Search This Blog

Sunday 19 June 2022

KIVULI (THE CATCHING SHADOW) - 2

 





    Simulizi : Kivuli (The Catching Shadow)

    Sehemu Ya Pili (2)



    Wiki nzima iliyofuatia Johari alikuwa mtu mwenye huzuni, na alijaribu kuficha hisia zake asionekane huzuni yake. Ila huzuni ilimtawala hivi kwamba bosi wake kazini alimuuliza baada ya kikao kimoja , kama ana tatizo lolote lililomtatiza, pia wafanyakazi wezie ‘walinotisi’ na kumuuliza kulikoni. Hadi mteja wa benki hiyo bwana Jama Bhanji ambaye alihudumiwa ‘private’ kwenye benki hiyo mara kwa mara na Johari alinotisi huzuni ya Johari na alimuhoji kulikoni alipoa sana.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kwa kuwa Malcom alikuwa tayari keshaenda nje nchi kama kawaida yake -maana yeye Malcom alikuwa akifanya kazi wizarani kuhusu masuala ya mashirikiano ya kimataifa- Johari hakuwa hata na hamu ya kuwahi kwake, alibakia ofisini hadi jioni sana, katika ofisi yake hata kama alikuwa hana la kufanya alibaki kakodolea macho yake dirisha la kioo la ofisi yake iliyokuwa ghorofa ya nne ya jengo la benki hiyo ya NIB, hivyo akabaki hapo akiangalia jinsi giza lilivotua na majengo marefu ya mjini kati yakiwashwa taa ndipo aondoke kwenda kwake, huko mitaa ya Kijitonyama.

    Aliwaza na kuwazua na hatimaye akafanya maamuzi kuwa, kwa kuwa kashahangaika sana kwenda mahospitali ya nchini na nje ya nchi basi suluhisho lililobaki ni kwenda kwa mganga wa kienyeji. Maamuzi yake yalifika huko kwasababu alifahamu fika tatizo lake lilitokana na kuhusika na kundi la kiharifu na kiuaji la mapanya. Na alifahamu fika kuwa wezie waliokuwa katika kundi hilo eidha walikufa kinyama ama kupotea, aidha Johari alielewa kuwa yeye pekee ndiye alliyesalia katika lile kundi la mapanya na kwamba kukosa kwake kupata ujauzito ni sehemu ya lana ya matendo yale maovu. Hivyo kwa imani kubwa aliamini mganga wa kishirikina ndiye angekuwa na msaada mkubwa sana kwake kwa tatizo hilo lake la muda mrefu.

    Basi, siku moja wakati mumewe yuko nje nchi, bi. Johari alifunga safari ya mbali hadi katika kijiji kilichoitwa Sadani, kilichokuwa porini mbali kweli na kwenye kutisha. Huko alienda kumuona mganga. Mganga aliyekuwa mashuhuri, na watu toka kona zote za Tanzania nzima walienda kwa nguli huyo wa kishirikina kupata nusura ya matatizo yao.



    Na Johari alipowasili tu kwa mganga huyo alikubali kuwa kweli alienda kwa mganga na sio matani. Kwanza palikuwa chini ya mti mnene na mkubwa wa mbuyu uliotisha na kufuka moshi, ulioning’inizwa vitambaa vyeusi na vyekundu na mahirizi makubwa makubwa yaliyotuna na kupumua. Johari aliingia kwa mganga huyo huku akitetemeka na kujifunga vizuri kanga zake alizovaa huku kaukumbatia mkoba wake alokwenda nao hapo. Mganga mwenyewe alikuwa pande la mtu, aliyejaa mahirizi na macheni ya mifupa ya wanyama na yale maganda ya konokono na viumbe wa baharini, usoni kajichora kwa maandishi meupe, huku akiwa kavalia kaniki na huku yuko kifua wazi.



    Kabla hata Johari hajaeleza shida yake huyo mganga alimtolea macho makali sana Johari, macho makali kama ya chuki na kuanza kuongea, “Kweli leo umenijia wewe mwanamke mbaya. Hata waungwana unawapa mtihani, mizimu ya mababu zetu wa Sadani unawapa wakati mgumu kukupokea wakiwa wametulia, wanatetemeka kwa uovu ulioshuhudia na uovu wa watu uliojihusisha nao”, aliongea mganga huyo, na Johari alijikuta akiangausha chozi alielewa kuwa mganga kashafahamu maovu yote yanayomletea mkosi uliomfanya afike hapo mizimuni.

    “Wewe mama unaitwa Johari Chande na mumeo anaitwa Malcom”, aliongea mganga na Johari kwa uchungu akaitikia, “tawile ‘baba’ angu ndio mimi, Johari”, na mganga akaendelea, “shida yako ni kupata mtoto, ila hupati kutokana na mkosi na nuksi ulizopata baada ya kuwa moja ya wafuasi wa kundi la kijambazi waliowahi kuua familia nzima na wewe ulikuwako siku ya tukio ukishuhudia”, aliendelea mganga huyo nguli, na Johari akaitikia, “tawile mganga”.

    “Wezio woote, waliohusika wamepatwa na vifo vya kutisha na wengine kupotea, ila wewe walau umepewa utasa tu. Ila bado hujakubali unahaha kupata mtoto kama hivi kwa kututafuta waganga”, aliongea mganga huyo na kuangalia juu mawinguni, huku Johari akimtazama pia kwa hofu, kwa muda mganga huyo alibaki akiangalia mawinguni na ghafla akamgeukia Johari na kumkazia macho na kuendelea kuongea kuwa, waungwana wake, yani akimaanisha mizimu ya mababu zake wanampa hizo nguvu za kimiujiza wanayo dawa ya kutibu utasa wa Johari na kumsaidia kupata watoto, ila tatizo ni ugumu wa masharti, na mganga akamuuliza Johari kama yu tayari kufuata masharti magumu ya mganga. Na mganga akamsisitizia kuwa si jambo la kirahisi tu kukubali masharti hayo, na kwamba hatomtajia hayo masharti mpaka Johari ayakubali kwa moyo wote kabisakabisa kuwa vyovyote yatakavyokuwa hayo masharti kwa ugumu wake, yawe mepesi ama magumu kwelikweli shurti lazima ayatimize. Kuwa Johari ilimbidi akubali kutenda masharti kabla hajatajiwa na kuwa akishatajiwa basi hakuwa na jinsi ingine zaidi ya kuyatimiza. Johari alijikuta katika wakati mgumu sana, akawa kabaki kamtolea macho mganga. Hivi kweli akubali tu masharti kabla hajatajiwa, aliwaza, yakiwa magumu je itakuwa vipi ilihali ndio mganganga keshasema akimtajia sharti ayafanye hayo masharti.



    Basi mganga akamuamuru Johari aondoke akatafakari ili kuamua kama yu radhi kutimiza masharti yeyote atakayopewa na mganga ama la. Na mganga akamwambia Johari kuwa akirejea tena aende na mbuzi wa kafara wa rangi yeyote ili walau kufidia vile vifo vya familia ile iliyouwawa na kundi la Mapanya, na pia aende na fedha zisizopungua milioni tano. Na akamsisitizia Johari kuwa iwe ni siri yake kati yake na mganga kuwa anatafutia hapo dawa ya kupata ujauzito. Na mganga akamsisitizia Johari tena kuwa akiwa anaondoka akumbuke kuwa, atakapoamua kurejea kwa mganga huyo, awe tayari kaamua kufuata masharti ya kiganga, na kumkumbusha kuwa siku akishamtajia masharti hayo basi Johari atakuwa kama aliyevulia nguo maji hivyo sharti lake ayaoge.



    Baada ya kuondoka kwa mganga Johari alitafakari sana, kwanza alionywa asimwambie mtu hivyo hakuwa na mwengine wa kushiriki nae hayo mawazo yake, pili sasa alitafakari kuwa hadi wakati huo, hakuwa akiyajua hayo masharti ya mganga, ila mganga alimuambia kuwa siku akienda tena na akatajiwa hayo masharti ni lazima ayakubali bila ya kuyakataa, hivyo Johari aliwaza kuwa lazima afikie mkataa na kuamua hasaa kufuata masharti ya mganga.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Johari aliwaza sana itakuwa vipi kama masharti ni magumu mno, ila kichwani mwake zikamjia picha akicheza na watoto wake ambao pengine mganga angemsaidia kuwapata, pia aliona jinsi Malcom angefurahia uzao huo na mkewe, hivyo Johari akaamua kuwa ataenda tena kwa mganga na kukubali masharti atakayopewa yawe magumu kwa vyovyote vile, yeye atakuwa yu radhi na tayari kuyafanya.



    Basi siku ikawadia na Johari akaelekea tena huko kijiji cha Sadani kwa mganga. Na siku hiyo alienda na mbuzi mweusi na pesa taslim ambazo mganga alimwambia aende nazo.

    Mganga alimtakia Johari kuwa ni mwanmke jasiri sana kwa kurejea tena kukabiliana na masharti magumu ambayo angemtajia. Basi mganga akamchinja yule mbuzi na kutoa kama kafara kwa mizimu ya mababu zake.

    Kisha akaanza kumpa masharti Johari na kumuambia kuwa, namna pekee ya Johari kupata watoto ni kuzaa na kichaa, yani mwehu, mwendawazimu wa akili, mwanamume aliyechizi kabisa muokota makopo.

    Johari alishtuka sana. Alishtuka kwa maana hakutarajia sharti hilo hata kidogo. Ila mganga akamsisitizia kuwa hiyo ndio njia pekee ya kwake Johari kuweza kupata watoto vyenginevyo, asahau uzao. Na mganga kwa hasira alimkumbusha Johari kuwa masharti hayo ni lazima ayafuate, kwamba sasa ilikuwa ni lazima kwa Johari kumtafuta chizi muokota makopo na kulala nae ili azae na huyo chizi na kwamba Johari hakuwa na chaguzi tafauti na kulitekeleza sharti hilo ‘la aina yake’ alilompa.



    Huo ulikuwa ni mtrihani mkubwa kwa Johari. Hakufikiria kabisa kuwa mganga angeweza kumpa sharti kama hilo. Njia nzima akiwa anarejea Dar machozi yalimtirirka akiwaza wapi atapata mtu chizi, na ‘atamkovisi’ vipi chizi hadi alale nae na aliwaza sana kuwa ikigundulika ‘mishe’ yake hiyo ya kutembea na wehu wa akili waokota makopo, ili apate watoto kama masharti ya mganga yatakavyo, uso wake ataufichia wapi, na alifikiria sana kwanini yeye Johari mfanyakazi wa benki kubwa kama NIB na mke wa Malcom Munyisi, mtu tajiri na alojaa uzungu uzungu, mfanyakazi wizarani, kwanini yeye ilimlazimu kulala na machizi ili kuzaa. Ila alikumbuka kuwa ni maovu yake yanyomtafuta na kumkimbiza, yakimfuatilia kama kivuli kila aendako.

    ........................



    Malcom aliporejea toka nje ya nchi na kutembelea kijijini kwa mama yake, ndugu zake walimjia juu zaidi na safari hiyo wakamwambia kuwa wamemtafutia mchumba hivyo kazi yake ilikuwa kumuacha tu Johari na kumuoa huyo mwari mpya wa uhakika wa kuleta mtoto katika familia yao ya akina Munyisi.



    Na Malcom hakuficha kitu kwa mkewe akamwambia alichoambiwa na ndugu zake, mama zake wadogo, mashangazi na wajomba, kuwa katafutiwa mchumba. Mbaya zaidi sasa kwa Johari huyo mchumba aliyetafutwa akaanza kumpigia simu Malcom. Hivi kwamba wakati mmoja Johari alipokea moja ya simu hizo na kumtukana sana huyo mwanamke.



    Basi, siku moja Johari alikuwa kampitia mfanyakazi mwezie aliyeishi maeneo ya huko Mbezi Beach, ili waende mahala. Johari akiwa kakaa kwenye gari lake akimsubiri huyo mwezie atoke, mara akamuona mwanamume mmoja aliyevalia rafu sana, nywele zimetimka, yuko peku, akikatiza mbele ya gari lake akielekea mbele ya duka la rejareja lililokuwa mtaa huo. Moja kwa moja Johari alielewa huyo mtu alikuwa ni chizi mwendawazimu muokota makopo. Na akabaki akimtazama jinsi yule chizi alivyokuwa akifanya uchizi wake na mambo ya hovyo akielekea kwenye duka la mtaa.



    Johari aliona jinsi, watu waliokuwa wamekaa wakianza kumcheka yule chizi. Na mara muziki ukasikika toka ndani ya duka. Na yule chizi akaanza kucheza huo mziki kwa furaha kabisa na wale wa dukani wakaendelea kumshangilia na kumcheka sana, walimgeuza kituko chao. Johari mwenyewe alijikuta akicheka vituko ambavyo yule chizi alikuwa akifanya kwa ‘kusakata’ muziki.



    Mara rafiki yake aliyekuwa akimsubiri aliingia kwenye gari na kukaa kwenye kiti cha pembeni ya Johari huku akiomba radhi kwa kumchelewesha.

    Na Johari aliondoa gari eneo hilo kuelekea kwenye safari yao waliyokuwa wakielekea. Walipokuwa njiani Johari alimuuliza rafiki yake juu ya yule chizi aliyekuwa akicheza mziki, na rafiki yake akamwambia kuwa yule mtu ni kichaa kabisa muokota makopo ambaye huzururazurura mitaani kwao na kuwa aliishi kwenye boma la nyumba ambayo haijakamilika jirani kabisa na pale palipokuwa na duka. Na kwamba hakuna mtu aliyefahamu yule chizi anaitwa nani, ama ndugu zake ni akina nani na wapi ama kwa namna gani aliupata uchizi, ila watu walipenda tu kumuona akicheza muziki na kumgeuza kituko chao na kumcheka.

    Johari alisisimka mwili wake kusikia habari za yule chizi. Alianza kufikiria sana kichwani mwake kuwa huenda kapata aina ya chizi sahihi ambaye angefaa katika kutimiza masharti aliyopewa na mganga ili alale nae na kupata ujauzito. Aliwaza sana Johari na kujiapia kuwa lazima amchunguze yule chizi vizuri ili amjue tabia zake na kuelewa namna gani atamuingia na kumshawishi hadi afanye nae tendo la ndoa.



    Na kweli, Johari alifanya uchunguzi wake na akapajua yule chizi alipokuwa akilala, aina ya taka alizokuwa akila na zuri zaidi alilofurahia ni kuwa chizi yule hakuwa na tabia ya kupiga watu. Johari alidhamiria kabisa kuwa lazima alale na chizi yule.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Usiku mmoja baada ya chunguzi zake kwisha, Johari alimfungia safari yule chizi. Ilikuwa ni usiku wa manane, Johari alifika kwenye boma la nyumba ambayo haikukamilika ambako yule chizi alilala. Kwa hofu Johari aliingia hadi ndani ya boma hilo na kumkukuta yule chizi kalala. Kwa muda kidogo Johari alimmulika kwa tochi na kumtazama na Kuona jinsi alivyokuwa mchafu na kulala kwenye udongo na nyasi za boma hilo tena harufu ya uchafu wa mwili wa chizi huyo ilitapakaa boma zima, hakika Johari alihisi kinyaa.



    Mara yule chizi akaamka kutokana na mwanga wa tochi ambao Johari alimmulika nao. Na chizi yule alishtuka sana kwa maana hakuzoea ugeni bomani humo, hasa usiku manane. Johari mwenyewe alipoona yule chizi anaamka alishtuka hakujua yule chizi angewaruka kwa mtindo gani baada ya kumuona humo bomani.



    Basi Johari ambaye mkononi alikuwa kabeba mfuko wenye machungwa, aliingiza mkono mmoja mfukoni na kutoa chungwa na kuanza kula kwa kumringishia chizi yule. Mara yule chizi akamvamia Johari na kumpokonya mfuko wa machungwa aliobeba na lile chungwa alilokuwa akimlingishia kisha, yule chizi akaenda kujikunyata na kula yale machungwa haraka haraka. Wakati huo Johari alikuwa kamtolea macho yule chizi. Kwanza hadi wakati huo Johari alijiona jasiri sana kufika katika boma hilo na kendelea kuwamo humo usiku huo wa manane pamoja na huyo chizi. Ila sasa Johari alifikia ukomo wake wa kufikiri hakuelewa ataanzaanza vipi kuhamsha hisia za chizi, hivi kwamba wafanye tendo la ndoa humo bomani na yeye mwenyewe alijiwazia sana ‘msambwanda’ na mtu chizi hufanania vipi, kichwani mwake, Johari alikuwa na mawazo kama alfu hivi, aliwaza kama akifumwa bomani humo na chizi usiku huo watu wangemchukiliaje.

    Basi yule chizi baada ya kumaliza kula yale machungwa, ghafla akatulia na kumtizama Johari. Alimtazama kwa kutulia kabisa kama mtu mzima na timamu awezavyo kumuangalia mtu mwezie akiwa katulia, hadi Johari akastaajabu sana. Alistaajabu kwa jinsi ile yule chizi alivyotulia. Yule chizi alimungalia Johari machoni moja kwa moja na kutulia kabisa kama vile hakuwa na kawehuka kichwani.



    Kumbe yule chizi alitulia vile kutokana na uzuri aliokuwa nao Johari. Alimuona Johari kuwa ni mrembo sana. Pamoja na uchizi wake alitambua kuwa hakuwahi kuona mwanamke mzuri kama Johari. Yule chizi alimuangalia Johari hadi machozi yakaanza kumlenga na kuona haya akageukia pembeni.



    Johari hakutarajia kuwa mtu chizi anaweza kutulia namna hiyo, akabaki kaduwaa. Ila sasa aligundua kuwa, kama yule chizi aliweza kutulia namna ile basi kazi yake ilompeleka bomani mule ilikuwa nyepesi sana.



    Mara moja Johari akavua na kuangusha nguo zake alizovalia mwilini na kumfuata yule chizi, ambaye nae alipomuona Johari yuko utupu alishtuka sana. Pamoja na uchizi wake alitambua kuwa si kawaida kwa mwanamke kuwa utupu. Johari akamsogelea.

    Nia ajabu ilioje hadi wakati huo kile kinyaa alichokuwa akiona Johari kilimtoka kabisa na hakukisikia, hadi wakati huo alilenga tu kulala nae tu yule mwendawazimu.

    Katika hali ngeni kabisa kwa yule chizi, alijikuta kasisimka sana na mara Johari alikuwa juu yake. Naam!, kilichotendeka hapo ilikuwa ni starehe ambayo chizi yule hakuwahi kuipata. Ilikuwa ndio mara ya kwanza kwa yule chizi kufanya tendo lile la aina yake na kwa Johari ilikuwa ndio mara yake ya kwanza kufanya vile na mataahira, yani ni kama walijiondoa ubikira kila mmoja wa aina yake, khatari!.



    Johari akawa kafanikiwa lengo lake la kulala na chizi. Na usiku huo aliporejea kwake alikesha bafuni akioga akiwa haamini namna alivyofanikisha lile tendo na yule chizi. Hakuamini kama kweli msomi kama yeye alifanya alichokifanya, hakuamini kuwa yeye alikuwa ni jasiri wa kufanya kitu kama kile wakati aliona kuwa ni sharti zito sana pale alipotajiwa na mganga kuwa afanye vile, na ajabu aliona kuwa mbona ilikuwa na kauwepesi kidogo katika kutekeleza kuliko alivyokuwa akifikiria ugumu wake. Na alijishangaa na kujiuliza kinyaa chake cha kulala na chizi mchafu, anukae asieoga kilienda wapi muda wa tendo. Ni maswali mengi aliyojiuliza na akakosa majibu kichwani mwake.



    Basi, maisha yaliendelea na wiki chache tu mbele Johari alianza kupata dalili ambazo hakika yeye aliamini ni ujauzito. Na hata alipokwenda kumuona daktari majibu yalionesha hivyo kuwa alikuwa ni mjamzito. Ilikuwa ni furaha sana kwa Malcom, kwa maana alishamkatia tamaa mkewe, Malcom hakuwa akitarajia kama mkewe angeweza kuleta kiumbe duniani, ilikuwa ni miujiza kwenye ndoa yao.



    Ndugu zake Malcom walistaajabishwa sana na taarifa hizo, hawakuamini hata kidogo. Walijiuliza sana iwaje mgumba kapata ujauzito. Miezi tisa baadae, Johari alijifungua mtoto wa kiume, na kwa furaha Malcom akamuita mtoto huyo, Miujiza, kwa maana alikuwa ni muujiza kwa familia yake. Sasa mama yake Malcom, mdogo wake Malcom na ndugu wengine wakajikuta wana mapenzi ya dhati na Johari na kusahau viroja walivyokuwa wakimtendea. Sasa safari hiyo, Johari nae akawa anawaletea nyodo za ‘kimtindo’ za waziwazi katika kile kiitwacho kutesa kwa zamu, sasa Johari alionesha dhahiri kutopenda mtoto wake ashikweshikwe na ndugu wa mumewe na kujifanya mtoto wake anamlea kizungu sana na si kiswahiliswahili kama ndugu wa Malcom aliowachukulia kuwa hawana elimu walivyotaka kujishirikisha kwenye malezi ya mtoto.

    Johari alikuwa ndiye mwenye furaha zaidi baina ya wote waliofurahia kuzaliwa kwa Miujiza. Yeye kama mama alifahamu shuruba na masharti aliyopitia na kutimiza ili kumpata mtoto wake. N akichwani mwake Johari akawa kafikia mkataa mwengine kuwa lazima atembee tena na yule mwanamume chizi ili apate mtoto mwengine wa pili.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Kwake yeye Johari kutembea na yule chizi ilikuwa ni jambo rahisi sana, kwa maana Malcom alikuwa ni mtu mwenye kusafiri safiri sana kwenda nje ya nchi, hivyo Johari aliweza kuwa na uhuru wa kuamua kuchelewa kurudi nyumbani na kufanya lolote huko mitaani, ikiwemo kulala na machizi, bila ya kuhofia kujulikana na mtu yeyote wala kumtia wasi Malcom.

    Baada ya mwaka mmoja kupita, Johari, kwa awamu ya pili alirejea bomani kwa yule chizi. Na safari hiyo Johari alishangazwa kugundua kuwa yule chizi alimkumbuka vyema. Kwa maana safari hiyo ya pili, yule chizi alipomuona tu Johari machozi yalimdondoka toka kwenye macho yake hadi Johari mwenyewe akajikuta machozi yakimdondoka, hata bila ya kuelewa yule kichaa alilia nini kwa kumuona yeye Johari. Kumbe yule chizi alilia kwa mapenzi. Alimkumbuka vizuri Johari na urembo wake, na toka usiku ule wa mara ya kwanza wafanye tendo bomani yule chizi alimkumbuka na kumuwazia.



    Kwa namna hiyo, hiyo safari hiyo ya mara ya pili ilikuwa rahisi zaidi kwa Johari kumuingia chizi huyo na kulala nae , kwasababu chizi mwenyewe alikuwa kaingia ‘laini’, yani haleti papara, ‘mzigo’ kauelewa na picha alijua kulicheza, na chizi yule alikuwa na hamu kweli ya kulala na Johari.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog