Search This Blog

Tuesday 1 November 2022

NIKUITE NANI? - 1

 








IMEANDIKWA NA : HASSAN MBONECHE



*********************************************************************************



Simulizi : Nikuite Nani? 
Sehemu Ya Kwanza (1)


 Shamra shamra zilikithiri maeneo yote yazungukayo ukumbi mkubwa na mashuhuri mjini Moshi. Ufahamikao Kili home reaction, upatikanao jirani na kambi ya polisi, mkabala na jengo litambulikalo Big brother. Nje ya kumbi kulitawaliwa na biashara ndogo ndogo, hasa za matunda matunda, sharabu na vinywaji. Gari dogo, nazo zilitapakaa vya kutosha. Zilizowasukuma walinzi toka kampuni mbalimbali za ulinzi, KK, SGA na wale wa SUMA JKT GUARD kuwa makini nazo. Pasi na sahau wengine wadumishao ulinzi langoni. Lango la kuingilia. Ambako waliambatana na mabaunsa kadhaa.



Ingia ya watu ndani ya kumbi hiyo ilikuwa isiyohesabika. Watu wengi walishonana langoni, kugombania kuingia, ili wawahi kupata nafasi za kuketi. Hali iliyowapa wakati mgumu walinzi wa kukagua tiketi. Nyomi iliyopo ndani, haikutofautiana sana na ile ya nje. Hakika! Walikuwa watu wengi mno.



Ni usiku. Wa saa tatu. Pindi hayo yanaendelea, katika kuazimisha siku pendwa ya utoaji wa tuzo za UBUNIFU (Ubunifu Award). Ambazo huazimishwa kila mwaka, oktoba 22. Kwa kutoa tunuku kwa vijana wenye umri kati ya miaka kumi na nane hadi ishirini na tano, waliofanya vizuri katika uandishi wa risala zihusuzo maisha yao. Siku hiyo hutoa wasaa, kwa vijana waliowania tuzo hiyo, kusoma sehemu ndogo ya kazi zao kisha majaji huamua mshindi ni nani, baada ya kupima mtiririko wa uandishi. Kama kufuata kanuni na lugha fasaha itakiwayo ndani ya jamii.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Tukio lilianza rasmi saa 22:30 usiku, punde mgeni rasmi, Waziri wa habari sanaa, utamaduni na michezo, Bi. Anna Mwenda alivyowasili ukumbini. Uliopambwa kwa samani mbalimbali, zilizonakishiwa maridhawa kabisa na kupeperusha vyema bendera ya taifa, na bendera ya kampuni ya Ubunifu itoayo tuzo hizo, chini ya kampuni ndogo, iitwayo Tanuru la simulizi ihusikayo na uchapaji na usambazaji wa kazi mbalimbali za kisanaa. Hasa za uandishi wa vitabu aina zote na utengenezaji wa filamu.



Tamasha lilianza kwa hotuba, toka kwa watu mbalimbali, wahusikao na sanaa mkoa wa Kilimanjaro na kanda ya kaskazini kwa ujumla. Baadaye akafuatia Bi. Anna Mwenda, kutoa hotuba ndogo iliyowapa nafasi wanguzumzaji waanze kusoma risala zao. Wazungumzaji walikuwa watatu, wa kwanza; Nyoni Simba, wa pili; Zamoyoni Ndumba, ambaye ni msichana na wa mwisho; ni Abdul Vumilia. Zoezi hilo lilifunguliwa na Nyoni, akafuatia Zamoyoni, akamalizia Abdul. Ambaye alikuwa mshindi wa tuzo hiyo mwaka uliopita. Alichukua tuzo kupitia risala aliyoipa jina la FUNDO LA UMIVU, mkasa uliompata baba na mama yake miaka ya nyuma.



Aliposimama nyuma ya mimbari, watu wote wakawa kimya. Hakuna nong’ono lolote lililosikika, tofauti na watangulizi wake waliotumia takribani muda wa saa moja kuwasilisha kisomo chao. Sauti pekee zilizosikika, ni zile za kujikohoza, na kufanya majaribio ya vipaza sauti kutafuta kitoacho sauti vizuri.

“Asalam alaykhum!” alisema Abdul. Pindi akiikita vyema miwani yake ya macho imwezeshayo kumkuzia herufi. Ana matatizo ya macho, ya kutoona vizuri herufi ndogo.

“Waleykhum salam,” hadhira iliitikia.

“Tumsifu Yesu kristo.”

“Milele amina.”

“Baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu, naomba mniwie radhi, kwa kuleta ombi hili kwenu. Naomba tusimame, kwa dakika moja kumkumbuka marehemu mama yangu kipenzi, kabla sijaendelea,” alisema Abdul, akiivua ile miwani na kuiweka juu ya mimbari.



Hadhira ikatii. Walisimama kwa muda tajwa, ulivyomalizika waliketi vitini, kisha Abdul akaanza, baada ya kufuta chozi jembamba lililomtiririka.

“Ndugu zanguni, risala niisomayo, inaitwa NIKUITE NANI? Ni mkasa wa kweli, ulionipata. Nawaomba tuwe watulivu, ili tuweze kujuzana.”

“Kaka endelea…huwaga hukosei,” ilisikika hadhira, kwa sauti ya nguvu, iliyozalisha keneo la midomo yao lililoonyesha meno ya mbele yaliyo na mng’aro mweupe na mng’aro wa shaba kwa baadhi ya watu.

“Okay! Tulieni, mupate kunielewa. Utulivu huo usio kwenu tu, pia umfikie msichana mmoja aitwaye Jamila Namahala popote alipo. Ambaye ndiye anapaswa afikiwe na ujumbe uliomo ndani ya risala hii na wengine wengi kama yeye.”

__________



Maisha yangu yaligubikwa adha kubwa. Punde nilivyompoteza mama yangu mzazi, ama dada yangu pia. Kwani mama aliyenizaa, alikuwa mtoto wa baba yangu mzazi, ila waliingia kwenye mahusiano wakiwa hawafahamiani kama ni baba na mwana. Hadi walivyofikia hatua ya mimi kuzaliwa. Ufahamu ulijitokeza mara baada ya rafiki wa marehemu bibi yangu, Mwanjaa, kuwaandikia barua kuwataarifu, ukweli kuhusu mahusiano waliyonayo. Taarifa hiyo, ikapelekea kifo cha mama yangu na kuniondoa nyumbani nikiwa na umri mdogo tu. Wa miaka mitatu. Nilitoroka, nikiwa na lengo la kumtafuta mama yangu, kwenye makaburi aliyozikwa. Nilienda huko kwa sababu nami nilikuwa mmoja miongoni mwa watu waliohudhuria mazishi yake japo sikuwa na utambuzi wowote. Mwendo wa kutoka nyumbani tulikokuwa tunaishi mjini Tunduru, hadi makaburini, ulikuwa mrefu kidogo. Ukizingatia nilikuwa mdogo, basi nilitumia muda mwingi hasa, tofauti na watu wazima.



Nilipiga hatua taratibu, huku nikidondosha kilio na kulitamka neno mama, kitendo nilichowaachia mshangao, watu niliopishana nao, na wale niliowakuta wameketi sehemu. Lakini kati yao, hakuna aliyeingiwa na huruma ya kuniita, ama kunifuata anidodose kilichonisibu. Wote waliniacha, hadi nilivyowasili makaburini, na kufikia kukaa pembezoni mwa kaburi moja, ambalo sikuwa na uhakika kama ndiyo lile alilozikwa mama yangu. Tukio hilo, nililifanya saa 11 jioni, jua lishapoa, watu mbalimbali wakirejea makwao toka mihangaikoni. Nadhani na baba yangu pia, alikuwa mmoja miongoni mwao. Ila sina hakika kuhusu hilo, kwani baada ya kuondoka habari ziendeleazo nyumbani nika—achana nazo. Nilikaa pale makaburini hadi kiza kilivyoingia, huku nikiendelea kulia, na kujaribu kufukua udongo lengo niufikie mwili ulioko ndani.



Tofauti nami, sauti nyingine iliyosikika mahali pale ni sauti za ndege. Na majani yaliyopo ardhini, pale yaguswapo na mdudu. Ama yadondokewapo na kitu. Kiza kilivyozidi kutanda, nami nikazidi ongeza kilio, kilichoashiria kuogopa mazingira hayo hadi sauti ikaanza katika. Sikumbuki, ni muda gani, nikajikuta nimepitiwa na usingizi, nilivyokuja zinduka, nikaanza upya kulia, huku nikizunguka zunguka jambo lililonifanya nikanyage kanyage makazi ya watu walio na pumziko la milele.



Kilio changu kikasikika na wamama watatu, ambao sina hakika kama walikuwa wezi, au wanga, ambao sifahamu walitokea wapi nikakutwa nimezungukwa nao. Baadaye walionekana kujadiliana, majadiliano mafupi sana, kisha mmoja wao akanibeba tukatokomea pale makaburini. Kulivyopambazuka, nikajikuta niko safari, ndani ya gari, hiace ikichanja mbuga kuelekea sehemu ambayo hata sikuifahamu. Jirani, aliketi mmoja miongoni mwa wale wa—mama, aliyenibeba jana kule makaburini. Alikuwa katulia tuli, huku akipepesa pepesa macho yake kunielekezea. Tulivyofika eneo fulani la mji, gari ikasimama, akaninunulia maji madogo na vitu vichache vya kutafuna tafuna, naye pia alifanya hivyo baada ya muda safari ikaendelea, wangu fuadi ukitawaliwa na furaha sababu nasafiri, kilichonifurahisha zaidi, kule tuelekeako kulionekana mjini zaidi.



Kweli!



Tulivyowasili sehemu fulani, ambayo sikufahamu inaitwaje tuliteremka garini, tukaongoza kwenye gari nyingine, ambayo ilikuwa kubwa zaidi ya ile gari ya mwanzo. Tulipanda basi! Tukaendelea na safari, tena huku ilikuwa tamu haswa, kutokana na vitu fulani ambavyo vililiwaza abiria. Kama vile skrini, iliyotufanya tushuhudie burudani mbalimbali, pamoja na ugawaji wa vitu fulani vya kula. Vilevile huku abiria waliketi sitini pekee, hakukuwa na waliosimama simama kama ilivyokuwa kwenye hiace. Hakika safari ilikuwa tamu kwa upande wangu, sijajua wenzangu, kwao ilikuwaje, kwani muda mwingi sikuacha kutoa keneo nifurahishwapo na kile nikionacho runingani.

“Umependa eeh!” aliuliza yule mama aliyenichukua, ambaye ndiye aligeuka mzazi wangu kuanzia wakati ule alionichukua kule makaburini.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Ndiyo,” niliitikia, nikiwa nimetoa macho pima kuielekezea runinga iliyokuwa inaonyesha picha ya video ihusuyo mambo ya watoto.



Mwisho wa safari ulikuwa jijini Mbeya. Nilifahamu jina la mji huo baada ya kumuuliza yule mama. Niliyemtabua kwa jina la Shangazi Janeth. Tulivyoondoka kituo cha mabasi tukaenda nyumbani kwake, mtaa wa Isengo. Ambao uko jirani kabisa na uwanja wa ndege wa zamani uliokuwa unatumika jijini Mbeya. Makazi ya Shangazi Janeth hayakuwa ya kifahari, yalikuwa makazi duni, yaliyonipa mshangao namna alivyokuwa anaishi. Hayakuendana na yale ya nyumbani. Ila halikuwa jukumu langu kuchunguza mambo ya makazi, kilichonihusu ni namna ya kuishi na mama huyo.

__________



Maisha yangu rasmi yakahamia jijini Mbeya. Nikiwa mtoto wa mtaani, hasa wale wavaao nguo zilizochanika chanika, na kuenea uchafu karibia nguo zima. Suala la shule kwangu lilipita pembeni, ndiyo maana nikawa mtoto wa aina hiyo, si kwa matakwa yangu, bali ilichangiwa na hali ya uchumi wa yule niliyekuwa naishi naye. Lakini kutokwenda shule, sikuruhusu kuwa kigezo cha kunifanya nishindwe kujua kusoma. Nilifanya kila jitihada, ila sikutambua kama jitihada kwa kipindi hicho, nikafanikisha kujua kusoma na kuandika. Nilifahamu hayo, kupitia kwa mtoto aishiye jirani na pale tulipokuwa tunaishi. Pale nilipotembelea kwao, nikakuta anafundishwa, sikuacha kutega sikio na macho kwa makini nami nipate ufahamu. Kwani kuna kipindi ilifikia kujaa mori ya kufanikisha hilo kutokana na ugomvi niliowahi ushuhudia kipindi fulani, baba mmoja alivyokuwa anazodolewa kisa tu hajui kusoma halafu anajifanya sharobaro.



Naam! Namshukuru Mungu, urafiki na mtoto wa jirani, afahamikaye kwa jina la Siku ulinisaidia kuondoa ujinga. Nami nikajiona miongoni mwa werevu, katika werevu, japo si werevu wa majivuno. Vilevile namshukuru Mwenyezi Mungu, juu ya malezi aliyonipatia Shangazi Janeth. Yalikuwa malezi mema, ambayo katu siwezi yasahau. Kuanzia alivyonichukua kule makaburini, hadi nilivyopevuka na kujitambua. Yeye ndiye aliyechangia kuwa hivi nilivyo. Kanijenga kuwa mtu wa hekima, mwenye busara na kila lililo jema maishani mwetu. Jitihada zake, zilikuwa kubwa, sio kubwa tu, ni zaidi ya kubwa kuhakikisha nakuwa sehemu nzuri. Alinifanya kuwa mwanaye. Tamanio lake, siku moja anione nikiishi maisha yenye furaha na amani. Nakumbuka, kuna siku nikamsisitizia kuhusu ukamilishaji wa kile anachohitaji kwangu.

“Shangazi, nitaishi kwenye kauli zako. Kamwe sitokuangusha,” nilisema. Jioni moja alivyoniketisha mara baada ya kutoka mihangaikoni.



Shangazi Janeth, aligeuka kuwa mama yangu. Kuhusu baba akili ilikaa kando, ijapokuwa kuna siku nilikesha kumuuliza, naye kunihadithia mazingira tuliyokutana. Hadithi, iliyonifanya nijae utambuzi wa kutokuwa na wazazi wangu wote wawili, vilevile kutokuwa na jamaa mwingine zaidi ya Shangazi Janeth. Vipi naye akiondoka? Nilishawahi kujiuliza hivyo. Kwa mafikirio nitaishi maisha ya namna gani, ilhali sina ujanja wa kutafuta pesa.



Nilivyofikisha umri wa miaka kumi na tisa, ndipo nikaanza kuwa janja mtaani. Kama wadaivyo waswahili, kijana wa mjini. Hakuna mtaa wowote, ulionipiga chenga jijini Mbeya. Nilifahamu karibu mitaa yote, na baadhi ya miji ya pembezoni, katu haikunipiga chenga. Nilikuwa mjuvi, miongoni mwa wajuvi, huku kilichochangia niwe hivyo, ni shughuli ya uuzaji wa vyombo mbalimbali vya ndani mtaani. Katika pita pita hizo, nikabahatika, kuifahamu familia moja iliyojitanabaisha familia ya Mzee Namahala, mzee tajiri anayemiliki kampuni ya usafirishaji wa malori na semi—trailer zifanyazo safari toka Mbeya mjini kuelekea nchini Zambia na nyingine nchini Malawi.



Shughuli ya uuzaji wa vyombo mtaani, iliyonifanya niwe mbuka vumbi, mwoga jasho na kipigo cha miale yote ya jua kuifahamu familia hii vilivyo. Familia ya watu watatu, baba, mama na mtoto wa kike afahamikaye kwa jina la Jamila. Kwa sababu walikuwa wateja wangu wakubwa nijivuniao. Waliweka oda kwangu, kila nipatapo mzigo mpya, nisiache kuwapitishia, hasa yatokapo matoleo mapya ya vyombo. Nami kufanya hivyo. Ufahamu ukajenga mazoea. Kwa wote, hasahasa, mama mwenye nyumba, Mama Jamila, kutokana na wingi wa matani aliyonayo. Yaliyochangia tukutanapo, kuumiza mbavu za wengi kwa kicheko. Naam! Familia hii iligeuka kuwa sehemu namba mbili ya malezi yangu. Kwani ilifikia kipindi, sikuacha kuwatembelea hata kama sina biashara yoyote. Siku niendavyo hivyo, huwa na maongezi mengi sana, yahusuyo maisha, yote yakinihusu, namna navyotakiwa niwe ili niweze kutoboa kimaisha. Kufanikiwa!



Mara nyingi wosia wao ulikuwa wa mkazo sana, hasa walivyokuja tambua sina elimu yoyote ya darasani, zaidi ya ile ya mtaani. Kutokana na imani zilizowajaa kichwani mwao, kwamba sitoweza kupata ajira yenye uhitaji wa uthibitisho wa makaratasi yaonyeshayo uwezo wa elimu ya darasani. Sikuishia hapo, ufahamu ulienda mbali zaidi. Kutambua maisha wanayoishi, na malengo kemkem waliyonayo, yote yahusuyo mtoto wao Jamila. Hata nilivyowahi muuliza mwenyewe alinithibitishia kile nilichosikia.

“Sahihi! Nahitaji niwe mtu wa kumtii Mwenyezi Mungu, kupitia kwa mwana wake mpendwa Yesu kristo aliye hai,” nakumbuka, kauli hii alinitamkia Jamila, msichana mlokole, apataye umri wa miaka ishirini. Alinizidi mwaka mmoja.



Jambo lililonifanya nimwonee donge, na kumhusudu sana, kuwa ana malengo mema, ukilinganisha na yangu. Ambayo hata mwenyewe nilishindwa kufahamu yanaegemea wapi. Kwani, mambo kuhusu Mwenyezi Mungu yalinipita kushoto. Sikuwahi japo dakika moja kuhudhuria jengo takatifu liabudilo maneno yake.

“Nahitaji ipate tokea siku, dunia initambue juu ya huduma nitayoitoa,” alisema Jamila.

Kauli zake kwangu zilikuwa za maumivu. Alikuwa na maono, ambayo katu kwangu hayakuwepo. Alikuwa na maono makubwa mno, ilhali nikikumbuka langu, kwa mara ya mwisho, nilikuwa na ono la kununua suruali ya jeans niwaringishie wenzangu siku ya sikukuu. Nilijiona mjinga kwake.



Maono yale, yakanifanya niwe mfuatiliaji mzuri wa mambo yake, nikawa mwingi wa kuhitaji kumsikia aongeapo, ukizingatia maneno aongeayo yalikesha kujaza faraja na moyo wa matumaini kwa yeyote amsikiaye. Nikapanga ratiba, kila siku jioni, kuanzia saa kumi na mbili, kuhudhuria nyumbani kwao, lengo kusikiliza mahubiri yake, ifikapo saa moja usiku nijongee nyumbani, ila isivyo bahati, muda huo niliopanga haukuwa rafiki kwake. Kila niendapo kwao, sikubahatika kumkuta, niulizapo wazee wake wakanifahamisha, jambo lililonifanya niendelee kumhusudu Jamila, na kumuona mtu mkubwa mno, zaidi ya wazazi wake. Kwamba anahangaika kutafuta maarifa, yatayoigeuza dunia, ambayo watu wote watamuangalia na kumpatia heshima kutokana na maneno yenye hekima atayokesha kuwahubiria. Ule utajiri wa wazazi wake, wote nikauona upo kwake, na nikajawa na fikra, kwamba yeye ndiye aliyeifanya familia hiyo kuwa tajiri.

“Jamila muda kama huu huwa kanisani kwenye mafundisho. Hurudi saa nne usiku, hivyo ni mchana pekee ndiyo huwa ana muda wa kutosha,” walisema wazazi wake. Kauli iliyonifanya niamini moja kwa moja pasi na chembe ya shaka.



Ikanilazimu nibadili ratiba, badala ya jioni, nikapanga muda ambao mara nyingi Jamila hupatikana nyumbani. Mchana! Nikafanikiwa. Kila nilivyoenda kwao muda huo nikawa namkuta kisha kunitekelezea hitajio langu. Naam! Alikuwa mhubiri mzuri, maneno yake yalinijenga, na kunifanya niendelee kumtukuza kama watu wengine niwaonao wana thamani kwangu. Nikichanganya na ono langu kuhusu elimu aliyonayo, elimu ya chuo kikuu, nikazidisha. Kiasi kwamba nilishindwa kuchangia mada atoazo kwa kuamini kila aongeacho ni sahihi. Sababu tu, ana elimu ya juu, mimi hata elimu ya chekechea sijaipata. Hivyo oni langu, niliamini haliwezi kuwa na ushawishi wowote kwake.



Miezi mitatu baadaye, nikawa mmoja miongoni mwa waumini wazuri wa mahubiri yake. Japo sikufahamu, kama ana waumini wengine zaidi yangu. Niliiva maandiko takatifu toka kitabu cha biblia, huku nikikosa chembe ya maandiko toka kwenye kitabu cha imani yangu. Furkani. Niliiva, hadi ikafikia hatua, nami kuwahubiria wenzangu, watendao matendo yasiyoridhisha ndani ya jamii yetu. Nilikosa tu, utunuku, wa kuitwa mchungaji, kama wapendavyo kuita vijana wengi wamgunduapo mtu apendaye dini vilivyo.



Kwa namna nilivyoiva, nikajijengea tabia ya ufahari. Ufahari wa kufahamu mambo, na kuwa na kingi kiu, cha uhitaji wa kuwahubiria wenzangu kila siku na kila mahali nchini. Kila nipatapo, na kukuta zogo, kidume nilijipachika, kwa kununua zogo, kisha kuwahubiria kilichopo moyoni katika kuijenga jamii iliyo sawa kimaadili. Ila nilisahau kitu kimoja tu. Cha kuwafuatilia wale niwahubiriao namna watekelezavyo mahubiri yangu. Tabia hii, alikuwa nayo mhubiri wangu pia, jambo lililonifanya jioni moja nijulize, kulikoni? Mwalimu wangu hafuatilii yale akeshayo kunipatia kama nayatendea kazi. Nilimtilia shaka!

__________



“Aaah!...mhubiri, upo?” aliniuliza kijana mmoja. Alivyokutana nami barabarani, nikielekea nyumbani kwa kina Jamila, mchana wa saa saba.

“Nipo kiongozi. Mafundisho yamenichukulia muda wangu mwingi sana. Kiasi kwamba nashindwa kuzurura zurura,” nilimwambia. Macho yangu yakiwa pima usoni kwake. Kumsaili namna apokeavyo kauli yangu.

“Ni vizuri sana. Ila mafundisho yako vyema? Maana ulimwengu wa sasa, sina hakika, kama kahaba anaweza toa fundisho la ki—Mungu,” alisema, huku akinipiga moja ya bega langu pindi akijitahidi kunivuka aendelee na safari. Kauli hiyo ikanifanya nigwaye, fuadi ukapokea unyong’onyo na kukata morali ya kuendelea na safari.



Baadaye ikabidi nigeuze macho nimwangalie yule kijana. Kweli! Nilimuona, hakupotea kwenye mboni zangu. Nikaishia kutumbua macho kumwelekezea na kushuhudia namna adundavyo, hali iliyonipa utambuzi wa moja kwa moja, kwamba kamsahau muumba wake. Kwani achilia mbali, alivyokuwa anadunda, suruali yake aliivaa makalioni. Kitendo hicho kikanipa mshituko, na kunihimiza kuhamisha mboni zangu toka kwake, kisha kuyaelekezea kiunoni kwangu. Kuichunguza suruali niliyovaa. Ilikuwa sehemu sahihi. Kiunoni! Kutaka kujihakikishia, niliivuta tena kwa juu na kuyarejesha tena kwa yule kijana. Awamu hii sikumuona.

“Any way! Acha niendelee na mipango yangu,” nilijisemeza. Nikapiga hatua mbili nikasimama.



“Somo la leo nitalielewa kweli? Maana kaniharibia ari niliyonayo,” nilijisemeza kwa mara nyingine.

Nikajipa muda wa kuichangamsha akili yangu, kufikiria nichukue uamuzi gani. Takribani sekunde kumi, ndipo nikapata muafaka.

“Acha nirudi nyumbani.”



Nikarejea nyumbani. Nikitawaliwa na unyong’onyo wa kutosha. Hali iliyombainisha Shangazi Janeth. Niliyemkuta kaketi barazani akichambua mchele. Hakika! Sikuweza ificha hali niliyonayo, iliyochangia nianze kupatwa na maumivu ya kichwa pasi na kutarajia. Kwa sababu ya ufikiriaji.

“Dully!” Shangazi Janeth aliniita.



Nami nikapiga jicho kumsaili. Huku nikipunguza mwendo, kumwashiria aendelee kuzungumza namsikiliza.

“Kulikoni? Hauko kawaida mwanangu. Kipi kimekutatiza?” aliniuliza. Wakati huo akitua ungo wa mchele chini na kujiweka sawa, kwa ajili ya mapokeo ya majibu yangu.

“Shangazi, nipo kawaida. Hamna kinachonitatiza.”

“Hapana! Wajihi wako unaonyesha hali uliyonayo moyoni. Hauko sawa. Njoo niambie, niweze kukusaidia.”



Nikajifikiria kwa muda. Takribani sekunde nane, kisha nikapiga hatua hadi pale alipo. Nikajiunga kuketi mkekani, alipoketi, naye akajiweka sawa kwa mara nyingine, ili asiwe na wasiwasi wa kujihisi kaketi vibaya. Ama kuna kiungo cha mwili nakiona, ambacho hakipaswi kuonwa nami.



Kikapita kimya kifupi. Baadaye akaanzisha maongezi, baada ya kujikohoza kidogo, kulainisha koo.

“Acha kunificha mwanangu. Uliondoka hapa ukiwa na ari kubwa mno. Sasa imekuaje…,” alisema, ila hakumalizia kauli yake. Nilimkatisha.

“Kuna watu hawapendi kuwaona wenzao wakiwa na furaha.” Nilisema .

“Kivipi?”

“Kuna mtu nimekutana naye hapo juu kanikatisha mori ya kwenda kupata mahubiri, kwa sababu ya kumuita mhubiri wangu kahaba.”

“Haa! Sasa umeshindwa kuendelea na mambo yako kwa sababu ya hako ka—msemo? Mwanangu, acha kuwa muathirika wa dunia ya sasa.”

“Una maanisha nini?”

“Dunia ya sasa, ina vingi vioja kwetu binadamu. Wengi wetu, tumejawa na tabia, ya kuamini upande mmoja wa msemo, hata kama kile kizungumzwacho kina hitaji kuzungumziwa pande mbili. Wengi wetu tuna tabia, ya kurithishana matukio. Yaani, endapo nitakuwa na uhasama na jirani yangu, basi nawe, kwa sababu ni rafiki yangu, ama jamaa yangu, nitahitaji ujenge uhasama na huyo mtu hata kama hamjawahi kukosana. Uambiwayo unapaswa kuyapima, na si kuyatolea maamuzi punde tu ulivyosikia. Hakutakiwa kuyaamini maneno yake, na kuyaruhusu yakutawale akilini. Utajisikiaje, siku utayogundua kile ulichosikia hakina ukweli? Wakati huo ushatolea maamuzi.”

“Lakini, wahenga walishatupatia kauli. Ambazo daima hulandana na ukweli. Kama ule usemao…” nilisema, ila sikuhitimisha kauli yangu. Shangazi Janeth alidakia.

“Hiyo misemo hata nawe unaweza ibuni. Usiishi kwa misemo, utapotea.”

“Nimekuelewa shangazi.”



Tukahitimisha maongezi. Kisha nikaondoka kuelekea chumbani kwangu. Huko nikaanza upya kufikiri. Ila si kufikiria ile kauli imhusuyo Jamila, mhubiri wangu. Nilikuwa nafikiria kauli za shangazi Janeth. Moja baada ya nyingine, hadi nikapitiwa na usingizi. Nilivyozinduka, nilizinduka na taswira ya Jamila. Imejaa tele usoni. Nilijikuta naanza kumpambanua, namna alivyo, na mienendo yake ilivyo.

“Inawezekana vipi? Mtu mlokole, ana kila chembe ya utiifu na hofu ya Mwenyezi Mungu, awe kahaba?” nilijiuliza. Moyo ukisheheni mshawasha wa kuonana naye, nithibitishe nilichosikia. Kwani juu ya kuzielewa kauli nilizoambiwa na shangazi Janeth, nilisumbuliwa na imani ya misemo iliyobuniwa na watu waitwao wahenga. Hasa ule usemao lisemwalo lipo.

“Hapana. Lazima nithibitishe hili. Yamkini kweli ni kahaba. Ila, atawezaje kuwa na ndoto za kulitangaza neno la Mungu duniani? Kahaba, halafu atoe maandiko ya kidini, watu si watamdharau. Haiwezekani,…” nilijisemeza. Mithili ya mtu aliyerukwa wenda wazimu.

__________



Mchana! Kama ilivyo ada. Kiguu na njia. Jasho likinitiririka taratibu, karibu sehemu zote za maungo ya mwili wangu. Isipokuwa pale palipobeba jinsia. Kiasi kwamba, hata nguo nilizovaa zililowana. Hasahasa shati, chapachapa, mithili nimemwagiwa maji, nikisherehekea siku ya uzao wangu. Siku hii, sikuwa tofauti na watu wa shamba. Wale wachafukao, kutokana na utumiaji wa nguvu nyingi watembeapo. Halmashauri ya kichwa changu, ikikesha kumfikiria Jamila pekee. Alinipa msongo wa mawazo, kama mwanamke niliye na mahusiano naye ya kimapenzi, kanitenda. Hakubanduka, hadi nilipofika eneo nililohitaji. Nyumbani kwao!



Kabla sijabisha hodi niingie nikajipumzisha, kwa kuegemea ukuta, usawa wa karibu na mlango wa kuingilia ndani. Lengo, linikauke kidogo lile jasho ndipo niingie. Nilitumia takribani dakika mbili kukamilisha hilo tukio, baada ya hapo nikasimama kuuendea mlango. Nikajiweka vyema tayari kwa kubisha hodi, ila katikati ya matayarisho yangu, nilishtushwa na kauli toka ndani. Iliyoonekana kutamkwa na watu wengi.

“Aaaah!...shoga yangu mie, hivi utajisikiaje ukija kubainika kazi yako ni kuuza…” niliisikia sauti ya kike ikitamka hivyo. Sauti za ujana, zilizonibainishia kutambua waliopo ndani ni vijana. Ina maana Jamila na rafikize.

“Nakuambia acha. Nimepewa bure hivi, ya nini kuvibania? Mara kuwa na mmoja, mara eeh! Wanatoa msisitizo huo huku wakisahau ili uwe na kipato kingi lazima uwe na njia nyingi za kutumia uweze kuingiza kipato hicho,” alisema Jamila. Kauli iliyonipa utata wa kutambua maana.



Nikasita! Kwa muda mchache, kisha nikaendelea kuruhusu masikio yangu, kusikiliza kile kiongelewacho.

“Hivi, huyo unayemhubiria neno la Mungu hafahamu kazi yako ya pili kuwa ni mwana—danguro?”

“Mmmh! Acha tu. Mwenzenu nimebanwa hadi nashindwa kujinasua.”

“Inabidi ufanye, umkatae. Usije jichumia dhambi nyingi kwa unafiki.”

“Inabidi nifanye hivyo mwenzenu. Ila sijajua nitaanzaje, maana kaniganda kama ruba. Ama sijui anahitaji anitongoze, hivyo anashindwa gia ya kuniingilia. Na akinitongoza, atanipatia ladha gani itayoniridhisha? Ilhali nishazoea mihogo…”

“Eheheheeeeee…! Kama umeshindwa, tuambie watoto wa mjini tukupatie maujanja.”

“Litakuwa jambo la heri. Haya nielezeni.”

“Kuanzia kesho, ama leo atapokuja, weka kisingizio cha ugonjwa. Jidanganyishie kwa siku mbili tatu, halafu utawekwa kisingizio cha kudumu, cha huohuo ugonjwa, kwa kujifanya umelazwa.”

“Hospitali ipi watayokubali kufanya hivyo?”

“Si lazima hospitali. Hata hizi zahanati za huku mtaani. Tafuta hela tu. Hilo litafanikiwa.”

“Ushauri mzuri sana. Yafaa kuutekeleza sasa.”

“Haa!”

“Haa, nini? Nimemchoka huyu mtu ki—ukweli.”



Hatimaye morali, ikashuka. Moyo ukaruhusu upoozi, uliofanya mwili wangu uishiwe nguvu. Hata hamu, ya kuingia ndani ikanitoka, sikuhitaji tena, baada ya kutambua najipendekeza. Mithili ya kijana mtongozaji. Anayeng’ang’aniza akubaliwe sehemu asiyopendwa. Hakika! Nilighafirika mno. Nikajaa hasira, na tamanio la kuwaingilia ndani nikatembeze kichapo. Ila sikuweza kufanya hivyo, baada ya kuingiwa na tafakuri, iliyonishinikiza nirejee nyumbani nikapoze, machungu yaliyonitawala.



Mwendo ukawa mdogo mdogo. Mawazo yalinizidi, hasira, nayo ikachipuza kitu fulani kipya maishani mwangu. Kitu kiitwacho kulipa kisasi kwa sababu ya kufanyiwa dhihaka na mtu niliyethubutu kumthamini. Nilivyowasili nyumbani, nikapokelewa na shangazi Janeth, kama ilivyo desturi yake. Tena alinipokea kwa bashasha sana, kwani aligundua mapema tatizo nililonalo kabla sijamwambia.

“Dully!” aliniita. Alipenda kuniita hivyo kwa ufupi. Akimaanisha Abdul.

“Naam! Shangazi.”

“Nilikuambia toka mwanzo. Acha kuwa muathirika wa dunia ya sasa. Kwanini unapenda kuruhusu akili yako iumie kwa kitu usicho na uhakika nacho?”

“Shangazi!...” nilimuita. Ila kabla sijaendelea na kauli yangu, alinikatiza.

“Kamwe, usimuangushe, yule akufanyiaye mema maishani mwako, hata kama unasikia sifa mbaya zimhusuzo kwa jirani. Usipende kumhukumu mtu, kwa maneno ya watu. Kwani, hujui, kapatwa na nini hadi awe hivyo kwa wakati huo.”

“Na vipi kuhusu anayekuthamini, ukigeuka, anakuchukia?”

“Huyo hana tofauti na mnafiki. Ila hupaswi kumlipizia yale atendayo mafichoni. Mlipe kwa yale akutendeayo hadharani.”

“Hata kama hayo ya mafichoni yanakudhorotesha sana tofauti na yale akutendeayo hadharani?”

“Sahihi! Mema utayomlipa, yatamfanya ajitafakari juu ya yote akutendeayo. Halafu mwisho, atapata uamuzi gani achukue juu yako.”

“Kwa hiyo unanishauri nini kuhusu Jamila?”

“Ushauri wangu. Pale utapopata nafasi ya kuzungumza naye, na kufahamu ukweli wa dondoo ulizozisikia. Ndipo nitakushauri. Sasa siwezi kukushauri. Lakini pia, maamuzi ya ushauri huamuliwa na akili yako.”

“Hapo sijakuelewa.”

“Ushauri wangu si chochote kwako. Hauwezi kukusaidia, tena tatizo lenyewe, lihusialo binadamu. Inakuwa ngumu sana kuutekeleza. Bali utatekeleza kwa nguvu kilichopo moyoni mwako. Ukitekeleza wa kwangu, utatekeleza kwa mashaka. Ukiwa na hofu, kwamba ushauri wangu si mzuri. Na kuijenga akili, madhara yatayojitokeza kuhusu kile nilichokushauri, unitupie lawama. Sasa ya nini ufikie huko?”

“Hapana! Nauhitaji sana.”

“Basi ukionana na Jamila. Akakuambia sehemu ndogo ya maisha yake, ukija nieleza, nitakushauri nini ufanye juu yake.”

“Ahsante sana shangazi. Ngoja nihangaikie hilo.”

“Vyema. Ila nakukumbusha, mwanamke, ndiye mtu anayepatiwa mkazo wa kuthaminiwa sana katika jamii yetu. Hivyo epuka, kuwa sehemu ya uharibifu wa thamani yake.”

“Ondoa shaka shangazi.”







Baada ya maongezi hayo nilielekea chumbani kwangu kwa ajili ya kujipumzisha kwa muda, kabla sijaendelea na shughuli nyingine niliyopanga kuifanya. Pumziko langu halikuwa jema. Lilikuwa pumziko lililosheheni mawazo yote yamhusuyo Jamila. Kufananisha mipango aliyojipangia awe nayo na tabia niliyoisikia. Baadaye nikahamia kwa wazazi wake. Kuwatafakari, kama wanafahamu kuhusu kile nilichosikia. Kufikia hapo nikajawa na mshawasha wa kwenda tena nyumbani kwao. Awamu hii, lengo kuonana na wazazi wake. Nikawahadithie dondoo nilizosikia. Nilijivika u—wema, japo ndiyo asili yangu, kwa kuamini niendacho kufanya kitakuwa msaada kwa Jamila.



Nikaamka! Nikajitathmini, nilivyojiona niko katika muonekano bora utakiwao na jamii, nikaanza safari. Tena nilikuwa natembea kwa uharaka mno, niwahi. Sehemu ya pili, nikiwa na lengo la kumkuta Jamila, ili naye asikie sifa atunukiwazo. Baada ya mwendo, wa takribani dakika ishirini, nilibisha hodi nyumbani kwao. Bahati iliyoje, ilijibiwa mapema mno, kikiambatana na kitendo cha kufunguliwa mlango. Sura ya mama yake ikajibainisha mbonini.

“Aah! Mluga luga,” alisema mama Jamila. Kauli iliyonifanya nitoe kenuo la domo langu.

“Dah! Niandalie maji ya kuoga bi. Mkubwa,” nilimtania.



Kicheko kikafuatia!http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



Baada ya kuhitimisha kuvua malapa nikapiga hatua hadi sebuleni. Nikajitupia sofani. Mama Jamila akiwa kaketi sofa jirani na lile nililoketi. Macho yake yakiwa pima kunisaili. Nikahema kidogo, sanjari na kujikohoza, baada ya hapo maongezi yakaanza.

“Inavyoonekana umechoka sana,” alisema mama Jamila.

“Dah!...kawaida,” nilimjibu, huku nikiji—kung’uta kung’uta suruali yangu iliyojaa vumbi kwa chini usawa wa fundo la unyayoni.

“Mmnh! Kuna jipya? Maana uso wako unanionyesha,…” alisema, ila hakumaliza kutamka, nikamkatisha.

“Kwanza Jamila yupo?”

“Hapana! Katoka. Vipi ulichonacho kinamhusu?”

“Ndiyo. Ila hata nikikufikishia hamna kitachoharibika,” nilisema. Ila ghafla, nikajikuta nimepatwa na wazo fulani akilini mwangu. Lililonifanya nijitafakari kwa muda, wakati huo mama Jamila akiketi sawia kusubiri kusikia kwa makini kile nilichomhaidi kumwambia.

“Nitaonekana vipi niongeacho kikiwa cha uongo? Maana sina uhakika, sitaonekana mbaya kweli, mwishowe tuchukiane?” nilijiuliza. Wajihi wangu ukidhihirisha unyonge, ulioashiria uogofyaji wa jambo.

“Kulikoni kimya tena?” aliuliza mama Jamila. Swali lililonishtua, na kunitoa kwenye tafakuri yangu.

“Liwalo na liwe. Lazima nilitoe. Ili lisiweze kunifanya mtumwa wa fikra,” nilijisemeza. Taratibu nikiyatua macho yangu kwenye wajihi wa mama Jamila.

“Nina jambo mama, linitatizalo. Kwa siku chache niponalo, linamhusu Jamila,…” nilisema na kuweka tuo. Mama Jamila akadakia.

“Ushampenda nini?...eti baba, unahitaji muwe wapenzi?” aliuliza huku akitoa cheko lililokenua domo lake Jambo lililonipa bahati ya kushuhudia meno yake meupe yavutiayo.



Japo alikuwa anaukaribia uzee, ila hakuacha urembo wake uzeeke. Kama wadaivyo vijana, kama hapa ni mzee yuko hivi, vipi enzi za ujana wake? Naam! Mama Jamila ni mrembo. Urembo wake hauna tofauti na mwanaye. Wamebahatika, tena wamebahatika haswa, kiasi kwamba hawakosi kuacha matamanio kwa wanaume marijali waonekapo sehemu. Hata nami pia, sikukwepa kuwa sehemu ya watamaniao kwani siku zote nitembeleazo juu ya mafundisho nipatayo na maongezi mengine tuyajadiliayo, nilikesha kuwatathmini, na kutathmini namna waume walionao wanavyowafaidi. Hadi ilifikia hatua, kutamani kuona sehemu ndogo ya nyama ya maungo yao, nyama za paja na matiti. Hasahasa mama Jamila. Huyu nilimtamani sana nione sehemu hizo, kutokana na umbo alilobarikiwa. Lilikuwa zaidi ya mwanaye. Isitoshe mwanaye Nilishawahi, mshuhudia siku moja matiti yake alivyokuwa ananipatia mafundisho. Alivaa blazia kubwa, iliyochangia matiti yatoke toke ainamapo.

“Hapana mama. Si hilo.”

“Lipi ulilonalo? Niambie, niko tayari kukusikiliza.”

“Mama! Jamila anafanya shughuli gani?” nilimuuliza. Macho yangu yakiwa pima usoni kwake. Nikamshuhudia akishtuka. Mshituko, uliomhimiza kuinuka kidogo. Muinuko uliomfanya hadi aache kushikilia sehemu ilindayo thamani ajivuniayo. Sehemu ibebayo jinsia yake. Kitendo cha kuachia, akatengeneza mwaya, ulioshinikiza macho yangu kutazama huko. La haula! Fuadi wangu ukalipuka shangwe. Hata ule unyonge uliosalia salia ukapotea kabisa. Nilishuhudia fahari yake. Ajivuniayo siku zote. Nilishuhudia kuanzia mapaja yalivyonona vyema, hadi kunako. Hakuvaa kitu ndani. Hivyo fahari yake ilijibarizi huku ikiwa imefichwa na askari wafupi wafupi walioonekana wametoka kufanyiwa usafi siku chache zilizopita.



Pasipo kutaraji, akili ikanibadili, hata yale niliyopangilia kuyatamka yakapotea, huku surualini, mwenye jinsia akijikazana kutafuta nafasi ya kujichanua. Mama Jamila alilishuhudia hilo, hali iliyomfanya aanze kuona tahayari.

“Vipi?” aliniuliza. Kwa lengo la kutaka kunipotezea kile nilichokishuhudia. Kabla sijamjibu, nikakumbuka kauli ya Shangazi. ‘mwanamke, ndiye mtu anayepatiwa mkazo wa kuthaminiwa sana katika jamii yetu. Hivyo epuka, kuwa sehemu ya uharibifu wa thamani yake.’



Nikapoa ghafla. Jicho la mama Jamila likinisaili, muda mwingi akitazama kwenye suruali, usawa wa makazi ya mwenye jinsia na machoni. Naam! Niliduwaa kwa muda nikitafakari, nifanyaje? Ukizingatia nimekaa muda mrefu pasipo ingia ndani ya fahari ya mwanamke.

“Nimshawishi nini? Ili nijipatie utamu wake,” niliwaza. Baada ya kuwa na kumbukizi, baba mwenye nyumba hayupo na mwanae pia. Hivyo kulikuwa na wasaa mzuri, wa kufanya mambo kwa uhuru. Sikuishia hapo kumbukizi ikaenda mbali, kwa kukukumbuka maneno ya vijiweni, kabla sijaanza pata mafundisho kwa Jamila ‘Wa—mama wengi siku hizi wanapenda vijana, kwa sababu ndiyo wenye damu zinazochemka kwa shughuli’ kupitia kauli hii, nikajipa imani, kuna uwezekano mkubwa wa kutusua fahari ya mama Jamila, ambayo kupitia muono nilioufanya, ilinipa ishara, fahari yake, ni farahi iliyoumbwa vyema, kwa ukubwa wa kiwango cha kati. Na iliyobarikiwa mnato, wa kubana kitu kiingiacho.



Wakati wote macho yake yalikuwa kwangu. Nahisi naye alikuwa anatafakari, kama nitafakarivyo. Japo sina hakika tafakuri yake ilihusiana na nini. Punde, nikamshuhudia akinyanyuka pale alipoketi. Akapiga hatua chache akanifikia nilipo. Akajitupia sofani. Kitendo kilichofanya tubanane, sababu lilikuwa sofa lililotengenezwa, maalumu kwa ukaaji wa mtu mmoja.

“Nini shida, umepoa ghafla?” aliniuliza, huku mmoja ya mkono wake akishika kidevu kuinua kichwa changu kuelekezea aliko. Lengo tuangaliane. Akafanikisha!

“Mwili wangu umeishiwa nguvu ghafla. Na kujawa uhitaji wa jambo fulani,” nilisema. Macho pima usoni kwake. Nikisaili sura ilivyorembeka.

“Nikikupa ut…” alisema, lakini hakumalizia azungumzacho, nikadakia.

“Itakuwa heri. Maana hapa nilipo napata mateso ya hali ya juu. Mwenye jinsia huku ndani analilia kupoozwa.”

“Nifuate basi,” alisema mama Jamila, akiwa kashaamka kuelekea alikoniambia.



Baada ya mwendo wa sekunde kadhaa, tukafika sehemu husika, chumbani kwao. Nikaduwaa, ila baadaye niliishinda hofu, na kuchukulia kawaida. Haikuchukua muda mrefu, tukaanza mambo ya hapa na pale, akili yangu ikipambanua kwanini mama huyo kawa rahisi kwangu niitumbue fahari yake. Iliyolipiwa mahari nyingi na mumewe. Nikapata wazo, aidha, ananipenda toka muda, ndiyo maana alikuwa mcheshi kwangu, ama kwa sababu mumewe hayupo kwa muda mrefu baada ya kufunga safari kuelekea nje ya nchi. Michezo ilikuwa mingi, iliyoruhusu kila mmoja aguse mwili wa mwenziye. Huku nikigubikwa na furaha kupitiliza, sababu ni tamanio nililonalo kwa muda mrefu.



Kuhusu wosia wa shangazi, hapa haukufua dafu. Niliupuuzia, na hatimaye kufuata hisia zilizokithiri kwa muda huo. Muda mchache baadaye, kila mmoja akawa Kama alivyozaliwa. Jambo lililonifanya nizidi kufurahi mno, nilishindwa kupiga vigele gele tu kushangilia. Tamanio lilivyotuelemea, kila mmoja akajiandaa kwa mtanange kamili. Mama Jamila akajiachia kitandani, miguu juu, kunipa nafasi ya kushuhudia fahari yake vyema, huku ikiwa imetepeta kwa ute ute uliotoa ishara zote za uhitaji wa kuingiliwa. Nami, mwenye jinsia, alidhihirisha mishipa ya misuli kwa uwazi, kutoa uhakika, kwamba yuko tayari kwa kazi. Sikukawiza, taratibu nikapanda juu yake, na kumwelekeza Abdul wangu moja kwa moja langoni mwa mama huyo. Punde, nikaanza sikia miguno, iliyonitaarifu, mwenye jinsia anakata mawimbi katika safari yake ya kufikia sehemu hitajika.



Shughuli ikaanza. Ila haikuchukua hata sekunde nne, simu ya mama Jamila ikaita. Akasogeza moja ya kono lake, akaivutia karibu. Alivyotazama jina la mpigaji, alikumbana na jina la Jamila. Akanituliza, kwamba, nifanye taratibu kile kiendeleacho, aweze kupata nafasi ya kuzungumza. Nikafanya hivyo! Nikawa nasukuma mashine taratibu, ili yule azungumzaye asitambue yupo mchezoni. Baada ya sekunde chache, alizotumia kutafakari, akapokea.

“Mama!...mama!... Jamila kapata ajali, hali yake mbaya yuko hospitali, kalazwa…” ilisikika sauti ya upande wa pili. Iliyomfanya impatie mshituko wa nguvu, ulioweza kunisukuma hadi nikatoka relini.



Akainuka! Na kuketi pale kitandani. Wajihi ukabadilika, akaonekana mwingi wa wasiwasi, mithili ya mfumaniwa wa mapenzi.

“Tutakutana siku nyingine, acha nishughulike na hili kwanza,” alisema. Taratibu akivaa nguo zake.



Nami sikuwa na budi, nilianza vaa za kwangu, tulivyomaliza, nikamshauri tuelekee wote katika harakati za kufahamu hali ya Jamila. Maana, nilisikia yale maongezi aliyoambiwa. Ila cha kushangaza, hakuafikiana nami. Alikataa, kata kata. Jambo lililonipa shauku ya ufahamu wa mengi. Kati ya mama na mtoto. Dakika sita baadaye, tukawa tupo nje, mama Jamila akionekana mwenye kuchanganyikiwa zaidi, kijacho chembamba, kikibarizi usoni, huku nikikazia ushauri wangu wa kwenda wote. Lakini hakubadili msimamo. Hakuhitaji niende.

“Hapana. Hupaswi kwenda,” alikazia. Macho yakiwa pima kwangu. Yaliyojaa kila ishara ya kunitathmini.



Mwishowe niliafiki. Nikamwacha aende zake, nami kupiga hatua kuelekea nyumbani. Ila nilipofika umbali fulani, nikasita. Halmashauri ya kichwa changu, ikapata wazo la kupambanua nini kilichojificha ndani ya familia hiyo. Kuhusu hawa wanawake. Punde, nikapata wazo jipya. Nimfuatilie hadi hospitalini. Nikafanya hivyo!



Nikageuza uelekeo, nikaufuatilia ule alioelekea. Ila kwa kujiiba—iba, asiweze kugundua. Kwani tulitofautiana umbali wa mita takribani mia moja na kumi. Dakika kadhaa baadaye, nikamuona akisimamisha bajaji. Nami nikamuita dereva bodaboda, nikamuamuru aifuatilie hiyo bajaji hadi mwisho wa safari. Akaridhia!



Tulienda hivyo hadi hospitali. Nikateremka, kisha kufanya malipo, na hatimaye kuzidi kumfuatilia anakoelekea. Wodini! Nikabahatika. Kwani, hakuzunguka sana, akaifikia wodi husika. Nahisi alikuwa anapatiwa maelekezo na yule aliyempatia taarifa awali. Ndiyo maana ikamuwia wepesi wa ufahamu. Hatua hiyo, nikafanya tena tafakuri, nini nifanye, ila shauku yangu kubwa ni kuingia wodini, na ikafanikiwa, baada ya kujihalalishia lolote litalojiri, nitajitahidi kupambana nalo. Nikakaza miguu kutembea kwa kasi. Akili yangu ikiwa na lundo tele la mawazo, kufikiria namna nitavyokabiliana naye mama Jamila. Hali iliyonifanya niparamiane na watu.

“Aaah!...samahani kaka yangu. Ni mawazo,” nilisema. Nikimuambia kijana mmoja tuliyegongana hadi akatupa mzigo aliokamatia mkononi. Taratibu nikiinua uso wangu kumuangalia. Hamadi!...

“Usilazimishe mambo. Ukikataliwa, kubali katalio. Kwani kufanya ulazimishaji, utakufanya uingie kubaya,” alisema kijana huyo. Akiwa anaokota ule mzigo wake.



Maneno aliyotamka nikayahusisha moja kwa moja na kile nachofanya. Ikanibidi nijiulize, kafahamu vipi nang’ang’aniza jambo? Sikupata jibu. Hata ile shauku ikapotea na kunijaza mawazo kwa mara nyingine.

“Acha nirudi nyumbani. Nitakuja kesho,” nilijisemeza nafsini. Huku nikigeuka kurudi nitokako.



Nyumbani nikapokelewa na shangazi. Kwa bashasha sana, iliyojaa kila uashirio wa kuniondolea fukuto la tafakuri nililonalo. Kana kwamba ana taarifa kunihusu juu ya kile kilichonisibu.

“Hayo ndiyo maisha,” alinipokea kwa hiyo kauli. Macho kayatumbua kwangu, mithili ya mdeni wake.

“Unamaanisha nini?” nilimuuliza. Huku nikivuta kigoda nikaketi jirani naye.

“Daima, malipo ya wabaya hayabadiliki. Si wabaya tu, hata wema watendao ubaya kwa jaribio. Hizi nchi zetu, dunia ya leo, wanawake wengi hutawaliwa na imani. Watongozwapo na waume hutanguliza imani ya kuolewa. Dhana hii, huwaondolea vitu vingi sana, husaulisha akili zao katika utendaji wa mambo mengine, huielekeza katika utendaji wa jambo gani wafanye kulinda, na kutengeneza hitajio la ndoa. Si hivyo tu, pia hukesha kujibidiisha katika urembaji wa maumbo yao, waweze kupata waume wenye hali nzuri kiuchumi. Asilimia kubwa, ni wale wanukiao utajiri. Wanashindwa kabisa, kubidiisha akili zao, katika utafutaji, wa rasilimali njema zitazowafanya wawe wanawake wa nguvu ulimwenguni. Nasema haya kwa sababu…”

“Kwa sababu gani shangazi?”

“Wanawake wenye hizi dhana, hubadilika ni vigumu. Wakijibadilisha, itakuwa kwa muda tu, wakati huo wakiendeleza kutafuta sehemu waliyoiaminisha uhitaji. Wakifanikiwa kuipata, wakatoswa, huwa na jutio.”

“Unawazungumziaje watu wa namna hiyo?”

“Hakika! Warudio kwako kwa msamaha, ulioambatana na jutio ndani, kamwe usiwasamehe.”

“Hata kama nina mapendo naye?”

“Yeah! Kwani ipo siku, atabadilika, na kukufanya…” alisema, ila hakumaliza kama ilivyo ada, ya kawaida yangu. Nilidakia, ilhali sikuwa na utimilifu wa jambo la kulizungumza.

“Ila upendo una nguvu kubwa sana shangazi.”

“Sio sawa na kumbukizi.”

“Kwa hiyo unanishaurije?”

“Huwaga sibadiliki. Kukushauri, hadi utapokamilisha kile nilichokuambia mwanzo. Ila…”

“Nini?”

“Naomba uniahidi, nini hitajio lako, ambalo unahitaji ipate tokea siku, hata kama utakuwa umeondoka duniani, unahitaji watu wabakio, na wale wa vizazi vijavyo wakukumbuke?”

“Nahitaji kumbadilisha kahaba kuwa mwanamke mwenye nguvu ulimwenguni,” nilisema, macho pima kwa shangazi.

“Hongera. Naamini, Mwenyezi Mungu ataniweka nishuhudie kiapo hicho.”

“Insha—Allah! Atatujalia.





SONGA NAYO...



Kipepo cha wastani kilipamba jiji la Mbeya. Kilicholeta ubaridi wa mbali, uliokumbusha watu wenye afya zilizokosa ustahimilivu kutafuta mavazi ya kujikinga nao. Nami nikiwa mmoja miongoni mwao. Hali hiyo ilinisukuma kuvaa koti fulani kuukuu, lililojaa ramani lukuki ya kuchanika chanika. Ambalo alinipatia Shangazi Janeth kipindi fulani nilivyokuwa naugua. Sikusahau boshori juu. Chini raba, na suruali ya jeans, ilhali ndani nilitanguliza traki.



Nilivyojihakikisha niko vyema kwa matembezi mtaani, niliondoka taratibu chumbani kwangu. Nilivyogusa uga wa nyumba tuishiyo, nikamkuta Shangazi, kaketi kwenye mkeka wa ukili, akipiga nyimbo taratibu, zilizomsukuma kutingisha kichwa kufurahia aimbacho. Mithili ya wamama wa kipwani.

“Natoka,” nilisema. Nikiwa nimesimama karibu yake. Sauti yangu ikamfanya anyanyuke pale alipoketi na kunifuata nilipo.

“Nakusihi…” alisema na kutulia.

“Nini tena?”

“Naamini, huu ndiyo mwanzo wa kutekeleza kile ulichoniahidi.”

“Ndiyo shangazi.”

“Ni vizuri. Lakini nakukumbusha jambo. Usisahau kauli nikuambiazo, zina mengi ya kujifunza. Vilevile, kamwe, usijenge udiriki wa kutumainia akilini na moyoni mwako uamuapo kumsaidia mtu.”

“Una maanisha nini?”

“Wengi wetu, tunavyodiriki kutoa msaada kwa mtu, hutengeneza imani fulani, ambayo hujaza tamanio, msaada utavyokuwa na manufaa kwa yule nimsaidiaye siku za mbeleni nami nitahitaji anisaidie. Hali inayojenga utumwa muda mwingine, ambao kimsingi, hauna umuhimu endapo imani hii haitokuwepo.”

“Ondoa hofu shangazi kuhusu hilo. Sitodiriki kuwa na uchu wa fadhila kutoka kwa Jamila kwa yale nitayomfanyia yenye kumsaidia.”

“Litakuwa jambo jema. Kamwe baadaye usije ukageuka. Kumtaka kingono mtoto wa watu, kisa umemsaidia.”

“Usihofu.”



Tulivyohitimisha maongezi nikaendelea na safari. Nikiwa na nuio la kuanza rasmi harakati za kumsaidia Jamila. Aondokane na uhalisia uliopo moyoni mwake, awe na uhalisia mwingine usiopindisha. Uhalisia huru wa kimaisha utaomfanya ang’are muda wote. Atimize yale aliyoniahidi anatamani aje kuyafanya siku moja. Nilipiga mwendo wa haraka hadi Mwanjelwa. Hapo nikadaka bajaji, nikamuamuru dereva anipeleke hospitalini, kule alikolazwa Jamila. Japo akili yangu iliniaminisha kuwa kitendo kile ni geresha tu. Lengo atimize alichozungumza na rafikize jana.

“Lakini kwanini anatumia njia hiyo kunifikishia ujumbe? Anashindwaje kuniambia moja kwa moja haitaji mazoea nami?” nilijiuliza, taratibu dereva bajaji akijitahidi kuvuka vilima vya hapa na pale kuelekea nitakako.



Si hayo tu. Nilijiuliza maswali mengi sana, hadi tulivyofika eneo husika. Hospitali ya Mkoani. Nikamlipa dereva kiasi chake cha nauli. Nikateremka na kuangaza huku na kule, mithili ya watu wa intellijensia wahisio kusakamwa kila wakati. Baadaye nikapiga hatua kulifuata lango la kuingilia. Mrindimo wa mawazo ukiendelea, lakini awamu hii nilikuwa nafikiria Jamila kawezaje kuwasuka madaktari ili afanikishe alichopanga dhidi yangu.

“Mambo kama haya hufanyika kwenye hospitali za chini. Kama vile vituo vya afya na zahanati. Hospitali kubwa kama hii hawezi fanyia utoto. Itakuwa anaumwa kweli. Maskini, Mwenyezi Mungu anisamehe kwa kumhisi vibaya,” nilijisemeza, nikiwa nishavuka lango la kuingilia na kuambaa ambaa na uga wa majengo ya hospitali hiyo.



Baada ya kuvuka mita chache toka langoni nikapiga tuo, kwa ajili ya kutafakari kwa kina mawazo niliyonayo. Hapa nikapata wasaa wa kufanya ulinganifu kati ya yule nayehitaji nimsaidie pamoja nami. Ulinganifu wa kimaisha, kuanzia sehemu aishiyo, uwezo wa kiuchumi walionao, pasi na sahau uwezo wa kielimu. Vyote kanizidi, mimi nilikuwa kapuku kwake. Sikuwa na chembe ya ushawishi itayoniwezesha kusimama sehemu kushindanishwa.

“Nitaianza vipi hii harakati hadi nifanikiwe nimshawishi huyu mtu?” nilijiuliza. Fuadi nao ukiruhusu ushindwa, kwa kuamini fukara hawezi kutoa mchango wa kueleweka kwa tajiri.

“Mawazo yangu kwa mtu wenye elimu ya juu, hayana tofauti na matendo ya kuku. Hawezi kuyaelewa,” niliendelea kujisemeza. Lakini ghafla, nikapatwa wazo jipya nafsini. Lililonifanya moyo uende mputa mputa kwa sababu ya kuoanisha wazo lipi lipo sahihi.

“Hata kama maisha yetu ni ya ufukara, ila kamwe usije kujidharau. Uwe mbele ya mafukara wenzako, mbele ya matajiri na watu wenye elimu zao, usisite kuonyesha nguvu uliyonayo. Una nguvu kubwa, nguvu ambayo ukiitendea kazi unaweza badili dunia kwa sekunde moja na kuacha historia kubwa itayokufanya ukumbukwe daima. Sasa kama una uwezo wa kubadili dunia, utashindwaje kubadili mwenendo wa mtu?” nilikumbuka kauli hiyo. Ambayo aliniambiaga shangazi kipindi cha nyuma.



Kumbukizi hii ikaniongezea matumaini, kwamba ninaweza, na ninachopaswa ni kujidhatiti kuhakikisha sirudi nyuma.

“Binadamu hatujakamilika. Kila mtu ana kasoro, tumia kasoro ya yule aliyoko mbele yako kuonyesha u—mwamba ulionao,” niliendelea kukumbuka, na kupeleka fikra zangu mbali zaidi kwa kukumbuka kasoro aliyonayo Jamila.

“Juu ya uwezo wa kielimu, na uchumi mkubwa wa kimaisha kwao, ana tatizo moja linalomfanya limvunjie heshima,” nilijisemeza, baada ya kukumbuka tatizo analotuhumiwa kumkithiri. U—kahaba.



Kumbukizi hizo zikanichukulia muda mwingi, na kunitengeneza kuwa zezeta kiasi kwamba nilishindwa kuwa makini na liendelealo pembeni yangu. Mlinzi wa langoni ndiye akaja kunishtuza, na kunihimiza nielekee sehemu ninayohitaji kwenda kwa sababu maeneo hayo hayaruhusiwi mtu yeyote asiyehusika na uhitaji wa matibabu ama mtumishi wa hospitali kuwepo humo ndani.



Nikaja zinduka mithili ya mtu aliyefungwa na nguvu za giza. Hali iliyochangia nijae kigugumizi wakati wa kuondoka. Niliyumba huku na kule, nilipokuja kaa sawa, nilishtuka namparamia mbaba mmoja ambaye afya yake haikuwa imara.

“Kijana?” aliniita.

“Samahani mzee wangu. Naomba uniwie radhi, ni mawazo…,” nilisema kwa mkupuo, lengo nisimpatie mwanya wa kuzungumza. Lakini nilishindwa. Naye akawa chap kudakia.

“Una sababu ya kufunga safari uliyosafiri?” aliniuliza yule baba.



Nikaduwaa! Swali lake kwa kiasi fulani likanifanya nitafakari kwa mara nyingine sababu ya kufanya kile niendeleanacho.

“Si jamaa yangu, hatuna uhusiano wa damu, inakuaje nadiriki kujivisha kazi nisiyoalikwa? Ina maana jamaa zake hawajapata taarifa hizi?” nilijiuliza, takribani sekunde kumi na tano. Ila fikra zikabadilika ghafla nilipokumbuka jitihada zake za kupanua ufahamu wangu ijapokuwa si za kutoka moyoni.

“Nafanya hili, kulipa mema aliyonitendea,” nilijisemeza na kuanza upya kupiga hatua kuelekea wodini.



Hatua zangu zilikuwa fupi fupi, na za mwendo wa taratibu zilizonichukua dakika saba hadi kufikia wodi aliyolazwa Jamila, ila cha kushangaza, nilivyopiga jicho kitandani alipokuwa kalazwa, niliambua shuka jeupe likiwa limetandikwa vyema kurembesha kitanda. Hakuwepo, ina maana alisharuhusiwa. Ama kahamishwa wodi.



Kujihakikishia, nilimuuliza mmoja wa wagonjwa waliopo mule wodini. Ambaye kitanda chake kilikuwa jirani na cha Jamila.

“Huyo dada kasharuhusiwa asubuhi ya leo,” alinijibu mgonjwa niliyemuuliza. Jibu pekee ambalo niliridhika nalo na kunifanya nianze safari kurudi nitokako. Bali si nyumbani, lengo nifike nyumbani kwa kina Jamila.



Nilivyolivuka lango la kuingilia nikamuita mmoja mwa madereva bodaboda. Nikamueleza azma ya wito wangu naye kutii baada ya sekunde chache tu, tulivyokubaliana malipo nayopaswa kulipa. Kwa mwendo wa wastani, tulichagiza mitaa huu na ule, mwishowe tukaishia nyumbani kwa kina Jamila. Nikateremka. Nikatoa kiasi cha pesa nikamkabidhi yule dereva akaondoka, kisha nikapiga hatua hadi mlangoni.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



Sikujitafakari, nilibisha hodi ikaitikiwa kwa muda mchache tu toka nilivyohitimisha kauli yangu. Kikafuatia kimya kifupi, baada ya hapo nikaanza kusikia purkushani za kitasa kufunguliwa. Mlango ulivyofunguliwa sura ya mama Jamila ikajibainisha, lakini ghafla nikamshuhudia akiurudisha mlango kwa kasi na kufuunguka. Hakutaka niingie ndani jambo lililonifanya nihamaki na kuupa kazi ubongo wa kuanza kujiuliza maswali ambayo nilishindwa kuyapatia jibu.



Baadaye ikanibidi nishike kitasa na kujitahidi kukinyonga nyonga ili mlango ufunguke lakini ilishindikana. Mlango uligoma kufunguka. Ila niliendelea kung’ang’ana kwa kuwaita waje wanifungulie, napo sikufanikiwa, mwishowe nilibwaga manyanga na kurudi nyumbani kwetu.



Nilivyofika nyumbani nilifikia chumbani kwangu. Nikaanza kujifikirisha upya kulikoni? Takribani dakika tatu, nikapata jibu la hisio, kwamba kile nilichoambiwa kipo sahihi. Jamila anajihusisha na tabia ile chafu na wazazi wake wanafahamu. Lakini kwanini waliniongopea? Lengo lao nini?



Nilijiuliza mengi, hadi nikapitiwa na usingizi, ambao sifahamu ulinichukua kwa muda gani mpaka pale nilipokuja kuamshwa na shangazi kwa ajili ya chakula cha usiku.

“Una nini?” aliniuliza shangazi. Pindi akitua sahani lililo na chakula mezani.

“Naona kiapo changu kinaenda kuangamia. Sina hakika kama nitakifanikisha, kwani yule niliyemuamini sasa kaanza kuonyesha matendo ya waziwazi ya kutohitaji mazoea nami.”

“Abdul! Haijalishi hatua zipi utapitia, amini kile unachokiamini. Ule msemo wa tenda wema nenda zako, huu si wakati wake. Kwani haohao wanenao hivyo, ndiyo wataokupa maneno yote machafu pale utapomuacha kumsaidia mtu aliyekusaidia. Hata kama mhusika hataki, ila ukiona afanyacho hakistahili kwenye jamii, tumia huruma yako kwa usiri kumsahihisha.”

“Na vipi kuhusu ushauri wako?”

“Bado hujafahamu uhalisia wa Jamila ni upi. Katu sibadiliki, kwani sijatawaliwa na moyo wa ugeugeu. Nitakushauri ukiwa na uhakika kuhusu hicho kitu. Tena uhakika huo, uupate toka kwa mhusika mwenyewe na sio kwa kusikia maneno ya watu mtaani ambayo mara nyingi hayanaga ukweli zaidi ya dhanio. Pambana, mwisho wa siku nitakutaarifu ushauri ambao ni mwema na katu hautoujutia pale utapothubutu kuutumia.”

__________





“Hivi ni roho ya aina gani uliyonayo mwanangu? Mbona kila kijana mwenye nia njema nawe wam…”

“Kwanza badilisha kauli. Mimi sio mwanao.”

“Hee!...we mtoto wewe? Umepatwa na nini? Ama ushaanza kupandwa na ukichaa?”

“Niko timamu. Kila nifanyacho nacho kipo sahihi hamna ninachobahatisha.”

“Unatuchafua siye. Kila kukicha haushauriki. Unataka uambiwaje hiyo tabia uiache? Unatuchafua siye tunaokulea.”

“Kwa hiyo unanishaurije?”

“Badilika. Tii yale ambayo yalikithiri moyoni mwako kipindi cha nyuma. Ama unahitaji ukiondoka ukumbukwe kwa lipi? Hee!...niambie, jina gani ungependwa uitwe, sema unataka uitwe nani ukiondoka ulimwenguni?”

“Hey!...stop, wacha kunipigia makelele. Una huruma sana? Wacha nikupashe, kamwe sitobadilika. Nilipenda kuwa mtu mwema sana, mwenye malengo mapana, yenye kuibadili dunia kupitia maisha ya watu kipindi cha nyuma. Lakini, wanaume wamebadilisha maono yale na kuingiza maono mengine kichwani mwangu. Maono yaliyojaa hasira kali na kisasi.”

“Ila si wote waliokukosea.”

“Niwaonao hawana hatia, ndiyo hao niwakataao. Ila mtu atayepinga katazo langu lazima awe halali yangu.”

“Ina maana na Abdul naye?”

“Yeah! Akizidi kunifuatilia lazima aone uhalisia wa roho yangu.”

“Ila kahisi jambo kukuhusu.”

“Tena wa aina hiyo siwaachi. Si unakumbuka historia yangu huko nyuma? Mwanaume, hana tofauti na sumu katika maisha yangu. Ndiyo maana nadiriki kuyatenda yote uyaonayo. Kawaulize, wanaume wote waliopita na mimi kwenye shughuli niifanyayo, wanajuta.”

“Lakini kwanini unakuwa hivyo?”

“Ulikuwa wapi kuniuliza hilo swali siku zote hadi unitupie lawama kwamba nafanya tendo ovu lisilohitajika kwenye jamii, mara…”

“Naomba basi unihadithie nipate dondoo za ufahamu.”

“Swali lako nitakujibu kwa vitendo. Ila kwa uchache, kuna vijana wa kiume, ambao walisababisha katizo la uhai wa mama yangu. Kipindi hicho nikiwa na umri wa miaka kumi tu. Vijana wale walimbaka mama yangu hadi akakata roho. Nilivyowatathmini kwa umri hawakutofautiana na wanaye wa kuwazaa. Iliniuma sana, ila sikuwa na uwezo wa kumtetea. Kwani nilivyojaribu kuomba msaada, niliambulia kupigwa, mwishowe nami nikab…”

“Ulibakwa?”

“Sasa nitakuaje na huruma na watu wa aina hiyo? Ambao walikatisha ndoto zangu nikiwa robo ya safari?”

“Mmmh!...pole sana.”

“Haisaidii. Kwa sababu bado nina umivu kubwa sana moyoni mwangu. Na lazima, nihakikishe linatimia kwa asilimia zote. Tena miongoni mwa watendewa, wataokumbwa na adha hiyo mumeo yumo.”

“Mzee Namahala?”

“Yap!”

“Kwani wewe ni nani?”

“Ukitaka kunifahamu vyema, subiri siku nitayomshughulikia.”



Ni maongezi baina ya Jamila na mama yake (mlezi). Maongezi ambayo yaliwachukua muda mwingi kufikia tamati, na yalivyohitimishwa, yalihitimishwa kwa onyo kali kwenda kwa mama lililompa wakati mgumu kulielewa, vilevile kufikiria achukue uamuzi gani.

“Endapo haya niliyokueleza yatavuja, utakuwa halali yangu. Baki nayo moyoni mwako, usimwambie mtu yeyote, ukishindwa ondoka ndani ya nyumba hii,” alisema Jamila. Wakati huo kamsogelea mama yake na kumwelekezea uso kuonyesha mkazo kuhusu kile aongeacho.



Juu ya utu uzima uliomkithiri, mama huyo hakusita kutii alichoambiwa. Hakufurukuta, wala hakuinua kidole kujikuna, alitulia tuli huku akijifikirisha kilichopo ndani ya Jamila. Ana nini? Hadi awe na kisasi na mumewe, aliyemtambua kama baba yake mzazi hapo nyuma.

“Sasa Jamila ni nani? Na alikutana vipi na mzee Namahala?” alijiuliza mengi, ila hakufanikiwa kupata jibu.

“Huyu lazima akombolewe,” alijisemeza mama huyo.

__________



Akili yangu haikutulizana, namna nitavyolipa zile fadhila nilizopatiwa. Kinisukumacho kufanya hivyo, ni kwa sababu yule aliyenitendea mema anasadikiwa kuwa na matendo ya ovyo tofauti na nilivyomfahamu hapo awali. Sikuhitaji kumkimbia, kisa anatuhumiwa hivyo. Ya nini kumkimbia? Wakati aliutoa muda mwingi kwa ajili yangu? Inanilazimu kumsaidia hata kama yale mema aliyonitendea, ya kuongeza ufahamu bongo yangu alifanya kwa hali ya basi tu.



Juu ya nia hiyo, sikukosa sitasita. Nitamsaidiaje mtu asiyehitaji kusaidiwa? Ila nikikumbuka fadhila zake, nikaona kama namsaliti. Simtendei haki, kwanini? Nilijiuliza pasi na jibu.

“Kama ameweza kuutumia muda wake kwangu, kwanini nami nisiutumie muda wangu kwake?” nilijiuliza, wakati huo kiguu na njia uelekeo nyumbani kwao.



Mwendo wa dakika arobaini na tano ukanifikisha mahali hapo. Ilivyo bahati, wote, nikiwa na maana mama na mtoto; niliwakuta nje. Ila sura zao hazikuonyesha kukaramka. Zilijaa mikunjo iliyonipa utambuzi hamna maelewano mazuri baina yao. Sikujalisha hilo, niliwasabahi na kuwaonyesha bashasha tele kana kwamba hakuna nilichogundua.



Baada ya hitimisho la salamu kikapita kimya kifupi takribani dakika mbili. Baadaye nikajivika umwamba kutaka kuonyesha udume wangu, kuufukuza ule ukimya kwa kumvaa vaa Jamila.

“Jamila!...kuna jambo nimelisikia huko mtaani naomba ufafanuzi wako,” nilisema. Nikiwa nimetupa jicho pima kumsaili. Naye akafanya vivyo hivyo, alinitupia jicho kali ambalo hajawahi nionyesha tangu nilivyomfahamu. Ambalo lilinitambulisha lina dharau tosha na chuki nzito dhidi yangu. Nilihisi hivyo, ila si kwa mkazo sana kwa sababu sikufahamu kilichopo moyoni mwake.



Nilivyotupa jicho kwa mama, naye alikuwa na muangalio wake ambao kama ulinitahadharisha nisiendelee kuzungumza na Jamila, lakini sikulitambua hilo, nikajivika kimbelembele kwa mara nyingine nikakazia swali langu.

“Jamila, sijaamini nikisikiacho. Hivyo nikaona vyema nije uniweke wazi maana zile sifa hazifanani na uliv…” sikumalizia kauli yangu. Akanikatisha.

“Ina maana hufahamu kuwa kimya nacho ni jibu? Hebu niondokee hapa usije niharibia siku. Tena, kaa mbali nami, mazoea tuliyonayo mwanzo sasa mwisho.”



Dah!



Kilichofuatia ni tahayari upande wangu. Hakika! Nilijisikia kuhaibika ijapokuwa sikuweka wazi hali hiyo. Ikanibidi niage, kiunyonge sana kwa sababu akili yangu ilianza kupambanua matokeo ya kile kilichonisibu yatakuaje.



Moja kwa moja nilirejea nyumbani wajihi wangu ukiendelea kuniweka wazi nitokako mambo hayako vyema. Kiasi kwamba hadi shangazi alilitambua hilo. Na kuonyesha shauku ya kunitupia neno ila kabla hajaruhusu utamkaji alikatishwa na sauti fulani ya kike iliyotoka nyuma yetu.

“Abdul! Unataka kuniambia ushafahamu shughuli afanyayo Jamila?” ilisikika sauti hiyo. Ambayo ilitoka kwa mama yake Jamila.

“Ndiyo nafahamu japo sina uhakika nayo. Maana nilivyotamka kumuuliza mwenyewe si unaona jibu alilonipatia?”

“Juu ya kufahamu, kuna kitu unahitaji kufanya kumhusu?”

“Nina lengo la kumuondoa kwenye huo utumwa kama kweli anajihusisha na hiyo shughuli.”

“Mmmmh! Abdul. Fanya kama alivyokuambia. Achana naye. Jamila ana lake moyoni. Ana kisasi kikubwa sana kwa watu wenye jinsia kama yako. Kiasi kwamba mtu tofauti na siye tunaoishi naye pale akifahamu kuwa kamfahamu lazima ajenge uhasama naye.”

“Haijalishi hilo. Nina nia ya kutumia muda wangu kumsaidia kama alivyoutumia wa kwake kunisaidia. Na kwanini hamkuniambia ukweli mwanzo nilivyowauliza?”

“Hakutaka na haitaji mpaka sasa watu wafahamu kuwa anajihusisha na biashara ya kuuza mwili…”

“Kwa sababu gani?”

“Kisasi alichonacho!”

“Kisasi cha aina gani hicho hadi awe hivyo?”

“Kama utaweza, tafuta siku nyingine umuulize. Lakini sikushauri…”

“Sawa. Niache nifanye kile nilichopangilia kwa kwa lengo la kumsaidia.”

“Abdul, nahisi unataka kuangamia, kwani wanaume aliopita nao hadi sasa tangu aanze hiyo shughuli haifahamiki walipo na hali walizonazo.”

“Ina maana unawafahamu? Anawauwa? Ama anafawafanyaje?”

“Sina hakika, ila nahisi.”

“Kwangu hatofanikiwa.”

“Haya acha nijionee kitachojiri.”

“Tumuombe Mwenyezi Mungu.”



Baadaye mama Jamila akaondoka. Akatuacha siye tumetumbuliana macho pima huku bongo zikichakata tulichosikia. Dakika mbili mara baada ya kuondoka nikamuona shangazi akinivamia kwa kasi na kunitingisha tingisha huku akiambatanisha na kauli fulani.

“Umeivaa…umeivaa, mwanangu umeiva,” alisema shangazi. Kauli ambayo katu sikuielewa kwa haraka anamaanisha nini. Ikanibidi niipambanue, kwa kujiuliza maana amaanishayo. Nilitumia takribani sekunde hamsini nikitafakari hiyo kauli, ilivyokamilika dakika, ndipo nikapata utambuzi. Baada ya kukumbuka kuna siku ashawahi nitamkie na kunieleza maana yake.

“Aaah!...nimefuzu,” nilikumbuka hiyo maana. Ambayo naye aliisikia pindi wanapatiwa mafunzo ya mgambo kipindi cha nyuma na askari wa jeshi la wananchi.

“Upo vizuri kijana wangu. Yale nikuambiayo nimeona unayatekeleza.”

“Kivipi shangazi?”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Hujaruhusu kumuamini yule mtu hata kama anaishi karibu na umtakaye. Hivyo ndivyo itakiwavyo. Kwani ungelijaribu kukubaliana naye ingelikuwa haina utofauti na kuacha malengo yako, na kufanyia kazi malengo ya mwingine. Big up! Naamini kila kitu kitakaa vyema, pambana utimize ulichoniahidi.”

“Bado tu hujafikia hatua ya kunishauri juu ya kusikia taarifa zote hizi zimuhusuzo?”

“Bado. Ila,…nitakupa kauli, ambayo itakuwa mwongozo kwako kufikia kile ukitakacho. Kwanza yakupasa ukumbuke mwanamke ndiye mtu aliyepewa kipaumbele cha kuthaminiwa. Hivyo mwanamke ni thamani, afanye asiichezee thamani yake. Kisha mwambie, asitengeneze mazingira yatayochangia mumewe awe mtu wa kujilaumu muda wote. Na kujiona kakurupuka katika uoaji ilhali walikuwa na mahusiano mazuri ya kimapenzi nyuma na ya muda mrefu.”

“Hamna shida shangazi. Nakuhakikishia nia lazima itimie.”



ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog