa ambaye ni yule bwana anayekunywa pombe.Akajileta mtegoni.Akasogeza kiti karibu nami.“Wewe ni mtanzania kumbe..ama unaibiaibia Kiswahili. Nimefurahi kukusikia ukisema Kiswahili.”Nikatabasamu, nikalegeza jicho kimaksudi.“Yeah! Mtanzania halisi…..na wewe je?”“Mimi ndio orijino kabisa.” Alijibu. Nikacheka tena.“Dah!! Miezi miwili sijarudi nyumbani aisee. Maisha haya.” Nililalamika.“Aaah! Mimi kila wiki huwa naenda aisee.”Maongezi yakawa maongezi. Kama bahati alinipendelea vile. Yule bwana alikuwa na tabia za kibongo. Akaniingizia mada za mapenzi.Sasa nane usiku tukawa tunatafuta chumba kwa ajili ya kutimiziana haja. Yeye akinitaka kimwili na mimi nikimtaka kipesa.Alilipia chumba cha bei ghali sana. Nilimshuhudia wakati anauacha mkoba wake mapokezi. Nikagundua mchezo unataka kuharibika.Nikajipa moyo. Nikaenda hadi chumbani!!Hapakuwa na jipya huko. Mzee huyu mwenye matamanio. Alinivagaa na kuanza kunisumbua huku na huko. Sikuwa na hisia hata kidogo. Niliwaza pesa tu.Nilipomtazama umri wake nikagundua huyu hana lolote la kuweza kunishinda. Akili ya maajabu ikanivaa, nikajikuta nimevamiwa na wazo kuwa kama nisipokuwa makini naweza kutumika kimwili na nisipate chochote kile.Nikaamua kutumia nafasi moja tu kusawazisha mambo haya!!!Pata potea!!“Mh!! Hauna kinga?” nilimuuliza baada ya kuwa nimempelekesha akalegea kabisa macho yake na nikajua kuwa alikuwa anahitaji mwili wangu.Ni hapa nilikuwa napahitaji.“Sina mpenzi wangu…njooo tu hivyo hivyo” akajibu. Nikamtukania mama yake kimoyomoyo kwa ujinga aliozaa.Nikasimama. Nikamtazama kwa jicho la kimapenzi huku moyo wa chuki ukimtusi. Ubongo unaohitaji pesa nao ukifanya kazi kwa bidii kubwa.“Ngoja niende kuchukua mpenzi wangu, naogopa mimba mwenzako, ujue nimeolewa eeh!!” nilimlaghai. Akaingia mkenge. Nikachukua upande wangu wa kanga, nikashusha ngazi mpaka mapokezi.Nikamkuta mwanadada mweupe akiwa ameuchapa usingizi.“Nipatie mkoba wa mzee!!” nilimwambia huku nikiwa nimetega mkono!! Moyo ukiwa hauamini kama nitafanikiwa.“Mmm. Hapana mwambie aje mwenyewe dada, hajaturuhusu kumkabidhi yeyote zaidi yake.” Alinipinga yule dada kwa kingereza chake kibovu kisha akaendelea kuuchapa usingizi. Nilitamani sana kumrukia nimkabe. Lakini alikuwa ametenganishwa na nondo. Nisingeweza hata kumgusa.Niliondoka pale nikiwa nimetaharuki sana, mpango ulikuwa unakaribia kushindikana sasa, na asubuhi inayofuata nilitakiwa kusafiri kuelekea Mbeya.Nikapanda hadi juu kule chumbani nikaufungua mlango kwa ghadhabu kubwa.Yule bwana akashtuka.“Ndio ujinga gani huu huku Zambia I hate such embarrassment!!” nililalamika.“Nini tena mamito.” Aliniita kimapenzi akiwa amelegea.“Yaani hadi kuchukua kinga I need to go with you!!”“He!! Wamekunyima?” aliponiuliza swali hilo, nikajikuta Napata nafasi ya mwisho.“Fanya hivi naomba umpigie umwambie anipe!! No discussion!!” niliwaka, zile hasira za kutaka kuikosa pesa ile zilikuwa zimenipanda.Mbongo akachukua simu akainyanyua. Nikaomba mizimu yote asije akasemam maneno mengi kwenye simu.“Halo!! Chumba namba 12….mpe huyo dada nilichomuagiza…na muache mambo ya kipumbavu” akakoroma kwa kiingereza kilichonyooka. Kisha akakata simu kwa hasira.Sikusema neno!! Nikafungua mlango, nikatoka.Nikiwa nimeukunja uso kwa ghadhabu nikafika mapokezi. Yule dada usingizi ulikuwa umekatika!! Tukatazamana!!Yeye anaogopa na mimi naogopa!!!Maskini yule dada bila kujua kwamba ameambiwa anipatie kinga. Akadhani yule mbongo amemaanisha ule mkoba. Akaniomba msamaha kwa kila namna kisha kwa ukarimu kabisa akanipatia ule mkoba. Ulikuwa mzito kiasi. Nilipotaka kuondoka yule dada aliyekuwa amejikita katika kutafuta anachojua yeye, aliniita, nikageuka na kumshangaa kidogo.“Unatakiwa kuweka sahihi.” Alinielezea kwa ukarimu.Nikaona kama huyu binti ana nia mbaya na mimi. Nikabaki wima najiuliza iwapo niende mbele ama nirudi. Tukatazamana kwa sekunde kadhaa. Nikaona isiwe tabu. Nikarejea nikachukua kalamu niweze kuweka sahihi. Mara nikasikia fujo za mlango kufunguliwa.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Nikaomba Mungu usiwe mlango wa yule jamaa mbongo. Kisha nikasikia hatua kubwa kubwa zikitambaa.“How long does it take to…to…..hell..” (Inachukua muda gani ku…ku…. ). Ilisikika sauti yenye kitetemeshi cha hasira. Alikuwa yule mbongo.Sasa badala ya kuweka sahihi nikabaki kulishikashika tu lile daftari na kalamu. Mkojo ukatoka safari yangu ya mbali na sasa ulikuwa unahitaji kutoka. Nikabana miguu yangu!! Mkoba mkononi.Ninafumaniwa Isabela mimi!!Nikataka nikimbie!! Miguu ikawa mizito. Sikuwahi kufanya kitendo cha wizi hivyo lazima hali kama hii ingenitokea.ingenitokea.“Iam sorry boss..i have already given her (samahani mkuu..nimempatia tayari.)” yule dada wa mapokezi alijitetea kwa uoga.Mara vile vishindo vikasita.Yakafululiza matusi ya nguoni kutoka kwa yule mlevi wa kibongo.Hapo sasa nikaangusha saini yangu.Narudi vipi na ule mkoba sasa!! Nikajikaza nikaanza kuondoka.Nilipogeuka nikakutana na kosa ambalo nililitegemea. Yule dada wa mapokezi alikuwa amebonyea chini tena.Asante! Nilimshukuru kwa kitendo hicho.Ghafla nikabadili uelekeo. Nikaelekea katika vyoo.Upande huu, nikaambaa na korido hadi nikaufikia mlango wa kutokea. Nikamuachia tabasamu mlinzi aliyekua kwa nje na yeye akatabasamu. Tabasamuu la kizee. Kisha nikatoweka. Nikapiga hatua kwa hatua hadi nikalifikia geti kuu la kutokea. Hapa nilitakiwa kuandika jina. Nikaandika jina lililokuja kichwani mwangu lakini sio jina sahihi.Geti likafunguliwa. Mimi na mkoba wangu. Nikatoka.Nilipogeuka nyuma nikakutana na maneno mazuri ya kupendeza.The Savoy Hotel12 Buteko AvenueNdolaZambiaHaya hayakuwa yananihusu. Niligeuka na kutazama mbele. Nikaanza kutokomea. Nikashtuliwa kwa kuguswa begani.Nikageuka upesi nikaikuta amani ambayo nilikuwa naihitaji.Samson…jemedari wa kisukuma.Akanikumbatia kunipongeza. Lile joto lake likanikumbusha mengi. Nikapuuzia.Oparesheni ilikuwa imekamilika.****Pesa zilikuwa kwa mafungu yanayolingana. Zilikuwa zinang’ara kuonyesha kwamba hazikuwa zimepitia mikono mingi.Ilikuwa saa kumi alfajiri. Sasa nikiwa pamoja na Samson tulipita katika vijiwe ambavyo wenzetu walikuwa wanalala. Wote wakaamshwa. Hatimaye tukawa na mkutaniko wa pamoja wa kwanza tangu tuwe katika ardhi ile.Niliwakumbusha juu ya ahadi yangu!! Sasa ilikuwa imetimia.Hakuna aliyekuwa anafahamu thamani ya kwacha ya Zambia katika shilingi ya kitanzania. Hilo halikutupatia shida. Nikawachukua wenzangu watano wa kwanza. Nikaliendea basi linalotoka Ndolla kuelekea Mbeya mjini.“Kwacha ngapi?” niliuliza. Akanijibu. Nikalipia nafasi za watu watano.Wakaingia garini. Kiongozi wao akiwa JescaNikarejea na kuwachukua wengine. Hawa kiongozi wao akawa Jenipher.Kundi la nne nikalikabidhi kwa Samson.Kisha nikabakisha kundi lililosalia mikononi mwangu.John!! Akiwa ameambatana nami!! Nilichukua siti ya watu wawili. Nikamuweka John kisha nikambebesha mfuko fulani.Hakuruhusiwa mtu kukaa pale.Safari ikaanza huku maelekezo yota ya tunakutana vipi yakiwa kwa viongozi wa msafara.Hatimaye tukaiacha Ndolla majira ya saa kumi na mbili. Safari ya kurejea Tanzania.*****Pesa zilibaki nyingi sana. Hivyo tuliamini kabisa hakuna kitakachoharibika. Jesca alikuwa na akiba yake, Jenipher na Samson vilevile.(Mshikemshike )TUNDUMA, Mbeya.Mji ulikuwa umetulia sana. Hapakuwa na harakati za hapa na pale. Ilinishangaza sana kwa boda kama hii kuwa katika utulivu huu.Tulikuwa tukihangaika kutafuta mahali pa kulala. Nyumba za kulala jirani na kituo cha mabasi zilikuwa zimejaa. Hivyo ilitulazimu kidogo kuzunguka. Hatukupata mahali pa kulala kwa wingi tuliokuwa nao. Sasa tuliamua kuishi maisha yetu ya Zambia. Tukaamua kulala katika stendi ya mabasi.Baada ya kufikia uamuzi huo. Sasa mwenye kutafuta chakula aliruhusiwa lakini pa kulala tulikuwa tumeamua kabisa ni hapo hapo stendi.Wanaume watatu waliamua kusindikizana kwenda kutafuta chakula.Mkuu wa msafara huo Jesca aliwapatia pesa wakatoweka kwa ahadi ya kurudi upesi.Ahadi ikavunjwa maradufu!! Hawakurudi.Hadi tuliposinzia. Haikuwa kama yaliyomkuta Samson kule Ndola. Hawa hawakurudi kabisa.Kesho yake. Tulipotoa taarifa polisi tulikutana na taarifa ya vifo vya watu watatu kwa kukatwa na mapanga.Walikuwa wenzetu!! Lakini hatukukiri!! Hatukuhitaji kuwa karibu kabisa na polisi. Kwa kifupi hatukuwa tunajua hatma yetu. Hasahasa mimi ambaye nilikuwa na siri nzito.Baada ya taarifa hizo kutapakaa. Tukajua nini kinachoendelea ndani ya mji wa Tunduma. Majambazi wa ajabu walikuwa wameuvamia mji. Hawa walikuwa na hadhi ya kuitwa majambazi wastaarabu. Walibandika matangazo kabisa kuwa kama mwanaume anatembea usiku basi awe na tahadhari aidha simu ama kiasi cha pesa shilingi. Elfu hamsini lakini bila hilo wakikutana ama zao ama zake.Kumbe ndicho kimewasibu wenzetu!! Nilisikitika kuzipoteza roho hizi.Asubuhi hiyo nilitaka kwenda kubadili pesa. Lakini bahati mbaya sikuwa na kitambulisho chochote. Nikaitupa kazi hiyo kwa Samson. Akazunguka mtaani kuzibadili baada ya kugundua kuwa Kwacha moja ni sawa na shilingi 0.3 ya kitanzania.Baada ya zoezi lile kukamilika na kupata pesa ya kutosha sasa kila mmoja alitakiwa kuubeba mzigo wake mwenyewe. Aliyesema kuwa anaishi Dar alipewa nauli aondoke zake, wa Arusha naye vilevile. Na pesa ya ziada kila mmoja alipewa.“Muutangaze ushuhuda huu bila kuipunguza wala kuongeza neno!” niliwaambia wakati tunaagana. Kila mmoja alikuwa na furaha huku wakiniona mimi kama Mungu wao. Sikujali sana!!Safari ya Mwanza tukabaki watano. Mimi, Jesca, John, Jenipher na Samson.****Siku ya safari kama ilivyo kawaida nikalipia siti ya watu wawili, Jesca na Jenipher wakakaa siti moja huku Samson akikaa peke yake.Alama ya John shingoni ilinikwaza sana. Nilitamani aweze kutuona. Lakini alikuwa anauona ulimwengu wake mwenyewe.Safari nzima ilikuwa tulivu sana. Nilikuwa natafakari mambo mengi sana. Nilitamani kwenda Makambako kwa mama lakini niliamini haukuwa wakati sahihi.Nilihitaji nkujua kitu kuhusu Maria. Maana alinitokea kule porini siku ya kwanza kabisa na kamwe sikumuona tena.Nini kilimsibu? Nilijiuliza.Tulipita miji mbali mbali. Tukaipita Makambako, nikainama nikajifuta machozi, tukaiacha Mafinga, tukaingia Iringa mjini. Na hapa hatukusimama sana tukaendelea na safari.Sasa gari lilisimama!! Hatukushangaa sana. Tulidhani ni kwa madhumuni ya kuchimba dawa. Lakini hatukuiona dalili hiyo.Dereva akateremka. Akaangaza gari lake bila kuona tatizo.Akaangaza tena. Hakuna tatizo.,Msaidizi wake naye akashuka. Hakuna msaada!!Wakashuka mafundi wakajaribu kugusa hapa na pale. Gari lilikuwa limezima.Walijaribu kufanya kila wanaloweza lakini hapakuwa na matumaini. Dakika zikaanza kwenda. Masaa yakaenda. Hatimaye jioni.Abiria wakashindwa kuvumilia. Wakatoa matusi mengi lakini haikusaidia. Gari halikuweza kuwaka.Duh! Leo tunalala njiani!! Nilimweleza John japo hakunisikia.John alichoweza kuona ni chakula na mengineyo lakini si watu!! Na watu halisi pia hawakuweza kumuona yeye.Simu ilipigwa ili gari jingine liweze kuja kutuchukua. Basi lilifika likiwa na abiria wengine. Likazimishwa ili tuweze kubananishwa wote twende Dodoma. Abiria walilaani kitendo kile kwa lugha zote, huku wakilalamikia usalama wao.“Kama hutaki basi hili hapa lala utasafiri kesho!!.” Zilikuwa kauli ngumu kutoka kwa mpigadebe. Hakuna aliyependezwa na kauli hiyo. Wakati huu sikuweza kukaa na John badala yake tulikuwa tumesimama. Ni Jesca pekee aliyepata nafasi ya kukaa. Yalikuwa mateso.Walipofanikiwa kutubananisha kama viroba. Dereva akisifiwa na wapambe wake akaingia garini aweze kuendesha tuondoke.Ikaanza tena kama utani, akachokonoa kwa mara ya kwanza likagoma, akajaribu mara ya pili bado hali ileile.Akajaribu tena na tena. Injini haikuweza kuwaka. Kila mmoja akawaza lake.Watu wakakimbilia kwenye imani za kishirikina.Lakini huyo mshirikina ni nani? Hakuna aliyejua.Abiria wakashuka. Kila mmoja akarejea kwenye basi alilokuwa amepanda awali. Hapakuwa na safari tena.Usiku ukafika wanakijiji wakapika chakula na kutuuzia kwa bei mbaya sana. Hatukuwa na ujanja tukanunua.Saa nne usiku mambo yakananza kubadilika. Hali ya hewa ilibadilika na kuwa ya kushangaza hata wanakijiji walikiri kuwa hiyo haijawahi kutokea. Badala ya baridi kali la Iringa sasa lilitanda joto.Joto hilo ni kama lilimshtua John. John akasimama akataka kuondoka. Nikamzuia. Akawa anatumia nguvu!! Nikamzuia John, John akanitazama kwa jicho la hasira. Macho yake yakiwa mekundu sana.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/John alikuwa ananiona? Nilijiuliza.Lile joto likazidi. Abiria wakashuka garini.Kuna kitu hapa!! Mapambano mapya!! Nikajisemea huku nikiendelea kumzuia John.John sasa akanizidi nguvu.Akanitoka. Akashuka chini. Nikajaribu kumkimbilia.Huko nikamkuta akiwa anafanya jambo la ajabu. John alikuwa anajarfibu kuisukuma gari kwa kuitikisa.Ajabu! Ikaanza kutikisika kweli. Mtikisiko ule ukawashtua wengi. Sasa vilio vikaanza kusikika. Kila mtu kuitetea nafsi yake.Watu wakashuka upesi kwa kugombania mlango. Basi likaanguka.Lilipoanguka John akatazama mahali. Na mimi nikageuza jicho kutazama. Yalikuwa makaburiMakaburi yaliyo na historia ya kushangaza. Makaburi ambayo yalimtoa nishai mchina alipojaribu kupitisha umeme juu yake. Umeme ukagoma kuwaka.Haya yalikuwa makaburi ya Kiyeyeu.Yalikuwa yanafuka moshi wa dhahabu!!Vita!!ITAENDELEA

SITAISAHAU FACEBOOK - 3

    https://pseudepigraphas.blogspot.com/2019/11/sitaisahau-facebook.html
    Simulizi : Sitaisahau Facebook
    Sehemu Ya Tatu (3)

    Taarifa ile kila mmoja kati yangu na huyo rafiki yangu tulipokea kimshtuko. Hasahasa mimi. Nilijiuliza kwa nini? Sikupata jibu.Maisha yakaendelea!!Hapakuwa na mauzauza tena. Na kizuri zaidi hatimaye mama alizinduka kutoka katika usingizi ule wa kifo. Suzi akajivutia kwake kwamba ni maombi yamemwamsha, mimi sikuwa na lolote la kusema.Mama hakuwa na kumbukumbu yoyote ile, alibaki kushangaa shangaa tu. Kwetu ilikuwa siku ya furaha sana. furaha iliyopitiliza. Sasa mama aliweza kula peke yake na hakuhitaji msaada tena. Walau furaha yangu ikarejea huku nikisahau kuhusu imani za kishirikina na kuamini mama alikuwa katika ugonjwa wa kawaida tu!!Sasa vipi kuhusu John na ile ndoto niliyoiota? Nilijiuliza. Maana mama alikuwa amezinduka lakini John bado hakuonekana. Chuo kilishindwa kusema lolote maana mwanafunzi wa chuo kikuu anachukuliwa kama mtu mzima hakuna anayemlinda, hakuna uzio uliowekwa kumzuia asitoke, hivyo maisha ya mwanafunzi wa chuo yapo mikononi mwa msomaji mwenyewe. Chuo kitasema nini kuhusu kutoweka kwa John!! Ajabu ni kwamba hakutoweka katika mazingira yoyote yanayoelezeka bali ni ghafla tu akagundulika kuwa hayupo chuoNami nikaichukulia ile taarifa kama ilivyo. Kwanza upendo wangu kwa John ulikuwa umepoa sana. nilikuwa nimeanza kuhisi kuwa huyu si mtu mzuri kwangu.****(Mimba ya maajabu)Baada ya siku tatu. Mama akiandamana na dada yangu Suzi walirejea Makambako. Kama kawaida pesa ilikuwepo. Kwa nini sasa mama yangu asipate jambo la kukumbukwa maishani. Na Suzi naye apate la kujitambia kwa walokole wenzake. Nikawapandisha ndege. Sasa nikabaki kuishi peke yangu tena!! Sikuwa na uoga mkubwa japo sikumruhusu rafiki yangu huyu kuondoka. Tukaendelea kuishi wote.Usiku huu ambao mama yangu alikuwa ametoweka nilikumbwa na hisia ama jambo la ajabu katika mwili wangu.Kichwa kilikuwa kinauma, nilijaribu kumeza dawa lakini hazikunisaidia sana zaidi ya kuniweka katika majaribu ya kupitiwa na usingizi.“Maria!! Mi nalala shosti.” Nilimwambia rafiki yangu. Aliyekuwa amejikita katika kuangalia filamu. Hivyo hakuitilia maanani sana taarifa yangu.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Mguu na njia nikakivamia kitanda nikaanza kuutafuta usingizi. Mara hizo hisia za kuumwa kichwa zikatoweka. Nikawa katika hisia nyingine zinazokera. Nikaanza kumkumbuka sana John . nikaukumbuka usiku ule mimi na yeye katika hoteli ya kifahari. Nikakumbuka pia jinsi nilivyoanza kuishi naye kama mchumba wangu. Mara nikayakumbuka mapenzi yake.Ni hapa sasa nikaanza kuhangaika!! Nilikuwa namuhitaji John.Nilikuwa nahitaji awe nami kitandani!! Lakini hakuwepo.Nilitaka kujilazimisha kuamka niweze kukabiliana na hisia hizi lakini sikuweza. Nikahisi macho mazito sana!!Mara likawa giza nene!! Kisha ndani ya sekunde kadhaa nikajihisi kama nina mikono ya ziada najipapasa. Mh!! Nikataka kufumbua macho bado yalikuwa mazito.*****Nilikuwa nimejilaza na kanga niliyokuwa nimeivaa wakati naandaa chakula. Ile mikono ya ziada nikawa naisikia kabisa ikiiondoa bila idhini ya akili yangu!! Nikajilazimisha kuamka. Sikuweza. Sasa nilikuwa sina nguo mwilini.Kisha ile hali ya kumkumbuka John ikazidi. Nikawa katika kuhitaji huduma fulani hivi ambayo ni John pekee aliweza kunitimizia.Penzi……..Sikuchukua muda mrefu nikapata kile ninachokitamani. Lakini lilikuwa kama gogo limeniangukia kifuani. Nikaanza kupalangana kulitoa. Pumzi zikazidi kuniishia lile gogo halikutoka kifuani kwangu.Sijui kama zilikuwa dalili za kufa ama vipi.Jamani nakufaaa! Nilipiga mayowe. Sijui kama sauti ilikuwa inatoka ama la! Hofu ya kifo ikanitawala.“He!! We naye unalala uchi? Kulikoni leo?” Niliisikia sauti ikiniuliza. Nikadhani bado nina lile gogo kifuani. Nikanyanyuka kwa nguvu sana. Maria alikuwa akitazamana nami uso kwa uso. Alinishangaa nami nikamshangaa.“Unaota wewe!”“Kwani kuna nini?” Nilimuuliza huku nikijishangaa kweli nipo kitandani, uchi kabisa. Halikuwepo lile gogo pale kitandani.Wasiwasi ukatanda!“Kweli ni ndoto..ndoto mbaya.” Nilimuunga mkono Maria.****Haikuwa ndoto kama nilivyodhani na kujiaminisha kuwa ile kanga ilitoka bahati mbaya katika mwili wangu. Kichefuchefu na kukosa hamu ya kula vikaanza kuniandama, mara niwe nataka vyakula vichachu, mara nikivipata navichukia. Ile hali ikanifanya nihisi ninakaribia kuugua ama nina ugonjwa tayari. Mtu menye pesa kama mimi kwa nini niugue niendelee kukaa ndani wakati kuna hospitali zinaweza kunihudumia vyema.Majuma matatu baada ya hali ile nikafikia uamuzi wa kwenda hospitali.Sikumshirikisha Maria kwa sababu nilihisi ni jambo la kawaida sana. Nikajikokota hadi hospitali. Daktari akanipokea nikamueleza kila dalili inayonifanya nijihisi aidha nina malaria ama ugonjwa mwingine wowote ule. Sikuwaza hata kwa mbali majibu aliyoyatoa daktari.Mimba!!! Una mimba Isabela, yalikuwa majibuSijui kama akili iliniruka name nikaruka nikamkunja daktari ama ni mizimu ilifanya hivyo. Sijui!!Daktari akatapatapa akanitoa na kunituliza. Huku akisisitiza kuwa ninayo mimba. Na majibu hayo yapo sahihi. Alikuwa ameghadhabika kiasi.Maajabu haya!! Nimeipatia wapi hiyo mimba.Mimi ni muelimishaji wa mambo ya kimapenzi na mahusiano na jinsi ya kujilinda na magonjwa ya zinaa na mimba zisizotegemewa. Sasa nina mimba ya maajabu!! Anayeelimisha ameibeba…..Nimshirikishe Maria? Nilijiuliza. Nikasita. Maria alikuwa mropokaji sana angeweza kunisambazia habari hiyo na heshima yangu ikashuka. Sikuwa tayari kuabika mbele ya maelfu ya wanafunzi anaoniheshimu sana.Nikimueleza mama atanilaani!! Maana alikuwa akiniamini sana, bora basi angekuwepo John ningesema ni ya kwake.Sasa hapa namsingizia nani?Hapana sina mimba mimi!! Nilijikataa penye ukweli.Nikaenda hospitali nyingine. Jibu lilikuwa MIMBA.Akili ikahama, na nikaanza kuamini kumbe ule mtihani wa mama kupoteza fahamu ulikuwa mdogo sana. kumbe tatizo likikukumba wewe ndio utaugundua uzito wake.Nikimbilie wapi Isabela mimi!!! Nilitaharuki.Hisia zangu zikaenda kwenye lile gogo usiku ule. Nikajiona nimedhalilishwa kupewa mimba na gogo.Tena ndotoni!! Chumbani kwangu.Eeh!! Mungu nionee huruma mja wako. Nilikumbuka kumshirikisha sasa Mungu. Baada ya miezi kadhaa ya raha bila kufanya ibada.*****Dada yangu Suzi. Alikuwa ni mlokole lakini licha ya hayo yote alikuwa jasiri katika kutunza siri. Hili lilifahamika kwetu sote tangu tukiwa wadogo. Alitunza siri nyingi sana kifuani mwake. Siri za baba, siri za mama, zote alizibeba bila kuzitoa. Ama kwa hakika alikuwa mtu wa kipekee mwenye kifua haswa.Nikamuona mlokole huyu ni mtu sahihi katika kumueleza linalonisibu.Nikampigia simu tukapanga wakati tulivu kabisa wa kuzungumza.Tukapendekeza iwe usiku. Mumewe akiwa ameingia kazini.Usiku ukafika nikampigia simu.Baada ya salamu za hapa na pale nikautua mzigo.“Dada, yaliyonikuta ni makubwa mdogo wako…” nilianza kumuelezea mkasa ulivyokuwa huku nikisita kumshirikisha ukweli kuwa kuna ndoto ikiambatana na hisia ilinishika na nikahisi nafanya mapenzi ndotoni. Nilihofia ataleta ushauri wa kwenda kwa wachungaji feki kuombewa. Sikutaka kabisa kusikia mambo yake ya kilokole.Nilipomaliza ukawa wakati wake kunishauri ama kusema lolote.Kwa sauti tulivu tena iliyojaa unyenyekevu Suzi alianza kunieleza neno kwa neno.Sasa nikaanza kutetemeka alipoyatamka haya. Nikaketi chini, mapigo ya moyo yakaongezeka.Nikatamani nife kwa muda. Kisha nikakumbuka kuwa nilikuwa naogopa kufa!!! Nikalipuuzia wazo hilo.Wasiwasi ukazidi. Lakini Suzi alikuwa akiusema ukweli aliouficha moyoni kwa muda mrefu.Suzi aliongea huku akitia msisitizo kwa aliyokuwa anayasema.Ilikuwa ni historia ambayo sikuwahi kuisikia kamwe lakini sasa Suzi alikuwa ananifumbua macho. Uhusiano wa matukio alivyoupangilia ulinitia katika mashaka.Wakati nampigia simu wazo langu kuu lilikuwa kuitoa ile mimba ambayo hata sikuwa na uelewa imeingia vipi katika mwili wangu. Nikamdanganya kuwa mpenzi wangu amenipachika lakini hatukuwa na mpango wa kupata mtoto katika kipindi hicho.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/“Bela, Bela..usije ukathubutu kuitoa hiyo mimba!!! Usithubutu!!” alinikanya Suzi, hapo ni baada ya kunieleza kuwa kila msichana aliyethubutu kutoa mimba katika ukoo wetu alipoteza kizazi ama uhai.Maneno hayo yaliambatana na mifano kadhaa ya ndugu zangu ambao hadi leo hii wanalilia watoto. Umri unakwenda na hakuna dalili ya mimba. Wengine wanaachika na kuolewa tena lakini hakuna mabadiliko. Wanabaki kuwa wapweke na kumshushia lawama Mungu. Kumbe kuna siri mioyoni mwao. Mimba zilizotolewa!!Anti Rozi, mamdogo Sikujua, hao ni baadhi ya ndugu zangu waliokuwa wakinyanyasika katika ndoa zao kwa kuwa hawazai. Na kama na mimi ningethubutu basi ningekuwa katika mkondo huo.Maneno hayo makali kutoka kwa bingwa wa kutunza siri yakanichoma haswaa.Hapana!! Sipo tayari kudhalilishwa katika ndoa. Nilikiri.Kwa maongezi yale kati yangu na dada Suzi ilimaanisha kuwa sikutakiwa kuitoa ile mimba! Mimba ya gogo! Isabela niende kuzaa gogo. Hapana!Sasa ni kipi natakiwa kufanya hapa? Nilijiuliza bila kupata majibu. Ugumba sikuutaka na hata kuzaa na gogo n’do sikutaka kabisa kusikia.Suzi akaniaga nikakata simu!!Hofu kuu ilinitawala baada ya kuwa peke yangu tena. Bado nilikuwa nimeishikilia simu na nilikuwa natetemeka sana. Ni kama dunia ilikuwa imenigeukia na kunizomea baada ya kuwa imenivua nguo zote. Niliamini kuwa dunia ilikuwa inanionea. Haikuwa inanitendea haki hata kidogo. Kwa nini mimi kila siku, kwa nini wengine wanacheka, kilio kwangu tu kila siku? Mungu alikuwa ana upendeleo ama?Nililitazama tumbo langu dogo kisha nikafumba macho na kujenga picha jinsi litakavyokuwa siku za usoni. Tumbo kubwa kabisa na kila mmoja ataliona. Aibu kubwa! Halafu pia nitachekesha kiasi fulani, nilivyokuwa cha ufupi halafu na tumbo kubwa?? Fedheha.Kama hiyo haitoshi itafikia kipindi nitaugulia uchungu na hatimaye nitajifungua. Mtoto wa nani huyu? Nilijiuliza bila kupata jawabu sahihi. Sikutaka kujipatia jibu la gogo.Mawazo yakaniumiza kichwa nikameza dawa za kutuliza maumivu. Nikasinzia!Asubuhi nikashtuka kutoka usingizini. Tatizo lilelile haikuwa ndoto, nilikuwa na mimba. Nikawaza na kuwazua bado hapakupatikana jibu sahihi. Nikajaribu kupuuzia lakini suala hili liliniumiza kichwa.Sasa nikakumbuka kuwa nilikuwa na pesa za kutosha katika akaunti yangu. Sasa kwa nini niendelee kuhangaika kiasi hiki. Ina maana pesa haiwezi kutatua tatizo hili.Nikafikiria kugawana pesa zangu na mganga mwingine wa jadi. Lakini huyu sikutaka awe anatokea hapa Tanzania. Nilihitaji mgangamwingine kabisa kutoka nje ya nchi.Sikumshirikisha Maria, maana angegundua kuwa nina mimba. Hili nililiepuka sana.Kimya kimya nikampata mganga. Alijitambulisha kuwa anatokea Naijeria. Huyu alikuwa ananifaa.Nikamfungia safari! Alikuwa amejiundia ofisi yake nje kidogo ya jiji la Mwanza, maeneo ya Shamaliwa kata ya Igoma. Nililitazama tumbo langu dogo kisha nikafumba macho na kujenga picha jinsi litakavyokuwa siku za usoni. Tumbo kubwa kabisa na kila mmoja ataliona. Aibu kubwa! Halafu pia nitachekesha kiasi fulani, nilivyokuwa cha ufupi halafu na tumbo kubwa?? Fedheha.Kama hiyo haitoshi itafikia kipindi nitaugulia uchungu na hatimaye nitajifungua. Mtoto wa nani huyu? Nilijiuliza bila kupata jawabu sahihi. Sikutaka kujipatia jibu la gogo.Mawazo yakaniumiza kichwa nikameza dawa za kutuliza maumivu. Nikasinzia!Asubuhi nikashtuka kutoka usingizini. Tatizo lilelile haikuwa ndoto, nilikuwa na mimba. Nikawaza na kuwazua bado hapakupatikana jibu sahihi. Nikajaribu kupuuzia lakini suala hili liliniumiza kichwa.Sasa nikakumbuka kuwa nilikuwa na pesa za kutosha katika akaunti yangu. Sasa kwa nini niendelee kuhangaika kiasi hiki. Ina maana pesa haiwezi kutatua tatizo hili.Nikafikiria kugawana pesa zangu na mganga mwingine wa jadi. Lakini huyu sikutaka awe anatokea hapa Tanzania. Nilihitaji mgangamwingine kabisa kutoka nje ya nchi.Sikumshirikisha Maria, maana angegundua kuwa nina mimba. Hili nililiepuka sana.Kimya kimya nikampata mganga. Alijitambulisha kuwa anatokea Naijeria. Huyu alikuwa ananifaa.Nikamfungia safari! Alikuwa amejiundia ofisi yake nje kidogo ya jiji la Mwanza, maeneo ya Shamaliwa kata ya Igoma.Nyumba yake ilikuwa nzuri sana, tofauti na wale waganga waliotangulia ambao walikuwa wakiishi katika vibanda vya nyasi huku wakiwa mabingwa wa kuomba kuku na mbuzi kama njia ya kutibu tatizo.Huyu alikuwa katika nyumba nzuri sana. Huenda na tiba yake ilikuwa nzuri.Nilipokelewa vyema na kuandikisha jina langu getini. Nikafikishwa ofisini kwake. Na penyewe palivutia sana.Alikuwa anaye mkarimani wa kumsaidia kuweza kuwasiliana na wateja wasiojua kiingereza. Mimi sikuhitaji mfasiri nilikuwa najua kiingereza hivyo tulizungumza moja kwa moja.Alinisikiliza kwa makini, miwani yake machoni. Kisha akaanza naye kunipa maelekezo.Alitoa maelekezo mengi. Mwisho akaniambia nirejee usiku wa saa mbili aweze kunipatia tiba. Wakati huo ilikuwa saa kumi na moja jioni.Saa mbili nilikuwa kwa mganga tena. Sasa alinipeleka mahali anapotolea tiba.“Una mimba ya jini..jini la hatari..na ukilitoa kwa njia ya kuzaa.UTAKUFA! hakika UTAKUFA!” Alizungumza kwa msisitizo. Nikatetemeka kusikia suala la kufa.“Hongera umewahi sana..bado halijakomaa. Sasa unatakiwa ulitoe sasa hivi. Linatakiwa kutoka.”“Nitoe!.” Nilijikuta najibu huku ninatetemeka. Akacheka.“Vua nguo zako zote.” Alitoa maelekezo.Nikasita, akacheka tena. Kisha akanitazama.“Toa nguo zako!!.” Aliamuru kwa kiingereza chake chenye lafudhi ya Afrika magharibi. Alikuwa mweusi tii.Nikasalimu amri, mtaalamu huyu ndiye aliyekuwa ameshika mpini nami mikono yangu kwenye makali. Yeye mshindi.Nikasaula moja baada ya nyingine. Nikaacha chupi. Akakoroma huku akitetemeka. Nikaiondoa na hiyo iliyobaki. Sasa nijizibe wapi? Juu ama chini nikakosa maamuzi.Nikabaki katika mfadhaiko!.“Lala hapo kitandani!” aliamuru. Nikajilaza kitanda cha futi sita kwa sita chenye shuka jeupe kabisa.Mara taa ikazimwa. Giza likatawala. Kimya nacho kikatanda. Sauti ya mganga pekee akiunguruma kwa sauti ya chini ndiyo ilisikika. Mimi hofu tupu!Mara kitandani tukawa wawili. Mikono ikinipapasa. Tiba gani hii! Nilishangaa lakini sikuuliza.Katika hali isiyokuwa ya kawaida nikapatwa na kiu kikali sana ghafla. Kiu kilichokausha koo langu kabisa.“Thirsty (kiu)….” Nilinong’ona, mganga hakujibu. Nikajaribu tena kunong’ona sauti haikutoka. Lakini sikuwa katika uhitaji wa maji ya kunywa. Kuna kitu cha ziada nilikuwa nahitaji, sijui ni kitu gani sijui!! Lakini nilikuwa nahitaji.Mikono niliendelea kunipapasa. Sasa hakuwa anaunguruma tena lakini alikuwa anahema juu juu sana. Huku napapaswa huku nahisi kiu cha ajabu.Mara yule mganga akafika kifuani akaendelea kunishambulia. Kuja kutanabai alikuwa yu uchi! Hofu ya kubakwa ikanikumba. Nikajaribu kupiga kelele. Sauti haikutoka. Nikajaribu kumsukuma, alikuwa mzito kupita kiasi. Alikuwa na uzito kama lile gogo la usiku ule. Gogo lililonitia mimba. Kiu kikanifadhaisha na sasa sikuweza kujizuia zaidi nilitakiwa kupata kinywaji. Lakini sio maji wala soda.Mganga akazidi kunikumbatia. Nikafanya jaribio la kumn’gata ili asitimize kitendo chake cha kunibaka. Maajabu!! Ile ladha ya chumvichumvi la jasho ikanipendeza, nikaitamani na nikazidi kumng’ata, damu! Damu ikaanza kumtoka, sikutaka hata tone moja linipite kando. Alijirusha rusha lakini sikubanduka. Hadi pale kiu kiliponiisha.Wakati kiu kinaisha na yeye alikuwa ametulia tuli!Nimekunywa damu!! Nilighafirika. Nikasimama wima huku nikiwa siamini kabisa kilichotokea pale ndani. Nikatapatapa katika giza mara nikabonyeza bila kutarajia kitufe. Taa ikawaka!Macho yangu ana kwa ana na dude kubwa jeusi. Asili yake Naijeria likiwa limetulia kitandani. Shuka nyeupe sana bila hata tone la damu.Dude lile lilikuwa uchi wa mnyama. Lilitia kinyaa kulitazama maungo yake.Nikajifuta midomo nikaitazama. Hapakuwa na damu!! Na sikuwa na kiu tena. Kumbukumbu za kumshambulia yule mganga wa jadi zilikuwepo akilini na pia tukio la kumnyonya shingoni lilikuwa linaishi katika akili yangu. Sasa mbona hakuna damu. Mbona mashuka hayajachafuka.Nikavaa nguo zangu huku nikiziona dalili za kufa mbele yangu.Nikamtikisa yule daktari pale kitandani. Hakuamka. Na alidumu hivyo hadi nilipotoka. Hatua kwa hatua. Hadi nikatoka nje, hofu ikiwa inaniadhibu.Sikusimama sana barabarani nikapata taksi.“Nyegezi kona.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/“Nyegezi?” aliniuliza. Nikakubali.Akawasha gari tukaondoka. Sikutaka kuzungumza lolote. Nilikuwa najiuliza ni kipi kinanitokea mfululizo kiasi hicho.Simu yangu ikaita. Nikaitoa nikiamini ni Maria. Hakuwa yeye alikuwa Dokta Davis.Nikachelewa kupokea. Ikawa imekatika.Nikategemea atapiga tena! Hakupiga badala yake akatuma ujumbe.,“Nakutakia usiku mwema!”Sikumjibu.****Amani ikatoweka kabisa moyoni mwangu. Sikuyafurahia maisha yangu ya chuo. Sikuifurahia tena kazi niliyopewa na dokta Davis na kampuni yake.Nikiwa nimejaribu kwa waganga na kushindwa kupata msaada wowote. Na sikuwa nikiamini sana ulokole na imani za uponyaji sasa niliamua LIWALO NA LIWE. Nitailea mimba yangu hadi nitakapojifungua.Lakini nitakuwa na amani sana iwapo sitakuwa nachangamana na makundi ya watu. Na ili nisichangamane basi nilitakiwa kuiachia kazi niliyokuwa nimeipata. Kazi yenye kipato kizuri kabisa.Nikatokwa na machozi nilipofikiria kuandika barua ya kuacha kazi!! Roho iliniuma sana.“Na chozi langu likuangukie wewe uliyeniletea makwazo haya!!” nilitamka hayo wakati naweka nukta ya mwisho ya barua ile ya kumweleza Davis na kampuni yangu nia ya kuachana na kazi yao.Sikuweza kuwaelezea kuwa nilikuwa na mimba. Niliwaambia shule imenibana sana na utendaji wangu kimasomo ulikuwa umeshuka sana.Nikaituma kwa njia ya barua pepe kwenda kwa Dokta Davis.Barua ikawa imefika!Nikayasubiri majibu.Zile milioni milioni ziliniuma sana kuziacha ziende mbali nami.Lakini sikuwa na ujanja.Laana na zitue kwa mbaya wangu!!****Zilipita siku nne, kila siku nilikuwa napitia barua pepe yangu kutazama kama kuna majibu yoyote kutoka kwa Dokta Davis lakini mambo yalikuwa tofauti Davis hakupiga simu wala hakujibu ujumbe niliomtumia. Nilijiuliza je? Nimpigie simu ama niendelee kuvuta subira. Hali hiyo ya kungoja sana ikanitia mashaka, kumpigia simu pia nikasita kwa kukumbwa na maswali mengi. Kama hajaisoma ile e-mail itakuwaje? Na kama ameisoma pia nilitegemea maswali mchanganyiko ambayo yangeweza kunitia katika majaribu ya kumweleza Davis juu ya ile mimba ya kimaajabu! Jambo ambalo sikutaka kabisa litokee.Nikaendelea kuwa kimya!Siku zikasonga mbele. Amani finyu moyoni! Maria sasa akawa kama ndugu yangu, tuliendelea kuishi wote.*****Zilipokatika siku saba za kuikamilisha wiki moja, ustahimilivu ukanishinda, mateso ya nafsi yakanikita. Ujasiri ukaikimbia subira.Nikaamua kujaribu kupeleleza, kwanini? Davis hadi sasa hajasema neno.Sijui kwanini nilikuwa namuogopa Davis kwa kipindi hicho. Lakini sikuweza kumpigia simu.Nifanyeje? Nilijiuliza!Facebook! Jina hilo likanivamia kama jinamizi linalotisha lakini lenye msaada.Kwanini naogopa? Nilijiuliza.Ilikuwa saa moja usiku, nikiwa kitandani. Mkononi glasi ya juisi, kompyuta yangu ndogo ikiwa inamalizia hatua za kuwaka. Ilipomaliza, nikaingia katika mtandao. Tangu nitingwe na kazi niliyopewa na kampuni ya Dokta Davis na matatizo yaliyokuja baadaye nilikuwa nimeususa kabisa mtandao wa kijamii wa facebook, kwanza jina langu tayari lilikuwa kubwa pale chuoni hivyo nilikuwa napata usumbufu mtandaoni, pili sikuwa na muda kuingia kule mara kwa mara. Lakini siku hii nililazimika kuingia mtandaoni.Nia kubwa ikiwa kutazama akaunti ya Dokta, ni lini mara ya mwisho kuandika kitu mtandaoni. Kama ningejua hilo ningeweza kuhusisha hofu yangu ya kwamba aidha kuna jambo baya limemkumba Davis.Mdomo ukabaki wazi, nikapumbazwa na picha iliyokuwa katika akaunti yangu! Nikaitazama kwa makini! Haikuwa ndoto! Alikuwa yeye! Sasa ni lini ameiweka hapa? Nilijiuliza!Nikataka kumuita Maria, nikagundua hatakuwa na la kunisaidia. Kwanza ye mwenyewe hana hulka na mtandao huu!Nikabaki kuishangaa picha ya John! Alikuwa anatabasamu!John alizipata wapi namba zangu za siri za akaunti yangu ya facebook? Nilijiuliza bila kupata majibu.Mh! Au hii picha niliweka mwenyewe? Lini sasa? Nikajiuliza.Kwa hili sikushtuka sana. Nikajipa moyo kuwa huenda niliwahi kuiweka hii picha ya John bila kujitambua kutokana na kukolea katika penzi. Penzi la John ambaye hadi wakati huu hakuwa akifahamika ni wapi alipo. Nikiwa nimeamua kumpuuzia John na hiyo picha sasa nikaamua kuendelea na kile kilichonifanya niingie mtandaoni.Nikataka kuifungua akaunti ya Dokta Davis niweze kuikagua.Hata kabla sijaanza kuikagua akaunti ya Dotka, nikakutana na kitu kingine cha kushangaza, hapa sasa nilijikuta naitupa laptop na kuruka mbali nayo kama nimepigwa shoti ya umeme. Ama nimeona kitu cha kushtua sana.Ilikuwa picha nyingine, hii ilikuwa ina ujumbe juu yake 'In love with the guy!' marafiki zangu walikuwa wameishambulia kwa maoni, wengi wao wakisifia picha hiyo, huyu kwenye picha naye alikuwa anatabasamu, tofauti ya picha hizi ni kwamba John alikuwa amevaa fulana yake, lakini huyu mwingine alikuwa kifua wazi.Kwa mtazamo wangu hii picha ilikuwa picha mbovu, isiyokuwa na mvuto. Hasa hasa kwangu ambaye hadi kumsifia mvulana amependeza lazima nichunguze vitu vingi, sasa kati ya hizo sifa huyu hakuwanayo hata moja.Huyu hakuwa mwingine alikuwa ni yule mganga wa kinaijeria. Kamwe nisingeweza kumsahau maana nilimuona kwenye mwanga huku lile tukio la kujaribu kunibaka kisha akatulia tuli kitandani na lenyewe lilikuwa limenasa katika kichwa changu.Tatizo!!Bado nilikuwa wima natetemeka huku nikiiogopa ile laptop.Nani ameingia kwenye akaunti yangu na kufanya haya?Ujanja wa mtu muoga ni kukimbia shari. Palepale nikaitumia kanuni ile. Nikatimua mbio nikapishana na Maria alikuwa amekamata glasi iliyokuwa na juisi nikamsukuama yeye na glasi yake.Yeye akawahi kujizuia lakini glasi ikasambaratika vipande. Nikamsikia akitoa yowe la hofu!Maria, Maria njoo!! Nilimuita wakati huo tayari nikiwa sebuleni.Maria kwa hofu akanifuata. Nikamkumbatia. Mapigo yake ya moyo yalikuwa juu sana. Lakini yangu yalikuwa juu zaidi. Kila mmoja alikuwa katika kuogopa.Sikuweza kuzungumza chochote. Nikamvuta Maria tukaelekea chumbani. Nia yangu kumueleza kila kitu kilichonisibu hadi nikatimua mbio. Tulifika chumbani, ajabu Maria alikuwa anatetemeka kuliko mimi muhusika.Tulitulia kitandani, nikaisogeza laptop nikaanza kumuelekeza Maria, kile nilichokiona. Hasahasa picha ya yule mganga. Lakini sikumweleza lolote juu ya mimi kumfahamu.“Jamani Bela…wame’HACK’ akaunti yako..mbona haka kamchezo ka kawaida tu!.” Alinieleza.Ni kweli jambo hilo nilikuwa nalifahamu. Lakini huyu mganga amejuaje kuwa mimi naitwa Isabela hapa facebook? Nilijiuliza.Ok! Kama ni kweli ameingilia akaunti yangu na kunidhalilisha hivi. Naapa atakiona cha mtemakuni. Nilimuapia Maria. Wakati huo sikumbuki kuwa palikuwa pia na picha ya John.****CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Sikuwa katika utani. Nilikuwa nimekerwa na kitendo cha yule mganga kunifanyia huu upumbavu. Kesho yake pesa ikaongea nikawapa pesa nzuri maaskari. Nikawapa na ushahidi. Ndani ya Defender kwenda kumkamata yule mganga. Lile jaribio la kutaka kunibaka lilikuwa moja kati ya mambo yaliyonitia hasira.Niliikumbuka vyema njia na tulifika bila usumbufu.“Mzee alitutoka. Ni wiki sasa imekatika.” Mke wa mganga alitueleza kwa huzuni kuu. Moyo ukawa wa moto ghafla. Mganga amekufa!! Mbona tarehe ya ile picha na kifo cha huyu mganga vinashangaza sasa. Tarehe aliyoweka ile picha tayari alikuwa marehemu.Ewe! Mwenyezi Mungu nichukue mimi Isabela, dunia imenishinda!!! Nilisali kimoyomoyo. Mauzauza yalikuwa yamenizidi nguvu.Nilirejea nyumbani nikiwa mwingi wa mawazo. Sikumueleza lolote Maria. Nilimpita akiwa anajisomea. Zaidi ya salamu sikusema neno. Moja kwa moja chumbani nikajinyoosha kitandani nikaanza kulia.Nikiwa bado sijasinzia vizuri. Simu yangu iliita. Alikuwa ni rafiki yake na John.Kidogo nisipokee. Lakini alipopiga tena na tena nikaamua kupokea.“Mambo vipi shemu?”“Poa!” nilimjibu kwa kujilazimisha.“Sijakuelewa kabisa shem! Una matatizo gani?” aliniuliza.“Kwa nini mbona niko poa sema nimechoka tu.”“Umechoka ndo unaandika mambo gani sasa haya kwenye facebook?” alizungumza kwa hasira kidogo. Nikakaa kitako, usingizi hakuna tena!!!“Nimeandika nini kwani eeh!! Hebu ngoja.” Nikamkatia simu.Haraka haraka nikafungua simu yangu sehemu ya mtandao. Jasho lilikuwa linanitiririka. Sijui ni kipi kilikuwa kimeandikwa. Na ni nani ameandika kama ambaye ameiingilia akaunti yangu tayari alikuwa ni marehemu.“1986-201..REST IN PEACE ISABELLA” Ilisomeka hivyo katika akaunti yangu.Karibia kila mtu alikuwa anauliza kulikoni nimeandika hivyo.Lakini bora ningekuwa nimeandika mimi! Mimi hata sijaandika. Nikaanza kulia nikajigalagaza kitandani, nikavua nguo zangu. Nikavuruga nywele zangu. Nikalia kama mtoto.“Nimekukosea nini Mungu wangu eeeh!! Nimekosa nini sasa!!” nililaumu sana, uchungu ukanikaba kooni. Ukasafiri hadi moyoni, ukanisurubu kila upande. Suluba nisiyoelewa chanzo chake. Suluba kamilifu.Naelekea kuchnganyikiwa? Nilijiuliza. Lakini nikajicheka. Tangu lini mwendawazimu anautambua wazimu wake? Huenda mimi ni kichaa tayari.Munkari ya kusoma ikapotea na mitihani ilikuwa karibu kabisa.Liwalo na liwe!!Nilitamani sasa kwenda kwa viongozi wa kiroho waweze kunishauri na kuniombea kama inawezekana lakini tatizo lilikuwa katika kuwaeleza kuanzia mwanzo. Zile ndoto za John anaua na mengine yote. Niliogopa kuaibika.Nikakaa kimya na siri yangu, mateso pia yakabaki kuwa yangu!!!Nilipowaza mitihani, wazo la kuwa nina mimba pia likajileta pia katika orodha.(Sharti gumu!!)Ule ujumbe ulioonekana katika akaunti yangu, ulinishtua sana. Sasa sikuwa na ujanja tena nikafikia hatua ya kukubali kuwa yamenishinda na ninatakiwa kumshirikisha mtu mzigo huu.Kitu cha kwanza niliiondoa akaunti yangu ya facebook katika matumizi ‘deactivation’. Sikuhitaji tena kuwa katika mtandao huo. Baada ya hatua hiyo nikaandika barua ya kuomba ruhusa ya kutofanya mitihani hiyo iliyokuwa mbele yangu pale chuoni.Kwa kuwa nilikuwa nafahamika sikupata usumbufu nikapewa ruhusa hiyo upesi. Nikaamua kufunga safari kuelekea nyumbani. Lengo kuu likiwa kumueleza mama kila kitu kilichonitokea na kutishia uhai wangu. Sikuwa na ujanja mwingine.Usiku nilikuwa nimetingwa katika kujiandaa. Ni Maria pekee ambaye nilimueleza kuwa nitasafiri, na wakati huo alikuwa akinisaidia kufungasha mabegi yangu. Tayari kwa siku inayofuata.Ilikuwa saa sita kasoro dakika kadhaa. Nilitulia nikamtazama Maria na yeye akanitazama mimi. Kisha kila mmoja akageuka na kutilia maanani kile kinachosikika. Mlango ulikuwa unagongwa.Hakika ni palepale katika nyumba yangu niliyokuwa naishi.Nani huyu muda huu? Nilimuuliza Maria kana kwamba yeye alikuwa anamfahamu aliyepo mlangoni. Maria hakuwa na cha kunijibu.Nikiwa nimemshika mkono Maria tuliufikia malango, tukaulizia ni nani? Hakujibu. Tukauliza tena!! Kimyaa!!Kila mmoja akamshikia mwenzake kwa nguvu sana!!Ghafla mlango ukabamizwa kwa nguvu sana.Mungu wangu!! Watakuwa majambazi! Nilihisi.Kabla sijajua nini cha kufanya, mlango ulisukumwa bila kutoa kelele ukafunguka. Waaa!!Ghafla pakawa giza. Nikasukumwa kando na mikono ya baridi sana. Nikajaribu kupiga kelele sauti haikutoka. Nikajaribu tena sikuweza kabisa. Kisha nikasikia mlio mkubwa. Kisha kama gunia la mahindi kitu kikatua chini huku kikipiga kelele. Ilikuwa sauti ya Maria.Kama vile haitoshi nikashikwa tena na yule mtu mwenye mikono ya baridi. Akaanza kuniburuza. Moja kwa moja hadi chumbani kwangu.Akaninyanyua akanitupa kitandani.Nikajaribu tena kupiga kelele sauti haikutoka.Mara taa ikawashwa!! Chumba kikang’ara.Ana kwa ana na mtu ninayemfahamu!!Ni yule niliyemuandikia barua ya kuomba kuacha kazi!!Dokta Davis mbele yangu!!Dokta wa maajabu.Alikuwa amevalia suti nyeupe. Na hakuwa akitabasamu!!Nikajaribu kuzungumza, sikuweza!! Akacheka, nikamsikia.“Isabela……” aliponiita, nikajaribu kuitika sauti ikatoka.Maajabu haya!!“Milioni thelathini, mama yako mzazi, ama wewe!” alinieleza kwa utaratibu.Sikumuelewa. Nadhani hata yeye aliitambua hali hiyo.“Ni hivi..hadi sasa umetumia shilingi hizo…sasa unatakiwa kabla sijaweka saini yangu katika barua yako kuhalalisha wewe kuacha kazi nahitaji ufanye maamuzi. Nakupa wiki moja tu!! Uwe umerejesha pesa hizo, ama mama yako akae mbali nawe maisha yako yote na mwisho ni uchaguzi ujitoe wewe kwa usiku mmoja!!”“Usiku mmoja?” nilijiuliza. Ikawa tena kama ananisikia.“Usiku mmoja wewe na mimi na kisha nitakuacha huru na uamuzi wako wa kuamua kuacha kazi. Ole wako umueleze mtu…nitachukua maamuzi ambayo hautaamini”Sikuamini kama maneno hayo yanatoka kinywani mwa mtu huyu. Na ameweza vipi kufika Tanzania bila kunieleza. Mbaya zaidi amekuja nyumbani kwangu usiku mnene.Kabla sijamjibu lolote. Alizima taa. Kisha nikasikia mlango unafungwa. Nikaendelea kutulia kama nilivyo huku naogopa.Nilidhani yupo jirani na eneo lile. Sikuthubutu kusimama. Baada ya dakika kadhaa nikasikia hatua zikijongea kuja katika mlango wa chumba changu.Anarudi! Niliwaza nikaendelea kutulia. Jasho likilowanisha shuka zangu.Taa ikawashwa. Kwa ncha za macho nikamtazama aliyepo mbele yangu. Alikuwa ni Maria. Uso wake ukiwa umevimba.“Bela…nimeanguka mwenzako.” Alianza kunieleza. Nikageuka kumtazama huku nikipatwa na hisia za kumwogopa.“Mh!! Mbona hivyo Bela. Kimekusibu nini?” aliniuliza.Sikuwa na cha kumjibu. Nilibaki kushangaa. Maana niliamini na yeye amemuona dokta Davis lakini hakuonekana kujua lolote.Nilitamani sana kumueleza lakini hofu ya onyo la Dokta ilinitawala. Maria akanisogelea akanikumbatia. Nikahesabu alama kadhaa za vidole katika shavu lake. Huenda kabla ya kuanguka alipigwa kofi.Siku iliyofuata nilitakiwa kusafiri. Maria aliwahi sana kuniamsha lakini sikuwa na uwezo tena wa kusafiri. Onyo la Davis kuwa iwapo nitamwambia mtu yeyote atafanya anachojua.Niliunda sababu kadhaa nikafanikiwa kumshawishi Maria kuachana na safari hiyo. Alishangaa lakini hakuwa na jinsi maana msafiri nilikuwa ni mimi.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Siku ya pili hiyo zikasalia siku tano Dokta afanye yake aliyoyaahidi.Bado sikuwa nimepata jibu sahihi la kumpa. Milioni alizonitajia kwa kweli sikuwa nazo hata nusu yake. Kumuondoa mama yangu katika uso wa dunia ni jambo ambalo sikutaka kulisikia.Kulala na mimi usiku mzima. Lilikuwa ni sawa na tukio la kubakwa kwa hiari. Udhalilishaji!!Nikajilaani kumuamini sana Davis. Majuto yakaninyanyasa.Bila kumuaga Maria, niliamua kutoweka pale nyumbani kwangu na kwenda kupanga katika nyumba ya kulala wageni. Maeneo ya Igoma.Nilizima simu yangu! Siku zikazidi kukatika na sasa ilikuwa imesalia siku moja ya mimi kutamka jibu langu.Nikaiwasha simu yangu!! Nikaitafuta namba ya Davis. Nikafungua sehemu ya ujumbe nikamtumia.USIKU MMOJA MIMI NA WEWE. Nitakueleza wapi nipo uje!!Ujumbe ukapokelewa! Lakini haukujibiwa!!****Siku ya tukio ikafika!! Nilikuwa najaribu kumpigia simu Dokta huyu wa maajabu nimuelekeze wapi nipo lakini simu yake haikuwa inapatikana. Nilijaribu tena na tena bado hali ilikuwa ileile.Hofu ikanitawala! Huenda Davis ameamua kufanya anachojua yeye. Vipi kama ameamua kumtokomeza mama yangu!! Nilianza kulia baada ya kufikiria hayo.Nikiwa katika kulia simu ya chumbani ilianza kuita.Nikaitazama kisha nikaipokea.“Kuna mgeni wako..”“Mgeni?”“Anaitwa Davis.” Sauti ya muhudumu ilinijibu.Kulisikia jina hilo tu. Nikakurupuka kutoka kitandani bila kujua ni wapi ninakimbilia. Nilikuwa naogopa sana jambo ambalo lilikuwa linakuja mbele yangu. Kufanya mapenzi bila hiari na kiumbe cha ajabu sana.Haya yote niliyataka mwenyewe!! Sasa nikaanza kuhisi kuwa Davis hakuwa mtu mzuri kwangu!!Davis ni MCHAWI!!!Naenda kufanya mapenzi na mchawi!!Ghafla nikaijiwa na kumbukumbuku za chapa ya shetani 666, niulipokumbuka hili nikakumbuka na mshahara wangu ulikuwa una hizi namba, hata simu ya Osmani nayo ina 666, Davis aliwahi kunitumia nauli nayo ilikuwa na 666 na sasa nipo katika chumba namba 66 namsubiri huyu mfalme wa 666Hapana! Hapana! Niliipinga nafsi yangu. Na sasa nilikuwa nimeamua kumkimbia mchawi huyu. Kuikimbia chapa ya shetani!!!Nikawa najiandaa kukimbiaNilipokishika kitasa ili kuufungua nitoke nikakumbwa na kihoro! Mlango ukafunguka kama vile ulikuwa katika kungojea amri yangu!!Niliamini kabisa si muhudumu anayeweza kuingia katika chumba cha mteja bila ruhusa. Kwa hiyo kama sio muhudumu basi angekuwa Dokta.Hakika. Alikuwa ni yeye! Nikatazamana naye ana kwa ana, akapiga hatua mbili akawa ameingia vyema ndani ya chumba. Akaufunga mlango.Alitaka kuongea jambo lakini mlango ukagongwa tena, akasita kisha akaufungua! Alikuwa muhudumu."Barcadi, na Sprite!" aliagiza Davis bila kutoa malipo ya awali. Vinywaji alivyoagiza nilijua fika ni kwa ajili yangu na yeye!Mlango ukafungwa tena.Sasa aliufunga na funguo kisha akaziacha pale mlangoni zikining'inia.Mimi nilikuwa wima mkoba begani nikitetemeka.Davis akaliendea kochi kubwa hapo chumbani akaketi. Kisha kwa ishara akaniita!Naitwa na shetani! Nilihamaki. Nikasita kwenda."Hautaki?" aliuliza, sikumjibu!. Akaitwaa simu yake kubwa ya kisasa."Tabasamu kidogo nikupige picha Bela?" alinishawishi. Sikushawishika.Alipochoka kunichekesha nisiyecheka akatoweka na kwenda bafuni. Nikabaki chumbani peke yangu! Hapo likanivamia ghafla wazo la kutoroka! Funguo zilikuwa mlangoni! Kwanini nisikimbie? Nilijiuliza. Hapo sasa ndipo nikagundua kwanini sina ubavu wa kukimbia. Huyu bwana alikuwa anahodhi maisha ya mama yangu! Mwalimu Nchimbi.Nilipotambua hilo nikafadhaika. Nikakiendea kitanda nikajitupa, nikautupa na mkoba wangu!Ilikuwa lazima nifanye mapenzi na Davis ili kuokoa maisha yake.Nilifadhaika bila kujua nini la kufanya. Mlango wa maliwatoni ukafunguliwa. Kichwa kilikuwa kizito hata kunyanyuka kushuhudia ni kimbwanga gani kipya atakizua Dokta huyu!Akajikoholesha kama anayerekebisha koo. Nikaijua nia yake! Nikanyanyua kidogo! Macho wazi!! Yowe la uoga likanitoka kwa nilichokiona.Hili lilikuwa kubwa kupita yote!Kilichokuwa mbele yangu ni kiumbe kile kile kinachoitwa Davis.Lakini sasa hakuwa na nguo. Maungo yake yote yakawa yananidhihaki, japo alikuwa mweusi tii. Lakini ule mwanga pale ndani uliniwezesha kutambua kuwa alikuwa amelowana damu katika viungo vyake vya uzazi, na hiyo damu ilikuwa mbichi na ni kama ilikuwa inaendelea kumtoka lakini ajabu haikuwa inadondoka katika marumaru!Hapa sasa nilimsahau kwa muda mwalimu Nchimbi, nikauacha mkoba nikakimbilia mlangoni.Ajabu! Ule funguo haukuwepo tena mahala pake! Dokta akacheka sana huku akinifuata kwa hatua ndogo ndogo!Nilitegemea huenda nitapoteza fahamu. Lakini hiyo haikutokea niliendelea kushuhudia kiumbe huyu akinifuata.Alipochoka kunichekesha nisiyecheka akatoweka na kwenda bafuni. Nikabaki chumbani peke yangu! Hapo likanivamia ghafla wazo la kutoroka! Funguo zilikuwa mlangoni! Kwanini nisikimbie? Nilijiuliza. Hapo sasa ndipo nikagundua kwanini sina ubavu wa kukimbia. Huyu bwana alikuwa anahodhi maisha ya mama yangu! Mwalimu Nchimbi.Nilipotambua hilo nikafadhaika. Nikakiendea kitanda nikajitupa, nikautupa na mkoba wangu!Ilikuwa lazima nifanye mapenzi na Davis ili kuokoa maisha yake.Nilifadhaika bila kujua nini la kufanya. Mlango wa maliwatoni ukafunguliwa. Kichwa kilikuwa kizito hata kunyanyuka kushuhudia ni kimbwanga gani kipya atakizua Dokta huyu!Akajikoholesha kama anayerekebisha koo. Nikaijua nia yake! Nikanyanyua kidogo! Macho wazi!! Yowe la uoga likanitoka kwa nilichokiona.Hili lilikuwa kubwa kupita yote!Kilichokuwa mbele yangu ni kiumbe kile kile kinachoitwa Davis.Lakini sasa hakuwa na nguo. Maungo yake yote yakawa yananidhihaki, japo alikuwa mweusi tii. Lakini ule mwanga pale ndani uliniwezesha kutambua kuwa alikuwa amelowana damu katika viungo vyake vya uzazi, na hiyo damu ilikuwa mbichi na ni kama ilikuwa inaendelea kumtoka lakini ajabu haikuwa inadondoka katika marumaru!Hapa sasa nilimsahau kwa muda mwalimu Nchimbi, nikauacha mkoba nikakimbilia mlangoni.Ajabu! Ule funguo haukuwepo tena mahala pake! Dokta akacheka sana huku akinifuata kwa hatua ndogo ndogo!Nilitegemea huenda nitapoteza fahamu. Lakini hiyo haikutokea niliendelea kushuhudia kiumbe huyu akinifuata.Nikawa narudi kinyumenyume hadi nikafika mwisho. Davis akazidi kunisogelea. Sasa alikuwa amenifikia!Akanishika mkono! Kiganja chake kilikuwa cha baridi sana!! Akanitazama usoni, nami nikamtazama. Akaniachia kisha akasonya kwa dharau. Akakiendea kitanda akajirusha pale!Bado mashuka hayakuchafuliwa na damu mbichi.Hakika sikuwa tayari kufanya mapenzi na kiumbe kile cha ajabu!! Niliapa!Muwasho ulianza kama wa kawaida tu katika chuchu yangu moja, nikajikuna, muwasho ukapita.Mara ile chuchu ya pili nayo ikawasha nikaikuna ikatulia.Sasa zikawa zinawasha zote kwa pamoja, muwasho usiofanana na ule wa kumwagiwa upupu. Huu ulikuwa wa tofauti. Nikatazama kitandani yule Dokta alikuwa amesinzia. Nikaitoa Sidiria yangu ili nijikune vizuri. Nikabaki bila nguo kwa juu. Nikafanya jitihada za kujikuna!! Ile hali ya kujikuna ikautwaa uoga wangu nikahamia katika hisia za raha! Raha ya kujipapasa! Mazito!Ni heri ningekuwa na mikono mitatu huenda ningeweza kuipinga hali hii. Maana sasa kati kati ya mapaja muwasho ukazaliwa. Niache wapi? Nikune wapi? Nikajiuliza.Raha ikawa karaha!CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Nikaanza kulia huku nagalagala chini. Nilijikunja na kujikukunjua bila mafanikio! Nilihitaji msaada wa hali ya juu! Msaada wa kukunwa!Mara kama ameshtuka ndotoni yule kiumbe pale kitandani aligutuka. Akasimama akanitazama kisha akachuchumaa. Akanisogelea karibu zaidi. Sikuwa na nguvu mwilini.Hakuwa na nguo nami sikuwa na nguo!Kama vile alijua ninapowashwa! Akaanza kunikuna kwa namna ya kupapasa! Nikahisi raha ya kipekee ambayo sijawahi kuipata duniani. Bila kujitambua nikamkumbatia Dokta Davis.Akaendelea kunikuna! Sasa nilikuwa hoi.Fanya unalotaka! Ndivyo ningeweza kusema kama angeniuliza.Lakini hakuniuliza!Nikajikuta katika ulimwengu wa mahaba mazito! Kama kukunwa hakika nilipata mkunaji!Muwasho ukatoweka kabisa. Jasho mwili mzima.Nikapitiwa na usingizi kutokana na uchovu.*****Saa kumi na moja alfajiri hapakuwa na Dokta wala nguo zake pale ndani. Nilikuwa peke yangu.Maumivu kifuani kama niliegemezewa gogo! Maumivu haya yakanikumbusha ndoto za kuota nazini na gogo!Nikashtuka! Mbio mbio bafuni nikatapika!Kumbukumbu ya kufanya mapenzi na Davis usiku uliopita ilinijia kichwani!Yupo wapi sasa shetani yule? Nilijiuliza.Ile hali ya maungo ya Davis kuwa na damu ilinisisimua na kujiona kuwa sina thamani tena ulimwenguni.Kama sina thamani, bora nife! Niliamua!Nitakufa vipi sasa? Hilo likawa swali la kujiuliza. Nikayakumbuka maneno ya dada Suzi. Kuhusu utoaji mimba na madhara yake!Nikafikia maamuzi ya kutoa mimba! Kisha nitajua nini cha kufanya!Wakati natoka pale chumbani na kupita mapokezi nilikumbana na swali, "mwenzako bado yupo? Maana tunataka kufanya usafi". Mwenzangu? Mwenzangu nani? Wanamaamisha Dokta Davis. Sikuwajibu nikajongea na kupotea eneo lile.Nikaamua kurejea nyumbani kwangu. Tayari nilikuwa na taarifa kuwa mama anaendelea vizuri kiafya!Tumbo! Tumbo! Tumbo lilianza ghafla kuniuma, upande wa kushoto!! Nililalamika sana, dereva wa teksi akaegesha pembeni akaniuliza kulikoni.“Nipeleke hopitali!! Nipeleke nitakulipa” nilimsihi huku nikizidi kuugulia.Kama nilivyoomba akaendesha hadi hospitali iliyokuwa jirani. Alikuwa ni kati ya masalia ya watu wakarimu waliobaki hapa duniani. Aliwahi kuwaita manesi. Japo walichelewa lakini walikuwa kunibeba kutoka ndani ya gari lile.Moja kwa moja nikakimbizwa wodi ya wanawake!!Nikapatiwa huduma ya kwanza!!Baada ya muda damu ikaanza kunitoka!! Nilikuwa nimeingia katika siku zangu ama? Nilijiuliza bila kupata majibu!! Mjamzito naingia katika siku zangu!!Kadri damu ilivyokuwa inavuja ndivyo maumivu yalizidi kupungua na hatimaye kuisha kabisa.Majibu ya daktari yalikuwa kwamba. Ni tatizo la kawaida tu kwa mwanamke kuumwa tumbo akiwa anaingia katika siku zake. Lakini mimi nilikuwa mjamzito sasa!! Au mimba imetoka. Sikutaka kuondoka na dukuduku. Nilimvuta daktari tukazungumza kinagaubaga.Akafikia hatua ya kunipima ujauzito!!Hakuchukua muda mrefu akarejea. Alikuwa hajachangamka na ni kama alikuwa na jambo anahitaji kunieleza.“Ina miezi miwili sasa!!.” Aliniambia katika namna ya mshangao.“Ni maajabu wewe kuingia katika siku zako!!” aliendelea. Mimi nikiwa msikilizaji.“Kwa hiyo ni nini Dokta.”“Rudi baada ya siku saba. Kama ikiendelea hivyo. Ama la basi utakuwa mshtuko tu.” Alimaliza.Nikaondoka zangu huku nikiitazama dunia jinsi inavyonizomea.****Maria hakushangazwa na hali yangu ya kuvuja damu!! Aliamini ni kawaida tu kwa msichana. Hakujua kama nina mimba!!Siri nikabaki nayo. Mimi na daktari!!Siku ya kwanza, ya pili, ya tatu….damu zinaendelea kuvuja tena bila kukoma!!!! Kazi ikawa ipo kwangu kila mara kubadili nguo zangu.Siku ya nne, ya tano….bado tatizo likawa lile lile. Mateso sasa!!! Mimba gani hii!!!Sikuingoja siku ya saba ifike. Nikarejea hospitali.Daktari alinipokea vizuri. Nikampa kwa siri kiasi fulani cha pesa ili aweze kunihudumia kwa upendeleo.“Hadi leo bado damu inakutoka?” alishangaa daktari. Nikamthibitishia kuwa bado zinatoka tena mfululizo.Akakuna kichwa chake chenye mvi nyingi kasha akahamia kidevuni. Na penyewe akajikuna kwa muda.“Hebu njoo…” akanipeleka katika chumba kingine. Akanipima tena mimba.Daktari akashtuka!!!“Kwa mara ya kwanza katika miaka yangu 20 ya kazi!!!” alihamaki.“Nini? Nini dokta.” Niliuliza.“Wiki iliyopita ilikuwa na miezi mingapi vile.”“Miwili ulisema.”“Sasa imefikaje miezi sita leo???” aliniuliza. Nikahisi kuzizima. Nikakaa chini!!!Daktari naye alikuwa ana hofu!!****Ni kama daktari alikuwa haamini ambacho amekiona, katika mwili wangu na alichokuwa akifanya pale ni kunitoa tu katika hofu. Mabadiliko ya mimba yangu yalimfanya achanganyikiwe.Tulirejea katika chumba chake cha ofisi. Mazungumzo yaliyokuwepo ni juu ya kuitoa mimba ile.Daktari alikataa kata kata akidai kuwa mimba ikifikisha miezi sita na msichana akijaribu kuitoa basi lazima atapatwa na matatizo na kuna uwezekano wa kufa.Maelekezo ya daktari yaliyoambatanishwa na neno KUFA yalinipa ahueni ya nafsi kwa sababu nilikuwa nataka kufa. Sikuwa na ujasiri wa kujiua na hakika nilikuwa naogopa kufa.Lakini kufa kwa namna anayoitaja daktari hata hakunipa hofu badala yake nikavutika na kumsihi anisaidie kuitoa ile mimba.Mazungumzo yalikosa kabisa muafaka. Daktari yule alikuwa mbishi sana hakutaka kushiriki katika utoaji mimba huu. Nilipoona daktari huyu amekuwa na msimamo sana niliamua kutumia njia fulani ambayo hugeuza ukweli kuwa uongo na uongo kuwa ukweli. Nikaangusha mezani shilingi laki mbili. Akazikataa, nikaaga nikatoka. Niliporejea niliziongeza zikafika laki nne.Daktari akazikodolea macho, kisha akatazama kushoto na kulia.“Umekuja na nani?” akaniuliza.“Mwenyewe!” nikamjibu. Akatazama tena kushoto na kulia kisha akazikwapua zile pesa akazizamisha katika sehemu zake za siri. Nikakwepesha macho.Akanifanyia ishara ya mkono. Nikamfuata hadi katika chumba kilichokuwa na harufu kali ya madawa. Akakifunga na funguo tukabaki wawili tu! Kimya.Daktari alikuwa na hofu. Nililitambua hilo. Sikutaka kuuliza chochote.“Toa nguo zote.” Aliniamuru. Kauli yake ikanikumbusha kauli ya yule Mnaijeria aliyetaka kunibaka kwa kujifanya ananifanyia tiba ya asili. Huyu sasa alikuwa daktari, nikaamua kucheza pata potea. Kwanza nilikuwa natokwa damu. Sidhani kama angeweza kujaribu kunibaka.Nikaziondoa zote, wakati huo yeye alikuwa amejikita katika kuchanganya madawa yake ambayo sikuelewa kazi yake ni ipi. Nikabaki kumsubiri.Njoo hapa!! Aliniamuru huku akinielekezea kitandani.Geuka hivi!! Nataka kukuchochoma sindano. Nikageuka huku nikiwa katika uoga. Kifo! Nilikuwa naogopa kufa.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Nikahisi kitu cha baridi kikinipapasa. Nikauma meno yangu kungoja uchungu wa sindano. Nilingoja huo uchungu lakini hamna nilichohisi.“Acha kujikaza wewe sindano itakatikia ndani.” Alinigombeza daktari. Nikashangaa hizo lawama zinatoka wapi wakati mimi hata sijajibana. Alipoona simjibu kitu akanichapa kibao. Nikashtuka.“Mkubwa hivyo unaogopa sindano alaa!!” alinigombeza. Sikumjibu!!Nikatega tena aweze kunichoma!! Hali ikawa vile vile.“Sasa mimi nakuchoma hivyo hivyo.” Alichukua maamuzi yake binafsi.Nikageuka. Nikayasubiri maumivu!!Badala ya maumivu nikakumbana na yowe kubwa kutoka kwa daktari. Nilipogeuka na mimi nikiwa na hofu nikamkuta amekaa chini. Mbali na mimi. Alikuwa ana hofu!! Jasho likimtoka.“Daktari!!.” Nilimuita. Hakunijibu, alikuwa katika mshangao. Alikuwa akinitazama kwa wasiwasi.Nilikuwa siijui tena thamani ya kuwa na mavazi na aibu ya kuwa uchi. Nilitapatapa hivyohivyo pale ndani. Daktari akiwa bado ananishangaa.“Vaa nguo!” aliniamuru kwa sauti ya chinichini. Nikaziendea nguo zangu na kuzivaa.Kisha nikamfuata hadi ofisini!“Chukua pesa zako!!” alinikabidhi pesa zile. Nilisita kuzichukua akanisihi nizichukue. Nikatii!!Nini kimetokea daktari? Nilimuuliza. Hakunijibu bali alisikitika.Kisha akaanza kunielezea juu ya nini alichokiona. Ilikuwa ni alama ya maajabu katika mwili wangu sehemu za makalio. Mwili wangu ulikuwa umetoboka na matundu hayoyaliweza kuonyesha alama ya ‘666’.Mungu wangu!! Nikashangaa, daktari yeye akawa ni wa kusikitika tu!“Usipokuwa mkweli utakufa wewe na familia yako nzima kama wenzako.”“Wenzangu? Wapi”“Mnaomtumikia”“Nani?” nilihoji kwa hofu.“Mmiliki wa hiyo alama. Kwani siku wanakuwekea hawakukuambia.” Alinihoji kwa utulivu mkubwa.Nikawa kama mwendawazimu na sikuwa na lolote ninalojua kuhusu hiyo alama katika makalio yangu.“Daktari sijui lolote mbona.”“Haya shauri zako, atakufa mama, baba, mdogo wako, dada, shangazi, mjomba, wifi, na marafiki ikibidi kisha watakumalizia wewe tena kwa uchungu mkubwa.” Daktari alinieleza haya kama simulizi ya kawaida huku akinitajia orodha ya watakaokufa. Kwa lugha nyepesi alikuwa kama babu anayemsimulia mjukuu simulizi ya kutisha. Nikatetemeka sana!! Vifo!!“Sasa daktari jamani mimi ninakuficha nini. Mimi sijui kitu.” Nilishindwa kuendelea kuongea nikaanza kulia. Nililia sana maana nilikuwa nimekata tamaa. Mbaya zaidi nilikuwa nimepigwa chapa ya 666.Badala ya maumivu nikakumbana na yowe kubwa kutoka kwa daktari. Nilipogeuka na mimi nikiwa na hofu nikamkuta amekaa chini. Mbali na mimi. Alikuwa ana hofu!! Jasho likimtoka.“Daktari!!.” Nilimuita. Hakunijibu, alikuwa katika mshangao. Alikuwa akinitazama kwa wasiwasi.Nilikuwa siijui tena thamani ya kuwa na mavazi na aibu ya kuwa uchi. Nilitapatapa hivyohivyo pale ndani. Daktari akiwa bado ananishangaa.“Vaa nguo!” aliniamuru kwa sauti ya chinichini. Nikaziendea nguo zangu na kuzivaa.Kisha nikamfuata hadi ofisini!“Chukua pesa zako!!” alinikabidhi pesa zile. Nilisita kuzichukua akanisihi nizichukue. Nikatii!!Nini kimetokea daktari? Nilimuuliza. Hakunijibu bali alisikitika.Kisha akaanza kunielezea juu ya nini alichokiona. Ilikuwa ni alama ya maajabu katika mwili wangu sehemu za makalio. Mwili wangu ulikuwa umetoboka na matundu hayoyaliweza kuonyesha alama ya ‘666’.Mungu wangu!! Nikashangaa, daktari yeye akawa ni wa kusikitika tu!“Usipokuwa mkweli utakufa wewe na familia yako nzima kama wenzako.”“Wenzangu? Wapi”“Mnaomtumikia”“Nani?” nilihoji kwa hofu.“Mmiliki wa hiyo alama. Kwani siku wanakuwekea hawakukuambia.” Alinihoji kwa utulivu mkubwa.Nikawa kama mwendawazimu na sikuwa na lolote ninalojua kuhusu hiyo alama katika makalio yangu.“Daktari sijui lolote mbona.”“Haya shauri zako, atakufa mama, baba, mdogo wako, dada, shangazi, mjomba, wifi, na marafiki ikibidi kisha watakumalizia wewe tena kwa uchungu mkubwa.” Daktari alinieleza haya kama simulizi ya kawaida huku akinitajia orodha ya watakaokufa. Kwa lugha nyepesi alikuwa kama babu anayemsimulia mjukuu simulizi ya kutisha. Nikatetemeka sana!! Vifo!!“Sasa daktari jamani mimi ninakuficha nini. Mimi sijui kitu.” Nilishindwa kuendelea kuongea nikaanza kulia. Nililia sana maana nilikuwa nimekata tamaa. Mbaya zaidi nilikuwa nimepigwa chapa ya 666.“Ndio maana nimejishangaa sana, iweje leo nikubali kuchukua rushwa, nikubali kutoa mimba msichana. Ama kweli kila mwenye alama hii hatakataliwa na dunia kwa lolote.” Daktari alinong’ona kama anasema mwenyewe vile. Nilisikia kila kitu.Sasa nilikuwa nimechanganyikiwa!“Nitakusaidia.” Alinyanyua uso daktari akanieleza huku akinitazama vyema usoni.Nilifarijika sana kusikia maneno yale. Kisha akaendelea, “Lakini uwe mkweli kwa kila kitu. Ukijaribu tu kuficha lolote lile. Nasema ukijaribu kuficha lolote lile. Wewe, marafiki na ukoo wako wote utatokomea. Mimi nakueleza haya kama mzee wako, katika kipindi changu cha miaka ishirini ya udaktari nakutana na matukio mengi. Lakini hili ni la tatu katika maisha yangu. Wenzako wawili, mmoja miaka saba imepita na mwingine mwaka juzi, nilitaka kuwasaidia lakini wakaleta ujanja ujanja. Tuliwazika!! Aah!! Hatukuwazika insearch labda niseme tuliyafukia mabaki yao.” Alimaliza kunielezea kisha akashusha pumzi kali sana.Macho yangu nilihisi kama yanajilazimisha kutazama mbele. Machozi yalikuwa yamezidi. Mapigo ya moyo yalikuwa juu, sasa nikaanza kuamini niliyokuwa nayatazama katika filamu za kinaijeria. Kumbe uchawi upo? Hakika uchawi upo!!“Kesho njoo!!” alinipa ahadi hiyo.“Kwa hiyo sitatokwa damu tena?” niliuliza swali la kijinga.“Kwani mimi ndiye niliyekuwekea” Daktari naye akanipa jibu la kijinga kama nilivyotegemea.“Usimwambie mtu yeyote kuhusu maongezi haya.” alinionyaNikaaga! Kiguu na njia hadi nikaipata taksi.Njia nzima nilikuwa nawaza na kuwazua. Zile ndoto zangu za kumjengea mama nyumba nzuri, wadogo zangu kusoma shule za kimataifa, mimi kuwa maarufu zaidi chuoni, ndoto za kwamba nataka kuwa mtakatifu! Zote zilikuwa zimekufa. Sasa nilikuwa nahangahika huku na huko huku nikisurubika na mateso ya nafsi.Swali likajengeka katika kichwa changu. Dokta Davis linizuia nisimueleze mtu kuhusu mambo haya. Sasa daktari ananisihi nisifiche kitu. Hapa sasa nimuamini nani? Nilijiuliza.“Kata kushoto!!” nilimuelekeza dereva.Mawazo yangu yakawa yameishia hapo.Maria aliniona kuanzia mbali. Akanikimbilia, akafika akanikumbatia.“Da Bela jamani. Mbona mnyonge hivyo!.”“Nimemkumbuka sana John.” Nilidanganya, huku siri kubwa nikiwa nayo mwenyewe.Maria akaniongoza hadi ndani. Nikajibweteka kwenye sofa sebuleni. Maria akaniletea maji ya matunda niliyokuwa nayapenda, nikayagida kwa fujo kisha nikagundua kuwa nilikuwa na njaa. Chakula kilikuwa tayari!! Maria akanihudumia. Sasa niliweza kupumzika!! Sikutaka kwenda chumbani. Nililala sebuleni.Kila baada ya masaa kadhaa nilikuwa naamka na kubadilisha pedi na nguo ya ndani kisha kuoga. Hali hii japo ilikuwa haijatimiza hata mwezi kwangu ilikuwa mateso makubwa. Sasa sikuweza kwenda kwa marafiki wala nisingeweza kwenda. Nilijihisi ninanuka, japo Maria hakuwa ameniambia hata siku moja lakini nilijijua mwenyewew kuwa sikuwa kawaida hata kidogo.Siku hii ikamaliza bila tatizo!!(Mateso ya 666)Asubuhi ya siku iliyofuata niliwahi sana kuamka. Badala ya kumuomba Mungu anijalie uzima na aniepushe na matatizo haya mimi niliwekeza imani yangu yote iliyosalia kwa daktari yule ambaye hadi sasa sikuwa namfahamu jina lake.Saa nne kamili asubuhi. Nilikuwa katika mlango wa kuingia ofisini kwake. Japo kulikuwa na watu kadhaa waliohitaji kuonana naye. Mimi nilipewa kipaumbele, nikawapita nikaingia ndani.Ahaaa!! Binti! Vipi kwema? Alinichangamkia sana. Nikamjibu salamu yake. Nikakaa kitako kumsikiliza.“Ngoja niwaondoe hawa watu hapo nje. Wewe nitakupigia simu uje mahali.” Alininong’oneza. Nikamuelewa nikampatia namba yangu ya simu kisha nikaaga.****CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Sikuchoka kusubiria. Japo alichukua muda sana. Baada ya masaa mawili na nusu. Aliniita odisini kwake. Nikaenda upesi nikamkuta akiwa pamoja na mwanaume ambaye laiti kama ningekutana naye wakati ule ambao nilikuwa na jeuri ya pesa sidhani kama alikuwa na hadhi ya kupokea salamu yangu. Nilimsalimia kwa kuwa tu alikuwa pamoja na daktari.Nilipomsalimia badala ya kunijibu, akanikonyeza!! Nikataka kusonya nikasita.Kwa ncha za macho yangu nikamtazama mwanaume huyu, kuanzia mavazi yalivyochoka, amechakaa nywele zake na hata ngozi ilikuwa imepauka. Nikaamini hata akili yake haiku sawa. Nilipokumbuka jambo hili la akili kutokuwa sawasawa nikaamini atakuwa ni mgonjwa wa akili. Na daktari huyu alikuwa katika kumpa tiba. Kimoyomoyo nikamsamehe kwa kosa la jinai alilofanya la kunikonyeza.“Binti..kama nilivyokueleza jana!! Usisite kuusema ukweli wote. Ukificha haitakusaidia kitu zaidi ya kuuangamiza ukoo wako wote.” Alinieleza kwa utulivu. Yule tahira akacheka.“Sawa daktari.” Nilimjibu. Tahira akacheka tena!! Akaanza kunikera.“R.I.P mtu wako niliyekwambia ndio huyu.” Sasa daktari hakuwa akizungumza na mimi, bali alikuwa akisemezana na yule tahira. Nikashtushwa na hali ile, ina maana ananikabidhi mimi kwa yule chizi au alikuwa anamtania. Niliomba iwe hivyo lakini haikuwa. Alimaanisha.Sasa tahira akanivagaa akanishika mikono. Nikajitoa mikononi mwake akacheka!!“Nenda naye ofisini kwake huyo akakupe maelekezo. Anaitwa R.I.P”“Na yeye anaitwa nani.” Yule mtu niliyedhani ni tahira sasa aliuliza.“Jitambulishe binti.” Tahira alinieleza huku akinishika makalio. Kidogo nimtukane. Nikasita baada ya kuona daktari hakushtushwa na jambo hilo.Nitafanya nini sasa!! Nikaanza kufuata uelekeo alionipeleka. Mara kwa mara alikuwa anacheka. Tulipishana na watu wengi lakini hakuna aliyemshangaa. Huyu sio tahira!! Nililazimika kuaminiMlango ukafunguliwa nikaingia ndani!! Ofisi yake ilikuwa na hewa nzito sana ya madawa lakini yeye aliifurahia.Karibu ukae…aaah!! Usikae kwanza hebu njoo huku.” Akanivuta kwa nguvu, nikamfuata. Akafungua kabati moja kwa fujo.Mungu wangu!! Maiti!! Nikaruka pembeni, akacheka!!“Binti hawa nao walikuwa wajing wajinga tazama….njoo..njoo” akaniita. Nikasogea.Akavuta kabati jingine likafunguka.Maiti ya mwanamke. Akamgeuza. Alikuwa na alama ya 666 katika makalio yake. Maiti huyu nilikiri kuwa kabla ya kuwa hivi alikuwa mrembo sana.Sijui nini kilimuua maskini!!Akanipeleka katika kabati jingine akavuta tena. Akatoka mtoto mdogo. Hana kichwa na y eye ana alama ya 666..R.I.P kazi yake ilikuwa kucheka tu kama tahira. Wakati mimi nilikuwa katika hofu kuu.Sasa nilikuwa nimechanganyikiwa. Maiti karibia tano zilikuwa pamoja nasi, waziwazi. Amani ikatoweka moyoni.“Na wewe ukificha neno lolote tu!! Utakufa na vizazi vyote vitakavyofuata.” Aliongea bila kucheka sasa.Nilikuwa natetemeka.“Hata huyo uliyemkalia na yeye nadhani ni walewale..hebu funua.”“Wapi?” nilimuuliza, likiwa neno langu la kwanza hapo ndani.Akanionyesha kwa kidole. Ni pale nilipokuwa nimekaa. Nikafunua nikiwa natetemeka.“Mamaaa!!” nikapiga kelele. Kumbe nilikuwa nimekaa juu ya maiti. R.I.P akacheka sana!!Zile dharau zangu zikawa zimeishia hapa!! Nikamuheshimu!!!R.I.P hakujali kama nilikuwa nimeshtuka ama la! Aliendelea kuongeaongea huku akiwatukana matusi mazito ya nguoni wale maiti kama vile wanamsikia. Hakika alifanana na mtu aliyerukwa akili. Kuishi na maiti napo kazi sana huenda ndo maana amechanganyikiwa.“Ulisema unaitwa nani vile.”“Naitwa Isabela.”“He!! Unaitwa Isabela, yupo mwenzako humu hebu njoo umuone.” Akanivuta kwa kutumia nguvu sana hadi mkono ukashtuka. Yeye hakujali hayo. Akanivuta vuta hadi tukafikia kabati jingine. Nikajiandaa kushuhudia maluweluwe mengine.“Hili nalo lilikuwa linakula nini sijui likanenepa hivi. Majitu mengine mapumbavu sana ujue. Heri yako wewe haujanenepa sana.” Alizungumza peke yake.Akatumia mikono miwili akavuta. Likatoka bonge la mwanamke. R.I.P akaanza kucheka, kicheko kikubwa hadi akatoa machozi.“Anaitwa Isabela huyu, mpumbavu sana huyu alienda kunenepeana huko. Amewasumbua sana siku ya kumleta humu ndani. Kuna vindugu vyake, vyembamba hivyo basi likawa linawaponyoka. Linaanguka puu!!”alisimulia huku anacheka. Mimi sikuwa namuelewa.Kisha tukarejea tena mahali tulipokuwa nikalazimika kukaa juu ya lile jokofu la kuhifadhia maiti.“Au nimlete Isabela make nae, Isabela bonge.” Aliniuliza. Mimi nikawa namshangaa. Yaani alikuwa kama mpumbavu fulani.“Isabela….umewahi kufa wewe?” aliniuliza.Swali gani sasa hili la kijinga!! Nikawaza.“Bado”“Mwenzako niliwahi kufa. Na wewe una hamu ya kufa.”He!! Umewahi kufa….kivipi.”“Kwani mtu akifa anakuwaje?” aliniuliza, sikujibu.Akaendelea, “hebu tuachane na hayo..msichana mdogo kama wewe ukifa sio vizuri ujue.”“Kama ukiwa makini hautakufa. Tena wewe hautakufa, nitakusaidia usife sawa!!”“Sawa!!” nilijibu kwa nidhamu kubwa.“Njoo huku…”Nikamfuata hadi mahali patulivu kabisa. Sasa hii ilikuwa ofisi kweli. R.I.P akanipokea. Akaniacha ofisini kwa muda, kisha akaingia tena baada ya dakika kadhaa.Hakuwa yule tahira, hakuwa mchafum,chafu kama nilivyokueleza mwanzoni. Huyu alikuwa na hadhi ya yule mvulana ninayemuhitaji. Alikuwa mtanashati.Hakuwa akicheka hovyo! Alikuwa makini na mtaratibu.Roho Iliyo Potea (R.I.P). Alianza kwa kujitambulisha jina lake halisi. Kisha akaniupongeza sana kwa ujasiri wangu hadi kufika hapo.Akajieleza kwa ufupi maisha yake ya utafutaji huku na kule hadi alipojikuta akitafuta kwa njia za mashetani. Ni katika maelezo haya alinieleza juu ya namba 666. Nilishangazwa sana na maelezo yake lakini nilipiga moyo konde nikiamini tiba ipo.Baadaye akanieleza jinsi alivyojitoa katika harakati hizo za kumtumikia shetani. Haikuwa njia rahisi. Aliwapoteza ndugu zake kadhaa lakini mwisho akawa amejikomboa.Hiyo chapa uliyopigwa lazima ifutwe! Ni njia hiyo tu ya kukukomboa kutoka ufalme huo.Nilikuwa makini nikimsikiliza.!CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/ITAENDELEA

Blog